MKOA WA LINDI RS

MKOA WA LINDI RS Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MKOA WA LINDI RS, Media/News Company, Lindi.
(1)

Wataalam wa sheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria leo, Juni 8, 2026, wamewapatia mafunzo maalumu waandishi wa habari ...
08/06/2026

Wataalam wa sheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria leo, Juni 8, 2026, wamewapatia mafunzo maalumu waandishi wa habari mkoani Lindi kwa lengo la kuwawezesha kutoa elimu kwa wananchi kuhusu uwepo wa Kituo cha Huduma kwa Mteja pamoja na huduma mbalimbali za kisheria zinazotolewa kupitia kituo hicho, hatua inayolenga kuongeza uelewa wa wananchi na kuimarisha upatikanaji wa taarifa sahihi za masuala ya kisheria.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Wakili wa Serikali kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Erick Salila, amesema kuwa kituo hicho kimeanzishwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa huduma za kisheria kwa wananchi, hususan wananchi wanaohitaji msaada wa kisheria au kuwasilisha malalamiko yanayohusiana na ukiukwaji wa sheria, vitendo vya uhalifu, pamoja na masuala ya rushwa.

Ameeleza kuwa kupitia mafunzo hayo, waandishi wa habari wanatarajiwa kuwa mabalozi wa kuifikia jamii kwa kuhamasisha wananchi kutambua na kutumia huduma zinazopatikana katika kituo hicho.

Aidha, wananchi wenye malalamiko, maoni au wanaohitaji ushauri kuhusu masuala ya sheria wametakiwa kutumia Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuwasiliana kupitia Sanduku la Posta 315, Dodoma, simu ya bure 0800 004 004, simu ya kawaida 026 216 0360, barua pepe [email protected] au WhatsApp namba 0739 101 910.

 , Bw. Mwinjuma Mkungu, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Uchumi na Uzalishaji kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Lindi, akiz...
07/06/2026

, Bw. Mwinjuma Mkungu, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Uchumi na Uzalishaji kutoka Sekretarieti ya Mkoa wa Lindi, akizungumza na Dkt. Nazareth Madala, Mkurugenzi wa Ukuzaji Viumbe Maji nchini kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kuhusu mikakati ya kufufua Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji Nyengedi/Mtama.

Mazungumzo hayo yalifanyika walipokutana katika warsha ya kupitia ripoti ya mwisho ya utekelezaji wa Mradi wa ARNSA iliyofanyika mjini Songea Juni 5, 2026.

Katika mazungumzo yao, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeahidi kuanza kwa kulipa fidia ya maeneo yaliyotwaliwa pamoja na kuendeleza miundombinu ya uzalishaji wa vifaranga bora vya samaki. Hatua hiyo inatarajiwa kuwanufaisha wafugaji wa samaki katika Mkoa wa Lindi na kuongeza tija katika sekta ya ufugaji wa samaki.

Kwa upande wa Mkoa wa Lindi, tayari umeendelea kuunga mkono juhudi za kufufua kituo hicho kwa kukipatia nyavu maalum za kukuzia vifaranga (happa nets), vifaranga 40,000 vya samaki pamoja na chakula cha samaki. Msaada huo ni sehemu ya mkakati wa mkoa wa kuimarisha ufugaji wa samaki na kupunguza utegemezi wa samaki wa baharini pekee k**a chanzo cha mazao ya uvuvi na lishe kwa wananchi.


Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Lindi, ikiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Ziwena Omary, imefanya ziara ya kute...
06/06/2026

Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Lindi, ikiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Bi. Ziwena Omary, imefanya ziara ya kutembelea maeneo ya kihistoria ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara yaliyopo Wilaya ya Kilwa, kwa lengo la kujionea vivutio vya utalii na mchango wake katika kukuza uchumi wa wilaya, mkoa na taifa kwa ujumla.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 06 Juni, 2026, ambapo Bi. Ziwena aliambatana na Kamati ya ulinzi na usalama Mkoa, watumishi na waongoza watalii kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA). Katika ziara hiyo, wajumbe walipata fursa ya kutembelea na kujionea urithi wa kihistoria uliopo katika maeneo hayo, ikiwemo majumba ya masultani wa kale, magofu ya misikiti ya zamani, Ngome ya Wareno na mabaki mengine ya ustaarabu wa kale wenye historia kubwa katika Pwani ya Afrika Mashariki.

Aidha, Bi. Ziwena alishiriki zoezi la upandaji miti ya mikoko, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani na juhudi za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira pamoja na rasilimali za asili kwa maendeleo endelevu ya kizazi cha sasa na kijacho.

Ziara hiyo imeonesha dhamira ya Serikali ya kuendelea kuhifadhi na kutangaza maeneo ya kihistoria na vivutio vya utalii, sambamba na kuimarisha juhudi za utunzaji wa mazingira kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla.

05/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainabu Telack, amewataka wafugaji kuhamia katika maeneo maalumu yaliyotengwa kwa shughuli za ufugaji ili kuhakikisha hifadhi za misitu zinalindwa na kuhifadhiwa kwa uendelevu. Amesisitiza umuhimu wa kuzingatia mbinu za ufugaji wa kisasa ambazo zinachangia kuongeza tija huku zikilinda mazingira.

Mhe. Telack ametoa wito huo wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya mifugo kilichofanyika wilayani Kilwa, mkoani Lindi, Juni 4, 2026.

Leo, Juni 4, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainabu Telack, ameongoza kikao cha wadau wa sekta ya mifugo kilichofanyi...
04/06/2026

Leo, Juni 4, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainabu Telack, ameongoza kikao cha wadau wa sekta ya mifugo kilichofanyika wilayani Kilwa, mkoani Lindi, kikao ambacho kimewakutanisha wafugaji wa mifugo kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayohusu sekta hiyo na kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Telack amewataka wafugaji kuhakikisha migogoro kati ya wakulima na wafugaji inakoma kabisa. Amesisitiza kuwa migogoro hiyo inaweza kumalizika ikiwa kila upande utazingatia matumizi ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli zake. Wafugaji wametakiwa kubaki katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya ufugaji, huku wakulima wakitumia maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya kilimo.

Kikao hicho, kilichoongozwa na Mhe. Telack, kimeazimia mambo mbalimbali ikiwemo kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za matumizi bora ya ardhi kwa kuheshimu watumiaji wengine wa ardhi. Aidha, wafugaji hawaruhusiwi kwenda kununua mabua katika mashamba ya wakulima.

Vilevile, Mwenyekiti wa Wafugaji ameagizwa kuwasilisha mpango mkakati wa uchimbaji wa visima ili kusaidia kupunguza migogoro. Wafugaji wote wanaofuga mifugo katika hifadhi za misitu wametakiwa kuondoka mara moja. Kadhalika, wafugaji waliopo katika maeneo ambayo hayajatengwa kwa ajili ya shughuli za ufugaji wametakiwa kuondoka mara moja.

Vilevile, kikao kimeazimia kuwa watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanapaswa kupelekwa shule kwa ajili ya masomo badala ya kuendelea kujihusisha na shughuli za uchungaji wa mifugo pekee.

Kikao hicho kililenga kuboresha sekta ya mifugo kwa kuwakutanisha wafugaji ili kujadili changamoto zilizopo na kuweka mikakati madhubuti ya kuendeleza sekta hiyo kwa manufaa ya wafugaji na jamii kwa ujumla.

 : PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI - LINDIWilaya ya Kilwa, Juni 4, 2026.
04/06/2026

: PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI - LINDI

Wilaya ya Kilwa, Juni 4, 2026.

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, amefungua kikao cha wadau wa sekta za mifugo na uvuvi kinachofanyika katika W...
04/06/2026

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Zainab Telack, amefungua kikao cha wadau wa sekta za mifugo na uvuvi kinachofanyika katika Wilaya ya Kilwa. Katika kikao hicho, ameambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi, Bi. Zuwena Omary pamoja na viongozi wengine.

Kikao hicho ni sehemu ya mwendelezo wa vikao vya wadau vilivyoanza siku moja iliyopita, vikilenga kujadili fursa, changamoto na mikakati ya kuimarisha maendeleo ya sekta za mifugo na uvuvi mkoani Lindi.

Endelea kufuatilia kurasa zetu kwa taarifa, picha na matukio zaidi kutoka katika kikao hicho.


SDA YAIPANGUVU UMITASHUMTA NA UMISETA MKOA WA LINDI.Ikiwa msimu mpya wa UMITASHUMTA umeanza ngazi ya Mkoa , Lindi imepok...
04/06/2026

SDA YAIPANGUVU UMITASHUMTA NA UMISETA MKOA WA LINDI.

Ikiwa msimu mpya wa UMITASHUMTA umeanza ngazi ya Mkoa , Lindi imepokea vifaa vya michezo kutoka shirika lisilo la kiserikali Sports Develpoment Aid ( SDA) kwa lengo la kuipa nguvu mashindano hayo ya UMITASHUMTA ambayo yanalenga kuibua vipaji shuleni, hamasa ya ujifunzaji na kuimarisha afya.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, mkurugenzi wa Shirika hilo ndugu Ramso Lucas, amesema kuwa wanayo hali ya kuendelea kuunga juhudi za serikali katika kuendeleza kukuza michezo shuleni kwa lengo la kuibua vipaji, kutoa hamasa ya ujifunzaji shuleni na kuimarisha afya.

“tunaendelea kuhakikisha vijana wanapata fursa ya kuendelea kucheza na kujifunza, tukiamini kwamba, michezo inasehemu kubwa ya ujifunzaji mashuleni. Na kwa kutambua pia jitihada za serikali katika ku-organize michezo ya wanafunzi mashuleni na vyuoni . Tupo hapa leo kuunga mkono jitihada hizo“ Mkurugenzi SDA Ramso.

Vifaa vilivyokabidhiwa ni mipira 10 ya michezo zaidi, ikiwemo mipira ya pete, mipira ya miguu, mipira ya wavu pamoja na jozi za viatu 20.

Mkurugenzi huyo wa SDA ametoa wito kwa serikali kuendelea kuweka nguvu katika michezo kuwa sehemu ya ujifunzaji shuleni .

Kwa upande wake kaimu afisa elimu Mkoa wa Lindi Mwalimu Humphrey Sanga, amemshukuru mkurugenzi kwaniaba ya katibu Tawala Mkoa wa Lindi kwa jitihada zao za kuendelea kuunga juhudi za serikali za kukuza na kuendeleza michezo shuleni .

“ kwa ujumla tunashukuru sana Sport Development Aid, kwa namns mmekuwa mkishirikiana na sisi katika kuwa-support vijana na kuendeleza michezo katika mkoa wetu wa Lindi, mmekuwa nguzo imara sana katika maeneo ya michezo “ Mwalimu Sanga - Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Lindi.

Makabidhiano hayo yamefanyika Juni 3, 2026 katika ofisi za Mkuu wa Mkoa Lindi na kuhudhuriwa na wajumbe kadhaa wakiwemo viongozi wa michezo RAS Boma Sports Club, Afisa Utamaduni Mkoa na mjumbe wa viongozi wa k**ati ya uendeshaji UMITASHUMTA mkoa .

Kauli mbiu ya UMITAMSHUMTA 2026 Inasema “ Michezo na Sanaa Shuleni Daraja la Ajira, Afya na Ushindani wa Kimataifa “



Michezo

03/06/2026

Mhe. Telack amesisitiza kuwa bandari hiyo itahitaji kiwango kikubwa cha mazao ya uvuvi ili kukidhi mahitaji ya soko, hivyo amewahimiza kuzalisha samaki kwa wingi sambamba na kuachana na vitendo vya uvuvi haramu vinavyoharibu mazingira ya bahari na kuhatarisha upatikanaji endelevu wa rasilimali za uvuvi.

Aidha, ameelekeza shughuli za uvuvi zifanywe na watu wazima.

Kilwa, Juni 3, 2026


03/06/2026

“Amani ni msingi muhimu wa maendeleo kwa kuwa huwezesha wafugaji, wavuvi na wawekezaji kutekeleza shughuli zao kwa uhuru na tija. Aidha, amesema usalama ni nguzo muhimu katika kulinda rasilimali za mifugo na bahari dhidi ya vitendo vinavyoweza kuhatarisha uzalishaji na uendelevu wa sekta hiyo, k**a vile uvuvi haramu.“ Bi. Zuwena Omary


Address

Lindi
LINDI

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MKOA WA LINDI RS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MKOA WA LINDI RS:

Share