fmmanyara

fmmanyara Fm Manyara Radio ni Redio Bora inayopatikana wilayani Babati Mkoani Manyara.

FM Manyara inawafikia zaidi ya wasikilizaji Milioni Mbili kupitia masafa ya 92.3 katika mikoa ya Manyara,Arusha, Singida na Dodoma
Tunazalisha vipindi bora kila siku
Kwere Street

09/05/2026

Wafungwa,mahabusu tunakupenda Dkt Samia

Baadhi ya wafungwa na mahabusu wa magereza mbalimbali likiwemo la Ukonga wamemwambia Rais Samia Suluhu Hassan kuwa wanapenda sana na wanahitaji huruma yake dhidi yao.

Hayo yamesemwa leo Jumamosi Mei 9,2026 na mmoja wafungwa Lista Charles ambaye amebakisha miaka miwili kabla ya kumaliza kifungo chake wakati Dkt Samia alipotembelea banda lake la ushonaji lililopo viwanja Chuo cha Taalumu ya Urekebishaji Tanzania, kilichopo Ukonga.

" Mheshimiwa Rais kule gerezani watu wanahitaji huruma yako, wanakupenda sana hata leo nimekuja kutoka gereza la Ukonga wameniambia nenda fikisha salamu," amesema Charles

" Wanafuraha sana, kuna wale waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa umewabasilishia kifungo cha maisha, na wale waliokuwa kifungo cha maisha umewabadilisha hadi miaka 30," ameeleza.

Aidha Charles amesema kwa niaba ya wenzake amemuomba Dkt Samia kuendelea kuwaangalia wafungwa na mahabusu kwa kiongozi huyo ni mlezi, na wao wameshajifunza.

" Mimi nikiwa mmoja wao, tumeshajifunza na kusali bado tunahitaji huruma zako mheshimiwa Rais. Wafungwa na Watanzania watakuwa wanakuangalia mama wewe ni mlezi wa familia

Baada ya maelezo hayo Rais Dkt Samia ambaye alikuwa anafunga mafunzo ya uongozi wa ngazi juu ya kozi namba 28 na uongozo daraja la pili kozi namba 48 kwa mwaka 2025/ 26 ya Jeshi la Magereza nchini, amemwambia amemsikia.

09/05/2026

Dkt Samia: Haki, utu wa wafungwa wanawake uheshimiwe

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, ametaka utu, heshima na haki za wafungwa hususan wanawake ziheshimiwe, kwa kuwa wana mahitaji ya ziada na maumbile tofauti na wanaume.

Dkt Samia ametoa kauli hiyo leo, Jumamosi Mei 9, 2026 wakati wa hafla ya kuhitimisha mafunzo ya uongozi ngazi ya juu Kodi namba 48 kwa mwaka 2025/26 katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania.

"Kwa hiyo wale mnaochunga wafungwa wanawake, haki na utu wao naomba uheshimiwe. Ni wahalifu wamekosa wameadhibiwa, lakini utu wao naomba uheshimiwe," amesema.

Ametaka wafungwa hao, wapate nafasi yao k**a wanawake kwa kuwa maumbile yao ni tofauti na wanaume.

08/05/2026

Rais Samia: Vijana tuioneshe dunia Tanzania ni nchi ya amani*

RAIS Samia Suluhu Hassan, amewataka vijana Watanzania kuilinda amani ya Taifa kwa kulindana wenyewe na kuonesha dunia kuwa yaliyokea Oktoba 29, 2025 hayatatokea tena.

Amesema yaliyotokea Oktoba 29,2025 yalilitia doa Taifa hasa kwa kuwa inaaminika Tanzania ni nchi ya amani hivyo vijana wanamchango mkubwa wa kurejesha amani hiyo.

Rais Samia ameyasema hayo leo Mei 8,2026 wakati akizungumza na wananchi makundi ya mama lishe, machinga na vijana waliovaa fulana zenye maandishi ya ‘Never Again’ waliojitokeza kumsalimia, wakati akianza safari yake ya kutokea mkoani Dodoma kuelekea Dar es Salaam, kwa shughuli za kikazi.

“Vijana wangu nimepokea ujumbe wenu, na niwaombe sana k**a kweli mmekusudia ‘Never Again’ k**a fulana zenu zinavyosema, naomba mlindane wenyewe kwa wenyewe na msikubali kutiwa maneno ya kuharibu usalama wa nchi yetu na nchi yetu kwa ujumla,” amesema Rais Samia.

Ameeleza kuwa yaliyokea nyuma, yaliwakuta waliohusika na wasiohusika na vijana wengi wakak**atwa, akiwa k**a Mama akaamuru waachiwe akiamini wameshajifunza.

“Tanzania ni nchi ya amani hayajawahi kutokea yaliyorokea, sasa tuuoneshe ulimwengu yale yaliyotokea si ya kitanzania na si utanzania ni mambo ya kupandikiza, kwa hiyo sasa tuuoneshe ulimwengu na nawashukuru mmesema hapana ‘Never Again,” amesema Rais Samia.

Aidha, amewashukuru vijana hao kwa msimamo huo na kusema kuwa maneno hayo yamempa faraja kubwa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, amesema maana ya fulana za ‘Never Again’ na zenye rangi ya bendera ya Tanzania ni hawataki tena yaliyotokea Oktoba 29,2025 yatokee.

“Lugha hii ya kwenye fulana ni ya wasomi wa Dodoma wanaokuambia, hawataki tena yaliyotokea tena huko nyuma, wao ni wazalendo, wanaipenda nchi yao, wanaijali na wanaithamini,” amesema Rosemary.

Usikose kufatilia kipindi hiki maalum kitakachorushwa Fm Manyara radio 92.3. ni yapi maoni Yako ?
07/05/2026

Usikose kufatilia kipindi hiki maalum kitakachorushwa Fm Manyara radio 92.3. ni yapi maoni Yako ?






Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, ameanza ziara yake leo May 6, 2026 Wilayani Simanjiro kwa kuzindua ...
07/05/2026

Mkuu wa mkoa wa Manyara Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, ameanza ziara yake leo May 6, 2026 Wilayani Simanjiro kwa kuzindua mnara wa mawasiliano katika Kijiji cha Kimotorok, mnara huo uliogharimu zaidi ya milioni 200 mpaka kukamilika unatarajiwa kuhudumia wananchi wa kijiji Cha Kimotorok na vijiji jirani, Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa *Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan* imeendelea na juhudi za kuhakikisha wananchi wa maeneo ya pembezoni na vijijini wanapata mawasiliano ya uhakika Kwa kujenga minara ya mawasiliano kupitia mfuko wa mawasiliano Kwa wote (UCSAF).

"Mnara huo utarahisisha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuboresha usalama kwani mawasiliqno ni usalama pia" amesema RC Sendiga.

Vilevile RC Sendiga, ametembelea na kukagua Zahanati ya Oltotoi, ujenzi wa mradi wa maji Oltotoi awamu II na kukabidhi vifaa kwaajili ya ujenzi wa mradi huo utakao gharimu shilingi Milioni 297.537.

Sambamba na hilo ametembelea Kijiji cha Loiborsiret kwenye eneo mwekezaji la IRALOI RANCHING ambao wanajishughulisha na shughuli za utalii .

Mwisho wa ziara yake siku hii ya Leo, Mhe. Mkuu wa mkoa anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara katika Kata ya Loiborsiret.

Rais Samia amkaribisha Drogba kuwa Balozi wa Afcon 2027Rais Samia Suluhu Hassan amemkaribisha mshambuliaji wa zamani wa ...
06/05/2026

Rais Samia amkaribisha Drogba kuwa Balozi wa Afcon 2027

Rais Samia Suluhu Hassan amemkaribisha mshambuliaji wa zamani wa Ivory Coast, Didier Drogba, kuwa balozi maalum wa Tanzania kuelekea fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2027.

Rais Samia ametoa mwaliko huo leo Jumanne, Mei 5, 2026, Ikulu Chamwino jijini Dodoma wakati akizungumza naye, ikiwa ni siku chache baada ya Drogba kuwasili nchini na kushiriki Bunge la Bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo jana Mei 4, 2026.

Aidha, Rais Samia ameielekeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kushirikiana na nyota huyo wa zamani wa Chelsea F.C. katika kubadilishana uzoefu wa usimamizi na uendelezaji wa akademia za michezo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuimarisha sekta ya michezo nchini.

Kwa upande wake, Drogba ameshukuru kwa mwaliko huo na kuonesha utayari wa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza michezo.
Drogba anachukuliwa kuwa mmoja wa wanasoka waliopata mafanikio makubwa duniani na pia anasifiwa kwa mchango wake katika juhudi za amani nchini Ivory Coast mwaka 2005, alipotumia ushawishi wake kusaidia kukomesha mgogoro wa muda mrefu wa kivita.

Wawekezaji mkoani Manyara wametakiwa kuchangamkia fursa ya kuwekeza biashara mbalimbali ili kujiinua kiuchumi baada ya g...
06/05/2026

Wawekezaji mkoani Manyara wametakiwa kuchangamkia fursa ya kuwekeza biashara mbalimbali ili kujiinua kiuchumi baada ya gate la Mamire kufunguliwa kwa ajili ya kupitisha magari ya watalii.

Mkuu wa mkoa wa manyara Queen Sendiga ameyasema hayo leo wakati akiongea katika kikao cha k**ati ya uwekezaji mkoa wa Manyara , amesema serikali imafanikisha kufungua geti hilo, hivyo kunapofunguliwa biashara mbalimbali itasaidia wawekezaji kupata huduma muhimu na kukuza uchumi wa mkoa wa Manyara.

Kwa upande wake afisa biashara mkoa wa Manyara Ally Mokiwa , amesema mkoa wa Manyara una jumla ya wawekezaji 138 ambapo jitihada mbalimbali zinaendelea za kuweka mazingira bora na kuvutia uwekezaji.

Akiwasilisha ripoti ya tiseza , Katibu wa k**ati ya uwekezaji mkoa ambae pia ni k**anda wa uhamiaji mkoa Philon Phabian Kyetema amesema kiwango Cha miradi ya upanuzi kinazidi kuongezeka katika mkoa wa Manyara.

05/05/2026

Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William William Ruto Aipongeza NSSF Kwa Uwekezaji wa Dola Milioni 51 Nairobi

05/05/2026

Ruto amsifu Rais Samia kwa uongozi imara

Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto, amempongeza Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa uongozi bora na kusimama imara wakati wa vurugu za Oktoba 29,2025.

Aidha, amempongeza kwa mchango wake katika kuimarisha uhusiano wa pande mbili na ushirikiano wa kikanda kati ya Tanzania na Uganda.
Rais Ruto ametoa pongezi hizo mbele ya Bunge la Tanzania, wakati akilihutubia leo Mei 5, 2026, ikiwa ni ziara yake ya kwanza nchini tangu awamu ya pili ya utawala wa Rais Samia.

Rais Ruto pia ameeleza kufurahishwa kwake na namna Rais Samia anavyosimamia maendeleo na kuendeleza mshik**ano wa karibu zaidi kati ya nchi jirani.

“Ninapaswa kuupongeza uongozi bora wa Rais Samia Suluhu Hassan katika mkutano huu, hasa kwa kusimama imara,” amesema Rais Ruto.

05/05/2026

Ruto: Biashara Tanzania, Kenya yafikia Sh2.2 trilioni 2025

Rais wa Kenya, William Ruto, amesema biashara ya Tanzania na Kenya mwaka jana ilifikia Dola za Marekani 860 milioni (zaidi ya Sh2.223 trilioni).

Ruto ameyasema hayo leo, Jumanne Mei 5, 2026 alipolihutubia Bunge la Tanzania, wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku mbili nchini.

Amesema mataifa hayo yanategemeana ndiyo maana biashara yao mwaka 2025 ilifika Dola za Marekani milioni 860, (zaidi ya Sh2.223 trilioni.

Ameeleza mwaka huu matarajio ni biashara baina ya mataifa hayo, ifikie Dola bilioni 1 (zaidi ya Sh2.6 trilioni).

05/05/2026

Ruto: Kampuni za Kenya 500 zimewekeza bilioni 1.7 Tanzania

Rais wa Kenya, Dkt. William Ruto, amesema Kampuni 500 za Kenya zimewekeza Dola za Marekani bilioni 1.7 nchini Tanzania.

Amesema uwekezaji huo umeongeza ajira za mamilioni ya watu na kukuza mapato makubwa kwa serikali.

Rais Ruto ameyasema hayo leo Aprili 5, 2026, wakati akihutubia Bunge la Tanzania jijini Dodoma na kuongeza kuwa uwekezaji unaonesha kuimarika kwa uhusiano wa kibiashara kati ya mataifa hayo jirani.

Kadhalika, amesema masharikiano hayo pia yapo kwa kampuni za Kitanzania ambazo zimepanua shughuli za uwekezaji nchini Kenya.

Amezitaja Taifa Gas, Amson Group na Lake Gas k**a mifano ya kampuni zilizowekeza nchini Kenya.

Amesema uwekezaji huo wa miaka mitatu lakini wanaamini unaendelea kukuza na kuongeza uchumi wa mataifa hayo mawili kwa kasi kubwa.

“Kampuni kutoka Tanzania pia zimewekeza Kenya na niliwaambia Wakenya kwamba mwekezaji kutoka Tanzania ni mshirika wetu, wanatuletea pesa na tunatafuta muda mrefu kutafuta wawekezaji,” amesema Ruto na kuongeza zaidi kuwa;

“Nilimpa mpatia Mtanzania kiwanda cha uwekezaji kuna watu walilalama, wale walioniuliza kwanini Watanzania wamewekeza Kenya, niliwauliza awali kampuni ilimilikiwa na Wafaransa sasa inamalikiwa na Mtanzania kwanini hamkulalama kumilikiwa na Wafaransa,” amesema Ruto.


Address

Kwere, Babati
Manyara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when fmmanyara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to fmmanyara:

Share

Category