Zamaradi TV

Zamaradi TV NEWS, ENTERTAINMENT and LIFESTYLE channel that has varieties of programs including Series, Talk Shows

23/07/2025

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso, ameonyesha wazi kutoridhishwa na kasi duni ya utekelezaji wa Mradi wa Miji 28, unaotekelezwa katika Wilaya za Wanging’ombe na Makambako, mkoani Njombe. Akiwa katika ziara ya kikazi Julai 22, 2025, Waziri Aweso alibaini dosari kadhaa, ikiwemo kucheleweshwa kwa utekelezaji wa mradi huo na kuwepo kwa msimamizi wa mradi asiyekuwa na sifa zinazostahili.

Ameagiza hatua zichukuliwe mara moja dhidi ya wote wanaochelewesha utekelezaji, huku akiiagiza Kampuni ya Larsen & Toubro Limited, inayotekeleza mradi huo, kufanya kazi kwa bidii na kwa viwango vinavyostahili.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, ametoa rai kwa wakandarasi wazawa kuchukulia kwa uzito miradi wanayopewa.

23/07/2025

Wajumbe wa CCM Kiteto Wataka Viongozi Wao Wabadilike, Walalamikia Kutotatuliwa kwa Changamoto za Wananchi

Wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Kiteto, mkoani Manyara, wameonesha kutoridhishwa na mwenendo wa baadhi ya viongozi wa chama na serikali katika wilaya hiyo, wakisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakikosa ushirikiano na kushindwa kuwasaidia wananchi kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Wajumbe hao walitoa kauli hiyo Julai 23, 2025, wakati wa zoezi la upigaji kura za uchaguzi wa madiwani wa viti maalum kilichofanyika kwa mujibu wa taratibu za chama hicho.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wajumbe walisema kuwa licha ya wananchi kuendelea kuwa na imani na CCM, viongozi waliopo kwenye nafasi za utekelezaji hawajawa karibu vya kutosha na wanachama na wananchi kwa ujumla, jambo linalochangia kero nyingi kutopatiwa majibu kwa wakati.

23/07/2025

Jumatano hii kwenye MDAU KIJIWENI ametembelea kijiwe Cha fire na kupiga story na wadau Mbalimbali waliokuwa na kiu na shauku kupaza sauti zao kwaajili ya timu zao.

Ucheshi, utani , malumbano ya hoja Mbalimbali vyote vilitokea kwenye kijiwe hicho. Je upo kijiwe gani?

JUMATANO HII SAA 2:00 USIKU NA MARUDIO NI SAA 11:00 ASUBUHI , ZAMARADITV CHANNEL NO 413 KWENYE KISIMBUZI CHA AZAM TV.

23/07/2025

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, Julai 22, 2025, ametoa ufafanuzi kuhusu hatua ya Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) kusitisha kwa muda upokeaji wa wanafunzi wa shahada ya kwanza katika baadhi ya kozi za ualimu kwa mwaka wa masomo 2025/2026.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Prof. Mkenda amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mapitio ya kimkakati yanayolenga kuhakikisha kuwa mafunzo ya ualimu yanazingatia viwango bora na mahitaji halisi ya soko la ajira.

“Chuo kimeamua kwa muda kusitisha baadhi ya kozi hizo ili kupisha maboresho, na hilo linafanyika kwa ushauriano na wizara pamoja na Tume ya Vyuo Vikuu (TCU),” amesema Prof. Mkenda.

Taarifa ya UDOM iliyotolewa awali ilifafanua kuwa maamuzi hayo ni ya muda na hayahusishi kufutwa kabisa kwa programu hizo bali ni sehemu ya utaratibu wa kawaida wa tathmini ya kitaaluma.

23/07/2025

WAZIRI MKUU MAJALIWA AWEKA SHADA LA MAUA KATIKA MNARA WA MASHUJAA BELARUS

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, ameonesha heshima kwa mashujaa wa Jamhuri ya Belarus kwa kuweka shada la maua katika Mnara wa Kumbukumbu ya Mashujaa.

Hafla hiyo ni sehemu ya ziara yake rasmi nchini humo, ikilenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Belarus.

22/07/2025

Usiku wa Historia Msisili!
Leo ndio Usiku wa Kumvika Taji – na jina linalotajwa kila kona ni moja tu:
SARA DOMMY – RAIS WA MSISILI!

Baada ya kupitia joto la maisha, madeni ya “Kausha Damu”, na presha ya uhalisia, Sara Dommy leo anasimama kifua mbele si k**a msh*takiwa wa maisha, bali k**a kiongozi wa heshima, aliyechaguliwa na mtaa, kwa mtaa, na kwa ajili ya mtaa.

Usikose kutazama Malkia wa Mtaa kupitia ZamaradiTV Channel No.413 kwenye kisimbuzu cha AzamTV Kila Jumamosi na Jumapili saa 3:00 usiku na Marudio Jumapili na Jumatatu saa 8:00 Mchana.

Kwa Vipindi vilivyopita Tazama Kupitia Channel yetu ya Youtube

22/07/2025

MALKIA WA MTAA SARA DOMMY APANDISHWA HADHI!
Leo hii Msisili yatikisika!

Malkia wetu wa mtaa, Sara Dommy, anaandika historia mpya anapewa rasmi URAIS wa Msisili.

Usikose Kutazama Malkia wa Mtaa Kila Jumamosi na Jumapili saa 3:00 Usiku na Marudio Jumapili na Jumatatu saa 8:00 Mchana Kupitia ZamaradiTV.

Angalia pia Kupitia Youtube channel yetu kwa Vipindi vilivypita .

22/07/2025

Wakili maarufu nchini, Peter Kibatala, leo Julai 22, 2025, ameibuka katika Mahak**a Kuu ya Dodoma kufuatilia mashauri mawili yanayohusiana na kufutiwa usajili wa Glory of Christ Tanzania Church linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima, maarufu kwa jina la Ufufuo na Uzima.

Kibatala amesema shauri la kwanza ni Namba 16408 la Mwaka 2025, ambalo limefunguliwa na Dinali Mbaga na wenzake 51 dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP).

Kwa mujibu wa maelezo yake, shauri hilo liliitwa mahak**ani leo lakini halikusikilizwa kwa kina kutokana na taratibu za kimahak**a. “Kwa kawaida mashauri yanaendeshwa kwa njia mbili — ama kupitia mtandao (e-filing & virtual hearings) au kwa mahudhurio ya moja kwa moja mahak**ani,” aliongeza.

Amesema pia kuna shauri jingine la pili, lililofunguliwa na kanisa lenyewe, ambalo linapinga utaratibu uliotumika na mamlaka husika katika kulifutia usajili wake. Kibatala hakufafanua kwa undani kuhusu hoja za msingi kwenye shauri hilo la pili, lakini ameweka wazi kuwa linahusu haki na uhalali wa mchakato wa kisheria uliotumika dhidi ya taasisi ya kidini.

22/07/2025

Waziri wa Madini, Mheshimiwa Anthony Peter Mavunde, leo amekagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la kisasa la ghorofa nane la Kituo cha Jiomolojia Tanzania, TGC, linaloendelea kujengwa katika jiji la Arusha.

Mradi huo, unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 33, unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Madini na taasisi ya TGC, na unatarajiwa kuwa kitovu cha shughuli za uongezaji thamani madini ya vito, tafiti za kisayansi, pamoja na biashara ya madini nchini.

Katika ziara hiyo, Waziri Mavunde alipokea taarifa ya maendeleo kutoka kwa Mhandisi Julian Mosha wa Kampuni ya Skywards Lumocons Joint Venture, pamoja na msimamizi wa mradi kutoka TGC, Jumanne Nshimba.

Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri Mavunde alisema mradi huo ni wa kimkakati kwa sababu unakusudia kuwa na madarasa ya mafunzo, karakana, maabara ya kisasa ya madini, mabweni ya wanafunzi, na ofisi za chuo, huku pia ukiwa kituo cha One Stop Centre kwa wafanyabiashara wa madini.

Kwa upande wao, viongozi wa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini mkoani Arusha akiwemo Mwenyekiti wa AREMA Ndg. Alfred Mwaswenya na Mwenyekiti wa CHAMATA Ndg. Jeremia Kituyo, wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu ujenzi wa jengo hilo ambalo wamesema litaongeza fursa za ajira, ujuzi, na urahisi wa kufanya biashara katika mazingira salama na ya kitaalamu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mheshimiwa Kenani Kihongosi, amesema kuwa mradi huo utasaidia kuongeza mzunguko wa uchumi wa mkoa na kuiweka Arusha k**a kitovu cha madini ya vito Afrika Mashariki.

Jengo hilo linatarajiwa kukamilika ndani ya muda wa mkataba, na serikali imesisitiza dhamira yake ya kuifanya Tanzania kuwa kinara wa biashara na uongezaji thamani wa madini barani Afrika.

21/07/2025

WAZEE WA MILA WA KILUGURU WATOA BARAKA KWA KIBWANA SHOMARI KULEKEA PAMBANO LA NGUMI NA NKANE

Kuelekea pambano la ngumi la wachezaji wa Timu ya soka Ya Yanga Kibwana Shomari na Denis Nkane linalotarajia kufanyika Julia 26 mwaka huu jijini Dar es salaam wazee wa kimila Wa mkoani Morogoro wakiongozwa na chifu wa kabila la Waluguru Chifu Kingalu Mwana Banzi wa kumi na tano wamemfanyia masuala ya mila Mchezaji Kubwana Shomari Na kunpa Baraka zote kuelekea pambano hilo.

Akizungumza Mara baada ya kumfanyia mila mchezaji huyo wa Timu ya Yanga Kibwana shomari ,Chifu Kingalu amesema ana amini Kwamba mchezaji Kibwana Shomari ataenda kushinda katika pambano hilo kwa sababu kila kitu wameshakimaliza.

Kwa upande wake Kibwana shomari amejinasibu kumtwanga mpinzani wake Denis Nkane na Kuahidi kutoa kichapo kwa Mpinzani wake kwa Kuwa ameshajiandaa vya kutosha Hivyo suala la uahindi kwake ni lazima.

Pambano hilo linatarajia kufanyika tarehe 26 mwezi huu ambalo litawakutanisha wachezaji wa Timu ya Soka ya Yanga Pambano litakalokuwa la raundi tatu.

21/07/2025

"Hawana utu…” Maneno mazito kutoka kwa Sara Dommy, malkia wa mtaa, aliyefikia ukingoni mwa subira yake.

Akiwa na machozi yenye hasira na uchungu, Sara anasema mbele ya ummati wote - “Mbona nilivyokuwa na biashara nilikua nawalipa vizuri tu… mimi sio wa kwanza kukopa! Hawana utu!”

Uchungu wa mwanamke aliyepitia milima na mabonde kutoka kuwa mfanyabiashara anayelipa kwa wakati hadi kuwa mama anayechagua kati ya kumpeleka mtoto hospitali au kulipa deni.

Usikose kipindi cha MALKIA WA MTAA:Sara Dommy
Kila Jumamosi & Jumapili Saa 3:00 Usiku na Marudio: Jumapili & Jumatatu Saa 8:00 Mchana Kupitia ZAMARADI TV channel No.413 kwenye Kisimbuzi cha AzamTV pekee!!.

21/07/2025

ILIKUWA VITA YA KAZI!
Wadai na mdaiwa wote wanadai wako kazini!

Sara Dommy, malkia wetu wa mtaa, akiwa kwenye hali ya hamaki mbele ya kamera, alipigwa na butwaa pale wadai wa “Kausha Damu” walipomfuata nyumbani si kwa mazungumzo ilikua wanataka Chao tu.

Sara, akiwa anarekodi kipindi chake, anasema:
“Hii ndo kazi yangu kurekodi ‘Malkia wa Mtaa’”
Lakini wadai wakamjibu:
“Hata sisi tupo kazini hatujaja kurekodiwa!”

Vita alishuhudia Mpiga picha wetu

Address

Kinondoni

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zamaradi TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zamaradi TV:

Share

Category