Mbulu dc

Mbulu dc BOX 74,DONGOBESH,MBULU

KWA PAMOJA TUNAIJENGA MBULU YETU

06/06/2026

FURSA KWA VIJANA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU




KAYA 173 MBULU DC ZAPIMIWA ARDHI BURE NA KUKABIDHIWA HATI ZA KIMILA KWA UFADHILI WA UCRTNa Magreth MbawalaWananchi wa Ha...
04/06/2026

KAYA 173 MBULU DC ZAPIMIWA ARDHI BURE NA KUKABIDHIWA HATI ZA KIMILA KWA UFADHILI WA UCRT

Na Magreth Mbawala

Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wamepata ufadhili wa kupimiwa ardhi bure na kukabidhiwa hati za kimila na shirika lisilo la kiserikali la Ujamaa Community Resource Team (UCRT), kupitia mpango wa matumizi bora ya ardhi uliofanyika katika vijiji kumi.

Hafla hiyo ya kukabidhiwa hati za kimila imefanyika leo, Juni 4, 2026, katika Kata ya Endamilay, huku mgeni rasmi akiwa Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semindu.

Mradi wa matumizi bora ya ardhi umefanyika katika vijiji vya Garbab, Yaeda Kati, Endalat, Dirim, Endamilay, Endanachan, Murkuchida, Harar, Mamagi na Gembakw, na kugharimu kiasi cha shilingi milioni 150.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Semindu aliwashukuru sana UCRT kwa kuona umuhimu wa kupanga matumizi ya ardhi na kuwasaidia wananchi wa kaya duni kuweza kumiliki ardhi. Pia aliwaomba waendelee kuwafikiria wananchi hao kwani uhitaji bado ni mkubwa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Mhe. Yeconia Delless, aliishukuru UCRT kwa kupanga matumizi bora ya ardhi katika vijiji hivyo, akieleza kuwa mpango huo umepunguza migogoro ya ardhi na mipaka baina ya vijiji. Aidha, alisema wananchi sasa wana uwezo wa kukopa katika taasisi za fedha kwa kutumia hati hizo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Ndugu Abubakar Kuuli, alimshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mazingira yanayowezesha mashirika yasiyo ya kiserikali kushirikiana na serikali katika maendeleo ya wananchi. Pia aliishukuru UCRT na kuiomba iendelee kutoa msaada huo, kwani ni vijiji 25 tu kati ya vijiji 76 vilivyopata mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Sambamba na hilo, Mratibu wa Mradi wa Wilaya ya Mbulu, Bw. Dismas Metaya, aliushukuru uongozi wa Wilaya na Halmashauri kwa ushirikiano walioutoa katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi. Pia aliwasihi wananchi kuendelea kutunza mazingira kwa kuepuka ukataji holela wa miti.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na wananchi pamoja na viongozi mbalimbali kutoka vijiji na kata zilizonufaika na mradi huo.



MBULU DC YATHAMINI MCHANGO WA CITY INSTITUTE OF HEALTH KATIKA KUIMARISHA ELIMU, MICHEZO NA USTAWI WA WANAFUNZIHalmashaur...
02/06/2026

MBULU DC YATHAMINI MCHANGO WA CITY INSTITUTE OF HEALTH KATIKA KUIMARISHA ELIMU, MICHEZO NA USTAWI WA WANAFUNZI

Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imepokea kwa furaha msaada wa vifaa na fedha mbalimbali kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa City Institute of Health, Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya mchango wa taasisi hiyo katika kuunga mkono juhudi za Serikali za kuboresha sekta ya elimu, michezo na ustawi wa wanafunzi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Akizungumza leo tarehe 02 Juni 2026 katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Mkurugenzi Mkuu wa City Institute of Health, Ndugu Shaban Mwanga, alisema kuwa taasisi yake imeguswa na juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, jambo lililowahamasisha kutoa msaada huo kwa lengo la kuunga mkono maendeleo ya elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Msaada uliotolewa unajumuisha jezi na mipira kwa ajili ya kuimarisha na kuendeleza michezo mashuleni, mbuzi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Shule ya Msingi Dongobesh Viziwi ikiwa ni sehemu ya kuboresha lishe yao, pamoja na fedha za kuongeza meza katika Shule ya Sekondari Alexander.

Aidha, Mkurugenzi huyo alitoa motisha kwa mwalimu wa kujitolea anayefundisha masomo ya Sayansi katika Shule ya Sekondari Alexander kwa kuongeza kiasi cha shilingi 50,000 kwenye mshahara wake kila mwezi kwa kipindi cha miezi sita, sawa na jumla ya shilingi 300,000.

Akipokea msaada huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Ndugu Abubakar Kuuli, aliishukuru City Institute of Health kwa moyo wake wa kujitolea na ushirikiano katika kuunga mkono maendeleo ya jamii.

"Tunathamini sana mchango huu ambao umegusa maeneo muhimu ya elimu, michezo na ustawi wa wanafunzi wetu. Huu ni mfano mzuri wa ushirikiano kati ya taasisi binafsi na Serikali katika kuharakisha maendeleo ya wananchi. Tunatoa shukrani za dhati kwa City Institute of Health kwa moyo huu wa kizalendo na kujali jamii," alisema Ndugu Kuuli.

02/06/2026

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndugu Abubakar Kuuli akitoa shukrani zake kwa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha sekta ya afya ndani ya Halmashauri hiyo.
na utu tunasonga mbele






HABARI KATIKA PICHAWaheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo Mei 29,2026 wamepewa mafunzo kuhusu mabadi...
29/05/2026

HABARI KATIKA PICHA

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo Mei 29,2026 wamepewa mafunzo kuhusu mabadiliko ya tabianchi ikiwa ni muendelezo wa programu ya SCALE inayoendelea ndani ya Halmashauri.

Sambamba na hilo wameombwa kutoa ushirikiano mara wataalamu watakapofika katika maeneo yao na kusaidia kuhamashisha wananchi kushiriki mikutano itakayoitishwa ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.




Karibu tukuhudumie
29/05/2026

Karibu tukuhudumie



KITUO CHA AFYA CHA ZAIDI YA MILIONI 400 CHAFUNGULIWA KATA YA MARETADUNa Magreth Mbawala,Mbulu DCWananchi wa Kata ya Mare...
28/05/2026

KITUO CHA AFYA CHA ZAIDI YA MILIONI 400 CHAFUNGULIWA KATA YA MARETADU

Na Magreth Mbawala,Mbulu DC

Wananchi wa Kata ya Maretadu, Wilaya ya Mbulu, wanatarajiwa kunufaika na huduma bora za afya kufuatia ufunguzi wa Kituo cha Afya cha Maretadu kilichogharimu zaidi ya shilingi milioni 400 kujengwa.

Kituo hicho kilichofunguliwa leo Mei 28, 2026 na Katibu Tawala wa Wilaya ya Mbulu, Ndugu Paulo Bura, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mheshimiwa Michael Semindu kimegharimu shilingi milioni 442.5, ambapo Serikali Kuu imetoa shilingi milioni 400, Halmashauri ikachangia shilingi milioni 30 kupitia mapato ya ndani, huku wananchi wakichangia shilingi milioni 12.5.

Kituo hicho ambacho kimefunguliwa kwa kuanza kutoa huduma za wagonjwa wa nje (OPD) kinatarajiwa kuhudumia zaidi ya wananchi elfu 15 kutoka ndani na nje ya Kata ya Maretadu.

Akifungua jengo hilo la OPD, Ndugu Bura aliwapongeza wananchi wa Maretadu kwa ushiriki wao mkubwa katika utekelezaji wa mradi huo. Pia aliwataka kuendelea kutunza miundombinu hiyo kutokana na gharama kubwa zilizotumika kujenga kituo hicho.

Sambamba na hilo, aliwataka watumishi wa afya na wauguzi kutoa huduma kwa lugha nzuri na upendo ili kituo hicho kiwe faraja kwa wananchi badala ya kuwa chanzo cha malalamiko.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Mheshimiwa Yeconia Delles, aliwapongeza wananchi wa Maretadu kwa ushirikiano wao katika ujenzi wa kituo hicho na kuwasisitiza kuendelea kushirikiana na Serikali ili kukamilisha majengo yaliyosalia kwa ajili ya kuboresha zaidi huduma za afya.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Ndugu Abubakar Kuuli, aliishukuru Serikali kwa kuendelea kutoa fedha za kuboresha sekta ya afya wilayani hapa.

Alisema kuwa kuanzia mwaka 2021 hadi 2026, jumla ya vituo vya afya vitano vimeongezeka wilayani Mbulu.

Nae Mbunge wa Mbulu Vijijini, Mheshimiwa Dkt. Emanuel Nuwas, aliwapongeza wananchi na viongozi wote waliofanikisha ujenzi wa kituo hicho, akieleza kuwa wananchi walikuwa wakipata changamoto kubwa kufuata huduma za afya katika kata za Haydom na Dongobesh ambazo zipo mbali.



TANGAZO LA USAFI WA MAZINGIRA
28/05/2026

TANGAZO LA USAFI WA MAZINGIRA

TANGAZO LA MATONE YA VITAMIN A KWA WATOTO
28/05/2026

TANGAZO LA MATONE YA VITAMIN A KWA WATOTO

Address

Mbulu
Manyara

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255743583078

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbulu dc posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbulu dc:

Share

Category