18/08/2026
MUNGU NI MWEMA...
Matendo yake mema kwetu hayahesabiki.
Kwa hakika, kila siku anaendelea kutenda katika mapenzi yake, na kila tunapopata nafasi ya kutazama nyuma, tunagundua kuwa tumefika hapa kwa neema tu.
Kila wakati, usisahau kumshukuru Mungu kwa matendo yake makuu katika maisha yako.
Natumaini uko mzima wa siha njema, rafiki yangu.
Leo ni 18 August.
Na kwa muda mrefu sasa umekuwa sehemu ya familia ya TabasamuLetu Hub.
Huenda tayari unajua namna ya kutengeneza na kuzalisha bidhaa.
Au labda bado uko kwenye hatua ya kujifunza, ukiwa na ndoto ya siku moja kumiliki uzalishaji wako mwenyewe.
•Uzalisha.
•Unauza.
•Unajenga mfumo wa mauzo.
Na hatimaye, unajenga chanzo cha kipato kinachoweza kukua.
Hilo si tatizo.
Kwa sababu kuna jambo ambalo nimeamua kulifanya SEPTEMBA hii.
SADAKA YANGU YA SHUKRANI.
Nimewiwa kugusa maisha ya watu mbalimbali kupitia maarifa niliyonayo kwa kutoa mafunzo BURE–BILA ADA YA MWALIMU.
Na sitaki yafike kwa mtu mmoja tu.
Nataka kuwafikia:
Kanisa | Taasisi | Kikundi | Shule | Vijana | Wajasiriamali | Jamii mbalimbali
Na haijalishi uko Dar es Salaam au mkoa mwingine Tanzania.
Ikiwa kundi lako lina uhitaji wa kujifunza kuhusu utengenezaji wa bidhaa, tunaweza kuzungumza na kupanga namna ya kulifikia.
Lakini kuna jambo moja muhimu...
Haya siyo mafunzo ya kukaa tu na kusikiliza.
Nataka watu wajifunze, waone, waulize, washiriki na waondoke na ujuzi wanaoweza kuutumia.
Kwa hiyo, jukumu la washiriki litakuwa kugharamia malighafi na vifaa vitakavyohitajika kwa uzalishaji wa darasani.
Mafunzo yangu?
BURE.
Hii ni sehemu yangu ya kutoa shukrani.
Na huenda Septemba hii ikawa mwezi ambao kundi lenu litaanza kuona fursa ambayo lilikuwa haliijui.
Kwa hiyo k**a wewe ni:
Mratibu wa kikundi...
Kiongozi wa taasisi...
Mwalimu...
Kiongozi wa kanisa...
Au una kundi la watu wanaotaka kujifunza...
Hebu tuzungumze.
Usisubiri Septemba ifike ndipo uanze kutafuta nafasi.
Nitumie ujumbe leo kupitia:
+255 679 544 671
Niambie tu:
“TUNAHITAJI MAFUNZO.”
Kisha tutaangalia namna ya kuanza.
Maarifa yakikaa kichwani pekee hayabadilishi maisha.
Lakini yakitumika vizuri, yanaweza kuwa mwanzo wa mtu kujenga kitu chake mwenyewe.
Msirikale
TabasamuLetu Hub