Shamba Fm Radio

Shamba Fm Radio Official Page of Shamba Fm Radio. Sikiliza Live Online www.shambafm.co.tz

PAMBE ZA SHAMBA | JUMAMOSI HII! Je, madhara ya presha ya ndoa kwa vijana ni yapi? Presha ya kuoa au kuolewa mapema inawe...
14/08/2026

PAMBE ZA SHAMBA | JUMAMOSI HII!

Je, madhara ya presha ya ndoa kwa vijana ni yapi? Presha ya kuoa au kuolewa mapema inaweza kuathiri vipi maamuzi, mahusiano na maisha ya kijana?

Jumamosi hii, tunakutana kwenye Pambe za Shamba na Dkt. Leonard Mgina, Mtaalamu wa Saikolojia, kwa mazungumzo maalum yatakayogusa changamoto zinazowakabili vijana katika mahusiano na ndoa.

🗓️ Jumamosi, Agosti 15, 2026
⏰ Saa 4:00 asubuhi – 7:00 mchana
đź“» 88.5 Shamba FM

Usikose! Sikiliza, uliza swali na shiriki mtazamo wako.
Kwa pamoja tujenge uelewa bora kuhusu mahusiano na ndoa.




13/08/2026

WACHEZAJI HAWA TUWAITE MATAPELI AU NDIO VIWANGO VIBOVU?

Zipo baadhi ya sajili ziliwahi kufanyika kwenye ligi kuu ya Tanzania kwa nyakati tofauti na kuacha watu midomo wazi baada ya viwango vyao kuwa vibovu kwenye timu walizocheza.

Misimu kadhaa nyuma Azam FC waliwahi kumsajili mchezaji aliyefahamika k**a Allasane Diao kiwango chake kilikuwa gumzo ambapo ndani ya miaka miwili mchezaji huyu hakuwahi kufikisha magoli 10 ndani ya timu.

Mbali na hilo Simba mwaka 2022 waliwahi kumsajili Djan Georgijevic ambaye alidumu kwa miezi miwili tu huku akifunga goli moja tu na kuvunja mkataba na klabu ya Simba.

Ungana na mwana michezo wetu Stuaty Mohamed kwa orodha ya wachezaji wengine waliowahi kupita kwenye ligi kuu Tanzania na wakaonekana kuwa na viwango vibovu.




13/08/2026

USHINDANI WA MAKOCHA WAAHAMIA TIMU ZA TAIFA

Baada ya kumalizika kwa Kombe la Dunia 2026, ushindani wa makocha umehamia kwenye timu za taifa kubwa barani Ulaya. Uholanzi imemteua Xavi Hernandez kuwa kocha mpya kwa mkataba hadi 2030, akichukua nafasi ya Ronald Koeman.

Ujerumani nayo imemkabidhi mikoba JĂĽrgen Klopp, aliyesaini mkataba wa miaka minne baada ya Julian Nagelsmann kuondoka kufuatia matokeo ya Kombe la Dunia.

Kwa upande wa Ureno, Jorge Jesus amechukua nafasi ya Roberto Martinez, huku Ufaransa ikimpa Zinedine Zidane mkataba wa miaka minne hadi Kombe la Dunia 2030, akirithi mikoba ya Didier Deschamps.




MAFANIKO YAKE KATIKA KILIMO! Kilimo si jembe tu… ni maarifa, ubunifu, uvumilivu na matokeo! Kesho ndani ya KIVULINI tuna...
13/08/2026

MAFANIKO YAKE KATIKA KILIMO!

Kilimo si jembe tu… ni maarifa, ubunifu, uvumilivu na matokeo!

Kesho ndani ya KIVULINI tunakutana na Marko Barnaba Mjujulu, Mkubwa Bora Mkoa wa Iringa katika Kundi la Wakulima wa Mazao ya Nafaka, Mizi na Mikunde.

🎙️ Mada: MAFANIKO YAKE KATIKA KILIMO
đź“… 13 Agosti 2026
⏰ Saa 10:00 – 11:00 Jioni
📻 88.5 Shamba FM – Kilimo ni Maisha

Ungana nasi usikose kusikia safari yake, changamoto, mbinu na siri za mafanikio katika kilimo.




Kuelekea Mchezo wa Dabi ya Kariakoo kati ya Yanga na Simba utakaopigwa Leo Agosti 12, 2026 kwenye dimba la New Amaan Zan...
12/08/2026

Kuelekea Mchezo wa Dabi ya Kariakoo kati ya Yanga na Simba utakaopigwa Leo Agosti 12, 2026 kwenye dimba la New Amaan Zanzibar hili ndio jopo la wachambuzi wataohusika katika Mechi hiyo.

Ungana na Shamba Fm ili uwe sehemu ya kupata uchambuzii huo kuanzia Majira ya saa 12 Jioni pamoja na Mchezo kusika kuanzia Saa 2:30 Usiku




Wakati huku wanasema “Tuliwaambia anafanya mazoezi na timu ndogo, anakuja kuanza msimu na Klabu Kubwa” kuleee wanasema P...
12/08/2026

Wakati huku wanasema “Tuliwaambia anafanya mazoezi na timu ndogo, anakuja kuanza msimu na Klabu Kubwa” kuleee wanasema PESA ZIKO BENKI.

Leo hakuna suluhu wala sare ni mpaka bingwa apatikane katika mtanange wa watani wa jadi unaohusisha Vilabu vikubwa zaidi kutoka Kariakoo jijini Dar es salaam hapa ni Simba kule ni Yanga katika mchezo wa Ngao ya jamii.

Mchezo huo wa ufunguzi wa Ligi utapigwa majira ya saa 20:45 usiku visiwani Zanzibar ambapo tutakuleta matangazo mubashara ya mechi hiyo kutoka Shambani.




11/08/2026

SHERIA YA NDOA NA SERA YA ELIMU VINAKINZANA




Usikose mahojiano maalumu na muandishi wa habari za michezo kutoka Afrika Kusini Ayabonga Mthembu leo kupitia Shamba La ...
11/08/2026

Usikose mahojiano maalumu na muandishi wa habari za michezo kutoka Afrika Kusini Ayabonga Mthembu leo kupitia Shamba La Bibi ya Shamba Fm.

Ni kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 2:00 usiku




NDOA KWANZA AU FEDHA KWANZA?Katika kizazi cha sasa, kuna swali ambalo limekuwa likizua mijadala mikubwa, hasa miongoni m...
11/08/2026

NDOA KWANZA AU FEDHA KWANZA?

Katika kizazi cha sasa, kuna swali ambalo limekuwa likizua mijadala mikubwa, hasa miongoni mwa vijana “Mtu anapaswa kuoa au kuolewa akiwa na umri gani?”

Wapo wanaoamini kuwa ndoa haipaswi kusubiriwa sana. Kwamba ni bora watu wawili wanaopendana kuanza maisha pamoja, kujenga nyumba yao taratibu na kutafuta mafanikio wakiwa pamoja.

Lakini upande mwingine unasema, “Mapenzi pekee hayatoshi,” Kabla ya kuingia kwenye ndoa, mtu anapaswa kuwa na uwezo wa kujitegemea, kufikiri kwa ukomavu na angalau kuwa na msingi wa kifedha wa kuendesha maisha ya familia.

Hapo ndipo swali jingine linapokuja,

Fedha kwanza, ndoa baadaye? Au ndoa kwanza, fedha zikafuata?

Ukweli ni kwamba, hakuna jibu moja linaloweza kuwafaa watu wote.

Ndoa si suala la umri pekee wala fedha pekee, Ni safari inayohitaji utayari wa moyo, ukomavu wa fikra, uwajibikaji, uvumilivu, heshima na uwezo wa watu wawili kukabiliana na maisha pamoja.

Fedha ni muhimu, lakini kuwa na fedha hakumaanishi moja kwa moja kwamba mtu yuko tayari kwa ndoa, Vivyo hivyo, kuwa na umri mkubwa hakumaanishi mtu ana ukomavu wa kujenga familia.

Kwa hiyo, kabla hujauliza “nitaoa lini?” au “nitaolewa lini?” jiulize kwanza: Niko tayari kwa safari hii?

Kwa sababu mwisho wa siku, umri ni namba, fedha ni nyenzo, lakini utayari ndio msingi wa ndoa.

Wewe unaonaje? Ndoa kwanza, fedha baadaye au fedha kwanza, ndoa baadaye?




Address

Utalii Road
Iringa

Telephone

+255715729000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shamba Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shamba Fm Radio:

Shortcuts

Share

Category