14/01/2024
HONGERA MSUMBIJI, SARE YENU NI FUNZO KWETU NA TAIFA STARS....
Kwa ilivyozoeleka, si kawaida kuiona timu ya Misri inasuluhu na timu k**a ya Msumbiji. Tena wakiwa wametangulia wao, wakasawazishiwa, wakaongezwa ndiyo dakika za mwishoooni wanajitetea tena kwa Goli la PENATI ya VAR.ππ
Hiki ndiyo ninachotamani watu waelewe kuwa mambo yanabadilika. Hata uliyemtangulia kuzaliwa anakua anafikia kuwa mtu mzima mwenye nguvu na uwezo saa nyingine kuliko hata wale waliomtangulia.
Tusishangae siku tukaikosa Misri kwenye mashindano na BINGWA akawa mwingine. K**a mashindano yanahusisha timu zilizofuzu ujue ipo siku walioaminika ni wababe wa soka watapungua na wataibuka wengine na pengine baadae itakua ni k**a kuimba, kupokezekana.
Historia ya soka itabadilika kuliko kawaida....
Hili liwe funzo kwa timu yetu ya taifa. Matokeo haya yawe chachu kwa Taifa Stars inapoenda kumenyana na Morocco, iiendee k**a timu kubwa ndiyo lakini siyo k**a timu yenye haki pekee ya kushinda. Taifa Stars ijipange kushindana kufa kupona.