Uhondo TV

Uhondo TV π—”π—Ÿπ—Ÿ π—‘π—˜π—ͺ𝗦 𝗔𝗑𝗗 π—¨π—£π——π—”π—§π—˜π—¦
Contact usπŸ“© [email protected] /
πŸ“² +255 625662364

11/09/2026

KULA MAISHA KULA MAISHAπŸ˜…πŸ˜…

11/09/2026

Umoja wa Vijana wa Vyama vya Siasa vya Upinzani nchini umemtumia salamu za pole Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia kifo cha mumewe, Marehemu Hafidh Ameir Hassan.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Umoja huo, Masoud Mombo, amesema msiba huo umewakumbusha kuwa tofauti za kisiasa na kiitikadi hazipaswi kuondoa ubinadamu.

Mombo amesema katika kipindi hiki wanamwona Dkt. Samia kwanza k**a mama aliyepoteza mwenza wa maisha, hivyo wametoa pole na kuungana naye katika kipindi hicho kigumu cha maombolezo.

11/09/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi, amezitaka Mamlaka na Taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka za maandalizi ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El NiΓ±o zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba 2026.

Mhe. Ndejembi ametoa agizo hilo Septemba 11, 2026, jijini Dar es Salaam, baada ya kupokea taarifa ya utayari na maandalizi ya Serikali kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania kuhusu uwezekano wa kutokea kwa mvua hizo.

Akizungumza na viongozi pamoja na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, Ofisi ya Waziri Mkuu–TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi na taasisi zilizo chini ya wizara hizo, Makamu wa Rais amesisitiza umuhimu wa taasisi hizo kufanya kazi kwa pamoja na kuchukua hatua za tahadhari mapema.

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt. Ashatu Kijaji leo Septemba 11, 2026 amekabidhi vifaa vya kudhibiti wanyama wakali...
11/09/2026

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe.Dkt. Ashatu Kijaji leo Septemba 11, 2026 amekabidhi vifaa vya kudhibiti wanyama wakali na waharibifu hususan tembo, tukio lililoenda sambamba na ufungaji rasmi wa mafunzo maalum ya marubani wa ndege nyuki (drones) kwa maafisa kutoka Mamlaka za Hifadhi na Taasisi za Wizara.

Katika hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya ofisi za Wizara ya Maliasili na Utalii Mtumba Jijini Dodoma, Waziri Kijaji amekabidhi jumla pikipiki 55 kwa Wakurugenzi wa Halmashauri mbalimbali na Jumuiya za Hifadhi za Jamii za Wanyamapori (WMA) na Ndege Nyuki (Drones ) 40 kwa Makamishna wa Uhifadhi wa TANAPA, TAWA na Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro.

Dkt. Kijaji amesema tukio hilo ni utekelezaji wa mikakati ya matumizi ya teknolojia katika kuimarisha uhifadhi endelevu na ameziagiza Mamlaka zilizopokea vifaa hivyo kuhakikisha mabadiliko chanya na tija ya uwepo wa vifaa hivyo inaonekana kwa kuongeza ufanisi katika shughuli za kuondoa mgongano baina ya wanyamapori wakali na waharibifu na binadamu.

Amesisitiza kuwa vifaa hivyo vitumike kwa kazi zilizokusudiwa na sasa inategemewa kuwa kutokana na uwepo wa teknolojia hii ya matumizi ya ndege nyuki matukio ya wanyama wakali na waharibifu kuingia katika maeneo ya makazi ya wananchi yataanza kudhibitiwa mapema kabla wanyama hao hawajavuka mipaka ya hifadhi na kuingia kwenye makazi ya watu.

Vilevile Waziri Kijaji ameielekeza Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) kuhakikisha usimamizi madhubuti wa Jumuiya za Hifadhi za Jamii za Wanyamapori (WMA) ili ziweze kujisimamia kwa kuwaunganisha na wawekezaji wa uhakika ili waweze kuzalisha mapato ya kutosha, vilevile kupatiwa elimu juu ya matumizi ya mapato wanayokusanya.

Aidha Dkt. Kijaji amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya uhifadhi nchini kwa kutoa fedha zinazoiwezesha Wizara kupiga hatua kubwa katika kudhibiti mwingiliano baina ya wanyamapori wakali na waharibifu na binadamu, amesema Mhe. Rais anatimiza kwa vitendo dhamira yake ya kuacha tabasamu kwa watanzania kwa kuweka nguvu kubwa katika kutatua changamoto zinazowakabili.

11/09/2026

Mwanachama wa CHADEMA na Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano, Odero Charles Odero, ametoa pole kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kufuatia msiba wa kuondokewa na mume wake, huku akimuombea marehemu apumzike mahali pema.

Odero amewataka viongozi wa CHADEMA kutumia kipindi hiki cha msiba kufika na kutoa pole kwa Rais Samia na familia yake, akisisitiza kuwa misiba ni sehemu inayowaunganisha watu na kuwawezesha kusahau tofauti zao.

Amesema kauli ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, ya kuwataka viongozi na wafuasi wa chama hicho kufikisha salamu zake za pole kwa Rais Samia na familia yake inaonesha uungwana, ubinadamu na moyo wa maridhiano.

Odero amekumbusha pia kuwa Rais Samia aliwahi kutuma salamu za pole kwa CHADEMA wakati wa msiba wa mmoja wa waanzilishi wa chama hicho, Edwin Mtei. Hivyo, amewataka viongozi wengine wa CHADEMA, wakiwemo waliopo Zanzibar, kutumia nafasi hiyo kufika na kuhani msiba.

Mbunge wa Jimbo la Mwera Zanzibar na Mwenyekiti wa Mwera Development Foundation Mhe. Suleiman Mohamed Rashid, amekutana ...
11/09/2026

Mbunge wa Jimbo la Mwera Zanzibar na Mwenyekiti wa Mwera Development Foundation Mhe. Suleiman Mohamed Rashid, amekutana na viongozi wa kambi za wanafunzi kutoka shule sita na kutoa jumla ya Shilingi milioni sita, sawa na Shilingi milioni moja kwa kila shule, kwa ajili ya kusaidia shughuli za kambi hizo za maandalizi ya mitihani.

Kambi hizo zinahusisha wanafunzi wa Kidato cha Nne, Kidato cha Pili na Darasa la Saba, huku shule zilizonufaika zikiwa ni Skuli za Msingi Mtoni Kidatu, Kianga na Regeza Mwendo, pamoja na Skuli za Sekondari Mtoni Kidatu, Kianga na Regeza Mwendo.

Akizungumza wakati wa kukutana na viongozi wa kambi hizo, Mhe. Suleiman amesema mpango huo unalenga kuongeza motisha kwa wanafunzi, kukuza ufaulu na kuboresha mazingira ya kujifunzia ili kuwawezesha kufanya vizuri katika mitihani yao.

β€œLengo ni kuongeza motisha na kukuza ufaulu kwa wanafunzi, pamoja na kuboresha mazingira yao ya kujifunzia,” alisema Mhe. Suleiman.

Amesema uamuzi huo umetokana na kutambua kuwa bado kuna changamoto katika kiwango cha ufaulu, hivyo kuna umuhimu wa kuanza kuwekeza mapema katika elimu, hususan katika mazingira ya kujifunzia na maandalizi ya wanafunzi.

β€œTunajua hali ya ufaulu si nzuri, kwa hiyo tumeamua kufanya hivi ili tupate wanafunzi wenye ufaulu mzuri na pia kuwabaini wale wenye vipaji maalum,” alisema.

Mhe. Suleiman amesema mpango huo haujalenga tu kuongeza ufaulu, bali pia kutoa fursa ya kuwabaini wanafunzi wenye uwezo na vipaji mbalimbali ambao wanaweza kusaidiwa na kuendelezwa zaidi.

Amesema awali aliwahi kukutana na wanafunzi wa Kidato cha Nne waliofanya vizuri katika mitihani na kuwapatia zawadi, jambo lililomfanya kutafakari umuhimu wa kuwekeza katika ufaulu kabla ya matokeo badala ya kusubiri wanafunzi wafanye vizuri ndipo wapewe motisha.

β€œNiliwahi kukutana na wanafunzi wa Kidato cha Nne ambao walifaulu vizuri na kuwapa zawadi, lakini nikasema tuanze kwenye ufaulu. Tuanze kuboresha mazingira yao ya kujifunzia kuanzia mwanzo,” alisema.

Kwa mujibu wa Mhe. Suleiman, hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za kuweka mazingira yatakayowasaidia wanafunzi kuongeza ari ya kusoma, kujiandaa viz

10/09/2026

Daktari bingwa wa magonjwa ya ndani katika Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila, Conrad Agonza Kahyoza, ameachiwa kwa dhamana ya Shilingi milioni mbili baada ya kufikishwa katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam.

Kahyoza alifikishwa mahak**ani baada ya kuk**atwa na Polisi kwa tuhuma za kumshambulia askari wa Usalama Barabarani mwenye namba F.8886, Andrew, katika eneo la Lugalo.

Tukio hilo linadaiwa kutokea wakati askari huyo alipokuwa akizuia magari yaliyokuwa yakitumia barabara ya huduma (Service Road) kinyume na utaratibu.

10/09/2026

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Dodoma imemwachia huru kwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Melkisedek Kaijage, huku akipewa masharti kadhaa ya kutekeleza.

Kaijage ameachiwa huru leo, Alhamisi, Septemba 10, 2026, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahak**a ya Hakimu Mkazi Dodoma, Denisi Mpelembwa baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Serikali, Jonathan Chuwa, kuiambia mahak**a Serikali haina nia ya kuendelea na mashtaka hayo.

Chuwa ameiomba mahak**a kumwachia huru Kaijage, akieleza uamuzi huo unahusu mashtaka ya ugaidi na uhujumu uchumi yaliyokuwa yakimkabili, ikiwa hana kosa jingine la jinai linalomkabili.

Hata hivyo, kabla ya mahak**a kutoa uamuzi huo, Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Dodoma (RCO) aliwasilisha maombi yaliyoambatanishwa na kiapo, akiiomba mahak**a kumwekea Kaijage masharti ya mwenendo baada ya kuachiwa huru.

Akisoma uamuzi baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mpelembwa amemtaka Kaijage kuwa na wadhamini wawili ambao ni wakazi wa Mkoa wa Dodoma.

Wadhamini hao wanatakiwa kuwa na barua za utambulisho kutoka mamlaka za Serikali zinazotambulika, kusaini dhamana ya maneno ya Sh5 milioni kila mmoja na kuwa na vitambulisho halali.

Mahak**a imemtaka Kaijage kuripoti kwa RCO kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi kwa kipindi cha mwaka mmoja, saa 2:30 asubuhi, bila kukosa.

10/09/2026

KIGWANGALLA AFUNGUKA MAUMIVU YA MAISHA: AJALI, OPERESHENI 8+ NA KUTENGWA BARAZA LA MAWAZIRI

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla, amefunguka kuhusu vipindi mbalimbali vya maumivu na changamoto alivyopitia katika maisha yake, akieleza namna matukio hayo yalivyomfundisha kuwa mvumilivu na kustahimili misukosuko ya maisha.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Kigwangalla amesema hivi karibuni alikuwa karibu na rafiki yake aliyefiwa na baba yake mzazi, ambapo aliamua kumpa faraja kwa kuwa naye karibu, akieleza kuwa hakujua ni maneno gani ambayo yangeweza kumfuta machozi.

Amesema hali hiyo ilimkumbusha ajali aliyopata Agosti 4, 2018, ambapo alieleza kuwa alilia kwa uchungu alipowaona watoto wake kwa mara ya kwanza akiwa hospitalini Muhimbili.

Kigwangalla amesema tukio hilo lilimfundisha kuwa wakati mwingine mtu anayepitia maumivu makubwa hahitaji maneno mengi, bali uwepo wa watu wanaomjali.

Amesema baada ya ajali hiyo alipitia maumivu makali kutokana na kufanyiwa operesheni zaidi ya nane ndani na nje ya nchi, kabla ya baadaye kukabiliana na changamoto nyingine ikiwemo uchaguzi.

β€œMaisha yamenifundisha uvumilivu na ustahimilivu mkubwa sana. Ninaamini kuna sababu kwa kila kitu, na kwamba Mungu anajua zaidi,” amesema Kigwangalla.

Aidha, ameeleza kuwa alipitia maumivu mengine kisiasa baada ya kutokuwepo katika Baraza la Mawaziri, akisema awali aliamini alikuwa amefanya kazi nzuri yenye matokeo makubwa kwa uaminifu, uadilifu na bidii.

Kigwangalla amesema bado anaendelea na simulizi hiyo kuhusu maisha, maumivu na mafunzo aliyoyapata, akihitimisha kwa kusema:

β€œNITAENDELEA…”

10/09/2026

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, ametoa elimu kwa mama wa mapacha watatu, Maridhia Miraji, kuhusu namna bora ya kuwahudumia watoto hao ili waweze kukua vizuri, ikiwemo kuzingatia usafi, lishe na kinga dhidi ya maambukizi.

Dkt. Samizi amemuelekeza mama huyo namna ya kuwahudumia watoto njiti, hususan kuhakikisha wanapata joto la kutosha, lishe sahihi na uangalizi wa karibu, pamoja na kufuatilia afya zao kwa mujibu wa ushauri wa wataalamu wa afya.

Amesema malezi na uangalizi mzuri kwa watoto njiti ni muhimu katika kuhakikisha wanakua salama na kufikia hatua nzuri za ukuaji na maendeleo.

Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uhondo TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share