13/11/2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua rasmi Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Tanzania, nafasi ambayo inamfanya kuwa Waziri Mkuu wa 14 tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961.
Jina la Mwigulu liliwasilishwa bungeni leo Alhamisi saa 3:06 asubuhi na mpambe wa Rais kwa Spika wa Bunge, M***a Zungu, kabla ya kusomwa rasmi kwa wabunge ambao baadaye walilipigia kura na kulithibitisha kwa kauli moja.
Mwigulu, ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi mkoani Singida, anachukua nafasi ya Kassim Majaliwa, aliyelitumikia taifa kwenye wadhifa huo kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo (2015–2025).
Mbali na siasa, Mwigulu ni mwanamichezo kindakindaki. Ni mwanachama wa klabu ya Yanga SC na pia mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa klabu hiyo kongwe nchini. Zaidi, anajulikana k**a mlezi wa timu ya Singida Black Stars, ambayo kwa sasa inashiriki Ligi Kuu Bara na imefanikiwa kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika sherehe za kuipongeza Singida Black Stars baada ya kutwaa Kombe la Kagame 2025 zilizoandaliwa Oktoba 5, 2025 mjini Singida, Mwigulu alisema kwa fahari:
“Ninajisikia fahari kusema mimi ni mlezi wa Singida Black Stars. Mambo makubwa zaidi yanakuja; hili ni kombe la kwanza, lakini tunaliangalia la ligi na shirikisho. Vikombe vingine vinakuja kwa sababu timu imejipanga vizuri, hali ya kujiamini ipo, na mkoa unatoa motisha kubwa.”
Mwigulu pia ni mmoja wa viongozi waliowahi kuonyesha dhamira ya kukuza sekta ya michezo kwa mtazamo wa kiuchumi. Akiwa Waziri wa Fedha mwaka 2022, alinukuliwa akisema:
“Michezo si burudani tu — ni uchumi, ni ajira, ni diplomasia. Tutahakikisha vijana wanapata mazingira ya kustawi kupitia michezo.”
Kwa uteuzi huu, Tanzania inampokea Mwigulu Nchemba si tu k**a kiongozi wa kisiasa, bali pia k**a mhimili wa michezo na maendeleo ya vijana — mtu anayeunganisha uongozi, uchumi na michezo katika dira moja ya taifa.
NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************