05/06/2026
KARATU, ARUSHA
Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo amewataka wananchi wa Wilaya ya Karatu kuthamini na kulinda amani na utulivu wa nchi, akisisitiza kuwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa mazingira ya amani.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Karatu, kiongozi huyo alisema kuwa utulivu ndio msingi wa shughuli mbalimbali za uzalishaji na utoaji huduma, akibainisha kuwa bila amani hakuna biashara, hakuna kilimo, hakuna utalii, wala shughuli za usafiri k**a bodaboda na bajaji zinazoweza kufanyika kwa ufanisi.
Aidha, aliwataka wananchi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kudumisha umoja, mshik**ano na usalama wa maeneo yao ili kuwezesha maendeleo endelevu na ustawi wa jamii.
"Bila utulivu hakuna biashara, hakuna kulima, hakuna utalii, hakuna kuendesha bodaboda wala bajaji. Amani ni nguzo muhimu ya maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla," alisisitiza.
Mkutano huo ni sehemu ya ziara ya viongozi wa chama na Serikali ya kukutana na wananchi, kusikiliza kero zao na kueleza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.