30/07/2025
SERIKALI YATOA FEDHA YA VIFAA TIBA VYA SHILINGI MILIONI 200 KWA KITUO CHA AFYA HAYDOM.
Na, Magreth Mbawala, Mbulu DC.
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Daktari Shedrack Makonda amepokea fedha na kununua vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi Milioni 200 kwa ajili ya kituo cha afya Haydom, ikiwa ni fedha kutoka Serikali kuu.
Hayo yamesemwa leo Terehe 30/7/2025 na Daktari Makonda akiwa ofisini kwake Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.
Aidha, baadhi ya vifaa vilivyonunuliwa ni pamoja na Genereta kubwa, mashine ya kufulia, vitanda vya kujifungulia, vitanda na magodoro ya kulalia kwa ajili ya wodi, friji la kuhifadhi dawa, friji la kuhifadhi damu,mashine ya kufisha vidudu (sterilizer machine),drums za vyombo na vifaa vingine mbalimbali.
“Tulipanga bajeti ya Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya vifaa tiba kwenye Kituo cha Afya Haydom na tunashukuru serikali kuu imeleta yote na kufanikisha ununuzi wa vifaa tiba”. Alisema Dr.Makonda.
Mwisho, wananchi wa Kata ya Haydom wameishukuru Serikali kwa kuwaletea huduma za afya kwa karibu.