fmmanyara

fmmanyara Fm Manyara Radio ni Redio Bora inayopatikana wilayani Babati Mkoani Manyara.

FM Manyara inawafikia zaidi ya wasikilizaji Milioni Mbili kupitia masafa ya 92.3 katika mikoa ya Manyara,Arusha, Singida na Dodoma
Tunazalisha vipindi bora kila siku
Kwere Street

Selemani Mwalimu ‘Gomez’ Ni MwananchiNini Maoni yako?
11/08/2026

Selemani Mwalimu ‘Gomez’ Ni Mwananchi

Nini Maoni yako?


Rais Samia, Maaskofu Katoliki wajadili mustakabali mwema wa TaifaRais Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 10, 2026, amekutan...
10/08/2026

Rais Samia, Maaskofu Katoliki wajadili mustakabali mwema wa Taifa

Rais Samia Suluhu Hassan, leo Agosti 10, 2026, amekutana na kufanya mazungumzo na Maaskofu wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania kupitia Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), katika Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma.

Kwa muhibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na TEC, huku yakijadili masuala mbalimbali ya kitaifa yanayoigusa jamii, ikiwemo siasa, imani na maendeleo, pamoja na umuhimu wa kuendelea kudumisha amani, mshik**ano na kujenga mustakabali mwema wa Taifa.

Aidha, mazungumzo hayo yamegusia nafasi ya madhehebu na viongozi wa dini katika kulea jamii yenye maadili mema, uwajibikaji na mshik**ano, pamoja na mchango wao katika kuimarisha ustawi na maendeleo endelevu ya Taifa.

“Rais Samia amewashukuru Maaskofu hao kwa kuona umuhimu wa kukutana na kujadiliana naye masuala yenye tija kwa Taifa, akiwahakikishia dhamira yake ya kuendelea na utamaduni wa kushauriana na kushirikisha viongozi wa dini na makundi mbalimbali katika jamii kuhusu masuala muhimu ya kitaifa kila inapohitajika,”imeeleza taariga hiyo.

Rais Samia anawaita KizimkaziRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na...
10/08/2026

Rais Samia anawaita Kizimkazi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha na vijana wa Makachu pembezoni mwa bustani ya Forodhani, Zanzibar leo Agosti 10, 2026. Ikiwa ni maandalizi ya kuelekea kwenye kilele cha Tamasha la Kizimkazi linalotarajiwa kufanyika kuanzia Agosti 12-14 mwaka huu.



Jukwaa la burudani katika usiku wa Kizimkazi Festival 2026, litanogeshwa na mchanganyiko wa ladha ya muziki kutoka kwa w...
10/08/2026

Jukwaa la burudani katika usiku wa Kizimkazi Festival 2026, litanogeshwa na mchanganyiko wa ladha ya muziki kutoka kwa wasanii walioweka historia kwenye tasnia hiyo nchini. Ni mwendo wa kushangweka na kuzivuna fursa.


Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga  amewataka wananchi wa Mkoa wa Manyara na Watanzania kwa ujumla kujitokeza k...
09/08/2026

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Sendiga  amewataka wananchi wa Mkoa wa Manyara na Watanzania kwa ujumla kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kushiriki katika Mbio za Tanzanite Manyara Marathon zinazotarajiwa kufanyika Agosti 22, 2026, wilayani Babati, huku akieleza kuwa ushiriki wao utasaidia kuchangisha fedha kwa ajili ya kuboresha huduma za afya kwa watoto njiti.

RC Sendiga ametoa wito huo leo baada ya kushiriki mazoezi ya pamoja na wananchi mkoani Manyara, ambayo ni sehemu ya kampeni ya kuhamasisha wananchi kujiandikisha na kujiandaa kushiriki katika mbio hizo.

Hadi sasa zaidi ya washiriki 1,500 wamekwishajiandikisha, huku lengo likiwa ni kufikisha washiriki 3,000 kabla ya siku ya mashindano ambapo  Mbio hizo zitahusisha 200m kwa watoto, kilomita 5, 10, 21 na 42, huku washindi katika makundi mbalimbali wakitarijiwa kupata zawadi ikiwemo fedha taslimu na tuzo.

Mhe. Sendiga amesema ushiriki wa wananchi katika mbio hizo ni zaidi ya kushiriki michezo, bali ni sehemu ya kuchangia jitihada za kuokoa maisha ya watoto wanaohitaji huduma maalumu za afya.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Manyara  Suten Mwabulambo, amesema mbio hizi zitasaidia kuokoa maisha ya watoto wachanga na watoto njiti. 

Aidha, baadhi ya viongozi mbalimbali wakiwemo wakuu wa wilaya na wabunge wamesema wamejipanga kushiriki katika mbio hizo huku wakielezea namna watakavyohamasisha wananchi kushiriki katika mbio hizo za hisani.

Tanzanite Manyara Marathon inalenga kuchangisha zaidi ya shilingi bilioni 1.5, ambazo zitatumika kuboresha huduma za afya kwa watoto njiti, ikiwemo ujenzi wa jengo la huduma za watoto njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Hanang pamoja na ununuzi wa vifaa tiba katika Vituo vya huduma vya Afya katika Mkoa wa Manyara.


RC Sendiga aipongeza fm Manyara kwa kuhabarisha jamiiMkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, ameipongeza FM Manyara Radi...
08/08/2026

RC Sendiga aipongeza fm Manyara kwa kuhabarisha jamii

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Queen Sendiga, ameipongeza FM Manyara Radio kwa mchango wake katika kuhabarisha na kuelimisha jamii kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo.

Aidha, RC Sendiga amewakaribisha wananchi kushiriki katika Marathon ya Msaada kwa Watoto Njiti, inayotarajiwa kufanyika tarehe 22 Agosti mwaka huu.

Amesema marathon hiyo inalenga kuchangisha fedha pamoja na kuongeza uelewa wa jamii kuhusu umuhimu wa kuwasaidia watoto wanaozaliwa njiti kupata huduma stahiki za afya na nafasi ya kukua wakiwa na afya bora


07/08/2026

Samia aonya wanaoharibu miundombinu, ataka ilindwe

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewataka Watanzania kuwa walinzi wa mali za umma, akieleza kuwa mtu anayeharibu miundombinu hiyo, anateketeza kodi za wananchi.

Samia amefafanua kuwa fedha inayokusanywa na Serikali, kisha kutolewa k**a mchango katika utekelezaji wa miradi, hizo ni kodi za wananchi, hivyo hawatakubali ziteketezwe kiuhalisi.

Dkt Samia ameeleza hayo leo Agosti 7,2026 wakati akifungua na kutembelea Mradi wa Mabasi Yanayoenda Haraka Awamu ya Pili (BRT II) katika barabara ya Kilwa, Chang’ombe, Sokoine na Kawawa jijini Dar es Salaam.

“Anayefanya hivyo anachelewesha maendeleo ya Taifa, anarudisha nyuma Taifa, analihujumu Taifa, ni adui wa Taifa letu, tusikubaliane nao,” amesema Dkt Samia

Mbali na hilo, Rais Samia amewahisi vijana kutambua kuwa Tanzania ndio nyumbani hakuna kwingine, hivyo wasikubali kutumika bali watunze kila kilichomo nchini.

“Uharibifu wa miundombinu unaibebesha nchi gharama kubwa ya kuirejesha kwa kutumia fedha ambazo zingekwenda kutumika katika miradi mingine. Hakuna faida ya kufanya hivyo, zaidi ya huduma na shughuli za kiuchumi kudhoofika na kasi ya maendeleo ya Taifa kudorora,” amesema Rais Samia.


VITOL KUJENGA KIWANDA CHA KUSAFISHA MAFUTA GHAFI TANGAKampuni ya kimataifa ya Vitol Bahrain E.C. inatarajiwa kuwekeza ta...
07/08/2026

VITOL KUJENGA KIWANDA CHA KUSAFISHA MAFUTA GHAFI TANGA

Kampuni ya kimataifa ya Vitol Bahrain E.C. inatarajiwa kuwekeza takribani Shilingi trilioni 56 katika ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta ghafi mkoani Tanga, kupitia Mradi wa Tanga Regional Energy Hub.

Makubaliano ya utekelezaji wa mradi huo yamesainiwa kati ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Uganda National Oil Company (UNOC) na Vitol Bahrain E.C., yakishuhudiwa na Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni, Ikulu Dar es Salaam.

Mbali na kiwanda cha kusafisha mafuta ghafi, mradi huo utajumuisha ujenzi wa bohari la kuhifadhi mafuta, eneo la kupokelea mafuta bandarini pamoja na bomba la kusafirisha mafuta yaliyosafishwa kutoka Tanga kwenda Uganda.

Mafuta ghafi yatakayozalishwa nchini Uganda yatasafirishwa hadi Tanga kwa ajili ya kusafishwa kabla ya kurejeshwa Uganda kwa matumizi ya ndani na kusambazwa katika soko la Tanzania pamoja na nchi nyingine za Afrika Mashariki na Kati.

Mradi huo unatarajiwa kuifanya Tanga kuwa kitovu cha biashara na usindikaji wa mafuta katika ukanda, kuongeza usalama wa nishati, kuvutia uwekezaji zaidi, kuongeza mapato ya serikali pamoja na kufungua maelfu ya ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja.


07/08/2026

Samia ateua Majaji wa Uganda, Namibia Tume ya Ghasia za Uchaguzi

Rais Samia Suluhu Hassan leo Agosti 7, 2026 amezindua Tume ya Rais ya Uchunguzi wa Wahusika wa Ghasia na Ukiukwaji wa Sheria katika Matukio ya Ghasia Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025, yenye Makamishna sita, wakiwamo majaji wawili kutoka nje ya nchi.

Uzinduzi huo umefanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, ukifuatia uteuzi wa wajumbe wa tume hiyo uliofanywa Mei 18, 2026. Kuundwa kwa tume hiyo kunatekeleza moja ya mapendekezo ya Tume ya Kuchunguza Matukio ya Vurugu Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, iliyoongozwa na Jaji Mstaafu Mohamed Chande Othman.

Tume hiyo inaongozwa na Jaji wa Mahak**a ya Rufani, Jaji Shabani Lila, ambaye ni Mwenyekiti na Kamishna. Makamishna wengine kutoka Tanzania ni Jaji Mstaafu Gad Mjemmas, Jaji Mstaafu Awadh Bawazir na Jaji Mstaafu Aishieli Sumari, wote wakiwa ni majaji wastaafu wa Mahak**a Kuu.

Makamishna kutoka nje ya nchi ni Petrus Tileinge Damaseb wa Namibia na Cheborion Barishaki kutoka Uganda.

Damaseb anahudumu k**a Naibu Jaji Mkuu wa Mahak**a ya Juu ya Namibia na pia ni Jaji Mkuu wa Mahak**a Kuu ya Namibia, huku Barishaki akiwa Jaji wa Mahak**a ya Rufani ya Uganda, ambayo pia hufanya kazi k**a Mahak**a ya Kikatiba ya Uganda, pamoja na kuwa Jaji wa Kitengo cha Rufani cha Mahak**a ya Haki ya Afrika Mashariki.

07/08/2026

Kizimkazi Festival yabeba matumaini ya wananchi katika miradi

Wananchi wapata matumaini miradi itakayozinduliwa Kizimkazi Festival

Wakazi wa Kizimkazi visiwani Zanzibar, wamesema Tamasha la Kizimkazi litakuwa zaidi ya burudani, kwa kuwa litaambatana na uzinduzi wa miradi ya maendeleo itakayowanufaisha kiuchumi.

Miradi hiyo itakayozinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi ni Jengo la Maendeleo la Shehiya Kibuteni, Barabara ya Kichakachindi–Mtondooni (KM 3.1), Hoteli ya Cave, Tenki la maji la lita milioni 1.5 na mradi wa nyumba za Bopar.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi hao wamesema tamasha hilo limekuwa likiongeza ajira za muda kwa vijana, kukuza biashara na kuboresha huduma za kijamii.

Wamesema uzinduzi wa tenki la maji utasaidia kupunguza changamoto ya upatikanaji wa maji na kuboresha maisha ya wananchi.

Tamasha hilo lenye kaulimbiu ya 'Kizimkazi Kumenoga: Shangwe na Fursa' linatarajiwa kufanyika Agosti 12 hadi 14, mwaka huu.

Address

Kwere, Babati
Manyara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when fmmanyara posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to fmmanyara:

Shortcuts

Share

Category