12/08/2026
Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Benjamin Sitta, akiwaeleza Wananchi wa Kata ya Wasa katika Tarafa ya Kiponzelo Wilayani humo, juu ya umuhimu wa kuchangamkia fursa ya Mpango wa Bima ya Afya Kwa Wote, Bima inayogharimu kiasi cha Shillingi Laki Moja na Nusu (150,000/=) ikiwa na uwezo wa kuwahudumia watu sita katika familia.
DC Sitta alitoa ufafanuzi huo wakati akijibu hoja iliyoibuliwa na Mwananchi kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Ihomasa Kata ya Wasa Tarafa ya Kiponzelo Halmashauri ya wilaya ya Iringa Agosti 12, 2026.