02/06/2026
HABARI: Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imeendesha mafunzo ya rejea kwa maafisa ugani kuhusu matumizi sahihi na salama ya viuatilifu vya korosho katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, zoezi ambalo linatarajiwa kufanyika katika halmashauri zote za Mkoa wa Lindi.
Awali akizungumza, Meneja wa Zao la Korosho Mkoa wa Lindi, Humphrey Mlagalila, amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuhakikisha wataalamu wanaotekeleza zoezi la upuliziaji wanazingatia usalama na weledi, hatua itakayochangia kufikia lengo la kuongeza uzalishaji wa korosho hadi tani milioni moja nchini.
Akifungua mafunzo hayo Juni 01, 2026 Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva amesema Manispaa ya Lindi imepokea lita 37,886 za viuatilifu ambazo zinaendelea kusambazwa kwa wakulima kupitia vyama vya msingi, huku akitoa rai kwa wakulima kutoa ushirikiano kwa maafisa ugani ili kufikia lengo la uzalishaji.
Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube