Focus TV Tanzania

Focus TV Tanzania One of the Best Online TV Conveying Content and Adding Value for the Public Interest.

‎Mbwana Samatta ambaye ni nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) amefunguka kuelekea Mchezo wa hatua ya mtoa...
03/01/2026

‎Mbwana Samatta ambaye ni nahodha wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) amefunguka kuelekea Mchezo wa hatua ya mtoano dhidi ya wenyeji Morocco akisema kuwa Morocco ni timu kubwa na ina wachezaji wakubwa wenye uwezo wa kubadirika kulingana na timu pinzani wanayokutana nayo, ambapo ameeleza kuwa licha ya Ukubwa wa wachezaji wa Timu hiyo, wao wamejiandaa kukabiliana nao.

‎"Muda wote ambao nimecheza kwenye kikosi cha timu ya Taifa, nimeshakutana na Morocco si chini ya mara Tano mara sita, nadhani tukifikiri kwamba Morocco ambayo tumekutana nayo kwenye Michuano ya Qualification ya World Cup itakuwa ndio Morocco ambayo tutakutana nayo kesho, itakuwa ni Uongo"

‎"Hizi ni timu kubwa, Zina wachezaji wakubwa na Wanabadirika kadiri siku zinavyozidi kwenda na mechi by mechi"

‎"kwahiyo, tumewaona kwenye Michezo yao ya makundi, mwalimu ametengeneza details ambazo zitaisaidia timu Kwa ajili ya Mchezo wa kesho na tunatarajia mabadiriko ya kiuchezaji pia kwasababu Morocco ni timu ambayo inauwezo wa kubadirika pale inapocheza na mpinzani wa aina fulani"

‎"sisi tunajiandaa kukabiliana nayo kulingana na wachezaji wa Morocco watakavyokuja Kwa siku ya Kesho" - Amesema Samatta wakati akizungumza katika mahojiano Maalum Kupitia BBC.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameizawadia timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) k...
03/01/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameizawadia timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kiasi cha shilingi milioni 500 kufuatia kufanikiwa kufuzu hatua ya 16 bora katika michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON).

Taarifa hiyo imetolewa Januari 03, 2026 na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mwigulu Nchemba, wakati akizungumza na wachezaji pamoja na benchi la ufundi la Taifa Stars kwa njia ya simu kupitia kwa Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda.

Waziri Mkuu Dkt. Nchemba amesema kuwa, Rais Samia amewapongeza wachezaji, benchi la ufundi pamoja na Watanzania wote kwa mafanikio hayo ya kihistoria na kusisitiza kuwa serikali itaendelea kuwaunga mkono timu hiyo.

Aidha, Waziri Mkuu ameongeza kuwa, Rais Samia ameahidi kutoa zawadi nono zaidi endapo Taifa Stars itaendelea kufanya vizuri na kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo inayoendelea nchini Morocco.

‎Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema limefanyika Shambulizi kubwa kwenye Mji wa Caracas Nchini Venezuela, huku akiel...
03/01/2026

‎Rais wa Marekani, Donald Trump, amesema limefanyika Shambulizi kubwa kwenye Mji wa Caracas Nchini Venezuela, huku akieleza kuwa Rais wa Venezuela Nicolas Maduro na mkewe wamek**atwa na Marekani baada ya shambulizi hilo.

‎Hayo yamebainishwa Kupitia chapisho kwenye mtandao wake wa kijamii wa Truth Social, ambapo Rais huyo wa Marekani alithibitisha uwepo wa shambulizi kubwa lililofanyika kwenye mji mkuu wa Venezuela wa Caracas na kwamba Maduro na mkewe wamek**atwa na wamesafishwa kutolewa nje ya nchi hiyo.

‎"The United States of America has successfully carried out a large scale strike against Venezuela and its leader, President Nicolas Maduro, who has been, along with his wife, captured and flown out of the Country. This operation was done in conjunction with U.S. Law Enforcement. Details to follow. There will be a News Conference today at 11 A.M., at Mar-a-Lago. Thank you for your attention to this matter! President DONALD J. TRUMP"

‎Hali ya hatari ya kitaifa imetangazwa nchini Venezuela kufuatia shambulizi lililotokea katika Mji wa Caracas asubuhi mapema Jumamosi ya Januari 03, 2026.

‎Venezuela imetoa taarifa ikishutumu uchokozi mbaya sana wa kijeshi unaofanywa na Serikali ya sasa ya Marekani dhidi ya eneo la Venezuela.

📸 Truth Social, NBC News, BBC

03/01/2026

Mwanaume Akinipa Laki 5 lazima Afiwe 🙄 Umesikia au Tuongeze Sauti? 🫴

Video: Arise and Shine TV

K**a kungekuwa na Tuzo ya Mbunge wa Ndani wa Kufungulia Mwaka 2026, ingeenda Moja Kwa Moja Kwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma...
03/01/2026

K**a kungekuwa na Tuzo ya Mbunge wa Ndani wa Kufungulia Mwaka 2026, ingeenda Moja Kwa Moja Kwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Cleyton Revocatus Chipando (Baba Levo), kwanza amefanya Mapinduzi makubwa ya Status kutoka kuitwa Chawa na Sasa anaitwa Mheshimiwa, ambapo siku ya Kwanza Bungeni alijitambulisha kwamba yeye ni Mbunge aliyeangusha Mbuyu Jimboni kwake.

Kwanini Tuzo: Baba Levo ndani ya muda mfupi amefanya mambo mengi ya Kimkakati sana katika Jimbo lake kiasi cha kuvuka mategemeo na matarajio ya Wananchi Jimboni kwake na Mashabiki zake kwenye Mitandao ya Kijamii kote Nchini, kiufupi hawakutarajia kuona akitekeleza ahadi na harakati Nyingi zenye Tija Kwa Wananchi wa Jimbo lake kwa haraka kiasi kile jambo linalozidi kumuongezea alama Nyingi za kukubalika na kuaminika kwani ni hii ni Awamu yake ya Kwanza anakuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Ndani ya muda mfupi tangu Kuapishwa Rasmi kuwa Mbunge, Baba Levo ameonesha Wazi uongozi wa kushirikishi na kushirikisha Wananchi katika Matukio mbalimbali, Kiongozi anayezingatia matokeo yanayoonekana kwa macho kuvuna Imani ya Wananchi, kiongozi anayewajali na anayezungumza lugha ya Wananchi, na Kiongozi mwenye uwezo wa kuwashawishi na kuwaunganisha Wadau kujitolea kutatua Changamoto za Wananchi ikiwa ni Sehemu ya kurudisha Kwa Jamii.

Mbunge wa Jimbo gani anastahili Tuzo k**a ya Baba Levo?

✍️

🕺

03/01/2026

Shabiki wa Congo Ageuka Kivutio AFCON akiigiza Patrice Lumumba.

‎Christian Bella ambaye ni Msanii wa Muziki wa Rhumba mwenye asili ya Congo, baada ya kupata rasmi Uraia wa Tanzania Mwi...
03/01/2026

‎Christian Bella ambaye ni Msanii wa Muziki wa Rhumba mwenye asili ya Congo, baada ya kupata rasmi Uraia wa Tanzania Mwishoni mwa Mwaka 2025, alisema kuwa hilo ni jambo kubwa sana kwake Binafsi kwasababu ameishi Tanzania Kwa miaka mingi zaidi kuliko Congo.

‎"Nilikuja Tanzania nikiwa na miaka 17, nimeishi hapa zaidi ya miaka 20, hivyo hapa ndio Nyumbani, Tanzania imenilea, Tanzania ndio imefanya watu wajue Christian Bella ni nani. Duniani kote naenda na natambulika k**a mwanamuziki kutoka Tanzania hata k**a wanajua huyu ni Mkongo, lakini wanajua huyu Msanii anatokea Tanzania, anatangaza lugha ya Kiswahili, anaimba kiswahili, anaishi Tanzania, kwahiyo ninapoenda nje au popote pale natambulika k**a Msanii kutoka Tanzania. Kwahiyo ulikuwa wakati wa Mungu nipate Uraia rasmi wa Tanzania"

Hayo yalisemwa na Christian Bella the King of the Best Melodies siku chache baada ya kupata Uraia rasmi wa Tanzania.


Chief GodLove anasema unaweza kumpa msanii mkataba wa kumsimamia, ukampa nyumba na gari na kumpa sharti asivute bangi, l...
03/01/2026

Chief GodLove anasema unaweza kumpa msanii mkataba wa kumsimamia, ukampa nyumba na gari na kumpa sharti asivute bangi, lakini msanii anajibu kuwa hawezi kuacha Bangi.

Chief Godlove aliyaeleza hayo wakati wa mahojiano kupitia East Afrika Radio.

Ujumbe huo ni tafsiri ya kwamba kuna watu wana vipaji na uwezo mzuri lakini wanakwama kuviendeleza au kushindwa kupata msaada wa kushikwa mkono, kutokana na vitu au tabia ambazo hawawezi kuziacha.

Hii sio kwa Wasanii tu.

Mtazamo wako ni Upi?

02/01/2026

"Dunia yote inasubiri kusikia Morocco imetolewa na Tanzania AFCON 2025 Nyumbani kwao" - Makonda.

02/01/2026

Hamasa ya Serikali imechangia Taifa Stars kufuzu kuelekea 16 Bora ya Michuano ya Fainali za AFCON.

02/01/2026

Ibrahim Bacca na Feisal Salum (Feitoto), ni wachezaji waliofanya vizuri kwenye Mchezo wa Taifa Stars dhidi ya Tunisia.

Address

Iringa
51108

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Focus TV Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category