Hadithi Zetu

Hadithi Zetu Kila simulizi ina funzo, na kila hadithi ina maana. 🕯🖀
Hadithi Zetu inakuletea visa vinavyoakisi maisha yetu ya kila siku, huzuni, furaha na ushindi.
(7)

Karibu tushiriki simulizi zitakazokuburudisha na kukuza fikra zako. 🧠🌹
​Karibu kwenye familia! 🀝 Hadithi Zetu ni ukurasa wa Facebook ambao una lengo la kuchapisha kazi za fasihi andishi, simulizi, na makala mbalimbali. Ukurasa huu umeundwa ili kuhuisha na kueneza urithi wa hadithi na tamaduni za Kiafrika kupitia njia ya maandishi. Tunajitahidi kuwa jukwaa la kuelimisha, kuburudisha, na kuhamasisha

wengine kwa njia ya hadithi. Kwenye ukurasa wetu, utapata aina mbalimbali za kazi za fasihi andishi, ikiwa ni pamoja na hadithi za kusisimua, mashairi, riwaya fupi, na tamthilia. Tunajitahidi kuchapisha kazi zenye ubora na zinazogusa masuala mbalimbali yanayohusiana na jamii, utamaduni, upendo, mazingira, na masuala mengine ya kijamii. Mbali na kazi za fasihi andishi, tunatoa pia simulizi mbalimbali za kuvutia. Hizi ni hadithi za kusisimua, za kuburudisha, na zenye kuelimisha. Simulizi zetu zinaweza kuwa za kisasa au za jadi, zinazohusisha wahusika wenye maisha ya kuvutia na matukio ya kusisimua. Lengo letu ni kutoa burudani na kuwafanya wasomaji wetu kujisikia kushiriki katika ulimwengu wa hadithi. Pia, tunatoa makala mbalimbali kwenye ukurasa wetu. Makala hizi zinajadili mada mbalimbali za kijamii, utamaduni, sanaa, na masuala mengine yanayohusiana na fasihi na simulizi. Tunazingatia kutoa taarifa sahihi na za kuvutia ili kuhamasisha majadiliano na kuelimisha wasomaji wetu. Tunakaribisha wanachama wote wa jamii kuungana nasi kwenye ukurasa wetu wa Facebook, Hadithi Zetu. Tunahimiza ushiriki wa wadau wa fasihi, waandishi, wasomaji, na wapenda hadithi katika kuchangia kazi zao, kutoa maoni, na kushiriki maarifa na uzoefu wao. Tunatumai kuwa Hadithi Zetu itakuwa sehemu ambayo itawawezesha watu kugundua, kuelimika, na kufurahia upekee wa hadithi za Kiafrika na tamaduni zetu. Karibu sana kujiunga na jumuiya yetu na kushiriki katika uumbaji wa hadithi za kuvutia na za kuelimisha.

📌𝐌𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐃𝐀𝐌𝐔 𝐁𝐲 𝐆𝐞𝐚𝐟𝐫𝐞𝐲 𝐃𝐢𝐬𝐊𝐚𝐬"𝑵𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒋𝒖𝒎𝒃𝒂 𝒌𝒖𝒃𝒘𝒂 𝒘𝒂𝒕𝒐𝒕𝒐 𝒘𝒂𝒍𝒊𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒍𝒂 𝒌𝒊𝒇𝒂𝒉𝒂𝒓𝒊 𝒍𝒊𝒍𝒊𝒍𝒐𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒆𝒏𝒆𝒐 𝒍𝒂 𝑎𝒂𝒔𝒂𝒌𝒊...𝑎𝒖𝒛𝒊𝒌𝒊 𝒍𝒂𝒊𝒏𝒊...
10/07/2026

📌𝐌𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐃𝐀𝐌𝐔 𝐁𝐲 𝐆𝐞𝐚𝐟𝐫𝐞𝐲 𝐃𝐢𝐬𝐊𝐚𝐬

"𝑵𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒋𝒖𝒎𝒃𝒂 𝒌𝒖𝒃𝒘𝒂 𝒘𝒂𝒕𝒐𝒕𝒐 𝒘𝒂𝒍𝒊𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒍𝒂 𝒌𝒊𝒇𝒂𝒉𝒂𝒓𝒊 𝒍𝒊𝒍𝒊𝒍𝒐𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒆𝒏𝒆𝒐 𝒍𝒂 𝑎𝒂𝒔𝒂𝒌𝒊...
𝑎𝒖𝒛𝒊𝒌𝒊 𝒍𝒂𝒊𝒏𝒊 𝒖𝒍𝒊𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒖𝒌𝒊𝒔𝒊𝒌𝒊𝒌𝒂...
𝑟𝒂𝒍𝒊𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒘𝒂𝒏𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂 𝒏𝒂 𝑩𝒊𝒓𝒕𝒉𝒅𝒂𝒚 𝑷𝒂𝒓𝒕𝒚 𝒚𝒂 𝒎𝒕𝒐𝒕𝒐 𝒘𝒂 𝑎𝒇𝒂𝒏𝒚𝒂𝒃𝒊𝒂𝒔𝒉𝒂𝒓𝒂 𝒎𝒂𝒂𝒓𝒖𝒇𝒖, 𝑎𝒛𝒆𝒆 𝑲𝒊𝒃𝒘𝒂𝒏𝒂.
𝑟𝒂𝒈𝒆𝒏𝒊 𝒘𝒂𝒍𝒊𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒘𝒂𝒌𝒊𝒄𝒉𝒆𝒌𝒂, 𝒌𝒖𝒍𝒂 𝒏𝒂 𝒌𝒖𝒏𝒚𝒘𝒂.
𝑟𝒂𝒕𝒐𝒕𝒐 𝒘𝒂𝒍𝒊𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒘𝒂𝒌𝒊𝒌𝒊𝒎𝒃𝒊𝒂 𝒉𝒖𝒌𝒖 𝒏𝒂 𝒌𝒖𝒍𝒆.

𝑯𝒂𝒌𝒖𝒏𝒂 𝒂𝒍𝒊𝒚𝒆𝒌𝒖𝒘𝒂 𝒂𝒌𝒊𝒋𝒖𝒂 𝒌𝒘𝒂𝒏𝒗𝒂 𝒏𝒅𝒂𝒏𝒊 𝒚𝒂 𝒅𝒂𝒌𝒊𝒌𝒂 𝒄𝒉𝒂𝒄𝒉𝒆..."

𝗣𝗮𝘁𝗮 𝗚𝗵𝗌𝗻𝗱𝗌 𝗵𝘂𝘂 𝗞𝘄𝗮 𝗞𝘂𝗜𝗮𝗞𝘂𝗮 𝗵𝗮𝗜𝗮 ➡ https://selar.com/m/hadithizetu 𝗞𝘄𝗮 𝗊𝗵𝗶𝗹𝗶𝗻𝗎𝗶 2,500/= 𝗧𝘂.






















❀💞❀



𝗠𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗗𝗔𝗠𝗚            𝗊𝗘𝗔𝗊𝗢𝗡 01𝗕𝗬 𝘎𝘌𝘖𝘍𝘙𝘌𝘠 𝘋𝘐𝘚𝘔𝘈𝘚𝐊ila jiji lina siri zake, na nyuma ya magorofa marefu, fukwe za kuvutia...
07/07/2026

𝗠𝗝𝗜 𝗪𝗔 𝗗𝗔𝗠𝗚
𝗊𝗘𝗔𝗊𝗢𝗡 01
𝗕𝗬 𝘎𝘌𝘖𝘍𝘙𝘌𝘠 𝘋𝘐𝘚𝘔𝘈𝘚

𝐊ila jiji lina siri zake, na nyuma ya magorofa marefu, fukwe za kuvutia, na tabasamu za watu wenye nguvu ndani ya jiji la Dar es Salaam, kuna upande wa giza ambao wengi wanaogopa hata kuunong'ona. Upande huo ndio unaofunguliwa katika riwaya hii ya Mji wa Damu (Season 1).

​𝐊azi hii ya fasihi ya kijasusi na ya kusisimua (thriller/suspense) si tu hadithi ya kufikirika, bali ni kioo kinachoangazia jinsi tamaa ya madaraka, ushirikina wa siri, na usaliti unavyoweza kuwagharimu watu wasio na hatia. Kupitia mhusika mkuu, Inspector Daniel Malisa, msomaji anapelekwa kwenye safari ya kisaikolojia na mapambano ya hali ya juu ya kuutafuta ukweli uliogubikwa na damu na mifumo hatari.

​𝐌tunzi Geofrey Dismas amefanikiwa kwa ustadi mkubwa kuchora mandhari ya dhoruba, dhoruba ambazo hazipo angani tu bali pia ndani ya mioyo ya wahusika. Kila episode imesukwa kwa njia inayomfanya msomaji kuwa sehemu ya upelelezi huo, akiumiza kichwa kuunganisha doti za alama ya kifo na faili za zamani zilizofungwa kwa siri.

​𝐑iwaya hii inafaa kwa wapenzi wote wa hadithi za kusisimua, upelelezi, na michezo ya akili (mind games). Unapoanza kusoma ukurasa wa kwanza, jiandae kukata pumzi mpaka utakapofika neno la mwisho la msimu huu wa kwanza.
​Karibu kwenye mchezo, na uwe tayari kuona siri za zamani zikifufuka.

𝑷𝒂𝒌𝒖𝒂 𝒉𝒂𝒅𝒊𝒕𝒉𝒊 𝒉𝒊𝒊 𝒚𝒂 𝒌𝒖𝒔𝒊𝒔𝒊𝒎𝒖𝒂 𝒉𝒂𝒑𝒂 https://selar.com/m/hadithizetu 𝒌𝒘𝒂 𝒃𝒆𝒊 𝒚𝒂 𝑻𝒔𝒉𝒔 2,500/= ✹






















❀💞❀



LEO NI SIKU YA KIPEKEE KWANGU. 🙏🎉Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia zawadi ya uhai na kunifikisha siku hii ya kuz...
27/06/2026

LEO NI SIKU YA KIPEKEE KWANGU. 🙏🎉

Ninamshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia zawadi ya uhai na kunifikisha siku hii ya kuzaliwa. Neema zake zimekuwa nyingi kuliko ninavyoweza kuhesabu.

Ninamshukuru baba yangu pamoja na kumkumbuka kwa heshima na upendo mama yangu mpendwa ambaye sasa ni marehemu. Ingawa hayupo nasi kimwili, mchango wake, malezi yake na upendo wake vitaendelea kuishi moyoni mwangu milele. Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi. 🀍🕊

Ninaanza mwaka mpya wa maisha yangu nikiwa na imani, matumaini na moyo wa shukrani. Naomba Mungu aniongoze, anipe afya njema, hekima, amani na afungue milango ya mafanikio katika kila hatua ya maisha yangu.
Happy Birthday to me! 🎂🥳🎉

📌𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇📌𝐓𝐀𝐑𝐄𝐇𝐄  27 𝐉𝐔𝐍𝐄 2026 ❀💞❀
14/06/2026

📌𝐖𝐀𝐏𝐄𝐍𝐙𝐈 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈
⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇⬇
📌𝐓𝐀𝐑𝐄𝐇𝐄 27 𝐉𝐔𝐍𝐄 2026

❀💞❀



















𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: MJI WA DAMU 𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney 𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄: 05 (KANISA LA GIZA)𝑬𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂......Asubuhi ndani ya Dar es Sal...
10/06/2026

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: MJI WA DAMU
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄: 05 (KANISA LA GIZA)

𝑬𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂......

Asubuhi ndani ya Dar es Salaam ilikuwa nzito.

Mawingu meusi yalikuwa bado yametanda angani kana kwamba mji mzima ulikuwa umebeba laana isiyoonekana.

Inspector Daniel Malisa alikuwa bado amesimama sebuleni mwa mama yake.

Macho yake yalikuwa yamemkazia mwanamke huyo aliyekuwa akitetemeka mikono.

Kwa miaka yote
hakuwahi kumuona mama yake akiwa na hofu kiasi kile.
“Unamaanisha nini kusema Pastor Gideon alikuwa na siri na baba?” Malisa aliuliza kwa sauti nzito.
Mama yake akafuta machozi.
“Daniel
 baba yako alikuwa mtu mzuri.”
“Lakini?”
Alinyamaza.
Kisha akaenda taratibu mpaka kwenye kabati la zamani lililokuwa kona ya sebule.
Akafungua drawer ndogo.

Ndani kulikuwa na sanduku jeusi lililoonekana kuchakaa kwa miaka.
Mikono yake ilikuwa inatetemeka alipolitoa.
“Baba yako aliacha hili kabla hajafa.”
Malisa akalisogelea haraka.
“Mama
 kwa nini hujawahi kuniambia?”
“Nilikuwa naogopa.”
“Anaogopa nini?”
Mwanamke huyo akamwangalia moja kwa moja machoni.
“Kifo.”
Kimya kizito kikaingia.

Malisa akafungua lile sanduku polepole.
Ndani kulikuwa na:
picha za zamani,
documents,
flash ndogo,
na karatasi moja iliyokuwa imeandikwa kwa mkono.
Malisa akaichukua.
Maandishi yalikuwa ya baba yake.
“Kama unasoma ujumbe huu
 ina maana nimekufa. Usimwamini Pastor Gideon.”
Moyo wa Malisa ukapiga kwa nguvu.

Akaendelea kusoma.
“Tuligundua biashara kubwa ya watu wenye nguvu. Watu wanauawa, wanatoweka, na miili yao kutumika kwa mambo ya kutisha.”
Malisa akakunja uso.
Mama yake akaanza kulia kimya kimya.
“Tulijaribu kuwafichua
 lakini mmoja wetu alitusaliti.”
Malisa akainua macho taratibu.
“Ni nani aliyemsaliti?”
Mama yake akatikisa kichwa.
“Sikuwahi kujua
”
Lakini kabla hawajaendelea—
Ghafla nje ya nyumba

BREKI kali za gari zikasikika.

SKREEECH!

Malisa akageuka haraka dirishani.
Gari jeusi aina ya Prado lilikuwa limesimama nje ya geti.
Milango ikafunguliwa.
Wanaume wawili wenye silaha wakashuka.
“CHINI!” Malisa alipaza sauti.
BANG!
Risasi zikaanza kupasua vioo vya nyumba.
Mama yake akapiga kelele.
Malisa akamvuta chini haraka huku akitoa bastola yake.

BANG!
BANG!

Akajibu mashambulizi.
Mmoja wa washambuliaji akaanguka.
Lakini mwingine akaendelea kufyatua risasi kuelekea ndani.
Sebule ikaanza kusambaratika.
Vipande vya vioo vikawa vinaruka kila upande.
“Mama kaa chini!” Malisa alipaza sauti.
Kisha akaanza kutambaa mpaka dirishani.
Akamwona mshambuliaji wa pili akijaribu kuingia getini.
Malisa akavuta pumzi

aka-target.

BANG!

Mwanaume huyo akaanguka chini.
Kimya.

Harufu ya baruti ikajaa hewani.
Malisa akatoka nje haraka akiwa bado ameshika bastola.
Lakini kabla hajamfikia mmoja wa wale wanaume—
gari lingine likatokea ghafla.
Wale washambuliaji waliobaki wakabebwa na kutoroka kwa kasi.
“Damn it!”
Malisa akakanyaga kwa hasira.

Kisha akarudi ndani haraka.
“Mama uko sawa?”
Lakini

sebule ilikuwa kimya.
“Mama?”
Hakuna jibu.
Moyo wake ukaanza kwenda mbio.
Alikimbia mpaka jikoni.
Hakuna mtu.
Chumbani.
Hakuna.

Mlango wa nyuma ulikuwa wazi.

Na sakafuni

kulikuwa na simu ya mama yake ikiwa imevunjika.
Macho ya Malisa yakabadilika ghafla.
“Hapana
”
Walikuwa wamemteka.
Saa moja baadaye

ndani ya kituo maalum cha polisi.

Askari Peter alikuwa mbele ya screen kubwa akifuatilia camera za barabarani.

“Tulipoteza Prado pale Morocco,” alisema kwa hasira.
Malisa alikuwa amesimama nyuma yake akiwa kimya kabisa.
Uso wake ulikuwa umejaa hasira ambazo Peter hakuwahi kuziona kabla.
“Chief
”
“Hii si kazi tena,” Malisa alisema kwa sauti nzito.
“Hii imekuwa vita.”
Ghafla simu ikaingia.

UNKNOWN NUMBER.

Peter akamtazama.
Malisa akapokea polepole.
Sauti nzito ile ile ikasikika.
“Unaanza kuelewa maumivu sasa?”
“Uko wapi?” Malisa alisema kwa hasira.
“Kama unamtaka mama yako akiwa hai
”
Kimya kidogo.
“Acha kumfuata Pastor Gideon.”
“Ukimgusa mama yangu—”
“Utaua kila kitu.”

CLICK.

Simu ikakatwa.

Malisa akakaza ngumi mpaka mishipa ikasimama.
Peter akamwangalia.
“Ni wao?”
Malisa akatikisa kichwa.
Kisha akasema maneno yaliyomfanya Peter anyamaze:
“Nataka taarifa zote za Pastor Gideon. Zote.”
Usiku huo

kanisa la Pastor Gideon lilikuwa tulivu.

Waumini walikuwa wameondoka.
Mishumaa michache ilikuwa bado inawaka.
Lakini chini ya kanisa

ndani ya chumba cha siri

hali ilikuwa tofauti kabisa.
Mama wa Malisa alikuwa amefungwa kwenye kiti.
Uso wake ulikuwa umejaa hofu.
Mbele yake


Pastor Gideon alikuwa amesimama akiwa amevaa suti nyeusi.
Hakukuwa tena na tabasamu la upole la kichungaji.
Macho yake yalikuwa ya baridi.
“Nilikuambia zamani ukae kimya,” alisema polepole.
Mama wa Malisa akalia.
“Daniel hakuhusika
”
Pastor akacheka kidogo.

“Kosa la baba yake sasa linafufuka.”
Kisha akaenda mpaka ukutani.
Akasukuma sehemu ya mbao iliyofunguka taratibu.
Na nyuma yake

kulikuwa na chumba kingine.
Chumba kilichojaa alama za damu ukutani.
Mishumaa.

Picha za watu waliokufa.
Na katikati ya sakafu

ile alama ya duara kubwa.
Mama wa Malisa akaanza kutetemeka.
“Mungu wangu
”
Pastor Gideon akamwangalia taratibu.
“Watu wengi wanafikiri uchawi ni hadithi.”
Akatabasamu.

“Kumbe ni biashara kubwa kuliko zote duniani.”
Wakati huohuo

Inspector Malisa alikuwa njiani kuelekea kanisani.
Mvua ilikuwa inaanza tena.
Lakini hakujua

kwamba ndani ya gari lake

chini kabisa ya seat

kulikuwa na bomu dogo lililowashwa tayari.
Na timer yake

ilikuwa imebaki dakika tatu.
---------------

𝑻𝒖𝒏𝒂𝒌𝒐𝒎𝒆𝒂 𝒉𝒂𝒑𝒐 𝒍𝒂𝒌𝒊𝒏𝒊 𝒌𝒂𝒂 𝒎𝒌𝒂𝒐 𝒘𝒂 𝒌𝒖𝒍𝒂 𝒌𝒘𝒂𝒏𝒊 𝐒1-𝐒5 𝑰𝒕𝒂𝒌𝒖𝒋𝒊𝒂 𝒉𝒊𝒗𝒊 𝒌𝒂𝒓𝒊𝒃𝒖𝒏𝒊 𝒌𝒘𝒆𝒏𝒚𝒆 𝒅𝒖𝒌𝒂 𝒍𝒆𝒕𝒖 𝒍𝒂 𝑎𝒕𝒂𝒏𝒅𝒂𝒐𝒏𝒊.






















❀💞❀



𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈:𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈:𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄: 04𝑬𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂........Ndani ya Dar es Salaam
usiku ulikuwa mzito kuliko kawaida.Mvua ilikuwa imepungu...
09/06/2026

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈:
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈:
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄: 04

𝑬𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂........

Ndani ya Dar es Salaam

usiku ulikuwa mzito kuliko kawaida.
Mvua ilikuwa imepungua

lakini anga lilikuwa bado limefunikwa na mawingu meusi yaliyofanya mji mzima uonekane k**a unaelekea kuzimu.

Ndani ya apartment yake

Inspector Daniel Malisa alikuwa bado amesimama katikati ya sebule akiwa ameishikilia simu mkononi.

Maneno yale yaliendelea kumzunguka kichwani mwake.
“Muulize mama yako kuhusu usiku ambao baba yako alikufa.”
Alimeza mate polepole.
Kwa miaka yote

hakuwahi kuhoji sana kuhusu kifo cha baba yake.
Aliaminishwa kuwa ilikuwa ajali ya kikazi.
Na mama yake

hakupenda kabisa kuzungumzia jambo hilo.
Lakini sasa

kila kitu kilianza kubadilika.
Ghafla

sauti ndogo ikasikika nje ya mlango.
TIK.
Malisa akainua macho haraka.
Mwili wake wote ukawa alert.
Taribu

akaingiza mkono kwenye koti lake na kutoa bastola.

Kimya.

Kisha


TIK nyingine.
Safari hii karibu zaidi.
Malisa akaanza kutembea kuelekea mlangoni taratibu sana.
Macho yake yakawa makali.
Aliusogelea mlango kwa tahadhari

akaangalia kupitia tundu la mlango.

Hakuna mtu.
Lakini sekunde ile ile,
BANG!
Risasi ikapenya ukutani.
Malisa akajirusha chini haraka.
Kioo kikapasuka vipande.
BANG!
BANG!
BANG!
Risasi nyingine zikaanza kuingia ndani ya apartment.
“Sh*t!”
Malisa akajiviringisha nyuma ya sofa huku akijibu mashambulizi.

BANG!

Ukumbi mzima ukajaa harufu ya baruti.
Nje ya mlango

mwanaume aliyevaa hoodie nyeusi alikuwa amesimama akiwa ameshikilia bastola yenye suppressor.
Uso wake ulikuwa umefunikwa.
Alifyatua risasi nyingine mbili

kisha akaanza kuvunja mlango kwa teke.
BAM!
Mlango ukafunguka kwa nguvu.
Mwanaume huyo akaingia ndani haraka

lakini apartment ilikuwa kimya.
Akatembea taratibu huku bastola yake ikiwa mbele.
Macho yake yakizunguka kila kona.

Ghafla!

Malisa akaruka kutoka pembeni.
Wakagongana kwa nguvu.
Bastola ikaanguka sakafuni.
Wanaume hao wawili wakaanza kupigana kwa hasira.
Ngumi nzito zilianza kutua.
Mwanaume huyo alikuwa na nguvu sana.
Alimpiga Malisa tumboni mpaka akagonga meza ya kioo.

CRASH!

Vipande vya vioo vikatapakaa.
Lakini Malisa akainuka haraka.
Akamshika mshambuliaji shingo

akamgonga ukutani.
Kwa sekunde chache

hoodie yake ikateleza kidogo.
Na hapo

Malisa akaona kitu.
Alama ile ile ya duara na mistari mitatu

ikiwa imechorwa shingoni mwa mwanaume huyo.
Macho ya Malisa yakabadilika.

“Wewe ni nani?!”
Mwanaume huyo akacheka kwa sauti nzito.
“Ukweli una gharama, Inspector.”
Ghafla akatoa kisu kidogo

akamkata Malisa begani.
“Aaaagh!”
Malisa akaachia.
Na kabla hajajipanga—
mshambuliaji akaruka dirishani.
CRASH!

Akatoweka gizani.
Malisa akakimbia mpaka dirishani huku damu ikimtoka begani

lakini tayari gari jeusi lilikuwa linaondoka kwa kasi barabarani.
Akabaki akihema kwa nguvu.
Kisha macho yake yakatua kwenye kitu kilichoachwa sakafuni.
Pendant ile ile ya alama ya siri.
Safari hii
ikiwa na damu mpya.

Saa moja baadaye

hospitali ya Aga Khan.
Doctor alikuwa anashona jeraha la Malisa begani.
“Una bahati risasi haikukupata vizuri,” alisema.
Malisa alikuwa kimya.
Akili yake ilikuwa mbali.
Askari Peter alikuwa pembeni.
“Chief
 hii si kawaida tena.”

Malisa akamtazama.

“Hakuna kitu kawaida kwenye kesi hii.”
Peter akavuta pumzi.
“Kuna jambo niligundua
”
“Nini?”
“Gari lile lililotoroka kutoka hospitali
”
Malisa akaangalia juu.
“Tulilifuatilia kwa camera za barabarani.”
“Likafika wapi?”
Peter akasita kidogo.
“Kanisani kwa Pastor Gideon.”
Kimya kizito kikaingia mle chumbani.
Malisa akakaza taya.
“Una uhakika?”
“100%.”
Wakati huohuo

ndani ya kanisa la Pastor Gideon.
Mishumaa ilikuwa ikiwaka ndani ya chumba cha siri kilichokuwa chini ya jengo hilo.

Ukuta ulikuwa umechorwa alama zile zile za duara la damu.
Na katikati ya chumba

kulikuwa na meza kubwa ya mbao iliyozungukwa na watu watano waliovaa mavazi meusi.
Pastor Gideon alikuwa amesimama mbele yao.
Uso wake ulikuwa mzito.
“Inspector Malisa ameanza kusogea karibu sana,” alisema.
Mwanaume mmoja akasema: “Tumuue.”
Pastor akatikisa kichwa polepole.
“Hapana.”
“Kwa nini?”
“Kuna kitu bado hajui.”
Pastor akatembea kuelekea ukutani ambapo kulikuwa na picha ya zamani.

Picha ya watu watatu.
Baba wa Malisa.
Mzee Kibwana.
Na Pastor Gideon mwenyewe.

Pastor akaigusa picha ile taratibu.
“Daniel akijua ukweli wote mapema
 kila kitu kitaanguka.”
Mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa pazia jeusi akauliza:
“Na mtoto wa Kibwana?”
Pastor akafumba macho kwa sekunde chache.
“Bado ni muhimu.”
“Kwa ajili ya kafara?”
Kimya.
Hakuna aliyesema kitu.
Lakini jibu lilikuwa tayari limeeleweka.
Asubuhi iliyofuata


Malisa alisimamisha gari lake mbele ya nyumba ya mama yake eneo la Mikocheni.
Ilikuwa nyumba ya zamani aliyokulia.
Alihisi moyo wake ukipiga kwa nguvu aliposhuka.
Kwa miaka mingi

hakuwahi kuja hapo kuzungumzia kifo cha baba yake.
Lakini leo ilikuwa tofauti.

Aligonga mlango.

Mama yake akafungua.

“Mwanangu
”
Lakini tabasamu lake likapotea alipoliona jeraha begani mwa Malisa.
“Kuna nini Daniel?!”
Malisa akaingia ndani polepole.
“Mama
”
Sauti yake ilikuwa nzito.

“Nataka uniambie ukweli kuhusu baba.”
Uso wa mama yake ukabadilika ghafla.
“Daniel
”
“Usinifiche tena.”
Mama yake akaanza kutetemeka.
“Mambo mengine ni bora yabaki yamezikwa.”
“HAPANA!”
Malisa alipaza sauti kwa hasira.
“Watu wanakufa mama!”
Kimya.
Machozi yakaanza kujikusanya machoni mwa mwanamke huyo.
Kisha akaongea kwa sauti ya chini sana.
“Baba yako
 alikuwa karibu kuwafichua watu wenye nguvu.”
Malisa akasogea karibu.
“Akina nani?”

Mama yake akameza mate.
Kisha akasema maneno yaliyomgandisha damu kabisa,
“Pastor Gideon alikuwa rafiki mkubwa wa baba yako
”
“Alichomuua ni siri waliyoificha pamoja.”
Kimya kikazidi ndani ya nyumba.
Na kwa mara nyingine tena


jina la Pastor Gideon likarudi katikati ya jinamizi hilo.
Lakini Malisa bado hakujua

kwamba nje ya nyumba hiyo

kulikuwa na mtu aliyekuwa amewaangalia kupitia gari jeusi.
Na kwenye simu yake

kulikuwa na picha ya mama wa Malisa.
Kisha sauti nzito ikasema:
“Safari hii
 tutaumiza kile anachokipenda.”

𝑰𝒕𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂.......






















❀💞❀



07/06/2026

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: MJI WA DAMU
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney
𝐄𝐏𝐈𝐒𝐎𝐃𝐄: 04

Endelea....

Ndani ya Dar es Salaam

usiku ulikuwa mzito kuliko kawaida.
Mvua ilikuwa imepungua

lakini anga lilikuwa bado limefunikwa na mawingu meusi yaliyofanya mji mzima uonekane k**a unaelekea kuzimu.
Ndani ya apartment yake

Inspector Daniel Malisa alikuwa bado amesimama katikati ya sebule akiwa ameishikilia simu mkononi.
Maneno yale yaliendelea kumzunguka kichwani mwake.
“Muulize mama yako kuhusu usiku ambao baba yako alikufa.”
Alimeza mate polepole.

Kwa miaka yote

hakuwahi kuhoji sana kuhusu kifo cha baba yake.
Aliaminishwa kuwa ilikuwa ajali ya kikazi.
Na mama yake

hakupenda kabisa kuzungumzia jambo hilo.
Lakini sasa

kila kitu kilianza kubadilika.
Ghafla

sauti ndogo ikasikika nje ya mlango.
TIK.
Malisa akainua macho haraka.

Mwili wake wote ukawa alert.

Taribu
 akaingiza mkono kwenye koti lake na kutoa bastola.

Kimya.

Kisha


TIK nyingine.

Safari hii karibu zaidi.
Malisa akaanza kutembea kuelekea mlangoni taratibu sana.
Macho yake yakawa makali.
Aliusogelea mlango kwa tahadhari

akaangalia kupitia tundu la mlango.
Hakuna mtu.
Lakini sekunde ile ile—
BANG!
Risasi ikapenya ukutani.
Malisa akajirusha chini haraka.

Kioo kikapasuka vipande.
BANG!
BANG!
BANG!
Risasi nyingine zikaanza kuingia ndani ya apartment.
“Sh*t!”
Malisa akajiviringisha nyuma ya sofa huku akijibu mashambulizi.

BANG!

Ukumbi mzima ukajaa harufu ya baruti.
Nje ya mlango

mwanaume aliyevaa hoodie nyeusi alikuwa amesimama akiwa ameshikilia bastola yenye suppressor.
Uso wake ulikuwa umefunikwa.
Alifyatua risasi nyingine mbili

kisha akaanza kuvunja mlango kwa teke.

BAM!

Mlango ukafunguka kwa nguvu.
Mwanaume huyo akaingia ndani haraka

lakini apartment ilikuwa kimya.
Akatembea taratibu huku bastola yake ikiwa mbele.
Macho yake yakizunguka kila kona.
Ghafla—Malisa akaruka kutoka pembeni.
Wakagongana kwa nguvu.
Bastola ikaanguka sakafuni.
Wanaume hao wawili wakaanza kupigana kwa hasira.
Ngumi nzito zilianza kutua.
Mwanaume huyo alikuwa na nguvu sana.
Alimpiga Malisa tumboni mpaka akagonga meza ya kioo.

CRASH!

Vipande vya vioo vikatapakaa.
Lakini Malisa akainuka haraka.
Akamshika mshambuliaji shingo

akamgonga ukutani.
Kwa sekunde chache

hoodie yake ikateleza kidogo.
Na hapo

Malisa akaona kitu.
Alama ile ile ya duara na mistari mitatu

ikiwa imechorwa shingoni mwa mwanaume huyo.

Macho ya Malisa yakabadilika.
“Wewe ni nani?!”
Mwanaume huyo akacheka kwa sauti nzito.
“Ukweli una gharama, Inspector.”
Ghafla akatoa kisu kidogo

akamkata Malisa begani.
“Aaaagh!”
Malisa akaachia.
Na kabla hajajipanga—
mshambuliaji akaruka dirishani.
CRASH!
Akatoweka gizani.

Malisa akakimbia mpaka dirishani huku damu ikimtoka begani

lakini tayari gari jeusi lilikuwa linaondoka kwa kasi barabarani.
Akabaki akihema kwa nguvu.
Kisha macho yake yakatua kwenye kitu kilichoachwa sakafuni.
Pendant ile ile ya alama ya siri.
Safari hii

ikiwa na damu mpya.

Saa moja baadaye

hospitali ya Aga Khan.
Doctor alikuwa anashona jeraha la Malisa begani.
“Una bahati risasi haikukupata vizuri,” alisema.
Malisa alikuwa kimya.
Akili yake ilikuwa mbali.
Askari Peter alikuwa pembeni.
“Chief
 hii si kawaida tena.”
Malisa akamtazama.
“Hakuna kitu kawaida kwenye kesi hii.”
Peter akavuta pumzi.
“Kuna jambo niligundua
”
“Nini?”

“Gari lile lililotoroka kutoka hospitali
”
Malisa akaangalia juu.
“Tulilifuatilia kwa camera za barabarani.”
“Likafika wapi?”
Peter akasita kidogo.
“Kanisani kwa Pastor Gideon.”
Kimya kizito kikaingia mle chumbani.
Malisa akakaza taya.
“Una uhakika?”
“100%.”
Wakati huohuo

ndani ya kanisa la Pastor Gideon.

Mishumaa ilikuwa ikiwaka ndani ya chumba cha siri kilichokuwa chini ya jengo hilo.
Ukuta ulikuwa umechorwa alama zile zile za duara la damu.
Na katikati ya chumba

kulikuwa na meza kubwa ya mbao iliyozungukwa na watu watano waliovaa mavazi meusi.
Pastor Gideon alikuwa amesimama mbele yao.
Uso wake ulikuwa mzito.
“Inspector Malisa ameanza kusogea karibu sana,” alisema.
Mwanaume mmoja akasema: “Tumuue.”
Pastor akatikisa kichwa polepole.
“Hapana.”
“Kwa nini?”
“Kuna kitu bado hajui.”
Pastor akatembea kuelekea ukutani ambapo kulikuwa na picha ya zamani.

Picha ya watu watatu.
Baba wa Malisa.
Mzee Kibwana.
Na Pastor Gideon mwenyewe.
Pastor akaigusa picha ile taratibu.
“Daniel akijua ukweli wote mapema
 kila kitu kitaanguka.”
Mwanamke mmoja aliyekuwa amevaa pazia jeusi akauliza:
“Na mtoto wa Kibwana?”
Pastor akafumba macho kwa sekunde chache.
“Bado ni muhimu.”
“Kwa ajili ya kafara?”
Kimya.

Hakuna aliyesema kitu.
Lakini jibu lilikuwa tayari limeeleweka.
Asubuhi iliyofuata

Malisa alisimamisha gari lake mbele ya nyumba ya mama yake eneo la Mikocheni.
Ilikuwa nyumba ya zamani aliyokulia.
Alihisi moyo wake ukipiga kwa nguvu aliposhuka.
Kwa miaka mingi

hakuwahi kuja hapo kuzungumzia kifo cha baba yake.
Lakini leo ilikuwa tofauti.
Aligonga mlango.

Mama yake akafungua.
“Mwanangu
”
Lakini tabasamu lake likapotea alipoliona jeraha begani mwa Malisa.
“Kuna nini Daniel?!”
Malisa akaingia ndani polepole.
“Mama
”
Sauti yake ilikuwa nzito.
“Nataka uniambie ukweli kuhusu baba.”
Uso wa mama yake ukabadilika ghafla.
“Daniel
”
“Usinifiche tena.”
Mama yake akaanza kutetemeka.
“Mambo mengine ni bora yabaki yamezikwa.”
“HAPANA!”

Malisa alipaza sauti kwa hasira.

“Watu wanakufa mama!”
Kimya.
Machozi yakaanza kujikusanya machoni mwa mwanamke huyo.
Kisha akaongea kwa sauti ya chini sana.
“Baba yako
 alikuwa karibu kuwafichua watu wenye nguvu.”
Malisa akasogea karibu.
“Akina nani?”
Mama yake akameza mate.
Kisha akasema maneno yaliyomgandisha damu kabisa:
“Pastor Gideon alikuwa rafiki mkubwa wa baba yako
”
“Alichomuua ni siri waliyoificha pamoja.”
Kimya kikazidi ndani ya nyumba.
Na kwa mara nyingine tena
jina la Pastor Gideon likarudi katikati ya jinamizi hilo.

Lakini Malisa bado hakujua

kwamba nje ya nyumba hiyo

kulikuwa na mtu aliyekuwa amewaangalia kupitia gari jeusi.
Na kwenye simu yake

kulikuwa na picha ya mama wa Malisa.
Kisha sauti nzito ikasema:
“Safari hii
 tutaumiza kile anachokipenda.”

ITAENDELEA























❀💞❀



𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: MJI WA DAMU𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney EPISODE 3: RISASI GIZANIMvua ilikuwa bado inanyesha ndani ya Dar es S...
05/06/2026

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: MJI WA DAMU
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney

EPISODE 3: RISASI GIZANI

Mvua ilikuwa bado inanyesha ndani ya Dar es Salaam usiku huo.
Ndani ya hospitali ya maiti

harufu ya moshi ilikuwa imeanza kujaa hewani.
Inspector Daniel Malisa alikimbia kuelekea maabara ya Doctor Iwamoto mara baada ya kusikia mlio wa risasi kupitia simu ya askari wa zamu.
“Harakeni!” alipaza sauti huku akikimbia kwenye korido ndefu ya hospitali.

Askari wawili walikuwa nyuma yake.
Walipofika mlangoni

moshi mzito ulikuwa unatoka ndani ya chumba.
Malisa akausukuma mlango kwa nguvu.
BANG!

Kile alichokiona ndani

kilimfanya asimame ghafla.
Makabrasha yalikuwa yanawaka moto.
Kompyuta ilikuwa imevunjwa.
Vioo vilikuwa vimetapakaa sakafuni.
Na Doctor Iwamoto

alikuwa amelala chini kwenye dimbwi la damu.
“Doctor!”
Malisa alipiga magoti haraka pembeni yake.
Doctor alikuwa bado anavuta pumzi kwa shida.
Risasi ilikuwa imepita karibu na bega lake lakini damu ilikuwa nyingi.
“Call ambulance NOW!” Malisa alipaza sauti.
Doctor Iwamoto akamshika mkono kwa nguvu.
Macho yake yalikuwa yanatetemeka.

“Daniel
”
“Usiongee kwanza.”
“Listen to me
”
Malisa akasogea karibu.
Doctor akavuta pumzi kwa maumivu.
“Wanarudi tena
”
“Nani?”
“Ile
 circle
”
Malisa akakunja uso.
Doctor akaendelea kwa shida.
“Baba yako
 hakuuawa kawaida
”
Macho ya Malisa yakabadilika.
“Kuna kitu alikuwa amegundua
”
“Kitu gani?” Doctor akatikisa kichwa polepole.

“Mzee Kibwana
 Pastor Gideon
 na wengine
”
Kabla hajamaliza

mashine za umeme zikazima tena.
GIZA.
Askari mmoja akapaza sauti: “Chief!”
Kisha milio ya hatua za mtu akikimbia ikasikika upande wa nyuma wa maabara.
Malisa akatoa bastola yake haraka.

“HAPO HAPO!”
Hakuna aliyesimama.
Malisa akaanza kukimbia kuelekea mlango wa nyuma.
Mvua kali ilimpiga usoni alipofungua mlango huo.
Mbele yake

kivuli cha mtu mwenye hoodie nyeusi kilikuwa kinakimbia kuelekea parking.
“Simama!”
Mtu huyo akaingia kwenye gari jeusi aina ya Noah.
Engine ikawashwa.
Malisa akafyatua risasi mbili

BANG!
BANG!

Lakini gari likatoka kwa kasi gizani.
Malisa akabaki amesimama kwenye mvua

akisikia hasira zikimchemka ndani.
Dakika thelathini baadaye

Doctor Iwamoto alikuwa amepelekwa chumba cha upasuaji.
Inspector Malisa alikuwa amesimama nje akiwa kimya.
Askari Peter akasogea.
“Tumepata hii.”
Akampa kitu kidogo cha chuma kilichokuwa kimelowa damu.
Malisa akakitazama.
Ilikuwa ni pendant ndogo yenye alama ile ile ya duara na mistari mitatu.
“Imepatikana wapi?”
“Karibu na dirisha la nyuma.”
Malisa akaikaza mkononi.

Alikuwa ameanza kuelewa kwamba hii haikuwa kesi ya kawaida.
Kulikuwa na kundi.
Na kundi hilo lilikuwa limejipanga vizuri.
Wakati huo huo

ndani ya kanisa kubwa lililokuwa eneo la Oysterbay

Pastor Gideon alikuwa amekaa peke yake ofisini.
Mvua ilikuwa ikigonga vioo vya dirisha kwa nguvu.
Mbele yake kulikuwa na Biblia iliyofunguliwa

lakini macho yake hayakuwa kwenye maandiko.
Alikuwa anawaza.

Ghafla mlango ukagongwa.
TOK TOK.
“Ingia.”
Mwanaume mmoja mnene aliingia haraka akiwa amelowa mvua.
“Pastor
 tuna tatizo.”
Pastor Gideon akainua macho polepole.
“Nini kimetokea?”
“Doctor Iwamoto bado yuko hai.”
Kimya.

Pastor akasimama taratibu.
Uso wake ukabadilika.
“Mliniahidi kazi itaisha leo.”
“Muuaji alisema polisi walifika mapema.”
Pastor Gideon akaenda mpaka dirishani.
Akaangalia mvua nje kwa sekunde kadhaa.
Kisha akaongea kwa sauti ya chini sana.
“Daniel Malisa anatakiwa afe kabla hajajua ukweli.”

Mwanaume yule akameza mate.
“Na mtoto?”
Pastor akafumba macho kwa sekunde.
“Bado hatujamaliza naye.”
Mahali pasipojulikana

Elvin alikuwa bado amefungwa kwenye kile kiti.

Alikuwa amechoka kulia.
Mbele yake kulikuwa na televisheni ndogo iliyokuwa ikionyesha habari za usiku.
“
Polisi wanaendelea kuchunguza tukio la kutekwa kwa mtoto wa mfanyabiashara maarufu
”
Mtoto akalia kwa sauti ndogo.
“Mama
”
Ghafla mlango ukafunguliwa.

Mwanaume mwenye hoodie akaingia tena.
Safari hii

alikuwa amebeba tray yenye chakula.
Aliiweka mezani kimya kimya.
Elvin akamtazama kwa macho ya hofu.
“Naomba nirudi nyumbani
”
Kimya.

Kisha mwanaume huyo akakaa mbele yake polepole.
Kwa mara ya kwanza

akaanza kuongea kwa sauti tulivu.
“Unamfahamu baba yako vizuri?”
Elvin akafuta machozi.
“Ndiyo
”
“Baba yako ni mtu mbaya sana.”
Mtoto akatikisa kichwa haraka.
“Hapana!”
Mwanaume huyo akacheka kidogo.
“Kila mtu anaamini hivyo.”
Akasimama.

Kisha akaongeza:
“Lakini damu ya watu wengi iko mikononi mwa baba yako.”
Elvin akaanza kulia tena.
Na mwanaume huyo

akaondoka gizani.
Saa nane za usiku.
Inspector Malisa alikuwa amerudi nyumbani kwake.
Apartment ndogo ya kisasa iliyokuwa kimya sana.
Alivua koti lake lililolowa mvua kisha akaenda moja kwa moja kwenye kabati la zamani.
Akatoa box la chuma.
Ndani yake kulikuwa na vitu vya baba yake aliyefariki miaka mingi iliyopita.

Picha.
Documents.
Na newspaper clipping yenye headline:
“MPELELEZI AUAWA KWENYE KESI YA SIRI.”
Malisa akaivuta kwa hasira.
Alikuwa mdogo sana baba yake alipokufa.
Aliambiwa ilikuwa ajali ya kikazi.
Lakini sasa

kila kitu kilianza kuonekana tofauti.
Ghafla simu yake ikaita.
UNKNOWN NUMBER.
Mapigo ya moyo wake yakabadilika.
Akajibu polepole.
“Hallow?”
Sauti ile ile nzito ikarudi.
“Unaanza kuona ukweli sasa
”
“Wewe ni nani?”
“Muulize mama yako kuhusu usiku ambao baba yako alikufa.”
Malisa akasimama ghafla.
“Unasemaje?”
Lakini simu ikakatwa.

Uso wa Malisa ukaganda.
Kwa miaka yote

hakuwahi kumuuliza mama yake ukweli wa usiku huo.
Na kitu ndani yake kilikuwa kinamwambia

kwamba maisha yake yalikuwa karibu kubadilika milele.
Usiku huohuo

nje ya apartment yake

gari jeusi lilikuwa limepaki gizani.

Ndani yake

mwanaume mmoja alivaa gloves nyeusi huku akiunganisha suppressor kwenye bastola.
Akaangalia picha ya Inspector Malisa kwenye simu yake.
Kisha akasema taratibu:
“Samahani Inspector
 mchezo umeanza kuwa binafsi.”
Akatoka ndani ya gari

akaanza kuelekea kwenye jengo.

ITAENDELEA























❀💞❀



HADITHI: 𝐌𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐃𝐀𝐌𝐔MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒EPISODE 2: 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐀𝐋𝐈𝐘𝐄𝐏𝐎𝐓𝐄𝐀𝑬𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂.....Usiku ule ule ambao mwili wa mwanamke a...
03/06/2026

HADITHI: 𝐌𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐃𝐀𝐌𝐔
MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒
EPISODE 2: 𝐌𝐓𝐎𝐓𝐎 𝐀𝐋𝐈𝐘𝐄𝐏𝐎𝐓𝐄𝐀

𝑬𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂.....
Usiku ule ule ambao mwili wa mwanamke asiyejulikana uliokotwa ufukweni

ndani ya jumba la kifahari la Dar es Salaam

sherehe ilikuwa imegeuka vilio.
“Mwanangu yuko wapi?!”
Sauti ya Mzee Kibwana ilisikika ikitetemeka ndani ya ukumbi mkubwa uliokuwa umejaa wageni waliopanic.
Walikuwa wakikimbia huku na kule.

Walimu wa watoto walikuwa wakihesabu watoto waliobaki.
Walinda usalama walikuwa wakifungua CCTV kwa haraka.
Lakini Elvin

mtoto wa miaka kumi

alikuwa ametoweka kabisa.
Mama yake alikuwa analia huku ameshikiliwa na wanawake wengine.
“Haiwezekani! Haiwezekani!” aliendelea kurudia.
Mzee Kibwana aligeuka kwa hasira.
“Nani alikuwa analinda geti?!”
Mlinzi mmoja akasogea akiwa anatetemeka.
“Bosi
 hatukuona mtu akiingia wala kutoka
”

KIBAO!
Kibwana akampiga kofi kali mpaka akaanguka chini.
“Mjinga wewe!”
Ukumbi mzima ukawa kimya.
Mzee Kibwana alikuwa mtu anayeheshimika sana mjini.
Bilionea.
Mfanyabiashara mkubwa wa mafuta, hotel na usafirishaji.
Lakini watu waliomfahamu vizuri

walijua alikuwa mtu wa kuogopwa.

Na alipokuwa na hasira

hata marafiki zake walimkimbia.
Dakika ishirini baadaye

magari mawili ya polisi yaliingia ndani ya eneo hilo.
Inspector Daniel Malisa akashuka.
Uso wake ulikuwa bado mzito kutokana na simu ya ajabu aliyopigiwa ufukweni.

Alipofika mlangoni

Mzee Kibwana alimfuata haraka.
“Inspector! Tafadhali mpate mwanangu!”
Malisa akamtazama kwa makini.
“Mara ya mwisho kuonekana ilikuwa saa ngapi?”
“Dakika k**a arobaini zilizopita!”
“Alikuwa na nani?”
“Alikuwa anacheza nje!”
Malisa akageuka kwa askari wake.
“Hakikisheni hakuna mtu anatoka hapa.”
Kisha akaanza kuelekea eneo la bustani.

Mvua ilikuwa imepungua lakini ardhi ilikuwa bado imelowa.
Alitembea taratibu huku akichunguza kila kitu.
Ghafla

akaona kitu.
Simu ndogo ya mtoto ikiwa imeanguka karibu na maua.
Aliinama akaichukua.
Screen ilikuwa imepasuka.
Lakini kabla hajaisimamisha vizuri

macho yake yakatua kwenye kitu kingine.
Alama.

Ile ile alama iliyokuwa kwenye maiti ya mwanamke ufukweni.
Ilikuwa imechorwa kwenye ukuta wa bustani kwa rangi nyekundu.
Malisa akahisi mwili wake ukipata baridi.
“Impossible
” alinong’ona.
Askari Peter akasogea.
“Kuna nini mkuu?”
Malisa hakujibu.
Aliendelea kuitazama ile alama kana kwamba ilikuwa inamkumbusha jambo baya sana.
Kisha akauliza:
“Camera za CCTV zinafanya kazi?”
“Ndiyo.”
“Nataka footage zote.”
Ndani ya chumba cha CCTV

video zilianza kuchezwa moja baada ya nyingine.

Walimuona Elvin akicheza nje.
Kisha taa zikazimika.
Screen ikawa nyeusi kwa sekunde saba.
Na taa ziliporudi

Elvin hakuwepo tena.

Askari Peter akashangaa.
“Camera zote zimekatika kwa wakati mmoja
”
Malisa akakunja uso.
“Hii imepangwa.”
“Unafikiri nani anahusika?”
Malisa hakujibu.
Lakini kichwani mwake

alianza kuunganisha dots.
Maiti.
Alama.
Simu ya vitisho.
Na sasa utekaji.

Kulikuwa na mtu alikuwa anaanza mchezo mkubwa sana.
Wakati huo huo

mahali pasipojulikana.
Chumba kidogo chenye mwanga hafifu.
Elvin alikuwa amefungwa mikono kwenye kiti.
Macho yake yalikuwa yamejaa machozi.
“Kaka
 naomba nirudi kwa mama
”
Kimya.
Mbele yake alisimama mwanaume mmoja aliyevaa hoodie nyeusi.

Uso wake haukuonekana.
Aliendelea kumtazama mtoto huyo bila kusema kitu.
Kisha akaweka simu mezani.
Simu ikaanza kuita.
Screen ikaonyesha:
MZEE KIBWANA.
Mwanaume huyo akatabasamu polepole

akapokea.
“Hallow?! Mwanangu yuko wapi?!” Kibwana alipaza sauti.
“Ukiona damu inaanza kumwagika
” sauti ile nzito ikasema taratibu.
“Jua kwamba siri za zamani zimeanza kufufuka.”
“Unataka nini?!”
“Miaka kumi na tano iliyopita ulifanya kosa kubwa sana, Kibwana.”
Kimya.
Kwa mara ya kwanza

uso wa Mzee Kibwana ukabadilika.

Kana kwamba alikuwa amekumbuka kitu.
Kitu ambacho alitamani kisijulikane milele.
“Wewe ni nani?” akauliza kwa sauti ya chini.
Sauti ile ikacheka.
“Muulize rafiki yako Pastor Gideon.”
CLICK.
Simu ikakatwa.
Mzee Kibwana akabaki amesimama kimya.
Uso wake ukianza kutoka jasho.
Na Inspector Malisa

aliyekuwa amesimama mita chache kutoka hapo

alikuwa ameisikia kila kitu.
Usiku huo huo

ndani ya chumba cha uchunguzi wa maiti.
Doctor Iwamoto alikuwa akichunguza faili la zamani.
Mikono yake ilikuwa ikitetemeka.

Kwenye faili lile kulikuwa na picha za maiti kadhaa zilizokuwa na alama ile ile.
Kesi ya miaka kumi na tano iliyopita.
Kesi iliyofungwa ghafla.
Kesi iliyomuua baba wa Inspector Malisa.
Doctor alipofungua ukurasa wa mwisho

kitu kikaanguka kutoka ndani ya faili.

Ilikuwa picha ya zamani.
Picha iliyowaonyesha watu watatu wakiwa pamoja.
Mzee Kibwana.
Pastor Gideon.
Na

baba wa Inspector Malisa.
Doctor Iwamoto akavuta pumzi kwa nguvu.
“Mungu wangu
”
Ghafla taa zikazimika.
Chumba kikaingia gizani.
Kisha

sauti nzito ikasikika nyuma yake.
“Ulitakiwa kuacha yaliyopita yazikwe, Doctor.”
Doctor Iwamoto akageuka kwa hofu.
Lakini kabla hajaona vizuri

RISASI!
MLIO mkubwa ukapasua chumba.
Na faili lile la siri

likaanza kuteketea kwa moto.

ITAENDELEA























❀💞❀



Address

Magegele
Makambako
59122

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hadithi Zetu:

Shortcuts

Share