fmmanyara

fmmanyara Fm Manyara Radio ni Redio Bora inayopatikana wilayani Babati Mkoani Manyara.

FM Manyara inawafikia zaidi ya wasikilizaji Milioni Mbili kupitia masafa ya 92.3 katika mikoa ya Manyara,Arusha, Singida na Dodoma
Tunazalisha vipindi bora kila siku
Kwere Street

05/06/2026

Putin: Tanzania ni kiungo muhimu kati ya Afrika Mashariki na masoko ya dunia

Rais wa Urusi, Vladimir Putin, ameitaja Tanzania kuwa lango muhimu linalounganisha Afrika Mashariki na masoko ya dunia, akisisitiza kuwa nafasi ya nchi hiyo inaendelea kuwa ya kimkakati katika mfumo mpya wa uchumi wa dunia.

Akizungumza Juni 5 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) 2026, Putin amesema Tanzania ina nafasi inayofanana na ile ya Uzbekistan katika Asia ya Kati, kwa kuwa ni kiungo muhimu kinachounganisha uchumi wa kikanda na vituo vikubwa vya biashara duniani.

"Tanzania ina nafasi k**a hiyo katika Afrika Mashariki," amesema Putin wakati akizungumzia nchi ambazo nafasi zao za kijiografia na uhusiano wao wa kiuchumi zinazozifanya kuwa madaraja muhimu yanayounganisha maeneo mbalimbali ya dunia.

Ameeleza mataifa yanayoweza kuoanisha maendeleo yao ya ndani na mahusiano imara na vituo vipya vya ukuaji wa uchumi duniani yanazidi kuwa na umuhimu mkubwa kadiri mifumo ya biashara ya kimataifa inavyoendelea kubadilika.

Putin pia amegusia kile alichokitaja kuwa ni mabadiliko yanayoendelea katika mfumo wa biashara ya dunia, akisema biashara ya kimataifa inajiondoa katika misingi yake ya awali iliyowekwa chini ya Shirika la Biashara Duniani (WTO).

Kauli hizo zinakuja wakati Tanzania ikiendelea kuwekeza kwa kiwango kikubwa katika miundombinu ya usafirishaji, maendeleo ya bandari na kuimarisha mtandao wa biashara wa kikanda, hatua zinazozidi kuimarisha nafasi yake k**a lango kuu la biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.




05/06/2026

Tanzania yajitangaza kuwa kitovu kipya cha uwekezaji Afrika

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania imejipanga kuwa moja ya vituo vikuu vya uwekezaji barani Afrika kwa kufungua milango kwa kampuni za kimataifa kuwekeza katika miradi mikubwa ya kimkakati.

Dkt Samia amesema miongoni mwa maeneo yanayohitaji ushirikiano wa wawekezaji ni pamoja na maendeleo ya bandari, maeneo maalumu ya kiuchumi na sekta za uzalishaji zitakazochochea ukuaji wa uchumi na ajira kwa Watanzania.

Akizungumzia mradi wa kimkakati wa Bagamoyo, Rais Dkt Samia amesema :“Mradi wa Eneo Maalumu la Kiuchumi la Bagamoyo (BSEZ) ni mradi namba moja ambao tunakaribisha kampuni za kimataifa kushirikiana nasi.”

Dkt Samia ameeleza hayo leo Juni 5,2026 katika Jukwaa la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF) 2026, nchini Urusi katika mwendelezo wa ziara yake ya kikazi katika Taifa hilo. Katika mkutano uliuhudhuriwa na Rais wa Urusi, Vladmir Putin.

Kauli hiyo ya Dkt Samia inaonyesha namna Tanzania ilivyojijengea taswira mpya duniani k**a nchi yenye mazingira rafiki ya biashara na uwekezaji, huku Serikali ikiendelea kuweka miundombinu na sera zinazovutia mitaji ya ndani na nje ya nchi.




05/06/2026

Dkt Samia awavuta wawekezaji wa sekta ya madini kutoka Urusi

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania imebarikiwa kuwa na utajiri mkubwa wa madini muhimu duniani, yakiwemo Uranium, Nickel, Graphite, Helium na madini adimu yanayohitajika katika mapinduzi ya teknolojia na nishati.

Dkt Samia ametoa kauli hiyo leo, Ijumaa Juni 5, 2026 alipozungumza katika Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg (SPIEF 2026) nchini Urusi, alikokwenda kwa ziara ya siku mbili ya kikazi.

Amesema lengo la Serikali si kuendelea kuuza malighafi pekee, bali kujenga viwanda vya kuongeza thamani ili wananchi wanufaike zaidi kupitia ajira, mapato na ukuaji wa uchumi wa viwanda.

“Tunalenga kuondoka kuwa wazalishaji wa malighafi kuwa wazalishaji wa bidhaa iliyokamilika. Tunawakaribisha washirika kuwekeza nasi katika maeneo ya viwanda ambayo yatatoa tafsiri halisi ya faida ya madini,” amesema.

Jukwaa hilo limewakutanisha zaidi ya washiriki 24,000 kutoka zaidi ya nchi 140, wakiwemo wakuu wa nchi, wawekezaji na viongozi wa makampuni makubwa duniani.




05/06/2026

Dkt Samia aitangaza Tanzania katika jukwaa la dunia

Rais Dk Samia Suluhu Hassan, ameendelea kuiweka Tanzania kwenye ramani ya uchumi wa dunia, baada ya kushiriki Jukwaa la 29 la Kimataifa la Uchumi la St. Petersburg nchini Urusi.

Jukwaa hilo limewakutanisha zaidi ya washiriki 24,000 kutoka zaidi ya nchi 140, wakiwemo wakuu wa nchi, wawekezaji na viongozi wa makampuni makubwa duniani.

Kupitia ushiriki huo, Tanzania imepata fursa ya kutangaza vivutio vyake vya uwekezaji katika sekta za madini, nishati, utalii, kilimo na usafirishaji.

Hatua hiyo inaendelea kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a kitovu cha biashara na uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki.



04/06/2026

Rais Samia atunukiwa shahada ya heshima Urusi

Moscow

CHUO Kikuu mashuhuri nchini Urusi leo kimemtunukia shahada ya heshima ya Uzamivu (honoris causa) Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na uongozi usio kifani na mchango wake kwa maendeleo ya taifa lake.

Chuo hicho kinachojulikana kwa jina la Chuo Kikuu cha Urafiki wa Watu wa Urusi (RUDN) ni miongoni mwa vyuo mashuhuri duniani – kikijipatia sifa kutokana na kusomesha kada ya wasomi wa miaka ya mwanzoni ya Uhuru barani Afrika, Asia na Amerika ya Kusini na kujulikana kwa jina la Patrice Lumumba.

Akipokea shahada hiyo ya heshima – ya nane tangu aingie madarakani, Rais Samia alisema amepokea tuzo hiyo kwa unyenyekevu mkubwa na haichukulii k**a yake binafsi.

“Nilipopata taarifa ya kupewa hadhi hii, niliona kwamba hii heshima si yangu pekee bali ni kwa wale wote ambao elimu ina maana kwao. Kwa walimu wanaofundisha kote, kwa wanafunzi want guys maarifa na kwa wazazi wanaopambana kusomesha watoto wao.

“ Jina la chuo hiki, likichukua jina la mmoja wa viongozi wanamapinduzi wa Afrika la Patrice Lumumba ni kielelezo cha ushahidi wa uhusiano unaojali ukombozi, utu na umoja wa kweli,” alisema.

Rais Samia alitumia hotuba yake ya kupokea heshima hiyo kwa kueleza kuhusu umuhimu wa elimu akisema imebadili maisha ya watu na mataifa mbalimbali.

“Hakuna taifa linalotaka kuachwa nyuma katika dunia ya sasa yenye mabadiliko makubwa katika maeneo k**a vile akili mnemba na sayansi za mashine. Jambo kubwa kwa Tanzania na Afrika kwa ujumla si kwamba tuingie kwenye ushindani au la bali ni namna gani tutaingia kwenye ushirikiano na kufaidika na mabadiliko haya,” alisema.

Tukio hilo lilihudhuriwa na Naibu Waziri wa Sayansi na Elimu ya Juu wa Urusi, Konstantin Mogilevsky, ambaye katika hotuba yake alisema Rais Samia ametoa mchango mkubwa katika ukuzaji wa elimu nchini kwake katika kipindi cha miaka yake sita madarakani.

RUDN imekuwa na mahusiano ya muda mrefu na Tanzania, kikiwa kimesomesha zaidi ya Watanzania 1,100 tangu kianzishwe mwaka 1960 iliyopita na sasa wanafunzi wa Kitanzania 72 wanapata mafunzo katika ngazi mbalimbali chuoni hapo.


03/06/2026

Rais Samia alivyopokewa na Rais Putin Ikulu ya Kremlin

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokutana na Rais wa Urusi katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, Urusi leo Jumatano Juni 03, 2026.

Dk. Samia yuko nchini Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais Putin, katika ziara inayolenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi pamoja na kukuza ushirikiano katika sekta za uwekezaji na biashara.



03/06/2026

*Rais Samia alivyopokewa na Rais Putin Ikulu ya Kremlin*

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokutana na Rais wa Urusi katika Ikulu ya Kremlin Jijini Moscow, Urusi leo Jumatano Juni 03, 2026.

Dk. Samia yuko nchini Urusi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kwa mwaliko wa Rais Putin, katika ziara inayolenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Urusi pamoja na kukuza ushirikiano katika sekta za uwekezaji na biashara.



03/06/2026
02/06/2026

WANANCHI WAMSIFU RAIS SAMIA KWA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA MICHEZO

Hatua ya Timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 kucheza fainali ya Mataifa Bingwa Afrika (AFCON U17), imewaibua wananchi, walioyahusisha mafanikio hayo na uwekezaji uliofanywa na Dkt Samia Suluhu Hassan katika michezo.

Wananchi hao wameeleza hayo leo, Jumanne Juni 2, 2026 walipofika katika maeneo mbalimbali kulikofungwa skrini kubwa kushuhudia mechi ya fainali kati ya Serengeti Boys dhidi ya Senegal



02/06/2026

Simai: Kuna Yuda Serikalini anakwamisha maendeleo

Mwandishi Wetu

Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Simai Mohamed Said, amesema ndani ya Serikali kuna viongozi wanaomsaliti Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na kukwamisha maendeleo ya nchi.

Simai, ameijenga hoja yake hiyo akiwafananisha viongozi wasaliti na Yuda, huku akiwasihi waache kutumia majina ya viongozi wastaafu na kufanya siasa za 2030 mapema, jambo alilosema linalochonganisha na kuharibu utulivu.

Mbunge huyo, ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma leo, Jumanne Juni 2, 2026 alipochangia hoja katika mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, anaongoza Serikali yake na Watanzania kwa upendo na mshik**ano, lakini kufanikiwa kwa Taifa wakati mwingine kuna watu wanaotembea kinyume.

“Leo nambatiza mmoja aliyekuwepo ndani ya Serikali, ni Yuda. Nasema hivyo kwanini, sisi tunataka maendeleo ya nchi yetu, kosa la mama (Dkt Samia) ni wapi? Kwa sababu ya kumuamini mtu kumbe ni Yuda,” amehoji.

Amesisitiza kiongozi huyo msaliti ameibuka hadi katika nyumba za ibada akitafuta huruma za watu na kutumia majina ya viongozi wastaafu ilimradi aonyeshe anapendwa.

“Yuda huyu amesaliti ndugu zake, hata ile familia ambayo ilimlea kisiasa. Hawataki kumuona huyu Yuda. Hata huko nyuma amewahi kutajwa ni mzigo, lakini leo mzigo huu tunao ndani ya Serikali,” amesema.

Amesema tayari ameshawaumiza wengi, wengine walikuwa mbele na sasa wako nyuma, wako wafanyabiashara, watendaji ndani ya Serikali, wengine walikatwakatwa na wameathirika na wana msongo wa mawazo.

“Lakini Yuda tumeanza kumuona anaibuka katika nyumba za ibada kutafuta huruma ya wananchi na makundi mbalimbali, lakini nataka niseme, wabunge wenzangu na Serikali tuamkeni.

“Leo anapita akitaka kutuaminisha sisi kwamba Rais Magufuli (hayati John, Rais wa awamu ya tano) alimpenda sana yeye Yuda. K**a alimpenda kweli mbona alimrusha huko nje ya Dunia huko alitupwa, huko alitupwa,” amesema.

Amesema waliompenda hayati Magufuli wanajulikana na hadi sasa wapo, hivyo kiongozi huyo aliyefariki dunia Machi 21, 2021 aachwe apumzike kwa amani kwa kuwa alifanya kazi nzuri.


Address

Kwere, Babati
Manyara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when fmmanyara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to fmmanyara:

Share

Category