Focus TV Tanzania

Focus TV Tanzania One of the Best Online TV Conveying Content and Adding Value for the Public Interest.

Mgombea Ubunge Jimbo la Mafinga Mjini kupitia CCM, Dickson Lutevele maarufu Villa, tayari ametimiza haki yake ya msingi ...
29/10/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Mafinga Mjini kupitia CCM, Dickson Lutevele maarufu Villa, tayari ametimiza haki yake ya msingi ya kupiga kura kumchagua Rais, Mbunge na Diwani katika Kituo alichojiandikisha kikichopo Kata ya Kinyanambo Halmashauri ya Mji Mafinga Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa Oktoba 29, 2025.

Aliyekuwa Mbunge Jimbo la Kilolo mkoani Iringa, Justin Lazaro Nyamoga, tayari ametimiza haki yake ya msingi na takwa la ...
29/10/2025

Aliyekuwa Mbunge Jimbo la Kilolo mkoani Iringa, Justin Lazaro Nyamoga, tayari ametimiza haki yake ya msingi na takwa la kikatiba kushiriki uchaguzi kwa kupiga kura kumchagua Rais, Mbunge na Diwani katika kituo alichojiandikisha kilichopo Kijiji cha Luganga wilayani Kilolo Oktoba 29, 2025.

29/10/2025

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, tayari ametimiza haki yake ya Msingi na takwa la Kikatiba kwa Kupiga Kura kumchagua Rais, Mbunge na Diwani kwenye Kituo alichojiandikisha Kinondoni Flat 2 kilichopo Kata ya Gangilonga, ambapo mara baada ya Zoezi hilo ametoa wito kwa Wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi kupiga kura kuwachagua Viongozi wao, huku akisema kuwa Iringa ni Salama na hali ni Shwari kwenye Vituo Vyote katika Wilaya na Majimbo yote ndani ya Mkoa huo.

29/10/2025

Watu wa Imani, huwa Tunaanza na Mungu na Tunamaliza Mungu, kwasababu yeye ndiye ndiye Tumaini letu la Uhakika. 🙏

Tunawatakia Wapiga Kura Wote, Amani mwanzo mpaka mwisho wa Zoezi la Uchaguzi.

Note: Video ya Askari akiomba ilirekodiwa siku ya Kupokea Magari Mapya yaliyotolewa na Serikali. Imetumika Leo Oktoba 29 k**a Teaching Aid au Manual Guide 🤗

28/10/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Kilolo, Ritta Kabati, wakati akihitimisha Kampeni zake, ameahidi kushirikiana na Viongozi wa Dini kurejesha Upendo na kuimarisha mshik**ano wa wananchi na viongozi katika jimbo la Kilolo ili kuongeza na kuchochea kasi ya maendeleo katika Jimbo hilo.

Mkutano huo umefanyika Oktoba 28, 2025, katika Uwanja wa Shule ya Msingi Lundamatwe Kata ya Irole Jimbo la Kilolo mkoani Iringa, ambapo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilolo, John Kiteve, ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika tukio hilo.

28/10/2025

Msanii wa Kimasai awakosha Wahehe wa Kilolo Iringa wakati akitoa Burudani kunogesha mkutano wa Kuhitimisha Kampeni za CCM za Mgombea Ubunge Jimbo la Kilolo, Dkt. Ritta Kabati.

Mkutano wa kuhitimisha kampeni za Mbunge huyo, umefanyika Oktoba 28, 2025 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Lundamatwe Kata ya Irole Jimbo la Kilolo mkoani Iringa, ambapo mgeni rasmi katika tukio hilo alikuwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kilolo, John Kiteve.

28/10/2025

Shamra shamra za Kuhitimisha Kampeni za CCM Jimbo la Kilolo mkoani Iringa, zilianza na mapokezi ya Mgombea Ubunge wa Jimbo hilo, Dkt. Ritta Kabati, alafu wote wakaungana kwa vibe kwenda kumpokea Mgeni rasmi wa tukio hilo, John Kiteve, ambaye ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilolo.

27/10/2025

Serikali kupitia mradi wa TACTIC, imepanga kutumia kiasi cha Shilingi Bilioni 20 kwa ajili ya kutekeleza ujenzi wa Soko la Kisasa katika eneo lililopo Kata ya Kihesa katika Manispaa ya Iringa Mkoani Iringa.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, katika ziara yake ya kukagua hali na hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika halmashauri ya Manispaa ya Iringa.

27/10/2025

"Sisi Wanasiasa na Viongozi, tunapaswa tuwakimbilie Viongozi wa Dini, kupata msaada wa Kimungu, haipaswi viongozi wa dini wawakimbilie wanasiasa, wanapaswa wanasiasa wawakimbilie viongozi wa dini kwasababu kwenu ndiyo kuna usalama." - Amesema Mgombea Ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, aliposhiriki ibada katika Kanisa la Calvary Temple jijini Arusha.

27/10/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Mafinga Mjini Mkoani Iringa Kupitia CCM, Dickson Lutevele maarufu Villa, amehitimisha Kampeni zake za kuomba kura Kwa Wananchi wa Jimbo hilo, huku akiahidi kuhakikisha anatekeleza yote aliyoahidi pindi akishachaguliwa kuwa Mbunge wao.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MCC), Salim Abri Asas, ambaye pia ndiye Mratibu wa Kampeni Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika Ufungaji wa Kampeni za Kuomba kura Jimbo la Mafinga Mjini kwenye Mkutano uliofanyika Oktoba 26, 2025 katika Kijiji cha Ugute Kata ya Isalavanu Halmashauri ya Mji Mafinga Wilaya Mufindi Mkoani Iringa.

26/10/2025

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MCC), Salim Abri Asas, amewahamisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupiga kura kuwachagua viongozi ifikapo Oktoba 29, 2025, huku akiwatoa hofu na wasiwasi akisema kuwa katika siku hiyo amani itakupo, utulivu nao utakuwepo pamoja na ulinzi wa kutosha utakuwepo kwani uhakika wa mambo hayo umethibishwa na viongozi wa Serikali waliopewa mamlaka kusimamia Vyombo vya Ulinzi na Usalama.

MCC Salim Asas, ametoa wito huo Oktoba 26, 2025, alipokuwa mgeni rasmi kwenye mkutano wa kufunga Kampeni za CCM katika Jimbo la Mafinga Mjini, mkutano uliofanyika Kijiji cha Ugute kata ya Isalavanu Jimbo la Mafinga Mjini wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.

MCC Salim Asas, alitumia fursa hiyo kumnadi na kumombea Kura Mgombea Ubunge Jimbo la Mafinga Mjini, Dickson Lutevele (Villa), pamoja na madiwani wa kata zote zinazounda jimbo hilo, aidha, amemuombea Kura Mgombea Urais wa Tanzania Kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

26/10/2025

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MCC), Salim Abri Asas, alivyomnadi kwa Wananchi Mgombea Ubunge Jimbo la Mafinga Mjin, Dickson Lutevele maarufu Villa, kwenye Mkutano wa Kufunga Kampeni za Uchaguzi za Chama Cha Mapinduzi katika Jimbo hilo, akimtaja k**a Kijana mwema, mwenye moyo wa kujitolea, huku akisema kuwa endapo watampa ushirikiano, Jimbo hilo litakuwa na Mafanikio makubwa sana.

Mkutano wa Kufunga ramsi Kampeni hizo umefanyika Oktoba 26, 2025 katika Kijiji cha Ugute Kata ya Isalavanu Jimbo la Mafinga Mjini Wilaya ya Mufindi Mkoani Iringa.

Address

Iringa
51108

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Focus TV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category