Mbulu dc

Mbulu dc BOX 74,DONGOBESH,MBULU

KWA PAMOJA TUNAIJENGA MBULU YETU

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SIKU YA JUMATANO TAREHE 08/10/2025
03/10/2025

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SIKU YA JUMATANO TAREHE 08/10/2025





03/10/2025
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI
03/10/2025

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI





MGANGA MKUU WA WILAYA AMEKABIDHI VIFAA TIBA KWA FUNDI SANIFU VIFAA TIBA.Mganga mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Dr...
03/10/2025

MGANGA MKUU WA WILAYA AMEKABIDHI VIFAA TIBA KWA FUNDI SANIFU VIFAA TIBA.

Mganga mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Dr. Shadrack Makonda amekabidhi vifaa tiba vya shilingi 1,000,000 kwa fundi sanifu Tarehe 01.10.2025.

Vifaa hivi vimekabidhiwa katika ofisi ya Mganga mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu iliyopo katika jengo la Halmashauri.

“Fedha zilizotumika kununua vifaa hivi ni za uboreshaji idara ya afya kwa hiyo vifaa hivi vitamsaidia fundi sanifu kufanya kazi zake za ufundi wa vifaa tiba kwa ufanisi” Alisema Makonda.

Aidha, Makonda amemtaka fundi sanifu kutatua changamoto za vifaa kwenye Hospitali,vituo vya afya na Zahanati.

UKIPATA TANGAZO HILI MTAARIFU NA MWINGINE
02/10/2025

UKIPATA TANGAZO HILI MTAARIFU NA MWINGINE

TANGAZO KWA UMMA
01/10/2025

TANGAZO KWA UMMA

Siku 5 za Madaktari bingwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu
01/10/2025

Siku 5 za Madaktari bingwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu





MIRADI YA BILIONI 5.3  MBULU DC YAKAGULIWA NA TIMU YA UKAGUZI MKOA.Na, Magreth Mbawala,Mbulu DC.Timu ya wataalamu kutoka...
01/10/2025

MIRADI YA BILIONI 5.3 MBULU DC YAKAGULIWA NA TIMU YA UKAGUZI MKOA.

Na, Magreth Mbawala,Mbulu DC.

Timu ya wataalamu kutoka ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara imefanya ziara ya kukagua miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 5,330,975,932.80 kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 29-30/09/2025 ambapo jumla ya miradi thelathini na sita (36) ilikaguliwa.

Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo Shule ya Msingi Mangisa Mil. 88.6, ukamilishaji wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya Msingi shikizi Qatamarish Mil. 20, ukamilishaji wa vyumba 2 vya madarasa Shule ya Msingi Miqaw Mil. 12.5, ujenzi wa kituo cha Afya Masieda Mil. 586, ujenzi wa nyumba ya mwalimu na ukamilishaji wa chumba cha darasa Shule ya Msingi Masieda Mil. 63, ujenzi wa choo cha Wanafunzi Shule ya Msingi Gidhim Mil. 49.4, ukamilishaji wa OPD kituo cha Afya Maretadu Mil. 30, ukamilishaji wa chumba cha maabara Shule ya Sekondari Jakaya Kikwete Mil. 30, ujenzi wa choo cha Wanafunzi Shule ya Msingi Mareba Mil. 38.9,ukamilishaji wa chumba cha maabara Shule ya Sekondari Haydarer Mil. 20 na ukamilishaji wa chumba cha darasa na ujenzi wa vyoo vya Wanafunzi Shule ya Sekondari Geterer Mil. 32.5.

Ujenzi wa Shule mpya ya awali na Msingi katika eneo la Sekondari Dinamu Mil. 330.7, ukamilishaji wa vyumba 2 vya Madarasa Shule ya Msingi shikizi Genda Mil. 15, ukamilishaji wa vyumba 2 vya madarasa Shule mpya ya Msingi Ginyabudel Mil. 25, ukamilishaji wa ofisi ya kata Dinamu Mil. 10, ujenzi wa choo cha Zahanati Muslur Mil 29.4, ujenzi wa choo cha Zahanati Gidmadoy Mil. 27.1, ujenzi wa mabweni 2,madarasa 5 na vyoo matundu 8 katika Shule ya Sekondari Tumati Mil. 401.8, ujenzi wa Shule ya Amali ya Mkoa Bashay Bil. 1.6, ujenzi wa shule ya mkondo mmoja Dumanang Mil. 351, ujenzi wa uzio,ununuzi wa samani na kuweka pavement katika jingo la Halmashauri Mil. 778.2 na ukamilishaji wa nyumba ya Mkurugenzi pamoja na nyumba mbili za wakuu wa idara Mil. 30.

Chanzo cha fedha kwa miradi yote hiyo ikiwa ni mapato ya ndani Mil.216.5, Serikali kuu Bilioni 1.1 na wafadhili na fedha nyingine ikiwemo michango ya wananchi Bilioni 3.9.

TANGAZO TANGAZO
30/09/2025

TANGAZO TANGAZO

MIRADI YA BILIONI 4.7 YAKAGULIWA NA TIMU YA WATAALAMU (CMT) YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU.Na, Magreth Mbawala,Mbulu ...
26/09/2025

MIRADI YA BILIONI 4.7 YAKAGULIWA NA TIMU YA WATAALAMU (CMT) YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU.

Na, Magreth Mbawala,Mbulu DC.

Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu wamefanya ziara ya kukagua miradi ya shilingi Bilioni 4,764,666,012 kwa kipindi cha robo ya nne.

Ziara hiyo ilifanyika Tarehe 22-23/09/2025 katika kata mbalimbali ambapo jumla ya miradi thelathini na tatu (33) ilikaguliwa.

Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na Ujenzi wa Uzio na ununuzi wa samani kwenye jengo la Halmashauri Mil. 778,ukarabati na ujenzi wa madarasa ya elimu maalum na matundu ya vyoo Shule ya Msingi Dongobesh chini Mil. 163.6, ukamilishaji wa vyumba vya madarasa Shule ya Msingi Laghangesh Mil. 15,ujenzi wa madarasa na matundu ya vyoo Shule ya Msingi Mangisa Mil. 88.6,ukamilishaji wa jengo la utawala na nyumba ya mwalimu shule ya Sekondari Bashay Mil. 40,Ujenzi wa Shule mpya ya amali ya Mkoa Bil. 1.6,ukamilishaji wa vyumba vya madarasa shule ya msingi shikizi Masqaroda Mil. 20,ukamilishaji wa ofisi ya kata ya Masqaroda Mil. 10,ukamilishaji wa vyumba vya madarasa shule ya msingi shikizi Miqaw Mil. 12.5,ujenzi wa nyumba ya Mwalimu shule ya msingi Masieda Mil. 51 na ujenzi wa kituo cha afya kata ya Masieda Mil. 586.

Pia miradi ya ujenzi wa shule mpya ya awali na msingi Dinamu Mil. 330.7,ukamilishaji wa madarasa katika shule ya msingi Genda Mil. 25,ujenzi wa choo cha Zahanati Muslur Mil. 29.4,ukamilishaji wa darasa moja shule ya Msingi Muslur Mil. 15,ukamilishaji wa ofisi ya kata Dinamu Mil. 10,ukamilishaji wa vyumba vya madarasa shule ya Msingi Shikizi Genda Mil. 15,ukamilishaji wa nyumba ya mwalimu na vyumba viwili vya madarasa shule ya Msingi Getagujo Mil. 32.4,ujenzi wa choo na ukamilishaji wa nyumba ya mtumishi kwenye Zahanati Gidmadoy Mil. 29.5,ukamilishaji wa Hostel Shule ya Sekondari Maghang Mil. 50 na ujenzi wa madarasa ya awali,elimu msingi na matundu 12 ya vyoo Mil. 132.8 vilikaguliwa.

Aidha,chanzo cha fedha kwa miradi yote hiyo ni Serikali kuu ,Mapato ya ndani,Boost,SWASH,Sequip,WASH,GPE-Lannes,KOICA na TMCHIP

Address

Mbulu
Manyara

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255743583078

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbulu dc posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbulu dc:

Share

Category