UMTV

UMTV Chanel hii ya usambara Mountain tv ni kwa madhumuni ya kutoa elimu kwa vijana lakini kwa jamii nzima

Chanel hii ya usambara Mountain tv ni kwa madhumuni ya kutoa elimu kwa vijana lakini kwa jamii nzima
Elimu inaweza kuwa shuleni, kilimo utunzaji wa mazingira, Afya lakini pia namna ya kumjua Mungu. Usisahau kusubscribe ili uwe wa kwanza kupata habari mara tuu inapotumwa, like, comment, na share video zetu
Kwa mawasiliano zaidi whatsapp sms 0695559776
Email: [email protected]

08/06/2026

Maandamano na Yesu wa Ekaristi Takatifu siku ya Dominika ya mwili na damu ya Yesu kutoka makao makuu ya shirika la Masista wa Mama Yetu wa Usambara jimbo katoliki la Tanga

07/06/2026
DOMINIKA YA SHREHE YA MWILI NA DAMU YA KRISTODHAMBI NA KUKATA TAMAA YA MAISHANa Sr Paulina Mshana -UMTVMaadhimisho ya Sh...
07/06/2026

DOMINIKA YA SHREHE YA MWILI NA DAMU YA KRISTO
DHAMBI NA KUKATA TAMAA YA MAISHA
Na Sr Paulina Mshana -UMTV
Maadhimisho ya Sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana Wetu Yesu Kristo kutoka parokia ya Mt. Martin soni jimbo katoliki la Tanga Misa iliyoongozwanna Padre Amani Wami ambaye katika mahubiri yake amewahimiza waamini kujitathmini kiroho na kuacha vilema vya dhambi vinavyowatenga na upendo wa Mwenyezi Mungu.
Katika Sherehe hii ya Mwili na Damu ya Yesu Kristo ambayo kiliturujia huadhimishwa Alhamisi baada ya Dominika ya Utatu Mtakatifu, ilisogezwa mbele hadi Dominika kwa sababu za kichungaji ili kuwapa nafasi waamini wote kushiriki kikamilifu fumbo hilo la imani.
Katika mahubiri Padre Wami amehimiza kutafakari upendo wa Mungu usio na masharti, uliomfanya amtoe Mwanawe wa pekee, Yesu Kristo, kuwa mkombozi wa ulimwengu. Waamini walikumbushwa kuwa upendo huo hauna kipimo na unatolewa kwa kila mmoja bila ubaguzi.
Kujifunza Kutokana na Historia ya Waisraeli
Akitumia mfano wa somo la kwanza, mhubiri aligusia hotuba ya kihistoria ya Musa kwa Wana wa Israeli kabla ya kuingia nchi ya ahadi. Musa aliwakumbusha jinsi Mungu alivyowapenda na kuwatunza wakati wa mateso yao jangwani baada ya kuwakomboa kutoka utumwani Misri.
"Mungu alikuwa nao walipopata kiu na njaa; akawapa chakula kutoka mbinguni, akawanywesha maji kutoka kwenye mwamba, na kuwaponya dhidi ya nyoka wa moto," alieleza mhubiri huku akiwaasa waamini kutosahau wema wa Mungu hata pale wanapokuatana na majaribu wasikate tamaa bali wakimbilie kwa Yesu wa Ekaristi.
Waamini walitakiwa kuambatana na Mwenyezi Mungu zaidi kuliko kitu kingine chochote, wakitambua kuwa Yeye ndiye aliyewaumba.
Changamoto ya Vizuizi vya Dhambi na Kilema cha Rushwa
Kuhusu somo la Injili, ambapo Yesu anajitambulisha k**a "Chakula kilichoshuka kutoka mbinguni," mhubiri alifafanua tofauti kati ya chakula cha kawaida na Ekaristi Takatifu. Alibainisha kuwa tofauti na chakula cha kimwili kinachotoa nguvu za muda, Mwili na Damu ya Yesu Kristo hushibisha na kustawisha roho, na humfanya Kristo akae ndani ya kila mmoja anayemwamini.
Hata hivyo, swali gumu liliibuliwa kuhusu idadi kubwa ya watu wanaohudhuria ibada lakini wanashindwa kupokea Sakramen

08/05/2026

Genral Audience Vatican

08/05/2026

Hongera Papa kwa Mwaka mmoja wa kuwa Papa 8 mei

Wahitimu wa chuo cha Hoteli management kilichopo St Eugen Hostel  Momtessori Lushoto wahimizwa kufanya kazi kwa bidii wa...
06/05/2026

Wahitimu wa chuo cha Hoteli management kilichopo St Eugen Hostel Momtessori Lushoto wahimizwa kufanya kazi kwa bidii wakijituma na kutumia ujuzi walioupata kwa wakati wote wakiwa hapo chuoni

Sr Betlda Sebaiya amethibitisha kiwa hana wasiwasi na wanafunzi hao kwani wameiva na wanajua nini walichokuwa wanapaswa kufanya na kuwahimiza wasilegee bali watumie ujuzi huo kuleta manufaa yao binafsi na kwa jamii

28/04/2026

MZEE ALIYELAZIMISHA KUINGIA UKRISTO BABU YAKE ABATIZWA NA KUITWA JINA LA MJUKUU

IJUE JISTORIA YA MANOLO NA PAROKIA YA KWIZU

Wazee wawili wanaelezea historia ya Ukristo Jimbo katoliki la Same wakisimulia namna wamisionari walivyowaletea dini katika parokia ya Manolo na wamisionari hao walitokea Parokia ya Kilomeni

Wamisionari hao wakitembea kiwafikia waumini wa eneo la Kwizu (manolo) ambapo ni zaidi ya km 30 kutokea kilomeni
Historia ya Kwizu
Parokia ya Kwizu ni parokia Kongwe katika parokia za jimbo katoliki la Same, Kwizu ilihama kupelekwa eneo la manolo kwa sababu baada ya dini kuenea wakristo walipata wahudumu na kupata parokia hivyo waumini wa Kwizu walikuwa eneo la juu ya Parokia hiyo, hivyo aliyekuwa paroko wakati huo alilazimika kufuata waumini ndipo alipofanya maamuzi ya kuihamisha parokia hiyo mpaka eneo la manolo

Manolo
Asili ya neno Manolo ilikuwa ni sehemu ya kufanyia matambiko ambapo naada ya wavuno walitoa shukrani kwa kuchinja kula na kunywa

Lakini pia eneo hilo lilikuwa na jiwe la kunolea (Manolo) mapanga

Leo hii ni Parokia ya Roho Mtakatifu manolo jimbo katoliki la Same

KIPINDI HIKI CHA JIMBO KATOLIKI kitakujia hivi punde
Azam other channel no 016

PICHA ZA IBADA MISA TAKATIFU YA MAZISHI YA SR JULIANA E. KIVUNGE  SHIRIKA LA COLU ALOYEZIKWA KATIKA MAKABURI YA MASISTA ...
17/04/2026

PICHA ZA IBADA MISA TAKATIFU YA MAZISHI YA SR JULIANA E. KIVUNGE SHIRIKA LA COLU ALOYEZIKWA KATIKA MAKABURI YA MASISTA WA SHIRIKA WETU WA USAMBARA JIMBO KATOLIKI LA TANGA SIKU YA IJUMAA TR 17.04.2026
MISA IMEONGOZWA NA ASKOFU THOMAS J. KIANGIO JIMBO KATOLIKI LA TANGA

SR JULIANA KIVUNGE ALIKUWA AKISUMBULIWA NA SUKARI NA SHINIKIZO LA DAMU KWA MUDA MREFU LAKINI ALIKUWA AKIENDELEA NA MAJUKUMU YAKE YA KAWAIDA, ALIKUFA AKIWA NA UMRI WA MIAKA 86 NA MIAKA 61 YA MAISHA YA KUMTUMIKIA MUNGU K**A MTAWA ALIKUWA MCHESHI MPENDA WATU NA MWENYE ROHO YA IBADA MAISHA YAKE ALIPENDA KUWAHUDUMIA WATU K**A MKUNGA.

RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE APUMZIKE KWA AMANI MBINGUNI AMINA

Address

MONT
Lushoto
21701

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UMTV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share