03/01/2026
Mbwana Samatta ambaye ni nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) amefunguka kuelekea Mchezo wa hatua ya mtoano dhidi ya wenyeji Morocco akisema kuwa Morocco ni timu kubwa na ina wachezaji wakubwa wenye uwezo wa kubadirika kulingana na timu pinzani wanayokutana nayo, ambapo ameeleza kuwa licha ya Ukubwa wa wachezaji wa Timu hiyo, wao wamejiandaa kukabiliana nao.
"Muda wote ambao nimecheza kwenye kikosi cha timu ya Taifa, nimeshakutana na Morocco si chini ya mara Tano mara sita, nadhani tukifikiri kwamba Morocco ambayo tumekutana nayo kwenye Michuano ya Qualification ya World Cup itakuwa ndio Morocco ambayo tutakutana nayo kesho, itakuwa ni Uongo"
"Hizi ni timu kubwa, Zina wachezaji wakubwa na Wanabadirika kadiri siku zinavyozidi kwenda na mechi by mechi"
"kwahiyo, tumewaona kwenye Michezo yao ya makundi, mwalimu ametengeneza details ambazo zitaisaidia timu Kwa ajili ya Mchezo wa kesho na tunatarajia mabadiriko ya kiuchezaji pia kwasababu Morocco ni timu ambayo inauwezo wa kubadirika pale inapocheza na mpinzani wa aina fulani"
"sisi tunajiandaa kukabiliana nayo kulingana na wachezaji wa Morocco watakavyokuja Kwa siku ya Kesho" - Amesema Samatta wakati akizungumza katika mahojiano Maalum Kupitia BBC.