11/12/2025
TRUMP ASITISHA MAHAKAMA YA ICC ISIMCHUNGUZE
Utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umeitaka Mahak**a ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita, ICC, kuachana na mipango yoyote ya kumchunguza na hata kumshtaki Rais Trump na maafisa wa utawala wake pale watakapomaliza muda wao mwaka 2029.
Utawala wa Trump umeitaka mahak**a ya ICC kufanya marekebisho katika sheria yake ya msingi ili kuhakikisha haimchunguzi wala kumshtaki Rais huyo wa Marekani hapo baadaye.
Kwa mujibu wa DW – Swahili, Afisa wa serikali ya Trump aliyezungumza kwa sharti la kutokutajwa jina amesema Utawala huo umeahidi vikwazo dhidi ya mahak**a hiyo k**a itashindwa pia kuachana na uchunguzi wa awali dhidi ya wanajeshi wa Marekani kutokana na vitendo vyao nchini Afghanistan na kesi dhidi ya viongozi wa Israel.
Mahak**a ya ICC imekuwa ikikosolewa mara nyingi kwa kuwalenga zaidi viongozi wa Afrika pekee huku mfumo wa uendeshaji wake ambao umekuwa ukiwaogopa viongozi wa mataifa makubwa ukinyooshewa vidole na hivyo kuifanya mahak**a hiyo kukosa uhalali wa sababu za kuanzishwa kwake.
Uamuzi huu wa Trump ni ushahidi mwingine kwamba mahak**a hii imekuwa ikitumika kwa ajili ya malengo fulani mahsusi na siyo kutafuta haki k**a inavyodhaniwa na wengi