MKOA WA LINDI RS

MKOA WA LINDI RS Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MKOA WA LINDI RS, Media/News Company, Lindi.
(1)

21/12/2025

Mikoa yote anzisheni vitengo vya ukaguzi na muwe pia na vifaa vya kuchunguza majengo na miradi mingine badala ya kusubiri uchunguzi unaofanywa wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru-Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba, Lindi-Tanzania. Desemba 21, 2025


DKT MWIGULU AAGIZA ZIUNDWE TIMU ZA MIKOA ZA WAKAGUZI WA MIRADI Ataka watenge bajeti ya vifaa vya ukaguzi   Waziri mkuu D...
21/12/2025

DKT MWIGULU AAGIZA ZIUNDWE TIMU ZA MIKOA ZA WAKAGUZI WA MIRADI

Ataka watenge bajeti ya vifaa vya ukaguzi  

Waziri mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amemwagiza Waziri wa Nchi (OWM-TAMISEMI) awaandikie barua Wakuu wote wa Mikoa ili waunde timu za ukaguzi wa majengo na miradi kwenye mikoa yao k**a njia ya kukabiliana na wakandarasi wanaokiuka makadirio ya gharama za ujenzi (BOQ) wa miradi ya Serikali.  

“Yuko Mhandisi ambaye huwa anakagua miradi wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru. Wakuu wa Mikoa wote wawe na timu za vijana wa aina hiyo, ili wasiuziwe mbuzi kwenye gunia. Iwe ni utamaduni wa Serikali kufanya ukaguzi wa aina hiyo,” amesema Waziri Mkuu.  

Ametoa agizo hilo leo (Jumapili, Desemba 21, 2025) wakati akizungumza na viongozi na wananchi wa Wilaya za Ruangwa na Nachingwea, mkoani Lindi akiwa katika ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya maendeleo mkoani humo.  

Akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea, Waziri Mkuu amesema kuna baadhi ya miradi ambayo wakandarasi wake hawafuati BOQ.

“Unakuta BOQ inataka nondo za mm 16 lakini mkandarasi anaweka za mm 12. Kuna mahali zinatakiwa nondo sita, yeye anaweka nondo nne. Jengo likikamilika, huwezi kuona na kulinganisha makubaliano ya BOQ.  Nimeelekeza kila mkoa uwe na timu ya wataalamu wa kukagua miradi ya Serikali.”  

“Mikoa yote wawe na vitengo hivi na wawe pia na vifaa vya kuchunguza majengo na miradi mingine badala ya kusubiri uchunguzi unaofanywa wakati wa mbio za Mwenge wa Uhuru. Vitengo hivyo kazi yao ya kila siku ni kufuatilia miradi ili kubaini maeneo ambako Serikali imetoa fedha na hazijatumika vizuri ili tuweze kuchukua hatua,” amesisitiza.


WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU KASSIM MAJALIWA Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba a...
21/12/2025

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AKUTANA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU KASSIM MAJALIWA

Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba amekutana na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa nyumbani kwake Nandagala, Ruangwa mkoani Lindi.

Mhe. Dkt. Mwigulu amekutana naye wakati akiwa katika ziara ya siku tatu ya kikazi mkoani Lindi.


DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI LINDI–RUANGWA–NACHINGWEAWaziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ...
21/12/2025

DKT. MWIGULU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI LINDI–RUANGWA–NACHINGWEA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, leo Desemba 21, 2025 ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa Mradi wa Maji wa Lindi–Ruangwa–Nachingwea katika Kijiji cha Chimbila A, Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi.

Mradi huo wa maji unaochota maji kutoka Mto Nyangao uliopo Wilaya ya Lindi, unatekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA). Mradi utanufaisha jumla ya vijiji 56, ambapo vijiji 34 vipo Wilaya ya Ruangwa, vijiji 21 Wilaya ya Nachingwea na kijiji 1 Wilaya ya Lindi.

Ujenzi wa mradi huo unagharimu jumla ya shilingi bilioni 119 na hadi sasa umefikia asilimia 67% ya utekelezaji. Mradi ulianza kutekelezwa Februari 2023 na unatarajiwa kukamilika Juni 2026 kwa hatua ya kwanza. Hata hivyo, ifikapo Februari 2026 baadhi ya vijiji vitaanza kupata huduma ya maji safi na salama.

Akizungumza baada ya uwekaji wa jiwe la msingi, Mhe. Dkt. Mwigulu amesema ameridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi huo, akieleza kuwa maendeleo yaliyofikiwa yanazidi kiwango cha fedha kilichotolewa hadi sasa.

“Hivi ndivyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anavyotaka kuona kazi za maendeleo zikifanyika. Hapa tumeona asilimia ya utekelezaji ni kubwa kuliko fedha zilizotolewa hadi sasa,” amesema Dkt. Nchemba.

Aidha, Mhe. Dkt. Mwigulu ametumia fursa hiyo kumpongeza Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Kassim Majaliwa, kwa kuasisi mradi huo na kufuatilia kwa karibu upatikanaji wa fedha za utekelezaji wake, hatua ambayo imewezesha mradi kufikia hatua ya kuridhisha.


DKT. MWIGULU AKAGUA HALI YA BANDARI YA BARAZANI MKOANI LINDI Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 21, 2025 ameka...
21/12/2025

DKT. MWIGULU AKAGUA HALI YA BANDARI YA BARAZANI MKOANI LINDI

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 21, 2025 amekagua hali ya bandari ya Barazani mkoani Lindi na kuiagiza Mamlaka ya Bandari Tanzania kukamlisha kwa haraka michakato ya awali ya kitaalam ya ujenzi wa mradi wa Bandari ya Ngongo wilayani Lindi mkoani Lindi.

Amesema kukamilika kwa bandari ya Ngongo kutasaidia kuwaondolea adha watumiaji wa bandari inayotumika sasa ya Barazani ambayo hali yake haiendani na mahitaji ya sasa. Dkt. Mwigulu ameongeza kuwa kukamilika kwa ujenzi wa bandari ya Ngongo kutaleta chachu ya maendeleo mkoani humo kwani bandari ya Lindi imeanza kuchangamkiwa na wafanyabiashara, wakiwemo wa nchi jirani.

  ZAMU YA RUANGWA NA NACHINGWEA , DESEMBA 21, 2025.Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Desemba 21, 2025 ,...
21/12/2025

ZAMU YA RUANGWA NA NACHINGWEA , DESEMBA 21, 2025.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Desemba 21, 2025 , anaendelea na ziara yake Mkoani Lindi ambapo ataweka jiwe la Msingi mradi wa maji wola ya Ruangwa na kutembelea kuona na kukagua ujenzi wa jengo la halmashauri yaNachingwea .

Tufuatilie kupitia kurasa zetu kwa taarifa zaidi.

21/12/2025

WAZIRI MKUU ASISITIZA UHAKIKA WA UPATIKANAJI WA DAWA KATIKA MAENEO YA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA.

21/12/2025

RC LINDI AELEZA MAFANIKIO MAKUBWA YA ELIMU, AONESHA MATUMAINI MAKUBWA KWA KAMPASI YA UDSM LINDI

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack , ameeleza mafanikio makubwa ya sekta ya elimu mkoani Lindi wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi Chuo Kikuu Cha Dar es salaam kampasi ya Lindi.

Mhe. Telack amesema mkoa wa Lindi umeendelea kufanya vizuri kielimu, ambapo katika matokeo ya kidato cha sita mkoa ulifikia asilimia 96 ya ufaulu na kushika nafasi ya sita kitaifa katika matokeo darasa la 7.

Aidha, katika matokeo ya kidato cha nne, mkoa umefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya wanafunzi waliopata daraja la sifuri na daraja la nne.

Katika hatua nyingine, ameeleza mafanikio yaliyopatikana kupitia uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, hususan katika kutoa fedha za ujenzi wa miradi mbalimbali ya elimu, ikiwemo ujenzi wa shule za kisasa.

Miongoni mwa miradi hiyo ni shule ya kisasa ya LNG, ambayo itakuwa shule ya 23 kujengwa katika mkoa wa Lindi ndani ya kipindi cha uongozi wake.

Akizungumzia kuhusu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kampasi ya Lindi, Mhe. Telack amesema:

“Tunakiu kubwa na chuo hiki, ndiyo maana tulitoa eneo la hekari 113 na baadaye tukaliongeza kwa hekari 260. Aidha, tulitoa pia eneo jingine kwa ajili ya shughuli za kilimo, kwani chuo hiki kitakuwa kikitoa mafunzo ya kilimo.”

Mhe. Telack ameahidi kuendelea kusimamia kwa karibu matumizi ya fedha zitakazotolewa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wa Lindi. Vilevile, ameahidi kuendelea kushughulikia na kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wa mkoa huo.



WAZIRI MKUU AITAKA KAMPASI YA UDSM LINDI KUWA KITOVU CHA UBORA WA TAFITI NA UBUNIFU WA KILIMOWaziri Mkuu wa Jamhuri ya M...
20/12/2025

WAZIRI MKUU AITAKA KAMPASI YA UDSM LINDI KUWA KITOVU CHA UBORA WA TAFITI NA UBUNIFU WA KILIMO

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, amekiagiza Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kampasi ya Lindi kuhakikisha kinakuwa kitovu cha ubora wa wataalamu wa tafiti na ubunifu unaolenga kutatua changamoto halisi zinazowakabili wakulima, wafugaji na wavuvi nchini.

Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi la kampasi hiyo, Dkt. Mwigulu amesema kampasi hiyo mahususi kwa masuala ya kilimo inapaswa kujikita katika tafiti zitakazosaidia upatikanaji wa mbegu bora, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi pamoja na kuongeza tija katika uzalishaji wa kilimo, ufugaji na uvuvi.

Ameeleza kuwa Kampasi ya UDSM Lindi itachangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha sekta ya kilimo, ambayo ni uti wa mgongo wa uchumi wa Taifa, kupitia maendeleo ya elimu, sayansi, teknolojia na tafiti bunifu.

Ujenzi wa kampasi hiyo unagharimu jumla ya shilingi bilioni 14.8 za Kitanzania na umefikia asilimia 60 ya utekelezaji. Kampasi hiyo inatarajiwa kuanza kudahili wanafunzi katika muhula mpya wa masomo unaoanza Oktoba mwaka ujao.

Kampasi ya UDSM Lindi imejengwa katika eneo la Ngongo, wilayani Lindi, huku kituo cha tafiti kikijengwa katika Wilaya ya Ruangwa, mkoani Lindi.


DKT. MWIGULU AKAGUA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA LINDI.WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 20, 2025...
20/12/2025

DKT. MWIGULU AKAGUA UJENZI WA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA LINDI.

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 20, 2025 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi pamoja na kusalimia baadhi ya wananchi wanaopata huduma katika hospitali hiyo.


Address

Lindi
LINDI

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MKOA WA LINDI RS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MKOA WA LINDI RS:

Share