Mbulu dc

Mbulu dc BOX 74,DONGOBESH,MBULU

KWA PAMOJA TUNAIJENGA MBULU YETU

Timu ya Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imeendesha Mafunzo kwaajili ya uandaaji wa Mipango na Bajeti kat...
15/12/2025

Timu ya Wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imeendesha Mafunzo kwaajili ya uandaaji wa Mipango na Bajeti katika Mikoa na Maamlaka za Serikali za Mitaa katika Ukumbi mdogo wa Halmashauri ya Wilaya mapema hii leo 15/12/2025. Mafunzo haya yamefunguliwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Ndugu Juma Kilimba na kuendeshwa na Wataalamu wa Mipango na Bajeti ndugu Haygaru Karengi na Juma Lugwisha.

Aidha Mafunzo haya yamehudhuliwa na Wakuu wa Idara, Vitengo na Maafisa Bajeti yakilenga utengenezaji wa Bajeti inayolenga kujibu mahitaji ya jamii kuanzia ngazi ya Kijiji/Mtaa, Kata, Halmashauri, Wilaya, Mkoa, Wizara ya fedha hadi ngazi ya Bunge.

Pia Waendeshaji wa Mafunzo wamewataka Watalamu hawa kuzingatia Usimamizi bora wa rasilimali, Kipimo cha utendaji, Mwongozo wa utekelezaji wa maendeleo, uwajibikaji na uwazi, Kuchochea maendeleo ya kiuchumi, Kusaidia uratibu wa mahusiano na wadau wa Maendeleo na kuhakikisha usawa na mshikamano wa Kitaifa wakati wa uandaaji wa Mipango ya Bajeti.

KITENGO CHA LISHE KIMEHITIMISHA KIKAO CHAKE KWA AJILI YA MAANDALIZI YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027Kikao Maalum k...
15/12/2025

KITENGO CHA LISHE KIMEHITIMISHA KIKAO CHAKE KWA AJILI YA MAANDALIZI YA BAJETI KWA MWAKA WA FEDHA 2026/2027

Kikao Maalum kwaajili ya Maandalizi ya Bajeti ya kitengo cha lishe kwa mwaka wa fedha 2026/2027 kimefanyika katika ukumbi Mdogo wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo 15/12/2025 kikihudhuliwa na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ndugu Juma Kilimba, Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya Dkt. Shadrack Makonda, Maafisa Lishe na Watalamu mbalimbali kutoka Halmashauri ya Wilaya.
Aidha Vipaumbele vya bajeti hii vimelenga Kuimarisha upatikanaji wa Dawa na bidhaa za Lishe, Kuimarisha siku ya Afya na Lishe ngazi ya Kijiji, Kuimarisha mfumo wa utoaji Madini, Vitamini na Dawa za Minyoo ya Tumbo, Matumizi ya vyakula vilivyorutubishwa Kibailojia, Kuimarisha mfumo wa Elimu ya Lishe katika siku 1,000 za Mtoto, Kuimarisha miradi ya bustani za mbogamboga, miti ya matunda pamoja na mazao yaliyorutubishwa kibaolojia shuleni ( msingi na sekondari) n.k

TANGAZO TANGAZO TANGAZO
14/12/2025

TANGAZO TANGAZO TANGAZO

WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU WAKUPOKEA MAFUNZO JUU YA AFYA YA AKILI
12/12/2025

WATUMISHI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU WAKUPOKEA MAFUNZO JUU YA AFYA YA AKILI

11/12/2025

Nukuu mbalimbali za Mkuu wa Wilaya Mhe. Semindu

TANGAZO LA SEMINA
11/12/2025

TANGAZO LA SEMINA

DC SEMINDU AONGOZA KAMATI YA SIASA KATIKA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU Na. Nashon Bisek...
11/12/2025

DC SEMINDU AONGOZA KAMATI YA SIASA KATIKA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU

Na. Nashon Biseko, MDC

Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Mhe. Dkt Emmanuel Nuwas, Mbunge kutoka Jimbo la Mbulu Mjini Mhe. Zacharia Isaay, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mhe. Yeconia Maleyecky kwa kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndugu Abubakar Kuuli na Timu ya Watalaamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imetembelea Miradi mbalimbali inayoendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mapema leo tarehe 11.12.2025 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan.

Aidha Timu hii imekagua maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Karatu-Mbulu-Hydom-Sibiti River- Lalago-Maswa wa kiwango cha Lami wenye urefu wa Kilometa 389, Mradi unaendelea vizuri ikiwa kipande cha Mbulu Mji hadi Garbabi chenye urefu wa Kilometa 25 chenye thamani ya Shilingi 36,458,655,171/=Kinaendelea na ujenzi ikitegemewa kukamilika kwa ujenzi huu ifikapo Machi 2026, Ikiwa chanzo cha fedha za Mradi huu ni fedha kutoka Serikali kuu.

Pia Timu hii imekagua Mradi wa Madarasa Mawili na vyoo unaoendelea katika Shule ya Msingi Dongobesh Chini unaolenga kuondoa tatizo la ukosefu wa madarasa ya wanafunzi wenye Mahitaji Maalumu, Ukarabati wa Madarasa 8 na Ofisi 3 ikiwa Mradi huu unathamani ya Shilingi 163,600,000/= ambao chanzo chake ni fedha kutoka Serikali kuu kupitia Program ya BOOST.
Sambamba na Miradi hii timu hii imefika pia katika Ujenzi wa Kituo cha Afya Dinamu – Mamagi ambacho kinahusisha Majengo ya Wagonjwa wa nje, Kichomea taka cha kisasa na Choo cha Wagonjwa wa nje, Mradi huu unagharimu kiasi cha 250,000,000/= hadi kukamilika kwake.

DC SEMINDU AONGOZA KAMATI YA SIASA KATIKA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULUNa. Nashon Biseko...
11/12/2025

DC SEMINDU AONGOZA KAMATI YA SIASA KATIKA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU

Na. Nashon Biseko, Mbuludc

Kamati ya Siasa Wilaya ya Mbulu kupitia Tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe. Michael Semindu, Mbunge wa Jimbo la Mbulu Vijijini Mhe. Dkt Emmanuel Nuwas, Mbunge kutoka Jimbo la Mbulu Mjini Mhe. Zacharia Isaay, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mhe. Yeconia Maleyecky kwa kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndugu Abubakar Kuuli na Timu ya Watalaamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu imetembelea Miradi mbalimbali inayoendelea katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mapema leo tarehe 11.12.2025 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan.

Aidha Timu hii imekagua maendeleo ya Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Karatu-Mbulu-Hydom-Sibiti River- Lalago-Maswa wa kiwango cha Lami wenye urefu wa Kilometa 389, Mradi unaendelea vizuri ikiwa kipande cha Mbulu Mji hadi Garbabi chenye urefu wa Kilometa 25 chenye thamani ya Shilingi 36,458,655,171/=Kinaendelea na ujenzi ikitegemewa kukamilika kwa ujenzi huu ifikapo Machi 2026, Ikiwa chanzo cha fedha za Mradi huu ni fedha kutoka Serikali kuu.

Pia Timu hii imekagua Mradi wa Madarasa Mawili na vyoo unaoendelea katika Shule ya Msingi Dongobesh Chini unaolenga kuondoa tatizo la ukosefu wa madarasa ya wanafunzi wenye Mahitaji Maalumu, Ukarabati wa Madarasa 8 na Ofisi 3 ikiwa Mradi huu unathamani ya Shilingi 163,600,000/= ambao chanzo chake ni fedha kutoka Serikali kuu kupitia Program ya BOOST.
Sambamba na Miradi hii timu hii imefika pia katika Ujenzi wa Kituo cha Afya Dinamu – Mamagi ambacho kinahusisha Majengo ya Wagonjwa wa nje, Kichomea taka cha kisasa na Choo cha Wagonjwa wa nje, Mradi huu unagharimu kiasi cha 250,000,000/= hadi kukamilika kwake.

Kheri ya siku ya Uhuru
09/12/2025

Kheri ya siku ya Uhuru

HABARI PICHA:03/12/2025 Kikao kazi cha wadau kuhusu muundo na majukumu ya kamati ya usimamizi wa biashara ya Carbon.Kika...
05/12/2025

HABARI PICHA:

03/12/2025 Kikao kazi cha wadau kuhusu muundo na majukumu ya kamati ya usimamizi wa biashara ya Carbon.

Kikao kimehusisha wajumbe mbalimbali ikiwemo Wahadzabe kutokea Domanga Eshkesh ambao ni wanufaika wa mradi wa Carbon.

AGIZO LA  DC KUHUSU ELIMU YA LISHE KWA BABA NA MAMA LISHE LAANZA KUTEKELEZWA.Maafisa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya M...
04/12/2025

AGIZO LA DC KUHUSU ELIMU YA LISHE KWA BABA NA MAMA LISHE LAANZA KUTEKELEZWA.

Maafisa lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu leo tarehe 04/12/2025 wamepita na kutoa Elimu ya lishe kwa baba lishe na mama lishe katika mji wa Dongobesh ikiwa ni kutekeleza agizo la Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe.Michael Semindu.

Agizo hilo lilitolewa wakati wa kikao cha tathimini ya lishe kwa robo ya kwanza kilichoketi mnamo tarehe 07/11/1025.

Mhe. Semindu alitaka elimu ya lishe iwafikie baba na mama lishe kwa sababu kuna watu wengi wanapata huduma ya chakula kutoka kwao hivyo ni vyema wakawa na elimu hiyo.





WANAMICHEZO WAPOKELEWA KWA SHANGWE MBULU DC.Na Magreth Mbawala, Mbulu DC.Wanamichezo Maria John Tarmo na Mariam Elikana ...
04/12/2025

WANAMICHEZO WAPOKELEWA KWA SHANGWE MBULU DC.

Na Magreth Mbawala, Mbulu DC.

Wanamichezo Maria John Tarmo na Mariam Elikana Gadie jana tarehe 03/12/2025 wamepokelewa kwa shangwe kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu mara baada ya kurejea kutoka kwenye Mashindano ya kitaifa ya wanawake ya mchezo wa riadha.

Maria John Tarmo alishinda mshindi wa tatu kwenye mashindano ya kurusha mkuki kitaifa na mwakani 2026 anatarajia kwenda nchini Japan kuwakilisha nchi kimataifa.Huku Mariam Gadie akiwa ameshika nafasi ya tano kwenye riadha na kupelekea kupata ufadhili wa masomo katika Shule ya Sekondari Filbert Bayi iliyopo Kibaha.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mhe.Yeconia Maleyecky aliwapongeza sana kwa kufanya vizuri na kuwataka madiwani waibue vipaji kutoka kwenye kata zao.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Abubakar Kuuli aliwapongeza wanamichezo hao na kuwataka waendelee na mazoezi ili waendelee kufanya vizuri.Pia aliwaambia wakiwa na changamoto yoyote wasisite kufanya mawasiliano nae.

Aidha,Mbunge wa Mbulu Vijijini Mhe.Emanuel Nuwas,aliwapongeza wanamichezo hao kwa kuitangaza Mbulu Vijijini vizuri na kuwataka Maafisa michezo wa Halmashauri kuendelea kuibua vipaji zaidi.

Mwisho madiwani waliwapongeza wanamichezo kwa kufanya vizuri na kuahidi kuongeza bajeti katika eneo la michezo ili kuendelea kupata vipaji zaidi.



Address

Mbulu
Manyara

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255743583078

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbulu dc posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbulu dc:

Share

Category