23/12/2025
Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Joseph Sinde Warioba, amesema Serikali inapaswa kukubali makosa yaliyotokea Oktoba 29, akisisitiza kuwa hatua hiyo ni muhimu katika kulinda haki, amani na kuimarisha imani ya wananchi kwa Serikali.
Warioba ameyasema hayo alipofanya mazungumzo na moja ya chombo cha habari hapa nchini, ambapo amesema kuwa kukiri na kurekebisha makosa si dalili ya udhaifu, bali ni ishara ya uwajibikaji na uongozi unaojali maslahi ya Taifa kwa ujumla.
Aidha, amesisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vinapaswa kubaki huru, vikitekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, haki na usalama wa wananchi bila kuingiliwa na shinikizo la kisiasa.
100.5Kasulu