Swahili Times

  • Home
  • Swahili Times

Swahili Times Habari bila mipaka, saa 24.
(448)

21/08/2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa amekanusha taarifa kwamba tiketi zote za mchezo wa robo fainali ya CHAN 2024 zimenunuliwa na Kenya.

Rais Samia Suluhu amepewa tuzo maalumu na wakandarasi nchini kwa kuthamini mchango wake na hatua alizochukua kwenye sekt...
21/08/2025

Rais Samia Suluhu amepewa tuzo maalumu na wakandarasi nchini kwa kuthamini mchango wake na hatua alizochukua kwenye sekta ya ujenzi tangu aingie madarakani.

Tuzo hiyo imepokelewa kwa niaba yake na Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, katika tukio lililofanyika ukumbi wa The Super Dome, Dar es Salaam.

21/08/2025

Kiongozi wa Chama cha Democracy for the Citizens Party (DCP), Rigathi Gachagua, amerejea nchini Kenya baada ya ziara yake ndefu nchini Marekani na kupokelewa na maelfu ya wafuasi wake.

Gachagua anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara, hatua ambayo serikali imesema itafuatilia kwa karibu ili kuzuia uvunjifu wa amani.

21/08/2025

Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula amesema bodi inaandaa orodha ya waandishi wa Habari walioweka vyeti feki kwenye mfumo kwa ajili ya kuhakikiwa ili ikabidhiwe kwa Jeshi la Polisi.

Klabu ya Azam imetangaza kuachana na kipa wake, Mohamed Mustafa kutoka Sudan baada ya kufikia makubaliano ya pande mbili...
21/08/2025

Klabu ya Azam imetangaza kuachana na kipa wake, Mohamed Mustafa kutoka Sudan baada ya kufikia makubaliano ya pande mbili.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taif...
21/08/2025

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Samia Suluhu akiongoza Kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, leo jijini Dodoma.

Lengo la kikao ni uteuzi wa wagombea ubunge, wabunge wa viti maalum, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Viti Maalum.

21/08/2025

Viwango vya kubadilisha fedha za kigeni Agosti 21, 2025.
21/08/2025

Viwango vya kubadilisha fedha za kigeni Agosti 21, 2025.

Wananchi katika vitongoji mbalimbali Arusha wamekusanyika kushuhudia maonesho ya moja kwa moja yaliyolenga kutoa elimu j...
21/08/2025

Wananchi katika vitongoji mbalimbali Arusha wamekusanyika kushuhudia maonesho ya moja kwa moja yaliyolenga kutoa elimu juu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa umeme. Tukio hili ni sehemu ya kampeni za kitaifa zinazotekelezwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Nishati, UKAid na programu ya MECS, ambazo zilibuniwa kuunga mkono Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia wa 2024–2034.

Kupitia kampeni hizi, Tanzania inalenga kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2034, angalau asilimia 80 ya kaya zote nchini zinatumia mbinu safi, salama na endelevu za kupikia.

Jeshi la Polisi mkoani Mara linamshikilia mlinzi wa kampuni ya ulinzi ya Guard Force, Adili Matayo (31) kwa tuhuma za ku...
21/08/2025

Jeshi la Polisi mkoani Mara linamshikilia mlinzi wa kampuni ya ulinzi ya Guard Force, Adili Matayo (31) kwa tuhuma za kumjeruhi kwa risasi Deus Wambehu (16), Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Majimoto. Tukio hilo lilitokea alipokuwa akijaribu kuwakamata watu waliovamia mgodi wa dhahabu wa Chang Shen kwa lengo la kuiba mawe yadhaniwayo kuwa ni dhahabu.

Mwanafunzi huyo anaendelea na matibabu katika Kituo cha Afya Iramba.

20/08/2025

Rais Samia Suluhu ameizawadia timu ya Taifa (Taifa Stars) TZS milioni 200 ili kuwapa motisha katika mchezo wa robo fainali ya CHAN 2024 dhidi ya Morocco, utakaochezwa Agosti 22, 2025 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Swahili Times posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Swahili Times:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share