Shamba digital

Shamba digital Ukurasa rasmi Kwa ajili kuweka habari za kisiasa, jamiii na burudani pamoja michezo

16/08/2026
09/08/2026

MISUNGWI CUP YAGEUKA FURSA KWA WAJASIRIAMALI LUDETE

MISUNGWI CUP imeendelea kuwa chachu ya fursa za kiuchumi kwa wajasiriamali wadogo katika Kata ya Ludete, baada ya wafanyabiashara waliokuwa wamejitokeza kuuza bidhaa zao kupata nafasi ya kuwahudumia mashabiki waliofika kushuhudia michezo ya robo fainali.

Furaha na shangwe za mashabiki katika Uwanja wa Ludete Sekondari hazikuishia kwenye burudani ya soka pekee, bali mashindano hayo yamegeuka kuwa fursa kwa wajasiriamali wadogo kuuza bidhaa zao na kuongeza kipato.

Katika hatua ya kuonyesha umuhimu wa kuwaunga mkono wajasiriamali hao, Diwani wa Kata ya Ludete na mwandaaji wa mashindano hayo, Jumanne Misungwi, alifika katika eneo walilokuwa wakifanyia biashara na kununua bidhaa mbalimbali, kisha kuzigawa bure kwa wananchi waliokuwepo uwanjani

Akizungumza kuhusu hatua hiyo, Jumanne Misungwi amesema lengo ni kuunga mkono juhudi za wajasiriamali wadogo pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wao

Amesema michezo haipaswi kuangaliwa k**a burudani pekee, bali inaweza pia kuwa sehemu ya kuibua na kuunganisha fursa za kiuchumi kwa wananchi, hususan vijana na wajasiriamali wadogo.

Hatua hiyo imepokelewa kwa furaha na mashabiki waliokuwepo uwanjani, huku ikionyesha namna mashindano ya Misungwi Cup yanavyoweza kuwa jukwaa la michezo na wakati huo huo kuchochea shughuli za kiuchumi ndani ya Kata ya Ludete.

08/08/2026

Tazama Uwanja wa Mpira ambo unajengwa na timu ya Geita Gold Fc maeneo ya Magogo Manispaa ya Geita ulivyo kwa sasa baada ya pitch yake kuungua moto

07/08/2026

Kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Geita Neema Chozaire Yaahirishwa Hadi Kwa sababu ya ugonjwa

Kesi ya jinai inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Jimbo la Geita, Neema Chozaire, imeahirishwa katika Mahak**a ya Wilaya ya Geita baada ya mtuhumiwa kutajwa kuwa mgonjwa.

Katika shauri hilo, Bi. Chozaire anakabiliwa na mashtaka ya kupanga njama za kuwaua askari wa Jeshi la Polisi. Kesi hiyo ilikuwa imepangwa kusikilizwa leo, lakini haikuendelea kutokana na hali yake ya afya

Wadhamini wawili wa Bi. Chozaire waliiambia mahak**a kuwa afya ya mtuhumiwa bado haijaimarika, hivyo wakaomba shauri hilo liahirishwe hadi atakapokuwa katika hali nzuri ya kuhudhuria mahak**ani

Baada ya kusikiliza maombi hayo, mahak**a ilikubaliana na ombi hilo na kuahirisha kesi hiyo hadi Agosti 10, 2026, ambapo itatajwa tena kwa hatua zaidi.

05/08/2026

VAR kazini

Address

Busanda/Geita
Geita

Telephone

+255766481788

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shamba digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share