Mbulu dc

Mbulu dc BOX 74,DONGOBESH,MBULU

KWA PAMOJA TUNAIJENGA MBULU YETU

DC SEMINDU AWAHIMIZA WATUMISHI KUONGEZA BIDII NA UWAJIBIKAJI KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHIWilaya ya Mbulu imeadhimisha ...
01/05/2026

DC SEMINDU AWAHIMIZA WATUMISHI KUONGEZA BIDII NA UWAJIBIKAJI KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI

Wilaya ya Mbulu imeadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani leo tarehe 01/05/2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Dongobesh, ambapo watumishi wa umma wamehimizwa kuongeza bidii, uwajibikaji na weledi katika utendaji wao wa kazi ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semindu, aliwataka watumishi kufanya kazi kwa kujituma na kuzingatia maadili ya utumishi wa umma ili kukabiliana na changamoto zinazowakabili wananchi.

“Ndugu wafanyakazi lisala yenu imebainisha changamoto zinazowakabili watumishi, niwaahidi kuzishughulikia niwaombe watumishi muendelee kufanya kazi kwa bidii, kujituma kwa uweledi na kusikiliza serikali yetu kwa usikivu ili kutatua changamoto za wananchi”. Alisema Semindu

Aidha, Semindu alisisitiza umuhimu wa watumishi kushiriki kikamilifu katika mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili vinavyoathiri jamii.
“Tunamatukio mengi ya ukatili na vitendo vingine vinavyofanana, niwaase watumishi kwa nguvu yenu na ushawishi wenu kuisaidia jamii kuacha vitendo hivyo kwani ni kinyume na sheria” Alisema Semindu

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, ndugu Abubakar Kuuli, ameishukuru Serikali kwa juhudi zake za kupunguza changamoto ya upungufu wa watumishi katika halmashauri.

“Mwaka 2020/2021 nilikuwa na upungufu wa watumishi 1398 lakini kwa kipindi hiki cha miaka 5 tumepata watumishi 744, upungufu uliobakia ni watumishi 654, kwahiyo nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuletea watumishi wengi” Alisema Kuuli

Aidha, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Mhe. Emanuel Nuwas, ameahidi kufikisha bungeni changamoto zilizowasilishwa na chama cha wafanyakazi, ikiwemo suala la kikokotoo kwa watumishi, ili zipatiwe ufumbuzi.

Maadhimisho hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kujadili masuala ya wafanyakazi, kuimarisha mshikamano, na kuweka mikakati ya kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi katika Wilaya ya Mbulu.



MBULU DC YAIBUKA KIDEDEA,YAIFUNGA MBULU TC KWENYE BONANZA LA MEIMOSI Na Magreth Mbawala,Mbulu DC.Halmashauri ya Wilaya y...
01/05/2026

MBULU DC YAIBUKA KIDEDEA,YAIFUNGA MBULU TC KWENYE BONANZA LA MEIMOSI

Na Magreth Mbawala,Mbulu DC.

Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imeonyesha ubabe wake kwenye michezo baada ya kuibuka mshindi dhidi ya Halmashauri ya mji Mbulu kwenye bonanza la michezo lililofanyika leo Mei 1,2026 kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Dongobesh.

Katika mtanange uliovuta hisia za mashabiki wengi,Mbulu Dc iliandika ushindi mnono kwenye mchezo wa mpira wa pete kwa kushinda bao 30 huku Halmashauri ya Mji Mbulu ikiachwa mbali kwa kupata goli 18.

Mbali na mpira pete,Mbulu DC iliendelea kuonyesha ubingwa wake kwa kutwaa ubingwa kwenye mbio za magunia,riadha na mbio za kukimbia na yai.

Bonanza hilo la michezo la meimosi lilipambwa na michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa pete,kuvuta kamba,mbio za magunia,riadha,kula matunda na kukimbia na yai.

Mwisho wa bonanza washindi walizawadiwa zawadi mbalimbali na pongezi nyingi kutoka pande mbalimbali.





HABARI KATIKA PICHA Matukio mbalimbali katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 01/05/2026 katika viwanja vya s...
01/05/2026

HABARI KATIKA PICHA

Matukio mbalimbali katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani 01/05/2026 katika viwanja vya shule ya Sekondari Dongobesh yakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu

TIMU YA TATHMINI NA UFUATILIAJI YATEMBELEA MIRADI YA SHILINGI BILIONI 2.1, YASISITIZA UWAJIBIKAJI NA TIJATimu ya tathmin...
01/05/2026

TIMU YA TATHMINI NA UFUATILIAJI YATEMBELEA MIRADI YA SHILINGI BILIONI 2.1, YASISITIZA UWAJIBIKAJI NA TIJA

Timu ya tathmini na ufuatiliaji ya halmashauri, ikiongozwa na Mkuu wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini, ndugu Haygaru Kalengi, imefanya ziara ya siku tatu mfululizo kukagua utekelezaji wa miradi yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 2.1.

Ziara hiyo imelenga kuhakikisha miradi yote inatekelezwa kwa kuzingatia viwango, thamani ya fedha, pamoja na kuleta tija inayokusudiwa kwa wananchi. Miradi iliyotembelewa inajumuisha sekta mbalimbali zikiwemo elimu, afya, miundombinu na maendeleo ya jamii.

Akizungumza wakati wa ukaguzi huo, ndugu Kalengi alisisitiza umuhimu wa uwajibikaji kwa watendaji na wakandarasi katika kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa. Alieleza kuwa halmashauri itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ili kuhakikisha rasilimali za umma zinatumika ipasavyo.

“Lengo letu ni kuhakikisha kila shilingi inayotolewa na serikali inaleta matokeo chanya kwa wananchi. Hatuwezi kuvumilia uzembe au ubadhirifu katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo,” alisema Kalengi.

Aidha, aliongeza kuwa ushirikiano kati ya wataalamu, viongozi wa maeneo husika pamoja na wananchi ni muhimu katika kufanikisha miradi hiyo.

“Tunasisitiza ushirikiano wa karibu baina ya wadau wote ili kuhakikisha miradi hii inaleta manufaa yaliyokusudiwa kwa jamii,” aliongeza.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi walieleza kuridhishwa na hatua ya halmashauri kufuatilia kwa karibu miradi hiyo, wakisema hatua hiyo itaongeza uwazi na kuimarisha imani ya wananchi kwa serikali yao.

Ziara hiyo ni sehemu ya jitihada za halmashauri kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi, uwazi na kwa kuzingatia malengo ya kuboresha huduma kwa wananchi.

BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZWA KUONGEZA KASI YA UKUSANYAJI WA MAPATONa Magreth Mbawala,Mbulu DCBaraza la Madiwani la Halma...
30/04/2026

BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZWA KUONGEZA KASI YA UKUSANYAJI WA MAPATO

Na Magreth Mbawala,Mbulu DC

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, leo Aprili 30, 2026, limeketi na kujadili masuala mbalimbali, ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2026.

Akihutubia baraza hilo, Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semindu, amelitaka baraza kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato, akisisitiza kuwa mapato ya ndani ndiyo msingi wa maendeleo ya halmashauri.

Mhe. Semindu aliwahimiza madiwani na wataalamu kuwa wabunifu katika kubuni na kuibua vyanzo vipya vya mapato, sambamba na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji ili kuongeza ufanisi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Mhe. Dkt. Emanuel Nuwas, amesema kuwa kupitia ushirikiano kati yake na baraza, imewezekana Shule ya Sekondari Bishop Hhando kuanzisha masomo ya kidato cha tano na sita.

Aidha, Mhe. Dkt. Nuwas aliwataka Waheshimiwa Madiwani kuorodhesha vitongoji ambavyo havina umeme ili viweze kuingizwa katika mipango ya usambazaji wa umeme, akibainisha kuwa katika awamu ya kwanza, vitongoji 59 vitapatiwa huduma hiyo.

Vilevile, alimpongeza Mkuu wa Wilaya kwa kupeleka wataalamu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika kata mbalimbali, hatua iliyosaidia kuongeza idadi ya wananchi wanaopata vitambulisho.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Mhe. Yeconia Delles, aliwapongeza wataalamu wa elimu kwa matokeo mazuri ya wanafunzi wa darasa la saba na kidato cha nne, akihimiza juhudi zaidi ziendelee kudumishwa ili kuongeza ufaulu.

BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZWA KUONGEZA KASI YA UKUSANYAJI WA MAPATONa Magreth Mbawala,Mbulu DCBaraza la Madiwani la Halma...
30/04/2026

BARAZA LA MADIWANI LAHIMIZWA KUONGEZA KASI YA UKUSANYAJI WA MAPATO

Na Magreth Mbawala,Mbulu DC

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, leo Aprili 30, 2026, limeketi na kujadili masuala mbalimbali, ikiwemo utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2026.

Akihutubia baraza hilo, Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, Mhe. Michael Semindu, amelitaka baraza kuongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato, akisisitiza kuwa mapato ya ndani ndiyo msingi wa maendeleo ya halmashauri.

Mhe. Semindu aliwahimiza madiwani na wataalamu kuwa wabunifu katika kubuni na kuibua vyanzo vipya vya mapato, sambamba na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji ili kuongeza ufanisi.

Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini, Mhe. Dkt. Emanuel Nuwas, amesema kuwa kupitia ushirikiano kati yake na baraza, imewezekana Shule ya Sekondari Bishop Hhando kuanzisha masomo ya kidato cha tano na sita.

Aidha, Mhe. Dkt. Nuwas aliwataka Waheshimiwa Madiwani kuorodhesha vitongoji ambavyo havina umeme ili viweze kuingizwa katika mipango ya usambazaji wa umeme, akibainisha kuwa katika awamu ya kwanza, vitongoji 59 vitapatiwa huduma hiyo.

Vilevile, alimpongeza Mkuu wa Wilaya kwa kupeleka wataalamu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) katika kata mbalimbali, hatua iliyosaidia kuongeza idadi ya wananchi wanaopata vitambulisho.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu, Mhe. Yeconia Delles, aliwapongeza wataalamu wa elimu kwa matokeo mazuri ya wanafunzi wa darasa la saba na kidato cha nne, akihimiza juhudi zaidi ziendelee kudumishwa ili kuongeza ufaulu.




TANGAZO LA MEI MOSI
30/04/2026

TANGAZO LA MEI MOSI

HABARI KATIKA PICHAKikao cha baraza la madiwani kikiendelea katika ukumbi mkubwa wa halmashauri muda huu kwaajili ya kup...
30/04/2026

HABARI KATIKA PICHA

Kikao cha baraza la madiwani kikiendelea katika ukumbi mkubwa wa halmashauri muda huu kwaajili ya kupokea taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha Robo ya tatu (Januari -Machi) kikiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Yeconia Deless.

Heri ya siku ya wafanyakazi duniani.
30/04/2026

Heri ya siku ya wafanyakazi duniani.

MATUKIO KATIKA PICHAKitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo Aprili 29,2026 kim...
29/04/2026

MATUKIO KATIKA PICHA

Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo Aprili 29,2026 kimefanya Maadhimisho ya siku ya Dunia ya Kijani ambayo hufanyika kila mwaka mwezi Aprili.

Katika maadhimisho hayo, jumla ya miti 100 ikiwemo ya matunda na kivuli imepandwa katika Shule ya Msingi Dongobesh Viziwi.

Sambamba na hilo Elimu juu ya utunzaji na uhifadhi wa Mazingira ilitolewa na wataalamu kutoka kitengo hicho,ikiwemo faida za kutunza mazingira na matumizi ya nishati safi ya kupikia.




WANANCHI WOTE MNAKARIBISHWA
29/04/2026

WANANCHI WOTE MNAKARIBISHWA

29/04/2026

SIKU ZOTE WATREAT WENZAKO K**A WATU, USIWATRTREAT K**A VITU.

Kauli hii imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu tarehe 28.04.2026 katika hafla ya kuwapongeza walimu wa shule za Sekondari kwa kufanya vizuri katika matokeo ya kidato cha Nne 2025

Address

Mbulu
Manyara

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255743583078

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbulu dc posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbulu dc:

Share

Category