09/05/2026
Wafungwa,mahabusu tunakupenda Dkt Samia
Baadhi ya wafungwa na mahabusu wa magereza mbalimbali likiwemo la Ukonga wamemwambia Rais Samia Suluhu Hassan kuwa wanapenda sana na wanahitaji huruma yake dhidi yao.
Hayo yamesemwa leo Jumamosi Mei 9,2026 na mmoja wafungwa Lista Charles ambaye amebakisha miaka miwili kabla ya kumaliza kifungo chake wakati Dkt Samia alipotembelea banda lake la ushonaji lililopo viwanja Chuo cha Taalumu ya Urekebishaji Tanzania, kilichopo Ukonga.
" Mheshimiwa Rais kule gerezani watu wanahitaji huruma yako, wanakupenda sana hata leo nimekuja kutoka gereza la Ukonga wameniambia nenda fikisha salamu," amesema Charles
" Wanafuraha sana, kuna wale waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa umewabasilishia kifungo cha maisha, na wale waliokuwa kifungo cha maisha umewabadilisha hadi miaka 30," ameeleza.
Aidha Charles amesema kwa niaba ya wenzake amemuomba Dkt Samia kuendelea kuwaangalia wafungwa na mahabusu kwa kiongozi huyo ni mlezi, na wao wameshajifunza.
" Mimi nikiwa mmoja wao, tumeshajifunza na kusali bado tunahitaji huruma zako mheshimiwa Rais. Wafungwa na Watanzania watakuwa wanakuangalia mama wewe ni mlezi wa familia
Baada ya maelezo hayo Rais Dkt Samia ambaye alikuwa anafunga mafunzo ya uongozi wa ngazi juu ya kozi namba 28 na uongozo daraja la pili kozi namba 48 kwa mwaka 2025/ 26 ya Jeshi la Magereza nchini, amemwambia amemsikia.