
09/06/2025
*NYAKAGWE FC KUTUPA KARATA YA MWISHO DHIDI YA BUSHINGWE FC LEO MAPUNG'O 2025*
Timu ya Nyakagwe FC, iliyocheza fainali ya Mapung’o Cup mwaka Jana 2024, inatarajia kushuka dimbani leo kumenyana na Bushingwe FC kutoka Kakola, katika mchezo muhimu wa mwisho wa hatua ya makundi ya Mapung’o Cup 2025.
Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Soko la Jumatano uliopo Kijiji cha Nyakagwe, Butobela, Wilaya ya Geita kuanzia saa kumi jioni.
Kundi A lina jumla ya timu tatu ambazo ni Nyakagwe FC, Mabasi FC na Bushingwe FC. Hadi sasa, Nyakagwe FC na Mabasi FC wote wana pointi moja kila mmoja, huku Bushingwe FC wakiwa hawajacheza mchezo wowote—hii ikiwa mechi yao ya kwanza kwenye mashindano haya.
Mashindano ya Mapung’o Cup 2025 yamedhaminiwa na mdau maarufu wa soko, Pascal Mapung’o, anayefahamika zaidi k**a King Mapung’o.
Mchezo wa leo una umuhimu mkubwa kwa pande zote, hasa kwa Nyakagwe FC ambao wanahitaji ushindi ili kujihakikishia nafasi nzuri ya kusonga mbele
na aje!