Hadithi Zetu

Hadithi Zetu Kila simulizi ina funzo, na kila hadithi ina maana. 🕯️🖤
Hadithi Zetu inakuletea visa vinavyoakisi maisha yetu ya kila siku, huzuni, furaha na ushindi.
(7)

Karibu tushiriki simulizi zitakazokuburudisha na kukuza fikra zako. 🧠🌹
​Karibu kwenye familia! 🤝 Hadithi Zetu ni ukurasa wa Facebook ambao una lengo la kuchapisha kazi za fasihi andishi, simulizi, na makala mbalimbali. Ukurasa huu umeundwa ili kuhuisha na kueneza urithi wa hadithi na tamaduni za Kiafrika kupitia njia ya maandishi. Tunajitahidi kuwa jukwaa la kuelimisha, kuburudisha, na kuhamasisha

wengine kwa njia ya hadithi. Kwenye ukurasa wetu, utapata aina mbalimbali za kazi za fasihi andishi, ikiwa ni pamoja na hadithi za kusisimua, mashairi, riwaya fupi, na tamthilia. Tunajitahidi kuchapisha kazi zenye ubora na zinazogusa masuala mbalimbali yanayohusiana na jamii, utamaduni, upendo, mazingira, na masuala mengine ya kijamii. Mbali na kazi za fasihi andishi, tunatoa pia simulizi mbalimbali za kuvutia. Hizi ni hadithi za kusisimua, za kuburudisha, na zenye kuelimisha. Simulizi zetu zinaweza kuwa za kisasa au za jadi, zinazohusisha wahusika wenye maisha ya kuvutia na matukio ya kusisimua. Lengo letu ni kutoa burudani na kuwafanya wasomaji wetu kujisikia kushiriki katika ulimwengu wa hadithi. Pia, tunatoa makala mbalimbali kwenye ukurasa wetu. Makala hizi zinajadili mada mbalimbali za kijamii, utamaduni, sanaa, na masuala mengine yanayohusiana na fasihi na simulizi. Tunazingatia kutoa taarifa sahihi na za kuvutia ili kuhamasisha majadiliano na kuelimisha wasomaji wetu. Tunakaribisha wanachama wote wa jamii kuungana nasi kwenye ukurasa wetu wa Facebook, Hadithi Zetu. Tunahimiza ushiriki wa wadau wa fasihi, waandishi, wasomaji, na wapenda hadithi katika kuchangia kazi zao, kutoa maoni, na kushiriki maarifa na uzoefu wao. Tunatumai kuwa Hadithi Zetu itakuwa sehemu ambayo itawawezesha watu kugundua, kuelimika, na kufurahia upekee wa hadithi za Kiafrika na tamaduni zetu. Karibu sana kujiunga na jumuiya yetu na kushiriki katika uumbaji wa hadithi za kuvutia na za kuelimisha.

📌Maelekezo......Following Love
18/04/2026

📌Maelekezo......

Following Love




















Sehemu ya Pili.....Salma?" Machibya alishangaa. "Salma gani, mama?"​"Salma dereva wa bajaji. Amesema wewe ni kijana mwam...
17/04/2026

Sehemu ya Pili.....

Salma?" Machibya alishangaa. "Salma gani, mama?"
​"Salma dereva wa bajaji. Amesema wewe ni kijana mwaminifu na unatafuta kazi kwa udi na uvumba. Nina kazi ya haraka, unapatikana?"
​Machibya alikaa mkao wa kueshimu kitandani. "Napatikana Mama. Kazi gani hiyo?"

​"Sihitaji maelezo mengi kwenye simu. Njoo eneo la Area D, nyumba namba 42. Nitakulipa shilingi laki tano kwa kazi ya saa nne tu."
​Laki tano? Kwa saa nne? Machibya alihisi k**a anaota. Alivuta pumzi ndefu. "Sawa Mama, nakuja sasa hivi."


​Machibya alivaa nguo zake zilizopauka kwa haraka, akajifuta uso kwa maji ya baridi na kuelekea Area D. Moyo ulimdunda kwa matumaini, lakini sehemu ndogo ya akili yake ilikuwa ikijiuliza; kazi gani hiyo ya laki tano kwa muda mfupi kiasi hicho?

​Alipofika kwenye nyumba hiyo ya kifahari, alimkuta mwanamke mmoja aliyejifunga khanga moja, macho yake yakiwa mekundu k**a mtu aliyekuwa akilia.
​"Wewe ndiye Machibya?" mwanamke huyo aliuliza kwa sauti ya chini huku akitazama huku na kule kuhakikisha hakuna anayewaona.
"Ndiyo mimi Mama."

"Ingia ndani haraka," mama huyo alimvuta mkono.
​Walipoingia sebuleni, harufu ya ajabu ilimpiga Machibya puani. Haikuwa harufu ya pafyum, wala haikuwa harufu ya chakula. Ilikuwa harufu ya chuma na shombo.
​"Mama, kazi yenyewe ni ipi?" Machibya aliuliza akianza kupata wasiwasi.

​Mama Hilda hakujibu. Alimwongoza mpaka chumba cha ndani kabisa. Alifungua mlango kwa mikono inayotetemeka. Machibya alipochungulia ndani, alihisi dunia inazunguka.
​Kwenye sakafu ya marumaru, kulikuwa na mwili wa mwanamume mmoja ukiwa umelala kwenye dimbwi la damu.

Machibya alirudi nyuma kwa mshtuko, lakini kabla hajageuka kukimbia, alihisi kitu cha baridi na kigumu kikigusa kisogo chake.
​"Usipige kelele kijana," sauti ya kiume na nzito ilisikika nyuma yake. "Ukijaribu kutoroka, unakuwa maiti ya pili hapa ndani. Kazi yako ni rahisi; nisaidie kuutoa huu mwili hapa na kuupoteza. Ukimaliza, laki tano yako ipo mezani... Ukikataa, utazikwa kwenye shimo moja na huyu mzee."
​Machibya alijikaza kuitazama sura ya yule aliyekufa sakafuni. Macho yake yalimtoka! Alikuwa ni yule Mzee aliyemnyang'anya bajaji miezi mitano iliyopita, Mzee Mwita Chacha!

​.......

HADITHI: 𝐊𝐈𝐒𝐀𝐒𝐈 𝐂𝐇𝐀 𝐌𝐍𝐘𝐎𝐍𝐆𝐄MTUNZI: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺MSIMU: 01SEHEMU: 01Ni majira ya saa moja asubuhi katika mtaa mmoja ulio...
16/04/2026

HADITHI: 𝐊𝐈𝐒𝐀𝐒𝐈 𝐂𝐇𝐀 𝐌𝐍𝐘𝐎𝐍𝐆𝐄
MTUNZI: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺
MSIMU: 01
SEHEMU: 01

Ni majira ya saa moja asubuhi katika mtaa mmoja uliopo pembezoni mwa jiji la Dodoma. Machibya alikuwa amejilaza chali, macho yake yakiwa yameganda kwenye bati chakavu la chumba chake lililojaa madoa ya kutu, kana kwamba anasoma ramani ya hatma ya maisha yake.

​Kichwa chake kilikuwa kizito. Aligeuka kulia na kutazama kideli cha kuwekea unga; kimekauka mpaka kimeanza kupata vumbi. Akatazama ngazi ya viungo; hakukuwa na hata ganda la kitunguu wala harufu ya nyanya.

​"Maisha gani haya?" alijisemea kwa sauti iliyovunjika, kisha akasonya kwa uchungu. "Hivi leo nikidondoka hapa, hospitali nitaenda na nini? Sina bima, sina akiba... sina hata mia mbovu."
​Mawazo yake yalirudi nyuma, miezi mitano iliyopita. Kipindi hicho Machibya alikuwa "mamba" wa barabara, dereva wa bajaji mahiri jijini Dodoma. Siku hiyo, akiwa kijiweni na washikaji zake wakipiga stori, kivuli cha Mzee mmoja kilifunika kijiwe chao.

​Alikuwa Mwalimu Mwita Chacha, maarufu k**a "Mzee Kauzu". Mwalimu wa hesabu mstaafu ambaye sura yake haikuwahi kujua rangi ya tabasamu tangu akiwa darasani.
​"Kijana... okoa muda. Lete funguo zangu!" sauti ya Mzee Mwita ilikata hewa k**a kisu.
Machibya aliduwaa. Mapigo ya moyo yalimwenda mbio k**a bajaji iliyofeli breki mteremko wa kuelekea mkoani.
"Mzee, sijakuelewa..."
"Kijana, unaelewa wazi huwa sipendi kurudia mara mbili!"

​Bila maelezo, Mzee Kauzu alichukua chombo chake na kutokomea nacho, akimwacha Machibya akiwa ameshika hewa. Tangu siku hiyo, nyota ya Machibya ilizima.

****
​Akiwa bado amezama kwenye dimbwi la mawazo, mlio wa simu yake ulimshtua. Ilikuwa namba ngeni. Aliipokea kwa kusita.
​"Hallo!" Sauti ya mwanamke wa makamo ilisikika upande wa pili.
"Hallo, nani mwenzangu?" Machibya aliuliza kwa sauti ya kinyonge.
"Unaongea na Mama Hilda. Namba yako nimepewa na rafiki yako aitwaye Salma," sauti hiyo ilijitambulisha.

Itaendelea.....

HADITHI: 𝐊𝐈𝐒𝐀𝐒𝐈 𝐂𝐇𝐀 𝐌𝐍𝐘𝐎𝐍𝐆𝐄MTUNZI: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺MSIMU: 01SEHEMU: 01Ni majira ya saa moja asubuhi katika mtaa mmoja ulio...
16/04/2026

HADITHI: 𝐊𝐈𝐒𝐀𝐒𝐈 𝐂𝐇𝐀 𝐌𝐍𝐘𝐎𝐍𝐆𝐄
MTUNZI: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺
MSIMU: 01
SEHEMU: 01

Ni majira ya saa moja asubuhi katika mtaa mmoja uliopo pembezoni mwa jiji la Dodoma. Machibya alikuwa amejilaza chali, macho yake yakiwa yameganda kwenye bati chakavu la chumba chake lililojaa madoa ya kutu, kana kwamba anasoma ramani ya hatma ya maisha yake.

​Kichwa chake kilikuwa kizito. Aligeuka kulia na kutazama kideli cha kuwekea unga; kimekauka mpaka kimeanza kupata vumbi. Akatazama ngazi ya viungo; hakukuwa na hata ganda la kitunguu wala harufu ya nyanya.

​"Maisha gani haya?" alijisemea kwa sauti iliyovunjika, kisha akasonya kwa uchungu. "Hivi leo nikidondoka hapa, hospitali nitaenda na nini? Sina bima, sina akiba... sina hata mia mbovu."
​Mawazo yake yalirudi nyuma, miezi mitano iliyopita. Kipindi hicho Machibya alikuwa "mamba" wa barabara, dereva wa bajaji mahiri jijini Dodoma. Siku hiyo, akiwa kijiweni na washikaji zake wakipiga stori, kivuli cha Mzee mmoja kilifunika kijiwe chao.

​Alikuwa Mwalimu Mwita Chacha, maarufu k**a "Mzee Kauzu". Mwalimu wa hesabu mstaafu ambaye sura yake haikuwahi kujua rangi ya tabasamu tangu akiwa darasani.
​"Kijana... okoa muda. Lete funguo zangu!" sauti ya Mzee Mwita ilikata hewa k**a kisu.
Machibya aliduwaa. Mapigo ya moyo yalimwenda mbio k**a bajaji iliyofeli breki mteremko wa kuelekea mkoani.
"Mzee, sijakuelewa..."
"Kijana, unaelewa wazi huwa sipendi kurudia mara mbili!"

​Bila maelezo, Mzee Kauzu alichukua chombo chake na kutokomea nacho, akimwacha Machibya akiwa ameshika hewa. Tangu siku hiyo, nyota ya Machibya ilizima.

****
​Akiwa bado amezama kwenye dimbwi la mawazo, mlio wa simu yake ulimshtua. Ilikuwa namba ngeni. Aliipokea kwa kusita.
​"Hallo!" Sauti ya mwanamke wa makamo ilisikika upande wa pili.
"Hallo, nani mwenzangu?" Machibya aliuliza kwa sauti ya kinyonge.
"Unaongea na Mama Hilda. Namba yako nimepewa na rafiki yako aitwaye Salma," sauti hiyo ilijitambulisha.

"Salma?" Machibya alishangaa. "Salma gani, mama?"
​"Salma dereva wa bajaji. Amesema wewe ni kijana mwaminifu na unatafuta kazi kwa udi na uvumba. Nina kazi ya haraka, unapatikana?"
​Machibya alikaa mkao wa kueshimu kitandani. "Napatikana Mama. Kazi gani hiyo?"

​"Sihitaji maelezo mengi kwenye simu. Njoo eneo la Area D, nyumba namba 42. Nitakulipa shilingi laki tano kwa kazi ya saa nne tu."
​Laki tano? Kwa saa nne? Machibya alihisi k**a anaota. Alivuta pumzi ndefu. "Sawa Mama, nakuja sasa hivi."


​Machibya alivaa nguo zake zilizopauka kwa haraka, akajifuta uso kwa maji ya baridi na kuelekea Area D. Moyo ulimdunda kwa matumaini, lakini sehemu ndogo ya akili yake ilikuwa ikijiuliza; kazi gani hiyo ya laki tano kwa muda mfupi kiasi hicho?

​Alipofika kwenye nyumba hiyo ya kifahari, alimkuta mwanamke mmoja aliyejifunga khanga moja, macho yake yakiwa mekundu k**a mtu aliyekuwa akilia.
​"Wewe ndiye Machibya?" mwanamke huyo aliuliza kwa sauti ya chini huku akitazama huku na kule kuhakikisha hakuna anayewaona.
"Ndiyo mimi Mama."

"Ingia ndani haraka," mama huyo alimvuta mkono.
​Walipoingia sebuleni, harufu ya ajabu ilimpiga Machibya puani. Haikuwa harufu ya pafyum, wala haikuwa harufu ya chakula. Ilikuwa harufu ya chuma na shombo.
​"Mama, kazi yenyewe ni ipi?" Machibya aliuliza akianza kupata wasiwasi.

​Mama Hilda hakujibu. Alimwongoza mpaka chumba cha ndani kabisa. Alifungua mlango kwa mikono inayotetemeka. Machibya alipochungulia ndani, alihisi dunia inazunguka.
​Kwenye sakafu ya marumaru, kulikuwa na mwili wa mwanamume mmoja ukiwa umelala kwenye dimbwi la damu.

Machibya alirudi nyuma kwa mshtuko, lakini kabla hajageuka kukimbia, alihisi kitu cha baridi na kigumu kikigusa kisogo chake.
​"Usipige kelele kijana," sauti ya kiume na nzito ilisikika nyuma yake. "Ukijaribu kutoroka, unakuwa maiti ya pili hapa ndani. Kazi yako ni rahisi; nisaidie kuutoa huu mwili hapa na kuupoteza. Ukimaliza, laki tano yako ipo mezani... Ukikataa, utazikwa kwenye shimo moja na huyu mzee."

​Machibya alijikaza kuitazama sura ya yule aliyekufa sakafuni. Macho yake yalimtoka! Alikuwa ni yule Mzee aliyemnyang'anya bajaji miezi mitano iliyopita, Mzee Mwita Chacha!

​𝑱𝒆, 𝑴𝒂𝒄𝒉𝒊𝒃𝒚𝒂 𝒂𝒕𝒂𝒌𝒖𝒃𝒂𝒍𝒊 𝒌𝒖𝒖𝒃𝒆𝒃𝒂 𝒎𝒘𝒊𝒍𝒊 𝒘𝒂 𝒂𝒅𝒖𝒊 𝒚𝒂𝒌𝒆? e, Machibya atakubali kuubeba mwili wa adui yake? 𝑵𝒂 𝒉𝒖𝒚𝒐 𝒌𝒘𝒂𝒏𝒂𝒖𝒎𝒆 𝒎𝒘𝒆𝒏𝒚𝒆 𝒃𝒖𝒏𝒅𝒖𝒌𝒊 𝒏𝒊 𝒏𝒂𝒏𝒊?
​USIKOSE SEHEMU YA PILI...

















📌NAWALETEA HII SOON🔥
24/03/2026

📌NAWALETEA HII SOON🔥

SEHEMU YA PILI👉🏽Katikati ya duara hilo, kikiwa kimechomekwa kwenye ardhi, kulikuwa na Fimbo ya Mninga. Haikuwa fimbo ya ...
11/03/2026

SEHEMU YA PILI

👉🏽Katikati ya duara hilo, kikiwa kimechomekwa kwenye ardhi, kulikuwa na Fimbo ya Mninga. Haikuwa fimbo ya kawaida; ilikuwa na nakshi za kale zinazofanana na mapigo ya moyo, na juu yake kulikuwa na kito kikubwa kilichokuwa kikibadilika rangi—kutoka bluu ya bahari hadi nyekundu ya jua.

👉🏽​Bibi Busara alinyosha mkono wake uliotetemeka. Alipoigusa tu, nishati ya joto ilipita mwilini mwake, ikiondoa maumivu ya uzee na kuijaza nafsi yake amani isiyo na kifani.

👉🏽Sauti ya upole, k**a sauti ya maji yanayotiririka, ilisikika akilini mwake, ​"Hii ni Fimbo ya Matumaini. Haitumiki kwa ajili ya utukufu wako, bali kwa ajili ya hitaji la mwenye njaa, mgonjwa, na aliyepotea."
​Bibi Busara aliishika fimbo ile kwa nguvu. Usiku ule, Msitu wa Giza haukuwa giza tena. Kila hatua aliyopiga kurudi kijijini, maua madogo ya mwanga yalikuwa yakichanua mahali alipokanyaga. Mapambazuko ya kijiji hicho yalikuwa karibu kubadilika milele.

👉🏽Asubuhi iliyofuata, jua lilichomoza kwa rangi ya chungwa iliyokolea, likiashiria siku nyingine ya joto kali. Bibi Busara alitoka nje ya kibanda chake akiwa ameshika fimbo yake mpya. Kwa macho ya kawaida, ilionekana k**a fimbo ya zamani ya mti, lakini moyoni mwa bibi, alijua kuwa amebeba roho ya msitu na mbinguni.

Kilio Kichakani

👉🏽​Alipokuwa akitembea kuelekea kijijini kufuata maji, alisikia sauti ya maumivu ikitokea nyuma ya kichaka cha miiba. Alisogea taratibu na kumkuta Juma, kijana mdogo aliyekuwa anajulikana kwa mbio na wepesi wake. Juma alikuwa amelala chini, uso wake ukiwa umeloa jasho la maumivu. Mguu wake wa kulia ulikuwa umevimba sana na kugeuka rangi baada ya kuanguka kwenye jabali wakati akitafuta matunda ya mwitu.

Itaendelea.....

📌BIBI NA FIMBO YA MAAJABU✨👉🏽​Katika kingo za mbali za Kijiji cha Utulivu, mahali ambapo upepo unanong’ona siri za kale k...
10/03/2026

📌BIBI NA FIMBO YA MAAJABU✨

👉🏽​Katika kingo za mbali za Kijiji cha Utulivu, mahali ambapo upepo unanong’ona siri za kale kupitia majani ya mibuyu, aliishi bibi mmoja aliyeitwa Bibi Busara. Nyumba yake ilikuwa ndogo, iliyojengwa kwa udongo mwekundu na kuezekwa kwa nyasi kavu, ikiwa imejitenga kidogo na makazi mengine ya wanakijiji.

👉🏽​Nyuma ya nyumba yake kulikuwa na kizuizi cha kutisha: Msitu wa Giza. Kwa karne nyingi, msitu huo ulijulikana kwa miti yake mirefu iliyofunika mwanga wa jua, na sauti za ajabu zilizosikika usiku. Hakuna kijana shujaa wala mwindaji stadi aliyethubutu kuingia ndani zaidi ya hatua kumi; walisema msitu huo unaishi na unalinda siri ambazo binadamu haruhusiwi kuzijua.

➡​Kipindi cha Majaribu

👉🏽​Wakati huo, Kijiji cha Utulivu kilikuwa kimepoteza jina lake. Hakukuwa na utulivu. Kiangazi cha muda mrefu kilikuwa kimekausha mito, na njaa ilikuwa imeanza konyesha makucha yake. Watoto walikuwa wakilia kwa njaa, na wazee walikuwa wakitazama anga kavu kwa matumaini yaliyofifia.
​Bibi Busara, licha ya uzee wake na mgongo uliopinda kidogo, hakukata tamaa. Kila alfajiri, alikuwa akielekea ukingoni mwa Msitu wa Giza kuomba amani na neema kwa ajili ya watu wake. Aliamini kuwa moyo mweupe ni nguvu kuliko silaha yoyote.

➡​Usiku wa Ajabu

👉🏽​Siku moja, usiku wa manane ukiwa umetanda na mwezi ukiwa umejificha nyuma ya mawingu mazito, tukio la ajabu lilitokea. Bibi Busara alikuwa ameketi nje ya kibanda chake, akitafakari hali ya kijiji. Ghafla, anga lilipasuka! Mwanga mkali wa rangi ya dhahabu na zambarau ulishuka k**a nyota inayoanguka, ukielekea moja kwa moja kwenye moyo wa Msitu wa Giza.
​Tofauti na wengine ambao wangekimbia kwa hofu, Bibi Busara alihisi uvutano usio wa kawaida. Akiongozwa na nguvu ya ajabu, alichukua taa yake ya mafuta na kuanza kutembea kuelekea kule mwanga ulipotua. Miti ya Msitu wa Giza, ambayo kawaida ilikuwa ikitisha, ilionekana kumpisha njia. Matawi yalijikunja na mizizi ilijichimbia ndani kumtengenezea barabara ya hariri.

➡​Kupatikana kwa Fimbo

👉🏽​Alipofika katikati ya msitu, alikuta duara la mwanga lililokuwa likiwaka bila kuunguza kitu.

Itaendelea......

📌UTANGULIZI​Katika safari ya maisha, binadamu mara nyingi hufanya makosa. Wakati mwingine tunafanya makosa hayo kwa kuju...
17/01/2026

📌UTANGULIZI
​Katika safari ya maisha, binadamu mara nyingi hufanya makosa. Wakati mwingine tunafanya makosa hayo kwa kujua au kwa kutokujua, na mara nyingi tunapoyafanya, huwa tunasahau kabisa k**a tumewahi kuyatenda. Tunapoona hakuna athari ya papo hapo, huwa tunapuuzia na kuamini kuwa hakuna chochote kinachoweza kutokea.

​Hata hivyo, kila kosa lisilorekebishwa mapema lina gharama yake. Gharama ya kusahihisha makosa hayo katika siku za usoni mara nyingi huwa ni kubwa mno, ikisindikizwa na maumivu makali na machozi mengi sana. Hadithi hii ya CHUKIZO inatupa taswira ya kijana Leonard, ambaye baada ya miaka mingi ya mafanikio na starehe, analazimika kulipa gharama nzito kwa makosa ya siri aliyoyafanya wakati wa ujana wake akiwa chuo kikuu.

​Je, kosa la siri linaweza kufutika kwa muda, au litarudi k**a kivuli kumtesa mtendaji? Fuatilia kisa hiki cha kusisimua na chenye mafunzo mazito kuhusu uwajibikaji na matokeo ya maamuzi yetu, katika post inayofuata.

25/12/2025

HADITHI: 🕵️‍♂️ UJUMBE WA SAA 2:17
MTUNZI: GEOFREY DISMAS
SEHEMU: 02

ENDELEA.........

Mwanamke aliyesimama mbele yangu hakutikisa hata kidogo nilipomlenga kwa bastola.
“Shusha silaha,” alisema kwa sauti tulivu.
“Sina nia ya kukuua. Bado.”
Nilimtazama kwa makini.
Alikuwa na alama ndogo ya kovu karibu na jicho la kushoto, alama ya mtu aliyewahi kuona vita halisi.
“Mimi ni Inspector Aisha Kweka,” alisema.
“Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Jinai — CID.”
Jina hilo lilinigonga kichwani.
Nilikuwa nimesikia habari zake: jasusi wa k**e aliyewahi kuongoza operesheni ya siri dhidi ya mtandao wa magendo ya silaha mpakani.
“Mimi ni Daniel Mhando,” nikajibu.
“Afisa wa zamani wa Kitengo Maalum cha Ujasusi (Special Intelligence Unit – SIU).”
Akatabasamu kidogo.
“Nilijua tu.”
Kabla hatujaendelea, milango ya nje ililipuliwa kwa nguvu.
💥 BOOM!
Vipande vya mbao vikapaa hewani.

Taa za dharura zikazimika kabisa.
“WAMEWASILI,” Aisha alisema haraka.
“Kikosi cha Black Fang. Hawako hapa kwa mazungumzo.”
Nilichukua bastola yangu aina ya G***k 19, risasi 9×19mm Parabellum, nikahakikisha magazine ipo sawa.
Aisha akatoa bunduki fupi ya Heckler & Koch MP5, risasi 9mm, silaha ya kimya inayopendwa na vikosi maalum.
Nje, nilisikia sauti nzito ya injini.

Magari mawili ya Toyota Land Cruiser V8, rangi nyeusi, vioo vyeusi—hakuna namba za usajili.
“Wanakuja kwa sababu ya wewe,” Aisha alisema huku akijificha nyuma ya ukuta.
“Ulichokijua miaka mitano iliyopita… bado ni siri hatari.”
Risasi ya kwanza ikapiga ukuta.
PAH!
Vipande vya ukuta vikamwagika.
Nilijibu kwa risasi mbili mfululizo, sio kwa lengo la kuua, bali kuzuia.
Nje, nilimuona mmoja wao:
amevaa mavazi meusi ya kivita, kofia ya chuma, na bunduki aina ya AK-103, risasi 7.62×39mm.

“Hawa si wahuni,” nikasema.
“Hawa ni wanajeshi waliopitia mafunzo.”
“Ndiyo,” Aisha akajibu.
“Ndiyo maana mkuu wako wa zamani, Kamishna Musa Mbele, aliuawa.”
Jina hilo lilinifanya nihisi moto moyoni.
Kamishna Mbele hakuwa tu mkuu wangu, alikuwa mlezi wangu katika ulimwengu wa siri.
“Kuna mtu ndani ya jeshi,” Aisha aliendelea.
“Cheo cha juu. Anawapa taarifa zako zote.
👉 Na anataka ufe leo.”
Gari moja likasimama karibu na mlango.
Mlango wa nyuma ukafunguka.

Mtu mmoja akashuka polepole.
Alivaa suti ya gharama, bila silaha inayoonekana.
Nilimtambua mara moja.
Naibu Kamishna wa Polisi – DCP Victor Nyalandu.
“Daniel,” alisema kwa sauti tulivu.
“Bado unakimbia?”
Hapo ndipo ukweli ukanigonga k**a risasi.

👉 Mtu niliyemwamini zaidi… ndiye aliyekuwa nyuma ya kila kitu.
Aisha akanitazama.
“Chaguo ni lako sasa,” alisema.
“Tuondoke, au ubaki hapa na ukweli wako.”
Risasi nyingine zikaanza kupigwa.
Nilivuta pumzi ndefu.
Nikachagua.

🕵️‍♂️🔥 ITAENDELEA......

HADITHI: 🕵️‍♂️ UJUMBE WA SAA 2:17MWANDISHI: GEOFREY DISMASSEHEMU: 01Saa 2:17 usiku, simu yangu ikatetemeka kwa ukali juu...
24/12/2025

HADITHI: 🕵️‍♂️ UJUMBE WA SAA 2:17
MWANDISHI: GEOFREY DISMAS

SEHEMU: 01

Saa 2:17 usiku, simu yangu ikatetemeka kwa ukali juu ya meza.
Sikutarajia ujumbe wowote kwa saa hiyo. Watu niliowahi kufanya nao kazi walijua kanuni moja: usiwasiliane usiku k**a hakuna hatari.
Nilichukua simu taratibu.
Ujumbe ulikuwa mfupi, bila jina.
“USIWAAMINI. WAKO KARIBU.”
Nilihisi damu ikipanda kichwani.

Maneno hayo hayakuwa ya kawaida. Hayakuwa ya kutishia, lakini yalikuwa na uzito mzito, uzito wa mtu anayejua zaidi yangu.
Nilisimama na kusogea dirishani.
Barabara ilikuwa kimya sana, kimya cha aina ile kinachokufanya usijisikie salama. Hakukuwa na gari, wala mtu. Lakini silika yangu, ile niliyojifunza katika miaka ya kazi za siri, iliniambia ukweli mmoja: sikuwa peke yangu.

Nilimkumbuka mkuu wangu wa zamani, Kapteni Mbele.
Alikuwa akisema mara kwa mara:
“Ujumbe usio na jina ni hatari kuliko risasi. Risasi unaiwona, ujumbe hauuoni.”
Niliporudi mezani, taa zikazimika ghafla.
Giza lilikata kila kitu.
Sekunde chache baadaye, umeme wa dharura ukawaka kwa mwanga hafifu mwekundu.

Ndipo nikasikia sauti ya miguu nje ya mlango wangu.
Ilikuwa polepole, k**a mtu asiye na haraka, au mtu anayejua sitoroki.
TOK… TOK… TOK…
Mlango ukagongwa mara tatu.
Sauti ya kiume ikasema kwa utulivu wa kutisha:
“Fungua. Ni sisi.”
Maneno hayo yalinigandisha.
Katika maisha yangu yote ya kazi za kijasusi, nilikuwa nimefanya kazi na watu wengi, lakini sikuwahi kuwa na timu iliyojiita ‘sisi’.
Nilisogea taratibu hadi kabatini na kufungua droo ya chini. Bastola yangu ilikuwa pale. Nilipoik**ata, moyo wangu ukapiga kwa nguvu zaidi.

Lakini ndipo nikagundua kitu kibaya kuliko vyote.
Simu yangu…
haikuwa tena mkononi mwangu.
Nilitazama meza. Haikuwepo.
Nilitazama sakafuni. Haikuwepo.
Hakukuwa na mtu aliyeingia, lakini simu ilikuwa imetoweka.
Ndipo nikasikia sauti nyingine nyuma yangu, ndani kabisa ya nyumba.
“Ujumbe ulikufikia, sivyo?”
Niligeuka haraka, nikielekeza bastola mbele yangu.

Alikuwa mwanamke. Amevaa koti jeusi, uso wake ukiwa umetulia kupita kiasi.
“Nani wewe?” niliuliza.
Akatabasamu kwa tabasamu dogo lisilo na furaha.
“Jina langu halina umuhimu. Muhimu ni huu ukweli mmoja, kuna mtu unayemwamini…
👉 na ndiye anayekuuza.”
Kabla sijauliza swali lingine, kengele ya hatari ikalia kwenye kichwa changu.
Hii haikuwa tena hadithi ya ujumbe wa ajabu.
Ilikuwa mwanzo wa vita ya siri.
Na saa ilikuwa bado…
2:17 usiku.

😶‍🌫️🔥 ITAENDELEA…








Inaendelea......Polisi walifika ndani ya dakika 30, wakiongozwa na Inspector Mary Christian, mpelelezi wa mkoa wa Arusha...
19/11/2025

Inaendelea......

Polisi walifika ndani ya dakika 30, wakiongozwa na Inspector Mary Christian, mpelelezi wa mkoa wa Arusha. Alitizama eneo la tukio kwa macho makali.

“This isn’t just murder. This is surgical execution.”

Inspector Mary alikuwa ni moja ya maafisa wa askari maridadi na wenye uwezo mkubwa sana katika jeshi la polisi. Alipta mafunzo katika vyuo mbalimbali ndani ya bara la Afrika na hata nje ya nchi. Ni afisa pekee ambaye alipata nafasi ya kufanya kazi kwenye idara ya polisi ya mji wa Los Angel (LAPD). 

 

UKWELI ULIOJIFICHA

Katika uchunguzi wa uliofanyanyika, hakukua na alama za kuvunjwa kwa mlango

Kamera za CCTV zilitumiwa kifaa cha “blackout EMP”,  “hakuna rekodi yoyote, hawa washenzi walikuwa wamejipanga.” Alijisemea Inspector Mary.

Rehema alikuwa ameanza kuchunguza dawa mpya ya sumu ya silaha za kijeshi. Awali uchunguzi huu ulipingwa na wataalamu wengine kutoka nje ya nchi lakini serikali ya Tanzania walijidhatiti kuhakikisha mpango huo muhimubunaendelea.

Jambo la ajabu zaidi, faili lote la utafiti wa Rehema lilikuwa limefutwa kutoka kwenye kompyuta na backups zilikuwa zimeharibiwa kimfumo.

***

Njiro, Arusha – saa 12:00 jioni

Mvua iliacha kunyesha. Inspector Mary alisimama mbele ya mwili wa Rehema.

“We're dealing with professionals. Cold-blooded killers,” alisema kwa sauti ya chini.

Kilichosalia ni maswali zaidi ya majibu.

 

 KIVULI CHA ZAMANI – DAR ES SALAAM

 

Dar es Salaam – Makao Makuu ya Polisi – Saa 3:11 asubuhi

Kamanda Nasoro Mtei aliingia ofisini akiwa amechelewa kwa dakika tano. Si kawaida yake. Alikuwa mtu wa muda, mwenye mazoea ya kijeshi tangu enzi zake Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kambi ya Ruvu. Lakini leo hakuamka mapema. Ndoto ya usiku iliyomhusu mkewe aliyefariki miaka mitatu iliyopita bado ilimzidi nguvu. Alijikuta amekaa kitandani kwa dakika 20 akitafakari maisha.

Ofisi yake ilikuwa imepangwa kwa ustadi. Ubao wa whiteboard ulioandikwa kwa maandishi mekundu na meusi ya uchunguzi wa utekaji wa mwaka jana bado ulikuwepo.

Inaendelea Kwenye Channel yetu gusa Link kwa Bio

Address

Magegele
Makambako
59122

Telephone

+255768465103

Website

https://podcasters.spotify.com/pod/show/hadithizetu, https://www.selar.co/m/hadithiz

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hadithi Zetu:

Share