Monfm TZ

Monfm TZ Radio station that produces programs that educate and entertaining community

04/06/2026

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amewapongeza vijana wa timu ya taifa ya Tanzania ya chini ya miaka 17, Serengeti Boys, kwa mafanikio na hatua ya heshima waliyoifikia katika michuano ya AFCON U-17.

Akizungumza Bungeni jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Juni 4, 2026, Dkt. Nchemba alisema amefurahishwa na kiwango walichoonyesha vijana hao na kuwataka kuendelea kujituma ili kufikia mafanikio makubwa zaidi siku zijazo.

“Ninawapongeza sana vijana wetu wa Serengeti Boys kwa hatua kubwa na ya heshima waliyofikia katika michuano ya AFCON U-17. Ninaamini kuna siku kombe litakuja na wala si siku nyingi,” alisema Waziri Mkuu.

100.5MHz

04/06/2026

Wizara ya ujenzi imetoa majibu kwa maswali yote ya wabunge kuhusu ujenzi wa barabara za mbalimbali nchini.

Maswali hayo yamejibiwa na Naibu Waziri Mhe. David Mwakiposa Kihenzile kwa niaba ya Waziri wa ujenzi Mhe. Abdallah Hamis Ulega

100.5MHz

04/06/2026

Rais Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari na Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN University) kwa kutambua uongozi wake, mageuzi katika sekta ya elimu, juhudi zake za kuimarisha diplomasia ya Tanzania, pamoja na mchango wake katika kuimarisha hadhi ya Tanzania kimataifa.

100.5MHz

Mwanamuziki   ameweka wazi ilikuwa ni ndoto yake siku moja kufanya kolabo na   hii ni kutokana na kuikubali sana sauti y...
04/06/2026

Mwanamuziki ameweka wazi ilikuwa ni ndoto yake siku moja kufanya kolabo na hii ni kutokana na kuikubali sana sauti yake. Wawili hao wameshirikiana kwa sasa kupitia wimbo maalum wa kombe la dunia "Dai Dai"

100.5MHz

Mabadiliko yanahitaji watu, watu wenye ujuzi, nidhamu, ubunifu na uzalendo, wanaoelewa kwamba maarifa lazima yahudumie m...
04/06/2026

Mabadiliko yanahitaji watu, watu wenye ujuzi, nidhamu, ubunifu na uzalendo, wanaoelewa kwamba maarifa lazima yahudumie maslahi ya pamoja, na Chuo Kikuu cha RUDN kinasaidia Tanzania katika mabadiliko haya kwa kuandaa vijana wetu kuwa tayari kulitumikia taifa lao." - Rais Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada ya Heshima na Chuo Kikuu cha RUDN, Urusi

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia na linaendelea kumhoji mtu mmoja aitwaye Peter Willium (28), Mhangaza, mkazi...
04/06/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia na linaendelea kumhoji mtu mmoja aitwaye Peter Willium (28), Mhangaza, mkazi wa Itale, Wilaya ya Chato, kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi (ambaye jina na anwani yake imehifadhiwa kwa sababu za kisheria).

Tukio hilo limetokea Mei 31, 2026, majira ya saa 12:00 jioni, katika pori la Ichwankima lililopo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Burigi, Chato. Inadaiwa kuwa, mtuhumiwa alimk**ata mwathirika na kumvutia vichakani ndani ya hifadhi hiyo, kabla ya kutekeleza kitendo hicho cha kikatili.

Hata hivyo, mtuhumiwa alipotenda unyama huo, aliendelea kumzuia mwathirika huku akiwapigia simu ndugu wa mwathirika na kuwadai watume pesa ili amwachie huru, akitishia kumdhuru iwapo hawatatii matakwa hayo.

Kufuatia taarifa hizo, Jeshi la Polisi liliweka mtego uliowezesha kuk**atwa kwa mtuhumiwa huyo.
Uchunguzi wa tukio hilo unakamilishwa sambamba na taratibu zote za kisheria ili mtuhumiwa afikishwe mahak**ani.

Jeshi la Polisi limewapongeza na linawasihi wananchi kuendelea kufichua vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na wanafunzi, pamoja na kulinda haki, usalama na ustawi wa makundi hayo.
Aidha, Jeshi la Polisi limesisitiza kuwa halitasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo vya uhalifu.

100.5MHz

Mahak**a ya Wilaya ya Dodoma imewahukumu William Chilenga (25), Masafa Mwaluganje (19) na Aman Leonard (25) kifungo cha ...
04/06/2026

Mahak**a ya Wilaya ya Dodoma imewahukumu William Chilenga (25), Masafa Mwaluganje (19) na Aman Leonard (25) kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kosa la ubakaji wa kundi.

Washtakiwa walitenda kosa hilo Disemba 12, 2025 katika Kijiji cha Hombolo, Wilaya ya Mtumba mkoani Dodoma, ambapo walimbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 42.

Baada ya tukio hilo, walik**atwa na kufikishwa Mahak**ani kujibu mash*taka yaliyokuwa yakiwakabili.

Hukumu hiyo ilitolewa Juni 2, 2026 na Hakimu Mfawidhi Lugoye baada ya mahak**a kuridhika na ushahidi uliowasilishwa na upande wa mashtaka na kuwatiwa hatiani kwa kosa hilo.

100.5MHz

Katika kutimiza lengo la kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na kuwaunganisha wananchi wa Mtwara kwa ujumla, Mhe. Joel Nana...
04/06/2026

Katika kutimiza lengo la kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na kuwaunganisha wananchi wa Mtwara kwa ujumla, Mhe. Joel Nanauka, Mbunge wa Mtwara Mjini, rasmi ametangaza kuanzishwa kwa Mtwara Festival, jukwaa jipya la kijamii na kiuchumi lenye lengo la kufungua fursa za uwekezaji, biashara, utalii, sanaa, michezo na maendeleo ya vijana katika
Mkoa wa Mtwara na Ukanda wa Kusini mwa Pwani.

Mradi huu unalenga kuitangaza na kuitumia kikamilifu fursa zilizopo ndani ya Mtwara Development Corridor, kwa kuunganisha wadau mbalimbali wa maendeleo, sekta binafsi,
wawekezaji, wabunifu, vijana na wananchi kwa ujumla.

Miongoni mwa shughuli kuu za Mtwara Festival ni mashindano makubwa ya soka ya CRDB Nanauka Cup, Uchumi Forum, REDE yatakayoshirikisha vijana na jamii kwa ujumla k**a
sehemu ya kukuza vipaji, mshik**ano wa kijamii na uchumi wa wananchi.

Uzinduzi rasmi wa Mtwara Festival utafanyika Juni 13, 2026 katika Viwanja vya
Nangwanda Sijaona, huku shughuli mbalimbali za festival zikiendelea katika kipindi chote cha mwezi Juni hadi kufikia kilele chake mwezi Julai 2026.

100.5MHz

Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania inaendelea kuwa salama dhidi ya ugonjwa wa Ebola huku Serikali ik...
04/06/2026

Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amesema Tanzania inaendelea kuwa salama dhidi ya ugonjwa wa Ebola huku Serikali ikiendelea kuimarisha mifumo ya tahadhari, ufuatiliaji na utoaji wa elimu kwa wananchi kuhusu magonjwa ya mlipuko.

‎Ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa papo la Mbunge wa Viti Maalum, Mhe. Asha Salum Moto, ambaye alitaka kujua namna Serikali ilivyojipanga kukabiliana na ugonjwa wa Ebola unaoripotiwa katika baadhi ya nchi jirani.

‎"Mpaka sasa tuko salama, nchi yetu iko salama. Ni jambo la kumshukuru Mungu. Hata hivyo, kwa kuwa Tanzania si kisiwa, tunaendelea kuchukua hatua zote za tahadhari ili kuhakikisha usalama wa wananchi wetu unaendelea kuwepo," Amesema Dkt. Mwigulu.

‎Amesema Serikali inaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu namna ya kujikinga na magonjwa ya mlipuko, kuimarisha ufuatiliaji mipakani pamoja na kuhimiza utoaji wa taarifa mapema pale dalili za magonjwa hayo zinapojitokeza.

100.5MHz

Bunge la Wawakilishi la Marekani limepitisha azimio la kumzuia Rais Donald Trump kuchukua hatua zaidi za kijeshi dhidi y...
04/06/2026

Bunge la Wawakilishi la Marekani limepitisha azimio la kumzuia Rais Donald Trump kuchukua hatua zaidi za kijeshi dhidi ya Iran.

Hata hivyo, azimio hilo bado linahitaji kupitishwa na Bunge la Seneti.

100.5MHz

Address

Murusi Street
Kasulu

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Monfm TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category