Flowin vitus

Flowin vitus Journalist, Newswriter &Reporter, RedioPresenter &GraphicDesigner, DigitalContentCreator

Kwa mujibu wa  Idara ya mahak**a nchini Kenya Jaji wa Mahak**a ya Juu zaidi nchini humo Mohammed Khadhar Ibrahim amefari...
17/12/2025

Kwa mujibu wa Idara ya mahak**a nchini Kenya Jaji wa Mahak**a ya Juu zaidi nchini humo Mohammed Khadhar Ibrahim amefariki dunia akiwa na Umri wa miaka 69.

Idara hiyo ya mahak**a ya nchini kenya imethibitisha kifo cha Jaji Ibrahimi kuwa kimechangiwa na hali yake ya kiafya iliyodhoofika baada ya kuugua kwa muda mrefu .

Hata hivyo Ibrahim amekuwa Jaji wa Mahak**a hiyo ya Juu tangu ilipoanzishwa kulingana na katiba mpya mwaka 2011.

Kuhusu taarifa za mwanetu ufafanuzi umetolewa.......
17/12/2025

Kuhusu taarifa za mwanetu ufafanuzi umetolewa.......

Ajali iliyotokea Jana Dec 16,2025 la Karasha Wilayani Mbozi Mkoani Songwe, ambayo imesababisha vifo vya Watu watano na W...
17/12/2025

Ajali iliyotokea Jana Dec 16,2025 la Karasha Wilayani Mbozi Mkoani Songwe, ambayo imesababisha vifo vya Watu watano na Wengine Tisa kujeruhiwa katika Eneo Barabara Kuu ya Mbeya-Tunduma.

Ajali hiyo imehusisha gari ya Mitsubishi Canter Boxbody la SGA Mbeya, iliyokuwa likisafirisha fedha kutoka Tunduma Kwenda Mbeya, Pikipiki aina ya Fekon na Gari ya Abiria Toyota Coaster lililokuwa likielekea Tunduma Mbeya, ambapo wawili waliofariki ni Askari waliopoteza maisha waliofahamika k**a CPL Chirungu Misango John na PC Amina Japhari Hamisi.

Kufuatua Uchunguzi wa awali wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe umeeleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni Uzembe wa Dereva wa Coaster, aliyegonga pikipiki na kupoteza mwelekeo na kusababisha kugongana Uso kwa Uso na Canter, pia imechangiwa na mwendokasi katika eneo la makazi ya watu.

Matukio Ya mwisho wakati Familia ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma, Jenista Mhagama ikiweka udongo ...
16/12/2025

Matukio Ya mwisho wakati Familia ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma, Jenista Mhagama ikiweka udongo kwenye kaburi la mpendwa wao ambaye amezikwa leo Desemba 16, 2025 katika makaburi ya Center B yaliyopo kwenye kijiji cha Ruanda wilayani Mbinga, Ruvuma.

✍️
,

Saivi hatuandiki nioshe ni mwendo wa kupewa kesi tu...πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
14/12/2025

Saivi hatuandiki nioshe ni mwendo wa kupewa kesi tu...πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚

14/12/2025

Mwili wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Mhe. Jenista Mhagama, Rasmi umewasili mkoani Ruvuma ukipokelewa na maelfu ya wananchi, viongozi wa serikali, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wanaoendelea kuomboleza kifo chake.

Mwili umepelekwa nyumbani kwake katika mtaa wa Makambi, Manispaa ya Songea, kwa ajili ya kuendelea na taratibu na shughuli mbalimbali za mazishi ambayo yanatarajiwa kufanyika tarehee 16/12/2025.

,

14/12/2025

Kumbe mambo yalianzia kwa kirikuu.......???

Nabii Ebo Noah kutoka nchini Ghana ameripotiwa kuk**atwa na vyombo vya usalama baada ya kusambaza madai ya uongo kuwa ul...
14/12/2025

Nabii Ebo Noah kutoka nchini Ghana ameripotiwa kuk**atwa na vyombo vya usalama baada ya kusambaza madai ya uongo kuwa ulimwengu utasambaratika ifikapo Desemba 25 mwaka huu.

Inadaiwa kuwa Noah alianza hata maandalizi ya kujenga safina, akidai ingetumika siku hiyo k**a njia ya kuokoa watu taarifa ambazo zilisambaa kwa kasi kupitia mitandao ya kijamii na majukwaa mbalimbali na kusababisha hofu, sintofahamu na taharuki miongoni mwa wananchi ndani na nje ya Ghana.

Aidha, mamlaka za usalama nchini Ghana zimekanusha vikali madai hayo, zikisema hayana msingi wowote wa ukweli. Zimeeleza kuwa hakuna ushahidi wa kisayansi wala taarifa rasmi zinazothibitisha uwepo wa hatari k**a hiyo, na kwamba ujumbe uliosambazwa ni wa kupotosha umma.

Hata hivyo, mamlaka hizo zimetoa wito kwa wananchi kuwa makini na wahakikishe wanathibitisha taarifa kabla ya kuziamini au kuzisambaza kwa wengine, hususan taarifa zinazoweza kusababisha hofu au kuvuruga amani ya jamii.

Uzuri wanaume hata wakiwa hawafahamiani mambo yanaenda k**a kawaida na kila mtu atapata jina lake kwenye mazungumzo........
14/12/2025

Uzuri wanaume hata wakiwa hawafahamiani mambo yanaenda k**a kawaida na kila mtu atapata jina lake kwenye mazungumzo......

Maafisa usalama Nchini Marekani wamesema shambulio la risasi katika Chuo Kikuu cha Brown huko Rhode Island limetokea Dec...
14/12/2025

Maafisa usalama Nchini Marekani wamesema shambulio la risasi katika Chuo Kikuu cha Brown huko Rhode Island limetokea Dec 13,2023, na kusababisha vifo vya wanafunzi wawili na wengine tisa kujeruhiwa katika chuo hicho cha Ivy League.

Chuo kikuu cha Providence kimeendelea kuwa chini ya tahadhari kali (lockdown) kwa saa kadhaa baada ya mtuhumiwa aliyekuwa na silaha kuingia katika jengo ambako wanafunzi walikuwa wakifanya mitihani.

Maafisa walisema hawaamini kuwa kuna tishio mahsusi linaloendelea kutoka kwa mtuhumiwa huyo, Meya wa Providence Brett Smiley alisema mwishoni mwa Jumamosi.

Aidha, kutokana na vyombo vya usalama kuendelea kukagua maeneo na kufanya msako, amri ya kubaki ndani (shelter-in-place) kwa ajili ya chuo na maeneo ya jirani itaendelea kwa sasa.

Hata hivyo zaidi ya maafisa 400 wa vyombo vya usalama walipelekwa kazini siku ya Jumamosi wakati polisi wakimsaka mtuhumiwa wa shambulio hilo.

Mwanamieleka kutoka nchini Marekani John Cena rasmi ametangaza kustaafu mieleka baada ya kumaliza mchezo wake wa mwisho ...
14/12/2025

Mwanamieleka kutoka nchini Marekani John Cena rasmi ametangaza kustaafu mieleka baada ya kumaliza mchezo wake wa mwisho usiku wa kuamkia leo.

Siku chache zilizopita, nyota huyo wa WWE alitangaza uamuzi wake wa kustaafu rasmi mchezo wa mieleka baada ya kulitumikia kwa takribani miaka 25.

John Cena aliyezaliwa mwaka 1977 alianza mieleka mwaka 1999 akiwa k**a mcheza mieleka wa kulipwa (professional wrestling) katika Ultimate Pro Wrestling (UPW), kabla ya kujiunga na WWE mwaka 2002.

Kufuatia uamuzi huo mashabiki wengi wameonekana kushangazwa na kuwahuzunisha ambapo wengi wao walionyesha kutofurahishwa na hatua hiyo, wakisema bado walitamani kumuona akiendelea katika mchezo huo.

Nini Unakumbuka zaidi kutoka kwa John Cena?
✍️FlowinVitus

13/12/2025

Address

Iringa

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Flowin vitus posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share