Darajani 1905

Darajani 1905 Darajani 1905 ni ukurasa unaokuletea habari za Chelsea kwa lugha ya kiswahili.
(5)

Darajani 1905 ni ukurasa unaokuletea habari kwa ufupi kuhusu kinachoendelea klabuni Chelsea na wachezaji wake.

MABINGWA WA DUNIA ndani ya  na  na
25/07/2025

MABINGWA WA DUNIA ndani ya na na

MABINGWA WA DUNIA💙🏆Tunaanzia hapa Crown FM
25/07/2025

MABINGWA WA DUNIA💙🏆
Tunaanzia hapa Crown FM

Kwa mujibu wa taarifa, klabu ya Ajax imekataa ofa iliyowasilishwa na Chelsea ikitaka kumsajili beki raia wa Uholanzi ana...
24/07/2025

Kwa mujibu wa taarifa, klabu ya Ajax imekataa ofa iliyowasilishwa na Chelsea ikitaka kumsajili beki raia wa Uholanzi anayecheza kwa klabu hiyo, Jorrel Hato mwenye miaka 19. Chelsea inategemewa itawasilisha ofa nyingine kumtaka beki huyo anayeripotiwa kukubali kujiunga na Chelsea

Kuna timu ilicheza jana, dakika 90 walishinda 1-0 alafu mechi ikaenda penati penati, wakafungwa penati 5-6 alafu kombe w...
24/07/2025

Kuna timu ilicheza jana, dakika 90 walishinda 1-0 alafu mechi ikaenda penati penati, wakafungwa penati 5-6 alafu kombe wakapewa waliofungwa.....yani hata mashabiki wao hawakuelewa🤣🤣🤣🤣

Nimetumiwa eMail kutoka Chelsea kuhusu kuyarudisha matawi yote ya mashabiki wa Chelsea yaliyokuwepo hapo kabla na tumepe...
24/07/2025

Nimetumiwa eMail kutoka Chelsea kuhusu kuyarudisha matawi yote ya mashabiki wa Chelsea yaliyokuwepo hapo kabla na tumepewa utaratibu wote wa namna ya kuyarudisha!

Kwa wale watakaofika kwenye Party la Mabingwa wa Dunia tarehe 26-July tutapata nafasi ya kulijadili hili jambo ikiwemo kupata sehemu maalumu ambayo tutakuwa tunakutana k**a makao yetu makuu kwa Tanzania nzima.

Kuna faida nyingi sana kuwa sehemu ya tawi kuliko kubaki tu k**a shabiki!

Tosin Adarabioyo yupo nchini Nigeria ambako ndiko asili yake ilipo na hapa alitembelea kwenye moja kati ya nyumba za vio...
24/07/2025

Tosin Adarabioyo yupo nchini Nigeria ambako ndiko asili yake ilipo na hapa alitembelea kwenye moja kati ya nyumba za viongozi wa nchi hiyo na jambo zuri kabisa alitembelewa na tawi la mashabiki wa Chelsea waliopo nchini Nigeria. Hii ndiyo faida ya kuwa sehemu ya tawi na tawi letu litazinduliwa tena hivi karibuni.

"Unapojiunga na Chelsea basi moja kwa moja unajua kwamba klabu hii ya kubeba kila aina ya ubingwa. Ukiwa unaenda kwenye ...
24/07/2025

"Unapojiunga na Chelsea basi moja kwa moja unajua kwamba klabu hii ya kubeba kila aina ya ubingwa. Ukiwa unaenda kwenye kiwanja cha mazoezi unakutana na picha nyingi za mataji mbalimbali ambayo klabu imewai kuyatwaa hapo kabla na wewe unakuwa na huo mtazamo na hayo matarajio na presha inaongezeka kwamba msimu huu ni lazima tubebe taji lolote. Tunatakiwa kuwa kwenye picha mojawapo ya ubingwa."
- amesema Tosin Adarabioyo

🚨Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwandishi Fabrizio Romano, beki wa Ajax, Jorrel Hato ameiomba klabu yake kumruhusu aon...
23/07/2025

🚨Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwandishi Fabrizio Romano, beki wa Ajax, Jorrel Hato ameiomba klabu yake kumruhusu aondoke ajiunge na Mabingwa wa Dunia, Chelsea mara baada ya uwepo wa taarifa kwamba nyota huyo amefikia makubaliano binafsi na Chelsea.

PARTY LA MABINGWA MEDIA TOURMabingwa wa Dunia kutoka Tanzania, siku ya ijumaa itakuwa siku busy sana kwetu kujiandaa na ...
23/07/2025

PARTY LA MABINGWA MEDIA TOUR
Mabingwa wa Dunia kutoka Tanzania, siku ya ijumaa itakuwa siku busy sana kwetu kujiandaa na Party la Mabingws litakalofanyika huko Kigamboni.

Tutaanza Crown FM kuuwasha moto kuanzia saa 4 asubuhi
Kisha moto utahamia UFM Radio kuanzia saa 10 jioni
Na moto utapelekwa tena pale Clouds FM kuanzia saa 3 usiku

Kote huko tutapita kuhakikisha Dunia nzima inatambua kwamba MABINGWA WA DUNIA tunaitawala dunia.

Unatamani kuwa sehemu ya kushiriki PARTY LA MABINGWA?
Kiingilio ni Tsh. 30,000
Wasiliana na admin mkuu kwa simu namba 0682739814

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwandishi Fabrizio Romano, Mabingwa wa Dunia wamefikia kwenye hatua nzuri kuweza kufiki...
23/07/2025

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mwandishi Fabrizio Romano, Mabingwa wa Dunia wamefikia kwenye hatua nzuri kuweza kufikia makubaliano juu ya mahitaji binafsi na kiungo raia wa Uholanzi anayecheza klabu ya RB Leipzig, Xavi Simons.

Taarifa zinasema klabu yake ipo tayari kumruhusu mchezaji huyo kuondoka k**a na wao watapewa nafasi ya kumpata kiungo wa Chelsea ambaye msimu uliopita alikuwa kwa mkopo kwa klabu ya Borrusia Dortmund kwa mkopo, Carney Chukwuemeka.

Xavi Simons anatakiwa pia na Arsenal na Bayern Munich.

Hatuna mzamini tumebeba KOMBE LA DUNIA, tukipata mzamini si ndiyo tutabeba KOMBE LA GALAXY......waambieni MABINGWA WA PL...
23/07/2025

Hatuna mzamini tumebeba KOMBE LA DUNIA, tukipata mzamini si ndiyo tutabeba KOMBE LA GALAXY......waambieni MABINGWA WA PLUTO na MARS wajiandae, huku dunia washatushindwa🤣🤣🤣

🚨Taarifa zinasema Manyumbu wameonyesha nia ya kuanzisha mazungumzo ya kumsajili Nicolas Jackson ambaye kipaumbele chake ...
22/07/2025

🚨Taarifa zinasema Manyumbu wameonyesha nia ya kuanzisha mazungumzo ya kumsajili Nicolas Jackson ambaye kipaumbele chake ni kuendelea kusalia kwa klabu MABINGWA WA DUNIA. Taarifa zinasema licha ya kipaumbele chake kuendelea kubaki kwa MABINGWA WA DUNIA, mshambuliaji huyo raia wa Senegal hajafunga milango kwa klabu nyingine zitakazoonyesha nia ya kumtaka.

Taarifa zilizopo pia zinasema MABINGWA WA DUNIA bado wanavutiwa na winga wa Manyumbu, Alejandro Garnacho ambaye klabu hiyo ipo tayari kumruhusu kuondoka hivyo kuna uwezekano biashara ya mabadilishano ikachukua nafasi kwa MABINGWA WA DUNIA kumchukua Garnacho na Manyumbu kumchukua Nicolas Jackson.

Address

Kahama

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Darajani 1905 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Darajani 1905:

Share