Mashujaa FM

Mashujaa FM Mashujaa Fm tunapatikana mkoa wa lindi, makao makuu yapo manispaa ya Lindi ... tupigie simu kutangaz

17/06/2026

VIDEO: Kupitia mfuko wa Hifadhi Skimu wa NSSF watu waliojiajiri katika sekta binafsi wanayonafasi ya kujiwekea akiba na kunufaika kwa kupata mafao pamoja na bima ya matibabu.

Hayo yameelezwa na Afisa wa NSSF Mkoa wa Lindi, Joel Hamuli.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

17/06/2026

VIDEO: “Waajiri watakaolipa malimbikizo yote ya michango ya wanachama kabla au baada ya kufikia Oktoba 31, 2026 na kuendelea kulipa michango hiyo kwa wakati hadi Desemba 31, 2026, watasamehewa tozo wanazodaiwa kwa asilimia 75 na kulipia asimilia 25 iliyosalia” - Meneja wa NSSF Mkoa wa Lindi, Juma Namuna

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

HABARI: Jamii imetakiwa kutoa taarifa kwa wakati kuhusu matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu ili yaweze kufikishwa kw...
17/06/2026

HABARI: Jamii imetakiwa kutoa taarifa kwa wakati kuhusu matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu ili yaweze kufikishwa kwa mamlaka husika na kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

Wito huo umetolewa na Philemon Thomas, Afisa Uchunguzi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora wakati wa mafunzo ya uhamasishaji uliofanyika katika kijiji cha Shuka, Halmashauri ya Mtama mkoani Lindi.

Amesema ushirikiano wa wananchi katika kutoa taarifa za matukio ya ukiukwaji wa haki za binadamu ni muhimu katika kuhakikisha haki zinazingatiwa, zinalindwa na wahusika wanachukuliwa hatua stahiki.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

HABARI: Watu wanane, wakiwemo wafanyakazi wawili wa Boeing, wamefariki dunia baada ya ndege ya Jeshi la Anga la Marekani...
16/06/2026

HABARI: Watu wanane, wakiwemo wafanyakazi wawili wa Boeing, wamefariki dunia baada ya ndege ya Jeshi la Anga la Marekani aina ya B-52 kuanguka na kuwaka moto muda mfupi baada ya kupaa kutoka Kituo cha Jeshi la Anga cha Edwards, California.

Ajali hiyo imetokea Jumatatu wakati ndege hiyo ikiwa katika misheni ya kawaida ya majaribio. Moshi mkubwa mweusi ulionekana ukifuka kutoka eneo la tukio huku vikosi vya uokoaji vikifika haraka.

Kanali James Hayes amesema wote waliokuwamo ndani ya ndege hiyo wamefariki na uchunguzi wa chanzo cha ajali unaendelea. Shughuli katika kituo hicho zimesitishwa kwa muda.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

15/06/2026

HABARI: Kijana mmoja anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 30-35 ambae jina lake alijafahamika amekutwa amefariki dunia karibu na stendi ya maegesho ya maroli iliyopo wilayani Nachingwea mkoani Lindi.

Akithibitisha tukio hilo Mganga mfawidhi wa hospitali ya Wilaya ya Nachingwea, Dkt. Shukrani Nsikini, amesema kuwa mwili huo umekutwa tayari umeharibika kwani ni zaidi ya siku sita nyuma tangu apoteze maisha huku mkono wake wa kushoto umekutwa ukiwa umevunjika hali ambayo inaashiria alijeruhiwa.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

HABARI: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza kuwa Jumatano Juni 17...
15/06/2026

HABARI: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ametangaza kuwa Jumatano Juni 17, 2026 itakuwa siku ya mapumziko rasmi Zanzibar kwa ajili ya kuukaribisha Mwaka Mpya wa Kiislamu 1448 Hijria.

Tangazo hilo limetolewa leo Juni 15, 2026 Ikulu Zanzibar, likilenga kuwapa wananchi, hususan Waislamu, fursa ya kuupokea mwaka mpya kwa ibada, dua na matendo mema huku wakiiombea nchi amani na maendeleo.

Dkt. Mwinyi amewahimiza wananchi kutumia kipindi hicho kujitathmini, kuimarisha uchamungu na kuendeleza maadili mema yatakayochangia kujenga jamii yenye mshikamano na ustawi.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

13/06/2026

HABARI: Mnada wa pili wa ufuta kwa chama kikuu cha Ushirika Lindi Mwambao umefanyika wilayani Kilwa mkoani Lindi na kuuza zaidi ya tani elfu 2 kwa bei ya juu tsh. 2,700 huku bei ya chini ikiwa tsh. 2580.

Akizungumza baada ya mnada, makamu mwenyekiti wa Lindi Mwambao, Hassan Mnumbe, ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya msingi kuwa na chekecheke waweze kusafisha ufuta kabla ya kufika ghala kuu.

Aidha, wakulima wamefurahishwa na bei za mnada huo na kuwapa matumaini ya kuzidi kuzalisha zaidi, huku wakiomba iongezeke zaidi kwani zao hilo halina pembejeo za ruzuku.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

12/06/2026

VIDEO: Mpango wa Taifa wa Kutokomeza Ajira kwa Watoto unaonesha kuwa asilimia 25 ya watoto nchini wanajihusisha na kazi mbalimbali, huku sekta zisizo rasmi zikitajwa kuwa miongoni mwa maeneo yanayoongoza kwa kuwaajiri watoto.

Hayo yameelezwa na Afisa Kazi Mkoa wa Lindi, Festo Boyi, akiwa kwenye mahojiano maalum Mashujaa FM.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

12/06/2026

VIDEO: Afisa Kazi Mkoa wa Lindi, Festo Boyi, amesema kuwa sheria hairuhusu kuajiriwa kwa mtoto mwenye umri chini ya miaka 14. Aidha, mtoto mwenye umri wa miaka 14 na kuendelea anaweza kufanya kazi nyepesi kwa kibali cha afisa ustawi wa jamii na mzazi au mlezi.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

Address

Wailes
Lindi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mashujaa FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mashujaa FM:

Share

Category