Shamba Fm Radio

Shamba Fm Radio Official Page of Shamba Fm Radio. Sikiliza Live Online www.shambafm.co.tz

PICHA 10  RC JAMES NDANI YA IRINGA DREAM CAR FESTIVAL.Hizi hapa picha 10 za Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James katika Ta...
23/08/2025

PICHA 10 RC JAMES NDANI YA IRINGA DREAM CAR FESTIVAL.

Hizi hapa picha 10 za Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James katika Tamasha la Iringa Dream Car Festival lililofanyika Leo Agosti 23, 2025 Wilaya Kilolo Mkoani Iringa

Cc:

📸

SHAMBA FM YADHAMINI IRINGA DREAM CAR FESTIVAL Shamba fm redio ni moja  Kati ya wadhamini waliofanikisha tukio la Iringa ...
23/08/2025

SHAMBA FM YADHAMINI IRINGA DREAM CAR FESTIVAL

Shamba fm redio ni moja Kati ya wadhamini waliofanikisha tukio la Iringa Dream Car Festival lililofanyika leo Agosti 23 2025 Wilayani Kilolo.

Na haya ni matukio mbalimbali ya Picha yakimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Iringa Kheri James pamoja na Meneja wa Shamba Fm Laurian Deogratus katika tamasha hilo .

Cc:

📸



TANZANIA SAMIA CONNECT YAFANA Watu wamejitokeza kwa wingi mkoani Arusha katika mbio za Jogging pamoja na mazoezi ya viun...
23/08/2025

TANZANIA SAMIA CONNECT YAFANA

Watu wamejitokeza kwa wingi mkoani Arusha katika mbio za Jogging pamoja na mazoezi ya viungo ikiwa ni sehemu ya kilele cha tamasha la Tanzania Samia Connect

Mazoezi hayo yaliyofanyika leo agost 23 2025 yameanzia katika uwanja wa mgambo na kutamatikia Uzunguni eneo ambalo kilele cha tamasha hilo kitafanyikia .

Tanzania samia Connect imeasisiwa na mkuu wa mkoa wa arusha Kenani Laban Kihongosi lenye lengo la kuyasherekea mafanikio yaliyopatikana mkoani Arusha katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan

Picha za magari mbalimbali yaliyoshiriki Iringa Dream Car Festival Leo Agosti 23, 2025 katika msafara unaoelekea katika ...
23/08/2025

Picha za magari mbalimbali yaliyoshiriki Iringa Dream Car Festival Leo Agosti 23, 2025 katika msafara unaoelekea katika Viwanja vya IOP Wilaya Kilolo ndani ya Mji Mdogo wa Ilula 📷

BODI YA TOSCI YAAGIZWA KUSIMAMIA MIKAKATI TASNIA YA MBEGUWaziri wa Kilimo Hussein Bashe ameisisitiza Bodi mpya ya Wakuru...
22/08/2025

BODI YA TOSCI YAAGIZWA KUSIMAMIA MIKAKATI TASNIA YA MBEGU

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe ameisisitiza Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kusimamia mikakati ya usimamizi wa tasnia ya mbegu nchini na kuhakikisha inaimarisha juhudi za kuhamasisha na kuendeleza kampuni za ndani zinazojihusisha na uzalishaji wa mbegu.

Waziri Bashe ametoa msisitizo huo leo Agosti 22, 2025 jijini Dodoma, wakati akizindua rasmi Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) na kuongeza kuwa msisitizo wa kusimamia mikakati ya usimamizi itapunguza utegemezi wa mbegu kutoka katika kampuni za nje ya nchi ili kufikia malengo ya kuzalisha tani 600,000 ifikapo mwaka 2030.

Aidha, Waziri Bashe ameongeza kuwa TOSCI inajukumu la kuwalinda wakulima na kuendeleza kuongeza uzalishaji wa mbegu za asili na kuweka muongozo wa mbegu hizo hasa katika mazao ya chakula.

Sambamba na hayo, ameielekeza TOSCI kuhakikisha kuwa mkulima anaenufaika na bei ya ruzuku ni yule aliyesajiliwa na mbegu hizo ziwafikie wakulima kwa wakati.

TOSCI YAAGIZWA KUSHIRIKIANA NA TAKUKURU KUDHIBITI MBEGU FEKI NCHINITaasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) ...
22/08/2025

TOSCI YAAGIZWA KUSHIRIKIANA NA TAKUKURU KUDHIBITI MBEGU FEKI NCHINI

Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) imetakiwa kushirikiana kwa karibu na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kudhibiti uuzaji na usambazaji wa mbegu feki kwa kuwa tatizo hilo ni kubwa kwa wakulima na maendeleo ya kilimo nchini.

Agizo hilo limetolewa leo Agosti 22, 2025 na Waziri wa Kilimo nchini Hussein Bashe jijini Dodoma, wakati akizindua rasmi Bodi mpya ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI).

Waziri Bashe amesema kuwa ni lazima TOSCI na TAKUKURU waimarishe ushirikiano wao ili kuwabaini na kuwachukulia hatua kali za kisheria wahusika wote wanaojihusisha na vitendo hivyo ambavyo vinaathiri maendeleo ya kilimo kwa wakulima nchini.

Kwa mujibu wa Wizara ya kilimo, mahitaji ya mbegu bora kwa mwaka nchi Tanzania ni tani 127,650 katika mwaka 2025/2026, ambapo uzalishaji wa mbegu bora ndani ya nchi unatarajiwa kuongezeka kutoka tani 63,526.54 hadi tani 90,000 huku upatikanaji wa mbegu bora nchini unatarajiwa kuongezeka kutoka tani 79,700.62 hadi tani 105,000.

KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO AIPONGEZA TPHPAKatibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Mweli, ameipongeza Mamlaka ya Afya ya...
22/08/2025

KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO AIPONGEZA TPHPA

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Gerald Mweli, ameipongeza Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) kwa kulinda masoko ya mazao ya kilimo nje ya nchi na kusimamia kwa weledi ukaguzi wa mazao.

Akizungumza jana Agosti 21, 2025 katika ziara yake TPHPA Ngaramtoni mkoani Arusha, Mweli amesisitiza umuhimu wa taarifa za mara kwa mara kuhusu mwenendo wa biashara ya mazao na kuielekeza TPHPA kuwasilisha ripoti za kila wiki ili kusaidia kutatua changamoto na kuwaongoza wakulima kuelewa mahitaji ya masoko ya kimataifa.

Aidha, Mweli amesifu maboresho ya maabara za TPHPA yenye mashine za kisasa za kuchambua mabaki ya viuatilifu, akisema hatua hiyo imeongeza uaminifu wa mazao ya Tanzania kimataifa na kulinda afya ya walaji wa ndani.

Shamba Fm tunampongeza Meneja wetu Laurian Deogratius (DJ White)   kwa kutimiza mwaka mwingine wa maisha Tunakutakia afy...
22/08/2025

Shamba Fm tunampongeza Meneja wetu Laurian Deogratius (DJ White) kwa kutimiza mwaka mwingine wa maisha

Tunakutakia afya, baraka na mafanikio makubwa zaidi katika safari yako ya maisha na kazi.
Happy Birthday Boss 🎂 Neno moja kwakeeeee.

Baada ya kumaliza bila kufungwa katika mechi za hatua ya makundi wenyewe wanaita UNBEATEN, Timu ya Taifa ya Tanzania Tai...
22/08/2025

Baada ya kumaliza bila kufungwa katika mechi za hatua ya makundi wenyewe wanaita UNBEATEN, Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars wana kibarua cha kuvuka hatua ya robo fainali dhidi ya Timu ya Taifa ya Morocco.

Mechi hiyo inatarajiwa kupigwa leo Agosti 22, 2025 majira ya saa mbili kamili usiku k**a ilivyo kawaida huku uchambuzi ukianza saa moja na nusu.

Tuandikie maoni yako, unaiona Stars ya Morocco ikitoboa dhidi ya Morocco?

Picha za Matukio mbalimbali za Mkuu wa mkoa wa Iringa Kheri James kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo Agosti 21, 2...
21/08/2025

Picha za Matukio mbalimbali za Mkuu wa mkoa wa Iringa Kheri James kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo Agosti 21, 2025 katika viwanja vya Mwembetogwa Iringa

Cc:

📸



EAC NA COMESA WAWEKA KAMBI KUTAFUTA SULUHU SOKO LA MATUNDA NA MBOGAMBOGA – ARUSHAWadau kutoka nchi 29 wanachama wa Jumui...
21/08/2025

EAC NA COMESA WAWEKA KAMBI KUTAFUTA SULUHU SOKO LA MATUNDA NA MBOGAMBOGA – ARUSHA

Wadau kutoka nchi 29 wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) na wadau wa Jumuiya ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) wametia kambi Mkoani Arusha kwa ajili ya kujadili namna bora ya kupata suluhu juu ya soko la mbogamboga na matunda.

Akizungumza katika kikao hicho leo Agosti 21, 2025 Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Gerald Mweli amesema kukiwa na takwimu sahihi za wakulima itasaidia kupata ufumbuzi wa changamoto zao.

“Tukiweza kujua takwimu sahihi maana yake tunaweza kuwasaidia wakulima wetu vizuri, kila mkulima ambaye analima mazao ya mbogamboga lazima tujue anatumia mbegu gani, mbolea gani na afisa gani anamfikia ambapo hizi taarifa lazima ziwekwe kwenye mfumo wa pamoja”, amesema Mweli.

Mweli amesema licha ya hayo yote kujadiliwa pia wakulima waliopo nchini wana bahati kwani hayo yanaendelea wakati nchi ipo katika mkakati wa ajenda 10/30 unaofikia 2030 unaolenga kukifanya kilimo kuwa biashara.

MAPENZI YAMFANYA AMTOE ROHO MUMEWE - IRINGAMwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Elizabeth Kihombo mwenye umri wa mia...
21/08/2025

MAPENZI YAMFANYA AMTOE ROHO MUMEWE - IRINGA

Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina la Elizabeth Kihombo mwenye umri wa miaka 46 ambaye kwa sasa anapatiwa matibabu kituo cha afya cha Mdabulo amekatisha uhai wa mume wake anayefahamika kwa jina la Philimon Lalika mwenye umri wa miaka 49 kisa wivu wa mapenzi.

Akizungumza Agosti 20, 2025 Kamanda wa Polisi mkoani Iringa katika Kijiji cha Ihefu, Kata ya Mdabulo, Tarafa ya Ifwagi Wilaya ya Mufindi Mkoa wa Iringa amesema mwanaume huyo alikuwa ni mkulima na mkazi wa Kijiji hicho alichomwa na kisu tumboni na mkewe na hatimaye utumbo kutoka nje.

Tukio hilo lilitokea wakati ambapo wawili hao wakiwa wamelala na kisha kukazuka ugomvi kati yao ndipo mwanamke huyo akamuua mume wake na kisha akanywa sumu ya Organsphet ambayo ni dawa ya kuhifadhia nafaka ili na yeye afe.

Address

Utalii Road
Iringa

Telephone

+255715729000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shamba Fm Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Shamba Fm Radio:

Share

Category