Habari Za Nyarugusu CAMP

Habari Za Nyarugusu CAMP Ukurasa unaotoa taarifa za Kambini Nyarugusu kwa sekta zote. Kuna wakati tunaenda kitaifa & kimataifa

🀣 : Mwalimu Mkuu na mke wa bodaboda waliyeshikwa wakivunja amri ya 6 watembezwa uchiNi huko Kenya, katika Kaunti ya Siay...
25/10/2025

🀣 : Mwalimu Mkuu na mke wa bodaboda waliyeshikwa wakivunja amri ya 6 watembezwa uchi

Ni huko Kenya, katika Kaunti ya Siaya ambako Mwalimu Mkuu wa shule na mke wa bodaboda walishikwa mchana wa hiyo Alhamisi Oktoba 23, 2025 wakivunja amri ya 6.

Mume wa mwanamke huyo, kwa hasira; akaamua kuvua mkewe na Mwalimu Mkuu nguo na kuwapandisha kwenye pikipiki ambapo alianza kuwazungusha maeneo yote yenye watu wengi mjini ili watu wawaone na kujifunza kitu kuhusiana na kula tunda kwa mke wa mtu πŸ˜‚πŸ˜‚
..✍🏼 Mwaga wino kwenye maoni kutuambia kile ambacho utakuwa umejifunza kuhusiana na maamuzi ya huyu bodaboda.

πŸ›‘ : Mchungaji wa kanisa la Alfa na Omega raia wa Marekani mwenye asili ya DRCongo aaga dunia huko Indiana PolisNi Mchung...
25/10/2025

πŸ›‘ : Mchungaji wa kanisa la Alfa na Omega raia wa Marekani mwenye asili ya DRCongo aaga dunia huko Indiana Polis

Ni Mchungaji Pascal wa kanisa la Alfa na Omega raia wa Marekani mwenye asili ya DRCongo aliyeaga dunia hiyo Ijumaa Oktoba 24, 2025 mjini Indiana Polis huko Marekani.

Chanzo chetu cha siri kuhusiana na habari hii kilichopo huko USA kimesema kuwa, Mchungaji Pascal aliyetokea kwenye kambi ya Malawi na anayetajwa kuwa wa asili ya Bashi wa Bukavu alipatwa na mauti njiani mapema asubuhi akitokea nyumbani kwake na kujielekeza kwenye kazi yake ya duka.

Yote yalianzia pale Mchungaji Pascal alipowa ndani ya gari na kuanza kusikia moyo kuwaka moto sana. Bila kuchelewa, akaamua kulisimamisha baada ya kushindwa kabisa kutembeza na kupiga simu kwa msaada wa dharura.

Dakika chache baadaye, polisi na wasamaria wema wengine wakawasili eneo alipokuwa amepaki gari; wakamkuta akiwa kwenye hali mbaya zaidi. Bila kuchelewa wakapigia gari la wagonjwa simu ambapo gari hilo liliwasili hapo Mchungaji akiwa tayari ameshakata roho.

Mpaka sasa, mpango wa mazishi ya Mchungaji Pascal ambaye ameacha mjane wa kabila la Wabembe na zaidi ya watoto 3 haujatangazwa.

Mchungaji Pascal atakumbukwa na wengi kwa ukarimu wake alipokuwa dukani kwake kuuzia wateja wake nguo, samaki na dagaa toka Ziwa Viktoria na Tanganyika pamoja na chakula cha asili ya Afrika.

Uongozi wa #"HNC" unatoa pole kwa ndugu, jamaa na marafiki kwa kumpoteza mpendwa wao, Mungu azidi kuwafariji na kumpumzisha marehemu kwa amani.

⚽ : GHI1 Bilombe kula sahani moja na Baraka Mosa hiyo Ijumaa Oktoba 24, 2025 ndani ya dimba la E3 kusaka mpinzani wa You...
23/10/2025

⚽ : GHI1 Bilombe kula sahani moja na Baraka Mosa hiyo Ijumaa Oktoba 24, 2025 ndani ya dimba la E3 kusaka mpinzani wa Young Boys FC walioisafirisha Q1 Mtetezi kwenye ligi ya Shabani Cup 2025

Nani atatoboa kwa pambano hilo la kibabe la hiyo Ijumaa ili kukutana na Young Boys waliowatandika Q1 Mtetezi kwenye hatua ya 8 bora?

⚽ : Pichani ni majina ya timu zilizofuzu katika hatua ya 16 bora kwenye ligi ya Shabani Cup ambamo 4 ziliponea chupuchup...
18/10/2025

⚽ : Pichani ni majina ya timu zilizofuzu katika hatua ya 16 bora kwenye ligi ya Shabani Cup ambamo 4 ziliponea chupuchupu kwa kupitia dirishani (best looser)

Kulikuwa na hali ya kutoelewana kuhusu maamuzi yaliyochukuliwa ili best looser wa mwisho kati ya S2 Sports na Mauzo B2 aweze kupatikana.

Ukweli ni kwamba S2 Sports ilicheza michezo mitatu, ikafunga mchezo moja, wakatoka sare mchezo moja na kupoteze mechi moja. Hivyo S2 ikaonekana na pointi 4 na goli 1 ya kufunga na magoli 2 ya kufungwa wakawa wamepigwa
kadi tisa(9).

Mauzo Dragon nao walicheza michezo miwili ya dakika 90 na kutowasili kwenye kikao cha taaluma kwa ajili ya mchezo moja. Wakawa na pointi 4 na goli 1 la kufunga na magoli 2 ya adhabu kwa kutokushiriki kikao cha taaluma wakawa wamepigwa kadi 4 pekee. Kwa ufafanuzi huo, Mauzo Dragon waliwapiku S2 Sport kwa kigezo cha kupigwa kadi 4 huku wenzao S2 wakiwa walipigwa jumla ya kadi 9.
..✍🏼K**a mdau na mchambuzi wa soka, ni mechi gani ya kifo na ni upi ubashiri wako kwa timu zitakazofuzu kwenye hatua hii ya mtoano?

⚽ : Uongozi wa Young Africans SC wampa talaka Kocha waoIkiwa zimepita saa chache toka Yanga SC ipoteze kwa kufungwa bao ...
18/10/2025

⚽ : Uongozi wa Young Africans SC wampa talaka Kocha wao

Ikiwa zimepita saa chache toka Yanga SC ipoteze kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Silver Strikers ya Malawi katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa mtoano wa CAF Champions League, viongozi wa timu hiyo wamemua kufanya maamuzi mazito ya kuvunja mkataba na Kocha wao.

Yanga wamemfuta kazi Kocha wao Mkuu Romain Folz na kutangaza kuwa nafasi yake itakaimiwa kwa muda na Kocha Msaidizi Patrick Mabedi.

Roman Folz amejiunga na Yanga SC July 26 2025 akitokea Mamelod Sundowns ya Afrika Kusini alikokuwa anatumika nafasi ya Kocha Msaidizi.
..✍🏼 Mwaga wino kutupa maoni yako kuhusiana na uamuzi huo mzito ukiofanywa na viongozi wa Young Africans SC.

⚽ : Ninasumbuliwa eti nitoe matokeo ya mchezo kati ya R1 Sport Mabingwa wa mabingwa na majirani zao Club United kwenye g...
15/10/2025

⚽ : Ninasumbuliwa eti nitoe matokeo ya mchezo kati ya R1 Sport Mabingwa wa mabingwa na majirani zao Club United kwenye gozi la hiyo Jumanne Oktoba 14, kwani ilikuwaje jamani?

Mara R1 kachapwa, mara Club United wametandikwa na kuwa chanzo cha R1 kumpa Kocha wao kipondo hadi kumtoa meno ya sebuleni.

Mwenye zile za ndani aje huku chemba kwenye maoni tusemezane maana naambiwa eti mpaka sasa baadhi ya mashabiki wa R1 wapo uwanjani wakati mechi ilichezwa hiyo Jumanne Oktoba 14, 2025.

πŸ›‘ : Zikiwa zimesalia saa chache ili Kigogo wa Kambi ahutubie wakimbizi na waomba hifadhi kambini Nyarugusu hiyo Alhamisi...
15/10/2025

πŸ›‘ : Zikiwa zimesalia saa chache ili Kigogo wa Kambi ahutubie wakimbizi na waomba hifadhi kambini Nyarugusu hiyo Alhamisi Oktoba 16, unahisi ni mada zipi nzito zilizozama katika vichwa vya waanga hao wa vita?

πŸ›‘ : Ofisi ya Makazi kwa ushirikiano na shirika la UNHCR watangaza mkutano mkuu na jamii za Wakimbizi hiyo Alhamisi Oktob...
13/10/2025

πŸ›‘ : Ofisi ya Makazi kwa ushirikiano na shirika la UNHCR watangaza mkutano mkuu na jamii za Wakimbizi hiyo Alhamisi Oktoba 16, 2025

Kujuwa undani zaidi, pitia tangazo hili (ona picha) ambalo linaweka wazi kuwa kikao hicho kwa jamii ya Warundi utafanyika mida ya saa tatu kwenye uwanja wa zone ya 10 na kwa Wakongomani mkutano huo utafanyika mida ya saa saba mchana kwenye uwanja wa D1, zone ya 1.

πŸ›‘ : Tuambie jinsi hali ilivyo Ijumaa hii Oktoba 10, 2025 kwenye zone yako ao kijijini kwakoNinaambiwa kuwa amani na usal...
10/10/2025

πŸ›‘ : Tuambie jinsi hali ilivyo Ijumaa hii Oktoba 10, 2025 kwenye zone yako ao kijijini kwako

Ninaambiwa kuwa amani na usalama kwenye zone zote ungekuwa k**a ilivyo leo kambi ya Nyarugusu ingetangazwa bora. Nasikia hakuna cha mchiriko wala mlio wa pikipiki kwenye kona zote za Kambi.

πŸ›‘ : Baadhi ya wakimbizi walalamikia kunyan'ganywa simu zao kubwaNi taarifa ambayo imetufikia muda mfupi uliopita kwamba ...
08/10/2025

πŸ›‘ : Baadhi ya wakimbizi walalamikia kunyan'ganywa simu zao kubwa

Ni taarifa ambayo imetufikia muda mfupi uliopita kwamba kikosi cha usalama kwa maana ya Askari polisi na Sungusungu wameanza Jumatano hii Oktoba 8, 2025 kuweka kwa vitendo maelekezo yanayozagaa ya Mkuu wa Kambi ya kunyan'ganya baadhi ya wakimbizi simu zao kubwa baada ya mchakato wa k**ata k**ata ya pikipiki na baiskeli zinazomilikiwa na wakimbizi na waomba hifadhi kinyume na utaratibu na baadhi ya wakimbizi na waomba hifadhi kambini Nyarugusu, mkoani Kigoma.

Baadhi ya wasiri wetu wamesema kuwa, wakimbizi 4 walinyan'ganywa simu zao aina za smartphones kabla ya mchana kati wakati baadhi ya raia hao wanaotajwa kutokea DRC walipokuwa wakiwarekodi Polisi au Sungusungu wakati wa operesheni hizo za k**ata k**ata za pikipiki, baiskeli pamoja na simu kubwa ambapo walikuwa wanalazimishwa kufuta vyote walivyokuwa wakinasa kabla ya kuwapa wana usalama.

Hali hii ya k**ata k**ata ya simu imeongeza wasiwasi kwa wakimbizi na waomba hifadhi ambao wameonyesha wazi kuwa Uongozi wa Kambi haujatangaza rasmi kuhusu kunyang’anywa kwa simu wakati operesheni iliyotangazwa awali ya kuziorodhesha bado kuanza.

Baadhi ya wakimbizi na waomba hifadhi wanazidi kulaani vikali tabia hiyo ya vyombo vya usalama kuanza kunyan'ganywa kwa simu zao ambazo ndizo zimebaki kuwa wakombozi wao kwa kipindi hiki ambapo chakula kinachogawiwa kwa wakimbizi kimekuwa kisichotosheleza. Hivyo, wameomba shirikila la UNHCR na wateteaji wa haki za binadamu waingilie kati ili kuweka mambo sawa kwao k**a binadamu wanaotakiwa kuthaminiwa k**a watu wengine na sio k**a nyama.

πŸ›‘ : Taarifa ya kuorodheshwa kwa simu kubwa inayosambaa baada matangazo ya Makazi kuhusu pikipiki na baiskeli yaongeza ma...
08/10/2025

πŸ›‘ : Taarifa ya kuorodheshwa kwa simu kubwa inayosambaa baada matangazo ya Makazi kuhusu pikipiki na baiskeli yaongeza maumivu kwa wakimbizi na waomba hifadhi huko Nyarugusu

Ni taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu, Bw. Siasa Manjenje kwamba viongozi wa Jamii wataanza hivi karibuni mchakato wa kuorodhesha simu zote kubwa katika vijiji vyao katika kambi hiyo iliyopo wilayani Kasulu mkoani Kigoma.

Baada ya tangazo la wiki chache zilizopita kwa wakimbizi kutomiliki pikipiki, Bw. Manjenje alitoa tangazo lingine kuhusu kunyan'ganywa kwa baiskeli na taarifa nyingine mpya ya mwanzoni mwa wiki hii kuhusu kuanza kuorodheshwa kwa simu zote kubwa na viongozi wa Jamii katika kambi hiyo.

Wengi wanaoendelea kujadili kuhusiana na taarifa hiyo inayosambaa ya kuorodheshwa kwa simu kubwa wanahisi kuwa operesheni hiyo inayotarajiwa kuanza hivi karibuni imetolewa baada ya video zilizonasa matukio ya baadhi ya matukio likiwemo tukio la kwenda kunyan'ganya baadhi ya vifaa muhimu vya studio ya Spy Mkorofi wa kijiji cha G3 na vile vya Kasaco Tv na kupelekwa mahali pasipojulikana.

Aidha, ofisi hiyo ya Mkuu wa Kambi imeonya wale wanaopiga picha na kunasa video kiholela kambini humo kuwa ni kinyume na sheria huku mikazo ikiwekwa kwamba mkimbizi ama muomba hifadhi anatakiwa kuwa na redio sio simu kubwa.

Taarifa hiyo ya simu kubwa kuorodheshwa imekuwa gumzo kwenye vijiwe vingi kambini, hali inayodhaniwa kuwa itakuja kuongeza idadi ya wagonjwa wa mioyo na presha na kuchangia kwa vifo vingi kwa wakimbizi na waomba hifadhi.

Kutokana na tamko hilo la simu kubwa kuorodheshwa na lile la kunyan'ganywa kwa baiskeli, wapo waliopendekeza kufanyika kwa maandamano ya amani kambini Nyarugusu hiyo Oktoba 10, 2025 jambo ambalo mmoja wa Askari polisi ambaye jina lake halijatajwa ameshauri kuachana nalo kwa kile alichosema kuwa maswala haya yanajadiliwa ngazi za juu ili kuja kupatiwa suluhu.
..✍🏼 Tupe maoni yako kuhusiana na amri hizo nyundo zinazoshushwa na Kigogo wa Kambi.

πŸ›‘ : Mmoja wa wakimbizi aliyekuwa kibarua kwenye shirika la World Vision afutwa kazi na kutamkiwa kufutwa ukimbizi kwa ku...
01/10/2025

πŸ›‘ : Mmoja wa wakimbizi aliyekuwa kibarua kwenye shirika la World Vision afutwa kazi na kutamkiwa kufutwa ukimbizi kwa kufoji sahihi ya mmoja wa Maofisa wa Mkuu wa Kambi (MoA)

Selemani Baruti Kashindi ndilo jina la mmoja wa wakimbizi aliyekuwa kibarua kwenye shirika la World Vision Tz ambaye alifutwa kazi na kuambiwa kuwa atavuliwa hadhi ya ukimbizi baada ya kukutwa na kesi ya kufoji sahihi ya mmoja wa Maofisa wa Mkuu wa Kambi (MoA) kwenye fomu ya mkimbizi mwenza kambini Nyarugusu, mkoani Kigoma.

K**a wasemavyo; "Za mwizi 40", hayo yalijiri hiyo Jumanne Septemba 30, 2025 wakati ugawaji wa chakula ulipokuwa ukiendelea kwenye kituo cha 1 ambapo Bwana Selemani B. Kashindi alitajwa na mkimbizi mwenza aliyeshindwa kujitetea alipokuwa akihojiwa kuhusiana na sahihi feki iliyotiliwa shaka kwenye fomu yake ya kupokelea chakula.

Mpaka sasa hatma kuhusiana na kesi hiyo inayomkabili Selemani haijajulikana ila bado tunazidi kuifuatilia taarifa hii ili kuja kuwadondoshea kina chake hapo baadaye.

Address

Nyarugusu
Makere

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari Za Nyarugusu CAMP posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share