25/09/2025
2025.09.25 Mazishi ya Askofu Mkuu Novatus Rugambwa.
( MEDIA)
VATICAN
KARD, POROLIN, ASK. MKUU RUGAMBWA ALIKIWA MWADILIFU NA UKWELI ALIUTANGAZA.
Alikabiliana kwa imani yake na mfano wa upendo katika ugonjwa,kwa kufanya hata katika fursa hii kujibakidhi kwa mapenzi yake na kwa ujenzo wa watu wa Mungu,hasa kwa wale wote ambao kwa imani walimuuguza na kumfuatilia hadi mwisho wa maisha yake hapa duniani.Alikuwa mwadilifu wa maisha na ushuhuda wa mamlaka na uaminifu wa ukweli ambao aliutangaza na kuuishi.
Na Angella Rwezaula – Vatican.
Alhamisi tarehe 25 Septemba 2025, Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican, aliongoza ibada ya Misa kwa ajili ya kumuaga kwenye makao ya Milele, Askofu Mkuu Novatus Rugambwa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, akisaidia na Askofu Mkuu Msaidizi wa Vatican Edigar Pena Para, Maaskofu wakuu wengine, maaskofu na mapadre. Katika mahubiri Kardinali Parolin yake alisema "tunaadhimisha misa hii kwa ajili ya mazishi ya Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye tarehe 16 Septemba iliyopita aliaga dunia baada ya ugonjwa wa muda mrefu, Bwana alimwita kwake. Kardinali Parolin aliendelea kueleza wasifu wake kuwa, alizaliwa huko Bukoba nchini Tanzania kunako tarehe 8 Oktoba 1957, na baada ya kupewa daraja la upadre kunako mwaka 1986, tangu 1991 kwa miaka mingi alitoa huduma yake katika Diplomasia ya Kiti Kitakatifu.
Kardinali Parolin wakati wa Mahubiri ( MEDIA)
Shughuli zake za kwanza zilifanyika huko Amerika ya Kusini, Afrika, Asia na Oceania. Baada ya kipindi, k**a Katibu Mkuu wa Baraza la Kipapa la Uchungaji wa Wahamiaji na wasafiri kuanzia 2007 hadi 20210, Papa Benedikto XIV alimteua kuwa Askofu Mkuu na Balozi wa Vatican huko Angola na Sao Tome na Prince. Baadaye alikuwa Mwakilishi wa Kipapa wa Honduras, Balozi wa Vatican wa New Zeland, Mwakilishi wa Kitume wa Oceania ya Pasifiki na visiwa vyake mbali mbali vya Ghuba hiyo.