Hadithi Zetu

Hadithi Zetu ᴋᴀʀɪʙᴜ sᴀɴᴀ ᴋᴀᴛɪᴋᴀ ᴍᴀᴋᴛᴀʙᴀ ʏᴀ ʜᴀᴅɪᴛʜɪ. ᴜᴋᴜʀᴀsᴀ ʜᴜᴜ ɴɪ ᴍᴀᴀʟᴜᴍᴜ ᴋᴡᴀ ᴋᴀᴢɪ ᴢᴀ ғᴀsɪʜɪ & ᴍᴀᴋᴀʟᴀ ᴍʙᴀʟɪᴍʙᴀʟɪ. Pia, tunatoa makala mbalimbali kwenye ukurasa wetu.

Hadithi Zetu ni ukurasa wa Facebook ambao una lengo la kuchapisha kazi za fasihi andishi, simulizi, na makala mbalimbali. Ukurasa huu umeundwa ili kuhuisha na kueneza urithi wa hadithi na tamaduni za Kiafrika kupitia njia ya maandishi. Tunajitahidi kuwa jukwaa la kuelimisha, kuburudisha, na kuhamasisha wengine kwa njia ya hadithi. Kwenye ukurasa wetu, utapata aina mbalimbali za kazi za fasihi andi

shi, ikiwa ni pamoja na hadithi za kusisimua, mashairi, riwaya fupi, na tamthilia. Tunajitahidi kuchapisha kazi zenye ubora na zinazogusa masuala mbalimbali yanayohusiana na jamii, utamaduni, upendo, mazingira, na masuala mengine ya kijamii. Mbali na kazi za fasihi andishi, tunatoa pia simulizi mbalimbali za kuvutia. Hizi ni hadithi za kusisimua, za kuburudisha, na zenye kuelimisha. Simulizi zetu zinaweza kuwa za kisasa au za jadi, zinazohusisha wahusika wenye maisha ya kuvutia na matukio ya kusisimua. Lengo letu ni kutoa burudani na kuwafanya wasomaji wetu kujisikia kushiriki katika ulimwengu wa hadithi. Makala hizi zinajadili mada mbalimbali za kijamii, utamaduni, sanaa, na masuala mengine yanayohusiana na fasihi na simulizi. Tunazingatia kutoa taarifa sahihi na za kuvutia ili kuhamasisha majadiliano na kuelimisha wasomaji wetu. Tunakaribisha wanachama wote wa jamii kuungana nasi kwenye ukurasa wetu wa Facebook, Hadithi Zetu. Tunahimiza ushiriki wa wadau wa fasihi, waandishi, wasomaji, na wapenda hadithi katika kuchangia kazi zao, kutoa maoni, na kushiriki maarifa na uzoefu wao. Tunatumai kuwa Hadithi Zetu itakuwa sehemu ambayo itawawezesha watu kugundua, kuelimika, na kufurahia upekee wa hadithi za Kiafrika na tamaduni zetu. Karibu sana kujiunga na jumuiya yetu na kushiriki katika uumbaji wa hadithi za kuvutia na za kuelimisha.

Inaendelea......Polisi walifika ndani ya dakika 30, wakiongozwa na Inspector Mary Christian, mpelelezi wa mkoa wa Arusha...
19/11/2025

Inaendelea......

Polisi walifika ndani ya dakika 30, wakiongozwa na Inspector Mary Christian, mpelelezi wa mkoa wa Arusha. Alitizama eneo la tukio kwa macho makali.

“This isn’t just murder. This is surgical execution.”

Inspector Mary alikuwa ni moja ya maafisa wa askari maridadi na wenye uwezo mkubwa sana katika jeshi la polisi. Alipta mafunzo katika vyuo mbalimbali ndani ya bara la Afrika na hata nje ya nchi. Ni afisa pekee ambaye alipata nafasi ya kufanya kazi kwenye idara ya polisi ya mji wa Los Angel (LAPD). 

 

UKWELI ULIOJIFICHA

Katika uchunguzi wa uliofanyanyika, hakukua na alama za kuvunjwa kwa mlango

Kamera za CCTV zilitumiwa kifaa cha “blackout EMP”,  “hakuna rekodi yoyote, hawa washenzi walikuwa wamejipanga.” Alijisemea Inspector Mary.

Rehema alikuwa ameanza kuchunguza dawa mpya ya sumu ya silaha za kijeshi. Awali uchunguzi huu ulipingwa na wataalamu wengine kutoka nje ya nchi lakini serikali ya Tanzania walijidhatiti kuhakikisha mpango huo muhimubunaendelea.

Jambo la ajabu zaidi, faili lote la utafiti wa Rehema lilikuwa limefutwa kutoka kwenye kompyuta na backups zilikuwa zimeharibiwa kimfumo.

***

Njiro, Arusha – saa 12:00 jioni

Mvua iliacha kunyesha. Inspector Mary alisimama mbele ya mwili wa Rehema.

“We're dealing with professionals. Cold-blooded killers,” alisema kwa sauti ya chini.

Kilichosalia ni maswali zaidi ya majibu.

 

 KIVULI CHA ZAMANI – DAR ES SALAAM

 

Dar es Salaam – Makao Makuu ya Polisi – Saa 3:11 asubuhi

Kamanda Nasoro Mtei aliingia ofisini akiwa amechelewa kwa dakika tano. Si kawaida yake. Alikuwa mtu wa muda, mwenye mazoea ya kijeshi tangu enzi zake Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kambi ya Ruvu. Lakini leo hakuamka mapema. Ndoto ya usiku iliyomhusu mkewe aliyefariki miaka mitatu iliyopita bado ilimzidi nguvu. Alijikuta amekaa kitandani kwa dakika 20 akitafakari maisha.

Ofisi yake ilikuwa imepangwa kwa ustadi. Ubao wa whiteboard ulioandikwa kwa maandishi mekundu na meusi ya uchunguzi wa utekaji wa mwaka jana bado ulikuwepo.

Inaendelea Kwenye Channel yetu gusa Link kwa Bio

Habari! 🎉Karibu kwenye Modea Store – Viatu kwa bei ya Jumla.Hapa utapata viatu vya bei nafuu sana kwa oda za jumla, ofa ...
18/11/2025

Habari! 🎉
Karibu kwenye Modea Store – Viatu kwa bei ya Jumla.
Hapa utapata viatu vya bei nafuu sana kwa oda za jumla, ofa za kila wiki, na bidhaa mpya kila siku. 👟📦

Jiunge na group letu hapa 👇
👉 https://chat.whatsapp.com/KQWyunvOVuoK2xBSUKflcD

Karibu sana! 😊

KIJANA SAMSON:"Upendo ni jambo la ajabu, hauhitaji kelele ili kusikika, wala ushahidi mkubwa ili kuthibitisha uwepo wake...
17/11/2025

KIJANA SAMSON:

"Upendo ni jambo la ajabu, hauhitaji kelele ili kusikika, wala ushahidi mkubwa ili kuthibitisha uwepo wake. Mara nyingi, hukaa kimya ndani ya moyo na kupiga taratibu, lakini kwa uthabiti ambao hauwezi kufananishwa na kitu chochote.

Kuna nyakati moyo humkumbuka mtu wake hata k**a dunia imekuwa kimya. Huo si udhaifu, bali ni uwezo wa kupenda kwa kina zaidi ya maneno. Ni k**a upepo unaobeba harufu ya mahali unapotamani kurudi, hauonekani, lakini unaeleweka.

Naamini kuwa kila upendo wa kweli una njia yake ya kurudi. Una uvumilivu wake, upekee wake, na muda wake maalum. Wakati mwingine watu hukaa mbali, lakini hisia zao hubaki karibu. Wakati mwingine maongezi hushuka, lakini ukaribu wa mioyo haukatiki.

Hivyo, katika kila kimya kinachopita, bado naamini. Kwa sababu moyo unaotuma upendo kwa dhati, hauko peke yake, upendo huo hutafuta, huona, na hatimaye hupata mahali pake pa kustarehe.

Mimi nipo hapa, nikiwa na moyo ulio tayari kupenda kwa utulivu, kwa uaminifu, na kwa uzuri wake wote."

📢 TUNAUZA KWA JUMLA NA REJAREJA💃 Bidhaa za urembo & fashion kwa bei nafuu sana!✨ Ubora wa hali ya juu, huduma ya uhakika...
16/10/2025

📢 TUNAUZA KWA JUMLA NA REJAREJA
💃 Bidhaa za urembo & fashion kwa bei nafuu sana!
✨ Ubora wa hali ya juu, huduma ya uhakika.

🚚 Tunatuma mikoa yote — gharama za usafiri ni za mteja.
🤝 Uaminifu wetu ni 100% 💯

📞 Wasiliana nasi sasa:
📱 0768 465 103 (WhatsApp ipo)

😂😂😂😂😂😂
04/10/2025

😂😂😂😂😂😂

𝑰𝒍𝒊𝒑𝒐𝒊𝒔𝒉𝒊𝒂.....Moyo wake ulianza kudunda kwa kasi. Mvua ilianza kunyesha kwa nguvu zaidi maana tayari kuliuwa na kimvua ...
16/09/2025

𝑰𝒍𝒊𝒑𝒐𝒊𝒔𝒉𝒊𝒂.....

Moyo wake ulianza kudunda kwa kasi. Mvua ilianza kunyesha kwa nguvu zaidi maana tayari kuliuwa na kimvua cha rasharasha. Kivuli kile kilijificha tena. Daudi alipiga hatua tatu mbele, Bila tahadhari, mara mlio ulisikika kwa sauti ya chini Phhhhh!

Risasi iliyotoka kwenye bastola yenye silencer ilipenya upande wa kulia wa shingo yake, ikikatiza mishipa muhimu ya damu. Alitetemeka kidogo, kisha akaanguka chini kimya.

𝑺𝒂𝒔𝒔 𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂....

Mhalifu wa Kimya

Aliyehusika hakuwa mtu wa kawaida. Alivaa suti ya mvua ya kijeshi (tactical rain suit), na usoni aliweka barakoa ya usiku (thermal face mask). Bunduki aliyotumia ni SIG Sauer P226 Suppressed, bastola yenye uwezo wa kulenga kwa ukamilifu hadi mita 30 bila kutoa sauti hata kidogo.

Aliingia kwenye maabara kuu kwa kutumia keycard feki aliyotengeneza kutoka kwenye taarifa za ndani. Ndani ya chumba cha sumu, Dk. Rehema Yusuf alikuwa ameinama kwenye darubini ya kisasa, akiandika matokeo ya majaribio yake.

Hakuweza hata kusikia mlango ukifunguliwa – lakini alipoangalia kwenye kioo cha chumba, aliona mwanga wa mtu akikaribia.

“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.

Mtu hakujibu. Alimsogelea, akamk**ata kwa kasi, akampiga ganzi kwa sindano ya midazolam, akamvuta hadi sakafuni.

Kisha kwa kutumia sindano nyembamba, aliingiza potassium chloride kwenye mishipa yake ya mkono wa kushoto. Dawa hiyo, ikizidi kiasi, husababisha msh*tuko wa moyo ndani ya sekunde 45.

Rehema alikufa macho yakiwa wazi, mdomo wake ukiwa wazi k**a aliyekuwa anaomba msaada.

Taarifa Za Kifo

Asubuhi yake, mwili wa Daudi uligunduliwa na mlinzi wa mchana, Juma Kandoro, ambaye kwa kawaida huwa anaingia kazini saa moja asubuhi lakini siku hiyo aliwahi kidogo, saa 12 alikuwa ameshatia timu. Alishangaa kuona Daudi amelala chini na bado  bastola  kaye ikiwa mikononi mwake. Alipochunguza ndani ya maabara, alikuta damu ndogo kwenye sakafu na mwili wa Dk. Rehema akiwa amelala upande mmoja, macho yametumbua.

Simu ya dharura ilipigwa mara moja, “Hapa ni BioPharma Arusha! Tuna vifo viwili! Mlinzi na daktari wa maabara! Tafadhali njooni haraka!”

𝑰𝒕𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂......

゚viralシ

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒SEHEMU: 04𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......"Mauaji mengine. Daktari mwingine wa kiwanda cha ...
16/09/2025

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎
MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒
SEHEMU: 04

𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......

"Mauaji mengine. Daktari mwingine wa kiwanda cha dawa. Mji wa Malampaka. Walakini hakuna dalili za uhalifu wa kawaida. Ni mtaalamu mwingine wa sumu.”
Subira alimtazama Kamanda wake kwa mshangao, “Sir… they’re striking again.”
“Two attacks within 12 hours. This is coordinated.”
Kamanda Nasoro alibana meno, kisha akasema kwa sauti ya amri:
“Cancel Dar. Tuelekee moja kwa moja Arusha. Tuwahishe Simiyu timu ya pili. This is no longer a local murder case. We’re dealing with a serial killer, or worse… an organization.”

𝑺𝑨𝑺𝑨 𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨.............

ARUSHA – NJIRO – SAA 10:15 JIONI

Walipofika eneo la tukio, walikuta Inspector Mary akiwa ameweka kambi. Alikuwa ameshaweka mkanda wa Kamandaa usalama (crime scene tape) kuzunguka eneo lote. Maiti za Daudi na Dk. Rehema tayari zilikuwa zimeondolewa, lakini damu iliyo kwenye sakafu na athari za sindano kwenye mkono wa Rehema zilikuwa bado freshi.

Subira alichuchumaa karibu na sakafu, “Injection mark is clean. Straight to the vein. Whoever did this, alijua anachofanya.”
Kamanda Nasoro alichukua picha ya bastola ya Daudi aliyokuwa ameshikilia mpaka mwisho wa maisha yake, “Hii bastola ilikuwa loaded?”
“Ndiyo. Risasi zote 12 bado zipo. Hakuweza hata kupiga moja.”
Nasoro alitazama kamera za CCTV zilizozimwa kwa EMP.
“This is tactical. They planned this for weeks. Kila hatua imepangwa. They don’t just want these scientists dead, wanataka kazi zao zipotee kabisa.”

FILE LA KESI – “PROJECT SALAAM”

Baada ya uchunguzi wa awali, Subira alipata nyaraka zilizoonesha kuwa Dk. Rehema alikuwa sehemu ya mradi wa siri wa serikali unaoitwa “Project Salaam”. Mradi huo ulikuwa unahusu utafiti wa dawa zinazoweza kudhibiti silaha za kemikali, hasa kwa ajili ya ulinzi wa taifa dhidi ya mashambulizi ya kigaidi.
Kitu cha kushangaza zaidi? Dk. Rehema alikuwa akishirikiana na Dk. Hamza Rajabu, yule aliyekufa Simiyu.
Kamanda Nasoro alinyamaza kwa muda, macho yake yakitazama faili hilo, “This is bigger than I thought… Hawa watu hawauwi tu, wanazima utafiti mzima. Lazima kuna mtu mkubwa anawashika mkono.”

Kamanda Nasoro akajiapiza moyoni, “Sitapumzika hadi niwak**ate. Nikiwa hai au mfu.”
Lakini hakuwa anajua, mauaji haya yalikuwa tu mwanzo. Na mtego tayari ulikuwa umewekwa kwa ajili yake.

KIFO KIMYA – SIMIYU

Simiyu –Malampaka – Saa 6:42 usiku
Usiku ulikuwa mzito. Anga la kijiji cha Malampaka lilikuwa limetandwa na mawingu meusi, yasiyo na nuru hata ya mwezi. Barabara ya vumbi iliyopitia mbele ya nyumba ya Daktari Hamza Rajabu, mtaalamu wa utafiti wa molekuli katika kiwanda cha dawa cha Biogene Africa Ltd, ilikuwa kimya – si kawaida kwa maeneo haya ambayo watoto hupiga kelele hadi saa tatu usiku.

Ndani ya nyumba hiyo ya vyumba vitatu, kulikuwepo na uhai wa hatari. Saa 6:27 usiku, mtu asiyejulikana alivunja usalama wa milango ya elektroniki kwa kutumia kifaa cha kuvuruga security signal kinachojulikana k**a CodeJammer X90 – kifaa kinachotumika na maajenti wa kijasusi kudukua mifumo ya usalama ya majengo.
Mhalifu huyo aliingia kwa utulivu, akiwa amevalia sare ya kawaida ya kiwanda – madoadoa ya bluu na beji bandia ya kiwanda hicho. Bastola yake ilikuwa ya kimya, aina ya Walther PPK, maarufu kwa matumizi ya kijasusi tangu enzi za Vita Baridi.

Dkt. Hamza: Damu ya Mwanasayansi

Dk. Hamza alikuwa ameketi sebuleni akipitia faili la kidigitali lililokuwa limefungwa kwa password encryption. Alikuwa anachunguza taarifa za vifo vya wenzake wawili: Dk. Rehema Yusuf wa Arusha, na mtaalamu wa maabara wa Dar es Salaam aliyepotea wiki mbili zilizopita. Moyo wake haukuwa na amani.

Alishtuka kwa sauti ya kitu kilichoanguka jikoni. Kabla hajainuka, alisikia mlio mdogo k**a upepo – phhhh!
Risasi ya kwanza ilimgonga begani. Hakuweza kupiga kelele. Alijaribu kutambaa kuelekea mlango wa mbele, lakini mhalifu alimsogelea haraka na kumpiga sindano moja ya sumu ya sodium thiopental, ambayo humfanya mtu kupoteza fahamu ndani ya sekunde 15. Kisha akampiga sindano ya pili ya potassium chloride, iliyosababisha moyo wake kusimama kabisa.
Kabla hajaondoka, mhalifu huyo alichukua USB flash iliyokuwa mezani, ndicho kilichokuwa kinatafutwa.

Uchunguzi Wa Polisi – Usiku Uleule
Kufuatia taarifa ya majirani waliomsikia Hamza akigugumia, SP (Superintendent of Police) Samwel Kibwana, Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya ya Bariadi, aliwasili na timu yake saa 8:02 usiku. Aliongozana na ASP (Assistant Superintendent of Police) Khadija Musa, mtaalamu wa uchunguzi wa kisayansi wa vituo vya uhalifu (forensics).

ASP Khadija alipiga picha mwili wa Dk. Hamza, akatazama alama ya sindano mkononi.
“This is precision work. No signs of struggle, no broken locks. They knew him, or knew how to get in,” alisema huku akipiga picha kwa simu yake yenye app ya ballistic evidence capture.
SP Kibwana alichungulia chini ya meza na kuona casing moja ya risasi – .32 ACP, risasi maarufu kwa bastola za kijasusi, “Walther PPK. Bastola ndogo, kimya, deadly,” alisema.

Taarifa Kufika TISS – Mwanza
Saa mbili baadaye, tukio hilo liliripotiwa kwa Afisa Usalama wa Taifa Mkoa wa Simiyu, Senior Intelligence Officer (SIO) Abbas Kimario, aliyekuwa akifuatilia shughuli za kiwanda hicho kwa miezi miwili. Aliwasiliana na Makao Makuu ya Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) jijini Dodoma, na kutoa taarifa ya hatari, "Wataalamu wa viwanda vya dawa wanauawa kwa utaratibu unaoonyesha involvement ya majeshi au maajenti waliopitia mafunzo maalum ya ‘Black Ops’. Kuna uwezekano wa uvujaji wa siri za kitaifa."

Mpango wa Kitaifa Wa Kuzuia Mauaji Zaidi
Kutoka Arusha, ACP (Assistant Commissioner of Police) Nasoro Mtei alipokea taarifa hizo akiwa bado eneo la mauaji ya Rehema. Alisimama kimya kwa dakika moja kabla hajageuka kwa Detective Subira Hassan, aliyekuwa akipanga picha za CCTV zilizokuwa corrupted, “Prepare a report to IG’s office. Tuweke suala hili chini ya ‘Operation Mauti Kimya’ – a joint task force between TISS, CID na JWTZ,” alisema Nasoro, “Yes, sir,” Subira alijibu kwa ukaidi wa kazi.

Silaha, Mbinu na Njama

Taarifa kutoka kwa SIO Abbas zilionyesha kwamba mtu aliyemuua Dk. Hamza alitumia mbinu za kijeshi k**a vile, “Room Clearing” – kusafisha chumba kwa utaratibu wa haraka bila kugusa vitu.
“Needle kill” – mbinu ya kutumia sindano kimya kwa kudunga mishipa mikuu.
“EMP Jammer” kuvuruga CCTV na mitandao ya ndani.
Taarifa hizo zilipelekea kuamini kuwa huu haukuwa mhalifu wa kawaida bali mtu aliyepitia mafunzo ya kijasusi, au labda ni afisa wa zamani wa vikosi maalum.

****
Kufikia saa kumi alfajiri, vifo vitatu vya wanasayansi waliojikita katika utafiti wa dawa vilikuwa vimegusa mikoa mitatu tofauti ndani ya masaa 24: Arusha, Simiyu na Mwanza.
Kamanda Nasoro alitazama ramani ya Tanzania, akawasha red marker. Alichora mstari kutoka Arusha hadi Mwanza, kupitia Simiyu, akasema, “They’re moving in a pattern. Naona wanalenga sehemu fulani. But what’s the next target? Dodoma? Dar?”
Subira alitazama faili la “Project Salaam,” macho yake yakiwa hayapepesi.
“Sir… If the pattern holds, the next victim is in Dodoma. And he’s still alive.”

𝑰𝑻𝑨𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨.......

📌Hongera sana brother  unazidi kutuwakilisha vyema huko.
15/09/2025

📌Hongera sana brother unazidi kutuwakilisha vyema huko.

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒SEHEMU: 02𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.Mtu hakuji...
08/09/2025

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎

MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒

SEHEMU: 02
𝑰𝑳𝑰𝑷𝑶𝑰𝑺𝑯𝑰𝑨......

“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.
Mtu hakujibu. Alimsogelea, akamk**ata kwa kasi, akampiga ganzi kwa sindano ya midazolam, akamvuta hadi sakafuni.
Kisha kwa kutumia sindano nyembamba, aliingiza potassium chloride kwenye mishipa yake ya mkono wa kushoto. Dawa hiyo, ikizidi kiasi, husababisha msh*tuko wa moyo ndani ya sekunde 45.
Rehema alikufa macho yakiwa wazi, mdomo wake ukiwa wazi k**a aliyekuwa anaomba msaada.

𝑺𝑨𝑺𝑨 𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨.....

Taarifa Za Kifo

Asubuhi yake, mwili wa Daudi uligunduliwa na mlinzi wa mchana, Juma Kandoro, aliyeshangaa kuona bastola ya Daudi ikiwa bado mikononi mwake. Alipochunguza ndani ya maabara, alikuta damu ndogo kwenye sakafu na mwili wa Dk. Rehema akiwa amelala upande mmoja, macho yametumbua.

Simu ya dharura ilipigwa mara moja, “Hapa ni BioPharma Arusha! Tuna vifo viwili! Mlinzi na daktari wa maabara! Tafadhali njoo haraka!”
Polisi walifika ndani ya dakika 30, wakiongozwa na Inspector Mary Christian, mpelelezi wa mkoa. Alitizama eneo la tukio kwa macho makali.
“This isn’t just murder. This is surgical execution.”

UKWELI ULIOJIFICHA

Katika uchunguzi wa awali:

Hakuna alama za kuvunjwa kwa mlango
Kamera za CCTV zilitumiwa kifaa cha “blackout EMP” – hakuna rekodi
Rehema alikuwa ameanza kuchunguza dawa mpya ya sumu ya silaha za kijeshi
Jambo la ajabu zaidi, faili lote la utafiti wa Rehema lilikuwa limefutwa kutoka kwenye kompyuta na backups zilikuwa zimeharibiwa kimfumo.

Njiro, Arusha – saa 12:00 jioni
Mvua iliacha kunyesha. Inspector Mary alisimama mbele ya mwili wa Rehema.
“We're dealing with professionals. Cold-blooded killers,” alisema kwa sauti ya chini.
Kilichosalia ni maswali zaidi ya majibu.

KIVULI CHA ZAMANI – DAR ES SALAAM

Dar es Salaam – Makao Makuu ya Polisi – Saa 3:11 asubuhi

Kamanda Nasoro Mtei aliingia ofisini akiwa amechelewa kwa dakika tano. Si kawaida yake. Alikuwa mtu wa muda, mwenye mazoea ya kijeshi tangu enzi zake Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kambi ya Ruvu. Lakini leo hakuamka mapema. Ndoto ya usiku iliyomhusu mkewe aliyefariki miaka mitatu iliyopita bado ilimzidi nguvu. Alijikuta amekaa kitandani kwa dakika 20 akitafakari maisha.

Ofisi yake ilikuwa imepangwa kwa ustadi. Ubao wa whiteboard ulioandikwa kwa maandishi mekundu na meusi ya uchunguzi wa utekaji wa mwaka jana bado ulikuwepo. Kamera ndogo ya CCTV ilikuwa imefungwa juu ya ukuta wa kushoto, na mezani kulikuwa na bastola yake ya kawaida – G***k 17 Gen5, bastola iliyotumika sana na maofisa wa upelelezi duniani kote, yenye risasi 17 kwenye magazini, rahisi kutumia na sahihi hata katika mapigano ya karibu.

Alipokaa, simu yake ya mezani ikaita, “Kamanda Nasoro, kuna tukio la mauaji Arusha. Wamekufa watu wawili – mlinzi na daktari wa sumu. Mauaji ni ya kimya sana, hakuna dalili za uvamizi,” ilisema sauti ya Detective Subira Hassan, mpelelezi wake wa karibu.
Nasoro alikunja nyuso, “Arusha? Daktari wa sumu?” alirudia, kisha akainuka na kusimama mbele ya dirisha kubwa lililokuwa linaangalia bahari ya Hindi.
Subira aliendelea, “Na faili lake la kazi limefutwa. Kuna ushahidi mdogo sana, lakini hii staili ya mauaji inafanana na ile kesi ya miaka miwili iliyopita… ile ya ‘Mtengeneza Sumu wa Tabata’.”
Kamanda alitulia, akashika kidevu chake, “I thought we buried that case…”
“So did I. But this feels like a continuation. Au copycat killer.”
Aliisogelea bastola yake, akaichukua taratibu na kuiweka kwenye koti lake la suti ya kijivu, “Prep the case files. Book two seats to Arusha. Tuna kazi.”

****

SAA 7:45 MCHANA – UWANJA WA NDEGE – JULIUS NYERERE

Nasoro na Subira walikuwa tayari kupanda ndege ya Shirika la Precision Air. Kabla hawajaondoka, Subira alipokea ujumbe kwenye simu yake ya mkononi kutoka kwa Detective Samwel Kibwana wa kanda maalumu ya kipolisi, Simiyu.
“Mauaji mengine. Daktari mwingine wa kiwanda cha dawa. Mji wa Malampaka. Walakini hakuna dalili za uhalifu wa kawaida. Ni mtaalamu mwingine wa sumu.”
Subira alimtazama Kamanda wake kwa mshangao, “Sir… they’re striking again.”
“Two attacks within 12 hours. This is coordinated.”
Kamanda Nasoro alibana meno, kisha akasema kwa sauti ya amri:
“Cancel Dar. Tuelekee moja kwa moja Arusha. Tuwahishe Simiyu timu ya pili. This is no longer a local murder case. We’re dealing with a serial killer, or worse… an organization.”

𝑰𝑻𝑨𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨...........

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎MTUNZI:  𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒SEHEMU: 01MAAFA YA NJIRO – ARUSHAArusha, Tanzania – Mtaa wa Njiro – Saa 3:...
04/09/2025

HADITHI: 𝐌𝐋𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐅𝐎

MTUNZI: 𝐆𝐄𝐎𝐅𝐑𝐄𝐘 𝐃𝐈𝐒𝐌𝐀𝐒

SEHEMU: 01

MAAFA YA NJIRO – ARUSHA

Arusha, Tanzania – Mtaa wa Njiro – Saa 3:07 usiku.
Baridi ya jiji la Arusha ilikuwa imekithiri kiasi kwamba hata mbwa waliokuwa wakirandaranda mitaani walikuwa wamejibanza chini ya magari yaliyokuwa yameegeshwa kandokando ya barabara. Mvua nyepesi ilikuwa ikinyesha kwa kasi isiyo na sauti nyingi, ikiambatana na upepo uliotoka maeneo ya mlima Meru.
Katika kando ya mtaa huo wa Njiro, kulikuwepo na majengo makubwa ya Tanzania BioPharma Ltd, moja ya makampuni yanayoongoza kwa kutengeneza dawa za kupambana na magonjwa ya mlipuko. Kiwanda hicho kilihifadhi baadhi ya kemikali adimu ambazo zilihitaji ulinzi wa hali ya juu lakini usiku huu, hali ilikuwa tofauti.

Mlinzi wa usiku, Daudi Mshana, alikuwa na miaka 52, mstaafu wa Jeshi la Wananchi. Alivaa koti la kijeshi la zamani, suruali ya rangi ya kaki, na viatu vilivyokuwa vimechakaa kwa miaka ya huduma. Mikononi mwake, alibeba bastola aina ya Ta**us G2C, yenye risasi 12 ndani ya magazini. Bastola hiyo ndogo lakini ya kuaminika ilimsaidia kujihami nyakati za hatari, japo kwa miaka mitano hakuwahi kulazimika kuitumia. Hii ilimfanya asiwe na wasiwasi hasa anapokuwa eneo lake la lindo ijapokuwa utulivu wa kia siku haukumfanya kupoteza umakini.

Tochi aliyokuwa amevaa kichwani ilikuwa ikitoa mwangaza hafifu. Alipita kwenye lango kuu la maegesho ya magari, akapita mbele ya jengo la maabara. Usiku huu kulikuwa na ukimya usio wa kawaida. Wafanyakazi wa usiku waliokuwa maabara walikuwa wachache miongoni mwao ni Dk. Rehema Yusuf, mtaalamu wa sumu (toxicologist) aliyekuwa akifanya uchunguzi juu ya dawa mpya ya kuzuia sumu ya sarin inayotumika vitani.

Katikati ya doria yake, Daudi aliona kivuli kikisogea kwa kasi nyuma ya tanki kubwa la kuhifadhia kemikali.
“Heeeh! Nani huyo?” sauti yake ilivuma kwa ukali, mikono ikishika bastola tayari. Hakujibiwa.
Akasogea taratibu, macho yake yakiwa makini. Moyo wake ulianza kudunda kwa kasi. Mvua ilianza kunyesha kwa nguvu zaidi maana tayari kuliuwa na kimvua cha rasharasha. Kivuli kile kilijificha tena. Daudi alipiga hatua tatu mbele, Bila tahadhari, mara mlio ulisikika kwa sauti ya chini Phhhhh!
Risasi iliyotoka kwenye bastola yenye silencer ilipenya upande wa kulia wa shingo yake, ikikatiza mishipa muhimu ya damu. Alitetemeka kidogo, kisha akaanguka chini kimya.

****
Mhalifu wa Kimya

Aliyehusika hakuwa mtu wa kawaida. Alivaa suti ya mvua ya kijeshi (tactical rain suit), na usoni aliweka barakoa ya usiku (thermal face mask). Bunduki aliyotumia ni SIG Sauer P226 Suppressed, bastola yenye uwezo wa kulenga kwa ukamilifu hadi mita 30 bila kutoa sauti hata kidogo.
Aliingia kwenye maabara kuu kwa kutumia keycard feki aliyotengeneza kutoka kwenye taarifa za ndani. Ndani ya chumba cha sumu, Dk. Rehema Yusuf alikuwa ameinama kwenye darubini ya kisasa, akiandika matokeo ya majaribio yake.

Hakuweza hata kusikia mlango ukifunguliwa – lakini alipoangalia kwenye kioo cha chumba, aliona mwanga wa mtu akikaribia.
“Who are you?” aliuliza kwa Kiingereza.
Mtu hakujibu. Alimsogelea, akamk**ata kwa kasi, akampiga ganzi kwa sindano ya midazolam, akamvuta hadi sakafuni.

Kisha kwa kutumia sindano nyembamba, aliingiza potassium chloride kwenye mishipa yake ya mkono wa kushoto. Dawa hiyo, ikizidi kiasi, husababisha msh*tuko wa moyo ndani ya sekunde 45.
Rehema alikufa macho yakiwa wazi, mdomo wake ukiwa wazi k**a aliyekuwa anaomba msaada.

𝑰𝒕𝒂𝒆𝒏𝒅𝒆𝒍𝒆𝒂........

Usiahau kutembelea page mpya ya










25/08/2025

nisapoti.com/Hadithizetu

🌟 HADITHI MPYA! 🌟"SMS YA MWISHO" – Hadithi ya kusisimua, kuhuzunisha na yenye mafunzo makubwa kuhusu maisha, mapenzi na ...
17/07/2025

🌟 HADITHI MPYA! 🌟
"SMS YA MWISHO" – Hadithi ya kusisimua, kuhuzunisha na yenye mafunzo makubwa kuhusu maisha, mapenzi na siri nzito zinazofichwa na ujumbe mmoja tu wa mwisho... 📱💔

🆓 Inapatikana BURE kabisa!
📲 Pakua sasa kupitia duka letu la Hadithi Zetu kwa Selar:
👉 https://selar.com/5m27a12576

Usikose simulizi hii ya kipekee ambayo imemgusa kila msomaji aliyeipata!

---

🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖
🔖

UTANGULIZIKatika dunia ya leo ya teknolojia na haraka ya maisha, upendo wa kweli unaonekana kuwa jambo adimu — jambo la hadithi. Lakini vipi k**a moyo mmoja unaweza kugusa mwingine bila hata kuonana? Vipi k**a ujumbe mmoja wa maandishi unaweza kuwa mwanzo wa mapenzi ya maisha?“SMS YA MWISHO” n...

Address

Magegele
Makambako
59122

Telephone

+255768465103

Website

https://podcasters.spotify.com/pod/show/hadithizetu, https://www.selar.co/m/hadithiz

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi Zetu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Hadithi Zetu:

Share