UMTV

UMTV Chanel hii ya usambara Mountain tv ni kwa madhumuni ya kutoa elimu kwa vijana lakini kwa jamii nzima

Chanel hii ya usambara Mountain tv ni kwa madhumuni ya kutoa elimu kwa vijana lakini kwa jamii nzima
Elimu inaweza kuwa shuleni, kilimo utunzaji wa mazingira, Afya lakini pia namna ya kumjua Mungu. Usisahau kusubscribe ili uwe wa kwanza kupata habari mara tuu inapotumwa, like, comment, na share video zetu
Kwa mawasiliano zaidi whatsapp sms 0695559776
Email: [email protected]

Pumzika kwa Amani Sr Olimpya Mushi
18/11/2025

Pumzika kwa Amani Sr Olimpya Mushi

TANZIA TANZIA TANZIA TANZIA Uongozi wa Shirika la Masista wa Mama yetu wa Usambara Jimbo katoliki la Tanga wanasikitika ...
17/11/2025

TANZIA TANZIA TANZIA TANZIA
Uongozi wa Shirika la Masista wa Mama yetu wa Usambara Jimbo katoliki la Tanga wanasikitika kutangaza kifo cha Sr Olympya Mushi kilichotokea Hospitali ya Ocean Road Dar es Salaam
Mazishi yatafanyika siku ya Jumatano Tr 19/11/2025 Makao Makuu ya Shirika Korogwe Kwamndolwa
Roho ya Marehemu Sr Olympya ipate Rehema kwa Mungu ipumzike kwa Amani

14/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. M***a Azan Zungu pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. George Mcheche Masaju mara baada ya kufungua rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jijini Dodoma tarehe 14 Novemba, 2025.


14/11/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwasili Bungeni kwenye ufunguzi wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Novemba 14, 2025 Jijini Dodoma.


14/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la Polisi mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma tarehe 14 Novemba, 2025.


14/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan Ameeleza Sababu ya kutoa msamaha kwa makundi yote yaliyok**atwa kwa kusababisha Vurugu Oktoba 29.2025 kwa kunukuu katika kitabu cha Luka sura 23:34 Yesu akasema baba uwasamehe kwakuwa hawajui walitendalo.


14/11/2025

Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan baada ya kumaliza kumuapisha waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu. Amemuhusia mambo kadhaa ili kumuwezesha kufanya kazi yake kwa umakini na maslahi ya Taifa.

Kwa umri wako vishawishi ni vingi vya marafiki ndugu, jamaa na wengine, vishawishi ni vingi. Nafasi yako ile haina rafiki haina ndugu, haina jamaa. Ni nafasi ya kulitumika taifa hili…”


14/11/2025

Rais Samia Suluhu Hassan leo anatarajiwa kumuapisha Mbunge wa Iramba Magharibi, Dk Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dk Moses Kusiluka imeeleza Dk Mwigulu ataapishwa saa nne asubuhi katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma. Rais Samia aliteua jina la Waziri Mkuu kutekeleza Ibara ya 51 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Toleo la 2005.

Ibara ya 51(1) ya katiba hiyo inamtaka Rais ateue mbunge wa kuchaguliwa kutoka katika jimbo la uchaguzi anayetokana na chama cha siasa chenye wabunge wengi zaidi bungeni.

Katiba inaeleza k**a hakuna chama cha siasa chenye wabunge wengi zaidi, atateuliwa Waziri Mkuu anayeelekea kuungwa mkono na wabunge walio wengi. Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari alilieleza Bunge kuwa Dk Mwigulu ana sifa za kuwa Waziri Mkuu kwa kuwa ni mchapakazi, msikivu na ana upeo wa mambo.



✍️

14/11/2025

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MAADHIMISHO YA SIKU YA UGONJWA WA KISUKARI DUNIANI.


14/11/2025

Ziara ya wataalamu wa misitu kutoka Jimbo la Hunan, nchini China, imeingia hatua ya pili baada ya ujumbe huo kutembelea Makao Makuu ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) yaliyopo Itega, Dodoma. Lengo la ziara hiyo ni kuweka msingi wa ushirikiano wa muda mrefu katika masuala ya uhifadhi, utafiti na utalii wa kiikolojia kati ya taasisi hizo mbili.

Mazungumzo yaliyofanyika jana yalihitimishwa kwa makubaliano ya awali ya kuandaa makubaliano ya ushirikiano (MoU) kati ya TFS na Idara ya Misitu ya Hunan. Makubaliano hayo yataainisha maeneo mahsusi ya ushirikiano, yakiwemo tafiti za pamoja, ubadilishanaji wa wataalamu na kukuza utalii wa mazingira asilia, hususan katika hifadhi za misitu.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Kamishna wa Uhifadhi wa Misitu, Prof. Dos Santos Silayo, alisema makubaliano hayo yatatoa dira mpya ya ushirikiano wa kimataifa katika kulinda misitu, kukuza tafiti za pamoja na kuendeleza utalii unaohusisha jamii katika shughuli za uhifadhi.

“Tumeafikiana kuandaa mfumo wa ushirikiano wa muda mrefu utakaowezesha kubadilishana wataalamu, teknolojia za uhifadhi, na kukuza tafiti za pamoja za utalii wa kiikolojia. Hii ni fursa kubwa ya kuimarisha diplomasia ya uhifadhi na kulinda misitu yetu kwa manufaa ya vizazi vijavyo,” alisema Prof. Silayo.

Kwa upande wake, Kiongozi wa Ujumbe wa Wachina ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Misitu ya Hunan, Jianga Rui, alisema Serikali ya China imeweka dhamira ya kuanzisha uhusiano wa kindugu kati ya hifadhi za misitu za nchi hizo mbili. Alisema dhamira hiyo inalenga kuimarisha uelewa wa pamoja kuhusu uhifadhi wa mazingira na maendeleo ya utalii wa misitu.

“Tumevutiwa na mfumo wa Tanzania wa usimamizi wa hifadhi na namna jamii inavyoshirikishwa katika uhifadhi. Tunataka kujifunza kutoka kwenu na kuanzisha miradi ya pamoja itakayokuza uhusiano wa kirafiki na kukuza utalii wa mazingira asilia,” alisema Jianga Rui.

Aliongeza kuwa, kwa mujibu wa taratibu za ndani za mkoa wa Hunan, ushirikiano huo utapitia njia za kidiplomasia. Hivyo, baada ya kurejea China, timu yake itawasilisha taarifa rasmi kwa mamlaka husika ili kura.


14/11/2025

Zoezi la ukusanyaji wa taarifa na takwimu kwa ajili ya tathmini ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Wizara ya Maliasili na Utalii kwa mwaka 2022/2023 – 2025/2026, limeonekana kuwa chachu ya maboresho zaidi ya shughuli zinazotekelezwa na taasisi za wizara hiyo pamoja na jumuiya za kijamii nchini.

Hayo yamebainika jijini Arusha katika zoezi hilo linaloongozwa na Mtaalamu Mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Prof. Francis Mwaijande, likihusisha taasisi na wadau mbalimbali wa sekta ya maliasili na utalii.

Mkuu wa Chuo cha Misitu Olmotonyi, Dkt. Joseph Makero, amesema zoezi hilo litasaidia chuo hicho kujipanga kikamilifu katika uundaji na utekelezaji wa mikakati inayochochea maendeleo endelevu ya mazao ya misitu.

“Zoezi hili lenye lengo la kuandaa Mpango Mkakati mpya wa Wizara (2026/2031) limetupa elimu ya namna bora ya kuandaa na kutathmini mikakati ili iweze kutumika katika kupanga hatua nyingine za maendeleo kwa miaka ijayo,” amesema Dkt. Makero.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Waongoza Watalii Tanzania (TTGA), Lembris Luipuko, amepongeza utaratibu wa wizara kufanya zoezi hilo kwa ushirikiano na wadau ambalo linaibua matumaini ya neema zaidi kwa wanachama wao na kwamba matokeo ya tathmini hiyo yatakuwa chachu ya maendeleo endelevu ya sekta ya utalii, uboreshaji wa miundombinu na vivutio vya utalii nchini.

Zoezi hilo pia limehusisha taasisi mbalimbali zikiwamo Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) pamoja na Chama cha Waendesha Utalii Tanzania (TATO).


Address

MONT
Lushoto
21701

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UMTV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share