Swahili Times

Swahili Times Habari bila mipaka, saa 24.
(448)

"Wana-CCM, wapenzi wa CCM na wale wakereketwa wa CCM,  endeleeni kukiimarisha chama chetu, kinatumainiwa na walio wengi....
20/12/2025

"Wana-CCM, wapenzi wa CCM na wale wakereketwa wa CCM, endeleeni kukiimarisha chama chetu, kinatumainiwa na walio wengi. Nakishukuru kwa kunilea katika kipindi chote mpaka hapa, bado ni mwanachama hai." - Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania akiwaaga wananchi wa Ruangwa

Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili nchini Uganda ambapo atamwakilisha Rais Samia Suluhu katika Mkuta...
20/12/2025

Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewasili nchini Uganda ambapo atamwakilisha Rais Samia Suluhu katika Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Nchi za Maziwa Makuu, utakaofanyika Desemba 21, 2025.

Rapa maarufu kutoka Canada, Drake, amepoteza dola 200,000 (takriban milioni 500) baada ya kumwekea dau Bondia Jake Paul,...
20/12/2025

Rapa maarufu kutoka Canada, Drake, amepoteza dola 200,000 (takriban milioni 500) baada ya kumwekea dau Bondia Jake Paul, akiamini angemshinda bingwa wa zamani wa uzito wa juu, Anthony Joshua, katika pambano lililofanyika Miami, Marekani.

Kuelekea pambano hilo, Drake alichapisha picha kwenye mtandao wa Instagram ikionesha dau la dola 200,000 aliloweka kwa Jake Paul.

"Duniani kote hakuna fedha inayoitwa ya serikali; serikali ni mratibu tu. Miundombinu yote inayojengwa ni fedha yenu [wa...
20/12/2025

"Duniani kote hakuna fedha inayoitwa ya serikali; serikali ni mratibu tu. Miundombinu yote inayojengwa ni fedha yenu [wananchi], iwe imekusanywa siku hiyo hiyo au iwe ya mkopo." - Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri Mkuu akiweka jiwe la msingi ujenzi wa Kampasi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mkoa wa Lindi

"Serikali imeendelea kuimarisha Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kwa kuongeza bajeti kutoka TZS bilioni 464 mwaka 2020/202...
20/12/2025

"Serikali imeendelea kuimarisha Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu kwa kuongeza bajeti kutoka TZS bilioni 464 mwaka 2020/2021 hadi bilioni 916.7 kwa mwaka 2025/2026 ikiwa ni ongezeko la asilimia 98 ndani ya miaka minne." - Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri Mkuu

1. Real Madrid: TZS trilioni 16.82. Manchester United: TZS trilioni 16.53. FC Barcelona: TZS trilioni 144. Liverpool: TZ...
20/12/2025

1. Real Madrid: TZS trilioni 16.8

2. Manchester United: TZS trilioni 16.5

3. FC Barcelona: TZS trilioni 14

4. Liverpool: TZS trilioni 13.5

5. Manchester City: TZS trilioni 13.2

Chanzo: Forbes

Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo amesema Taifa Stars haikuvalia vazi linalowakilisha taifa wakati ikiwasili Morocco ...
20/12/2025

Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo amesema Taifa Stars haikuvalia vazi linalowakilisha taifa wakati ikiwasili Morocco kwenye mashindano ya AFCON kutokana na Tanzania kutokuwa na vazi rasmi la Taifa.

Ndimbo ameongeza kuwa hata vazi la Kimaasai, ambalo wengi wamelitaja, si utambulisho rasmi wa taifa, kwani hata Kenya kuna kabila la Kimaasai.

20/12/2025

  Jumamosi Desemba 20, 2025
20/12/2025



Jumamosi Desemba 20, 2025

Simba SC imemtambulisha raia wa Afrika Kusini, Steve Barker kuwa kocha wake mkuu.Barker alikuwa akiinoa Stellenbosch ya ...
19/12/2025

Simba SC imemtambulisha raia wa Afrika Kusini, Steve Barker kuwa kocha wake mkuu.

Barker alikuwa akiinoa Stellenbosch ya nchini humo.

Rais Samia Suluhu Hassan amezungumza na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Mahusiano ya Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika ya Ku...
19/12/2025

Rais Samia Suluhu Hassan amezungumza na Waziri Mstaafu wa Mambo ya Mahusiano ya Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika ya Kusini, Dkt. Grece Naledi Mandisa Pandor aliyefika Ikulu Ndogo Tunguu, Zanzibar kuwasilisha ujumbe maalum wa Rais wa Afrika ya Kusini, Cyril Ramaphosa.

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Uvuvi iliyopo Kilwa mkoani Lindi.Amesem...
19/12/2025

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo amekagua maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Uvuvi iliyopo Kilwa mkoani Lindi.

Amesema kukamilika kwa mradi huo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza kipato na kubadili maisha ya Mtanzania pamoja na kuongeza pato la Taifa.

Address

Kinondoni

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Swahili Times posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Swahili Times:

Share