Musk TV

Musk TV Stay With Me 💕

Mimi ni kijana umri wangu ni miaka 36, ila sijajua k**a huo umri bado ni kijana, nimeoa na tayari nina watoto watatu.Dad...
22/12/2025

Mimi ni kijana umri wangu ni miaka 36, ila sijajua k**a huo umri bado ni kijana, nimeoa na tayari nina watoto watatu.
Dada Mimi ni mfanya Biashara, tuna duka Moja ambalo anakaa mke wangu na wafanyakazi wawili, Mimi mara nyingi ni mtu wa kusafiri kufanya Biashara zingine mikoani.

Alhamisi nilipigiwa simu na wateja wakiuniuliza mbona duka limefungwa, hiyo ilikuwa mida ya saa nne asubuhi, nikampigia simu mke wangu Ili nimuulize vipi inakuaje mpaka muda huo hawajafungua, ila simu ikawa haipatikani, nikampigia kijana ambaye ni mfanyakazi wa pale dukani ambaye huwa anasaidiana na mke wangu, kijana akaniambia kuwa mke wangu aliwaambia kuanzia alhamisi mpaka ijumamosi hawafungui, wata fungua jumatatu, kikawaida jumapili huwa duka Langu hatufungui, nilivyo ambiwa hivyo nikashangaa, ikabidi nimpigie mdada wa kazi hapa nyumbani ndo akaniambia mke wangu ameaga anaenda kwenye mkesha atarudi jumamosi, niliishiwa nguvu nikakosa Cha kufanya.

Ilibidi nifanye haraka haraka nirudi dar, ijumaa usiku nikawa nimefika nyumbani sikumkuta mke wangu, nikatulia tu nikawa nimemsubiri Kwa hamu sana aniambie ni kwanini afunge Biashara siku tatu wakati tuna mzigo ambao tume uleta Kwa ajili ya sikukuu hizi,

Dada huwezi amini mke wangu alivyo rudi nyumbani jumamosi mida ya saa tatu asubuhi alifika tu na kufungua geti alivyo niona tu nimekaa kibarazani akaniambia Kwa sauti ya juu anataka talaka tuachane Kwa madai eti MUNGU kamuonyesha Mimi ndo sababu ya yeye kutokufanikiwa, nikamwuliza mafanikio gani anataka? K**a ni gari anatembelea mbili ni yeye aamue atumie lipi, nikashangaa kaingia ndani kachukua begi akaondoka.

Toka jana jumamosi mke wangu kaondoka nyumbani, taarifa za chini naambiwa kaenda kupanga, kaniachia watoto hapa mpaka simuelewi, mtoto huyu mdogo ana mwaka mmoja na miezi miwili na yeye kamuacha.

Najiuliza Nini kimemkuta mke wangu hata sielewi, hatukuwahi hata kukwazana kiasi Cha kufikia kuachana, na kabla ya kwenda mkoani alinishauri yeye mwenyewe tununue kiwanja tujenge kiwanda Cha kufyatua matofali tena akawa ananisisitiza sana kuhusu hicho kitu halafu leo ananiambia Mimi ndo kikwazo kwenye maisha yake.

Nilimpa uhuru wa kutumia pesa ndiyo mana hata gari zote za kutembelea alikuwa anatumia yeye, Mimi siyo mpenzi wa kutembelea gari nikiwa mjini, napendelea pikipiki ila kitu Cha ajabu Leo nakuja Kuambiwa Mimi ndo chanzo Cha yeye kutokufanikiwa, najiuliza ni mafanikio gani anataka!!

Zerobrainer team
20/12/2025

Zerobrainer team

Mtu sie nyau, Nan huyu jamani
20/12/2025

Mtu sie nyau, Nan huyu jamani

Tukutane kwenye kikao Cha wanaume 2026 tupange mipango mioya tutapataje pesa 2026 hiyo
19/12/2025

Tukutane kwenye kikao Cha wanaume 2026 tupange mipango mioya tutapataje pesa 2026 hiyo

Kitale, kingpusi na Jitu bonge la combination
19/12/2025

Kitale, kingpusi na Jitu bonge la combination

Bora ukae kwenye hili kabila maana hawana mpango na pesa kabisa Yani
19/12/2025

Bora ukae kwenye hili kabila maana hawana mpango na pesa kabisa Yani

Mwanaharakati wa mazingira wa Kenya Truphena Muthoni (22) pichani amevunja rekodi ya dunia kwa kukumbatia mti zaidi ya m...
11/12/2025

Mwanaharakati wa mazingira wa Kenya Truphena Muthoni (22) pichani amevunja rekodi ya dunia kwa kukumbatia mti zaidi ya masaa 72(siku tatu) mfululizo bila kula wala kunywa

Kwa rekodi hiyo mpya mwanaharakati huyo amejishindia pesa zaidi ya milioni 1 ya Kenya (zaidi ya milioni 18 za tz) pamoja na zawadi mbalimbali zenye thamani ya mamilioni na ofa ya kwenda kukaa hotel ya nyota 5 katika jiji la Mombasa.

Pia anatarajiwa kutambuliwa rasmi na kuingizwa kwenye kitabu cha kumbukumbu za maajabu duniani (World Guinness Records). Picha zaidi kwenye comments

Vipi mdau ungeweza kukumbatia mti zaidi ya masaa 72 mfululizo bila kukaa wala kula?

Address

Nyantare
Kigoma

Telephone

+255627726379

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Musk TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Musk TV:

Share