15/05/2025
𝐒𝐈𝐌𝐔𝐋𝐈𝐙𝐈: 𝑱𝑨𝑹𝑰𝑩𝑼 𝑳𝑨 𝑼𝑺𝑯𝑰𝑵𝑫𝑰
𝐌𝐓𝐔𝐍𝐙𝐈: 𝑮𝑬𝑶𝑭𝑹𝑬𝒀 𝑫𝑰𝑺𝑴𝑨𝑺
𝐒𝐄𝐇𝐄𝐌𝐔: 03
ɪʟɪᴘᴏɪsʜɪᴀ........
Martin alifika kazini baada ya dakika 20 na hakika na kuketi katika kiti chake. Alianza kutafakari mambo yaliyotokea nyumbani kwake mapema asubuhi, aliumia sana, alisikia sauti ndani mwake inamwambia, ‘You are not a Victim but a victor.’ Alistuka na kuketi vizuri kwenye kiti chake cha kiboss ofisini kwake, kisha akatabasamu. Akiwa bado katika tabasamu akasikia simu yake ya mezani inaita, akaipokea haraka, “Hallo, Mr. Martin hapa….”
“Ooh! Habari, unaongea na Dkt. Egube Ike, nimekupigia kukutaarufu kuwa niko tayari kufanya kazi na wewe na kwa kuanza nitakupatia mradi wa 2.5 Billion nahitaji mradi ukamilike kwa haraka sana.”
“Sir, are you serious?” Martin aliuliza kqa mshangao kwakuwa hakutarajia alichokisikia kwenye simu hiyo. Alifurahi na kumshukuru sana Dkt. Egube. Alimuita secretary wake na kumpa maelekezo na mara moja kazi ikaanza.
𝑺𝑨𝑺𝑨 𝑬𝑵𝑫𝑬𝑳𝑬𝑨......
Jioni alirudi nyumbani akiwa hoi na njaa pia, alimkuta mkewe anatazama television, alimsalimu mkewe lakini aliambulia msonyo wa karne akajiongeza mwenyewe kimya kimya hadi mezani ambako nako hakukuta chakula chochote licha ya kuacha pesa za kutosha. Alidhani pengine chakula kipo jikoni, alipofika alikuta kulikuwa na dalili kuwa kulipikwa lakini hakuna kilichobaki kwa ajili yake! Alitaka kwenda kumuuliza mkewe lakini akaona haitakuwa sawa kufanya hivyo na itasababisha ugomvi kitu ambacho hakutaka kitokee.
Alirudi sebleni ambako alichukua kibegi chake na kuingia ndani, akijitupa kitandani taratibu usingizi ukaanza kumnyemelea, hajutaka hilo litokee mapema hivyo, alioga na kisha kubadili nguo. Akachukua funguo za gari lake na kuelekea nje alikolipaki, aliingia na kisha kuondoka taratibu, akak**ata barabara iliyokuwa inaelekea mjini huku akisikiliza mziki wa injili toka kwa msanii maarufu nchini Nigeria. Alifika kwenye mataa na kusimama baada ya taa nyekundu kuwaka, baada ya dakika k**a moja taa ya kijani iliwaka naye akaweka gia ya kuondokea na kupinda kushoto hadi katika mgahawa maarufu F&J restaurant, mgahawa unaomilikiwa na ndugu wawili, aliagiza chalula apendacho na kisha baada ya dakika kadhaa akiwa anaendelea kula aliagiza chakula kingine kwa ajili ya mkewe, japo jikoni kulikuwa kuna dalili kuwa kulipikwa, aliamini pengine mkewe alimpikia mlinzi.
Alibeba kile chakula na kurejea nyumbani kwake, akimkuta mkewe bado anatazama television, hakutaka kuongea nae maneno mengi sana, akimuekea kile chakula mezani na kumwambia, “Mke wangu chakula chako kiko hapa mezani, usiku mwema.”
Mkewe wala hakujibu kitu na Martin alilizoea hilo kutoka kwa mkewe hivyo hakujisumbua sana.
Aliingia kulala na baada ya muda mkewe aliingia chumbani. Martin alikumbuka kuwa kuna habari njema hajamueleza mkewe hivyo ikabidi amueleze, “Mke wangu nimekumbuka kitu, leo nimepata contract ya 2.5 Billions…Mungu amekuwa mwema sana kwetu.” Martin alimueleza mkewe lakini badala yake alipokea msonyo ule ule wa karne kisha mkewe akavuta shuka lake na kugeukia ukutani.
Asubuhi Martin mtu wa kazi aliamka na k**a kawaida yake alijiandaa na kupita mezani lakini hakukuta chochote akaendelea na safari yake kuelekea kazini hakutaka kumuamsha mkewe alimuachia fedha kwa ajili ya chakula na matumizi yake binafsi ikiwa ni kawaida yake kumpa mkewe kila mwezi kiasi cha million 2 kwa ajili ya matumizi yake binafsi kwa kuwa hafanyi kazi na alikataa kufanya kazi mara baada ya kumpoteza mtoto wao kwa madai kuwa anahitaji muda ili awe sawa.
Annabelle alipoamka alikuta kiasi cha pesa cha shilingi milioni 3 tofauti na ilivyokuwa awali kuwa kila mwisho wa mwezi hupewa milioni 2. Alizichukua zote na kuziweka katika kisanduku chake ambacho hukitumia kuhifadhi pesa zake. Alijiandaa na kisha akachukua ufunguo wa gari lake aina ya Benz na kuondoka kuelekea kwa rafiki yake aitwaye Juliet. Walipoonana walikumbatiana kwa kuwa hawakuwa wamekutana kwa muda mrefu sana.
Walianza maongezi yao na Annabelle akamueleza rafiki yake kila kitu juu ya kile kilichotokea hadi mtoto wao akauawa. Juliet alimpa pole rafiki yake na kumshauri kukaa mbali na Martin kwani kuna uwezekano akamuua pia ili ajipatie utajiri, maneno yale yalimuingia Annabelle na akayabeba k**a yalivyo.
Anabelle aliporudi nyumbani alianza kutafakari juu ya mambo ambayo aliambiwa na rafiki yake naye alihisi kuwa ni kweli kwa kila kitu alichoambiwa na rafiki yake, hapo hasira na chuki dhidi ya Mumewe iliongezeka.
Njioni mumewe alirejea akiwa na hamu sana na mkewe lakini hakujua ni kwa namna gani mkewe alivyo jazwa sumu. Alifika na kukuta mkewe amelala tofauti na alivyozoea akitazama television. Alienda kuoga na kisha akarejea sebleni, alikaa kwa muda kidogo kisha akanyanyuka na kwenda chumba alicholala mkewe. Alipofika alikuta mkewe amelala kihasara hasara, akahisi damu inamchemka kuliko kawaida, mapigo ya moyo wake yakaanza kumwenda mbio mbio, jogoo la mjini likawika shamba. Martin akamsogelea mkewe pale kitandani na kuanza kumpapasa mkewe mapajani taratibu mkono wake ukielekea kibo na mawenzi, akiwa anakaribia kibo mara mkewe akastuka alipomuona mumewe alimsukuma kwangu. Martin akadondoka chini!
“Honey nini hiki sasa?” Martin alimuuliza mkewe kwa mshangao.
“Nini kuhusu nini?” Annabelle naye akajibu kwa swali huku akiwa amefura kwa hasira.
“Baby kwanini unaninyima haki yangu?”
“Haki ipi? Nakuuliza wewe muuaji haki ipi?”
“Annabelle wewe ni mke wangu tena wa ndoa na hii ni haki yangu unaninyima kwa miezi mitano sasa why are you doing this to me?” Martin alimlalamikia mke wake.
“Mke! Haki! Hivi unadhani kwa kwa kile ulichokifanya kwa mtoto wetu bado unayo haki juu yangu? Hapana Martin, huna haki hiyo tena na kwa taarifa yako, huu ni mwanzo tu, utateseka sana.” Annabelle alimueleza mumewe maneno ambayo kwa hakika yalimuumiza sana Martin. Baada ya kumueleza maneno yale Annabelle akachukua mto mmoja kwenda kulala chumba cha wageni. Hili hakulitegemea japo anaelewa wazi kuwa mkewe huyo anamchukia sana lakini hadi kulala vyumba tofauti, hii ilimuwashia taa ya kijani, hakutaka kumzuia alimuacha kisha akarejea kitandani. Alitazama kaptula yake tayari ilikuwa inaunyevu unyevu sehemu ya mbele, akatikisa kichwa kisha akachukua taulo yake na kuingia bafuni kuoga, alipomaliza alijiweka sawa kisha akalala.
Asubuhi ikafika Martin alijiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini, alipofika mlangoni alikumbuka kuwa yeye na mkewe hawakulala chumba kimoja, hivyo akaamua kwenda kumjulia hali mkewe, aligonga mlango lakini hakujibiwa aliamua kuufungua. Akiingia ndani ya chumba kile na kukuta mkewe yuko kwenye usingizi mzito huku akijigeuza kuelekea upande mwingine, Martin alitabasamu kisha akaufunga mlango na kuelekea kazini. Annabelle alipoamka alijiandalia kifungua kinywa kisha akakumbuka kumpigia mama yake simu. Mama yake alipokea na kumuuliza anaendeleaje.
“Mama naendelea vizuri ila namkumbuka tu mwanangu mama….” Annabelle alianza kulia wakati akimuelezea juu ya hali yake na namna alivyomkumbuka Ruth.
“Mwanangu, Juliet ameniambia kila kitu ni kwanini hukuniambia mapema…. Huyo mwanaume inaonekana wazi ni mshirikina, hizo mali ni kwasababu ya kutoa watu kafara sasa ameamua hadi kumtoa kafara mtoto wake mwenyewe, unbelievable!”
“Mama ninaumia sana kwa kweli, mtoto mwenyewe alikuwa mmoja k**a dawa halafu kirahisi rahisi tu anakufa jamanii mamaaa.” Annabelle aliendelea kumueleza mama yake kwa uchungu.
“Pole mwanangu, usijali I've to do something before it's too late…. Usijali mwanangu ila naomba uwe makini sana na huyo mwanaume.”
“Sawa mama nitakuwa makini sana.” Annabelle alimaliza kuongea na mama yake na kisha wakakata simu.
Mama yake Annabelle aliamua kumpigia simu Martin na kuanza kumtukana na kumtuhumu kuwa amemuua mjukuu wake, Martin akijitetea sana lakini hakuna kitu kilichobadilika, mama mkwe huyo aliendelea kumtuhumu kuwa mali zote alizonazo ni kwa sababu alitoa kafara ya watu ili awe tajiri. Hii ilimuumiza sana Martin aliamua kukata simu. Alitaka kupata msaada kutoka kwa mtu, na mtu pekee aliyemfikiria alikuwa ni Juliet!
ɪᴛᴀᴇɴᴅᴇʟᴇᴀ.............