Focus TV Tanzania

Focus TV Tanzania One of the Best Online TV Conveying Content and Adding Value for the Public Interest.

12/08/2026

Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamin Sitta, akiwaeleza Wananchi wa Kata ya Wasa katika Tarafa ya Kiponzelo Wilayani humo, juu ya umuhimu wa kuchangamkia fursa ya Mpango wa Bima ya Afya Kwa Wote, Bima inayogharimu kiasi cha Shillingi Laki Moja na Nusu (150,000/=) ikiwa na uwezo wa kuwahudumia watu sita katika familia.

DC Sitta alitoa ufafanuzi huo wakati akijibu hoja iliyoibuliwa na Mwananchi kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Ihomasa Kata ya Wasa Tarafa ya Kiponzelo Halmashauri ya wilaya ya Iringa Agosti 12, 2026.

12/08/2026

Wananchi wa Kata ya Wasa Tarafa ya Kiponzelo Halmashauri ya wilaya ya Iringa wameunga Mkono wazo lililotolewa na Mwananchi mwenzao akitamani maonesho ya Wakulima ya Nanenane yafanyike mpaka ngazi ya Kata ili kuchochea uchumi wa wananchi wa kipato cha chini Vijijini.

Hoja hiyo imeibuliwa kwenye Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamin Sitta, Ziara iliyoambatana na Mkutano Maalum wa Kusikiliza wananchi, Mkutano uliofanyika Kijiji cha Ihomasa katika Kata ya Wasa Tarafa ya Kiponzelo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa Agosti 12, 2026.

12/08/2026

alionesha kushtushwa na Kero ya Mwananchi wa Kijiji cha Ihomasa Kata ya Wasa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, akidai kuwa Mbwa wa watu katika Kijiji hicho wanavamia mashamba na Kula mahindi mabichi, akiomba kero yake itatuliwe na wenye Mbwa hao wafundishwe namna nzuri ya kuwafuga Mbwa wao.

Hayo yametokea Agosti 12, 2026 katika Ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamin Sitta, Ziara iliyoambatana na Mkutano Maalum wa Kusikiliza na kutatua Changamoto na kero za Wananchi katika Kata ya Wasa Tarafa ya Kiponzelo Halmashauri ya wilaya ya Iringa.

11/08/2026

Kitonga Marathon imezinduliwa rasmi mkoani Iringa, mbio zinazotarajiwa kufanyika Oktoba 31, 2026 katika Barabara ya Mlima Kitonga uliopo Kata ya Ilula Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, zikihusisha wakimbiaji wa Kilomita 5, 10 na 21 kutoka ndani na nje ya mkoa wa Iringa.

Uzinduzi wa Mbio hizo za Kitonga Marathon zenye kauli mbiu isemayo 'Tunza Mazingira, Wekeza Kilolo', umefanyika Agosti 11, 2026 ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Estomin Kyando, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, ambaye hakufanikiwa kufika katika tukio hilo.

Kitonga Marathon imezinduliwa rasmi mkoani Iringa, mbio zinazotarajiwa kufanyika Oktoba 31, 2026 katika Barabara ya Mlim...
11/08/2026

Kitonga Marathon imezinduliwa rasmi mkoani Iringa, mbio zinazotarajiwa kufanyika Oktoba 31, 2026 katika Barabara ya Mlima Kitonga uliopo Kata ya Ilula Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, zikihusisha wakimbiaji wa Kilomita 5, 10 na 21 kutoka ndani na nje ya mkoa wa Iringa.

Uzinduzi wa Mbio hizo za Kitonga Marathon umefanyika Agosti 11, 2026 ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Estomin Kyando, ambaye alimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, ambaye hakufanikiwa kufika katika tukio hilo.

Habari Kamili ipo hapa
👇

Kitonga Marathon imezinduliwa rasmi mkoani Iringa, mbio zinazotaraj...

10/08/2026

Sehemu ya Hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, iliyowachekesha Wageni kwenye hafla ya Uzinduzi wa Hoteli Mpya ya Golden Glow iliyopo Kihodombi Kata ya Isakalilo Manispaa ya Iringa Agosti 09, 2026.

10/08/2026

Hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, iliyomgusa moja kwa moja Mkurugenzi wa Hoteli Mpya ya Golden Glow pamoja na wawekezaji wengine katika mkoa wa Iringa wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Hoteli hiyo iliyopo Kihodombi Kata ya Isakalilo ndani ya Manispaa ya Iringa Agosti 09, 2026.

10/08/2026

Mkoa wa Iringa umejipanga kuzindua Kliniki Maalum ya Watumishi wa Umma wa mkoa huo ikilenga kuwakutanisha kwa karibu Watumishi na waajiri wao, ambapo Kliniki hiyo itasimamia kauli mbiu isemayo 'Watumishi Iringa Sema na Mwajiri'.
‎
‎Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Iringa, Nuru Sovellah, anayeshughulikia masuala ya Utawala na Usimamimizi wa rasilimali watu katika mkoa huo, ambapo amesema kuwa Kliniki hiyo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Agosti 13, 2026, na mgeni rasmi katika uzinduzi huo atakuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James.
‎
‎

10/08/2026

Mkurugenzi wa Hoteli Mpya ya Golden Glow Iringa, Ernest Henry Mtavilalo, alitoa Shukrani zake za dhati pamoja na cheti Maalum akimshukuru Mke wake Kwa upendo na ushirikiano wake mpaka wakafanikiwa ndoto yao ya kujenga Hoteli Mpya ya Kisasa ya Golden Glow.

Tukio lilifanyika mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, aliyekuwa Mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hoteli hiyo iliyopo Kihodombi Kata ya Isakalilo ndani ya Manispaa ya Iringa.

10/08/2026

Mkurugenzi wa Hoteli Mpya ya Golden Glow, Ernest Henry Mtavilalo, akitoa salamu za Shukran mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, aliyekuwa Mgeni rasmi katika hafla ya Uzinduzi wa Hoteli hiyo iliyopo Kihodombi Kata ya Isakalilo ndani ya Manispaa ya Iringa.

Address

Iringa
51108

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Focus TV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category