MKOA WA LINDI RS

MKOA WA LINDI RS Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from MKOA WA LINDI RS, Media/News Company, Lindi.
(1)

  Kumbukizi
14/10/2025

Kumbukizi

ZIMEBAKI SIKU 16 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.Kura yako Haki Yako Jitokeze kupiga kura Oktoba 2025.
13/10/2025

ZIMEBAKI SIKU 16 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU.

Kura yako Haki Yako Jitokeze kupiga kura Oktoba 2025.






KATIBU TAWALA MKOA WA LINDI  BI  ATASHIRIKI UCHAGUZI MKUU 29,2025 .Kura yako Haki yako Jitokeze kupiga kura Oktoba 29, 2...
13/10/2025

KATIBU TAWALA MKOA WA LINDI BI ATASHIRIKI UCHAGUZI MKUU 29,2025 .

Kura yako Haki yako Jitokeze kupiga kura Oktoba 29, 2025.






13/10/2025

Mradi wa Ujenzi wa Shule ya Sekondari Mtuanana Halmashauri ya Nachingwea unagharimu zaidi ya Milioni 560 umefikia hatua za mwisho ambapo wanafunzi ambao wakisagiri umbali mrefu kutafuta elimu sasa changamoto hiyo imepata ufumbuzi .

Hayo yameelezwa mara baada ya timu ya ufuatiliaji na tathimini kutoka Mkoani Lindi kutembela mradi huo na kuona namna ambavyo umetekelezwa .

Shule hiyo imeanza kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2025 . Kazi umaliziaji inaendelea.

SIKU HAZIGANDI , OKTOBA 29, 2025 LINDI TUNAUNGANA NA WATANZANIA WOTE KUANDIKA HISTORIA YA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.k...
12/10/2025

SIKU HAZIGANDI , OKTOBA 29, 2025 LINDI TUNAUNGANA NA WATANZANIA WOTE KUANDIKA HISTORIA YA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025.

kura yako Haki yako Jitokeze kupiga Kura Oktoba 29,2025.

ZIMEBAKI SIKU 18 KUELEKA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025.
11/10/2025

ZIMEBAKI SIKU 18 KUELEKA UCHAGUZI MKUU OKTOBA 29, 2025.

MIRADI YA ZAIDI BIL 2 YATEMBELEWA NA TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHIMINI YA MKOA, WILAYANI NACHINGWEA. Timu ya ufuatiliaji ...
10/10/2025

MIRADI YA ZAIDI BIL 2 YATEMBELEWA NA TIMU YA UFUATILIAJI NA TATHIMINI YA MKOA, WILAYANI NACHINGWEA.

Timu ya ufuatiliaji na tathimini ya Mkoa wa Lindi imefanya ufuatiliaji na tathimini ya miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Nachingwea leo Oktoba 10, 2025 ambapo miradi yenye thamani ya zaidi ya Bilioni mbili imetembelewa katika Tarafa ya kilimarondo na Naipanga.

Timu hiyo ambayo imeongozwa na katibu Tawala Msaidizi Mkoa seksheni ya Mipango na uratibu Ndugu Juhudi Mgallah akiambatana na wataalamu kutoka mkoani na Halmashauri, wamefanya ufuatiliaji wa pamoja na tathimini katika miradi ifuatayo; ujenzi wa shule Tatu za sekondari ambazo kila moja imegharimu zaidi ya Milioni 560, Shule hizo ni Shule ya Sekondari Mtuanana, Shule ya Sekondari Chiumbati Shuleni na Shule ya Sekondari Amani, umaliziaji wa Nyumba ya Afisa Tarafa ya kilimarondo Milioni 35, ujenzi wa Nyumba ya Mwalimu Shule ya Sekondari kilimarondo Milioni 37, ujenzi wa Mabweni mawili yenye matundu 16 kwa thamani ya Milioni 283 na ujenzi wa mabweni mawili bila choo kwa thamani ya Milinioni 256.

Aidha, timu hiyo inatarajia kuendelea na ufuatiliaji siku ya pili Oktoba 11, 2025 katika wilaya hiyo na baadae kutoa mrejesho wa pamoja kwa ajili ya kuongeza ufanisi katika kufanikisha miradi kwa viwango vyenye vinavyohitajika.





RAS LINDI SPORTS CLUB YAKABIDHI KOMBE LA SHIMIWI KWA RAS. RAS AWAPONGEZA .Timu ya RAS Lindi Sports Club imekabidhi Kombe...
10/10/2025

RAS LINDI SPORTS CLUB YAKABIDHI KOMBE LA SHIMIWI KWA RAS. RAS AWAPONGEZA .

Timu ya RAS Lindi Sports Club imekabidhi Kombe la Nidhamu kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi (RAS), baada ya kushiriki mashindano ya michezo ya SHIMIWI 2025 yaliyofanyika jijini Mwanza.

Katika hafla hiyo, Mwenyekiti wa timu Ndugu. Ramadhan Khatibu amemshukuru Katibu Tawala Mkoa kwa kuiwezesha timu kushiriki kikamilifu katika mashindano hayo, pamoja na kutoa shukrani za dhati kwa niaba ya familia ya marehemu Afisa Michezo wa Mkoa, Bw. Chiza Gwidegembya, aliyefariki dunia wakati timu ikiwa kwenye mashindano.

Kwa upande wake, Katibu Tawala Mkoa wa Lindi Bi. Zuwena Omary amewapongeza wanamichezo wa timu hiyo kwa Kuonesha mfano bora kinidhamu na kurejea wakiwa na Kombe la Nidhamu, Medali na Cheti vya Ushiriki pamoja na medali ya mshindi wa mbio za mita 800.

“Niwapongeze kwa namna mlivyoshiriki mashindano haya na kwa mafanikio haya mliyoyapata. Kombe hili la nidhamu nalipokea k**a msingi wa kuhakikisha Lindi tunaendelea kuwa na nidhamu, uwajibikaji na umoja katika kazi na michezo ili tuweze kufikia malengo tuliyojiwekea” alisema RAS Lindi.

Aidha, RAS aliwataka watumishi wa serikali kuendelea kumuenzi marehemu Chiza Gwidegembya kwa kuendeleza yale yote mema aliyoyaacha,hasa katika uongozi, utendaji kazi, na mapenzi kwa michezo na kusisitiza umuhimu wa kuwa na mipango endelevu ya mashindano na hafla za michezo ili kuimarisha ushirikiano na kuongeza ari ya ushindani.

“Tuwasaidie viongozi wetu wa klabu kuandaa hafla za kimichezo kwa bajeti zilizo ndani ya uwezo wetu ambazo zitatujenga kimichezo na kujenga ushawishi miongoni mwa watumishi wenzetu kwa kupata matokeo mazuri na kuweka nia thabiti ya kushindana” Ameongeza.

ICU YA ZAIDI YA MIL 600 YASHUSHWA NACHINGWEA.
10/10/2025

ICU YA ZAIDI YA MIL 600 YASHUSHWA NACHINGWEA.



MRADI WA HEWA TIBA HALMASHAURI YA RUANGWA
10/10/2025

MRADI WA HEWA TIBA HALMASHAURI YA RUANGWA



ZIMEBAKI SIKU 19 KUELEKEA OKTOBA 29,2025 TUPIGE KURA .
10/10/2025

ZIMEBAKI SIKU 19 KUELEKEA OKTOBA 29,2025 TUPIGE KURA .

10/10/2025

Tunajivunia Mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita

Address

Lindi
LINDI

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MKOA WA LINDI RS posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MKOA WA LINDI RS:

Share