Mashujaa FM

Mashujaa FM Mashujaa Fm tunapatikana mkoa wa lindi, makao makuu yapo manispaa ya Lindi ... tupigie simu kutangaz

HABARI: ‎Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Leo XIV, ametoa mwito wa kusitishwa kwa mapigano ulimwenguni kote wak...
24/12/2025

HABARI: ‎Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Leo XIV, ametoa mwito wa kusitishwa kwa mapigano ulimwenguni kote wakati wa sikukuu ya Krismasi.

‎Akiwa katika makazi yake ya mapumziko ya Castel Gandolfo, nje kidogo ya mji wa Roma mnamo Disemba 23, 2025, Papa ameeleza hamu yake ya kuona ulimwengu ukisherehekea kuzaliwa kwa Mwokozi katika mazingira ya utulivu na amani.

‎Katika ujumbe wake huo kuelekea Disemba 25, Papa ameeleza kusikitishwa kwake na msimamo wa Urusi ambao unaonekana kukataa ombi la kusitisha mapigano nchini Ukraine kwa ajili ya siku hiyo takatifu.

‎ “Ninatoa tena wito wangu kwa watu wote wenye mapenzi mema, kuheshimu siku ya amani, angalau katika sikukuu ya kuzaliwa kwa Mwokozi wetu," alisema Papa, huku akisisitiza kuwa ni jambo la kuhuzunisha kuona milio ya risasi ikiendelea wakati wa sherehe za amani.

‎Kiongozi huyo ameweka wazi kuwa lengo lake ni kuona dunia ikipata angalau saa 24 za amani kamili, bila kujali ukubwa wa mizozo iliyopo.

Mwito huu unakuja wakati hali ya usalama nchini Ukraine ikiendelea kuwa tete, ambapo taarifa za kijeshi zinaashiria kuwa majeshi ya Ukraine yamelazimika kujiondoa katika mji mmoja muhimu upande wa Mashariki kufuatia mashambulizi makali kutoka kwa Urusi.

‎Kuhusu uwezekano wa yeye kuitembelea Ukraine kufuatia mwaliko wa Rais Volodymyr Zelensky, Papa Leo XIV amesema "anatumai hivyo," ingawa amekiri kuwa bado ni vigumu kupanga tarehe rasmi ya safari hiyo kwa sasa.

‎Papa alikutana na Rais Zelensky mapema mwezi huu wa Disemba, katika juhudi za kutafuta suluhu ya kudumu ya kidiplomasia katika eneo hilo.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube .

24/12/2025

VIDEO: Kupitia pata ushauri wa kijisiriamali wa ufugaji wa kuku uliomtajirisha Daktari aliyeajiriwa kwa wiki moja.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

24/12/2025



Leo Askofu Dkt. Bagonza asema 'koneksheni' zitaangamiza Tanzania, ahoji uaminifu na kuaminika katika jamii iliyokata tamaa, akemea vikali utegemezi wa mifumo iliyopo akisisitiza tumaini bado lipo nchini.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

24/12/2025

VIDEO: Edna Kahema kupitia kipindi cha amethibitisha kununuliwa gari na Mkurugenzi mkuu na Meneja mkuu wa katika kurahisisha utendaji wake wa kiofisi.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

24/12/2025



Leo Utetezi wa Tundu Lissu waizindua ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) na kuamua kuziba matobo ya vielelezo vilivyokataliwa mahakamani.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

Cheza IZEE LOTTO kwa JERO tu!Chagua NAMBA 9 kati ya 1-40 na unaweza kushinda hadi TZS Milioni 20 PAPO HAPOCHEZA kwa kute...
24/12/2025

Cheza IZEE LOTTO kwa JERO tu!
Chagua NAMBA 9 kati ya 1-40 na unaweza kushinda hadi TZS Milioni 20 PAPO HAPO
CHEZA kwa kutembelea https://bit.ly/nationallotterytz SASA.

18+. Cheza Kistaarabu. ITHUBA ni mwendeshaji rasmi wa Bahati Nasibu ya Taifa.

MICHEZO: Timu ya Titanic FC kutoka Nachingwea imefanikiwa kutinga fainali ya Ligi ya Mkoa wa Lindi 2025 baada ya kuibuka...
23/12/2025

MICHEZO: Timu ya Titanic FC kutoka Nachingwea imefanikiwa kutinga fainali ya Ligi ya Mkoa wa Lindi 2025 baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Kilwa Stars ya Kilwa, katika mchezo wa nusu fainali uliopigwa kwenye Uwanja wa Ilulu, Manispaa ya Lindi, tarehe 23 Desemba 2025.

Titanic FC walianza kufunga bao la kwanza mapema dakika ya 4 kupitia kwa Joseph Kiporo, kabla ya Peter Masihi kuisawazishia Kilwa Stars dakika ya 25. Hata hivyo, dakika mbili baadaye, Mohammed Morgan aliihakikishia Titanic ushindi kwa kufunga bao la pili na la ushindi dakika ya 27

Kwa matokeo hayo, Titanic FC itamenyana na Lindi Soccer kwenye fainali inayotarajiwa kuchezwa Disemba 27, 2025 katika dimba hilo hilo la Ilulu, Lindi.

Fainali hiyo itakuwa ya kipekee kwani zimekutana timu zilizoshika nafasi ya pili kwenye hatua ya makundi.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

23/12/2025

HABARI: Chama kikuu cha Ushirika Lindi Mwambao kimefanya mkutano mkuu maalumu Disemba 22, 2025 kilichofanyika Kijiji cha Hoteli tatu Halmashauri ya Kilwa kikiwa na ajenda ya kusoma taarifa ya fedha kwa mwaka 2024, kukiambatana na mapokezi ya gari jipya kwa matumizi ya ofisi.

Akisoma taarifa hiyo Mkaguzi kutoka Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO) - Omary Shariff amesema taarifa ya fedha ya chama hicho inahakisi hali halisi ya fedha hivyo kupata hati inayoridhisha.

Nae mgeni rasmi Katibu tawala wa Wilaya ya Kilwa Yusuph Mwinyi ametoa pongezi wa viongozi wa chama hicho kwa usimamizi na weledi nzuri katika utendaji unaoepusha migogoro.

Kwa upande wake Mrajis msaidizi Mkoa wa Lindi Kenneth Shemdoe ametoa rai kwa wanachama kuongeza kiwango cha hisa kuendana na thamani halisi ya fedha kwa sasa. Huku wanachama wakiridhishwa na mwenendo wa chama hicho.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube .

23/12/2025



Leo X-mass kuwa chini ya ulinzi maalumu kuanzia ibadani hadi sehemu za starehe.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube .

23/12/2025



Leo Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amewataka wakandarasi kuwashirikisha wananchi katika hatua za ujenzi wa barabara.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube .

23/12/2025

Unataka MAMILIONI ya haraka?Cheza SPIN4CASH kuanzia TZS 1000 tu na ushinde hadi TZS MILIONI 4 chap kwa haraka! PIGA*149*88 #, kwa Wakala au tembelea https://bit.ly/nationallotterytz.18+. Cheza Kistaarabu. ITHUBA ni mwendeshaji rasmi wa Bahati Nasibu ya Taifa.

MICHEZO: Timu ya Lindi Soccer kutoka Manispaa ya Lindi imefanikiwa kutinga fainali ya Ligi ya Mkoa wa Lindi 2025 baada y...
22/12/2025

MICHEZO: Timu ya Lindi Soccer kutoka Manispaa ya Lindi imefanikiwa kutinga fainali ya Ligi ya Mkoa wa Lindi 2025 baada ya kuiondoa Rajam FC ya Ruangwa kwa mikwaju ya penalti 5–3, kufuatia sare ya bao 1–1 ndani ya dakika 90 za mchezo wa nusu fainali uliopigwa katika Uwanja wa Ilulu, mkoani Lindi, tarehe 22 Desemba 2025.

Goli la Lindi Soccer lilifungwa na Mohammed Macho dakika ya 24, kabla ya Justin Simao kuisawazishia Rajam FC kwa mkwaju wa penalti dakika ya 72. Hali hiyo ilisababisha mchezo kuamuliwa kwa mikwaju ya penalti, ambapo Lindi Soccer walionyesha umakini zaidi na kushinda kwa penalti 5–3.

Nusu fainali ya pili ya ligi hiyo itachezwa kesho, tarehe 23 Desemba 2025, katika Uwanja wa Ilulu, ambapo timu za Kilwa Stars ya Kilwa na Titanic FC ya Nachingwea zitakutana kuwania tiketi ya kucheza fainali dhidi ya Lindi Soccer.

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

Address

Wailes
Lindi

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mashujaa FM posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mashujaa FM:

Share

Category