07/06/2026
DOMINIKA YA SHREHE YA MWILI NA DAMU YA KRISTO
DHAMBI NA KUKATA TAMAA YA MAISHA
Na Sr Paulina Mshana -UMTV
Maadhimisho ya Sherehe ya Mwili na Damu Takatifu ya Bwana Wetu Yesu Kristo kutoka parokia ya Mt. Martin soni jimbo katoliki la Tanga Misa iliyoongozwanna Padre Amani Wami ambaye katika mahubiri yake amewahimiza waamini kujitathmini kiroho na kuacha vilema vya dhambi vinavyowatenga na upendo wa Mwenyezi Mungu.
Katika Sherehe hii ya Mwili na Damu ya Yesu Kristo ambayo kiliturujia huadhimishwa Alhamisi baada ya Dominika ya Utatu Mtakatifu, ilisogezwa mbele hadi Dominika kwa sababu za kichungaji ili kuwapa nafasi waamini wote kushiriki kikamilifu fumbo hilo la imani.
Katika mahubiri Padre Wami amehimiza kutafakari upendo wa Mungu usio na masharti, uliomfanya amtoe Mwanawe wa pekee, Yesu Kristo, kuwa mkombozi wa ulimwengu. Waamini walikumbushwa kuwa upendo huo hauna kipimo na unatolewa kwa kila mmoja bila ubaguzi.
Kujifunza Kutokana na Historia ya Waisraeli
Akitumia mfano wa somo la kwanza, mhubiri aligusia hotuba ya kihistoria ya Musa kwa Wana wa Israeli kabla ya kuingia nchi ya ahadi. Musa aliwakumbusha jinsi Mungu alivyowapenda na kuwatunza wakati wa mateso yao jangwani baada ya kuwakomboa kutoka utumwani Misri.
"Mungu alikuwa nao walipopata kiu na njaa; akawapa chakula kutoka mbinguni, akawanywesha maji kutoka kwenye mwamba, na kuwaponya dhidi ya nyoka wa moto," alieleza mhubiri huku akiwaasa waamini kutosahau wema wa Mungu hata pale wanapokuatana na majaribu wasikate tamaa bali wakimbilie kwa Yesu wa Ekaristi.
Waamini walitakiwa kuambatana na Mwenyezi Mungu zaidi kuliko kitu kingine chochote, wakitambua kuwa Yeye ndiye aliyewaumba.
Changamoto ya Vizuizi vya Dhambi na Kilema cha Rushwa
Kuhusu somo la Injili, ambapo Yesu anajitambulisha k**a "Chakula kilichoshuka kutoka mbinguni," mhubiri alifafanua tofauti kati ya chakula cha kawaida na Ekaristi Takatifu. Alibainisha kuwa tofauti na chakula cha kimwili kinachotoa nguvu za muda, Mwili na Damu ya Yesu Kristo hushibisha na kustawisha roho, na humfanya Kristo akae ndani ya kila mmoja anayemwamini.
Hata hivyo, swali gumu liliibuliwa kuhusu idadi kubwa ya watu wanaohudhuria ibada lakini wanashindwa kupokea Sakramen