fmmanyara

fmmanyara Fm Manyara Radio ni moja ya Redio Bora inayopatikana Mkoani Manyara wilayani Babati . Kwere Street

Usikose kufuatilia kipindi hiki
04/12/2025

Usikose kufuatilia kipindi hiki





Usikose kusikiliza kipindi
27/11/2025

Usikose kusikiliza kipindi







Usikose kusikiliza kipindi
27/11/2025

Usikose kusikiliza kipindi

Team , Swali la Leo ni hili hapa, kwenye Radio watapiga simu na kujibu kisha mshindi mta mtaja mwisho wa kipinidiKwenye ...
24/10/2025

Team , Swali la Leo ni hili hapa, kwenye Radio watapiga simu na kujibu kisha mshindi mta mtaja mwisho wa kipinidi
Kwenye social media naomba mpost tuu atakae jibu wa kwanza kwa usahihi ndio mshindi,
Mki post naomba muombe collabo na page ya Oryx enregies Tanzania,
Majibu tutatoa baadae tatu,
*Zawadi za leo*
Redioni-Kikombe
Social media-Tshirt + wrist band

Jaza mtungi wa Oryx Gas, kwangu na tuma code kwa 15393, ujishindie pikipiki, mafuta, vifaa vya nyumbani na zawadi kibao ...
24/10/2025

Jaza mtungi wa Oryx Gas, kwangu na tuma code kwa 15393, ujishindie pikipiki, mafuta, vifaa vya nyumbani na zawadi kibao papo hapo!
Kila ukijaza, ni nafasi ya kushinda!

GESI YENTE, Kila mtu apate!

Endelea kutusikiliza redioni na ujishindie zawadi kali zaidi ya zote!Fuatilia vipindi vyetu, shiriki promosheni zetu na ...
24/10/2025

Endelea kutusikiliza redioni na ujishindie zawadi kali zaidi ya zote!
Fuatilia vipindi vyetu, shiriki promosheni zetu na wewe unaweza kuwa mshindi wa pikipiki, mafuta au vifaa vya kifahari nyumbani!

GESI YENTE, Kila mtu apate!

Sema ukweli, nani hataki Harrier Anaconda au iPhone 17 Pro Max?Ziko Reward Hub ya Premier Bet - mahali ambapo alama zina...
21/10/2025

Sema ukweli, nani hataki Harrier Anaconda au iPhone 17 Pro Max?
Ziko Reward Hub ya Premier Bet - mahali ambapo alama zinageuka kuwa zawadi nono 🔥
Wapigie bure 📞 0800750032 kufahamu kuhusu ofa hii zaidi!
Reward Hub — Maskani ya Zawadi! 🎁


Mgombea Urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama Cha mapinduzi CCM Dokta Samia Suluhu Hassan amesema serik...
03/10/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia chama Cha mapinduzi CCM Dokta Samia Suluhu Hassan amesema serikali inaendeleaje na mazungumzo na serikali ya India katika kuhakikisha Bei ya mbaazi inapanda Ili wakulima wa mbaazi wanufaike na zao Hilo.

Dokta Samia amesema hayo Leo wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Hanang mkoani Manyara baada ya kuanza kampeini zake rasmi katika mkoa wa Manyara, amewataka wananchi waendelee kuwa watulivu wakati serikali ikiendelea na mazungumzo.

Kwa upande wake mgombea ubunge wa Jimbo la Hanang Asia halamgha, amemshukuru Dokta Samia Kwa kuleta maendeleo katika wilaya ya Hanang katika sekta ya maji,umeme,barabara pamoja na elimu na kuwaomba wananchi kumchagua Kiongozi huyo.

Aidha, Waziri mkuu mstaafu Fredrick Sumaye amesema wananchi wa Hanang wamejupanga kumpigia kura Kiongozi huyo kutokana na kazi kubwa ya maendeleo aliyoifanya katikati kipindi chote Cha uongozi wake.

Dokta Samia Suluhu Hassan kesho October 4 atazungumza na wananchi wa mkoa wa Manyara katika viwanja vya stendi ya zamani na kunadi sera zake.

Sherehe ya maazimisho ya mwaka mmoja wa UMOJA SALAMU CLUB🎉🎊🍾
26/09/2025

Sherehe ya maazimisho ya mwaka mmoja wa UMOJA SALAMU CLUB
🎉🎊🍾

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga,amewaonya viongozi wa sekta binafsi ambao wamekuwa wakijifanya miungu watu kuacha ...
11/09/2025

Mkuu wa mkoa wa Manyara Queen Sendiga,amewaonya viongozi wa sekta binafsi ambao wamekuwa wakijifanya miungu watu kuacha tabia ya kuwanyanyasa wafanyakazi ikiwemo kutowapatia mikataba

Sendinga amesema hayo Leo katika kikao Cha kusikiliza na kutatua kero za wananchi, ambapo miongoni mwa kero iliyowasilishwa ni baadhi ya waliokuwa walimu wa shule ya Aldersgate kudai mafao yao ambayo waliyatumikia kwa kipindi walichofanya kazi shuleni hapo.

Awali baadhi ya walimu akiwemo aliyekuwa mkuu wa shule hiyo ambae amefanya kazi Kwa kipindi Cha zaidi ya miaka 15, wamesema licha ya kufanya kazi Kwa kipindi hicho hawajawakewa mafao yao baada ya kustaafu ambapo wameiomba serikali iwasaidie kwakuwa waliondolewa shuleni hapo bila utaratibu.

Awali baadhi ya viongozi wa shule hiyo, wamesema malalamiko hayo sio ya kweli kwani walimu hao walikuwa wakijitolea.

Aidha , kufuatia malalamiko hayo , Sendiga amemuagiza katibu tawala wa mkoa wa Manyara kufuatilia nyaraka shuleni hapo ili achukue hatua zaidi za kisheria.

Kampuni ya Mati Super Brands ltd kupitia Taasisi yake isiyo ya kiserikali Mati foundation, imeanza rasmi mradi wa kukabi...
10/09/2025

Kampuni ya Mati Super Brands ltd kupitia Taasisi yake isiyo ya kiserikali Mati foundation, imeanza rasmi mradi wa kukabidhi pikipiki za magurudumu matatu zinazotumia nishati ya umeme kwa watu wenye ulemavu nchini ili kuwasaidia kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa ufanisi zaidi.

Hafla ya makabidhiano imeongozwa na Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo inayozalisha na kusambaza vinywaji changamshi, David Mulokozi ambaye ameeleza kuwa watu wenye mahitaji maalumu katika jamii hasa wale wanaojishughulisha na shughuli mbalimbali za kuingiza kipato wanahitaji kuwezeshwa kwa miundombinu bora ili waweze kuchangia uchumi wa taifa kupitia shughuli wanazozifanya.

Baadhi ya wanufaika wa vyombo hivyo vya usafiri ambao ni walemavu wanaojishugulisha, Bi Aisha Wenga na Ramadhani Omari kutoka katika wilaya ya Babati mitaa ya wang’warayi na mji mpya wameishukuru ‘Mati foundation’ kwa kugusa maisha ya jamii yenye makundi maalumu wakieleza kuwa jitihada hizo zinakwenda kuleta chachu na kuongeza ufanisi katika shughuli zao.

Meneja mradi wa mati foundation Isack Piganio amesema taasisi hiyo ikishirikiana na mati super brand imekuwa ikijitolea kurudisha kwa jamii sehemu ya faida yake, huku mradi huu wa ugawaji pikipiki za magurudumu matatu ukiwa ni miongoni mwa miradi mingine ambayo wameendelea kuifanya.

Taasisi hiyo imeeleza mpango wake wa kutoa pikipiki zaidi ya 2000 kwa makundi ya watu maalumu ili kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili katika shughuli za utafutaji.



Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Manyara imefanikiwa kurejesha madawati 20 yaliyofanyiwa ubadhi...
02/09/2025

Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Manyara imefanikiwa kurejesha madawati 20 yaliyofanyiwa ubadhirifu katika shule ya msingi Oltepeleki iliyopo katika Kijiji Cha Loiborsiret wilayani Simanjiro.

Taarifa hiyo imetolewa na kaimu mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Manyara Adam Mbwana, amesema mzabuni alilipwa shilingi milioni 5 Kwa ajili ya kutengeneza madawati 50 ya shule hiyo ambapo aliwasilisha madawati 30 pekee.

Amesema madawati 20 yaliyobaki yenye thamani ya shilingi milioni 2 yalifanyiwa ubadhirifu na mtendaji wa Kijiji Kwa kushirikiana na mzabuni, ambapo TAKUKURU ilifuatilia na kurejesha fedha hizo na madawati hayo yamekamilika na kuanza kutumika.

Aidha, amesema katika kipindi Cha April -june TAKUKURU ilifuatilia miradi ya maendeleo 7, na katika uchunguzi ilipokea malalamiko 38 kati ya hayo 26 yalihusu Rushwa na kesi 6 zilifunguliwa mahakamani,11 zinaendelea mahakamani, kesi 3 zimeamriwa na kati ya hizo jamhuri imeshinda kesi 2 .

tz

Address

Kwere, Babati
Manyara

Telephone

+255689727210

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when fmmanyara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to fmmanyara:

Share

Category