13/07/2026
DAR ES SALAAM | Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema itaendelea kutumia maonesho ya biashara k**a jukwaa muhimu la kutangaza bidhaa zinazozalishwa visiwani, kuwatafutia wazalishaji na wajasiriamali masoko mapya pamoja na kuvutia uwekezaji unaochochea ukuaji wa uchumi.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Ayoub Mohammed Mahmoud, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Zanzibar yaliyofanyika katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).
Amesema ushiriki wa Zanzibar katika maonesho hayo umeendelea kutoa fursa ya kuitangaza Zanzibar k**a kitovu cha biashara na uwekezaji, sambamba na kuandaa mazingira ya kunufaika na fursa zinazotokana na Soko Huru la Afrika (AfCFTA).
Aidha, amewataka wazalishaji na wafanyabiashara kuendelea kuboresha ubora wa bidhaa zao, kutumia vifungashio vinavyokidhi viwango vya kimataifa na kuimarisha huduma kwa wateja ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Zanzibar katika soko la Afrika Mashariki na masoko mengine ya kimataifa.
Mhe.Ayoub amesema licha ya Zanzibar kuwa na eneo dogo kijiografia, ina uwezo mkubwa wa kuzalisha bidhaa na huduma zenye ubora na ushindani, akibainisha kuwa uwekezaji katika rasilimali watu, ubunifu na matumizi ya teknolojia ni nguzo muhimu zinazochangia kuibua fursa mpya za biashara, uwekezaji na ajira kwa wananchi.