UMTV

UMTV Chanel hii ya usambara Mountain tv ni kwa madhumuni ya kutoa elimu kwa vijana lakini kwa jamii nzima

Chanel hii ya usambara Mountain tv ni kwa madhumuni ya kutoa elimu kwa vijana lakini kwa jamii nzima
Elimu inaweza kuwa shuleni, kilimo utunzaji wa mazingira, Afya lakini pia namna ya kumjua Mungu. Usisahau kusubscribe ili uwe wa kwanza kupata habari mara tuu inapotumwa, like, comment, na share video zetu
Kwa mawasiliano zaidi whatsapp sms 0695559776
Email: [email protected]

25/09/2025

2025.09.25 Mazishi ya Askofu Mkuu Novatus Rugambwa.

( MEDIA)
VATICAN

KARD, POROLIN, ASK. MKUU RUGAMBWA ALIKIWA MWADILIFU NA UKWELI ALIUTANGAZA.

Alikabiliana kwa imani yake na mfano wa upendo katika ugonjwa,kwa kufanya hata katika fursa hii kujibakidhi kwa mapenzi yake na kwa ujenzo wa watu wa Mungu,hasa kwa wale wote ambao kwa imani walimuuguza na kumfuatilia hadi mwisho wa maisha yake hapa duniani.Alikuwa mwadilifu wa maisha na ushuhuda wa mamlaka na uaminifu wa ukweli ambao aliutangaza na kuuishi.

Na Angella Rwezaula – Vatican.
Alhamisi tarehe 25 Septemba 2025, Kardinali Pietro Parolin, Katibu wa Vatican, aliongoza ibada ya Misa kwa ajili ya kumuaga kwenye makao ya Milele, Askofu Mkuu Novatus Rugambwa katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, akisaidia na Askofu Mkuu Msaidizi wa Vatican Edigar Pena Para, Maaskofu wakuu wengine, maaskofu na mapadre. Katika mahubiri Kardinali Parolin yake alisema "tunaadhimisha misa hii kwa ajili ya mazishi ya Askofu Mkuu Novatus Rugambwa ambaye tarehe 16 Septemba iliyopita aliaga dunia baada ya ugonjwa wa muda mrefu, Bwana alimwita kwake. Kardinali Parolin aliendelea kueleza wasifu wake kuwa, alizaliwa huko Bukoba nchini Tanzania kunako tarehe 8 Oktoba 1957, na baada ya kupewa daraja la upadre kunako mwaka 1986, tangu 1991 kwa miaka mingi alitoa huduma yake katika Diplomasia ya Kiti Kitakatifu.

Kardinali Parolin wakati wa Mahubiri ( MEDIA)
Shughuli zake za kwanza zilifanyika huko Amerika ya Kusini, Afrika, Asia na Oceania. Baada ya kipindi, k**a Katibu Mkuu wa Baraza la Kipapa la Uchungaji wa Wahamiaji na wasafiri kuanzia 2007 hadi 20210, Papa Benedikto XIV alimteua kuwa Askofu Mkuu na Balozi wa Vatican huko Angola na Sao Tome na Prince. Baadaye alikuwa Mwakilishi wa Kipapa wa Honduras, Balozi wa Vatican wa New Zeland, Mwakilishi wa Kitume wa Oceania ya Pasifiki na visiwa vyake mbali mbali vya Ghuba hiyo.

Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Dkt. Lazoro B. Mambosasa, amewataka maaf...
25/09/2025

Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Dkt. Lazoro B. Mambosasa, amewataka maafisa،wakaguzi na askari kuendelea kuwa wazalendo katika kutunza mali za Jeshi la Polisi zinazotolewa na serikali kwa gharama kubwa ili ziendelee kutoa huduma bora kwa jamii.

DCP. Dkt. MAMBOSASA amesema hayo katika mapokezi ya gari mpya ya kisasa aina ya TATA (Macopollo) lililonunuliwa na Chuo hicho kwa ajili shule ya udereva Kilwa Road (VTC) Academy Driving School ambapo kitatoa mafunzo ya udereva wa abiria (PSV).

Dkt. Mambosasa amesema basi hilo litasaidia kuwanoa na kuwajengea uwezo madereva kuwa mahiri wenye ujuzi na weledi wanaokwenda kuhudumia wasafiri wakiwa wanajiamini na kutoa huduma bora.

Dkt. Mambosasa amewakumbusha kusimamia mafunzo kwa weledi na kutoa madereva mahiri ili kuzuia na kudhibiti ajali za barabarani zinazotokea kwa uzembe na kuleta madhara kwa watu na miundombinu mingine.

Kwa upande wake Mkuu wa Mafunzo chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam ACP Andrea G. Legembo amesema yeye na wakufunzi anaowasimamia watahakikisha wanatunza gari hilo na kufundisha kwa mujibu wa Sheria,taratibu,kanuni na miongozo inayohusu madereva wa abiria ili kutoa madereva wanaozingatia Sheria za barabarani na kuhakikishia watumiaji wengine wa barabara kuwa salama.

Mkuu wa kitengo cha udereva Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Deus Sokoni, ameahidi kuendelea kutoa elimu ya usalama barabarani kwa madereva na kuwajengea uelewa wa masuala ya sheria na umuhimu wa utoaji huduma bora kwa mteja na hivyo kupunguza malalamiko.


Mishoni mwa Katekesi ya Papa alitangaza mpango wa maombi siku ambayo Kanisa linaadhimisha kumbukumbu ya Mtakatifu Yohane...
25/09/2025

Mishoni mwa Katekesi ya Papa alitangaza mpango wa maombi siku ambayo Kanisa linaadhimisha kumbukumbu ya Mtakatifu Yohane XXIII na kumbukumbu ya kufunguliwa kwa Mtaguso II wa Vatican.

Aliwaalika wote kusali kwa ajili ya amani katika mwezi mzima wa Oktoba,uliowekwa wakfu kwa Rozari Takatifu,binafsi,katika familia,na katika jumuiya.

Pia Papa aliwataka wale wanaohudumu mjini Vatican kusali Rosari katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kila siku saa 1:00,jioni.

Rozari ya Amani katika Uwanja wa Mtakatifu Petro Jumamosi, tarehe 11 Oktoba  2025 siku ambayo Kanisa linamkumbuka Mtakatifu Yohane XXIII, Papa wa Waraka wa Pacem huko Terris na ujumbe wa radio unaowasihi viongozi wa Marekani na USSR "kuleta amani" katika kilele cha Mgogoro wa Kombora la Cuba. Na siku ile ile ya ilikuwa ya ufunguzi wa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican tarehe 11 Oktoba 1962, na siku  maarufu ya "hotuba kwa mwezi," inayojulikana ya  Papa Roncalli, mwishoni mwa siku kuu ya amani.

Kwa njia hiyo, Baba Mtakatifu Leo XIV  mara baada ya Katekesi yake, Jumatano tarehe 24 Septemba akiwageukia waamni na mahujai waliofika katika Uwanja wa Mtakatifu Petro alitangaza mpango wa maombi, uliopangwa kufanyika saa 12 kamili, masaa ya Ulaya na saa 1.00  kamili  masa ya Afrika Mashariki, jioni, katika muktadha wa Jubilei ya Tasaufi ya Maria Papa alisema: “Wapendwa kaka na dada, mwezi wa Oktoba, unaokaribia sasa, umejitolea hasa kwa Rozari Takatifu katika Kanisa. Kwa hiyo, ninamwalika kila mtu, kila siku ya mwezi ujao, kusali Rozari kwa ajili ya amani, kibinafsi, katika familia zao, na katika jumuiya zao.” Papa Leo XIV aliendelea kusema kuwa “pia ninawaalika wale wanaohudumu mjini Vatican kusali sala hii katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kila siku saa 1:00 jioni.”
Kwa namna ya pekee, jioni ya Jumamosi, tarehe 11 Oktoba, saa 12:00 jioni, tutafanya hivyo kwa pamoja katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, wakati wa Mkesha wa Jubilei ya Tasaufi ya Maria, pia kukumbuka kumbukumbu ya kufunguliwa kwa Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican


Jiwe la msingi la Ubalozi wa Vatican wa baadaye nchini Malawi uliwekwa Septemba 22, 2025, katika mji mkuu, Lilongwe. Ask...
25/09/2025

Jiwe la msingi la Ubalozi wa Vatican wa baadaye nchini Malawi uliwekwa Septemba 22, 2025, katika mji mkuu, Lilongwe. Askofu mkuu Gian Luca Perici ambaye ni Balozi wa Vatican nchini Zambia na Malawi alibariki jiwe la msingi la Makao Makuu mapya ya Uwakilishi wa Kipapa. Hadi sasa, ujumbe wa kidiplomasia wa Vatican nchini Malawi ulikuwa na makao yake mjini Lusaka, Zambia. Kwa hiyo ujenzi wa Ubalozi wa Vatican katika moyo wa nchi unawakilisha hatua muhimu, inayolenga kuimarisha uhusiano kati ya Vatican na Malawi. "Nyumba ya Papa" haitakuwa kitovu cha shughuli za kidiplomasia tu, bali pia ni ishara halisi ya ushirika na ukaribu, mahali pa kukutana na mazungumzo katika huduma ya amani na maendeleo.

Sherehe hiyo ilihudhuriwa na wawakilishi wengi wa kikanisa na mamlaka za kiraia. Waliowakilisha Kanisa Katoliki ni Monsinyo Martin Anwel Mtumbuka, Askofu wa Karonga na Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Malawi (MCCB), Askofu Mkuu George Desmond Tambala wa Lilongwe, na Monsinyo Peter Sababu, Askofu wa Dedza. Wawakilishi wa taasisi hizo walihudhuria hafla hiyo kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Halmashauri ya Manispaa ya Lilongwe, Kamisheni Kuu ya Tanzania, Baraza la Taifa la Sekta ya Ujenzi, na Kampuni ya Terrastone Limited inayohusika na ujenzi wa jengo hilo.


Taarifa kwa Umma cc
25/09/2025

Taarifa kwa Umma
cc

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Adv. Angelina Marco Lubela, amekutana na kuzungumza na viongozi wa dini kutoka madheheb...
25/09/2025

Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Adv. Angelina Marco Lubela, amekutana na kuzungumza na viongozi wa dini kutoka madhehebu mbalimbali na kuwahimiza kuendelea kudumisha amani, utulivu, na mshik**ano katika jamii ili kujenga jamii yenye amani na utulivu.

Akizungumza na Viongozi hao katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Mhe. Angelina amesisitiza kuwa viongozi wa dini wana nafasi muhimu katika malezi ya jamii na kuchangia katika maendeleo ya nchi kupitia mafundisho yao yanayo sisitiza amani na upendo miongoni wa jamii. 

"Serikali inatambua mchango wenu mkubwa katika kujenga maadili na kuimarisha amani, sisi k**a Serikali tunaamini kwamba bila ya amani hakuna maendeleo kwa hiyo, tunawaomba muendelee kuitumikia jamii kwa uaminifu na kuhubiri upendo na utulivu," amesema Mhe. Angelina.

Sambamba na hayo amewaomba viongozi hao kuhamasisha waumini wao kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo, ikiwa ni pamoja na kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 kwa amani na utulivu.

Kwa upande wao, viongozi wa dini wametoa shukrani zao Kwa Mkuu wa Wilaya kwa kuwaalika na kuwasikiliza, huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na serikali katika kuhudumia jamii na kuhakikisha amani ya nchi inalindwa.

Katika Mkutano huo uliohitimishwa kwa dua maalum ya kuiombea nchi na viongozi wake, Viongozi wa dini zote kwa kauli moja wakubaliana na kuipitisha siku ya Jumatano ya Septemba 01, 2025 kuwa siku maalum ya kuliombea taifa kuelekea Uchaguzi Mkuu, maombi ambayo yatatanguliwa na maandamano ya amani kwa Viongozi hao na baadae kuhitimishwa katika Viwanja vya Right to Play Wilayani Serengeti.


  Licha ya kupata ushindi katika michezo mitatu ya kiushindani ikiwemo mchezo dhidi ya watani wao wa Jadi katika mchezo ...
25/09/2025

Licha ya kupata ushindi katika michezo mitatu ya kiushindani ikiwemo mchezo dhidi ya watani wao wa Jadi katika mchezo wa ngao ya Jamii ukipita katika kurasa za mitandao ya kijamii mashabiki wengi wa klabu hiyo wanaonekana kutopenda aina ya mpira timu hiyo inaocheza kwasasa ukilinganisha na siku za awali.

Share nasi kutuambia l wewe unaonaje aina ya mpira wa kocha Folz.


Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, akiwa bado katika Mkoa wa Njombe, anat...
23/09/2025

Mgombea Mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel Nchimbi, akiwa bado katika Mkoa wa Njombe, anatarajiwa kuzungumza na wananchi leo Septemba 23, 2025, kupitia mikutano midogo ya kampeni ambayo itafanyika katika maeneo ya Wanging’ombe, Makete, na hatimaye kumalizia siku ya leo kwa kufanya mkutano mkubwa Njombe Mjini.

Dkt. Nchimbi anaendelea na kampeni za CCM kwa ajili ya kunadi sera na Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa kipindi cha 2025-2030, huku akimuombea kura mgombea Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na wagombea wengine wa Ubunge na Udiwani.


Spika wa Bunge la taifa nchini DRC, Vital Kamerhe, amejiuzulu. Alikuwa mada ya ombi ambalo lilipaswa kupigiwa kura wakat...
23/09/2025

Spika wa Bunge la taifa nchini DRC, Vital Kamerhe, amejiuzulu. Alikuwa mada ya ombi ambalo lilipaswa kupigiwa kura wakati wa kikao cha mashauriano katika makao makuu ya Baraza la Wawakilishi mjini Kinshasa. Hatimaye, amewasilisha barua ya kujiuzulu kwake kwa Kongamano la viongozi, ambalo huwaleta pamoja viongozi wa makundi ya wabunge, kulingana na wabunge kutoka chama chake, UNC.

Vital Kamerhe amejiuzulu wadhifa wake k**a Spika wa Bunge la taifa siku ya Jumatatu alasiri, Septemba 22. Kulingana na vyanzo kadhaa katika Baraza la Wawakilishi, ikiwa ni pamoja na wabunge walionukuliwa na Radio Okapi, amewasilisha barua ya kujiuzulu kwake kwa kongamano la viongozi kutoka makundi mbalimbali ya wabunge.

Vital Kamerhe amejiuzulu wadhifa wake Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Uamuzi huu unakuja baada ya siku kadhaa za mvutano uliochochewa na ombi lililowasilishwa na wabunge kutoka chama cha rais cha UDPS na vyama vingine, wakimtuhumu kwa utovu wa usimamizi na kuzuia usimamizi wa bunge.

Walalamikaji walimkosoa Kamerhe kwa kukosa kuafikiana na vipaumbele vya serikali, haswa usimamizi usio wa wazi wa pesa za bunge. Licha ya majaribio yake ya kutuliza hali, Kamerhe alishindwa kupata uungwaji mkono wa kutosha. Baadhi ya waangalizi wanaona hili k**a suluhu la ndani la matokeo ndani ya Muungano Mtakatifu, unaolenga kuimarisha udhibiti wa UDPS kwenye taasisi hiyo.

Kujiuzulu kwa Kamerhe kunafungua njia ya uchaguzi wa haraka wa ofisi mpya ya Bunge, chini ya uongozi wa muda wa Naibu Spika Isaac Tshilumbayi. Mustakabali wa Bunge la taifa haujulikani, na nafasi hii inaweza kuibua mijadala kuhusu mageuzi ya kitaasisi na mapambano dhidi ya kutokujali.

Wakati kikao cha mashauriano kikiitishwa kuchunguza ripoti ya Tume Maalumu iliyoundwa kuchunguza malalamiko dhidi ya wajumbe 5 wa ofisi hiyo, akiwemo Vital Kamerhe mwenyewe, bado kinasubiriwa.


Ujumbe wa wahadhiri waandamizi wa Chuo Kikuu Cha Waislam cha Morogoro (MUM) ukiongozwa na Dkt. Pazi Mwinyimvua Semili .u...
22/09/2025

Ujumbe wa wahadhiri waandamizi wa Chuo Kikuu Cha Waislam cha Morogoro (MUM) ukiongozwa na Dkt. Pazi Mwinyimvua Semili .ulitembelea Ubalozi wa Tanzania-Jakarta na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Indonesia, Mheshimiwa Macocha Moshe Tembele,

Ujumbe huo upo nchini Indonesia kwa ziara ya kikazi kufuatia mwaliko wa Taasisi ya Asia-Muslim Charity Foundation (AMCF) ulipata fursa pia ya kutembelea Chuo Kikuu cha Muhammadiyah Makassar na kufanya mazungumzo na uongozi wa chuo hicho.

Miongoni mwa masuala muhimu yaliyojadiliwa na kukubalika ni pamoja na umuhimu wa kuanzisha Ushirikiano wa Kitaaluma kati ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) na Chuo Kikuu Cha Muhammadiyah Makassar hususani katika maeneo ya tafiti za pamoja na programu za ubadilishanaji wa wahadhili na wanafunzi.

Aidha, Taasisi ya Asia-Muslim Charity Foundation imeridhia kutoa msaada wa vifaa kwa ajili ya redio ya Chuo cha MUM ambayo pamoja na mambo mengine hutumika kwa ajili ya mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa fani ya Mawasiliano ya Umma.


Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Kipapa la Habari za Kimisionari FIDES, ilibainisha kuwa Padre mmoja aliuawa kati...
22/09/2025

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Kipapa la Habari za Kimisionari FIDES, ilibainisha kuwa Padre mmoja aliuawa katika shambulizi la kuvizia kando ya barabara nchini Nigeria.

Kulingana na ushuhuda uliokusanywa na vyombo vya habari vya eneo hilo, Padre Eya, ambaye alikuwa Paroko wa Kanisa la Mtakatifu Charles huko Eha-Ndiagu, alikuwa mwathirika wa shambulio la kuvizia kando ya barabara. Padre huyo alikuwa akirejea katika parokia yake wakati watu wawili waliokuwa na silaha wakiwa kwenye pikipiki waliposimama kando ya gari lake, wakifyatua tairi zake. Mara baada ya gari kulazimika kusimama, walimpiga risasi kadhaa karibu.

Ikiwa hali zilizoripotiwa na mashahidi ni sahihi, halikuwa jaribio la utekaji nyara lililoshindikana bali mauaji yaliyolengwa. Habari za kuuawa kwa padre huyo zilithibitishwa na Monsinyo Cajetan Iyidobi, Chansela wa Jimbo kuu la Nsukka, katika ujumbe wake kwa waamini unaosomeka hivi:

“Nimeshtuka sana, kwa uchungu na huzuni, lakini kwa kujisalimisha kabisa kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu na tumaini thabiti la ufufuko wa wafu, ninawataarifu kifo cha kusikitisha cha ndugu yetu mwingine, Padre Mathayo Eya. Polisi wameanzisha msako wa kuwasaka wauaji wa Padre Eya na kuwak**ata watu 38 ambao baadhi yao wanashukiwa kuhusika na mauaji hayo.

Serikali ya Mkoa wa Enogu imeweka zawadi ya naira milioni 10 (k**a euro 5,700) kwa atakayetoa taarifa za wauaji wa Padre huyo.


Ili kuishi imani yao kwa uhalisi, katika muktadha ulio na maafikiano mengi, wanasheria wa Kikristo na mahakimu wameungan...
22/09/2025

Ili kuishi imani yao kwa uhalisi, katika muktadha ulio na maafikiano mengi, wanasheria wa Kikristo na mahakimu wameungana pamoja katika chombo kiitwacho Muungano wa Mahakimu na Wanasheria Wakatoliki ulipewa jina kwa (CMABAC). Mpango huu ulizinduliwa hivi karibuni na Askofu Mkuu wa Lubumbashi, Fulgence Muteba Mugalu, rais wa Baraza la Maaskofu  Katoliki nchini Congo (CENCO).

Lengo ni kukuza maadili ya Kikristo ndani ya mfumo wa mahak**a wa Congo kupitia programu za mafunzo, mafungo, na kubadilishana uzoefu. CABAC pia husaidia maskini ambao hawawezi kumudu ada za kisheria na kuingilia kati katika baadhi ya kesi, k**a vile unyakuzi wa ardhi.


Address

MONT
Lushoto
21701

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when UMTV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share