20/10/2025
SAIDA KAROLI.
Saida Karoli Amezaliwa mkoani Kagera tarehe 4 Aprili 1976 ni mwanamuziki wa nyimbo za asili ya Kihaya Saida alipata elimu ya msingi mwisho darasa la tano tu, ambapo ilibidi aache shule kutokana na kukosa msaada kutoka kwa baba yake ambaye hakuwa anaitazama sana elimu ya mtoto wake, hivyo hakuweza kuendelezwa
Saida alikulia katika kijiji cha Rwongwe mkoani Kagera na kutokana na mila za ukoo wake wasichana walikuwa hawaruhusiwi kushiriki katika shughuli za kimuziki. Hata hivyo kwa vile mama yake alikuwa na kipaji cha muziki alimpa moyo na kumfundisha masuala mbalimbali ya kimuziki
Akiwa na miaka 20 mama yake mzazi alifariki dunia lakini Saida aliendelea kujijengea kipaji chake cha uimbaji na upigaji ngoma
Kukua kwake kimuziki Kipaji cha usanii wa muziki kwa Saida kilijitokeza ghafla baada ya kujikuta akichukuliwa na kudhaminiwa na FM Productions Ltd waliokuwa mkoani Kagera wakitafuta wasanii wenye vipaji kwa ajili ya kuwaendeleza
FM ilimchukua Karoli wiki tatu tu kurekodi nyimbo yake ya kwanza ilotoka na kuish*tua Dar es Salaam mzima pamoja na nchi za jirani za Afrika Mashariki
Albamu yake ya kwanza ilizinduliwa tarehe 2 Septemba mwaka 2001 .
Albamu hiyo ilipata mafanikio makubwa na kupata umaarufu mkubwa sana kwakuwa albamu hiyo ilikuwa na vionjo vingi vya kabila la Kihaya
Albamu hiyo ilijulikana k**a Maria Salome. Japokuwa mashabiki wake waliibatiza jina la Chambua k**a Karanga kutokana na maneno aliokuwa anaimba katika nyimbo ya Maria Salome nyimbo iliobeba jina la Albamu
Albamu hiyo ilifuatiwa na ziara kubwa alizokuwa anafanya katika nchi za jirani k**a vile Burundi , Rwanda,Uganda na Kenya ambapo alipata mafanikio makubwa na Saida kujikuta akibatizwa na kupewa jina la malkia wa nyimbo za asili
Kutokana na uwezo alionao na kipaji katika masuala ya muziki ni rahisi kugundua kuwa
mwanamuziki huyo ana kiwango cha kuweza kupata mashabiki wa muziki wake mbali na
Tanzania na Afrika ya Mashariki.
Facian Muta promota na meneja maarufu miaka ya 20