Numeric Digital

Numeric Digital Welcome to Numeric Digital! Your ultimate destination for dynamic and diverse content that delves into the heart of national and international news.

At Numeric Digital, we strive to bring you insightful stories.

DAR ES SALAAM | Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itaendelea kutumia maonesho ya biashara k**a jukwaa muhimu la ...
13/07/2026

DAR ES SALAAM | Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itaendelea kutumia maonesho ya biashara k**a jukwaa muhimu la kutangaza bidhaa zinazozalishwa visiwani, kuwatafutia wazalishaji na wajasiriamali masoko mapya pamoja na kuvutia uwekezaji unaochochea ukuaji wa uchumi.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed Mahmoud, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Zanzibar yaliyofanyika katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Amesema ushiriki wa Zanzibar katika maonesho hayo umeendelea kutoa fursa ya kuitangaza Zanzibar k**a kitovu cha biashara na uwekezaji, sambamba na kuandaa mazingira ya kunufaika na fursa zinazotokana na Soko Huru la Afrika (AfCFTA).

Aidha, amewataka wazalishaji na wafanyabiashara kuendelea kuboresha ubora wa bidhaa zao, kutumia vifungashio vinavyokidhi viwango vya kimataifa na kuimarisha huduma kwa wateja ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Zanzibar katika soko la Afrika Mashariki na masoko mengine ya kimataifa.

Mhe.Ayoub amesema licha ya Zanzibar kuwa na eneo dogo kijiografia, ina uwezo mkubwa wa kuzalisha bidhaa na huduma zenye ubora na ushindani, akibainisha kuwa uwekezaji katika rasilimali watu, ubunifu na matumizi ya teknolojia ni nguzo muhimu zinazochangia kuibua fursa mpya za biashara, uwekezaji na ajira kwa wananchi.

DAR ES SALAAM | Vijana wa Tanzania wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya bahari, huku Chuo cha Bahari D...
13/07/2026

DAR ES SALAAM | Vijana wa Tanzania wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika sekta ya bahari, huku Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) kikieleza kuwa wahitimu wake wanaendelea kupata ajira ndani na nje ya nchi, hususan katika mataifa ya Mashariki ya Kati kutokana na mahitaji makubwa ya wataalamu wa ubaharia.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) Julai 13, 2026, Nahodha na Mwalimu kwa Njia ya Vitendo Daraja la Pili wa DMI, Master Kelly Mwandambo, amesema ubaharia ni taaluma yenye fursa nyingi za ajira na kipato kizuri, hivyo vijana wanapaswa kuichagua k**a taaluma ya ndoto zao.

Mwandambo amesema mafunzo ya ubaharia yanafuata viwango vya kimataifa vinavyosimamiwa na Shirika la Kimataifa la Bahari, hali inayowafanya wahitimu wa DMI kuwa na uwezo wa kushindana katika soko la ajira duniani kwa kuwa wanapata mafunzo yanayolingana na yanayotolewa katika nchi nyingine ikiwemo Marekani.

Aidha, amewataka wazazi na walezi kuwahamasisha watoto wao kujiunga na Chuo cha Bahari Dar es Salaam, akieleza kuwa taasisi hiyo inatoa mafunzo kuanzia ngazi ya cheti hadi Shahada za Uzamili (Masters), hatua inayowafungulia wahitimu fursa za ajira katika sekta ya bahari duniani.

Kwa upande wake, Mkufunzi Msaidizi wa DMI na Mhandisi wa Baharini, Winfrida Winsislaus Ngalu, amesema wanafunzi wanaojiunga na chuo hicho wanapata fursa mbalimbali za ufadhili wa masomo, ikiwemo mikopo ya serikali kutoka HESLB, kuanzia ngazi ya cheti, nafasi za Samia Scholarship, mikopo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar pamoja na METFUND kwa wanaosoma kozi zinazohusiana na ubaharia.

Amesema pamoja na ufadhili huo, wahitimu wa DMI wameendelea kuwa miongoni mwa wataalamu wanaohitajika zaidi katika soko la ajira la kimataifa, jambo linaloifanya sekta ya bahari kuwa moja ya maeneo yenye mustakabali mzuri kwa vijana wanaotafuta taaluma yenye ajira za uhakika na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa Taifa.

13/07/2026

RAIS DKT. SAMIA AKIFUNGUA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA MAWAKILI WA SERIKALI, AICC, ARUSHA

19/11/2025

DODOMA | Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndg. Kenani Laban Kihongosi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Ukumbi wa Jakaya Kikwete Jijini Dodoma hii leo Novemba 19, 2025.

#

15/11/2025

ZANZIBAR | Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza katika hafla ya Kuwaapisha Mawaziri wateule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, ambapo hafla hiyo ya uwapisho ilifanyika katika Viwanja vya Ikulu -Zanzibar.

15/11/2025

WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA

Ameziagiza hospitali zote nchini zihakikishe wajawazito wanapofika hospitali wahudumiwe kwa haraka ili kuokoa maisha ya mama na mtoto.

15/11/2025

WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA MKOA WA DODOMA

Atoa maagizo kwa Wizara ya Afya, MSD na hospitali zote nchini.

Ataka wajawazito wasisubirishwe mapokezi wanapofika hospitali

Wagojwa waipongeza Srtikali kwa kuboresha huduma za afya

DODOMA \ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza msamaha maalum kwa vijana wa...
14/11/2025

DODOMA \ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza msamaha maalum kwa vijana waliohusishwa na vurugu wakati wa kipindi cha uchaguzi, ambao walijikuta wakifuata mkumbo bila kufahamu uzito wa matendo yao.

Akitangaza uamuzi huo wakati akilihutubia Bunge la 13 leo Novemba 14, 2025, Rais Samia alisema lengo la msamaha huo ni kuwapa nafasi vijana hao kurejea katika familia zao na kuanza upya maisha yao wakiwa na maadili na uelewa zaidi.

Uamuzi huu umepokelewa k**a hatua muhimu ya kuhimiza maridhiano, umoja na ustawi wa taifa.

13/11/2025

DODOMA \ Maneno ya Dkt. Mwigulu Nchemba baada ya Kuthibitishwa kuwa Waziri Mkuu leo Hii Bungeni Dodoma.

Address

P.o Box 4100
Dar Es Salaam
0255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Numeric Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share