Watani wa Jadi

Watani wa Jadi Official Page ya Watani wa Jadi. Habari zote Exclusive za Yanga na Simba utazipata hapa 24/7. Hii ni Official Page ya Watani wa Jadi kwenye Mtandao wa Facebook.

Habari zote Exclusive kutoka kwenye klabu za Yanga na Simba utazipata hapa muda wote 24/7
Habarika na Sisi

16/11/2025

Mchambuzi wa soka nchini, Ibrahim Ambokile maarufu k**a Chuma cha Mjerumani, ameonyesha masikitiko yake baada ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kushindwa kuwepo kwenye hafla ya uzinduzi wa shule ya soka ya Yanga () .

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

15/11/2025

Rais wa Yanga, Injia Hersi Said , ameweka wazi sababu za kumwalika kocha wa zamani wa Mamelodi Sundowns na Al Ahly, Pitso Mosimane, kushiriki katika hafla ya uzinduzi wa Yanga Soccer School iliyofanyika katika viunga vya Shule ya Msingi Muhimbili, jijini Dar es Salaam.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) imeanza kwa kasi, ambapo Yanga Princess walianzia safari yao ya msimu huu ugenini Ruangwa, mk...
15/11/2025

Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) imeanza kwa kasi, ambapo Yanga Princess walianzia safari yao ya msimu huu ugenini Ruangwa, mkoani Lindi, wakikabiliana na Ruangwa Queens.

Mchezo huo ulimalizika kwa Yanga Princess kupata ushindi mnono wa mabao 3-0. Precious Christopher aling’ara kwa kufunga mabao mawili, huku Aregash Tadese akikamilisha karamu hiyo kwa bao la tatu. Ushindi huo unampa kocha Edna Lema mwanzo mzuri katika mbio za kutafuta taji msimu huu.

Katika mchezo mwingine, mshambuliaji wa Simba Queens, Jentrix Shikangwa, ameanza msimu kwa moto ule ule aliouonyesha mwaka jana baada ya kutupia hat-trick, akiisaidia timu yake kushinda 4-0 dhidi ya Bilo Queens kwenye Uwanja wa KMC Complex. Aisha Juma naye aliongeza bao la nne na kufungua ukurasa wake wa mabao msimu huu.

Matokeo hayo yanawaweka Simba Queens kileleni mapema kwenye msimamo, huku wakionesha dhamira ya kutaka kurejesha ubingwa.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Msimu mpya wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) 2025/26 unaanza leo Ijumaa, ambapo Yanga Princess watakuwa ugenini mkoani Lindi...
14/11/2025

Msimu mpya wa Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) 2025/26 unaanza leo Ijumaa, ambapo Yanga Princess watakuwa ugenini mkoani Lindi kumenyana na Ruangwa Queens, huku Simba Queens wakifungua kampeni yao kwenye Uwanja wa KMC Complex dhidi ya Bilo Queens.

Yanga Princess tayari wamewasili Ruangwa kwa ajili ya mtanange huo wa ufunguzi, wakiwa na dhamira kubwa ya kuanza safari ya kulisaka kwa nguvu taji lao la kwanza tangu kuanzishwa kwa ligi.

Upande wa Simba Queens, wao wanarudi kwenye vita ya kulitwaa tena taji waliloliachia kwa JKT Queens msimu uliopita, wakianza msimu huu kwa kasi na matumaini mapya.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Mlinda lango wa Simba SC, Moussa Camara, anatarajiwa kupitia upasuaji wa goti unaoweza kumweka nje ya dimba kwa takriban...
14/11/2025

Mlinda lango wa Simba SC, Moussa Camara, anatarajiwa kupitia upasuaji wa goti unaoweza kumweka nje ya dimba kwa takribani wiki 10, kufuatia jeraha alilopata kwenye mchezo wa hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United uliochezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Camara amekuwa akikumbana na tatizo hilo tangu msimu uliopita, na kwa mujibu wa taarifa za kitabibu, upasuaji ndio njia pekee itakayomwezesha kurejea katika ubora wake.

Simba imeeleza kuwa kipa huyo atasafiri kesho Jumamosi kuelekea Morocco kwa ajili ya upasuaji na mwendelezo wa matibabu.

Kutokana na kutarajiwa kwake kukaa nje kwa muda mrefu, jukumu la kusimama langoni litabaki mikononi mwa Yacoub Suleiman, ambaye tayari amecheza mechi nne msimu huu akimrithi Camara.

Hussein Abel ataendelea kubaki k**a kipa namba tatu, huku nafasi yake ya kupata dakika ikiwa bado finyu ndani ya kikosi hicho.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua rasmi Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpy...
13/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua rasmi Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Tanzania, nafasi ambayo inamfanya kuwa Waziri Mkuu wa 14 tangu nchi ipate uhuru mwaka 1961.

Jina la Mwigulu liliwasilishwa bungeni leo Alhamisi saa 3:06 asubuhi na mpambe wa Rais kwa Spika wa Bunge, M***a Zungu, kabla ya kusomwa rasmi kwa wabunge ambao baadaye walilipigia kura na kulithibitisha kwa kauli moja.

Mwigulu, ambaye ni Mbunge wa Iramba Magharibi mkoani Singida, anachukua nafasi ya Kassim Majaliwa, aliyelitumikia taifa kwenye wadhifa huo kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo (2015–2025).

Mbali na siasa, Mwigulu ni mwanamichezo kindakindaki. Ni mwanachama wa klabu ya Yanga SC na pia mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa klabu hiyo kongwe nchini. Zaidi, anajulikana k**a mlezi wa timu ya Singida Black Stars, ambayo kwa sasa inashiriki Ligi Kuu Bara na imefanikiwa kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Katika sherehe za kuipongeza Singida Black Stars baada ya kutwaa Kombe la Kagame 2025 zilizoandaliwa Oktoba 5, 2025 mjini Singida, Mwigulu alisema kwa fahari:

“Ninajisikia fahari kusema mimi ni mlezi wa Singida Black Stars. Mambo makubwa zaidi yanakuja; hili ni kombe la kwanza, lakini tunaliangalia la ligi na shirikisho. Vikombe vingine vinakuja kwa sababu timu imejipanga vizuri, hali ya kujiamini ipo, na mkoa unatoa motisha kubwa.”

Mwigulu pia ni mmoja wa viongozi waliowahi kuonyesha dhamira ya kukuza sekta ya michezo kwa mtazamo wa kiuchumi. Akiwa Waziri wa Fedha mwaka 2022, alinukuliwa akisema:

“Michezo si burudani tu — ni uchumi, ni ajira, ni diplomasia. Tutahakikisha vijana wanapata mazingira ya kustawi kupitia michezo.”

Kwa uteuzi huu, Tanzania inampokea Mwigulu Nchemba si tu k**a kiongozi wa kisiasa, bali pia k**a mhimili wa michezo na maendeleo ya vijana — mtu anayeunganisha uongozi, uchumi na michezo katika dira moja ya taifa.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Jijini Rabat, Morocco — Mchezo wa Alhamisi, Novemba 13, 2025 kati ya DR Congo na Cameroon unatarajiwa kuwa zaidi ya pamb...
12/11/2025

Jijini Rabat, Morocco — Mchezo wa Alhamisi, Novemba 13, 2025 kati ya DR Congo na Cameroon unatarajiwa kuwa zaidi ya pambano la kawaida. Kwa Wacongo, huu ni mchezo wa heshima, historia na motisha isiyo ya kawaida.

Ushindi katika mchezo huo utakuwa tiketi ya DR Congo kufuzu hatua ya mwisho ya mchujo wa Kombe la Dunia 2026 kwa ukanda wa Afrika hatua muhimu kuelekea ndoto ya kucheza michuano mikubwa zaidi ya soka duniani, itakayofanyika Marekani.

Lakini zaidi ya hadhi ya michezo, serikali ya DR Congo imeweka dau nono la kuwatia nguvu wachezaji wake: Dola milioni 1 (sawa na Shilingi bilioni 2.5) kwa kila mchezaji na afisa wa benchi la ufundi endapo timu hiyo itapata ushindi dhidi ya Cameroon.

Hatua hiyo imetafsiriwa k**a njia ya kuongeza morali kwa kikosi cha “The Leopards” kuhakikisha wanapambana hadi dakika ya mwisho.

Kikosi cha DR Congo, kinachowajumuisha nyota kadhaa wanaocheza soka nje ya nchi, kinajivunia uwepo wa mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC, Fiston Mayele, ambaye kwa sasa anakipiga katika klabu ya Pyramids FC ya Misri.

Kwa mujibu wa ratiba, mchezo wa kwanza wa siku hiyo utawakutanisha Gabon na Nigeria katika Uwanja wa Moulay Hassan kuanzia saa 1:00 usiku kwa saa za Tanzania. Baada ya hapo, macho yote yatageukia Uwanja wa Al Barid, ambapo DR Congo itavaana na Cameroon kuanzia saa 4:00 usiku.

Mshindi wa mchezo wa DR Congo na Cameroon atakutana na mshindi wa pambano kati ya Gabon na Nigeria katika fainali itakayopigwa Novemba 16, 2025, kwenye Uwanja wa Moulay Hassan kuanzia saa 4:00 usiku.

Kwa sasa, kinachosubiriwa ni jambo moja tu — je, The Leopards wataandika ukurasa mpya wa fahari ya taifa lao, au Cameroon watavunja ndoto hizo mapema? Muda utasema, lakini kila ishara inaonyesha pambano hili halitakuwa la kawaida.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Baada ya kusambaa kwa taarifa mtandaoni zikidai kuwa mchezaji wa Yanga SC, Aziz Andabwile, amefungua kesi ya madai dhidi...
12/11/2025

Baada ya kusambaa kwa taarifa mtandaoni zikidai kuwa mchezaji wa Yanga SC, Aziz Andabwile, amefungua kesi ya madai dhidi ya klabu yake katika Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) akidai malipo ya fedha za usajili, hatimaye nyota huyo ameamua kuweka wazi ukweli.

Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Andabwile amekanusha vikali madai hayo, akieleza kuwa hana mgogoro wowote na klabu yake na kwamba taarifa hizo hazina ukweli wowote.

Akiandika kwa uwazi, Andabwile amesema:
“Habari Wananchi. Napenda kuchukua nafasi hii kuliweka sawa jambo linaloendelea mtandaoni kuhusu mimi na Klabu yangu ya Yanga.
Mimi ni mchezaji wa Young Africans Sports Club na haki zangu za kimkataba tayari nilishalipwa.
Niwaombe ndugu waandishi wa habari kuwa na vyanzo sahihi vya taarifa ili kutoleta taharuki kwa wachezaji kwenye timu zao.
Mwisho, niwaombe radhi wote ambao wamekwazika na sintofahamu iliyojitokeza. Asanteni.”

Kauli hiyo imefunga mjadala uliokuwa ukitawala mitandao ya kijamii, huku mashabiki wengi wa Yanga wakimpongeza Andabwile kwa kuweka ukweli hadharani na kudumisha heshima ya klabu yao.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Moto wa Morice Abraham ndani ya kikosi cha Simba SC hauzimiki! Kila anapogusa mpira, mashabiki wanasimama, wapinzani wan...
11/11/2025

Moto wa Morice Abraham ndani ya kikosi cha Simba SC hauzimiki! Kila anapogusa mpira, mashabiki wanasimama, wapinzani wanatetemeka, na wachambuzi wanakiri — Simba imelamba dume kweli msimu huu!

Kocha wa zamani wa Simba, Fadlu Davids, ambaye ndiye aliyemleta Morice nchini akitokea RFK Novi ya Serbia, amekiri wazi kuwa kusajili kiungo huyo ni moja ya maamuzi bora zaidi aliyowahi kufanya akiwa Msimbazi.

Sasa akiwa kocha wa Raja Casablanca ya Morocco, Fadlu amemimina sifa kemkem kwa Morice, akimtaja k**a mchezaji wa kipekee mwenye kipaji cha asili na akili ya mpira isiyo ya kawaida.

“Licha ya umri wake kuwa mdogo, Morice ni hazina kubwa kwa Simba na hata Taifa Stars. Nilihitaji sekunde chache tu kumtambua — ni aina ya wachezaji wanaoleta tofauti uwanjani,” amesema Fadlu kwa mujibu wa Mwanaspoti.

Na kweli, maneno ya kocha huyo yanaonekana kutimia. Tangu Morice avae jezi nyekundu ya Simba, amekuwa mhimili wa kati, akitawala dimba kwa utulivu, ubunifu na pasi za moto zinazoamua matokeo.

Mashabiki wa Simba sasa wanasema wazi “Huyu ndiye injini yetu mpya!”
Na k**a ataendelea kwa kasi hii, Morice Abraham anaonekana kuwa nguzo mpya ya mafanikio ya Simba SC, mchezaji ambaye moto wake bado haujazimika bali ndio kwanza umeanza kuwaka!

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Kalenda ya FIFA imetupatia pumzi fupi kwenye ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara, lakini kwa wapenzi wa soka huu si muda wa...
11/11/2025

Kalenda ya FIFA imetupatia pumzi fupi kwenye ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara, lakini kwa wapenzi wa soka huu si muda wa kupumzika huu ni wakati wa mapambano ya kimkakati!

Kwa timu zilizokuwa moto, mapumziko haya yanaweza kupunguza kasi lakini kwa zile zilizokuwa zikisuasua, huu ndio wakati wa kuzaliwa upya! Ndiyo maana kipindi hiki ni kipimo cha ubora wa benchi la ufundi, nidhamu ya wachezaji, na ubunifu wa viongozi wa klabu.

Kikubwa sasa ni kurejesha nguvu na morali. Wachezaji wanapaswa kutumia muda huu kujijenga kimwili na kisaikolojia ligi ni ndefu, presha ni kubwa, na ushindani ni mkali. Mazoezi yawe ya kitaalamu, yakilenga kurudisha nishati, kuimarisha umoja wa kikosi, na kuongeza uelewano ndani ya uwanja.

Wale waliokuwa benchi kwa muda mrefu Huu ndio wakati wao wa kuonyesha thamani yao! Mechi za kirafiki ziwe jukwaa la kuonyesha ubora, kupambana kwa nafasi, na kuchochea moto wa ushindani ndani ya timu.

Kwa makocha – ni muda wa kufanya “homework” ya kweli! Kurudia video za mechi, kuchambua makosa ya kimbinu, na kuboresha mifumo ya uchezaji. Kila sekunde ya mapumziko iwe ni fursa ya kujifunza na kuimarika.

Na kwa viongozi wa klabu – huu ndio wakati wa kupanga mbinu za dirisha dogo la usajili. Tambueni maeneo yenye upungufu, fanyeni uamuzi wa kimkakati, na hakikisheni timu inarudi uwanjani ikiwa imara zaidi kuliko ilivyokuwa.

Kwa ujumla, mapumziko haya si ya kulala – ni ya kujenga nguvu mpya, ari mpya, na roho mpya ya ushindi! Ligi ikirudi, mashabiki wanataka kuona moto ule ule – au zaidi ya hapo!

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Klabu ya Yanga SC imepanga kufanya uzinduzi wa jezi zake rasmi zitakazotumika kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingw...
11/11/2025

Klabu ya Yanga SC imepanga kufanya uzinduzi wa jezi zake rasmi zitakazotumika kwenye hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu huu, hafla itakayofanyika kesho Jumatano.

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo, Ali Kamwe, amewataka wanachama na mashabiki wa Yanga kujipanga vyema kwa tukio hilo muhimu, akiahidi kwamba jezi hizo zitakuwa za kiwango cha juu cha kimataifa, zikiwa na ubunifu na ubora unaoendana na hadhi ya klabu hiyo kubwa barani Afrika.

“Kwa mujibu wa ratiba tuliyo nayo, Mwanachama wa Yanga aanze kujiandaa mapema. Inawezekana kabisa jezi zikazinduliwa Jumatano. Hatutaki kuchelewa, tunataka mashabiki wazipate mapema, wazivae, wapendeze, na wajipange kwa safari ya kuelekea New Amaan Complex,” alisema Kamwe.

Yanga SC itaanza rasmi kampeni za hatua ya makundi ya CAF Champions League kwa kuikaribisha AS FAR ya Morocco kwenye mchezo wa kwanza utakaopigwa Novemba 22 katika uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

Msimu huu, uongozi wa Yanga umeamua kutumia Uwanja wa Amaan k**a uwanja wao wa nyumbani katika michezo yote ya Ligi ya Mabingwa, ikiwa ni sehemu ya mpango wa klabu hiyo wa kuipanua hadhi ya timu kimataifa na kutoa burudani kwa mashabiki wake wa visiwani.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Mkurugenzi wa kampuni ya Jayrutty, Joel Rwegasira, aliahidi mapema mwaka huu kwamba basi jipya la kifahari aina ya IRIZA...
11/11/2025

Mkurugenzi wa kampuni ya Jayrutty, Joel Rwegasira, aliahidi mapema mwaka huu kwamba basi jipya la kifahari aina ya IRIZAR la klabu ya Simba SC lingewasili nchini mwishoni mwa mwezi Oktoba au mwanzoni mwa Novemba. Hata hivyo, hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa, jambo lililoibua maswali miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka kuhusu nini hasa kimechelewesha mchakato huo.

Katika mahojiano yake na vyombo vya habari, Rwegasira alieleza kuwa taratibu zote za ununuzi na usafirishaji zilikuwa zimekamilika, na kwamba kampuni yake ilikuwa imejipanga kuhakikisha Simba inapata gari la kisasa lenye viwango vya kimataifa.

Hadi sasa, Jayrutty wala Simba SC hawajatoa tamko rasmi kuhusu kuchelewa kwa basi hilo. Hata hivyo, mashabiki wengi bado wana matumaini kuwa ahadi hiyo itatekelezwa, kwani basi hilo limekuwa likionekana k**a alama ya ukuaji na hadhi mpya ya klabu hiyo kongwe nchini.

K**a kampuni na klabu zitatoa taarifa kamili hivi karibuni, huenda mashabiki wakapata majibu ya moja kwa moja kuhusu mustakabali wa basi hilo la ndoto ya Simba SC.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Watani wa Jadi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share