Hadithi Zetu

Hadithi Zetu ᴋᴀʀɪʙᴜ sᴀɴᴀ ᴋᴀᴛɪᴋᴀ ᴍᴀᴋᴛᴀʙᴀ ʏᴀ ʜᴀᴅɪᴛʜɪ. ᴜᴋᴜʀᴀsᴀ ʜᴜᴜ ɴɪ ᴍᴀᴀʟᴜᴍᴜ ᴋᴡᴀ ᴋᴀᴢɪ ᴢᴀ ғᴀsɪʜɪ & ᴍᴀᴋᴀʟᴀ ᴍʙᴀʟɪᴍʙᴀʟɪ. Pia, tunatoa makala mbalimbali kwenye ukurasa wetu.

Hadithi Zetu ni ukurasa wa Facebook ambao una lengo la kuchapisha kazi za fasihi andishi, simulizi, na makala mbalimbali. Ukurasa huu umeundwa ili kuhuisha na kueneza urithi wa hadithi na tamaduni za Kiafrika kupitia njia ya maandishi. Tunajitahidi kuwa jukwaa la kuelimisha, kuburudisha, na kuhamasisha wengine kwa njia ya hadithi. Kwenye ukurasa wetu, utapata aina mbalimbali za kazi za fasihi andi

shi, ikiwa ni pamoja na hadithi za kusisimua, mashairi, riwaya fupi, na tamthilia. Tunajitahidi kuchapisha kazi zenye ubora na zinazogusa masuala mbalimbali yanayohusiana na jamii, utamaduni, upendo, mazingira, na masuala mengine ya kijamii. Mbali na kazi za fasihi andishi, tunatoa pia simulizi mbalimbali za kuvutia. Hizi ni hadithi za kusisimua, za kuburudisha, na zenye kuelimisha. Simulizi zetu zinaweza kuwa za kisasa au za jadi, zinazohusisha wahusika wenye maisha ya kuvutia na matukio ya kusisimua. Lengo letu ni kutoa burudani na kuwafanya wasomaji wetu kujisikia kushiriki katika ulimwengu wa hadithi. Makala hizi zinajadili mada mbalimbali za kijamii, utamaduni, sanaa, na masuala mengine yanayohusiana na fasihi na simulizi. Tunazingatia kutoa taarifa sahihi na za kuvutia ili kuhamasisha majadiliano na kuelimisha wasomaji wetu. Tunakaribisha wanachama wote wa jamii kuungana nasi kwenye ukurasa wetu wa Facebook, Hadithi Zetu. Tunahimiza ushiriki wa wadau wa fasihi, waandishi, wasomaji, na wapenda hadithi katika kuchangia kazi zao, kutoa maoni, na kushiriki maarifa na uzoefu wao. Tunatumai kuwa Hadithi Zetu itakuwa sehemu ambayo itawawezesha watu kugundua, kuelimika, na kufurahia upekee wa hadithi za Kiafrika na tamaduni zetu. Karibu sana kujiunga na jumuiya yetu na kushiriki katika uumbaji wa hadithi za kuvutia na za kuelimisha.

𝑰𝒍𝒊𝒑𝒐𝒊𝒔𝒉𝒊𝒂.....Moyo wake ulianza kudunda kwa kasi. Mvua ilianza kunyesha kwa nguvu zaidi maana tayari kuliuwa na kimvua ...
16/09/2025

𝑰𝒍𝒊𝒑𝒐𝒊𝒔𝒉𝒊𝒂.....

Moyo wake ulianza kudunda kwa kasi. Mvua ilianza kunyesha kwa nguvu zaidi maana tayari kuliuwa na kimvua cha rasharasha. Kivuli kile kilijificha tena. Daudi alipiga hatua tatu mbele, Bila tahadhari, mara mlio ulisikika kwa sauti ya chini Phhhhh!

Risasi iliyotoka kwenye bastola yenye silencer ilipenya upande wa kulia wa shingo yake, ikikatiza mishipa muhimu ya damu. Alitetemeka kidogo, kisha akaanguka chini kimya.

𝑺𝒂𝒔𝒔 𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂....

Mhalifu wa Kimya

Aliyehusika hakuwa mtu wa kawaida. Alivaa suti ya mvua ya kijeshi (tactical rain suit), na usoni aliweka barakoa ya usiku (thermal face mask). Bunduki aliyotumia ni SIG Sauer P226 Suppressed, bastola yenye uwezo wa kulenga kwa ukamilifu hadi mita 30 bila kutoa sauti hata kidogo.

Aliingia kwenye maabara kuu kwa kutumia keycard feki aliyotengeneza kutoka kwenye taarifa za ndani. Ndani ya chumba cha sumu, Dk. Rehema Yusuf alikuwa ameinama kwenye darubini ya kisasa, akiandika matokeo ya majaribio yake.

Hakuweza hata kusikia mlango ukifunguliwa – lakini alipoangalia kwenye kioo cha chumba, aliona mwanga wa mtu akikaribia.

“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.

Mtu hakujibu. Alimsogelea, akamk**ata kwa kasi, akampiga ganzi kwa sindano ya midazolam, akamvuta hadi sakafuni.

Kisha kwa kutumia sindano nyembamba, aliingiza potassium chloride kwenye mishipa yake ya mkono wa kushoto. Dawa hiyo, ikizidi kiasi, husababisha msh*tuko wa moyo ndani ya sekunde 45.

Rehema alikufa macho yakiwa wazi, mdomo wake ukiwa wazi k**a aliyekuwa anaomba msaada.

Taarifa Za Kifo

Asubuhi yake, mwili wa Daudi uligunduliwa na mlinzi wa mchana, Juma Kandoro, ambaye kwa kawaida huwa anaingia kazini saa moja asubuhi lakini siku hiyo aliwahi kidogo, saa 12 alikuwa ameshatia timu. Alishangaa kuona Daudi amelala chini na bado  bastola  kaye ikiwa mikononi mwake. Alipochunguza ndani ya maabara, alikuta damu ndogo kwenye sakafu na mwili wa Dk. Rehema akiwa amelala upande mmoja, macho yametumbua.

Simu ya dharura ilipigwa mara moja, “Hapa ni BioPharma Arusha! Tuna vifo viwili! Mlinzi na daktari wa maabara! Tafadhali njooni haraka!”

𝑰𝒕𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂......

゚viralシ

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒SEHEMU: 04𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......"Mauaji mengine. Daktari mwingine wa kiwanda cha ...
16/09/2025

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎
MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒
SEHEMU: 04

𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......

"Mauaji mengine. Daktari mwingine wa kiwanda cha dawa. Mji wa Malampaka. Walakini hakuna dalili za uhalifu wa kawaida. Ni mtaalamu mwingine wa sumu.”
Subira alimtazama Kamanda wake kwa mshangao, “Sir… they’re striking again.”
“Two attacks within 12 hours. This is coordinated.”
Kamanda Nasoro alibana meno, kisha akasema kwa sauti ya amri:
“Cancel Dar. Tuelekee moja kwa moja Arusha. Tuwahishe Simiyu timu ya pili. This is no longer a local murder case. We’re dealing with a serial killer, or worse… an organization.”

𝑺𝑨𝑺𝑨 𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨.............

ARUSHA – NJIRO – SAA 10:15 JIONI

Walipofika eneo la tukio, walikuta Inspector Mary akiwa ameweka kambi. Alikuwa ameshaweka mkanda wa Kamandaa usalama (crime scene tape) kuzunguka eneo lote. Maiti za Daudi na Dk. Rehema tayari zilikuwa zimeondolewa, lakini damu iliyo kwenye sakafu na athari za sindano kwenye mkono wa Rehema zilikuwa bado freshi.

Subira alichuchumaa karibu na sakafu, “Injection mark is clean. Straight to the vein. Whoever did this, alijua anachofanya.”
Kamanda Nasoro alichukua picha ya bastola ya Daudi aliyokuwa ameshikilia mpaka mwisho wa maisha yake, “Hii bastola ilikuwa loaded?”
“Ndiyo. Risasi zote 12 bado zipo. Hakuweza hata kupiga moja.”
Nasoro alitazama kamera za CCTV zilizozimwa kwa EMP.
“This is tactical. They planned this for weeks. Kila hatua imepangwa. They don’t just want these scientists dead, wanataka kazi zao zipotee kabisa.”

FILE LA KESI – “PROJECT SALAAM”

Baada ya uchunguzi wa awali, Subira alipata nyaraka zilizoonesha kuwa Dk. Rehema alikuwa sehemu ya mradi wa siri wa serikali unaoitwa “Project Salaam”. Mradi huo ulikuwa unahusu utafiti wa dawa zinazoweza kudhibiti silaha za kemikali, hasa kwa ajili ya ulinzi wa taifa dhidi ya mashambulizi ya kigaidi.
Kitu cha kushangaza zaidi? Dk. Rehema alikuwa akishirikiana na Dk. Hamza Rajabu, yule aliyekufa Simiyu.
Kamanda Nasoro alinyamaza kwa muda, macho yake yakitazama faili hilo, “This is bigger than I thought… Hawa watu hawauwi tu, wanazima utafiti mzima. Lazima kuna mtu mkubwa anawashika mkono.”

Kamanda Nasoro akajiapiza moyoni, “Sitapumzika hadi niwak**ate. Nikiwa hai au mfu.”
Lakini hakuwa anajua, mauaji haya yalikuwa tu mwanzo. Na mtego tayari ulikuwa umewekwa kwa ajili yake.

KIFO KIMYA – SIMIYU

Simiyu –Malampaka – Saa 6:42 usiku
Usiku ulikuwa mzito. Anga la kijiji cha Malampaka lilikuwa limetandwa na mawingu meusi, yasiyo na nuru hata ya mwezi. Barabara ya vumbi iliyopitia mbele ya nyumba ya Daktari Hamza Rajabu, mtaalamu wa utafiti wa molekuli katika kiwanda cha dawa cha Biogene Africa Ltd, ilikuwa kimya – si kawaida kwa maeneo haya ambayo watoto hupiga kelele hadi saa tatu usiku.

Ndani ya nyumba hiyo ya vyumba vitatu, kulikuwepo na uhai wa hatari. Saa 6:27 usiku, mtu asiyejulikana alivunja usalama wa milango ya elektroniki kwa kutumia kifaa cha kuvuruga security signal kinachojulikana k**a CodeJammer X90 – kifaa kinachotumika na maajenti wa kijasusi kudukua mifumo ya usalama ya majengo.
Mhalifu huyo aliingia kwa utulivu, akiwa amevalia sare ya kawaida ya kiwanda – madoadoa ya bluu na beji bandia ya kiwanda hicho. Bastola yake ilikuwa ya kimya, aina ya Walther PPK, maarufu kwa matumizi ya kijasusi tangu enzi za Vita Baridi.

Dkt. Hamza: Damu ya Mwanasayansi

Dk. Hamza alikuwa ameketi sebuleni akipitia faili la kidigitali lililokuwa limefungwa kwa password encryption. Alikuwa anachunguza taarifa za vifo vya wenzake wawili: Dk. Rehema Yusuf wa Arusha, na mtaalamu wa maabara wa Dar es Salaam aliyepotea wiki mbili zilizopita. Moyo wake haukuwa na amani.

Alishtuka kwa sauti ya kitu kilichoanguka jikoni. Kabla hajainuka, alisikia mlio mdogo k**a upepo – phhhh!
Risasi ya kwanza ilimgonga begani. Hakuweza kupiga kelele. Alijaribu kutambaa kuelekea mlango wa mbele, lakini mhalifu alimsogelea haraka na kumpiga sindano moja ya sumu ya sodium thiopental, ambayo humfanya mtu kupoteza fahamu ndani ya sekunde 15. Kisha akampiga sindano ya pili ya potassium chloride, iliyosababisha moyo wake kusimama kabisa.
Kabla hajaondoka, mhalifu huyo alichukua USB flash iliyokuwa mezani, ndicho kilichokuwa kinatafutwa.

Uchunguzi Wa Polisi – Usiku Uleule
Kufuatia taarifa ya majirani waliomsikia Hamza akigugumia, SP (Superintendent of Police) Samwel Kibwana, Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Bariadi, aliwasili na timu yake saa 8:02 usiku. Aliongozana na ASP (Assistant Superintendent of Police) Khadija Musa, mtaalamu wa uchunguzi wa kisayansi wa vituo vya uhalifu (forensics).

ASP Khadija alipiga picha mwili wa Dk. Hamza, akatazama alama ya sindano mkononi.
“This is precision work. No signs of struggle, no broken locks. They knew him, or knew how to get in,” alisema huku akipiga picha kwa simu yake yenye app ya ballistic evidence capture.
SP Kibwana alichungulia chini ya meza na kuona casing moja ya risasi – .32 ACP, risasi maarufu kwa bastola za kijasusi, “Walther PPK. Bastola ndogo, kimya, deadly,” alisema.

Taarifa Kufika TISS – Mwanza
Saa mbili baadaye, tukio hilo liliripotiwa kwa Afisa Usalama wa Taifa Mkoa wa Simiyu, Senior Intelligence Officer (SIO) Abbas Kimario, aliyekuwa akifuatilia shughuli za kiwanda hicho kwa miezi miwili. Aliwasiliana na Makao Makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) jijini Dodoma, na kutoa taarifa ya hatari, "Wataalamu wa viwanda vya dawa wanauawa kwa utaratibu unaoonyesha involvement ya majeshi au maajenti waliopitia mafunzo maalum ya ‘Black Ops’. Kuna uwezekano wa uvujaji wa siri za kitaifa."

Mpango wa Kitaifa Wa Kuzuia Mauaji Zaidi
Kutoka Arusha, ACP (Assistant Commissioner of Police) Nasoro Mtei alipokea taarifa hizo akiwa bado eneo la mauaji ya Rehema. Alisimama kimya kwa dakika moja kabla hajageuka kwa Detective Subira Hassan, aliyekuwa akipanga picha za CCTV zilizokuwa corrupted, “Prepare a report to IG’s office. Tuweke suala hili chini ya ‘Operation Mauti Kimya’ – a joint task force between TISS, CID na JWTZ,” alisema Nasoro, “Yes, sir,” Subira alijibu kwa ukaidi wa kazi.

Silaha, Mbinu na Njama

Taarifa kutoka kwa SIO Abbas zilionyesha kwamba mtu aliyemuua Dk. Hamza alitumia mbinu za kijeshi k**a vile, “Room Clearing” – kusafisha chumba kwa utaratibu wa haraka bila kugusa vitu.
“Needle kill” – mbinu ya kutumia sindano kimya kwa kudunga mishipa mikuu.
“EMP Jammer” kuvuruga CCTV na mitandao ya ndani.
Taarifa hizo zilipelekea kuamini kuwa huu haukuwa mhalifu wa kawaida bali mtu aliyepitia mafunzo ya kijasusi, au labda ni afisa wa zamani wa vikosi maalum.

****
Kufikia saa kumi alfajiri, vifo vitatu vya wanasayansi waliojikita katika utafiti wa dawa vilikuwa vimegusa mikoa mitatu tofauti ndani ya masaa 24: Arusha, Simiyu na Mwanza.
Kamanda Nasoro alitazama ramani ya Tanzania, akawasha red marker. Alichora mstari kutoka Arusha hadi Mwanza, kupitia Simiyu, akasema, “They’re moving in a pattern. Naona wanalenga sehemu fulani. But what’s the next target? Dodoma? Dar?”
Subira alitazama faili la “Project Salaam,” macho yake yakiwa hayapepesi.
“Sir… If the pattern holds, the next victim is in Dodoma. And he’s still alive.”

𝑰𝑻𝑨𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨.......

📌Hongera sana brother  unazidi kutuwakilisha vyema huko.
15/09/2025

📌Hongera sana brother unazidi kutuwakilisha vyema huko.

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒SEHEMU: 02𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.Mtu hakuji...
08/09/2025

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎

MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒

SEHEMU: 02
𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......

“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.
Mtu hakujibu. Alimsogelea, akamk**ata kwa kasi, akampiga ganzi kwa sindano ya midazolam, akamvuta hadi sakafuni.
Kisha kwa kutumia sindano nyembamba, aliingiza potassium chloride kwenye mishipa yake ya mkono wa kushoto. Dawa hiyo, ikizidi kiasi, husababisha msh*tuko wa moyo ndani ya sekunde 45.
Rehema alikufa macho yakiwa wazi, mdomo wake ukiwa wazi k**a aliyekuwa anaomba msaada.

𝑺𝑨𝑺𝑨 𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨.....

Taarifa Za Kifo

Asubuhi yake, mwili wa Daudi uligunduliwa na mlinzi wa mchana, Juma Kandoro, aliyeshangaa kuona bastola ya Daudi ikiwa bado mikononi mwake. Alipochunguza ndani ya maabara, alikuta damu ndogo kwenye sakafu na mwili wa Dk. Rehema akiwa amelala upande mmoja, macho yametumbua.

Simu ya dharura ilipigwa mara moja, “Hapa ni BioPharma Arusha! Tuna vifo viwili! Mlinzi na daktari wa maabara! Tafadhali njoo haraka!”
Polisi walifika ndani ya dakika 30, wakiongozwa na Inspector Mary Christian, mpelelezi wa mkoa. Alitizama eneo la tukio kwa macho makali.
“This isn’t just murder. This is surgical execution.”

UKWELI ULIOJIFICHA

Katika uchunguzi wa awali:

Hakuna alama za kuvunjwa kwa mlango
Kamera za CCTV zilitumiwa kifaa cha “blackout EMP” – hakuna rekodi
Rehema alikuwa ameanza kuchunguza dawa mpya ya sumu ya silaha za kijeshi
Jambo la ajabu zaidi, faili lote la utafiti wa Rehema lilikuwa limefutwa kutoka kwenye kompyuta na backups zilikuwa zimeharibiwa kimfumo.

Njiro, Arusha – saa 12:00 jioni
Mvua iliacha kunyesha. Inspector Mary alisimama mbele ya mwili wa Rehema.
“We're dealing with professionals. Cold-blooded killers,” alisema kwa sauti ya chini.
Kilichosalia ni maswali zaidi ya majibu.

KIVULI CHA ZAMANI – DAR ES SALAAM

Dar es Salaam – Makao Makuu ya Polisi – Saa 3:11 asubuhi

Kamanda Nasoro Mtei aliingia ofisini akiwa amechelewa kwa dakika tano. Si kawaida yake. Alikuwa mtu wa muda, mwenye mazoea ya kijeshi tangu enzi zake Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kambi ya Ruvu. Lakini leo hakuamka mapema. Ndoto ya usiku iliyomhusu mkewe aliyefariki miaka mitatu iliyopita bado ilimzidi nguvu. Alijikuta amekaa kitandani kwa dakika 20 akitafakari maisha.

Ofisi yake ilikuwa imepangwa kwa ustadi. Ubao wa whiteboard ulioandikwa kwa maandishi mekundu na meusi ya uchunguzi wa utekaji wa mwaka jana bado ulikuwepo. Kamera ndogo ya CCTV ilikuwa imefungwa juu ya ukuta wa kushoto, na mezani kulikuwa na bastola yake ya kawaida – G***k 17 Gen5, bastola iliyotumika sana na maofisa wa upelelezi duniani kote, yenye risasi 17 kwenye magazini, rahisi kutumia na sahihi hata katika mapigano ya karibu.

Alipokaa, simu yake ya mezani ikaita, “Kamanda Nasoro, kuna tukio la mauaji Arusha. Wamekufa watu wawili – mlinzi na daktari wa sumu. Mauaji ni ya kimya sana, hakuna dalili za uvamizi,” ilisema sauti ya Detective Subira Hassan, mpelelezi wake wa karibu.
Nasoro alikunja nyuso, “Arusha? Daktari wa sumu?” alirudia, kisha akainuka na kusimama mbele ya dirisha kubwa lililokuwa linaangalia bahari ya Hindi.
Subira aliendelea, “Na faili lake la kazi limefutwa. Kuna ushahidi mdogo sana, lakini hii staili ya mauaji inafanana na ile kesi ya miaka miwili iliyopita… ile ya ‘Mtengeneza Sumu wa Tabata’.”
Kamanda alitulia, akashika kidevu chake, “I thought we buried that case…”
“So did I. But this feels like a continuation. Au copycat killer.”
Aliisogelea bastola yake, akaichukua taratibu na kuiweka kwenye koti lake la suti ya kijivu, “Prep the case files. Book two seats to Arusha. Tuna kazi.”

****

SAA 7:45 MCHANA – UWANJA WA NDEGE – JULIUS NYERERE

Nasoro na Subira walikuwa tayari kupanda ndege ya Shirika la Precision Air. Kabla hawajaondoka, Subira alipokea ujumbe kwenye simu yake ya mkononi kutoka kwa Detective Samwel Kibwana wa kanda maalumu ya kipolisi, Simiyu.
“Mauaji mengine. Daktari mwingine wa kiwanda cha dawa. Mji wa Malampaka. Walakini hakuna dalili za uhalifu wa kawaida. Ni mtaalamu mwingine wa sumu.”
Subira alimtazama Kamanda wake kwa mshangao, “Sir… they’re striking again.”
“Two attacks within 12 hours. This is coordinated.”
Kamanda Nasoro alibana meno, kisha akasema kwa sauti ya amri:
“Cancel Dar. Tuelekee moja kwa moja Arusha. Tuwahishe Simiyu timu ya pili. This is no longer a local murder case. We’re dealing with a serial killer, or worse… an organization.”

𝑰𝑻𝑨𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨...........

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎MTUNZI:  𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒SEHEMU: 01MAAFA YA NJIRO – ARUSHAArusha, Tanzania – Mtaa wa Njiro – Saa 3:...
04/09/2025

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎

MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒

SEHEMU: 01

MAAFA YA NJIRO – ARUSHA

Arusha, Tanzania – Mtaa wa Njiro – Saa 3:07 usiku.
Baridi ya jiji la Arusha ilikuwa imekithiri kiasi kwamba hata mbwa waliokuwa wakirandaranda mitaani walikuwa wamejibanza chini ya magari yaliyokuwa yameegeshwa kandokando ya barabara. Mvua nyepesi ilikuwa ikinyesha kwa kasi isiyo na sauti nyingi, ikiambatana na upepo uliotoka maeneo ya mlima Meru.
Katika kando ya mtaa huo wa Njiro, kulikuwepo na majengo makubwa ya Tanzania BioPharma Ltd, moja ya makampuni yanayoongoza kwa kutengeneza dawa za kupambana na magonjwa ya mlipuko. Kiwanda hicho kilihifadhi baadhi ya kemikali adimu ambazo zilihitaji ulinzi wa hali ya juu lakini usiku huu, hali ilikuwa tofauti.

Mlinzi wa usiku, Daudi Mshana, alikuwa na miaka 52, mstaafu wa Jeshi la Wananchi. Alivaa koti la kijeshi la zamani, suruali ya rangi ya kaki, na viatu vilivyokuwa vimechakaa kwa miaka ya huduma. Mikononi mwake, alibeba bastola aina ya Ta**us G2C, yenye risasi 12 ndani ya magazini. Bastola hiyo ndogo lakini ya kuaminika ilimsaidia kujihami nyakati za hatari, japo kwa miaka mitano hakuwahi kulazimika kuitumia. Hii ilimfanya asiwe na wasiwasi hasa anapokuwa eneo lake la lindo ijapokuwa utulivu wa kia siku haukumfanya kupoteza umakini.

Tochi aliyokuwa amevaa kichwani ilikuwa ikitoa mwangaza hafifu. Alipita kwenye lango kuu la maegesho ya magari, akapita mbele ya jengo la maabara. Usiku huu kulikuwa na ukimya usio wa kawaida. Wafanyakazi wa usiku waliokuwa maabara walikuwa wachache miongoni mwao ni Dk. Rehema Yusuf, mtaalamu wa sumu (toxicologist) aliyekuwa akifanya uchunguzi juu ya dawa mpya ya kuzuia sumu ya sarin inayotumika vitani.

Katikati ya doria yake, Daudi aliona kivuli kikisogea kwa kasi nyuma ya tanki kubwa la kuhifadhia kemikali.
“Heeeh! Nani huyo?” sauti yake ilivuma kwa ukali, mikono ikishika bastola tayari. Hakujibiwa.
Akasogea taratibu, macho yake yakiwa makini. Moyo wake ulianza kudunda kwa kasi. Mvua ilianza kunyesha kwa nguvu zaidi maana tayari kuliuwa na kimvua cha rasharasha. Kivuli kile kilijificha tena. Daudi alipiga hatua tatu mbele, Bila tahadhari, mara mlio ulisikika kwa sauti ya chini Phhhhh!
Risasi iliyotoka kwenye bastola yenye silencer ilipenya upande wa kulia wa shingo yake, ikikatiza mishipa muhimu ya damu. Alitetemeka kidogo, kisha akaanguka chini kimya.

****
Mhalifu wa Kimya

Aliyehusika hakuwa mtu wa kawaida. Alivaa suti ya mvua ya kijeshi (tactical rain suit), na usoni aliweka barakoa ya usiku (thermal face mask). Bunduki aliyotumia ni SIG Sauer P226 Suppressed, bastola yenye uwezo wa kulenga kwa ukamilifu hadi mita 30 bila kutoa sauti hata kidogo.
Aliingia kwenye maabara kuu kwa kutumia keycard feki aliyotengeneza kutoka kwenye taarifa za ndani. Ndani ya chumba cha sumu, Dk. Rehema Yusuf alikuwa ameinama kwenye darubini ya kisasa, akiandika matokeo ya majaribio yake.

Hakuweza hata kusikia mlango ukifunguliwa – lakini alipoangalia kwenye kioo cha chumba, aliona mwanga wa mtu akikaribia.
“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.
Mtu hakujibu. Alimsogelea, akamk**ata kwa kasi, akampiga ganzi kwa sindano ya midazolam, akamvuta hadi sakafuni.

Kisha kwa kutumia sindano nyembamba, aliingiza potassium chloride kwenye mishipa yake ya mkono wa kushoto. Dawa hiyo, ikizidi kiasi, husababisha msh*tuko wa moyo ndani ya sekunde 45.
Rehema alikufa macho yakiwa wazi, mdomo wake ukiwa wazi k**a aliyekuwa anaomba msaada.

𝑰𝒕𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂........

Usiahau kutembelea page mpya ya










25/08/2025

nisapoti.com/Hadithizetu

🌟 HADITHI MPYA! 🌟"SMS YA MWISHO" – Hadithi ya kusisimua, kuhuzunisha na yenye mafunzo makubwa kuhusu maisha, mapenzi na ...
17/07/2025

🌟 HADITHI MPYA! 🌟
"SMS YA MWISHO" – Hadithi ya kusisimua, kuhuzunisha na yenye mafunzo makubwa kuhusu maisha, mapenzi na siri nzito zinazofichwa na ujumbe mmoja tu wa mwisho... 📱💔

🆓 Inapatikana BURE kabisa!
📲 Pakua sasa kupitia duka letu la Hadithi Zetu kwa Selar:
👉 https://selar.com/5m27a12576

Usikose simulizi hii ya kipekee ambayo imemgusa kila msomaji aliyeipata!

---

🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖

UTANGULIZIKatika dunia ya leo ya teknolojia na haraka ya maisha, upendo wa kweli unaonekana kuwa jambo adimu — jambo la hadithi. Lakini vipi k**a moyo mmoja unaweza kugusa mwingine bila hata kuonana? Vipi k**a ujumbe mmoja wa maandishi unaweza kuwa mwanzo wa mapenzi ya maisha?“SMS YA MWISHO” n...

📢 Punguzo Kubwa la Hadithi ya Jaribu la Ushindi!Wapenzi wa hadithi, Jaribu la Ushindi sasa inapatikana kwa bei mpya nafu...
17/07/2025

📢 Punguzo Kubwa la Hadithi ya Jaribu la Ushindi!

Wapenzi wa hadithi, Jaribu la Ushindi sasa inapatikana kwa bei mpya nafuu!

👉 Toka TSh 5,000 sasa ni TSh 2,500 tu!

Usikose kupata hadithi hii yenye msisimko, mafunzo na burudani kubwa!

Pakua sasa kupitia duka letu la Hadithi Zetu kwenye Selar:
https://selar.com/m4931y

Mungu alipotuumba wanadamu alituwekea na vipimo vya kutupima ili kutujua k**a kweli tunaweza kufuata au kuishi kwa kufuata maelekezo yake. Hata mzazi anapotaka kumpa kitu mwanaye, jambo la kwanza atampa mtihani mwanaye kumpima kujua jambo fulani na atakapojiridhisha basi atampatia kitu hicho. Ndani....

02/07/2025

Celebrating my 4th year on Facebook. Thank you for your continuing support. I could never have made it without you. 🙏🤗🎉

📌🎉✨ Leo ni Siku Yangu ya Kuzaliwa! ✨🎉Leo naandika haya nikiwa na moyo wa shukrani, tafakari, na upendo mwingi. Ni siku y...
27/06/2025

📌🎉✨ Leo ni Siku Yangu ya Kuzaliwa! ✨🎉

Leo naandika haya nikiwa na moyo wa shukrani, tafakari, na upendo mwingi. Ni siku yangu ya kuzaliwa siku ya kipekee ninayoichukulia kwa uzito na heshima, kwa sababu ni zawadi nyingine ya maisha kutoka kwa Mungu. Si kwa akili zangu, si kwa nguvu zangu, bali ni kwa rehema na fadhili zake zisizokoma.

Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuvuka mwaka mwingine wa maisha. Katika kila siku, nimejifunza, nimekua, na nimeendelea kujitambua.
Lakini pia leo naitazama siku hii kwa hisia mchanganyiko…
Mama yangu mpendwa tangu ulipoondoka mwaka 2022, maisha hayajawahi kuwa k**a zamani. Nakukumbuka sana leo. Upendo wako, busara zako, na maombi yako vinaishi ndani yangu kila siku. Siku k**a ya leo ningependa sana unione ukiwa na tabasamu lako la upendo.
Nakupenda, Mama. Naendelea kukuenzi kwa vitendo vyema. 🤍

Kwa upande mwingine, namshukuru sana Baba yangu kwa kuendelea kusimama imara, k**a nguzo ya familia yetu. Ametupa moyo wa matumaini na ujasiri licha ya yote. Pia nina bahati kuwa na kaka, dada, na mdogo wangu, ambao wamekuwa sehemu ya nguvu yangu, msaada wangu na marafiki wa kweli katika kila hatua ya maisha.
Na kwa rafiki zangu wa kweli, wale wachache wa kipekee waliobaki karibu nami kwa uaminifu, kwa maneno ya faraja, na kwa moyo wa dhati, asanteni sana. Urafiki wenu ni zawadi.

Leo siadhimishi tu siku yangu ya kuzaliwa. Naadhimisha nguvu ya upendo, familia, marafiki wa kweli, na uwepo wa Mungu katika maisha yangu. Mwaka mpya wa maisha umefika, na naupokea kwa imani, shukrani, na matumaini mapya.

Heri ya siku yangu ya kuzaliwa. Najisherehekea, lakini pia nawasherehekea wote walioko katika maisha yangu leo.
Mungu ni mwaminifu.

🤍𝑯𝑨𝑷𝑷𝒀 𝑩𝑰𝑹𝑻𝑯𝑫𝑨𝒀 𝑻𝑶 𝑴𝑬🤍







゚viralシ







𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝐽𝐴𝑅𝐼𝐵𝑈 𝐿𝐴 𝑈𝑆𝐻𝐼𝑁𝐷𝐼𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝐺𝐸𝑂𝐹𝑅𝐸𝑌 𝐷𝐼𝑆𝑀𝐴𝑆𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 04ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ......Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Mar...
03/06/2025

𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝐽𝐴𝑅𝐼𝐵𝑈 𝐿𝐴 𝑈𝑆𝐻𝐼𝑁𝐷𝐼
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝐺𝐸𝑂𝐹𝑅𝐸𝑌 𝐷𝐼𝑆𝑀𝐴𝑆
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 04

ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ......

Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Martin na kuanza kumtukana na kumtuhumu kuwa amemuua mjukuu wake, Martin akijitetea sana lakini hakuna kitu kilichobadilika, mama mkwe huyo aliendelea kumtuhumu kuwa mali zote alizonazo ni kwa sababu alitoa kafara ya watu ili awe tajiri. Hii ilimuumiza sana Martin aliamua kukata simu. Alitaka kupata msaada kutoka kwa mtu, na mtu pekee aliyemfikiria alikuwa ni Juliet!

sᴀsᴀ ᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.........

Alichukua funguo za gari na kutoka katika ofisi yake huku akimuelekeza secretary wake kukata mikutano yote aliyokuwa nayo siku hiyo na kuipangia tarehe nyingine. Aliingia ndani ya gari yake na kuelekea anakofanyia kazi Juliet katika kampuni ya simu ya MTN.

Juliet alikuwa nje ya jengo la makao makuu ya kampuni ya simu ya MTN, alikuwa akizungumza na mtu mara akaja kijana mmoja ambaye alimueleza kuwa kuna mtu amemuagiza amuite.
“Ni nani?” Juliet alihoji kwa mshangao.
“Simfahamu…Yuko pale kwenye maegesho ya gari.”
“Okey asante…. Naomba uniwie radhi, ngoja nikamuone huyo mtu.” Juliet alikubali wito kisha akamuaga mtu akiyekuwa anazungumza naye na kwenda kumuona mtu aliyeelekezwa kuwa yuko kwenye maegesho ya magari.

Juliet alipofika hakuamini, alikuwa ni Martin, mume wa Annabelle. Hasira zikamjaa, “Unafanya nini hapa?” Juliet alimuuliza Martin kwa hasira.
“Juliet salamu kwanza basi…”
“Hakuna haja ya salamu…. Sikia sema shida yako na uondoke!”
Martin alibaki akidua maana Juliet akiyeko mbele yake muda huo si Juliet yule aliyekuwa akimchangamkia na kumsifia kila wakipokutana. “Anyway, Juliet niko hapa kukuomba msaada!”
“Wa kumuua Annabelle?” Juliet alimuuliza Martin swali gumu na la ajabu sana.

“WHAT?” Martin aliuliza kwa shangao hakuamini alichokisikia kutoka kwa Juliet.
“Ooh! Ulidhani siri yako haitafichuka eeh? Ulidhani hatutajua kuwa wewe ndiye uliyemtoa kafara mwanao mwenyewe ili upate utajiri ulionao sasa na sasa unataka umuue na 7 yangu,hapo umekwama Martin.” Juliet aliongea maneno makavu makavu ambayo yalimduwaza Martin.
“Excuse Me! Juliet, what the hell are you talking about?” Martin aliuliza kwa mshangao.
“Martin, sina muda wa kupoteza na Wewe, kusanya makongoro yako na uondoke hapa sasa hivi…”
“Juli…”
“Martin ondoka haraka au nitaita walinzi, muuaji mkubwa wewe.”
Martin hakuwa na la kufanya aliamua kuingia ndani ya gari yake na kuondoka huku akiwa na machungu moyoni na kichwani mwake maneno k**a kafara, muuaji yalizidi kujirudia kichwani mwake. Martin alijikuta machozi yakimtoka, akaanza kulia kwa uchungu huku akimuuliza Mungu k**a kweli yeye ni mbaya kiasi hicho.

Akiwa kwenye dimbwi la mawazo mala bodaboda akakatiza mbele ya gari yake haraka akaanza kumkwepa na bahati mbaya akaenda kuigonga nguzo ya umeme iliyokuwa upande wa kulia, akazimia hapo hapo.
Martin alipoamka alijikuta yuko juu ya kitanda cha hospitali, alipotazama pembeni yake kulikuwa na chupa ya drip, alipojitazama akaona amefungwa budge maeneo mbali mbali ikiwemo kichwani. Alipotazama mlangoni alimuona nesi akiingia.

“Taratibu utajiumiza, tulia tu acha kuhangaika” Ilikuwa ni sauti ya upole ya nesi.
“Nimefikaje hapa nini kimetokea?” Martin aliuliza kwa shida kwa kuwa alikuwa anahisi maumivu sehemu mbalimbali za mwili wake.
“Umeletwa hapa na waaamaria wema, ulipata ajali ya gari!”
“Ooh! My God nimekumbuka…Daktari yuko wapi?” Martin alimuuliza yule nesi.
“Usijali daktari atafika muda si mrefu.” Nesi alijibu kwa sauti ya kiungwana sana iliyomvutia Martin hata kutamani aendelee kukaa hapo hospitali.
“Je, kuna mtu yeyote ungetaka kuwasiliana naye kumueleza juu ya hali yako?” Nesi alimuukiza Martin.
“Yeah yupo, simu yangu….”
“Hakuna simu iliyoletwa hapa pengine….”
“Wameshaiba wasamaria wema” Martin alijibu kimasihara hadi nesi akajikuta amecheka k**a ni mazuri.
“Unavituko sana wewe, usijali nipatie namba za mkeo nimpigie”
Martin akamtajia nesi yule namba za mkewe na kisha akampigia simu na kumueleza kuwa afike hospitali ya Mt. Joseph ili kumuona mumewe.
“Asante sana nesi, unaitwa nani?” Martin alimshukuru nesi yule na kumuuliza jina lake.
“Usijali ni sadaka tu hii, naitwa Sonia” Nesi alijibu kuhu akikagua kagua chupa ya drip.

Baada ya muda daktari alifika na kusalimiana na Martin. “Unajisikiaje?” Daktari aliuliza.
“Najisikia maumivu kiasi katika kichwa, mkono na mgongo” Martin alimuelezea daktari anavyojihisi.
“Ni sawa, hata hivyo hakuna majeraha makubwa uliyopata, nimekufanyia vipimo vyote uko salama hakuna mfupa uliovunjia, uko salama na haya msumivu ni yakawaida kabisa.” Daktari alimuelezea Martin ambaye alijisikia faraja sana kusikia kuwa hakupata madhara makubwa kutokana na ajali aliyopata.
Akiwa bado anazungumza na dakari, Annabelle aliingia akiwa hana hata chembe ya shauku kutaka kujua mmewe anaendeleaje.

𝑻𝒖𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒆 𝒂𝒖 𝒕𝒖𝒊𝒔𝒉𝒊𝒆 𝒉𝒂𝒑𝒂? 𝑾𝒆𝒌𝒂 𝒄𝒐𝒎𝒎𝒆𝒏𝒕 𝒉𝒂𝒑𝒐 𝒄𝒉𝒊𝒏𝒊 𝒎𝒅𝒂𝒖 𝒘𝒂𝒏𝒈𝒖

゚viralシfypシ゚viralシalシ ゚viralシ

Address

Magegele
Makambako
59122

Telephone

+255768465103

Website

https://podcasters.spotify.com/pod/show/hadithizetu, https://www.selar.co/m/hadithiz

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hadithi Zetu:

Share

Category