26/10/2025
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MCC), Salim Abri Asas, amewahamisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la kupiga kura kuwachagua viongozi ifikapo Oktoba 29, 2025, huku akiwatoa hofu na wasiwasi akisema kuwa katika siku hiyo amani itakupo, utulivu nao utakuwepo pamoja na ulinzi wa kutosha utakuwepo kwani uhakika wa mambo hayo umethibishwa na viongozi wa Serikali waliopewa mamlaka kusimamia Vyombo vya Ulinzi na Usalama.
MCC Salim Asas, ametoa wito huo Oktoba 26, 2025, alipokuwa mgeni rasmi kwenye mkutano wa kufunga Kampeni za CCM katika Jimbo la Mafinga Mjini, mkutano uliofanyika Kijiji cha Ugute kata ya Isalavanu Jimbo la Mafinga Mjini wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
MCC Salim Asas, alitumia fursa hiyo kumnadi na kumombea Kura Mgombea Ubunge Jimbo la Mafinga Mjini, Dickson Lutevele (Villa), pamoja na madiwani wa kata zote zinazounda jimbo hilo, aidha, amemuombea Kura Mgombea Urais wa Tanzania Kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.