Uhondo TV

Uhondo TV 𝗔𝗟𝗟 𝗡𝗘𝗪𝗦 𝗔𝗡𝗗 𝗨𝗣𝗗𝗔𝗧𝗘𝗦
Contact us📩 [email protected] /
📲 +255 625662364

Tanzania na Singapore zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji katika jitihada za kuongez...
09/06/2026

Tanzania na Singapore zimekubaliana kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji katika jitihada za kuongeza manufaa kwa wananchi wa nchi hizo mbili, kufuatia mazungumzo yaliyofanyika kati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Jamhuri ya Singapore, Tharman Shanmugaratnam.

Akizungumza leo Jumanne Juni 09, 2026 baada ya kumpokea Rais Tharman aliyewasili nchini kwa ziara ya kitaifa, Rais Samia amesema viongozi hao wamejadili namna ya kuufanya ushirikiano kati ya Tanzania na Singapore kuwa wenye tija zaidi na kutoa matokeo yanayoonekana katika maendeleo ya mataifa hayo mawili.

Rais Samia amesema pamoja na ukuaji wa biashara kati ya nchi hizo, bado kiwango kilichofikiwa hakijakidhi matarajio ya pande zote mbili.

Amebainisha kuwa kwa sasa biashara kati ya Tanzania na Singapore inafikia dola za Marekani milioni 299 huku Singapore ikiwa imewekeza kupitia miradi 36 nchini Tanzania.

Amesema makubaliano yaliyofikiwa yanalenga kuongeza biashara, kuvutia uwekezaji zaidi na kufungua fursa mpya za ushirikiano katika sekta mbalimbali za uchumi.

Kwa upande wa ushirikiano wa kidiplomasia, Rais Samia amesema Tanzania imeiomba Singapore kufungua ubalozi wake nchini ili kuimarisha zaidi mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi kati ya mataifa hayo.

Aidha, amesema nchi hizo mbili zimeanzisha mfumo wa mashauriano ya mara kwa mara ambao utasaidia kuratibu mikakati ya maendeleo na kushughulikia changamoto zinazoweza kujitokeza katika utekelezaji wa maeneo ya ushirikiano.

Katika sekta ya kilimo, Rais Samia amesema Tanzania imeonesha nia ya kushirikiana na Singapore katika mpango wa kuimarisha usalama wa chakula, hatua inayolenga kuongeza fursa za biashara ya mazao ya chakula na kuhakikisha upatikanaji wa chakula kwa uhakika katika nchi zote mbili.

Rais Samia pia amesisitiza umuhimu wa vijana katika maendeleo ya taifa, akieleza kuwa Dira ya Taifa 2050 imeweka mkazo mkubwa katika kuwawezesha vijana kwa kuwa ndio watakaobeba dhamana ya uongozi na maendeleo ya nchi katika miaka ijayo.

Ziara ya Rais Tharman Shanmugaratnam imeandika historia mpya katika mahusiano ya Tanzania na Singapore.

09/06/2026

Mradi wa Nickeli wa Kabanga ambao ni miongoni mwa uwekezaji mkubwa wa kimkakati wa madini na viwanda nchini Tanzania, umekaribia kuanza utekelezaji wake hatua ambayo imefikiwa kufuatia kikao cha ngazi ya juu cha kutoa taarifa kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu hatua iliyofikiwa katika majadiliano yanayoendelea na maandalizi ya mradi huo.

Taarifa hiyo iliyowasilishwa Ikulu na Bw. Keith Liddell, Mwanzilishi na Mwenyekiti Mtendaji wa Kabanga Nickel Limited na Lifezone Metals (NYSE: LZM), kwa kushirikiana na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemiah Mchechu, viongozi wote wawili walisisitiza tena nia yao ya kuuendeleza mradi huo kwa namna ambayo italeta faida kubwa zaidi kwa Tanzania.

"Ilikuwa heshima kubwa sana kukutana na Mhe. Rais, amesisitiza tena nia yake thabiti kwenye mradi huu na msaada wake katika kuuendeleza mradi huu chini ya mpango wa utekelezaji uliokubaliwa," alisema Bw. Liddell

Kwa upande wake Msajili wa Hazina Bw. Nehemiah Mchechu aliuweka mradi wa Kabanga k**a mradi wa mabadiliko makubwa na wenye uwezo wa kuchangia kwa kiasi kikubwa katika ukuaji wa viwanda nchini Tanzania, utengenezaji wa fursa mpya za ajira na kuchangia katika ukuaji wa uchumi.

Alisema lengo la Serikali siku zote limekuwa ni kuhakikisha kuwa uchenjuaji wa madini unafanyika nchini Tanzania ili nchi ipate faida kubwa zaidi kutoka kwenye rasilimali zake za madini, akikiri kwamba majadiliano ya mradi mkubwa k**a huu ni mgumu na yanachukua muda, lakini alisema mazungumzo ya hivi karibuni yamesaidia kutatua masuala kadhaa yaliyokuwa bado hayajakamilika na yameleta njia nzuri ya kusonga mbele kwa maslahi ya pande zote mbili.

Bwana Mchechu alibainisha kuwa mradi huo unatarajiwa kuleta faida kubwa kupitia ushiriki wa wazawa (local content), kodi, gawio, uhamishaji wa teknolojia na maendeleo ya viwanda, akisema mradi huu unaobadilisha mwelekeo, pamoja na uwekezaji mwingine wa kimkakati, una uwezo wa kuharakisha mabadiliko ya viwanda nchini Tanzania na malengo ya maendeleo ya muda mrefu.

Mradi wa Kabanga Nickel unatarajiwa kuifanya Tanzania kuwa mzalishaji mkuu katika mnyororo wa usambazaji wa madini muhimu duniani.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani  limetoa wito kwa Jamii kupuuza taarifa ya  madai ya kuokotwa kwa miili ya watu sita iliyo...
09/06/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limetoa wito kwa Jamii kupuuza taarifa ya madai ya kuokotwa kwa miili ya watu sita iliyokuwa ikielea katika Mto Ruvu, Wilaya ya Bagamoyo, Mkoani Pwani, likiwataka pia wanaosambaza taarifa hiyo ya uongo kuacha mara moja kwani zinaleta taharuki kwa jamii.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Kamishna Msaidizi wa Polisi, Salim Morcase katika taarifa yake kwa vyombo vya habari leo Jumanne Juni 09, 2026 amesema Polisi tayari wameanza kushughulikia suala hilo ili kuchunguza na kubaini chanzo chake na kwa atakayebainika, hatua kalu za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

"Kwa mara ya kwanza taarifa hiyo ilisambazwa tarehe 21.12.2016 na kutolewa ufafanuzi na aliyekuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna Robert Boaz. Pia tarehe 13.09.2025 taarifa hiyo ilisambazwa kwenye mitandao ya kijamii na ufafanuzi kuhusu ukweli wa taarifa hiyo ulitolewa tarehe 14.09.2025 na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani. Hata hivyo tarehe 08.06.2026 taarifa hiyo imeendelea kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii japokuwa ufafanuzi ulishatolewa mara mbili kuwa taarifa hiyo sio ya kweli." Imesema Taarifa ya Kamanda Morcase.

Kulingana na Kamanda Morcase, taarifa hizo zimekuwa zikisambazwa zaidi katika mitandao ya Instagram na Facebook.

09/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amempokea rasmi Rais wa Singapore, Tharman Shanmugaratnam, Ikulu jijini Dar es Salaam katika ziara ya kitaifa ya siku tatu nchini.

Mapokezi hayo yalihusisha saluti ya heshima ya mizinga 21 na gwaride la vikosi vya ulinzi. Baada ya mapokezi, viongozi hao wameanza mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano katika biashara, uwekezaji, uchumi wa kidijitali, maendeleo ya bandari, elimu, utalii na miundombinu.

Ziara hiyo pia inatarajiwa kushuhudia utiaji saini wa hati za makubaliano pamoja na ushiriki katika Jukwaa la Biashara na Uwekezaji Tanzania-Singapore.

08/06/2026

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Ally Hapi, amesema madai ya CHADEMA kuwa wakipewa dola watafanya makubwa kwa wananchi hayana msingi, akidai kuwa walipopewa nafasi ya kuongoza majiji na manispaa mbalimbali nchini walishindwa kuleta maendeleo yaliyotarajiwa na badala yake walikumbwa na migogoro pamoja na hoja za ukaguzi zilizobainishwa katika ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani Same mkoani Kilimanjaro, Hapi amesema viongozi wa CHADEMA wameendelea kutoa ahadi kubwa kwa wananchi wakati rekodi zao za uongozi katika maeneo waliyowahi kuongoza zinaonyesha tofauti.
"Hawa watu ni waongo, hawapaswi kuungwa mkono kwa namna yoyote ile. Tuwakatae kwa sababu wanachokisema hakilingani na matendo yao walipokuwa na nafasi za uongozi," alisema Hapi.

Aidha, Hapi amesema CCM, kupitia vijana wa chama hicho, imejipanga kujibu hoja zote zinazotolewa na CHADEMA kwa kutumia takwimu na taarifa sahihi ili kuonyesha kile alichodai kuwa ni upotoshaji unaoenezwa na viongozi wa chama hicho kwa wananchi.

Wananchi wa Wilaya ya Lushoto wamepata fursa mpya ya kunufaika na nishati safi ya kupikia baada ya wilaya hiyo kupokea r...
08/06/2026

Wananchi wa Wilaya ya Lushoto wamepata fursa mpya ya kunufaika na nishati safi ya kupikia baada ya wilaya hiyo kupokea rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi ya kilo sita kwa bei ya ruzuku unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA). Mradi huo umepokelewa na Mkuu wa Wilaya ya Lushoto, Mheshimiwa Zephania Sumaye, kwa niaba ya wananchi wa wilaya hiyo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kuhakikisha nishati safi ya kupikia inawafikia Watanzania wengi zaidi.

Hafla ya mapokezi ya mradi huo imefanyika katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Lushoto na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, maafisa kutoka REA pamoja na wawakilishi wa kampuni ya Manjis Logistics Limited, ambayo imepewa jukumu la kutekeleza mradi huo kwa kushirikiana na REA.

Mradi huo ni miongoni mwa miradi ya kimkakati inayotekelezwa na REA nchini kwa lengo la kuharakisha upatikanaji wa nishati safi na salama kwa wananchi, kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa, pamoja na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuhifadhi mazingira na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Msimamizi wa Mradi kutoka REA, ndugu Abdulrazack Mkomi, alisema kuwa mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia unaolenga kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia.

Alieleza kuwa kupitia mradi huo, REA kwa kushirikiana na Manjis Logistics Limited itasambaza jumla ya mitungi 3,255 ya gesi ya kilo sita kwa wananchi wa Wilaya ya Lushoto kwa bei ya ruzuku ya shilingi 17,500 kwa kila mtungi. Aliongeza kuwa wanufaika wa mpango huo watatakiwa kuwa na Kitambulisho cha Taifa (NIDA) ili kuwezesha utambuzi wa walengwa na kuhakikisha uwazi pamoja na usimamizi bora wa zoezi hilo.

“Madhumuni makubwa ya mradi huu ni kuwapa wananchi fursa ya kupata nishati safi kwa gharama nafuu, kuboresha afya zao na kupunguza athari zinazotokana na matumizi ya nishati zisizo rafiki kwa m

Mbunge wa Jimbo la Kondoa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amekabidhi sare za michezo kwa vija...
08/06/2026

Mbunge wa Jimbo la Kondoa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amekabidhi sare za michezo kwa vijana 200 kutoka shule za msingi na sekondari leo Jumatatu, tarehe 8 Juni 2026. Utoaji huo ni motisha kwa vijana hao wanaojiandaa kushiriki Mashindano ya Michezo ya Shule za Msingi - UMITASHUMTA na UMISSETA ngazi ya Mkoa.

Katika hafla fupi iliyofanyika Kondoa, sare hizo zilikabidhiwa kwa niaba ya Mhe. Mbunge na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi - UVCCM Wilaya ya Kondoa, Ndg. Saidi Issa Ndwata. Makabidhiano hayo yalishuhudiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa, Ndg. Shabani Millao.

Akizungumza na vijana hao, Ndg. Ndwata mewasii waoneshe vipaji vyao kwa uadilifu katika mashindano hayo kwani michezo sasa ni ajira halali. Amesisitiza pia umuhimu wa vijana kuepuka makundi rika yasiyofaa ambayo yanapelekea kujihusisha na vitendo vya kihalifu na kuwafanya wasishiriki katika shughuli za maendeleo.

Akihitimisha salamu za Mbunge, Ndg. Saidi ameeleza kuwa dhamira ya Mhe. Dkt. Ashatu ni kushirikiana na vijana katika nyanja mbalimbali ikiwemo michezo, kwa kuwa kundi hilo ni nguzo muhimu katika mnyororo wa maendeleo ya Taifa.

Utoaji wa sare hizi ni muendelezo wa mpango wa Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Kondoa, ambao umekuwa ukiratibiwa kila mwaka vijana wanaposhiriki mashindano hayo.

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Zanzibar (ZURA) imetangaza bei ya mafuta ambapo petroli imepanda kutoka...
08/06/2026

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Zanzibar (ZURA) imetangaza bei ya mafuta ambapo petroli imepanda kutoka shilingi 3,820 na sasa itauzwa kwa shilingi 3890 kwa lita.

Kwa upande wa dizeli imepanda kutoka 3,850 na sasa itauzwa kwa shilingi 3,890 kwa lita.

08/06/2026

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe Albert Msando, ameongoza ziara maalum ya viongozi wa Manispaa ya Ubungo katika chanzo cha uzalishaji maji Ruvu Juu kwa lengo la kujionea hali ya uzalishaji na usambazaji wa maji pamoja na kutafuta suluhu ya pamoja ya changamoto za huduma ya Maji.

Ziara hiyo imewahusisha Madiwani wa Manispaa ya Ubungo, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ubungo pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali za kufuatilia na kuboresha huduma ya maji kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe Msando amewataka madiwani kushiriki kikamilifu ili kubaini changamoto za maji katika kata zao na kupata uelewa wa kina kuhusu hatua zinazochukuliwa na DAWASA kuboresha huduma hiyo.

Aidha, ameielekeza DAWASA kutoa maelezo kuhusu mipango ya muda mfupi na muda mrefu ya kuimarisha upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Ubungo pamoja na kuwapa wananchi taarifa sahihi kuhusu hali ya huduma katika maeneo yao.

Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Mk**a Bwire, amesema ziara hiyo itasaidia viongozi kupata taswira halisi ya uzalishaji wa maji, mfumo wa usambazaji na mikakati inayotekelezwa kuboresha huduma kwa wakazi wa Ubungo.

Mhandisi Bwire ameeleza kuwa DAWASA inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuongeza uwezo wa uzalishaji na usambazaji wa maji, ikiwemo ufungaji wa pampu mpya katika mitambo ya uzalishaji.

“Mpaka sasa pampu sita kati ya nane zilizopangwa zimewasili nchini zimewasili, huku pampu mbili zilizobaki zikiendelea kukamilishwa kabla ya kuletwa. Tayari zoezi la ufungaji limeanza na pampu moja imefungwa, huku kazi ikiendelea kwa pampu nyingine,” amesema Mhandisi Bwire.

Ameongeza kuwa maboresho hayo yanatarajiwa kuongeza ufanisi wa uzalishaji na usambazaji wa maji, hatua itakayosaidia kupunguza changamoto za upatikanaji wa huduma katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Ubungo.

08/06/2026

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi (UWT), Mary Pius Chatanda Amesema Wanawake wametakiwa kutambua umuhimu na mchango wao katika familia na jamii kwa kujikita katika sekta mbalimbali ikiwemo madini, elimu na fursa za kiuchumi.

Chatanda amesema hayo wakati wa hafla ya ugawaji wa tuzo za Malkia wa Dhahabu , Geita ambapo amesema wanawake wana nafasi kubwa katika ujenzi wa
familia imara na maendeleo ya taifa, hivyo wanapaswa kutumia fursa zilizopo ili kujikwamua kiuchumi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Geita amewasisitiza wanawake kujitokeza na kushirikiana katika shughuli za maendeleo, huku washiriki wakihamasisha wenzao kuongeza jitihada katika shughuli za kiuchumi.

Kawaupande wao Malkia wa Dhahabu wamelipoke Tuzo hizo wamesema wanawake hawatakiwi kukatishwa tamaa kujihusisha katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kutoogopa kujiingaza katika baadhi ya kazi kwa kuwa na mitazamo hasi wakiamini ni ngumu.

Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Uhondo TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share