Sambaza Ufahamu, Tanzania

Sambaza Ufahamu, Tanzania Ni asasi ya kiraia inayoshughurika na uhifadhi wa utamaduni wa afrika.

23/12/2025

Mapema nimetembelea barabara ya Ghana Road kufuatia picha ya Mchoraji maarufu wa kazi ya Sanaa hapa Lindi.

Anayefahamika kwa jina la (Azizi Mkwachile Azizi) By Azizi Sign Art kutokana na picha aliyoichora kwenye kazi zake za sanaa.

Kutokana na picha hiyo sasa imenipeleka kwenye eneo alilolichora kwenye maeneo ya barabara ya Ghana Road iliyopo Manispaa ya Lindi.

Nimekuwekea kiunganishi hapa chini k**a utahitaji kuijua historia ya Ghana Road iliyopo Lindi
Click: https://www.facebook.com/share/v/1BxH34YCLy/

Tuambie kwenye Comment unampa asilimia ngapi kwenye uchora wake?

Abdulrasul muhibu
_Mchambuzi masuala ya jamii kazi za sanaa na mhifadhi wa utamaduni wa kiafrika.

Mapema Leo asubuhi Th 21/12/2025 waziri mkuu Daktari Lameck Mchemba amekwenda kukagua bandari ya Lindi, kufuatia hoja il...
21/12/2025

Mapema Leo asubuhi Th 21/12/2025 waziri mkuu Daktari Lameck Mchemba amekwenda kukagua bandari ya Lindi, kufuatia hoja iliyotolewa na mkuu wa mkoa katika taarifa yake ya Jana , kuomba marekebisho ya bandari.

16/12/2025

Tuendelee kudurusu durusu

07/12/2025

IFAHAMU HISTORIA YA BARABARA YA UHURU ILIYOPO MANISPAA YA LINDI TUNAPOELEKEA KUADHIMISHA MIAKA 64 YA UHURU YA TANGANYIKA.

Kupitia durusu durusu za historia leo hii nakusogezea historia ya barabara ya uhuru tunapoelekea kuadhimisha miaka 64 ya uhuru wa Tanganyika tokea ijipatie uhuru Th 09 Decemba 1961. Hivyo tutaidurusu barabara maarufu hapa lindi inayofahamika k**a barabara ya uhuru.

Kabla ya Tanganyika kupata uhuru mwaka 1961, barabara hii haikuitwa Barabara ya Uhuru k**a tunavyoijua leo. Ilifahamika k**a Queen Elizabeth Avenue, jina lililoashiria ushawishi na mamlaka ya utawala wa kikoloni wa Uingereza katika maeneo ya Afrika Mashariki. Jina hilo liliwekwa kwa heshima ya Malkia Elizabeth wa Uingereza.

Katika mji wa Lindi, kuitwa kwa barabara hii jina la Malkia kulikuwa pia ishara ya kuunga mkono mfumo wa utawala wa Muingereza ndani ya nchi ya Tanganyika.

Barabara hii ilikuwa kitovu cha uchumi wa wakati huo. Ilizungukwa na nyumba za wafanyabiashara wakubwa — hasa wafanyabiashara wa Asia (Wahindi) pamoja na Watanganyika waliokuwa wakijihusisha na biashara.

Ni muhimu kueleza kwamba Waingereza hawakuhusika moja kwa moja na biashara katika eneo hili, badala yake walijikita katika masuala ya uongozi na utawala. Hawakukaa kwenye maeneo haya ya biashara; maeneo haya ndiyo yaliyokuwa makazi na vituo vya shughuli za Watanganyika na wafanyabiashara wa Kihindi.

Katika enzi hizo, Barabara ya Uhuru ndiyo ilikuwa lango kuu la shughuli za kibiashara. Hapa ndipo palikokua na maduka, maghala na misururu ya biashara iliyoleta ajira nyingi kwa Waafrika waliokuwa wakifanya kazi za mikono, usafirishaji na huduma mbalimbali.

Mpaka leo, barabara hii inaendelea kuwa na umuhimu wake. Kwa yeyote anayefika Lindi, Barabara ya Uhuru ndiyo njia kuu inayoelekea Stendi Kuu ya Mabasi. Unapoingia mji wa Lindi ukielekea stendi, au unapotoka kuelekea safari zako, ni lazima kupita katika Barabara hii ya kihistoria — lango la kuingia na kutoka katika mji wa Lindi.

Na kisha ikafika tarehe 09 Desemba 1961
Siku ambayo Tanganyika ilitangazwa kuwa nchi huru. Wakazi wa Lindi hawakusita kuonesha shukrani na furaha yao. Walikusanyika na kubadilisha kibao cha barabara hii, wakiondoa jina la kikolon

04/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini Mhe. Mohamed Utaly ameahidi kutoa ushirikiano kwa kwa kila diwani lakini pia kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ili kwa Pamoja waweze kuleta maendeleo.

Utaly ameyasema hayo Disemba 03,2025 wakati akitoa salam zake kwenye mkutano wa kwanza wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Lindi ambao umefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Dock yard hall center.

Sambamba na Hilo ameahidi kushiriki kwenye masuala mbalimbali yatakayofanyika kwenye Halmashauri hiyo ikiwemo michezo na mambo mbalimbali yatakayoleta maendeleo.

Tuendelee kudurusu durusu
04/12/2025

Tuendelee kudurusu durusu

03/12/2025

Mstahiki Meya Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mhe. Twahili Mpuluji amesisitiza umoja na mshik**ano miongoni kwa Madiwani ili kufikia maendeleo.

Amaeyasema hayo Leo Disemba 03,2025 kwenye Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Madiwani lililofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Dock yard Hall center.

26/11/2025

WAWEKEZAJI WAOMBWA KUJA KUWEKEZA MANISPAA YA LINDI.

Hayo yamesemwa Leo Novemba 26,2025 na Mkuu wa Wilaya ya Lindi Mhe. Victoria Mwanziva Katika ukumbi wa mikutano wa Dock yard Hall Center mara baada ya kufunga kikao cha Baraza la Wafanyabiashara Wilaya ya Lindi ikihusisha Halmashauri ya wilaya Mtama na Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.

Aidha amesisitiza kuwa lengo la baraza hilo la wafanyabiashara ni kujadili masuala mbalimbali ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na fursa za uwekezaji sambamba na miradi mikubwa ya kimkakati k**a vile maboresho ya stendi na soko.

Sambamba na hilo amesema Lindi kuna fursa nyingi za uwekezaji kwani kuna mazingira mazuri na makubwa kwa ajili ya uwekezaji.

Katika hatua nyingine Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi Mwandishi Nchimbi amewapongeza washiriki na wadau mbalimbali kwenye kikao hicho cha baraza la wafanyabiashara kwa kujitokeza kwa wingi na kutoa maoni pamoja na michango mbalimbali ambayo kwa namna moja ama nyingine inapelekea kunyanyua sekta ya biashara na uwekezaji ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya Lindi na Mkoa kwa ujumla.


19/11/2025

Mkuu wa wilaya ya Lindi Mhe.Victoria Mwanziva ameiomba idara ya Afya Kuongeza Ubunifu Katika utekelezaji wa Afua Za Lishe.

Hayo ameyasema leo Novemba 19,2025 katika kikao cha tathmini ya Lishe robo ya kwanza kilichofanyika katika ukumbi wa kamishna wa Ardhi Mkoa wa Lindi.

Kura yako haki yako,Jitokeze kupiga kura.
20/10/2025

Kura yako haki yako,Jitokeze kupiga kura.

23/01/2025

Address

Uhurustreet
Lindi
023

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sambaza Ufahamu, Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sambaza Ufahamu, Tanzania:

Share