Simulizi NA Michezo Tz.

Simulizi NA Michezo Tz. Wakara wa simuilizi na matukio yote GRP special for story and others. post s. and share. every thing X move and pictures no. in my GRP

❤💋NAMBA 11TULIISHIA pale Haji alipoiba pesa za baba yake kule stationery na kutoweka akimtoroka.ENDELEA SASAMoja kwa moj...
06/06/2026

❤💋
NAMBA 11

TULIISHIA pale Haji alipoiba pesa za baba yake kule stationery na kutoweka akimtoroka.

ENDELEA SASA
Moja kwa moja Haji alifika hadi nyumbani kwao, kwa akili yake alijua lazima binti atakuwepo,
"Shikamoo" Alimsalimia mama yake huku akihema na kunyoosha moja kwa moja mpaka katika chumba cha Hellena

"Marahaba.....wewe vipi....mbona hurry hurry?" aliuliza mama huku akiwa ameshika rimoti ya kisimbuzi mkononi

Haji alipofungua chumba cha binti na kutazama ndani aligundua kuna mabadiliko, hakuna nguo wala chochote cha Hellena. Alitoka speed na kumtazama mama, kijana huyu alikuwa k**a mtu aliyechanganyikiwa

"Mama" aliita huku akishangaana na mamaye

"Nini, mbona sikuelewi?" mama aliuliza

"Hellen yuko wapi?" Aliuliza Haji halafu akaingiza mkono mfukoni simu inaita

"Amehama" mama alisema

"Msiwe mmemfukuza" alisema na kutoa simu mfukoni akaitazama ni Hellena anapiga, akatabasamu na kuipokea
"Mke wangu" Alitamka maneno yaliyomshtua mama yake kwani hiyo ni tabia mpya kabisa kwa mwanaye kupokea simu na kuongea neno zito k**a hilo mbele yake

"Mke???" mama aliuliza ila Haji hakuwa na time naye

"Uko wapi?" aliendelea kuongea na simu "Umehamia kichangani tayari?" aliuliza na kutembea hadi mlangoni akazungusha kitasa akatoka

"Wee Haji" mama aliita "Nani huyo unaongea naye?" alipata mkanganyiko baada ya kuhisi ni Hellena, ilikuwa ni kweli, lakini ni siku moja tu imepita tangu alipokuwa amempa onyo kali kuhusiana na msichana yule
"Hivi huyu.......yaani,......usikute anatoka na yule msichana jamani" alisema kwa hasira na kuzima TV yaani kutokana na hasira alihisi ilikuwa inamsumbua

Haji naye alikuwa anatembea mtaani mpaka akafika maeneo aliyokuwa amepanga kuonana na Hellena,
"Nimeshafika"

"Umeshafika wapi?"

"Si umeniambia hapa karibia na sokoni au?" aliuliza

"Ndio, mbona sikuoni"

"Kwani wewe uko wapi?" Aliuliza

"Niko kwenye hiki kibanda kilichoandikwa Therry Investment" alisema

"Sawa" aliongea

Kwa kuwa Haji alikuwa mwenyeji, alinyoosha mpaka pale pale alipokuwa binti, huwezi amini ni sokoni lakini Haji hakusita kumkumbatia mbele za watu, japo kulikuwa na giza ila taa ziliwamulika

Haji na Hellena walianza kupigana mate pale pale sokoni watu wanawashangaa, baada ya sekunde kadhaa waliachiana na kuondoka wakiwa wameshikana mikono

Walitembea hadi katika nyumba aliyokuwa amepanga binti, Haji na Hellena waliingia ndani ya chumba cha binti wakakuta bado kubichi, godoro limeegemezwa ukutani na mabegi ya nguo na viatu yapo pembeni

"Hellena" Haji alisema huku akitoa machozi

"Nini?"

"Sijui najisikiaje juu yako, nakupenda sana, nashangaa kila muda nakuwaza wewe" alisema Haji

Hellena alicheka kwa nguvu na kwa kejeli
"Achana na habari za kunipenda, mi nataka hela niliyokuomba"

"Nimeshakuletea mpenzi wangu" Alisema Haji huku akitoa kibunda cha pesa alizomuibia baba yake na kumkabidhi

"Ni shilingi ngapi?" aliuliza mtoto wa k**e

"Sijui maana sijazihesabu"

"Sogeza godoro hapo tuhesabu wote" Alisema binti na Haji alisogeza godoro wakaketi kwenye godoro na kuanza kuhesabu
Ni kweli kilikuwa kibunda cha noti nyingi sana lakini zilikuwa zimechanganyika mara buku buku, buku mbili mbili, elfu tano na elfu kumi hivyo zilipohesabiwa zilikuwa k**a laki mbili na elfu sita tu.

"Haya sasa" binti alisema "Mwanaume gani wewe? Sasa hii itanisaidia nini?" Aliuliza mtoto wa k**e

"Jamani kwani haitoshi?" Haji aliuliza, alikuwa amekwisha kuwa k**a mjinga mjinga

"Ndio" alisema mtoto wa k**e "Embu ona, kitanda ni laki na sitini (160k) na kisafirisha ni elfu 10 mpaka hapo imeshafika laki na sabini, hapo imebaki shilingi 46000 (elfu harobaini na sita) je unadhani jiko, chandarua, mapazia na kapeti nitanunuaje?" aliuliza binti kwa dharau na kuzitupa hela chini kwenye godoro "K**a huwezi kunihudumia achana na mimi" alisema kwa dharau na kutaka kuinuka

Haji alimuwahi mkono na kumvuta "Usinifanyie hivi mpenzi, naomba unisikilize...., nunua kitanda, hivyo vingine nitakuletea hela yake kesho"

"Weee, kesho? Mimi nilale bila kula, bila kufunga neti niumwe na mbu?, aku mi sitaki" alisema na kumlalia kijana begani "Baby" Hellena aliita "Si unanipenda kaninunulie basi hivyo vitu sa hivi?" aliongea kwa kudeka

"Mimi sasa saa hizi ntapata wapi hela? Naomba ulale hapa chini kesho nitaongezea ununue kitanda"

"Mi sitaki!" Binti alisema huku akijirusha juu na kuketi anajifanya k**a anataka kulia, mi nataka uende sasa hivi, k**a hutaki ondoka ndani kwangu"

"Mmh, tena"

"Ndio ondoka sasa hivi"

"Hapana mpe....."

"Nimesema tokaaaa" alifoka binti hadi Haji akaogopa na kuinuka kweli, alipoinuka tu hivi akataka kuziokota zile pesa zilizomwagwa kwenye godoro

"Unaokota Hela za nini? Ondoka zako mwenyewe mpaka uje na jiko hapa na kapeti na neti ndo utaruhusiwa kuingia ndani" alisema mtoto wa k**e

"Babe...." Haji alisema

"Usiniite baby, babe gani usiyejua kuhudumia?" alimfokea hadi Haji akatoka akiwa mpole.

Alipofika nje tu, Hellena alianza kucheka sana huku akionyesha kumdharau "Hahahaa, huuu, na utakoma mwaka, huu"
Mara ghafla simu yake ikaita, aliyekuwa anapiga ni Ibra
"Umeshindaje mke wangu?" Ibra alisema

"Safi dear, uko powa?" aliuliza

"Niko powa nambie love"

"Ibra nimemiss kukuona, njoo basi"

"Nije wapi?" aliuliza

"Nimehamia kichangani nimepanga"

"Mh lini?" aliuliza

"Leo leo"

"Haaah, upo na nani?" aliuliza

"Niko mwenyewe japo sijaweka vitu kiviiile"

"Nije kweli?" aliuliza Ibra

"Njoo kweli"

"Mmmh utanipa nini?" aliuliza Ibra

"Kwani wewe unataka nini?"

"Taam"

"Taam ipi, sukari au?"

"Hamna ile tamu kuliko zote"

"hahaha una vituko wewe"

"Kweli nije utanipa? Maana nina muda, na wewe ya kwako inaonekana taaam"

"Kwanini tam"

"Ulivyo mweupe, wee kitakuwa chekunduuuu?" alisema Haji

"Hahahaaaa, kwenda huko"
HUYU IBRA KAONYWA NA HAJI LAKINI NASHANGAA ANAENDELEA
JE IBRA ATAPEWA?

06/06/2026

IPHONE, SAMSUNG GALAXY NDIO SIMU UNAANDIKA "CROCODILE" IKULETEE 🐊🐊 ZA MKOPO KAENI KANDO😂 😅😅

Simulizi NA Michezo Tz. ❤💋NAMBA 10Tuliishia pale Ibra alipompigia simu Haji ili amueleze kwamba Hellena ameshamkubalia, ...
05/06/2026

Simulizi NA Michezo Tz. ❤💋

NAMBA 10

Tuliishia pale Ibra alipompigia simu Haji ili amueleze kwamba Hellena ameshamkubalia, lakini Haji akamtukana na kumtaka aachane na mke wake

ENDELEA SASA
"hahahahaaaaa........hahahaahah huuuuu" Hellena alicheka kwa furaha sana akiwa chumbani anavaa nguo zake
"Hahahaa....ni furaha, iliyoje? Yaani mshahara umetoka na vile vile nimefanikiwa kumkomesha huyu mwanaume mjinga mjinga" alisema kwa sauti ndogo, "Nitamuonyesha kwamba mimi ndo mtoto wa Mzee Temu, mjukuu wa Bi Kundikwa" alisema kwa furaha sana halafu akajipiga 'make up' nyembamba na kutoka chumbani, huyoooo.....kazini

Akiwa anazidi kufanya kazi, kuna sehemu ambayo yeye na wenzake walikuwa wakiweka simu ili isilowe maana walitumia maji sana katika usafi waliokuwa wakiufanya

Walipiga usafi, huzuni yote aliyokuwa nayo jana, leo imegeuka furaha ya ajabu, alijisifu sana.

Baada ya usafi Hellena aliisogelea simu yake, alikuta message 12, huku 1 ikiwa ni ya Voda Taarifa na 11 zikiwa za Haji

Hakuisoma ile ya Voda taarifa, la, alirukia za Haji

1. Hellena mpenzi wangu nimekuja kuamini wewe ndo mwanamke ambaye umeumbwa kwa ajili yangu

2. Samahani sana kwa yale maneno mabovu niliyokuambia juzi

3. Naomba unisamehe sana

4. Nakupenda na niko tayari kukuoa hata sasa hivi ukitaka

5. Tafadhali usimkubalie mwanaume yeyote

6. Hata Ibra achana naye

7. Nakupenda sana

8. Naomba usinisaliti

9. Naomba unirudie

10. Mimi ni wako tu

11. Nijibu basi nakosa amani kwa sababu yako honey

Hellena aliposoma messages hizi alicheka sanaaaa, alicheka mpaka machozi yakamtoka. Ndipo kabinti fulani kakamfuata, kambea kweli

"Vipi shoga mbona unacheka sana?" Aliuliza

"Hamna, niache, nina furaha zangu" alisema mtoto wa k**e

"Nini tena, umepata kazi nzuri au?"

"Ah wapi? Kuna mtu nimemkomesha Mwenzangu, text zake zinaonyesha amechanganyikiwa na mahaba ya Kirangi" alijisifu binti

"Umemfanyaje?"

"Hamna wala, ni ufundi tu, ukishaifinyia kwa ndani wanakuwaga hawana akili hawa" alisema wote wakacheka na kugonga.

Hellena aliamua kumjibu ujumbe mmoja Haji, na kumtumia hivi
"K**A UNATAKA TURUDIANE KWELI, MI NAKUBALI, ILA KWA MASHARTI HAYA
1. TUSIFANYE CHOCHOTE MPAKA TUOANE
2. UNIPE HELA NIKAPANGE NJE NA HAPO KWENU
3. USIWE NA MWANAMKE MWINGINE"

Aliituma hii message kwa Haji, yaani kutokana na kijana Haji alivyokiwa amepagawa na mapenzi wala hakusita kujibu, ilichukuwa sekunde chache tu kujibu hiyo sms

"NIKO TAYARI KWA KILA KITU, K**A NI HELA YA KUPANGA NITAKUPA LEO JIONI, NA PIA SITOKUWA NA MWANAMKE MWINGINE, KISHA NITASUBIRI MPAKA TUOANE"
Huyu kijana hana kazi, je, hela ya kumpa binti akapange ataipata wapi?

Hellena aliisoma akatabasamu, na kumtumia ujumbe baba yake mzazi
"Baba, muambie bibi ninashukuru sana sana sana, mambo yameshakaa mstarini sasa" Alituma ujumbe Hellena lakini baba hakujibu maana alikuwa hana SMS
Mshahara wa laki tatu sio mkubwa kwa mtu anayetaka kwenda kupanga, haitoshi hata kitanda na godoro, kisha kuna kodi na vikorokoro vingine

Hellena alimuacha katika mawazo makubwa Haji, alikuwa hajui ni saa ngapi ataipata hiyo pesa ampatie maana alikuwa hana kibarua chochote alikuwa akiishi kwa wazazi wake

Hellena alipotoka tu hivi, alienda moja kwa moja hadi kichangani, mbali kidogo na pale alipokuwa akifanya kazi. Alipofika tu hivi, Hellena aliwasiliana na dalali mmoja ambaye alimpeleka katika nyumba moja kulikuwa na vyumba vya kupangisha, alichokuwa anataka ni kupata nyumba ya kupanga tu hakutaka kuendelea kukaa kwa kina Haji, hii ni kwa sababu alijua kuna jambo linatakiwa litokee zito kabisa

Hellena alikiangalia chumba ni kizuri sana, kilikuwa kinapangishwa kwa sh 20000 kwa mwezi, akapiga hesabu, miezi sita ni shilingi laki na elfu ishirini (120000)
Alilipia kisha akamlipa dalali, na kuondoka wote kwa pamoja

Hellena alikuwa amebaki na shilingi 140000 (Laki na elfu arobaini) tu baada ya kulipa kodi, dalali na bodaboda, aliona inatosha godoro la 4 kwa 6 la kuanzia maisha, alinunua na kulipeleka kisha akaenda mpaka kwa kina Mama Sophie, yaani mama Haji

"Mama, mimi nataka nikapange" Alisema

"Hheeee! Mwanangu kwanini? Au tumekuudhi?" aliuliza mama

"Hapana mama, nimeishi hapa kwenu kwa muda mrefu sana, mmenijali na kunilea k**a mtoto wenu, ninahitaji nikapange sasa ili niweze kujifunza kujitegemea" alisema

"Kweli binti yangu?"

"Ndio mama"

"Umeshawaambia wazazi wako?"

"Hapana"

"Waambie kwanza ili wajue"

"Sawa hamna shida, nashukuru sana kwa ukarimu wenu mama"

"Sawa.....baba yuko katika biashara zake akirudi utamueleza"

"Naondoka sasa hivi"

"Sasa hivi?"

"Ndio, ila nitarudi kuja kuongea naye"

"Mbona ghafla?"

"Sio ghafla, nilipanga mda"

"Oooh, basi asante mwanangu karibu sana"

"Asante"

Hellena aliingia chumbani na kuanza kukusanya kila kilicho chake, kisha akatoka na kupakia kwenye bajaji, huyoooo, Kichangani.

Ile amefika hivi aliviweka ndani na kumpigia haji
"Baby" Alisema binti

"Nambie mke wangu"

"Nimeshalipia chumba, nimepungukiwa, sina kitanda, sina jiko wala vyombo wala kapeti, nisaidie hiyo hela" alimuamrisha

"Usijali ndio ninafanya mpango sasa hivi mpenzi" alisema Haji

"Okay nasubiri"

Haji alikuwa katika biashara za baba yake kule chuo cha SUA, baba Haji alikuwa na Stationery pamoja na kamgahawa kwa ajili ya wanafunzi.

Haji siku hiyo alijipendekeza akaingia katika stationery na kuamua kufungua droo moja, akakuta kitita cha pesa, akakichukua na kuamua kumtoroka baba yake akakimbia na pesa hizo......ITAENDELEA
USIKOSE NAMBA 11

FRIENDS WHO LIKE SIMULIZI NA MICHEZO 2022 TULIISHIA pale Hellena alipokuwa ameshaongea na Bibi yake, kisha akaingia ndan...
04/06/2026

FRIENDS WHO LIKE SIMULIZI NA MICHEZO 2022

TULIISHIA pale Hellena alipokuwa ameshaongea na Bibi yake, kisha akaingia ndani ya hospitali kwa ajili ya kuendelea na majukumu

ENDELEA SASA
Hellena siku ile alikuwa na furaha isiyokuwa na kifani, alifanya kazi vizuri sana hadi wakuu wake wa kazi walimsifia. Jioni alipanda bodaboda kisha akapelekwa nyumbani

Akiwa kwenye pikipiki aliwaza mambo fulani ya kujisifu
"Hahaha, hanijui vizuri huyu atanyooka mwaka huu.....alifikiri mimi wa mchezo mchezo, nimechoka kuchezewa mimi" aliwaza binti.
Alipofika mwisho wa safari alimlipa boda boda akaondoka, ile binti anataka kuingia getini kwa mama Sophie ghafla sauti ilisikika nyuma yake

"Mrembo Hellena" ilikuwa sauti ya kiume, akamgeukia na kutazama kumbe ni Ibra karudi tena, bado hajakata tamaa

"Abee" Binti aliitika kwa tabasamu pana, lililomfanya Ibra ajisikie mwanana na hata kutamani kuendelea kuongea naye.

"Umependeza" Alisema huku akimuangalia maeneo ya mwili

"Asante" Binti alijibu na kushika mdomo kwa aibu

"Vipi sasa, tutaweza kuonana please nina ya zaidi ya kuongea na wewe" Alimuuliza

"Hahaha, wala usijali kesho nitakupa taarifa kwa sababu kesho ni wikiend nafikiri ninaweza nikawa free kidogo" alisema Hellena

"Woow, nitashukuru sana k**a utakubali toanane"

"Usijali, tutachati"

Hapa nilijifunza kitu kimoja, kumbe mwanamke ukimkuta akiwa na furaha kiukweli atakujibu vyema sana, anyway tuendeleee!

Hellena na Ibra waliagana, binti akaingia ndani na kuendelea na kazi za nyumbani

*
Usiku saa 3 Haji na Ibra walionana
IBRA: mwanangu yule demu sa hivi anaeleweka
HAJI: Acha matani, amejibuje?
IBRA: amesema wikiendi nitaonana naye mahali
HAJI: Wow
Haji alifurahi sana maana alikuwa amejutia kujiingiza katika mahusiano na yule binti, hata hivyo aliona k**a vile kile kitu alichokuwa anakihitaji kitaenda kutokea, alitaka fursa ambayo ingemfanya akae mbali na binti

Haji aliwaza na kujua kwamba k**a binti ameamua kumkubalia Ibra, basi itakuwa ni kwa sababu amemchana akamuambia kwamba hamtaki, Haji alivuta pumzi ya furaha
"Yes, aniache niinjoy na watoto wakali" Aliwaza na kutabasamu

*****
Asubuhi na mapema Haji aliamka na kwenda kuketi sebuleni akawa anajisikia furaha sana. Wala hakujua kwanini ana furaha

Ghafla Hellena alitoka chumbani kwake akiwa anazifunga funga rasta zake kichwani ili akaoge, ndipo simu yake ikaita chumbani na kurudi akaenda kuipokea

"Hallo Ibra...." Ilikuwa sauti ya binti ambayo pia ilisikika sebuleni alipokuwa ameketi Haji, sauti hii ilimshtua sana haji

"Hallo, umeamkaje mrembo?"

"Nimeamka salama tu my dear, vipi wewe?" Hellena aliongea makusudi kwa sauti kubwa ili Haji asikie
Kweli haji alishtuka alipokuwa akisikia yale maneno

"Niko powa, nimekumiss sana Hellena natamani kila muda nikuone" Ibra alisema, binti akaweka loud speaker

"Mmmh kweli?" alisema binti na kucheka kwa sauti legevu

"Ndio"

"Nimekumiss piaaah!" alisema kwa kulegeza sauti zaidi

Haji alisimama sebuleni na kushika kiuno kwa hasira sana "Huyu Ibra ni mbwa na huyu mwanamke ni Malaya sana" Alisema kwa sauti ndogo Haji

"Haaah.....basi baadaye ukitoka utaniambia nije nikuchukue na pikipiki"

"Nitashukuru kwa hilo, halafu pia Ibra nafurahi sana unavyonijali, unanifanya nisikie furaha muda wote" alisema Hellena

"Usijali niko kwa ajili yako" Ibra alisema

"Ok, baadaye, ngoja nijiandae niende kazini"

"Poa dia mwaaaah" Ibra alisema

"Mmmwahh pia" Hellena alijibu mapigo

"Nakupenda" Ibra alisema ili kumpima imani binti k**a ameshaelewa mchongo

"Nakupenda pia" Alijibu

Kheeeeeee! Haji alipiga kelele mithili ya Nzengue yule anacheza vichekesho Seany TV halafu akashika kichwa na kuzunguka sebuleni anawaza amfanye nini binti.

Hellena alikata simu na kutoka chumbani akiwa anatabasamu, alipofika sebuleni alimkuta Haji amefura hasira

"Ulikuwa unaongea na nani?" aliuliza

"Nilikuwa naongea Ibra"

"Wewe mwanamke unanicheat?"

"Nakucheat vipi? Si uliniambia huwezi kuwa na mimi hunitaki? Si ulinishauri nimkubalie?" Aliuliza mtoto wa k**e

"Hapana, mimi ndo mume wako nitakupiga nikikuona naye tena" Alisema Haji kwa hasira "Futa namba yake" Alisema Haji huku akimshika binti"

"Usinishike" binti alijinasua na kuelekea bafuni

Ghafla mama Sophie alitokea lakini alikuta vurugu mechi limeshaisha "Vipi Haji mbona k**a ugomvi?"

"Hapana mama" Haji aliongea kwa hasira na kutoka nje, hajui amepatwa na nini ila hataki msichana awe na mahusiano na mtu mwingine kabisa

Kufika nje tu hivi, Ibra naye akampigia Haji anataka ampe taarifa kwamba mambo yameshakaa mshahazari. Kwa hasira Haji alipokea
"Kaka kaka, mtoto kashaku....." kabla hajamaliza sentensi Haji alimtukana

"We mbwa.....achana na mke wangu" Haji alisema kwa hasira......ITAENDELEA
USIKOSE NAMBA 10

SAPOTI NI NDOGO. K**A STORY SIO KALI, COMMENT HAPO CHINI TUANZE NYINGINE MPYA

ZISIPOFIKA LIKES 450 HATUTAWEZA KUENDELEA

SEHEMU YA 22Simulizi NA Michezo Tz. Baba akajibu “Hakuna anayeumwa wala msiba ila ninataka uje kuna mambo ya kujadili ka...
04/06/2026

SEHEMU YA 22
Simulizi NA Michezo Tz.

Baba akajibu “Hakuna anayeumwa wala msiba ila ninataka uje kuna mambo ya kujadili kati yako wewe, na sisi wazazi wako”
Nikaguna “Mh mbona ghafla”
Baba akasema “Nafikiri nauli inatosha kujia hiyo”
Nikasema “Sawa baba nitakutaarifu
Baba alinitakia usiku mwema, halafu alikata simu kisha nikaiweka simu mezani kwa nguvu na kuegemeza kichwa changu kwenye mkono niliouegesha mezani
JF akaniuliza “Vipi kuna shida?”
Nikamuambia “Baba anataka niende nyumbani kesho, au jumapili kwani ndiye kanitumia ile pesa k**a nauli
JF akashangaa na kuniuliza “Kuna shida nyumbani?”
Nikamjibu “Hakuna shida yoyote nyumbani, ila kuna vitu wanataka kudiscuss na mimi”
JF akaniuli “Huwa baba yako anafanya kazi gani?”
Nikamuambia “Baba yangu anapambana na kilimo” kichwani nilimficha kwani pia baba yangu ni mtaalam wa tiba za asili yaani mganga wa kienyeji.
Basi JF akaniambia “Nenda tu nyumbani ukawasikilize, pengine wanaweza kukupa mawazo yatayofanya maisha yako yakawa bora zaidi….ila babe…” alisema nikamsikiliza kwa makini k**alizia “Ukienda huko kumbuka kwamba ninakusubiri mwishoni mwa mwezi ujao tunafunga ndoa”
Nikamuambia “Ninalo hilo akilini wala hauna haja ya kunikumbusha ila tu uwe mkweli”
Akaniambia “Siwezi kukudanganya kwani wewe unanipa amani sana ya moyo”
Nikamuuliza “Kweli?” akajibu kwa kutikisa kichwa chake.

Basi nilisoma message za dada yangu nikakuta kumbe aliniambia mzee ananihitaji nyumbani kesho yake, lakini nilikuwa sijazifungua, nikamtumia baba ujumbe
“Ninaomba nije jumapili baba”
Mzee akanijibu “Hamna shaka”
*
Baadaye tulipata chakula na mimi niliomba kuoga kisha nilale maana nilikuwa nimechoka, ukijumlisha jana hatukulala vizuri kwani tulikuwa kwenye 🤦‍♀️🤦‍♀️ nilijikuta nataka kulala mapema, nikaenda chumbani kuna master nikaoga kisha nikaenda kulala zangu
*
Niliamka asubuhi na mapema tukaenda kumuona mama, round hii alikuwa anaendesha JF mwenyewe, tukamchukua mama maana aliruhusiwa, kisha tulirudi naye nyumbani.
Tukaanza kushikirikiana mimi na Maridhiya kufanya kazi za pale nyumbani, halafu baadaye tulitoka na JF akawa ananitembeza nipajue mjini kwao kidogo, tulipofika mahali akaniambia
“Kesho unaondoka na ndege asubuhi sana, lakini vile vile, sitamani sana tukae huku siku mbili nzima sijaiona”
Nilitabasamu na kumuambia “Unapendaa”
Akasema “Ya kwako tu ndo naipenda, ni tamu halafu unajua kuitoa yaani k**a vile unanisusia niifanye navyotaka”
Nikamuambia “Una vituko”
Akasema “Hapa jioni unaaga k**a vile ndo unasafiri, tunaenda mahali, nakuadhibu vikali, kisha saa saba nakuacha ulale narudi nyumbani, asubuhi nitakufuata nikupeleke uwanja wa ndege okay?”
Nikajibu “Okay Babe”
Basi tulienda kukata tiketi, kisha tulirudi nyumbani, tukakaa mpaka mida ya saa 11 jioni, akatoa taarifa naaga, nikasogea kwa yule mama, nikamuambia ninaondoka na nitarudi kipindi kingine
Mama akanishika mkono na kuniambia “Mungu aliye hai akutangulie” kisha akakohoa na kuendelea “Ukirudi kipindi kingine usije hivi, njoo ukiwa ni mke halali sawa ee?”
Nikacheka kwa aibu na kusema “Mi niko tayari ni kijana wako tu bado hajaamua, akiamua tu utaniona hapa”
Mama akasema “Nitamshauri, asiache mwanamke mzuri k**a wewe”
JF anacheka tu na mimi nacheka, tukamuaga mama na watu wengine wote halafu tukatoka na gari, hapo sio kwamba tunaenda safari, bali tunaenda hotelini tukaagane 🙈🙈🙈🙈
Tukaenda mpaka mji mmoja wa kishua, unajua kuna yale maeneo kila mkoa, unakuta wanakaa matajiri tupu, sasa hapo ndipo nilipopelekwa, mpaka ikabidi nimpe maua yake
Nikamuambia “Tangu niwe na wewe umenifanya niyajue maisha ya kifahari sana, sitokuangusha, kila mwaka nakuzalia madume, nioe haraka”
Akasema “Cha kushangaza tumeku….lana mara mbili tu siku zote”
Nikacheka huku nikiingia ndani ya chumba cha hoteli hiyo ya kifahari, akaniuliza “Tuagize msosi saa hizi au tusubiri kidogo”
Nikamuambia “chakula baadaye kidogo” huku nikiufunga mlango na kumsogelea nikamkumbatia halafu niko mdomoni mwake ni juisi ya mahaba tupu
Sijavua hata nguo moja, tushadondoka kitandani, sikujua saa ngapi kafungua suruali na kutoa dubwasha, sikujua saa ngapi kasogeza kofuli pembeni na kuiweka.
Nilikuja shtuka nikipiga kelele, baada ya msuguano wa kwanza tu na nilipojitega vizuri hivi, breake ilikuwa kengele, yote nyingine ndani
Nikamuambia “Subiri tuvue kwanzaa”
Akasema kwa hiyo nichomoe?”
Sikutaka kumjibu maana sikutaka ichomoke mwenzangu, nilichokifanya ni kumkumbatia tu na kumpa juisi ya maha….baaa
ITAENDELEEEEAAAAAAAAAAAAAA

JAMANI BOSS FRIENDS WHO LIKE SIMULIZI NA MICHEZO 2022 SEHEMU YA 21JF alinitazama kwa mshangao na kuniuliza “Unaongelea n...
03/06/2026

JAMANI BOSS
FRIENDS WHO LIKE SIMULIZI NA MICHEZO 2022

SEHEMU YA 21
JF alinitazama kwa mshangao na kuniuliza “Unaongelea nini? Hayo si ni mambo ya kuzungumza mimi na wewe tukiwa sehemu tulivu?”
Nilikaa kimya ila nilishaona kizingiti kikubwa tena mbele yangu, Mungu wa muhimu, Mume wa muhimu, na mimba tayari ninayo halafu sasa kibaya zaidi yeye anaeleweka kiuchumi mno.

Tulifika nyumbani, kulikuwa na nyumba ya ghorofa moja, tukaingia ndani, kulikuwa na kijana mmoja na msichana mmoja humo ndani, ambao walikuwa ni wafanyakazi, pia kulikuwa na mtoto ambaye ni mdogo sana, alipomuona JF alimrukia “Daddy” alikuwa ni mtoto wake, JF akambema
Mtoto akamuuliza “Where are the gifts you promised me”
JF akajibu “Oh My God, I will buy them tomorrow, forgive me my daughter”
Akachukua noti ya elfu tano na kumpa “Go and buy something for yourself”
Mtoto alifurahi “Thank you”
JF akamuweka chini na kumuacha, mtoto akakimbilia chumbani nafikiri kwa ajili ya kwenda kuficha pesa yake
Maridhiya akamuambia yule mfanyakazi wa k**e
“Ulishaandaa vitu vya kupika?”
Akajibu “Ndiyo kila kitu kiko tayari
Maridhiya alipita moja kwa moja mpaka jikoni, halafu JF alinishika mkono na kupanda pamoja mpaka upstairs yaani gorofani.
Kulikuwa na sehemu ya kukaa pia, ambapo tulikaa tukaanza kuongea, nikamuuliza
“Wewe unalalaga huku?”
Akajibu “Chumba changu hiki cha kulia, na cha kushoto huko ni cha maridhiya, sasa wewe utalala na maridhiya huku juu sawa?”
Nikamtania “Nikajua nitalala na wewe humu”
Akasema “Ah ah haitapendezaaa…”
Basi akanieleza nikamuuliza kile kitu “Mimi sina amani, nimepatwa na hofu juu ya dini”
Akanishika mkono na kunivuta nikainuka akanipeleka chumbani kwake, ile tumeingia ndani chumba kimepangwa vyema, nafikiri ni maridhiya baada ya kujua kuna ugeni, akaniambia embu fungua kabati hapo”
Nikafungua kabati la nguo, nilipochungulia ndani, nilikutana na nguo tofauti tofauti, kushoto kukiwa na suti na kulia kulikuwa na kanzu, zingine zimening’inizwa na zingine zimekunjwa vyema
Nikamuuliza “Unamaanisha nini?”
Akanijibu “I am a Muslim alhamdulillah”
Nikasema “Kweli??”
Akasema “Yeah, kwani hukujua….huoni hata tukikutana nakusisitiza kujisitiri”
Nikamuuliza “Mbona mama yako ametuombea kikristo”
JF akasema, mama yangu alikuwa mkristo akaolewa na baba muislam, baba alifariki, lakini pia mama alikuwa anasumbuliwa sana na vitu vingi, magonjwa majini na kadhalika, akasema yeye anataka kurudi kwe Yesu wake ndiko anahisi alikuwa anaipata amani
Sasa mtu mzima umpangie dini? Ndiyo akarudi katika dini yake, lakini alitusisitiza sisi tuwe na maamuzi yetu wenyewe, hivyo hakutulazimisha sisi kumfuata, halafu pia sisi tumelelewa katika njia mbili kwa hiyo tunaishi neutral si unaonaga namna navyokaa ee”
Nikasema “Ndiyo”
Akasema “sisi ni wakrislam, yaani dini zote mbili tumezishika ila mimi natambulika k**a muislam kamili wala usiwe na shaka”
Nilitabasamu kwa furaha na kumsogelea nikamkumbatia na kusema “Thank you babe” halafu tukakiss mdomoni.

Sasa shida yule mwanaume nilikuwa nikimbusu tu mdomoni hivi, alikuwa ananing’ang’ania anataka ulimi, hee akanishika kiuno na kunisogeza vizuri ile tunataka kukiss, nikasikia mlango umegongwa
“Bro” alisema maridhiya
“Naam” aliitika huku akiniachia
“Nimewawekea vinywaji hapa nje, mkitoka mjinafasi”
JF akajibu “Swadakta” halafu akaniambia “Tutoke sasa…. Si usharidhika?”
Tukatoka mpaka tukafika sebuleni kulikuwa na Wine, na Juice, akaniambia “Tunywe juisi…..halafu pia, sasa umeridhika kuwa mke wangu?”
Nikamjibu “Kesho asubuhi na mapema, ukitaka tufunge ndoa niko tayari”
Akaniambia “Come oon….wewe ni malkia wangu siwezi kukuoa kienyeji nataka tukafanye bonge la party….halafu honeymoon tunaenda Dubaiiiii”
Nikasema “Wow, babe fanya haraka, halafu si unajua haitakiwi mimba ikuwe ee”
Akasema “As soon as this month ends”
Nikajua mambo yanaenda kuwa safi baada ya muda mfupi, nikamuambia “I can’t wait, naona ni mbali sana…..”
Nilitoa simu yangu, nikafungua messages za rose, nikamuambia JF naomba unisaidie kusoma hizi message halafu uniambie nimjibu vipi”
Basi JF alipokea akaanza kuzisoma, akaniuliza “Huyu ni Rose wa pale ofisini?”
Nikamuambia “Ndiyo”
Akasema “Huyu msichana ni k**a mchawi hivi, yaani ana wivu sana na mimi”
Nikamuuliza “Ina maana mlishawahi kudate?”
Akasema “Ni kweli tulishawahi kuwa naye, ila baadaye nilimfumania na mwanaume mwingine, nikataka kumfukuza kazi akasema nimsamehe hata k**a simtaki tena kimapenzi basi nimuache afanye kazi, sasa nimekaa pale ameona sina time na mwanamke umekuja wewe type yangu, anaanza kuona wivu wa nini? Saa nyingine simuamini na ndiyo maana nimemfukuza pale maana mwishowe anaweza kuleta matatizo kwenye kampuni na kuichafua”
Nilivuta pumzi kisha nikamuuliza “Ulimfuma kweli au ndiyo ulilala naye ukamtelekeza”
Akaniambia “Siwezi kudanganya” huku akinipatia simu lakini, ghafla ukaingia ujumbe akausoma na kuniambia “Kuna mtu katuma pesa hapa sijajua ni nani”
Nikashangaa “Pesa?” huku nikiipokea ile simu, kwani sikuwa na miadi ya mtu yeyote kunitumia pesa, nilipoangalia ni shilingi elfu sabini na tano, na imetoka kwa wakala
Nikamuambia “Huyu atakuwa labda amekosea, k**a amekosea atarudisha k**a hajakosea atanipigia simu anielekeze ni ya nini”
Nikaweka simu mezani, JF akaniuliza “Una uhakika hujui ni …..” kabla hajamaliza sentensi, simu yangu iliita, na wote tuliitazama alikuwa ananipigia baba
Nikasema “Baba ananipigia”
JF akanitazama tu mi nasubiri anipe ruhusa ya kupokea, lakini alikaa kimya nikamuuliza “Nipokee?”
Akasema “Ndiyo pokea”
Nikapokea na kusema “Asalam alaykum”
Baba akasema “Walaikum salam Raya unaendeleaje”
Nikasema “Niko salama sana baba yangu…nyie je?”
Akajibu baba “Tuko salama kabisa….aaah mh kuna pesa nimekutumia kutoka kwa wakala Juma Kaziaka umeiona?”
Nikasema “Aaah kumbe ni wewe baba umetuma?”
Baba akajibu “Ndiyo ni mimi….ukajua umeokota embe chini ya mnazi ee”
Nikasema “Nilishangaa” huku nikichekea
Baba akasema “Pole sana, ila nimekutumia ni nauli hiyo, unapaswa ujiandae, kesho jumamosi au kesho kutwa jumapili uje nyumbani, kuna mambo mimi na mama yako tunataka tujadili na wewe”
Nikashtuka “Kuna shida nyumbani baba?”
JE KUNA NINI NYUMBANI? USIKOSE SEHEMU YA 22

Simulizi NA Michezo Tz. FRIENDS WHO LIKE SIMULIZI NA MICHEZO 2022 ISOMWE NA WAKUBWA TU 🔞 🔞 🔞 🔞 🔞 🔞 SEHEMU YA 16Vistari v...
01/06/2026

Simulizi NA Michezo Tz.
FRIENDS WHO LIKE SIMULIZI NA MICHEZO 2022
ISOMWE NA WAKUBWA TU 🔞 🔞 🔞 🔞 🔞 🔞

SEHEMU YA 16
Vistari viwili naviona, vyekundu vikimaanisha nina ujauzito, nilitetemeka nachukua kile kipimo nakitazama kwa makini huku nikisema
“Noo….nooo isiwe kweli mbona k**a nilikuwa siku salama jamani”
Nikachukua simu yangu ya zamani na kuangalia kwenye kalenda nione k**a nilikosea au la, ile nimeangalia hivi nikagundua kweli nilijichanganya sikuwa siku salama hata kidogo wakati natumikia adhabu ya JF.
Niliketi nikainamisha kichwa nikakishikilia kwa mkono, kisha nikasema
“JF sasa tulifanya nini hiki? Ungekuwepo basi ningekuzalia ila k**a hautakuwepo karibu yangu tena basi ujue sitaweza kudhalilika na hii mimba”
Nilikuwa nakumbukia jinsi shuleni nilivyokuwa na mashauzi, chuoni nilivyokuwa nawaponda wanawake waliozaa bila ndoa, nikajikuta kichwa kinaniuma sijui nilie au nifanye nini
Ubaya mmoja, mwenye mimba yake wala sijui k**a ni mzima au amekufa, sikutamani kumuambia mtu yeyote, nilitaka iwe siri yangu mimi na daktari ambaye atanipa dawa ya kutolea mimba ile

Nilijisemea “Hii dhambi nitakufa nayo peke yangu, Mungu unisamehe lakini sidhani k**a ni wakati sahihi sasa, ninahitaji kujiandaa kisaikolojia, sitamani mtoto wangu aje ateseke, hapana kwa kweli.

Nilipata mawazo, halafu sasa nimechanganya mawili, moja la kutekwa kwa baby, na lingine la kuwa na mimba isiyotarajiwa na ni ya baby pia…nikaanza kujiuliza
“Mwaka huu nina mkosi gani?”
Basi nilioga nikaswaki, kisha nikalala, usingizi unakuja kwa taabu lakini asubuhi ilifanikiwa kufika salama.
*
Nikiwa najiandaa ninawaza, niiwahi mapema ile mimba kabla haijaniletea mambo magumu niitoe, basi nilijiandaa kwenda kazini, nilipokuwa najiandaa nitoke, nilisikia simu inaita, nikaichukua nikaitazama ni yule dereva ambaye alipewa kazi na JF awe ananichukua.

Nikapokea simu kisha nikasema “Hallo Hakeem”
Hakeem akasema “Yes Raya, umeshaamka?”
Nikajibu “Ndiyo, ninatoka nyumbani hapa”
Akasema “Okay, ninakufuata hapo nikupeleke kazini”
Nikashangaa mpaka nikaguna kwanza “Mh”
Akakata simu, na mimi nikaketi kitandani, mara dada yangu akaniita
“We Raya huendi kazini leo?”
Nikasema “Ninaenda, nimeshajiandaa dada”
Akaniuliza “Hivi hizi Habari nazozisikia kuhusu JF vipi ni za kweli?”
Nikamuuliza “Habari zipi?”
Akasema “Kwamba ameuawa”
Yaani dada anazidi kutonesha kidonda changu bila hata mimi kutaka iwe hivyo, nikamuambia “Hata mimi nazisikia k**a wewe”
Dada akaniambia “Lakini huyu dada wa taifa huwa hatoi habari za uongo, huwa ana watu wanampa siri za kule kule ndani”
Nikajikuta namfokea “Dada usiseme hivyo, hujui tu mi najisikiaje, ninaumia nilikuwa najaribu kusahau halafu wewe unanikumbusha tena”
Dada akacheka “Hahahaa….basi pole mdogo wangu, kumbe alikuwa baby wako kweli, nilishasahau”
Wakati sijamjibu, nilipokea simu kutoka kwa dereva Hakeem, akaniambia amekwisha fika pale getini hivyo nitoke
Haraka nilichukua mkoba na kutoka, nilimuaga dada na kuelekea getini, kweli nilikuta gari imepaki, na mimi nilimsalimia hakeem kisha nikapanda gari na tuliondoka kuelekea kazini.

Nilipofika kazini, alinishusha kisha aliondoka zake, lakini nilipogeuka na kutazama nje ya jengo la ofisi, niligundua kuwa kuna hali ya tofauti kidogo,
Wafanyakazi walikuwa wamesimama nje, makundi makundi, halafu waliponiona wote walinigeukia ni k**a kulikuwa na jambo la simanzi ofisini, nilianza kutetemeka na kutaka kuanguka chini nikajikaza nikakusanya pochi yangu mbele chini ya tumbo na mimi nikaanza kuwakagua wote wananitazama kwa mshangao uliokuwa umejaa huzuni.
Nikawasalimu “Good morning guys”
Wakasema
“good morning” huku sauti zao zikipishana kwa sekunde kadhaa kwa kila mmoja
Nilikaa kimya k**a mshamba, niliungana nao pale nje, huku nikijiuliza kipi kilichotokea mpaka wananishangaa mimi,
Mara akatokea madam Chef na kunisogelea kwa karibu akaninong’oneza
“Ujikaze tafadhali….jikaze sana”
Nikajua kile kilichotangazwa siku zilizopita mtandaoni, basi kilikuwa cha kweli, na mimi nilivyokuwa na msongo wa mawazo, nilijikuta naishiwa nguvu na kuketi chini.
Madam alinisogelea akanishika na kuniambia “Jikaze raya”
Nikamuuliza “Boss JF amekufa???”
ITAENDELEAAAAAAA

SEHEMU YA 17

Hakunijibu kitu akawa ananiangalia tu,mimi nikajua kitu kimeshatokea, hivyo na ule uchovu wa kutokulala vyema usiku, plus msongo wa mawazo ya mimba na kadhalika, nikajikuta napoteza fahamu pale pale.
Nimekuja kushtuka, niko juu ya kitanda cha hospitali, wodini nikp peke yangu hakukuwa na wagonjwa wengine, mara nikasikia sauti ya kufoka huko nje ya wodi
“Mmefanya nini? Kwanini mnamtesa mwanamke wangu? Niliwaambia mumpigie makofi aingie halafu nyinyi mnakaa k**a kuna msiba hamjui kwamba ana msogo wa mawazo?
Hii sauti ilikuwa inafoka lakini ilikuwa ya kukwaruza, ikififia fifia k**a mtu anayesumbuliwa na mafua, mara mlango wa hospitali ukafunguliwa, ulipofunguliwa nikitazama sikuamini yule niliyemuona
Ni Boss JF makuja akiwa mzima kabisa, anatembea peke yake, licha ya kuchechemea kidogo huku uso wake ukionekana kukosa nuru na kuwa na wasiwasi, hadi kapungua maskini

Bila kujali dripu niliyotundikiwa, nilijikuta naamka kitandani nataka kushuka niende nikamrukie
“Boss JF” nilisema kwa mshtuko na machozi ya kutokuamini yakinitoka tayari.
Boss alisogea haraka “Baby….usishuke bado unaumwa”
Aliniambia huku akiwahi nilipokuwa kitandani akanishika kwa nguvu lakini alinilaza vizuri chali, tukashikana na kukumbatiana kwa nguvu huku nikizidi kulia na kumuita
“JF……….JF……….umerudi?? Nimekuwa na wasiwasi juu yako….”
Nilimkumbatia huku nikilia yeye akawa ananisugua mgongoni, akisema “Usilie Raya, nimepambana nirudi kwa ajili yako you were the only one, I was always thinking of”
Nikamuambia “Uko salama JF? Siamini…hawajakuumiza?”
Akaniambia “Nitakueleza kila kitu subiri kwanza utoke hapa hospitali, na nimeshangaa mpenzi wangu, nimeota ndoto nayo imekuwa kweli”
Nikauliza “Ndoto gani?”
Akasema “Nimeota ndoto una mimba yangu”
Nilishtuka na kumuachia nikamtazama huku nimeshika mashavu namtazama usoni “Nani kakuambia nina mimba?”
Akatabasamu na kusema “Daktari”
Nilibaki namtazama kwa ukaribu machoni, simaini k**a ni yeye kweli, nikamuambia “Nahisi naota, siamini k**a kweli umerudi, nijitikise ili k**a ni ndoto nishtuke mapema nilie”
Nikaanza kujitikisa akaanza kunicheka na kuniambia “Sitaki nione machozi yako tena, nimeumia sana kukuona unalia kwa sababu yangu….nakuahidi furaha siku zote” akanifuta machozi machoni na na kuniambia “Huu uzuri nitahakikisha hakuna mwingine ambaye atauonja tena”
Nilibaki namtazama tu….sina cha kusema nikamkumbatia tena kwa muda mrefu, huku wapambe wakituangalia na wengine wakirekoda video pale chumbani.
Baada ya muda, aliniachia na aliketi akawa anaangalia simu yake k**a vile alipokea ujumbe Fulani, akaniambia
“Ninatoka, ila baadaye Madam Chef atakuletea simu yako, tutawasiliana okay?”
Nikamuambia “But bado nina maswali mengi ya kukuuliza”
Akajibu “Utaniuliza baadaye usiku wa saa sita tukiwa pamoja” halafu akanishika shavuni na kuniambia “Bye”
Akaondoka huku akiniacha, mwishowe nikajiuliza ‘usiku wa saa sita? Nikiwa naye wapi?”
Ndipo aliingia madam Chef akiwa amefuatana na dada yangu, dada yangu akaniuliza “Umekumbwa na nini?”
Nikamuambia “Mi sijui”
Walinipatia mkoba kisha nikatoa simu na kutazama, ni saa 12 jioni, natakiwa niondoke pale maana afya yangu ilishakuwa sawa.
Basi nilipewa ruhusa nikaondoka nikifuatana na dada yangu, lakini aliyetupeleka ni yule dereva hakeem, halafu mimi nilipofika nilijilaza kitandani kwangu, halafu nikamtext JF WhatsApp,
“JF” nikaona imedeliver kwa tick mbili, nikamuongeza ya pili “Nisamehe k**a nakusumbua, ila ninakutaarifu kwamba niko nyumbani”
Alifungua zile message kisha akajibu “Okay, jiandae, ninataka tutoke tuende tukaongee”
Na mimi kwa kuwa nilitaka kujua kilichomtokea, basi, nilimuambia “Sawa najiandaa, ila sitalala huko”
Akaniambia “Tutalala wote, nataka tujadili mambo mengi, basi muda hautatosha na wa kurudi”
Nikasema “mmmh…kuhusu dada je?”
Akaniambia “Ngoja nimpigie”
Nikasema “Okay”
Niliendelea kukaa na kumshukuru Mungu, nikisema “Asante kwa kuwa amerudi salama”

Baada ya mda nilitoka na kuelekea chooni, nilimuona dada yangu akiwa anashughulika na mboga hapo hapo sebuleni, huku mtoto wake akifanya kazi za shuleni, nikaelekea tu chooni, humo humo ni bafuni pia, nikiwa huko nikaamua nioge moja kwa moja
Nikiwa naoga nikasikia amepokea simu na kuanza kuongea, kwa kuwa kulikuwa mbali sikuweza kusikia maongezi yake, lakini baada ya kutoka bafuni nilipita sikumuona sebuleni bali kwa mbali nilisikia sauti nje ikiongea, nikaenda zangu chumbani nikaenda kuvaa nguo na kutoka.

Nilipotoka nikasikia akiongea kwa sauti ndogo sana, na mimi nikasogea karibia na mlangoni kisha nikasikiliza
Nilisikia akiongea “Pole kwa majanga yaliyokukuta niliogopa sana” akasubiri ajibiwe upande wa pili nikajua kabisa anaongea na JF akaendelea kusema “Inaniuma sana kuitana shimeji na wewe…………..JF unajua namna nilivyowahi kukupenda na nimekusumbua mda mrefu ila umemaua kuja kunikomoa ukambeba mdogo wangu kweli? Sio haki kabisa”

Niliposikia hivyo nilianza kuondoka kwa kunyata, lakini nimefika kwenye kona tu dada akamuambia kwa sauti aliyoipunguza kidogo, akasema “JF k**a utamuoa mdogo wangu sawa, lakini naomba hata niionje ya kwako mara moja tu maana niliwahi sikia mama watoto wako akiisifia, yaani unaenda kuwa shemeji sijaiona hata kwa macho tu jamani?”
Hakika niliogopa nikasema “Khee,….kumbe dada anataka naye aionje…”

SEHEMU YA 18
Nilirudi chumbani kwangu nikajifungia halafu nikaketi kitandani bado ninawaza kile nilichosikia, sasa kuna nafsi moja ikaniambia
“K**a huyo mwanaume akikuoa, lazima atakuwa na ukaribu wa hali ya juu yeye na dada yako, so itakuwa rahisi sana dada kumshawishi mpaka akalala naye”
Nikajisemea “Wanaume walivyo wadhaifu kwenye maumbile yao, labda anipeleke mbali, sitaki ushemeji shemeji, dada yangu namjua vizuri”
Sikuishia hapo, nilimtumia message JF na kumuuliza “Umeshaongea na dada? Maana niko mdhaifu naweza kusinzia hapa”
Akaniambia “Nimeshaongea naye, jiandae ukishamaliza niambie, hakeem atakufuata”
Nikamuambia “Nimeshaoga hapa ni kuvaa tu”
Akasema “Okay, jisitiri vyema Hakeem asije akakutamani bure”
Nikatuma emoji za kucheka, kisha nikaanza kujiandaa, baada ya dakika kadhaa nikamuambia nipo tayari.

Hakeem alinifuata akanichukua akanipeleka mpaka kwenye hoteli moja ya kifaharai, pale usiku mmoja ilikuwa laki tatu kulala, ilikuwa hoteli ya kitajiri sana.
Nikamuuliza JF kwanini umeamua kunileta kwenye hoteli ya gharama hivi, si tungeenda tu nyumbani”
Akanijibu “Sasa laki tatu ni hela?”
Nikamuambia “Mh…kwetu sisi ni hela”
Akatabasamu na kuniambia “Nimekumiss sana, kisha nilikuwa sitaki tukae sehemu yenye mikelele kelele”
Alinisogelea kwa ukaribu kisha akanitazama machoni na kuniambia “Ukinitazma unaona nini?”
Nikamuambia “Ninaona uso wako hauna nuru, sijui kilichokutokea huko”
JF akaniambia “Nitakuelezea tukishakula, muda tukiwa tumelala, na ujue tunalala bila nguo ninahitaji unikande kande sehemu zinazouma, pia nina majeraha kidogo mwilini”
Nikamuambia “Pole mume wangu”
Alitabasamu na kuniambia “Asante mke wangu kipenzi”
Nilizidi kumtazama nikiwa napumua kwa kasi, nikamuuliza “JF una uhakika nina mimba?”
Akaniambia “Niliambiwa na Madam Chef, baadaye nikaambiwa tena na daktari”
Nikamuambia “Nilijua ninayo tangu jana, nilipata wasiwasi, nilihisi k**a hautorudi mtoto wako nitamuambia nini….lakini pia nina hofu”
Akasema “Hofu juu yangu? Hapana usiwe na wasiwasi nitakuwa salama”
Nikamuambia “Licha ya hofu juu yako, lakini najua dada yangu anakupenda, unajua hata ukinioa ukiwa na ukaribu naye itakuwa rahisi kukushawishi?”
Aliniachia na kuniambia “Unaniona mimi mrahisi sana kushawishika ee?”
Nikamjibu “Sio hivyo, ila dada yangu simuamini, ni mcharuko sana”
Akaniambia “ingekuwa ni kunishawishi angeshanishawishi tangu muda mrefu sana, ameniomba namba mara nyingi sana facebook, tangu kipindi ninaishi na mwanamke lakini hakuwahi hata siku moja kunipata, leo hii ndiyo anipate? Hapana siwezi kufanya hivyo”
Nikamuuliza “Kweli haitatokea?”
Akajibu “Kamwe”
Chakula kililetwa pale hotelini, tukawa tunakula na kulishana taratibu huku tunataniana, k**a saa na nusu hivi taratibu, nasikia raha nacheka cheka tu.
Mara achukue nyama k**a anatakak unilisha, anaizungusha zungusha mdomoni kwangu na kuirudisha anakula mwenyewe, na mimi najifanya nimesusa, na kununa “Sitakii….sitakiii”
Tuliendelea hivyo kwa kipindi kirefu, hata chakula hatukumaliza tulienda chumbani, akaniambia “Tukaoge au unanifanyia massage”
Nikamuambia “Nakufanyia kwanza massage…halafu nikamkumbatia na kukilaza kichwa changu mgongoni mwake nikamuuliza “Wait, kwanza kwani leo unaniadhibu?”
Akatoa sauti ya kuunguruma “Hapana sitaweza, bado mwili wangu haujakak**aa vizuri, wewe nikande tu”
Sikujibu kitu nililala mgongoni mwake huku mikono nimeizungusha nachezea kifua chake maana shati alilifungua vishikizo akawa ametulia kimya.
Dakika moja mbele aligeuka na kunishika kwa ukaribu akaniambia “Naweza kuupata ulimi wako?”
Sikumjibu niliweka mdomo karibu aufanye anachotaka yeye, sasa tumekumbatiana huku tunamung’unyana ndimi hivi nasikia imemsimama inanigusa kwenye kitovu changu, nikazidi kupagawa na kumuambia
“Sidhani k**a hautoniadhibu, mimi sitokubali ninahitaji kuadhibiwa kisawa sawa”
Akaniambia “Kumbuka unaumwa, na umetoka hospitali”
Akasema “Haijalishi, k**a nawashwa ugonjwa kidogo tu ndo uninyime kukunwa?”
Nikaushika mkanda wa suruali yake na kuufungua halafu kiganja changu nikakizamisha ndani ya suruali, nikaishika, a weee…..yeye nani?
Nikamlaza taratibu kitandani halafu nikaja kwa juu, nikamkumbatia kwa nguvu na kuanza kulalamika “I miss you” huku nikimpapasa mwilini, mara nikaanza kusikia akilalamika
“Hapo panauma, walinipiga kidogo”
Nikasema nikushike wapi usiumie, nitakukanda baada ya kufika kileleni”
Akacheka sana na kuniambia “Unapenda!”
Nikamuambia “Huoni hadi dada yangu anaitamani? Nimesikia akikuambia anataka aionje, sasa nishughulikie hadi nishindwe kutembea”
Akanigeuza akanilaza chali halafu akaanza kuvua nguo zake, akabaki na bo..xer tu, mimi akaanza kunikoboa nguo zangu, hakuniacha hata na kofuli, nimebaki namtazama tu kwa sababu siamini k**a tumeonana akiwa hai tena.

Alinikumbatia tukaanzak kubiringitana kitandani, midomo imeshikana, tunapigana mabusu, hata nikimpapasa halalmiki tena, mwishowe nikamgeuza na kuhakikisha nakaa juu yake, nikamuambia
“Kwa uwa mwili wako una maumivu, ngoja nijishughulikie peke yangu”
Nikaishusha kidogo bo….xer yake, kisha nikaishika maiki, na kuitegesha nanilii yangu juu yake nikaanza kujisugulisha ili kuloane vizuri, ile nimeiweka hivi, ikaingia taratibu, nilipagawa nikamkumbatia huku kiuno nikikifanya taratiiiibu kuhakikisha Napata burudan.

Nilimlalia halafu tukawa tunapeana raha huku tukipiga story
“Jamani JF wewe ya kwako ni tamu sana”
Akasema “Una uhakika utaipa raha kila maraha?”
Nikamjibu “Sitathubutu kukunyima….” Nilisema huku raha zikinikolea na kujikuta naanza kupiga mikelele
Alinigeuza, acha anishughulikie, utafikiri si yeye ametoka kutekwa na watu wasiojulikana

Alipomaliza alijilaza kando akawa anahema kwa nguvu, nikashuka na kwenda maliwatoni kisha nikarudi nikiwa nimejifunga taulo nikajilaza kando yake na kumuita
“Babe”
Akakaa kimya nikamtazama anaangalia darini nikainuka na kujilaza kifuani mwake nikamuita “Boss JF”
Akasema “Mi boss wako ila unanipa hadi vya ziada”
Nikamuambia “Sijajuta kuajiriwa, ila usije ukanisaliti nitakufa, kina rose watanisema sana”
Akaniambia “Hivi rose ni nani?”
Nikamjibu, “si ni secretary wako?”
Akaniambia “Secretary anaitwa Jane….”
Nikainua uso na kumtazama nikijiuliza amepoteza kumbukumbu au vipi, nikawa namshangaa na kumuuliza “Jane?”
Akasema “Yeah rose nimeshamsimamisha kazi”
Nilishangaa kidogo maana asubuhi Rose alikuwepo ofisini,
Akaniambia “Muhasibu mwa kampuni pia anaitwa John”
Nikashangaa, muhasibu kivipi maana mimi ndiye niliyekuwa muhasibu pale ofisini, nikamuuliza
“Sasa boss, mimi si ndo muhasibu, au hukumbuki vitu vingine”
Akanivuta na kunikumbatia kisha akaniambia kwa umakini
“Siwezi kusahau kirahisi hivyo, ila sikiliza wewe ni mwanamke wangu, siwezi kukuacha pale ofisini watakuletea matatizo, nimeamua nikuhamishie sehemu nyingine, kuna mahali nitakupeleka kesho”

Ghafla simu ya boss iliita, ilikuwa mezani, nikaenda kumchukulia na kumpatia jina la mpigaji aliandika My First Love💘, akashtuka na kusita “Huyu ananipigia saa hizi kuna nini?”
Nikakaa kimya, mimi namba yangu imeandikwa Rayuni, bila hata emoji, lakini aliyepiga anaitwa My First love tena ikifuatiwa na emoji ya mshale unachoma moyo
Nikatulia kimya huku moyo unanigonga paah, nikaona amemute simu na kuiweka pembeni
Nikamuuliza kwa hasira “Mbona hupokei simu???”
JE NI NANI HUYO ALIPIGA SIMU? 075423..53
USIKOSE SEHEMU YA 19

SEHEMU YA 19
JF alinitazama kwa makini usoni akaniambia “usiku huu ni wangu na wewe, huyu Ana story nyingi”
Nilijisikia vibaya nikajua basi mimi natumika halafu huyo first lover wake ndo anayelindwa zaidi, simu ikaite tena anapiga yule yule.
JF akaitazama bila kusema chochote
Nikasema “Pokea simu JF unanifanya nisikuamini tena”
JF alitabasamu kisha akaipokea ile simu, “Nafanya hivi kukuridhisha tu” halafu akaitia sikioni
“Hallo” alisema, nikasikia sauti tulivu imetoka upande wa mpigaji
“Samahani sana kaka J nimekupigia usiku huu, najua utakuwa umepumzika”
JF alishtuka na kuinuka akaketi akasema “Maridhiya….mbona umeshika simu ya mama usiku huu?”
Upande wa pili ukasema “Mama amepandwa presha tumemuwahisha hospitali….nimesema nikutaarifu”
JF alishtuka sana, akaketi vizuri na kusema “Yuko wapi, mpe simu niongee naye”
Maridhiya akajibu “Yuko wodini hatoweza kuongea saa hizi labda asubuhi”
Basi JF alimjia juu akamuambia “Sasa kwanini uchukue simu ya mama unipigie usiku huu? Unajua kwamba unaninyima usingizi? Kwanin unanifanyia hivi mdogo wangu? Hujui nimetoka kwenye matatizo?”
Aliongea kwa uchungu sana “Si ungesubiri asubuhi ndiyo unipe taarifa?”
Maridhiya akajibu “Nisamehe kaka, sikujua”
Mr JF akamuambia “Siku nyingine uwe makini” halafu akakata simu kwa hasira na kuiweka pembeni
Nikamuuliza “Babe kuna nini?”
Akaniambia “Mdogo wangu alichukua simu ya mama ananipigia, sasa bora nisingepokea ananipa wasiwasi, inabidi mara moja kesho niondoke niende mkoani kumuona mama….”
Nikamshika mgongoni na kusema “Pole mpenzi, atakuwa sawa”
Alikaa kimya huku akiwaza, kisha akaniambia “Usiwe na wivu kiasi hicho siwezi kukusaliti”
Nikamuambia “Sorry babe, nilipoona kopa, niliogopa sana si unajua nakupenda sana?”
Akasema “Najua”
Niliendelea kumkagua nikagundua ana majeraha mengi mgongoni, nikamuuliza mamna ilivyokuwa huko mbona walimpiga
Akadai kwamba, alipigwa kidogo wakati akijaribu kujitetea maana walitaka kumsafirisha kwa siri wampeleke mkoa mwingine akakae huko na asipatikane tena
Nikamuambia “Khaaa….kwa kosa kidogo tu lile? Yaani wanasiasa!” nikamuuliza “Lakini mbona usiku ule nilikutumia message na ulijibu kwani walikuteka saa ngapi
Akaniambia “Ile siku sio mimi nilijibu message, ila nilikuwa na wasiwasi kwa sababu, nilijua utakuwa unasubiri nikutaarifu nimefika, basi wale walionichukua niliwaomba sana wajibu message zako ili wakuondoe hofu”

Nilishangaa sana na kusema “Kumbe muda ile walikuwa wameshakuchukua”
Akajibu “Ndiyo, nilikuwa kwenye gari sijui hata wanaponipeleka, ila ukiwa na hela huwa hawakukazii sana, mara nyingi ukiomba maombi wanafanya maana wanajua watapata chochote kitu”
JF aliinuka na kuondoka kwenda bafuni, nikamfuata na tukaanza kuogeshana, tukachezea maji huko bafuni, nikamuambia k**a anaweza basi tujaribu bafuni kuna raha yake
Akasema “Nina stress ila kwako siwezi shindwa kukuchapa kidogo”
Basi likatokea la kutokea, tuliporudi ndani tulilala huku tumekumbatiana mpaka saa 11 tuliamshwa na sauti ya adhana.

Basi JF aliamka na kunisihi nijiandae kwani Hakeem angenifuata muda huo anipeleke nyumbani, akaniambia, baadaye k**a kuna vitu nimesahau ofisini niende nikavichukue halafu nijiandae na

Address

Dodoma
HTTPS://CHAT.WHATSAPP.COM/HAPFTL670VYD1BRSA3OCNB

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi NA Michezo Tz. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Simulizi NA Michezo Tz.:

Share