17/12/2025
Kwa mujibu wa Idara ya mahak**a nchini Kenya Jaji wa Mahak**a ya Juu zaidi nchini humo Mohammed Khadhar Ibrahim amefariki dunia akiwa na Umri wa miaka 69.
Idara hiyo ya mahak**a ya nchini kenya imethibitisha kifo cha Jaji Ibrahimi kuwa kimechangiwa na hali yake ya kiafya iliyodhoofika baada ya kuugua kwa muda mrefu .
Hata hivyo Ibrahim amekuwa Jaji wa Mahak**a hiyo ya Juu tangu ilipoanzishwa kulingana na katiba mpya mwaka 2011.