Habari Mkwama

Habari Mkwama karibuni kwenye Ukumbi wa Simzi_Media utakaokuwa unakuhabarisha matukio na mafunzo mbalimbali.

03/01/2026

Muhtasari wa habari za Venezuela

Haraka | Venezuela:

Milipuko mikubwa ilisikika na ndege za kivita zilionekana zikiruka juu ya mji mkuu wa Venezuela, Caracas.

๐Ÿ”ด Haraka | Reuters:

Kukatika kwa umeme katika eneo karibu na kambi ya kijeshi kusini mwa mji mkuu wa Venezuela, Caracas.

๐Ÿ”ด Haraka |

Magari ya kijeshi ya Israeli yafyatua risasi mashariki mwa kambi ya wakimbizi ya Jabali kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.

๐Ÿ”ด Haraka | Associated Press:

Angalau milipuko 7 ilisikika katika mji mkuu wa Venezuela, Caracas

๐Ÿ”ด Breaking | Vyombo vya habari vya Venezuela:

Mashambulizi ya anga yalilenga kambi kadhaa, ikiwa ni pamoja na eneo la kijeshi la Fort Tuna, kambi ya La Carlota, na uwanja wa ndege wa Iguirote

๐Ÿ”ด Breaking | Vyombo vya habari vya Venezuela:

Milipuko mipya katika bandari ya Caracas

๐Ÿ”ด Breaking | Vyanzo vya Palestina:

Breaking | Vyombo vya habari vya Venezuela: Milipuko katika bandari ya La Guaira katika jimbo la Vargas, bandari kubwa zaidi ya Venezuela

๐Ÿ”ด Breaking | Rais wa Colombia:

Mpango wa uendeshaji unaanzishwa kwenye mpaka na Venezuela, na kituo cha amri cha umoja kiko Cรบcuta, mji wa mpakani wa Colombia

๐Ÿ”ด Breaking | Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela:

Tunakataa uchokozi dhidi ya nchi yetu, ambao ni ukiukaji mkubwa wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa

๐Ÿ”ด Breaking | Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela:

Venezuela ina haki ya kujilinda halali kwa watu wake, eneo lake, na uhuru wake.

๐Ÿ”ด Haraka | Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela: Tutakabiliana na uchokozi wa kibeberu kwa kuamsha mipango yote ya ulinzi.

๐Ÿ”ด Haraka | Serikali ya Venezuela:

Uchokozi wa Marekani dhidi ya nchi yetu unatishia amani na utulivu wa kimataifa, hasa Amerika Kusini na Karibea.

๐Ÿ”ด Haraka | Serikali ya Venezuela:

Jaribio la kulazimisha vita vya kikoloni ili kuondoa mfumo wa Republican litashindwa.

๐Ÿ”ด Haraka | Serikali ya Venezuela:

Maduro atangaza hali ya hatari ya kitaifa nchini Venezuela.

๐Ÿ”ด Haraka | Rais wa Cuba:

Eneo letu salama liko chini ya mashambulizi makali na ugaidi wa serikali dhidi ya watu jasiri wa Venezuela na dhidi ya Amerika.

๐Ÿ”ด Haraka | Reuters, ikimnukuu afisa wa Marekani:

Marekani inaanzisha mashambulizi ndani ya Venezuela.

๐—ก๐—–๐—›๐—œ ๐—ฌ๐—˜๐—ง๐—จ ๐—œ๐—ก๐—”๐—ข๐—ก๐—š๐—ข๐—ญ๐—ช๐—” ๐—ž๐—ช๐—” ๐— ๐—œ๐—ฆ๐—œ๐—ก๐—š๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—” ๐—ก๐—” ๐—ฆ๐—›๐—˜๐—ฅ๐—œ๐—” ๐—ก๐—” ๐—ฆ๐—œ๐—ข ๐— ๐—”๐——๐—›๐—˜๐—›๐—˜๐—•๐—จ ๐—ฌ๐—” ๐——๐—œ๐—ก๐—œ - ๐—ฅ๐—”๐—œ๐—ฆ ๐——๐—ž๐—ง. ๐—ฆ๐—”๐— ๐—œ๐—”Mwenyekiti wa Chama Cha M...
02/12/2025

๐—ก๐—–๐—›๐—œ ๐—ฌ๐—˜๐—ง๐—จ ๐—œ๐—ก๐—”๐—ข๐—ก๐—š๐—ข๐—ญ๐—ช๐—” ๐—ž๐—ช๐—” ๐— ๐—œ๐—ฆ๐—œ๐—ก๐—š๐—œ ๐—ฌ๐—” ๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—•๐—” ๐—ก๐—” ๐—ฆ๐—›๐—˜๐—ฅ๐—œ๐—” ๐—ก๐—” ๐—ฆ๐—œ๐—ข ๐— ๐—”๐——๐—›๐—˜๐—›๐—˜๐—•๐—จ ๐—ฌ๐—” ๐——๐—œ๐—ก๐—œ - ๐—ฅ๐—”๐—œ๐—ฆ ๐——๐—ž๐—ง. ๐—ฆ๐—”๐— ๐—œ๐—”

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. ๐—ฆ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐—ฆ๐˜‚๐—น๐˜‚๐—ต๐˜‚ ๐—›๐—ฎ๐˜€๐˜€๐—ฎ๐—ป amesema kwa namna moja au nyingine kuna baadhi ya taasisi za dini zimejiingiza kwenye mkumbo ambao unaendelea wenye nia ovu ndani yake.

Akieleza juu ya uongozi wa nchi katika kufuata misingi ya katiba na sheria, Rais Dkt. Samia amesema Tanzania haina dini lakini Watanzania wana dini za madhehebu mbalimbali huku akisisitiza kuwa kikatiba na sheria za nchi hakuna dini na dhehebu lolote lenye uwezo waโ€™kuover rideโ€™ madhehebu mengine.

Akizungumza na Wazee wa mkoa wa Dar es salaam leo tarehe 2 Disemba 2025, Rais DKt. Samia ameyasema na kuyasisitizia haya kuhusu taasisi za dini nchini

โ€œViongozi wa dini msijivishe majoho ya kwamba nyinyi ndio mnaweza โ€˜kuover runโ€™ nchi hii, hakuna. Tutakwenda kwa kwa Katiba na Sheria ya Nchi hii.โ€

โ€œHatutaendeshwa na madhehebu yoyote ya dini, madhehebu ya dini na wafuasi waoโ€

โ€œubora wa dini upo miyoyoni kwetu, wale wanaoamini ndio wanajua ubora wa dini yao..โ€

โ€œhakuna โ€˜over ridingโ€™ hapa! Kwamba โ€œmimi dini yangu ndio itaover ride Tanzania na tamko nikilitoa ndio hilo hiloโ€.

โ€œ...hata wenyewe wanatofautiana, mimi toka nimekaa matamko 8 yametolewa na TEC, lakini ukienda chini chini wenyewe wanapingana, matamko yale hayafanyi kazi.. .waliosimama kwenye mstari wa haki wanaona ni batili iliyofanyika..hawaungani nao..โ€

โ€œTanzania yetu ni nchi ya umoja na mshik**ano, amani na utulivu ndio ngazo zetu, tusivurugwe ndugu zangu..โ€

* *

28/11/2025
28/11/2025
Ningekuwa Rais SamiaWatanzania huwa ni wavivu katika kufanya kazi japo Sio wote, hii hupelekea kuona K**a aliyenakipato ...
28/11/2025

Ningekuwa Rais Samia

Watanzania huwa ni wavivu katika kufanya kazi japo Sio wote, hii hupelekea kuona K**a aliyenakipato ni K**a amependelewa Kwahiyo huwa na wivu sana japo wapo watu wanapoona Yao yamebanwa huanzisha chokochoko lakini kwa hawa wa chini huwa ni wivu wa kipato. Na ugumu wa maisha hushawishiwa kuleta fujo kwa vihongo vya muda mfupi!

Kwahiyo ningekuwa Rais Samia kutokana na Hali k**a hii! Kwa Muda mfupi hadi vuguvugu liishe ningefanya hivi;

1. Ningeshauri mshahara wa wabunge upungue na posho ya kila siku ya wabunge ingepungua.

2. Mshahara wa wakuu wa mikoa na wilaya hawa wateuliwa wote mishahara ipungue!

3. Ningepunguza bei ya unga na mchele na sukari, na mafuta, kwasababu hivo Vitu vinawagusa wananchi moja kwa moja,

4. Kisha ningepunguza ushuru wa Ptrol, Disel na kupunguza nauli za usafiri wa mabadiliko na daladala,

5. ningesimamia ajira kupitia uongozi wa serikali wa eneo kuorodhesha majina ya vijana wote wasio nakazi, kuhakikisha wanapata kazi ima kuajiriwa au kujiajiri na Nani ngekuwa wajibu,

kuna baadhi ya vijana Sio K**a hamna kazi bali ni wavivu wa kufanya kazi, au wanachagua kazi, lakini ikiwa ni kosa ya jinsi kijana kukutwa bila kazi,
Wachache sana wangekuwa Uraiani.

Lakini kwasababu Mimi Sio samiha.

1. Nitabadilisha viongozi marakwamara,
2. Nitafukuza na kukemea watendaji wabovu
3. Nitaweka vikundi vya kuelimisha jamii umuhimu wa kuipende Tanzania na kuwa na amani
4. Nitaongea na taasisi mbalimbali kuhakikisha vijana wanabaki na amani kwa kuzungumza nao
5. Nitawakusanya wasomi kuweka matamasha na semina za kuzungumzia amani
6. Nitakubali maridhiano na wapinzani nakuyafanyia kazi watakayo kwa team ya pamoja
7. Nitatuma watu kwenda uzungumza na wahisani wa nje au kwenda mwenyewe kuomba POOโ€ฆ.

Ebu Sema Ungekua wewe ndio Mh. Samia ungefanyaje?!

Ndugu zake rais Magufuli Serikalini kipindi chake walikuwepo!?John Magufuli alikuwa na ndugu zake wakaribu walioviongozi...
27/11/2025

Ndugu zake rais Magufuli Serikalini kipindi chake walikuwepo!?

John Magufuli alikuwa na ndugu zake wakaribu walioviongozi katika nafasi mbalimbali za uongozi wakati wa uongozi wake. Baadhi ya ndugu zake walioviongozi ni:

- *Janeth Magufuli*: Dada yake, ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH)

- *M***a Sima Magufuli*: Kaka yake, ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TAPA).

- *Mansoor Magufuli*: Kaka yake, ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Bia ya Tanzania (TBL).

- *Joseph Magufuli*: Kaka yake, ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Ukishangaa ya Samia Shangaa na ya Magufuli

27/11/2025

*Wenzako wanapiga pesa ili waiharibu nchi yako,halafu wewe unashabikia na kuwa tayari kuumia kizoba...Kataa ujinga huo,nenda kafanye kazi*

Kuanzia February 2025 hadi September na utafiti unaonyesha kwa uharaka katika kipindi cha kuanzia January 2025 hadi September 2025 Zaidi ya USD 30,000,000 sawa na Tsh 7.5B+ (74,026,276,800.00 zilibgizwa nchini Tanzania kutoka kwen Taasisi ya ya Ford Foundation ya Marekani kwa ajili ya kusaidia makundi ya wanaharakati kufanya siasa.

Jiulize pesa hii nyingi ndani ya miezi 10 tu walioitoa wananufaika na nini na Tanzania?

Angalia list ya baadhi ya wanufaika wa mabilioni haya ambao wote ni wanaharakati nchiโ€ฆ

1. February, 2025 Ford Foundation waliipa Taasisi ya Twaweza ya Tanzania kiasi cha USD $2,015,000 kwa lengo la kuhamasisha demokrasia na uwajibikaji wa Serikali ya Tanzania k**a amabyo wao wenyewe wame report katika website yao hapa (fordfoundation.org/work/our-grantโ€ฆ)

2. February 2025, Ford Foundation waliidhinisha kiasi cha $315,000 Kwa taasisi inaitwa Tanzania Bora Initiative kwa lengo la kuwajengea uwezo vijana wa kitanzania kupashana na kuchakata habari mtandaoni za masuala ya Demokrasia. Reference (fordfoundation.org/work/our-grantโ€ฆ)

3. April 2025, Ford Foundation waliidhinisha kiasi cha TZS $300,000 kwa Amnesty International Tanzania kwa malengo waliyoyaita Core support for social justice groups in Tanzania and Uganda to continue reclaiming civic space and enhancing Social Justice Leaders protection mechanisms'' k**a inavyoonekana hapa katika link yao (fordfoundation.org/work/our-grantโ€ฆ)

4. May 2025, Ford Foundation waliidhinisha kiasi cha $200,000 kwa Tanzania Human Rights Defenders Coalition kwa ajili ya ku support harakati za haki za binadamu na watetezi wake hususani katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, ikiwa ni sambamba na kuwajengea uwezo hao wanaharakati k**a wanavyoeleza hapa katika link yao ( fordfoundation.org/work/our-grantโ€ฆ)

5. July 2025, Ford Foundation wakato kiasi vha USD 100,000 Kwa Jamii Forums kwa ajili ya malengo waliyoyaita ''General support for advocacy for freedom of expression, democracy, good governance, accountability and transparency via digital rights, and for building an inclusive digital community while empowering Netizens in Tanzania'' k**a wanavyoeleza hapa (fordfoundation.org/work/our-grantโ€ฆ).

6. September, 2025, Ford wakatoa kiasi cha $1,680,000 kwa Mzalendo Trust kwa ajili ya kujengea uwezo wanaharakati wa kisiasa mitandaoni k**a inavyooleza hapa katika link yao hapa (fordfoundation.org/work/our-grantโ€ฆ)

7. Zipo Taasisi zingine zaidi ya 10 ikiwemo Restless Tanzania, Mwanzo Dot ORG, Change Tanzania, Centre for Strategic Litigations na kadhalika ambazo kwa kipindi hicho hicho zimepokea Fedha nyingi sana toka Ford ambapo ni mabilioni k**a unavyoweza kuona katika database ya Ford.

Soma kwa utulivu uelimike ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญKwa sasa, Nchi ambazo zimeingia katika target ya CIA Kwa ajili ya regime change ukiacha Nchi...
27/11/2025

Soma kwa utulivu uelimike ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ˜ญ

Kwa sasa, Nchi ambazo zimeingia katika target ya CIA Kwa ajili ya regime change ukiacha Nchi zingine za Afrika ni *Namibia*, *Zambia* na *Tanzania* kwa sababu ya wanachokiita unfriendly terms za uchimbaji wa madini.

Kwa sababu ya Muda na Muhimu wa Jambo hili nitadokeza kuhusu Tanzania tu kwa leo.

Niliwahi kuandika siku moja kwamba kuna kitu kinaitwa Pax Americana ambayo ni sehemu ya Sera ya nchi za Nje ya Marekani inayosema Rasilimali zote duniani ni lazima ziwe nchini ya *Makampuni ya Marekani* na sio *China* au *Urusi*.

Aspect hii ya Sera ya nchi za Nje ya Marekani ndiyo *msingi* wa kuelewa uwepo wa *uasi* katika Nchi mbalimbali zenye madini kuanzia vikundi vya kigaidi k**a ISIS, Maandamano ya kupindua Nchi Kupitia liberal democracy au uvamizi wa kijeshi (through NATO) k**a ilivyotokea Libya.

Orodha ni ndefu lakini hii ni common knowledge Kwa wafuatiliaji wa masuala ya world politics.

Kilichotokea Libya, Sudan, Iraq, Iran, Syria, Congo, Mozambique, Nigeria, Bolivia, Venezuela, Nicaragua na Nchi nyingine nyingi ni manifestation ya suala hilihili moja katika Sura na Nchi tofauti.

Kwa hiyo, Makampuni ya *Marekani na Ulaya* yakikosa fursa ya kichimba madini wanayoyataka katika Nchi husika, basi k**a madini hayo ni very strategic kwao, ni lazima watafute njia ya kuharibu kwa sababu ni lazima yataangukia Kwa China au Urusi na pia geopolitically Marekani itataka izuie influence ya hao mahasimu wake wakuu.

Lakini Jambo lingine linaloongezeka Kwa Marekani k**a sababu ya kufanya regime change kwa Kupitia Assassination, CIA Gen Z organized protests, uvamizi wa kijeshi (Through NATO) inaweza kuwa kukataa kutekeleza Jambo lolote ambalo ni Strategic Kwa ajili ya maslahi mapana ya Marekani k**a vile kukataa kuweka Military Base, kupinga kutekeleza planned global measures k**a Mandatory Vaccination, Digital ID na mengine. Ukipinga vitu k**a hivyo jiandae kuletewa zengwe.

Hebu nirudi sasa kwenye mineral control na nije moja Kwa moja Tanzania na kinachoendelea ili tupate picha. Nataka niachane kidogo na issues zingine nijikite katika aspect ya madini pekee.

Nianze kwa kurejea makala inayodokeza ilivyo iliyoandikwa na Jon Emont mwaka huu katika *Wall Street Journal (WSJ)* yenye kichwa cha habari:

*"The Failed Crusade to Keep a Rare Earths Mine out of China's Hands"*

Nisingependa kutoa tafsiri ya Kiswahili ya Kichwa hicho cha habari nahisi nitaondoa ladha ya hoja iliyobebwa ila makala hii imesema Kwa Muhtasari chanzo cha chokochoko tunazoziona nchini kwetu.

Kubwa ni kwamba kulikuwa na jitihada kubwa mno inafanywa na kampuni za Marekani za kumiliki mgodi wa madini adimu (rare earth's minerals/elements) wa Ngualla kule Mbeya ambao una uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 37,200 za concentrates kwa mwaka.

Hivi karibuni mgodi huu umeangukia katika umiliki wa kampuni kubwa na mahiri katika uchimbaji na uchakataji wa madini haya ya China ya *Shenghe Resources.*

Kupoteza umiliki wa mgodi huu imekuwa pigo kubwa Sana Kwa *Marekani* na *Ulaya* Kwa sababu lengo lao lilikuwa ni kupata namna ya kuwa huru katika kupata chanzo cha madini haya Nje ya China Kwa sababu Kwa sasa China ndiyo inaongoza Kwa uwingi wa migodi na Teknolojia ya kuchimba na kuchakata. Ili kupata picha ya pigo hili, Jon (2025) anasema:

*"For years, a mining project in Africa (i.e Ngualla Project) HELD the PROMISE of helping FREE the WEST form it's DEPENDENCE on CHINA for rare earths. Some weeks ago it FELL under China's HANDS"*

Hapa pia sitatoa tafsiri ili nisipoteze maana. Hii ndio Hali halisi kwamba matumaini ya Marekani na Ulaya ya kumiliki mgodi wa Ngualla yameyeyuka Kwa hiyo upo haja kwao kuona namna ya kufanya *regime change* ili apatikane kiongozi ambaye atawasaidia kurudisha huu mgodi katika mikono yao.

Mwandishi mwingine, Emmiliano Tossou (2025) anasema;

*"Tanzania emerges as new front in US-China race for critical minerals (i.e rare earths elements)"*

Kwa hiyo k**a Nchi tayari tumeshakuwa a new HUB for US-China Rivalry over critical minerals.

Lakini hebu tujiulize kwa nini *rare earths elements* ni madini Muhimu Kwa Nchi za Marekani na Ulaya?

Kwanza ifahamike kwamba Marekani na Ulaya wanahangaika na hali ya China kuwa ndiye dominant katika madini haya Kwa sababu madini haya ni muhimu Sana katika kitengenza vitu k**a smart phones, laptops, electric cars na baya zaidi katika kutengeneza military technological equipments ikiwemo fighter jets Kwa hiyo ni hatari Sana Kwa usalama wa Nchi hizi endapo watakosa umiliki wa madini haya.

Na tayari Nchi ya China imeshaanza kuchukua hatua za udhubiti Kwa kuzuia Teknolojia ya kuchimba na kuchakata isitoke Nje ya China Jambo ambalo ni pigo kubwa Sana Kwa Marekani na Ulaya.

Nyuma ya miaka ya 2010 Marekani ilikuwa ina umiliki katika eneo hili lakini wakati huo China ilionekana imejikita zaidi katika kuwekeza kuwa na migodi na kukuza Teknolojia na hii ilipelekea hata US Magnet Materials Association kuandika onyo Kwa Marekani kuhusu hatari ya China kuibuka dominant katika eneo hili.

Lakini pamoja na hayo Marekani na Ulaya walishindwa kuipiku China Kwa sababu Ulaya mpaka sasa hawana mgodi wa Rare earths na Marekeni wanayo Kwa uchache huku wakitegemea kupata malighafi kutoka China Kwa kiwango kikubwa.

Gracelini Baskaran (2025) ambaye ni Director at the US centre for Strategic and International Studies anasema:

*"We have known it to be a strategic vulnerability for a long time since 2010, but it is so capital intensive to build the midstream processing"*

Madini haya yapo takribani ya aina 17 lakini hapa Nguala inaonekana kuna uwingi wa lithium, Neodymium na praseodymium ambayo ni muhimu Sana.

Kwa hiyo hii ndiyo sababu kubwa ya kiuchumi ya Marekani na Ulaya kuback up vurugu ili kuona namna ya kupata njia ya kuwa na umiliki wa mgodi huu.

Lakini pia ukifanya ufuatiliaji wa kiongozi wa vijana Gen Z anayejiita Habil ambaye anasema yeye ni Mtanzania na Kwa sasa anaonekana k**a ndiye mastermind Kwa vijana utagundua pia kwamba kijana huyu anaishi Ulaya, through discourse analysis ya maneno yake maana kuna wakati anajisahau anasema maneno k**a "... Kwa mfano k**a huku Ulaya.." na hii ni hali ya kawaida katika matumizi ya lugha unaweza kuajikuta unaexpose mambo bila kujua Kwa sababu mifumo ya kiakili ya lugha iko genuine haifanyi Kazi Kwa misingi ya uongo.

Pia kijana huyu inaonekana yupo Ujerumani na wenzake wengi wanoongoza space forums za tiktok huku wakijifanya wapo Tanzania.

La msingi zaidi ni kwamba kijana huyu ukimsikiliza katika YouTube amegusia huu mradi wa Ngualla na analaumu Kwa nini Serikali imewapa wachina. *What a coincidence?*

Kwa nini kijana huyu aende very specific kulaumu Serikali kuingia makubaliano ya uchimbaji na kampuni ya China? Hii ni connection ya msingi kabisa ya kwamba hawa vijana wako organized na mobilized na watu mahususi ambao wanatafuta njia ya kupindua Serikali ili wapate kiongozi atakayewapa fursa ya kumilikia madini haya.

Na inaonekana wanataka kutumia mbinu k**a ya Bolivia walivyomtoa Evo Morales ambapo walileta vurugu mara Tu baada ya uchaguzi mpaka Mkuu wa jeshi akamka Rais Morales ajiuzulu na kwenda Mexico.

Baada ya hapo walimuweka mtu wao katika walichokiita Serikali ya mpito lakini Kwa muda huohuo anafanya haraka kubadilisha Sheria za madini na kampuni za Marekani zikarudi na kuanza kuchimba madini.

Na katika Hali ya Bolivia ni kwamba hawa Gen Z project Yao inaishia Tu katika kutumika kushawishi wenzao kuleta machafuko na kufanikisha Serikali kudondoka lakini baada ya hapo wanawekwa pembeni na wale wahamasishaji wanapotea ghafla na wenyewe wazee wa Kazi wanaingia na kuset mambo yao.

Na ndiyo maana vijana hawa ukiwasikiliza target yao Kuu ni kwamba serikali iliyopo itoke na wanasema ili tupate Katiba Mpya ambayo inasimamia maslahi ya Nchi lakini ukiwauliza swali la *what is the post military take over implementation strategy?*

Hawawezi kukupa jibu maana hawajui. Hao wahamasishaji wako Nje ya Nchi na huyo kijana Habil hawamjui zaidi ya kusikia sauti yake Tu na yeye Mwenyewe kujisema kwamba ni Mtanzania Kwa hiyo alivyokuja (from nowhere) ndivyo atakavyotoweka (to anywhere) baada ya project kukamilika.

*Nini cha kufanya?*

La msingi ni kuhakikisha kuwa Kwa gharama yeyote vurugu hizi zinadhibitiwa k**a wanavyopambana Venezuela ambapo wamemuondoa Hugho Chaves (Kwa kumuua kwa sumu baada ya njia zingine kushindikana) na akaja Nicholus Maduro mwenye misimamo k**a mtangulizi wake na mpaka leo wamekutana na kisiki na Trump sasa anamshawishi Urusi ili amuachie Ukraine ili akaivamie kijeshi Venezuela k**a walivyofanya Libya na Urusi isije kumsaidia ili hatimaye aichukue Venezuela.

These people are very serious na Sisi lazima tuwe serious zaidi Yao. Kuhusu kuwalipa vijana ili waandamane ni mbinu Yao ya siku nyingi na likely wanatumia Ujerumani k**a hub ya kulead hizi movements huku wakiwatunia human rights activists wa Kenya na wengine.

Maisha ni bora kuliko kifoLakini kufa bora kuliko ufukara au umasikiniWengi tunaona wanakitafuta kifo wakati wanapofikwa...
26/11/2025

Maisha ni bora kuliko kifo

Lakini kufa bora kuliko ufukara au umasikini

Wengi tunaona wanakitafuta kifo wakati wanapofikwa na maisha magumu, na raha ya uhai ni riziki, adhabu ya mwizi nikukatwa mkono kwa mungu lakini kutokana na ugumu wa maisha, adhabu ya mwizi ni kuchomwa moto kwa binadam.

Kwahiyo hata waporaji mali za watu siku ya fujo tarehe 29, nisawa na wauaji, msitengeneze Propaganda kuonekana wauaji ndio wabaya zaidi kuliko waporaji.

Wizi na uporaji wa mali za uma haukubaliki nyote ni wauaji, hakuna safari ngumu k**a kunyanyuka baada ya kudondoka. Tunawatengaje wahanga walioharibiwa magari yao. Nyumba zilizoharibiwa hivi kuna mtanzania masikini asiyejua ugumu wa kujenga, mnafunika wizi usionekane k**a hatia kwasababu nyinyi ndio mlioufanya,

tunahitaji haki bila kuona haki za wengine hii ni haki kweli?!

Je huu ni uungwana!?

โ€™0

Yakwao hawayasemi wanakomalia Tanzania tuuuu!?
25/11/2025

Yakwao hawayasemi wanakomalia Tanzania tuuuu!?

Address

Dodoma

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari Mkwama posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Habari Mkwama:

Share