Watani wa Jadi

Watani wa Jadi Official Page ya Watani wa Jadi. Habari zote Exclusive za Yanga na Simba utazipata hapa 24/7. Hii ni Official Page ya Watani wa Jadi kwenye Mtandao wa Facebook.

Habari zote Exclusive kutoka kwenye klabu za Yanga na Simba utazipata hapa muda wote 24/7
Habarika na Sisi

28/05/2026

DAH....ILA MCHOME:: Mashabiki wa Simba mnasemaje?

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Allan Okello ameendelea kuvuna mafanikio ndani na nje ya Tanzania baada ya klabu yake ya zamani Vipers SC kuthibitisha k...
26/05/2026

Allan Okello ameendelea kuvuna mafanikio ndani na nje ya Tanzania baada ya klabu yake ya zamani Vipers SC kuthibitisha kuwa nyota huyo atapatiwa medali ya ubingwa wa Ligi Kuu Uganda msimu huu.

Kabla ya kutua ndani ya Young Africans S.C. katika dirisha dogo la Januari 2026, Okello alikuwa sehemu ya kikosi cha Vipers na aliisaidia timu hiyo kwa kufunga mabao matatu kabla ya kuhamia Jangwani.

Sasa “Star Boy” huyo ana nafasi ya kuandika historia ya kipekee kwa kutwaa medali mbili za ubingwa ndani ya msimu mmoja endapo ataiongoza Yanga kutetea taji la Ligi Kuu Tanzania Bara.

Okello anaendelea kuwa moto wa kuotea mbali kwa Wananchi baada ya juzi kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-1 dhidi ya Namungo FC, ushindi uliowarejesha Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi.

Tangu ajiunge na Yanga, Okello tayari amehusika kwenye mabao 18 akifunga mabao 11 na kutoa pasi saba za mabao, rekodi inayomfanya kuwa mmoja wa nyota wanaong’aa zaidi kwa sasa ndani ya ligi.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Allan Okello ameendelea kuwasha moto wa mabao ndani ya Young Africans S.C. baada ya kuiongoza timu hiyo kuibuka na ushin...
25/05/2026

Allan Okello ameendelea kuwasha moto wa mabao ndani ya Young Africans S.C. baada ya kuiongoza timu hiyo kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Namungo FC kwenye mchezo wa Ligi Kuu NBC uliopigwa Uwanja wa KMC Complex.

Wananchi walitangulia kupata bao dakika ya 26 kupitia Duke Abuya aliyemalizia shambulizi la kushtukiza, kabla ya Hassan Kabunda kuisawazishia Namungo na kufanya kipindi cha kwanza kumalizika kwa sare ya 1-1.

Kipindi cha pili kikawa mali ya “Star Boy” Okello. Nyota huyo aliifungia Yanga bao la pili dakika ya 53 baada ya kuuwahi mpira uliotemwa na kipa kufuatia krosi ya Max Nzengeli Dube, kabla ya kuhitimisha ushindi kwa bao la tatu dakika ya 84 akionyesha utulivu mkubwa ndani ya eneo la hatari.

Mabao hayo yamemfanya Okello kufikisha mabao 11 msimu huu, bao moja nyuma ya kinara Feisal Salum mwenye mabao 12. Pia ameweka rekodi ya kufunga katika michezo mitano mfululizo huku akipachika mabao mawili katika mechi nne mfululizo.

Ushindi huo umeirejesha Yanga kileleni mwa msimamo wa ligi kwa alama 60 baada ya kucheza michezo 25.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Simba SC imekwea tena kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu baada ya kuibuka na ushindi mwembamba lakini muhimu wa bao 1-0 dh...
24/05/2026

Simba SC imekwea tena kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu baada ya kuibuka na ushindi mwembamba lakini muhimu wa bao 1-0 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa KMC Complex.

Shujaa wa mchezo alikuwa Elie Mpanzu ambaye alihakikisha Wekundu wa Msimbazi wanasepa na pointi tatu baada ya kufunga bao pekee la mchezo kufuatia piga nikupige langoni mwa Dodoma Jiji.

Mpanzu ndiye aliyeanzisha presha baada ya kuangushwa ndani ya eneo la hatari na mlinda lango wa Dodoma Jiji, mwamuzi akaamuru penalti. Ingawa penalti ya Clatous Chama iliokolewa, kasi na umakini wa Mpanzu ulimfanya kuwahi mpira uliotemwa na kuusukuma wavuni.

Licha ya Simba kukosa umakini mkubwa wa kutumia nafasi walizotengeneza, ushindi huo umeiweka kileleni kwa alama 58, pointi moja mbele ya Young Africans S.C. ambao wanatarajiwa kushuka dimbani dhidi ya Namungo FC kesho.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Simba SC imeanza mapema harakati za kujenga kikosi cha moto kwa msimu ujao baada ya taarifa kueleza kuwa tayari imekamil...
23/05/2026

Simba SC imeanza mapema harakati za kujenga kikosi cha moto kwa msimu ujao baada ya taarifa kueleza kuwa tayari imekamilisha usajili wa beki wa kulia Nathaniel Chilambo anayetarajiwa kujiunga na Wekundu wa Msimbazi mara tu mkataba wake na Azam FC utakapomalizika mwezi ujao.

Inaelezwa Chilambo tayari amesaini pre-contract ya miaka mitatu, hatua inayoonyesha dhamira ya Simba kuimarisha kikosi chake mapema kabla ya kufunguliwa kwa dirisha la usajili.

Mbali na Chilambo, Simba pia inatajwa kumuwania kwa karibu winga Abdul Suleiman Sopu ambaye naye mkataba wake unaelekea ukingoni. Sopu, aliyewahi kupitia mfumo wa vijana wa Simba kabla ya kucheza Coastal Union na baadaye Azam FC, anatajwa kuwa sehemu ya mpango wa kuongeza makali ya safu ya ushambuliaji.

Wakati huo huo, taarifa za ndani zinaeleza kuwa nyota wengine waliokwishamwaga wino Msimbazi ni pamoja na kiungo Kelvin Nashon pamoja na winga Ramadhan Chobwedo.

Simba inaonekana kutaka kumaliza kila kitu mapema ili dirisha la usajili likifunguliwa, iwe ni suala la kutambulisha “vyuma” vipya tu mbele ya mashabiki wake.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Mashabiki wa Young Africans S.C. wameingiwa na hofu kidogo baada ya kiungo mshambuliaji wao tegemeo, Pacome Zouzoua, kus...
23/05/2026

Mashabiki wa Young Africans S.C. wameingiwa na hofu kidogo baada ya kiungo mshambuliaji wao tegemeo, Pacome Zouzoua, kushindwa kuendelea na mchezo dhidi ya Singida Black Stars na kuishia kucheza dakika 45 pekee.

Daktari wa Yanga, Moses Etutu, ameeleza kuwa Pacome alipata maumivu juu ya goti yaliyomlazimu kutotoka kipindi cha pili, licha ya Wananchi kuibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0.

Hata hivyo, taarifa za awali zinaeleza kuwa jeraha hilo halionekani kuwa kubwa sana, huku nyota huyo akitarajiwa kufanyiwa vipimo zaidi Jumamosi ili kubaini hali yake kamili.

Habari hiyo imekuja wakati Yanga ikijiandaa kwa mchezo mwingine muhimu dhidi ya Namungo FC Jumatatu kwenye Uwanja wa KMC Complex, kabla ya ligi kusimama kwa takribani wiki mbili kupisha kalenda ya FIFA.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Simba SC ipo kwenye presha kubwa ya kurejesha heshima Msimbazi baada ya mwekezaji na rais wa heshima wa klabu hiyo, Moha...
19/05/2026

Simba SC ipo kwenye presha kubwa ya kurejesha heshima Msimbazi baada ya mwekezaji na rais wa heshima wa klabu hiyo, Mohamed Dewji, kuwaahidi mastaa wa timu hiyo bonasi ya zaidi ya Sh 1 bilioni iwapo watatwaa mataji mawili yaliyobaki msimu huu; Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho la CRDB.

Inaripotiwa kuwa Mo Dewji alitoa ahadi hiyo katika kikao maalum na wachezaji pamoja na viongozi wa Simba, akisisitiza kuwa huu ni wakati wa kurejesha enzi za mafanikio za klabu hiyo.

Tayari morali imeonekana kupanda ndani ya kikosi hicho baada ya Simba kuichapa TRA United mabao 4-0 kwenye robo fainali ya Kombe la CRDB na sasa inajiandaa kuivaa Coastal Union kwenye nusu fainali Juni 20 mjini Arusha.

Inaelezwa kuwa bilioni hiyo ipo tayari mezani, huku Mo akiahidi kuongeza zaidi endapo timu hiyo itatimiza malengo yake ya msimu.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Presha ya mbio za ubingwa sasa imefikia kiwango cha juu kwa Young Africans S.C. ambao Ijumaa Mei 22 watashuka kwenye Uwa...
19/05/2026

Presha ya mbio za ubingwa sasa imefikia kiwango cha juu kwa Young Africans S.C. ambao Ijumaa Mei 22 watashuka kwenye Uwanja wa KMC Complex kuivaa Singida Black Stars katika mchezo muhimu wa raundi ya 24 ya Ligi Kuu NBC.

Baada ya kujikuta wakipoteza mchezo uliopita dhidi ya Dodoma Jiji FC, Wananchi sasa hawana nafasi tena ya kufanya makosa ikiwa wanataka kutimiza ndoto ya kutwaa ubingwa wa ligi kwa msimu wa tano mfululizo.

Licha ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 kwenye mchezo wa duru ya kwanza mjini Singida, Yanga wanaelewa wazi kuwa Singida BS si wapinzani wa kubeza. Ushindi ule ulitokana zaidi na umakini mkubwa wa kutumia nafasi walizozipata, jambo ambalo wanapaswa kulirudia tena mbele ya mashabiki wao.

Wakati Yanga wakiingia kambini kujiandaa na pambano hilo la lazima kushinda, Singida BS wao tayari wametua Dar es Salaam wakijiamini, huku msemaji wao Hussein Masanza akitamba kuwa wamekuja kuondoka na alama zote tatu.

Macho ya mashabiki sasa yataelekezwa KMC Complex kuona k**a Wananchi watarejea kwenye njia ya ushindi au Singida BS watazidi kuharibu hesabu za mabingwa hao watetezi.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Simba SC imewasili salama mkoani Tanga tayari kwa vita nyingine ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya wenyeji wao Coastal U...
19/05/2026

Simba SC imewasili salama mkoani Tanga tayari kwa vita nyingine ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya wenyeji wao Coastal Union, mchezo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa katika Uwanja wa Mkwakwani Alhamisi, Mei 21.

Mnyama wa Msimbazi anaingia kwenye pambano hilo akiwa na dhamira moja tu, kusepa na alama zote tatu ili kuendelea kushikilia presha kwenye mbio za ubingwa wa ligi msimu huu.

Mashabiki wa soka sasa wanasubiri kuona k**a Simba itaendeleza makali yake ugenini au Coastal Union wataitibulia hesabu mbele ya mashabiki wao wa nyumbani.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Safari ya kuelekea ubingwa wa Kombe la Shirikisho la CRDB Bank sasa imeingia pazito baada ya Tanzania Football Federatio...
18/05/2026

Safari ya kuelekea ubingwa wa Kombe la Shirikisho la CRDB Bank sasa imeingia pazito baada ya Tanzania Football Federation kuthibitisha ratiba ya michezo ya nusu fainali itakayotikisa majukwaa ya soka nchini mwezi Juni.

Macho na masikio ya mashabiki yataelekezwa mkoani Arusha Juni 20, ambapo Simba SC itashuka dimbani dhidi ya Coastal Union katika mchezo mkali utakaochezwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid kuanzia saa 10 jioni.

Juni 21, vita nyingine ya kusisimua itapigwa jijini Mwanza kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, huku Azam FC wakikabiliana na Young Africans S.C. katika pambano linalotabiriwa kuwa na presha kubwa na ushindani wa hali ya juu.

Ratiba hiyo sasa imezidi kuwapa hamasa mashabiki wa soka nchini wanaosubiri kuona nani atatinga fainali ya michuano hiyo yenye ushindani mkubwa msimu huu.

NB: USISAHAU KU-SUBSCRIBE CHANNEL YA WATANI WA JADI YOUTUBE
*********************************************

Address

Dar Es Salaam
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Watani wa Jadi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share