Mashujaa FM

Mashujaa FM Mashujaa Fm tunapatikana mkoa wa lindi, makao makuu yapo manispaa ya Lindi ... tupigie simu kutangaz

02/06/2026

HABARI: Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) imeendesha mafunzo ya rejea kwa maafisa ugani kuhusu matumizi sahihi na salama ya viuatilifu vya korosho katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, zoezi ambalo linatarajiwa kufanyika katika halmashauri zote za Mkoa wa Lindi.

Awali akizungumza, Meneja wa Zao la Korosho Mkoa wa Lindi, Humphrey Mlagalila, amesema mafunzo hayo ni muhimu katika kuhakikisha wataalamu wanaotekeleza zoezi la upuliziaji wanazingatia usalama na weledi, hatua itakayochangia kufikia lengo la kuongeza uzalishaji wa korosho hadi tani milioni moja nchini.

Akifungua mafunzo hayo Juni 01, 2026 Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva amesema Manispaa ya Lindi imepokea lita 37,886 za viuatilifu ambazo zinaendelea kusambazwa kwa wakulima kupitia vyama vya msingi, huku akitoa rai kwa wakulima kutoa ushirikiano kwa maafisa ugani ili kufikia lengo la uzalishaji.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

02/06/2026

MICHEZO: Afisa Utamaduni wa Mkoa wa Lindi, Makarage, amewataka wananchi na wadau wa michezo kujitokeza viwanjani kushuhudia vipaji vinavyooneshwa katika mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA, akisisitiza kuwa michezo ni chanzo cha ajira, afya na fursa mbalimbali kwa vijana. Wito huo ameutoa baada ya hafla fupi ya uzinduzi wa mashindano hayo yanayofanyika katika uwanja wa Ilulu, Manispaa ya Lindi

Baadhi ya walimu wa michezo wamesema wana matumaini ya kufanya vizuri katika mashindano ya mwaka huu licha ya kukabiliwa na changamoto za upungufu wa vifaa vya michezo, viwanja visivyokidhi mahitaji na muda mdogo wa kuwafundisha wanafunzi wakiwa shuleni.

Kwa upande wao, wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Shule ya Msingi Mtanga ya Wilaya ya Kilwa wameeleza kufurahishwa na ushiriki wao katika mashindano hayo, wakiahidi kufanya vizuri na kuitangaza vyema shule yao pamoja na Mkoa wa Lindi.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

01/06/2026

HABARI: Halmashauri ya Manispaa ya Lindi imezindua Kampeni ya Mwezi wa Lishe kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, inayohusisha utoaji wa matone ya Vitamini A, dawa za kutibu minyoo na tathmini ya hali ya lishe ambapo Kampeni hiyo itatekelezwa kuanzia leo Juni 1 hadi 30, 2026.

Kaimu Mganga Mkuu wa Manispaa ya Lindi, Abdillah Mbingu, amesema kampeni hiyo inalenga kuwafikia watoto elfu ishirini na mbili wenye umri wa miezi 6 hadi 59 kwa huduma mbalimbali za lishe na afya.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva, amewahimiza wazazi na walezi wenye watoto chini ya miaka mitano kujitokeza kwa wingi katika vituo vya kutolea huduma za afya ili watoto wao wapatiwe huduma hizo muhimu zinazotolewa bila malipo.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

30/05/2026

HABARI: Hatua ya kuimarisha sekta ya madini nchini imeendelea kufikiwa baada ya Serikali kusaini mikataba miwili ya ubia wa uchimbaji wa madini ya kinywe (graphite) wilayani Ruangwa, Mkoani Lindi, katika hafla iliyoshuhudiwa na Waziri wa Madini, Antony Mavunde.

Mikataba hiyo imehusisha kampuni ya Eminent Minerals Limited kupitia kampuni ya ubia ya Swala Graphite Corporation inayomilikiwa na Watanzania, pamoja na Grafica Graphite Corporation Limited inayomilikiwa na wawekezaji kutoka nje ya nchi.

Akizungumza katika hafla ya utiaji saini iliyofanyika leo Mei 30, 2026, Waziri Mavunde amesema hatua hiyo ni katika kuendelea kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji katika sekta ya madini nchini huku ukitarajiwa kuongeza ajira, mapato ya Serikali na kuchochea maendeleo ya wananchi wa Ruangwa na Mkoa wa Lindi kwa ujumla.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

HABARI: Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Kanda ya Kusini imeadhimisha kilele cha Siku ya CCT katika Mkoa wa Lindi, huk...
30/05/2026

HABARI: Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Kanda ya Kusini imeadhimisha kilele cha Siku ya CCT katika Mkoa wa Lindi, huku mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva. Jumuiya hiyo inajumuisha mikoa ya Lindi na Mtwara na inaundwa na jumla ya makanisa 12.

Akihubiri katika maadhimisho hayo, Askofu wa kanisa la KKKT Dayosisi ya kusini Mashariki Yeriko Nguema amewahimiza waumini kutumia fursa zilizopo katika maeneo yao ili kujiongezea kipato ambapo amesisitiza zaidi kundi la vijana kuachana na tabia ya kukaa vijiweni bila kujishughulisha na kazi za uzalishaji ikiwemo kilimo.

Mkuu wa wilaya ya Lindi Victoria Mwanziva, ameipongeza Jumuiya hiyo kwa kuandaa maadhimisho hayo huku akiwataka viongozi wa dini kuendelea kusimamia maadili na malezi ya kiroho kwa waumini sambamba na kuliombea Taifa liendelee kuwa na amani na utulivu.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

30/05/2026

VIDEO: Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Lindi imeokoa zaidi ya shilingi milioni thelathini zikiwemo pesa za wakulima wilayani Liwale kutokana na upotevu wa korosho zao ambazo zilipelekwa kwenye chama cha msingi cha Mkunya kupitia msimu wa kilimo 2024/25 kwa ajili ya kuuzwa lakini zikapotea katika hali ya kutatanisha.

Hayo yameelezwa Mei 29, 2026 na Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Stephen Mafipa, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambapo ameeleza baada ya kufatilia kwa makini walifanikiwa kuzirudisha pesa hizo na wakulima kulipwa stahiki zao.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

30/05/2026

MICHEZO: Wanafunzi 100 kutoka shule mbalimbali za msingi za Halmashauri ya Manispaa ya Lindi wamechaguliwa kuunda timu itakayoiwakilisha Manispaa hiyo katika mashindano ya UMITASHUMTA ngazi ya Mkoa wa Lindi,

Mratibu wa UMITASHUMTA Manispaa ya Lindi, Mwalimu Mzee, amesema licha ya kuwapo kwa vipaji vingi, idadi iliyohitajika ni wanafunzi 100 pekee watakaoshiriki michezo ya mpira wa miguu, handball, netball, volleyball pamoja na kwaya katika mashindano yatakayoshirikisha halmashauri sita za Mkoa wa Lindi.

Kwa upande wake, Afisa Michezo wa Manispaa ya Lindi, Jamal Lisuma, amesema ameridhishwa na maandalizi ya timu hiyo na kuwahimiza wananchi kujitokeza kushuhudia mashindano yatakayoanza Mei 31, huku wakitumia fursa hiyo kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Follow Us
Instagram
Facebook
Twitter
YouTube

HABARI: Wakulima wa chumvi wa Lindi na Mtwara wanatarajia kunufaika na kiwanda kipya cha kuchakata chumvi (Rafiki Salt)k...
30/05/2026

HABARI: Wakulima wa chumvi wa Lindi na Mtwara wanatarajia kunufaika na kiwanda kipya cha kuchakata chumvi (Rafiki Salt)kilichojengwa na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) katika eneo la Lingaula Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi.

Kiwanda hicho chenye uwezo wa kuchakata tani 25,000 kwa mwaka, kimezinduliwa Mei 29, 2026 na Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, ambaye amesema mradi huo unalenga kuwapatia wakulima soko la uhakika, kuongeza thamani ya chumvi yao na kukuza uzalishaji wenye tija.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Dr. Venance Mwasi, amesema kiwanda hicho kimegharimu Sh bilioni 4.5 hadi kukamilika kwake na kitakuwa kinanunua chumvi ghafi moja kwa moja kutoka kwa wakulima. Amesema mbali na kutoa huduma ya kuongeza thamani ya chumvi, kiwanda hicho pia kitatoa ajira pamoja na mafunzo kwa wazalishaji ili wajifunze uzalishaji wa chumvi kwa kutumia teknolojia ya kisasa.

Kwa upqnde wa wake Mwenyekiti wa Chama cha Wazalishaji wa Chumvi Tanzania (TASPA), Hawa Ghasia ameeleza matumaini yao kwa ujio wa kiwanda hicho kwa wazalishaji wa chumvi wa Mikoa ya Lindi na Mtwara kuwa utawasaidia kupata soko la uhakika la bidhaa yao na kupunguza changamoto ya kuuza chumvi kwa bei ya chini na kuongeza kipato kupitia uzalishaji wenye ubora zaidi.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

MICHEZO: Timu ya Soka ya wanawake Ruangwa Queens imekwama eneo la Igunga, Mkoani Tabora kutokana na changamoto ya kuishi...
29/05/2026

MICHEZO: Timu ya Soka ya wanawake Ruangwa Queens imekwama eneo la Igunga, Mkoani Tabora kutokana na changamoto ya kuishiwa mafuta wakati ikiendelea na safari kuelekea Mwanza kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Alliance utakaochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Nyamagana Mkoani Mwanza.

Akizungumza kupitia kipindi cha Full Game kinachorushwa na Mashujaa FM, Mwenyekiti wa Ruangwa Queens, Yusuph Mpame amesema timu hiyo inahitaji lita 70 za mafuta ya dizeli ili iweze kuendelea na safari yake kuelekea Mwanza kwa ajili ya mchezo huo muhimu.

Mpame amesema hali hiyo imeisababisha timu kusimama kwa muda eneo la Igunga huku wachezaji na benchi la ufundi wakisubiri msaada kutoka kwa wadau wa michezo na wasamaria wema ili waweze kuwahi mchezo wao dhidi ya Alliance.

Kuwasiliana na Mwenyekiti wa Ruangwa Queens, Yusuph Mpame piga namba 0713 087 047.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

28/05/2026

HABARI: Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Camilius Wambura kuhakikisha jeshi hilo linajenga imani zaidi kwa wananchi, sekta binafsi na jumuiya za kimataifa zilizopo nchini.

Rais Samia ametoa maelekezo hayo kufuatia matokeo ya utafiti wa Afrobarometer unaoonyesha kuwa ni asilimia 12 pekee ya Watanzania waliotaja kuwa wangelikimbilia polisi wanapopata changamoto za kisheria, hali inayoashiria changamoto ya imani kwa taasisi hiyo.

Amesema matokeo hayo ni ya kuzingatiwa kwa umakini ili kuboresha utendaji na uhusiano kati ya polisi na wananchi, akisisitiza kuwa lengo ni kuimarisha uhalali na uaminifu wa Jeshi la Polisi nchini.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

Address

Wailes
Lindi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mashujaa FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mashujaa FM:

Share

Category