15/09/2025
HABARI: Wananchi wa Kijiji cha Mihumo, kilichopo Kata ya Mihumo, Wilaya ya Liwale Mkoani Lindi, wamemkataa mwenyekiti wao wa kijiji wakidai kutokuwa na imani nae kutokana na utendaji wake wa kazi ambao wamedai hauruhusu maendeleo ya kijiji hicho kusonga mbele.
Katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijijini hapo, Septemba 14,2025 wananchi wameeleza kutoridhishwa na namna mwenyekiti huyo anavyosimamia shughuli za kijiji, wakimtuhumu kwa kutokuwa na uwazi katika matumizi ya fedha, kushindwa kushirikisha wananchi katika maamuzi muhimu, pamoja na kutowajibika ipasavyo katika majukumu yake ya kila siku.
Akizungumza baada ya kusikiliza malalamiko ya wananchi, Afisa Tarafa wa Tarafa ya Liwale Mjini Hasan Selemani akatoa agizo la siku 60 kwa ajili ya kufanyika uchunguzi wa kina juu ya tuhuma zinazomkabili mwenyekiti huyo.
Aidha, alieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuhakikisha haki inatendeka kwa pande zote mbili, na iwapo tuhuma zitathibitika, hatua za kisheria zitachukuliwa.
Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube