04/06/2026
Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amewapongeza vijana wa timu ya taifa ya Tanzania ya chini ya miaka 17, Serengeti Boys, kwa mafanikio na hatua ya heshima waliyoifikia katika michuano ya AFCON U-17.
Akizungumza Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Juni 4, 2026, Dkt. Nchemba alisema amefurahishwa na kiwango walichoonyesha vijana hao na kuwataka kuendelea kujituma ili kufikia mafanikio makubwa zaidi siku zijazo.
“Ninawapongeza sana vijana wetu wa Serengeti Boys kwa hatua kubwa na ya heshima waliyofikia katika michuano ya AFCON U-17. Ninaamini kuna siku kombe litakuja na wala si siku nyingi,” alisema Waziri Mkuu.
100.5MHz