Hadithi Zetu

Hadithi Zetu ᴋᴀʀɪʙᴜ sᴀɴᴀ ᴋᴀᴛɪᴋᴀ ᴍᴀᴋᴛᴀʙᴀ ʏᴀ ʜᴀᴅɪᴛʜɪ. ᴜᴋᴜʀᴀsᴀ ʜᴜᴜ ɴɪ ᴍᴀᴀʟᴜᴍᴜ ᴋᴡᴀ ᴋᴀᴢɪ ᴢᴀ ғᴀsɪʜɪ & ᴍᴀᴋᴀʟᴀ ᴍʙᴀʟɪᴍʙᴀʟɪ. Pia, tunatoa makala mbalimbali kwenye ukurasa wetu.

Hadithi Zetu ni ukurasa wa Facebook ambao una lengo la kuchapisha kazi za fasihi andishi, simulizi, na makala mbalimbali. Ukurasa huu umeundwa ili kuhuisha na kueneza urithi wa hadithi na tamaduni za Kiafrika kupitia njia ya maandishi. Tunajitahidi kuwa jukwaa la kuelimisha, kuburudisha, na kuhamasisha wengine kwa njia ya hadithi. Kwenye ukurasa wetu, utapata aina mbalimbali za kazi za fasihi andi

shi, ikiwa ni pamoja na hadithi za kusisimua, mashairi, riwaya fupi, na tamthilia. Tunajitahidi kuchapisha kazi zenye ubora na zinazogusa masuala mbalimbali yanayohusiana na jamii, utamaduni, upendo, mazingira, na masuala mengine ya kijamii. Mbali na kazi za fasihi andishi, tunatoa pia simulizi mbalimbali za kuvutia. Hizi ni hadithi za kusisimua, za kuburudisha, na zenye kuelimisha. Simulizi zetu zinaweza kuwa za kisasa au za jadi, zinazohusisha wahusika wenye maisha ya kuvutia na matukio ya kusisimua. Lengo letu ni kutoa burudani na kuwafanya wasomaji wetu kujisikia kushiriki katika ulimwengu wa hadithi. Makala hizi zinajadili mada mbalimbali za kijamii, utamaduni, sanaa, na masuala mengine yanayohusiana na fasihi na simulizi. Tunazingatia kutoa taarifa sahihi na za kuvutia ili kuhamasisha majadiliano na kuelimisha wasomaji wetu. Tunakaribisha wanachama wote wa jamii kuungana nasi kwenye ukurasa wetu wa Facebook, Hadithi Zetu. Tunahimiza ushiriki wa wadau wa fasihi, waandishi, wasomaji, na wapenda hadithi katika kuchangia kazi zao, kutoa maoni, na kushiriki maarifa na uzoefu wao. Tunatumai kuwa Hadithi Zetu itakuwa sehemu ambayo itawawezesha watu kugundua, kuelimika, na kufurahia upekee wa hadithi za Kiafrika na tamaduni zetu. Karibu sana kujiunga na jumuiya yetu na kushiriki katika uumbaji wa hadithi za kuvutia na za kuelimisha.

🌟 HADITHI MPYA! 🌟"SMS YA MWISHO" – Hadithi ya kusisimua, kuhuzunisha na yenye mafunzo makubwa kuhusu maisha, mapenzi na ...
17/07/2025

🌟 HADITHI MPYA! 🌟
"SMS YA MWISHO" – Hadithi ya kusisimua, kuhuzunisha na yenye mafunzo makubwa kuhusu maisha, mapenzi na siri nzito zinazofichwa na ujumbe mmoja tu wa mwisho... 📱💔

🆓 Inapatikana BURE kabisa!
📲 Pakua sasa kupitia duka letu la Hadithi Zetu kwa Selar:
👉 https://selar.com/5m27a12576

Usikose simulizi hii ya kipekee ambayo imemgusa kila msomaji aliyeipata!

---

🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖

UTANGULIZIKatika dunia ya leo ya teknolojia na haraka ya maisha, upendo wa kweli unaonekana kuwa jambo adimu — jambo la hadithi. Lakini vipi k**a moyo mmoja unaweza kugusa mwingine bila hata kuonana? Vipi k**a ujumbe mmoja wa maandishi unaweza kuwa mwanzo wa mapenzi ya maisha?“SMS YA MWISHO” n...

📢 Punguzo Kubwa la Hadithi ya Jaribu la Ushindi!Wapenzi wa hadithi, Jaribu la Ushindi sasa inapatikana kwa bei mpya nafu...
17/07/2025

📢 Punguzo Kubwa la Hadithi ya Jaribu la Ushindi!

Wapenzi wa hadithi, Jaribu la Ushindi sasa inapatikana kwa bei mpya nafuu!

👉 Toka TSh 5,000 sasa ni TSh 2,500 tu!

Usikose kupata hadithi hii yenye msisimko, mafunzo na burudani kubwa!

Pakua sasa kupitia duka letu la Hadithi Zetu kwenye Selar:
https://selar.com/m4931y

Mungu alipotuumba wanadamu alituwekea na vipimo vya kutupima ili kutujua k**a kweli tunaweza kufuata au kuishi kwa kufuata maelekezo yake. Hata mzazi anapotaka kumpa kitu mwanaye, jambo la kwanza atampa mtihani mwanaye kumpima kujua jambo fulani na atakapojiridhisha basi atampatia kitu hicho. Ndani....

02/07/2025

Celebrating my 4th year on Facebook. Thank you for your continuing support. I could never have made it without you. 🙏🤗🎉

📌🎉✨ Leo ni Siku Yangu ya Kuzaliwa! ✨🎉Leo naandika haya nikiwa na moyo wa shukrani, tafakari, na upendo mwingi. Ni siku y...
27/06/2025

📌🎉✨ Leo ni Siku Yangu ya Kuzaliwa! ✨🎉

Leo naandika haya nikiwa na moyo wa shukrani, tafakari, na upendo mwingi. Ni siku yangu ya kuzaliwa siku ya kipekee ninayoichukulia kwa uzito na heshima, kwa sababu ni zawadi nyingine ya maisha kutoka kwa Mungu. Si kwa akili zangu, si kwa nguvu zangu, bali ni kwa rehema na fadhili zake zisizokoma.

Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kuvuka mwaka mwingine wa maisha. Katika kila siku, nimejifunza, nimekua, na nimeendelea kujitambua.
Lakini pia leo naitazama siku hii kwa hisia mchanganyiko…
Mama yangu mpendwa tangu ulipoondoka mwaka 2022, maisha hayajawahi kuwa k**a zamani. Nakukumbuka sana leo. Upendo wako, busara zako, na maombi yako vinaishi ndani yangu kila siku. Siku k**a ya leo ningependa sana unione ukiwa na tabasamu lako la upendo.
Nakupenda, Mama. Naendelea kukuenzi kwa vitendo vyema. 🤍

Kwa upande mwingine, namshukuru sana Baba yangu kwa kuendelea kusimama imara, k**a nguzo ya familia yetu. Ametupa moyo wa matumaini na ujasiri licha ya yote. Pia nina bahati kuwa na kaka, dada, na mdogo wangu, ambao wamekuwa sehemu ya nguvu yangu, msaada wangu na marafiki wa kweli katika kila hatua ya maisha.
Na kwa rafiki zangu wa kweli, wale wachache wa kipekee waliobaki karibu nami kwa uaminifu, kwa maneno ya faraja, na kwa moyo wa dhati, asanteni sana. Urafiki wenu ni zawadi.

Leo siadhimishi tu siku yangu ya kuzaliwa. Naadhimisha nguvu ya upendo, familia, marafiki wa kweli, na uwepo wa Mungu katika maisha yangu. Mwaka mpya wa maisha umefika, na naupokea kwa imani, shukrani, na matumaini mapya.

Heri ya siku yangu ya kuzaliwa. Najisherehekea, lakini pia nawasherehekea wote walioko katika maisha yangu leo.
Mungu ni mwaminifu.

🤍𝑯𝑨𝑷𝑷𝒀 𝑩𝑰𝑹𝑻𝑯𝑫𝑨𝒀 𝑻𝑶 𝑴𝑬🤍







゚viralシ







𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝐽𝐴𝑅𝐼𝐵𝑈 𝐿𝐴 𝑈𝑆𝐻𝐼𝑁𝐷𝐼𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝐺𝐸𝑂𝐹𝑅𝐸𝑌 𝐷𝐼𝑆𝑀𝐴𝑆𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 04ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ......Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Mar...
03/06/2025

𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝐽𝐴𝑅𝐼𝐵𝑈 𝐿𝐴 𝑈𝑆𝐻𝐼𝑁𝐷𝐼
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝐺𝐸𝑂𝐹𝑅𝐸𝑌 𝐷𝐼𝑆𝑀𝐴𝑆
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 04

ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ......

Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Martin na kuanza kumtukana na kumtuhumu kuwa amemuua mjukuu wake, Martin akijitetea sana lakini hakuna kitu kilichobadilika, mama mkwe huyo aliendelea kumtuhumu kuwa mali zote alizonazo ni kwa sababu alitoa kafara ya watu ili awe tajiri. Hii ilimuumiza sana Martin aliamua kukata simu. Alitaka kupata msaada kutoka kwa mtu, na mtu pekee aliyemfikiria alikuwa ni Juliet!

sᴀsᴀ ᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.........

Alichukua funguo za gari na kutoka katika ofisi yake huku akimuelekeza secretary wake kukata mikutano yote aliyokuwa nayo siku hiyo na kuipangia tarehe nyingine. Aliingia ndani ya gari yake na kuelekea anakofanyia kazi Juliet katika kampuni ya simu ya MTN.

Juliet alikuwa nje ya jengo la makao makuu ya kampuni ya simu ya MTN, alikuwa akizungumza na mtu mara akaja kijana mmoja ambaye alimueleza kuwa kuna mtu amemuagiza amuite.
“Ni nani?” Juliet alihoji kwa mshangao.
“Simfahamu…Yuko pale kwenye maegesho ya gari.”
“Okey asante…. Naomba uniwie radhi, ngoja nikamuone huyo mtu.” Juliet alikubali wito kisha akamuaga mtu akiyekuwa anazungumza naye na kwenda kumuona mtu aliyeelekezwa kuwa yuko kwenye maegesho ya magari.

Juliet alipofika hakuamini, alikuwa ni Martin, mume wa Annabelle. Hasira zikamjaa, “Unafanya nini hapa?” Juliet alimuuliza Martin kwa hasira.
“Juliet salamu kwanza basi…”
“Hakuna haja ya salamu…. Sikia sema shida yako na uondoke!”
Martin alibaki akidua maana Juliet akiyeko mbele yake muda huo si Juliet yule aliyekuwa akimchangamkia na kumsifia kila wakipokutana. “Anyway, Juliet niko hapa kukuomba msaada!”
“Wa kumuua Annabelle?” Juliet alimuuliza Martin swali gumu na la ajabu sana.

“WHAT?” Martin aliuliza kwa shangao hakuamini alichokisikia kutoka kwa Juliet.
“Ooh! Ulidhani siri yako haitafichuka eeh? Ulidhani hatutajua kuwa wewe ndiye uliyemtoa kafara mwanao mwenyewe ili upate utajiri ulionao sasa na sasa unataka umuue na 7 yangu,hapo umekwama Martin.” Juliet aliongea maneno makavu makavu ambayo yalimduwaza Martin.
“Excuse Me! Juliet, what the hell are you talking about?” Martin aliuliza kwa mshangao.
“Martin, sina muda wa kupoteza na Wewe, kusanya makongoro yako na uondoke hapa sasa hivi…”
“Juli…”
“Martin ondoka haraka au nitaita walinzi, muuaji mkubwa wewe.”
Martin hakuwa na la kufanya aliamua kuingia ndani ya gari yake na kuondoka huku akiwa na machungu moyoni na kichwani mwake maneno k**a kafara, muuaji yalizidi kujirudia kichwani mwake. Martin alijikuta machozi yakimtoka, akaanza kulia kwa uchungu huku akimuuliza Mungu k**a kweli yeye ni mbaya kiasi hicho.

Akiwa kwenye dimbwi la mawazo mala bodaboda akakatiza mbele ya gari yake haraka akaanza kumkwepa na bahati mbaya akaenda kuigonga nguzo ya umeme iliyokuwa upande wa kulia, akazimia hapo hapo.
Martin alipoamka alijikuta yuko juu ya kitanda cha hospitali, alipotazama pembeni yake kulikuwa na chupa ya drip, alipojitazama akaona amefungwa budge maeneo mbali mbali ikiwemo kichwani. Alipotazama mlangoni alimuona nesi akiingia.

“Taratibu utajiumiza, tulia tu acha kuhangaika” Ilikuwa ni sauti ya upole ya nesi.
“Nimefikaje hapa nini kimetokea?” Martin aliuliza kwa shida kwa kuwa alikuwa anahisi maumivu sehemu mbalimbali za mwili wake.
“Umeletwa hapa na waaamaria wema, ulipata ajali ya gari!”
“Ooh! My God nimekumbuka…Daktari yuko wapi?” Martin alimuuliza yule nesi.
“Usijali daktari atafika muda si mrefu.” Nesi alijibu kwa sauti ya kiungwana sana iliyomvutia Martin hata kutamani aendelee kukaa hapo hospitali.
“Je, kuna mtu yeyote ungetaka kuwasiliana naye kumueleza juu ya hali yako?” Nesi alimuukiza Martin.
“Yeah yupo, simu yangu….”
“Hakuna simu iliyoletwa hapa pengine….”
“Wameshaiba wasamaria wema” Martin alijibu kimasihara hadi nesi akajikuta amecheka k**a ni mazuri.
“Unavituko sana wewe, usijali nipatie namba za mkeo nimpigie”
Martin akamtajia nesi yule namba za mkewe na kisha akampigia simu na kumueleza kuwa afike hospitali ya Mt. Joseph ili kumuona mumewe.
“Asante sana nesi, unaitwa nani?” Martin alimshukuru nesi yule na kumuuliza jina lake.
“Usijali ni sadaka tu hii, naitwa Sonia” Nesi alijibu kuhu akikagua kagua chupa ya drip.

Baada ya muda daktari alifika na kusalimiana na Martin. “Unajisikiaje?” Daktari aliuliza.
“Najisikia maumivu kiasi katika kichwa, mkono na mgongo” Martin alimuelezea daktari anavyojihisi.
“Ni sawa, hata hivyo hakuna majeraha makubwa uliyopata, nimekufanyia vipimo vyote uko salama hakuna mfupa uliovunjia, uko salama na haya msumivu ni yakawaida kabisa.” Daktari alimuelezea Martin ambaye alijisikia faraja sana kusikia kuwa hakupata madhara makubwa kutokana na ajali aliyopata.
Akiwa bado anazungumza na dakari, Annabelle aliingia akiwa hana hata chembe ya shauku kutaka kujua mmewe anaendeleaje.

𝑻𝒖𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒆 𝒂𝒖 𝒕𝒖𝒊𝒔𝒉𝒊𝒆 𝒉𝒂𝒑𝒂? 𝑾𝒆𝒌𝒂 𝒄𝒐𝒎𝒎𝒆𝒏𝒕 𝒉𝒂𝒑𝒐 𝒄𝒉𝒊𝒏𝒊 𝒎𝒅𝒂𝒖 𝒘𝒂𝒏𝒈𝒖

゚viralシfypシ゚viralシalシ ゚viralシ

𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝑱𝑨𝑹𝑰𝑩𝑼 𝑳𝑨 𝑼𝑺𝑯𝑰𝑵𝑫𝑰𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 03ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ........Martin alifika kazini baada ya dakika 20 na...
15/05/2025

𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝑱𝑨𝑹𝑰𝑩𝑼 𝑳𝑨 𝑼𝑺𝑯𝑰𝑵𝑫𝑰
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 03

ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ........

Martin alifika kazini baada ya dakika 20 na hakika na kuketi katika kiti chake. Alianza kutafakari mambo yaliyotokea nyumbani kwake mapema asubuhi, aliumia sana, alisikia sauti ndani mwake inamwambia, ‘You are not a Victim but a victor.’ Alistuka na kuketi vizuri kwenye kiti chake cha kiboss ofisini kwake, kisha akatabasamu. Akiwa bado katika tabasamu akasikia simu yake ya mezani inaita, akaipokea haraka, “Hallo, Mr. Martin hapa….”

“Ooh! Habari, unaongea na Dkt. Egube Ike, nimekupigia kukutaarufu kuwa niko tayari kufanya kazi na wewe na kwa kuanza nitakupatia mradi wa 2.5 Billion nahitaji mradi ukamilike kwa haraka sana.”

“Sir, are you serious?” Martin aliuliza kqa mshangao kwakuwa hakutarajia alichokisikia kwenye simu hiyo. Alifurahi na kumshukuru sana Dkt. Egube. Alimuita secretary wake na kumpa maelekezo na mara moja kazi ikaanza.

𝑺𝑨𝑺𝑨 𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨......

Jioni alirudi nyumbani akiwa hoi na njaa pia, alimkuta mkewe anatazama television, alimsalimu mkewe lakini aliambulia msonyo wa karne akajiongeza mwenyewe kimya kimya hadi mezani ambako nako hakukuta chakula chochote licha ya kuacha pesa za kutosha. Alidhani pengine chakula kipo jikoni, alipofika alikuta kulikuwa na dalili kuwa kulipikwa lakini hakuna kilichobaki kwa ajili yake! Alitaka kwenda kumuuliza mkewe lakini akaona haitakuwa sawa kufanya hivyo na itasababisha ugomvi kitu ambacho hakutaka kitokee.

Alirudi sebleni ambako alichukua kibegi chake na kuingia ndani, akijitupa kitandani taratibu usingizi ukaanza kumnyemelea, hajutaka hilo litokee mapema hivyo, alioga na kisha kubadili nguo. Akachukua funguo za gari lake na kuelekea nje alikolipaki, aliingia na kisha kuondoka taratibu, akak**ata barabara iliyokuwa inaelekea mjini huku akisikiliza mziki wa injili toka kwa msanii maarufu nchini Nigeria. Alifika kwenye mataa na kusimama baada ya taa nyekundu kuwaka, baada ya dakika k**a moja taa ya kijani iliwaka naye akaweka gia ya kuondokea na kupinda kushoto hadi katika mgahawa maarufu F&J restaurant, mgahawa unaomilikiwa na ndugu wawili, aliagiza chalula apendacho na kisha baada ya dakika kadhaa akiwa anaendelea kula aliagiza chakula kingine kwa ajili ya mkewe, japo jikoni kulikuwa kuna dalili kuwa kulipikwa, aliamini pengine mkewe alimpikia mlinzi.

Alibeba kile chakula na kurejea nyumbani kwake, akimkuta mkewe bado anatazama television, hakutaka kuongea nae maneno mengi sana, akimuekea kile chakula mezani na kumwambia, “Mke wangu chakula chako kiko hapa mezani, usiku mwema.”

Mkewe wala hakujibu kitu na Martin alilizoea hilo kutoka kwa mkewe hivyo hakujisumbua sana.

Aliingia kulala na baada ya muda mkewe aliingia chumbani. Martin alikumbuka kuwa kuna habari njema hajamueleza mkewe hivyo ikabidi amueleze, “Mke wangu nimekumbuka kitu, leo nimepata contract ya 2.5 Billions…Mungu amekuwa mwema sana kwetu.” Martin alimueleza mkewe lakini badala yake alipokea msonyo ule ule wa karne kisha mkewe akavuta shuka lake na kugeukia ukutani.

Asubuhi Martin mtu wa kazi aliamka na k**a kawaida yake alijiandaa na kupita mezani lakini hakukuta chochote akaendelea na safari yake kuelekea kazini hakutaka kumuamsha mkewe alimuachia fedha kwa ajili ya chakula na matumizi yake binafsi ikiwa ni kawaida yake kumpa mkewe kila mwezi kiasi cha million 2 kwa ajili ya matumizi yake binafsi kwa kuwa hafanyi kazi na alikataa kufanya kazi mara baada ya kumpoteza mtoto wao kwa madai kuwa anahitaji muda ili awe sawa.

Annabelle alipoamka alikuta kiasi cha pesa cha shilingi milioni 3 tofauti na ilivyokuwa awali kuwa kila mwisho wa mwezi hupewa milioni 2. Alizichukua zote na kuziweka katika kisanduku chake ambacho hukitumia kuhifadhi pesa zake. Alijiandaa na kisha akachukua ufunguo wa gari lake aina ya Benz na kuondoka kuelekea kwa rafiki yake aitwaye Juliet. Walipoonana walikumbatiana kwa kuwa hawakuwa wamekutana kwa muda mrefu sana.

Walianza maongezi yao na Annabelle akamueleza rafiki yake kila kitu juu ya kile kilichotokea hadi mtoto wao akauawa. Juliet alimpa pole rafiki yake na kumshauri kukaa mbali na Martin kwani kuna uwezekano akamuua pia ili ajipatie utajiri, maneno yale yalimuingia Annabelle na akayabeba k**a yalivyo.

Anabelle aliporudi nyumbani alianza kutafakari juu ya mambo ambayo aliambiwa na rafiki yake naye alihisi kuwa ni kweli kwa kila kitu alichoambiwa na rafiki yake, hapo hasira na chuki dhidi ya Mumewe iliongezeka.

Njioni mumewe alirejea akiwa na hamu sana na mkewe lakini hakujua ni kwa namna gani mkewe alivyo jazwa sumu. Alifika na kukuta mkewe amelala tofauti na alivyozoea akitazama television. Alienda kuoga na kisha akarejea sebleni, alikaa kwa muda kidogo kisha akanyanyuka na kwenda chumba alicholala mkewe. Alipofika alikuta mkewe amelala kihasara hasara, akahisi damu inamchemka kuliko kawaida, mapigo ya moyo wake yakaanza kumwenda mbio mbio, jogoo la mjini likawika shamba. Martin akamsogelea mkewe pale kitandani na kuanza kumpapasa mkewe mapajani taratibu mkono wake ukielekea kibo na mawenzi, akiwa anakaribia kibo mara mkewe akastuka alipomuona mumewe alimsukuma kwangu. Martin akadondoka chini!

“Honey nini hiki sasa?” Martin alimuuliza mkewe kwa mshangao.

“Nini kuhusu nini?” Annabelle naye akajibu kwa swali huku akiwa amefura kwa hasira.

“Baby kwanini unaninyima haki yangu?”

“Haki ipi? Nakuuliza wewe muuaji haki ipi?”

“Annabelle wewe ni mke wangu tena wa ndoa na hii ni haki yangu unaninyima kwa miezi mitano sasa why are you doing this to me?” Martin alimlalamikia mke wake.

“Mke! Haki! Hivi unadhani kwa kwa kile ulichokifanya kwa mtoto wetu bado unayo haki juu yangu? Hapana Martin, huna haki hiyo tena na kwa taarifa yako, huu ni mwanzo tu, utateseka sana.” Annabelle alimueleza mumewe maneno ambayo kwa hakika yalimuumiza sana Martin. Baada ya kumueleza maneno yale Annabelle akachukua mto mmoja kwenda kulala chumba cha wageni. Hili hakulitegemea japo anaelewa wazi kuwa mkewe huyo anamchukia sana lakini hadi kulala vyumba tofauti, hii ilimuwashia taa ya kijani, hakutaka kumzuia alimuacha kisha akarejea kitandani. Alitazama kaptula yake tayari ilikuwa inaunyevu unyevu sehemu ya mbele, akatikisa kichwa kisha akachukua taulo yake na kuingia bafuni kuoga, alipomaliza alijiweka sawa kisha akalala.

Asubuhi ikafika Martin alijiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini, alipofika mlangoni alikumbuka kuwa yeye na mkewe hawakulala chumba kimoja, hivyo akaamua kwenda kumjulia hali mkewe, aligonga mlango lakini hakujibiwa aliamua kuufungua. Akiingia ndani ya chumba kile na kukuta mkewe yuko kwenye usingizi mzito huku akijigeuza kuelekea upande mwingine, Martin alitabasamu kisha akaufunga mlango na kuelekea kazini. Annabelle alipoamka alijiandalia kifungua kinywa kisha akakumbuka kumpigia mama yake simu. Mama yake alipokea na kumuuliza anaendeleaje.

“Mama naendelea vizuri ila namkumbuka tu mwanangu mama….” Annabelle alianza kulia wakati akimuelezea juu ya hali yake na namna alivyomkumbuka Ruth.

“Mwanangu, Juliet ameniambia kila kitu ni kwanini hukuniambia mapema…. Huyo mwanaume inaonekana wazi ni mshirikina, hizo mali ni kwasababu ya kutoa watu kafara sasa ameamua hadi kumtoa kafara mtoto wake mwenyewe, unbelievable!”

“Mama ninaumia sana kwa kweli, mtoto mwenyewe alikuwa mmoja k**a dawa halafu kirahisi rahisi tu anakufa jamanii mamaaa.” Annabelle aliendelea kumueleza mama yake kwa uchungu.

“Pole mwanangu, usijali I've to do something before it's too late…. Usijali mwanangu ila naomba uwe makini sana na huyo mwanaume.”

“Sawa mama nitakuwa makini sana.” Annabelle alimaliza kuongea na mama yake na kisha wakakata simu.

Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Martin na kuanza kumtukana na kumtuhumu kuwa amemuua mjukuu wake, Martin akijitetea sana lakini hakuna kitu kilichobadilika, mama mkwe huyo aliendelea kumtuhumu kuwa mali zote alizonazo ni kwa sababu alitoa kafara ya watu ili awe tajiri. Hii ilimuumiza sana Martin aliamua kukata simu. Alitaka kupata msaada kutoka kwa mtu, na mtu pekee aliyemfikiria alikuwa ni Juliet!

ɪᴛᴀᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.............

Ni Simulizi gani ya kusisimua uliyowahi kuisoma kutoka kwa BEN R. MTOBWA?
13/05/2025

Ni Simulizi gani ya kusisimua uliyowahi kuisoma kutoka kwa BEN R. MTOBWA?

𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝑱𝑨𝑹𝑰𝑩𝑼 𝑳𝑨 𝑼𝑺𝑯𝑰𝑵𝑫𝑰𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 02ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ.....“Okey nenda kamuoneshe mama atafurahi sana.” “...
12/05/2025

𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝑱𝑨𝑹𝑰𝑩𝑼 𝑳𝑨 𝑼𝑺𝑯𝑰𝑵𝑫𝑰
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 02

ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ.....

“Okey nenda kamuoneshe mama atafurahi sana.”
“Asante baba…” Ritha akajibu kisha akaanza kupiga hatua kuelekea chumbani kwa mama yake, mara akakumbuka kitu.
“Baba leo utanipeleka cinema?” Ritha alimuuliza baba yake ikiwa ni ahadi aliyopewa na baba yake kabla hajafanya mtihani wa taifa.
“Oooh! Yeah lazima twende na umwambie mama yako leo ajiandae leo usiku tutakwenda Cinema kuna filamu mpya ya Ken Eric na Yul Edochie waigizaji mnaowapenda”

sᴀs ᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ......

“Asante baba, nakupenda”
“Nakupenda pia mwanangu” Martin naye alijibu na kumuacha binti yake aende kwa mama yake.
Martin alimuwekea utaratibu binti yake kuwa endapo anataka vitu vya kujifurahisha ni lazima avifanyie kazi, hawezi kuvipata bure tu. Hivyo ndivyo ilivyotekea kabla hajafanya mtihani, Ritha alimuomba baba yake ampeleke kwenye Cinema lakini baba yake alimwambia kuwa utaratibu ni ule ule, nilazima afaulu mtihani kwake ndipo anpekeke Cinema.

𝗨taratibu huu ulimsaidia sana Ritha kufanya vizuri shuleni kwani alijua kwakufanya hivyo basi angepata chochote anachotaka bila maswali.
Alipofika kidato cha tatu alipata likizo ya katikati ya mwaka yaani nusu muhula ambapo awali aliahidiwa akifaulu basi atapelekwa kijijini kupumzika na babu na bibi yake jambo ambalo Ritha alikuwa analisubiria sana.

𝗦iku ya safari iliwadia, na siku hiyo ilikuwa ni mwisho wa wiki yaani jumamosi, walidamka asubuhi na mapema kila mmoja akajiandaa kwa ajili ya safari. Waliingia ndani ya gari yao na kuanza safari kuelekea kijijini kwao.

𝗡inabell alianza kumchukia sana mume wake kwasababu ya kifo cha binti yao, Ruth. Martin alijitahidi kuomba msamaha kadri alivyoweza lakini ilishindikana, aliamua kumpa muda mkewe akiamini pengine ni kwasababu anapitia wati mgumu sana tika maisha yake baada ya kumpoteza binti yao kipenzi. Martin aliamua kuwa imara kwa ajili ya mkewe na hata yeye pia japo ndani ya moyo wake alikuwa na maumivu makali sana kwa kifo cha binti yao mpendwa. Juna wakati alikuwa akikaa ofisini huinamia meza yake na kuanza kulia kwa uchungu aliokuwa nao lakini akiwa na mkewe au watu wengine, huwa anajionesha k**a mtu imara na asiye na asiye na maumivu au majuto yoyote na hii ndiyo ilikuwa sababu ya mkewe kuzidisha chuki dhidi yake.

𝗕aada ya miezi mitatu kupita Martin aliamua kufanya kazi kwa bidii na alimuomba Mungu sana amsamehe na amtie nguvu katika kufanya kazi zake pengine mafanikio yangeweza kumfanya mkewe angalau apoteze mawazo na aanze kujivunia kuwa na mwanaume imara.
Siku moja asubuhi na mapema ikiwa ni mwanzo wa wiki, Martin alidamka k**a kawaida yake alijiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini. Alifika mezani na kukuta meza nyeupe, alimuita mkewe aliyekuwa anatazama picha ya binti yao, “Mke wangu…Mke wangu…. Annabelle si ninakuita!”

𝗠kewe alintazama na kisha akaendelea kutazama picha, Martin alianza kupandwa na hasira kidogo kutokana na dharau aliyooneshewa na mkewe. “Annabelle kwanini hujaniandalia chai wakati unajua kabisa kuwa huwa nakunywa chai nyumbani kabla sijaenda kazini?” Martin alimuuliza mkewe kwa sauti ya ukali kidogo.
“Eeeeh! Ishia hapo hapo muuaji mkubwa wewe…. Kimya, kwani jiko hulioni lilipo?” Annabelle alimjibu mumewe ambaye alibaki akidua kwa maneno ya mkewe.
“Annabelle! Ni wewe mke wangu unayasema haya?” Martin hakuamini kabisa alichokisikia lakini huo ndiyo ukweli kuwa mkewe alikuwa amebadilika sana, ilimuumiza sana hali hiyo lakini aliendelea kujitahidi kumuelewa mkewe kuwa bado anawati mgumu. Aliamua kubeba begi lake la kazini na kuondoka.

𝗠artin alifika kazini baada ya dakika 20 na hakika na kuketi katika kiti chake. Alianza kutafakari mambo yaliyotokea nyumbani kwake mapema asubuhi, aliumia sana, alisikia sauti ndani mwake inamwambia, ‘You are not a Victim but a victor.’ Alistuka na kuketi vizuri kwenye kiti chake cha kiboss ofisini kwake, kisha akatabasamu. Akiwa bado katika tabasamu akasikia simu yake ya mezani inaita, akaipokea haraka, “Hallo, Mr. Martin hapa….”

“Ooh! Habari, unaongea na Dkt. Egube Ike, nimekupigia kukutaarufu kuwa niko tayari kufanya kazi na wewe na kwa kuanza nitakupatia mradi wa 2.5 Billion nahitaji mradi ukamilike kwa haraka sana.”
“Sir, are you serious?” Martin aliuliza kqa mshangao kwakuwa hakutarajia alichokisikia kwenye simu hiyo. Alifurahi na kumshukuru sana Dkt. Egube.

𝗔limuita secretary wake na kumpa maelekezo na mara moja kazi ikaanza.

𝐼𝑇𝐴𝐸𝑁𝐷𝐸𝐿𝐸𝐴.....


゚viralシfypシ゚viralシalシ
゚viralシ

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: 𝖩𝖠𝖱𝖨𝖡𝖴 𝖫𝖠 𝖴𝖲𝖧𝖨𝖭𝖣𝖨𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝖦𝖤𝖮𝖥𝖱𝖤𝖸 𝖣𝖨𝖲𝖬𝖠𝖲𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 01ᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.....Jamaa mmoja kwa jina la Martin Okafor aliyetokea k...
23/04/2025

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: 𝖩𝖠𝖱𝖨𝖡𝖴 𝖫𝖠 𝖴𝖲𝖧𝖨𝖭𝖣𝖨
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝖦𝖤𝖮𝖥𝖱𝖤𝖸 𝖣𝖨𝖲𝖬𝖠𝖲
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 01

ᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.....

Jamaa mmoja kwa jina la Martin Okafor aliyetokea katika familia duni, alifanikiwa kumaliza elimu ya msingi kwa taabu na kufaulu vizuri kisha akaenda Sekondari kwa msaada wakanisa, ambako alifanya vizuri sana. Kanisa lilimfadhili katika elimu ya juu ambako alifaulu na kuwa msanifu majengo. Alifanya kazi kwa muda wa miaka kumi katika kampuni moja na baadae nwajiri wake alifurahishwa sana na nidhamu, kujituma kwake, uaminifu wake, namna alivyoongoza wenzake, ucha MUNGU.

Siku moja alimuita ofisini kwake, “Naam bosi nimesikia unaniita.” Martin aliitikia wito wa bosi wake.
“Ndiyo Martin, unaendeleaje na kazi?” Bosi wake mzee wa miaka 70 lakini ukimtazama ubaweza sema anamiaka 45 tu!
“Salama tu bosi, mafanikio ni makubwa.” Akijibu Martin huku akionesha tabasamu lake ambalo mara nyingi hulitumia katima majadiliano ya kibiashara.
“Vizuri, sasa Martin nimekuita hapa kuna jambo moja nataka kuongea na wewe…Umefanya kazi kwa muda wa miaka 10 sasa, tangu umekuja nimeona mafanikio makubwa sana katika kampuni yangu, nimepata faida kubwa ya kifedha lakini pia kuwa na wateja wengi hadi kampuni inazidiwa, yote hii ni kwa ajili ya ufanisi wako wa kazi iliotukuka ambao umewaambukiza hata wafanyakazi wengine, Asante sana Martin!” Bosi wake Martin alimshukuru Martin.

“Asante bosi wangu, sehemu hiyo ni sehemu tu ya utendaji kazi wangu na utekelezaji wa majukumu yangu.” Alijibu Martin huku akitabasamu. Kwake yeye pongezi na shukrani alizizoea sana ila siku hiyo ilikuwa tofauti na yeye aligundua hulo. Alihisi pengine anapandishwa cheo,
“Sasa, kutokana na utumishi wako uliotukuka, nimeonelea nikupatie kitu kidogo k**a sehemu ya shukrani yangu kwako…” Bosi wake Martin alitoa hundi aliyoitayarisha kwa muda mrefu.
“Bosi….” Martin hakuamini alichokiona, ilikuwa ni hundi ya dola za kimarekani milioni moja na nusu (USD 1,500, 000).
“Ndiyo Martin umeiheshinisha kampuni yangu, nami nakuzawadia kiasi hicho cha fedha k**a mtaji wa kuanzia, katengeneze biashara yako mwenyewe, nataka nikuone ukitumia uwezo wako na kipaji Mungu alichokujalia kutimiza ndoto zako.” Boss alimueleza Martin.
Kwa furaha aliyokuwa nayo Martin alishindwa kujizuia, alilia kwa furaha aliyokuwa nayo, hakuamini kile kinachomtokea.

Martin akafungua kampuni yake ndogo ya ujenzi na Kutokana na bidii yake ya kazi, uaminifu na kumaliza kazi kwa wakati, alipata tenda nyingi sana za watu binafsi, makampuni na hata kujenga miradi mbalimbali ya kiserikali. Miaka mitano baadae alikuwa amefanikiwa kwa kiasi kikubwa na kampuni yake ilikuwa inajulikana sana. Miezi michache baadae alikutana na binti aitwaye Annabelle Ike, walipendana na kisha kufunga ndoa na mwaka mmoja baadae wakapata mtoto wa k**e waliyemuita Ritha.

Wakati wote waliishi kwa furaha sana, Martin aliipenda familia yake sana na alifanya kila aliloweza kuhalikisha kuwa wakati wote anatimiza majukumu yake k**a mume na baba katika familia yake.
Ritha alifika umri wa kwenda shule, Martin alibeba jukumu la kuhakikisha kuwa binti yao anapata elimu bora. Pamoja na kazi nyingi alizokuwa nazo Martin, kamwe hakuacha kutenga muda wa kukaa binti yake kumsaidia kazi za shule kuongea naye ili kujua anakutana na changamoto gani.

Ninabell mke wa Martin na mama wa Ritha, siku zote alijiona ni k**a amepewa upendeleo kuwa na mwanaume k**a Martin. Ritha alikuwa akifanya vizuri sana shuleni, Martin alijivunia sana kuwa na binti huyo. Ritha alianza sekondari kidato cha kwanza ufaulu wake k**a ilivyokuwa shule ya msingi. Alipofika kidato cha 2 alifanya mtihani wa taifa uliokuwa kipimo cha kwenda kidato cha tatu, Ritha alifanya vizuri sana.

Alimpelekea matokeo baba yake, Mr. Martin ambaye alifutahishwa sana na matokeo yale, “Ooh! My Angel, ninajivunia sana wewe binti yangu…..Una A ngapi….1, 2, 3, 4, 5, 6…Dah! Am proud of you my Angel” Martin alimpingeza mwanaye.
“Am proud of you too dady…” Ritha alimwambia baba yake kwa sauti ya kudeka
“Umemuonesha mama yako?” Martin alimuuliza mwaye k**a kamuonesha matokeo yale mama yake.
“Hapana baba, yuko chumbani kwake…” Ritha alijibu huku akichukua matokeo yake kwa baba yake.
“Okey nenda kamuoneshe mama atafurahi sana.”
“Asante baba…” Ritha akajibu kisha akaanza kupiga hatua kuelekea chumbani kwa mama yake, mara akakumbuka kitu.
“Baba leo utanipeleka cinema?” Ritha alimuuliza baba yake ikiwa ni ahadi aliyopewa na baba yake kabla hajafanya mtihani wa taifa.
“Oooh! Yeah lazima twende na umwambie mama yako leo ajiandae leo usiku tutakwenda Cinema kuna filamu mpya ya Ken Eric na Yul Edochie waigizaji mnaowapenda”
“Asante baba, nakupenda”

ɪᴛᴀᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.......

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: UTATA: Nani muuaji?𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney 𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 01Ni majira ya saa 7 mchana  katika jiji la Arusha nc...
10/03/2025

𝐇𝐀𝐃𝐈𝐓𝐇𝐈: UTATA: Nani muuaji?
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: Geofrey Dismas Leogney
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 01

Ni majira ya saa 7 mchana katika jiji la Arusha nchini Tanzania, kila mmoja akiendelea na shughuli zake za kila siku. Jua na mawingu kila moja lijipambana kuchukua nafasi katika jiji hilo maarufu Afrika na Duniani wenyewe wanaliita Geneva of Afrika. Katika kiwanda cha kutengeneza madawa ya binadamu kiitwacho Lds Phamathetical Industry hali ilikuwa ni tofauti, nitakueleza baadae.

Kwanza unatakiwa kujua kuwa kwa miaka hiyo, kiwanda hiki kilikuwa maarufu kwa ubora wa madawa yake. Kiwanda hiki kilijijengea jina kubwa ndani na nje ya mipaka ya bara la Afrika kutokana na ubora wa madawa yaliyokuwa yanazalishwa na kiwanda hicho na kwa kutoa ajira kwa maelfu ya watu katika eneo hilo. Hata hivyo, siku moja, tukio baya lilitokea na kusababisha mshtuko mkubwa kwa wafanyakazi na hata mkoa wa Arusha kwa ujumla wake. K**a ujuavyo taarifa inapotoka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine inapofika kwa mtu wa pili huwa inafika ikiwa imeongezewa chumvi ili story inoge. Mtu wa pili naye akiipeleka kwa mtu wa tatu huwa anaipeleka akiongezea maneno mengine ili inoge zaidi, hivyo ndivyo ilivyokuwa kwenye taarifa hii ya kifo katika kiwanda hicho na kufanya kutokee taharuki kubwa sana kwenye mkoa huo na nje ya mkoa huo.

Tukio hili lilikuwa ni tukio la kifo cha mfanyakazi wa kiwanda hicho aliyeitwa Amiri Hassan Mgunya, mtaalamu wa kemia ndani ya maabara ya kiwanda hicho. Taarifa za kifo chake zilitolewa na mfanyakazi mwenzake aliyeitwa Suzan Andrew Msangi ambaye naye alikuwa ni mtaalamu wa katika maabara hiyo. Siku hiyo alikuwa ni mtu wa kwanza kufika kiwandani hapo kwa watu wanaofanya kazi ndani ya maabara hiyo.

Alipoingia alikuta taa zimewashwa isivyokawaida ya eneo hilo kwakuwa wanapoondoka huwa wanazima taa na ndivyo walivyofanya hata wakati wanaondoka. Kingine kilichomshangaza ni kuwa kulikuwa na mazingiera ya uharibifu k**a kulikuwa na mapambano kwani kulikuwa na uharibifu wa vifaa mbalimbali eneo hilo. Akiwa anaendelea kusogea sogea, alikutana na kitu kilichomsh*tua zaidi, damu! “Mungu wangu” alijikuta akitamka kwa mshangao aliposogea mbele zaidi aliona mwili wa mtu, alipokaribia zaidi aligundua ulikuwa ni mwili wa Amiri. “Mungu wangu! Amiri” alitamka tena.

Alipomtazama aliona mwili wake ukiwa na jeraha la risasi ambayo ilipigwa kwa nyuma na kutokezea mbele ya kifua chake. Alikimbia haraka kwenda nje kutafuta msaada, alikutana na mlinzi ambaye alishangaa kumuona akija mbio mbio. “Madamu kulikoni mbona mbiombio?” Mlinzi aitwaye Joram alimuuliza.
“Ni Amiri njoo haraka…” Suzan hakusubiri swali la Mlinzi Jorum, haraka aligeuza kukimbia ndani na mlinzi naye alifuata. Walipofika alishangaa kumuona Amiri akiwa amelala sakafuni aligumdua kuwa ni mwili tu ndoyo ulikuwa pale sakafuni lakini hakukuwa na uhai kwenye mwili huo. “Umemgusa?” Jorum aliuliza.
“Hapana!” Suzan akajibu huku machozi yakiwa yameanza kumtoka.

𝑰𝒕𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂.......

27/07/2024

Address

Magegele

59122

Telephone

+255768465103

Website

https://podcasters.spotify.com/pod/show/hadithizetu, https://www.selar.co/m/hadithiz

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hadithi Zetu:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share