Shamba Fm Radio

Shamba Fm Radio Official Page of Shamba Fm Radio. Sikiliza Live Online www.shambafm.co.tz

TRUMP ASITISHA MAHAKAMA YA ICC ISIMCHUNGUZEUtawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umeitaka Mahak**a ya Kimataifa ya Uh...
11/12/2025

TRUMP ASITISHA MAHAKAMA YA ICC ISIMCHUNGUZE

Utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umeitaka Mahak**a ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita, ICC, kuachana na mipango yoyote ya kumchunguza na hata kumshtaki Rais Trump na maafisa wa utawala wake pale watakapomaliza muda wao mwaka 2029.

Utawala wa Trump umeitaka mahak**a ya ICC kufanya marekebisho katika sheria yake ya msingi ili kuhakikisha haimchunguzi wala kumshtaki Rais huyo wa Marekani hapo baadaye.

Kwa mujibu wa DW – Swahili, Afisa wa serikali ya Trump aliyezungumza kwa sharti la kutokutajwa jina amesema Utawala huo umeahidi vikwazo dhidi ya mahak**a hiyo k**a itashindwa pia kuachana na uchunguzi wa awali dhidi ya wanajeshi wa Marekani kutokana na vitendo vyao nchini Afghanistan na kesi dhidi ya viongozi wa Israel.

Mahak**a ya ICC imekuwa ikikosolewa mara nyingi kwa kuwalenga zaidi viongozi wa Afrika pekee huku mfumo wa uendeshaji wake ambao umekuwa ukiwaogopa viongozi wa mataifa makubwa ukinyooshewa vidole na hivyo kuifanya mahak**a hiyo kukosa uhalali wa sababu za kuanzishwa kwake.

Uamuzi huu wa Trump ni ushahidi mwingine kwamba mahak**a hii imekuwa ikitumika kwa ajili ya malengo fulani mahsusi na siyo kutafuta haki k**a inavyodhaniwa na wengi



SPIKA ATANGAZA KIFO CHA MBUNGE JENISTA MHAGAMASpika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu (Mb),...
11/12/2025

SPIKA ATANGAZA KIFO CHA MBUNGE JENISTA MHAGAMA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu (Mb), ametangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Marehemu Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea tarehe 11 Desemba 2025 jijini Dodoma.

Katika taarifa hiyo, Spika ametoa pole kwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Peramiho, akisisitiza kuwa Bunge linaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, Amehimiza umoja, uvumilivu na subira wakati wote wa msiba huu mzito.

Ofisi ya Bunge imethibitisha kuwa itashirikiana kikamilifu na familia ya marehemu katika kupanga na kuratibu taratibu zote za mazishi, huku taarifa zaidi zikiendelea kutolewa kadiri maandalizi yanavyoendelea.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amina.

SPIKA ATANGAZA KIFO CHA MBUNGE JENISTA MHAGAMASpika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu (Mb),...
11/12/2025

SPIKA ATANGAZA KIFO CHA MBUNGE JENISTA MHAGAMA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu (Mb), ametangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Marehemu Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea tarehe 11 Desemba 2025 jijini Dodoma.

Katika taarifa hiyo, Spika ametoa pole kwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na wananchi wa Jimbo la Peramiho, akisisitiza kuwa Bunge linaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, Amehimiza umoja, uvumilivu na subira wakati wote wa msiba huu mzito.

Ofisi ya Bunge imethibitisha kuwa itashirikiana kikamilifu na familia ya marehemu katika kupanga na kuratibu taratibu zote za mazishi, huku taarifa zaidi zikiendelea kutolewa kadiri maandalizi yanavyoendelea.

Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi. Amina.



TYSON NA MAYWEATHER KUZICHAPA MACHI MWAKANIMkongwe wa ndondi wa Marekani Mike Tyson ametangaza kuwa pambano lake la maon...
10/12/2025

TYSON NA MAYWEATHER KUZICHAPA MACHI MWAKANI

Mkongwe wa ndondi wa Marekani Mike Tyson ametangaza kuwa pambano lake la maonesho na Floyd Mayweather Jr litafanyika barani Afrika mnamo mwezi Machi Mwaka 2026.

Tyson alithibitisha eneo na muda katika tukio la moja kwa moja, akisema itakuwa mwezi Machi na itakuwa Afrika huku akiongeza huenda Itakuwa ajabu na itavunja rekodi zote.

Nguli huyo mwenye umri wa miaka 59 atazichapa na Mayweather wanaopishana umri wa Miaka 11 ambapo Floyd ana umri wa Miaka 48 kwa sasa.

Je, unampa nani ushindi kati yao?

Kipindi cha michezo  “Viwanja 360” kipo hewani muda huu.Unatufuatilia kutokea wapi?Cc:
10/12/2025

Kipindi cha michezo “Viwanja 360” kipo hewani muda huu.

Unatufuatilia kutokea wapi?

Cc:



Leo tunasherehekea miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika safari ya uthubutu, umoja na moyo wa kizalendo. Heri ya Siku ya Uhuru...
08/12/2025

Leo tunasherehekea miaka 64 ya Uhuru wa Tanganyika safari ya uthubutu, umoja na moyo wa kizalendo.
Heri ya Siku ya Uhuru Tanzania!



KADI ZA NJANO 92 ZATOLEWA LIGI KUU NBCKwa mujibu wa Shirika la takwimu za michezo nchini Tanzania LiveBall, limesema kuw...
08/12/2025

KADI ZA NJANO 92 ZATOLEWA LIGI KUU NBC

Kwa mujibu wa Shirika la takwimu za michezo nchini Tanzania LiveBall, limesema kuwa hadi kufikia sasa Ligi Kuu ya NBC imefikisha kadi za njano 92 katika mechi zote zilizochezwa.

Klabu ya JKT Tanzania ndiyo klabu iliyoongoza katika takwimu hizo mara baada ya kupata kadi za njano 22 ikifuatiwa na Namungo yenye kadi za njano 14 huku Fountain Gate ikiwa na kadi za njano 12.

Hata hivyo, mchezaji kutoka Klabu ya Mbeya City Adilly Buha ndiye anayeongoza, mpaka sasa tayari ameoneshwa kadi za njano nne.

JKT TANZANIA HAIKAMATIKI LIGI KUU UPIGAJI PASI Klabu ya JKT Tanzania hadi sasa ndiyo klabu inayoongoza kupiga pasi kulik...
08/12/2025

JKT TANZANIA HAIKAMATIKI LIGI KUU UPIGAJI PASI

Klabu ya JKT Tanzania hadi sasa ndiyo klabu inayoongoza kupiga pasi kuliko timu yoyote mara baada ya kupiga pasi 3061.

JKT imepiga pasi hizo baada ya kucheza mechi 10 ikikusanya alama 17 huku ikiwa kinara wa ligi kuu ya Tanzania.

Timu nyingine zilizopiga pasi nyingi Ligi kuu ya NBC Tanzania bara ni,

Fountain Gate, pasi 2749
Young Africans, pasi 2714
Simba, pasi 2476
Mbeya City, pasi 2394

Kipindi cha michezo “VIWANJA 360” kipo hewanj muda huu.Unatufuatilia ukiwa wapi? Cc:
05/12/2025

Kipindi cha michezo “VIWANJA 360” kipo hewanj muda huu.

Unatufuatilia ukiwa wapi?

Cc:



SHETTA MEYA MPYA WA DARMadiwani wa Jiji la Dar es Salaam wamempitisha Diwani wa Mchikichini, Nurdin Juma maarufu k**a Sh...
04/12/2025

SHETTA MEYA MPYA WA DAR

Madiwani wa Jiji la Dar es Salaam wamempitisha Diwani wa Mchikichini, Nurdin Juma maarufu k**a Shetta, kuwa Meya mpya wa Jiji la Dar es Salaam, nafasi anayochukua kutoka kwa Omary Kumbilamoto aliyemaliza muda wake wa uongozi wa miaka minne.

Katika uchaguzi huo, Shetta alipata kura 48 za ndiyo kati ya wajumbe 51, akionesha uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa madiwani, Sambamba na hilo, John Mrema alichaguliwa kuwa Naibu Meya baada ya kupata kura 49 za ndiyo.

Hii inakuja baada ya Shetta kushinda kura za maoni ndani ya CCM kwa nafasi hiyo, akiwashinda wagombea wenzake katika uchaguzi uliofanyika kwenye Ukumbi wa CCM Wilaya ya Ilala ambapo alipata kura 25 dhidi ya 21 za mpinzani wake, Robert Manangwa.

Shetta, ambaye ni msanii wa Bongo Fleva aliyewahi kung’ara kupitia kundi la MISIFA CAMP chini ya Dully Sykes, sasa anaingia rasmi kwenye majukumu ya kuliongoza Jiji la Dar es Salaam.



Address

Utalii Road
Iringa

Telephone

+255715729000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shamba Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shamba Fm Radio:

Share

Category