Focus TV Tanzania

Focus TV Tanzania One of the Best Online TV Conveying Content and Adding Value for the Public Interest.

19/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amekerwa na hali ya kusuasua kwa Ujenzi na Ukamilishaji wa Kituo cha Afya katika Kijiji na Kata ya Mahuninga Tarafa ya Idodi halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambapo ametoa Maelekezo huku akiagiza wak**atwe wale Wazabuni wanaokwamisha mradi huo uliotakiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma za Afya miezi mitano iliyopita lakini mpaka Sasa umekwama katika hatua ya umaliziaji.

RC Kheri James ametoa Maelekezo na maagizo hiyo Desemba 18, 2025, katika Ziara yake ya Ukaguzi wa hali na hatua iliyofikiwa katika Ujenzi wa mradi wa Kituo hicho cha Afya.

Aidha, katika Ziara hiyo, RC Kheri James, amepata fursa ya kufanya Mkutano wa hadhara wa kuzungumza na Wananchi wa Kata ya Mahuninga pamoja na kusikiliza na kutatua kero na Changamoto zao zinazokwamisha shughuli zao na kuchelewesha Maendeleo.

19/12/2025

Jibu la Billnas 🤗🙌

Kuna namna hii picha ya Alikamwe na profile ya Hasheem Ibwe zinawavuruga wanasimba, picha ya Alikamwe kila ikionekana ni...
18/12/2025

Kuna namna hii picha ya Alikamwe na profile ya Hasheem Ibwe zinawavuruga wanasimba, picha ya Alikamwe kila ikionekana ni lazima kuna jambo limevuja kwenye uongozi wa Simba, na profile ya Ibwe ni maneno ya utani ambayo ameyatumia k**a kuwakera wapinzani wake Simba Sc baada ya kuwafunga Goli 2-0 kwenye mwendelezo wa mchezo wa ligi kuu ya NBC.

Dondosha Comment kipi kinakukera zaidi kati ya hizi picha mbili?😂🙌

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amekerwa na hali ya kusuasua kwa Ujenzi na Ukamilishaji wa Kituo cha Afya katika Ki...
18/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amekerwa na hali ya kusuasua kwa Ujenzi na Ukamilishaji wa Kituo cha Afya katika Kijiji na Kata ya Mahuninga Tarafa ya Idodi halmashauri ya Wilaya ya Iringa, ambapo ametoa Maelekezo huku akiagiza wak**atwe wale Wazabuni wanaokwamisha mradi huo uliotakiwa kukamilika na kuanza kutoa huduma za Afya miezi mitano iliyopita lakini mpaka Sasa umekwama katika hatua ya umaliziaji.
👇

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amekerwa na hali ya kusuasua kwa Ujenzi na Ukamilishaji wa Kituo cha Afya katika Kijiji na Kata ya Mahuninga Tarafa ya I...

17/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, ametoa siku 7 huduma ya maji isogezwe kwenye mradi wa Vijana mkoani humo.

RC Kheri James ametoa maelekezo hayo Desemba 17, 2025, alipotembelea shamba Darasa la uzalishaji miche bora ya parachichi linaloendeshwa na kikundi cha vijana 30 chini ya mradi wa SET (Skills for Employment Tanzania) kwa kushirikiana na 360 Connect.

17/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James, amesema zao la Parachichi ni Dhahabu ya ukanda wa Nyanda za Juu Kusini, hivyo kwa kutambua hilo, Serikali inaendelea kutoa ushirikiano kwa wadau wa maendeleo katika sekta ya kilimo ili kukuza fursa hiyo inayolenga kuchochea ukuaji wa uchumi wa mwananchi mmoja mmoja.

"tunalo jukumu la msingi, Serikali pamoja na wadau kuendelea kuimarisha ule myororo wa thamani kutoka shambani mpaka sokoni ili kila aliyeshiriki katika kilimo aweze kunufaika"

RC Kheri James ameyabainisha hayo Desemba 17, 2025, alipotembelea shamba Darasa la uzalishaji miche bora ya parachichi linaloendeshwa na kikundi cha vijana 30 chini ya mradi wa SET (Skills for Employment Tanzania) kwa kushirikiana na 360 Connect.

17/12/2025

Msemaji Mkuu Wa Serikali Gerson Msigwa amesema uwepo wa goli la mama kwenye mashindano ya AFCON 2027 Morocco utavunja rekodi kubwa ikiwa ni pamoja na kutoa zawadi kwa wachezaji wa Taifa Stars, huku akiweka wazi malengo ya Tanzania kwenye mashindano hayo ya mwaka huu kwamba ni kupata alama zaidi ya zile ilizopata kwenye fainali zilizopita.

Klabu ya Azam FC imejiunga rasmi na Chama cha Umoja wa Vilabu Barani Afrika ‘African Club Association’ ACA kinachoongozw...
17/12/2025

Klabu ya Azam FC imejiunga rasmi na Chama cha Umoja wa Vilabu Barani Afrika ‘African Club Association’ ACA kinachoongozwa na Rais wake Eng.Hersi Said ambaye ni Rais wa Yanga.

Azam inakuwa klabu ya pili kutoka nchini Tanzania kujiunga na chama hicho baada ya Yanga kuwa klabu ya kwanza kujiunga na Chama hicho huku mpaka sasa vikiwa ni vilabu viwili tu kutoka Tanzania ambavyo vimetangaza kujiunga na kuwa mwanachama wa African Clubs Association (ACA).

Mchezaji wa klabu ya Simba, Sc Jonathan Sowah amepewa adhabu ya kutoshiriki michezo mitano ya ligi kuu pamoja na faini y...
16/12/2025

Mchezaji wa klabu ya Simba, Sc Jonathan Sowah amepewa adhabu ya kutoshiriki michezo mitano ya ligi kuu pamoja na faini ya Shilingi milioni moja (1,000,000), Sowah amepewa adhabu hiyo kufuatia tukio la utovu wa nidham dhidi ya mchezaji wa Azam Himid Mao.

Klabu ya Simba Sc kwa kushirikiana na JayRutty wametoa ofa ya punguzo la bei ya jezi zake katika kipindi hiki cha msimu ...
16/12/2025

Klabu ya Simba Sc kwa kushirikiana na JayRutty wametoa ofa ya punguzo la bei ya jezi zake katika kipindi hiki cha msimu wa sikukuu ya Christmas na Mwaka Mpya ambapo jezi zote za klabu hiyo sasa zitauzwa kwa Tsh 12000 tofauti na Tsh Tsh. 45,000 ilivyokuwa inafahamika.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo Desemba 16, 2025 na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ahmed Ally amesema bei hiyo ya punguzo ni kwa siku 45 kuanzia leo Desemba 16, 2025 hadi Januari 30, 2026 na kubainisha kwamba klabu hiyo inalenga kwenda na kasi ya dunia huku akiongeza kuwa inaendelea kupambana na jezi feki.

“Tuko hapa kuwatangazia Wanasimba wote Tanzania na duniani kwamba tumetoa punguzo la bei ya jezi kutoka Tsh. 45,000 hadi Tsh. 12,000. Ofa hii ya sikukuu ni kwa jezi zote, za ligi, za kimataifa na za watoto. Jezi za watoto zimetoka na sasa zinapatikana madukani.”- Ahmed Ally.

“Pamoja na kwamba tunatoa punguzo la msimu wa sikukuu lakini pia tunapambana na jezi fake. K**a Mwanasimba alikuwa ananunua jezi fake Tsh. 15,000 sasa jezi original ataipata kwa Tsh. 12,000. Uamuzi ni kwako Mwanasimba.”- Ahmed Ally

“Bei hii ya punguzo inaanza leo Desemba 16, 2025 na itakwenda hadi Januari 30, 2026 hivyo tuna siku 45 za ofa hii. Na kuna watu wanakwenda nyumbani sikukuu, usikubali kwenda mikono mitupu, nunua jezi za Simba uende na zawadi.”- Ahmed Ally.

16/12/2025

ambo za Ally Kamwe mbele ya Ahmed Ally kuelekea kwenye mechi ya mashabiki wa Simba na Yanga Disemba 21, Huu utani sasa umefikia pabaya😂

Why "UTAMU"

Address

Iringa
51108

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Focus TV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category