Monfm TZ

Monfm TZ Radio station that produces programs that educate and entertaining community

05/09/2026

Utani wa kwa Mama Kachanga na ni utani wa ngumi kabisa huu.

100.5MHz

05/09/2026

K**a ulizipenda picha za na wakiwa Bali, basi jua haikuwa bahati mbaya ulifanyika uwekezaji wa pesa nyingi ili kupata picha zile.

Fahyma anasema ilimgharimu Dollar za Kimarekani Elfu 2 Mia 5 (2500) sawa na zaidi ya shilingi Milioni 6 za Kitanzania.

100.5MHz

05/09/2026

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera, Faris Buruhani, ameeleza kuwa historia itamuandika Rais Samia Suluhu Hassan k**a mwanasiasa nguli, shupavu na mstahimilivu zaidi nchini.

Akizungumza mbele ya maelfu ya wananchi katika Kata ya Ihanda, Wilaya ya Karagwe, Faris alibainisha kuwa uwezo wa Rais Samia wa kuongoza kwa utulivu na kusimama imara hata wakati wa nyakati ngumu unamfanya kuwa kiongozi wa mfano wa kuigwa.

Mkutano huo wa hadhara, ulioandaliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kagera mwishoni mwa wiki, ulijuisha mamia ya wananchi waliokusanyika kusikiliza mwelekeo wa chama na serikali.

Katika hotuba yake, Faris alisisitiza kuwa uongozi wa Rais Samia umeleta uimara na matumaini makubwa kwa Watanzania, jambo linalodhihirisha ukomaa wake wa kisiasa katika kuilinda na kuivusha nchi salama.

100.5MHz

Mkuu wa Majeshi nchini Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ametoa maagizo mapya yanayowataka askari polisi wote nchini...
05/09/2026

Mkuu wa Majeshi nchini Uganda, Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ametoa maagizo mapya yanayowataka askari polisi wote nchini humo kuvaa lebo za majina yao upande wa kulia wa kifua na beji pamoja na namba za utambulisho upande wa kushoto. Agizo hili linalenga kuongeza uwazi na uwajibikaji kwa maafisa wa usalama wanapokuwa kazini.

Aidha, Jenerali Muhoozi ameeleza kuwa wananchi wote wa Uganda wana haki ya kisheria kumtaka afisa yeyote anayewak**ata awatajie jina na namba yake ya beji. Aliongeza kuwa iwapo afisa husika atakataa kutoa taarifa hizo, mwananchi ana haki ya kugoma na kukaidi uk**ataji huo.

100.5MHz

05/09/2026

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba ameagiza Afisa Elimu Wilaya ya Bahi, Boniphace Wilson apandishwe cheo kufuatia Shule ya Bahi kuongoza kitaifa katika matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2025.

100.5MHz

Nilijutia kuondoka Simba. Hata siku ile niliposaini [Yanga], sikuwa na amani moyoni, lakini ilikuwa jambo ambalo nililaz...
05/09/2026

Nilijutia kuondoka Simba. Hata siku ile niliposaini [Yanga], sikuwa na amani moyoni, lakini ilikuwa jambo ambalo nililazimika kulikubali. Nafikiri baadhi ya viongozi wa Simba walijua, na bado wanajua ukweli kwamba nilitaka sana kuwa Simba.” - Clatous Chama, mchezaji wa Simba SC

100.5MHz

03/09/2026

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetajwa kuwa miongoni mwa taasisi za serikali zinazotekeleza majukumu yake kwa mafanikio yanayoonekana wazi kwa wananchi na taifa kwa ujumla, huku taasisi nyingine zikihimizwa kuiga mfumo wake wa utendaji.Mkoa

‎Pongezi hizo zimetolewa jijini Arusha katika hafla ya kuwashukuru walipakodi iliyowakutanisha viongozi wa serikali, watendaji pamoja na wadau mbalimbali, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude, na Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Dkt. Toba Nguvila, wameeleza kuwa mafanikio ya TRA yanapaswa kuwa mfano kwa taasisi nyingine za umma.

‎Miongoni mwa mafanikio yaliyotajwa ni kuboreshwa kwa mifumo ya utoaji huduma na ukusanyaji wa mapato, hatua inayodaiwa kuongeza ufanisi na kuwezesha taifa kupata matokeo yanayoonekana.

‎ Meneja wa TRA Mkoa wa Arusha, Deogratius Shuma, amesema mamlaka hiyo itaendelea kuboresha huduma zake ili kurahisisha ulipaji wa kodi na kuongeza ushirikiano na walipakodi.

100.5MHz

Tunawakiribisha siku ya kesho mchana kuanzia saa saba kamili mchana mpaka saakumi kamili jioni kwenye kipindi cha EXTRA ...
02/09/2026

Tunawakiribisha siku ya kesho mchana kuanzia saa saba kamili mchana mpaka saakumi kamili jioni kwenye kipindi cha EXTRA FLAVOUR (kipindi bora cha burudani) tutakua na mahojiano na msanii wetu wa nyumbani STAY B kuhusiana na safari yake mziki tangu alipo anza mpaka sasa

100.5MHz

02/09/2026

Rais Samia Suluhu Hassan amesema miji haipaswi kuwa michafu, akiwataka viongozi kuhakikisha usafi unasimamiwa ipasavyo.

100.5MHz

02/09/2026

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limebaini matukio ya wizi wa umeme katika maeneo ya Visiwani, Mwananyamala na Mivumoni, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo imekuja kufuatia operesheni ya ukaguzi wa mita na miundombinu inayolenga kudhibiti matumizi yasiyo halali, kulinda miundombinu ya shirika, na kuhakikisha huduma ya umeme inaendelea kutolewa kwa usalama na ufanisi.

Mhandisi wa TANESCO Mkoa wa Kinondoni Kaskazini, Mha. Underson Manyika, ameeleza kuwa timu ya wataalamu ilibaini baadhi ya wateja wakichepusha nyaya na kutengeneza miunganisho isiyo halali iliyosababisha mita kutosoma matumizi halisi.

Ameinisha kuwa hatua stahiki za kisheria zinaendelea kuchukuliwa dhidi ya waliohusika, kwani vitendo hivyo vinaliletea shirika hasara na kuhatarisha usalama wa mali na maisha ya wananchi.

Naye Afisa Usalama wa TANESCO, Bi. Lilian Nizim, amewasihi wananchi kuzingatia sheria na kutoingilia mita badala yake kutoa taarifa mapema pindi wanapobaini changamoto yoyote.

TANESCO imesisitiza kuwa itaendeleza ukaguzi huo wa mara kwa mara katika maeneo mbalimbali nchini ili kuimarisha utoaji wa huduma ya umeme wa uhakika, salama, na endelevu.

100.5MHz

Address

Murusi Street
Kasulu

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Monfm TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category