Mbulu dc

Mbulu dc HUDUMA NI JADI YETU, KARIBU MBULU DC KWA SASA TUKO DONGOBESH TUKUHUDUMIE

KARIBU BANDA LA MAONESHO LA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU KATIKA VIWANJA WA THEMI NJIRO ARUSHAMBULU  KWETUMBULU VIJIJIN...
07/08/2025

KARIBU BANDA LA MAONESHO LA HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU KATIKA VIWANJA WA THEMI NJIRO ARUSHA
MBULU KWETUMBULU VIJIJINI.�Ikulu MawasilianoWizara ya KilimoMifugo MbuluKilimo na Ufugaji TanzaniaWizara ya KilimoMbunge Mbulu Mjini Zacharia Paul IsaayMBULU VIJIJINI.�

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI WAMETAKIWA KUVIISHI VIAPO.Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbulu Vijijini Bw.Joseph Sa...
04/08/2025

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI WAMETAKIWA KUVIISHI VIAPO.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbulu Vijijini Bw.Joseph Sambo amewataka wasimamizi wasaidizi kuwa waaminifu na waadilifu katika shughuli zote za uchaguzi.

Hayo yamesemwa leo Tarehe 4/8/2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu akiwa anafungua mafunzo ya wasimamizi wa uchaguzi ndani ya kata yanayotarajia kufanyika kwa siku tatu mfululizo,kuanzia tarehe 4-8 Agosti,2025.

"Mmepewa dhamana kubwa sana,nyeti na muhimu kwa mustakabali wa taifa letu,twendeni tukafanye kazi hii kwa uzaendo mkubwa kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa letu na Watanzania kwa ujumla".Alisema Sambo.

Aidha,kabla ya mafunzo hayo,wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi walikula kiapo cha kutunza siri na kujitoa uanachama mbele ya Hakimu Mkazi Mhe.Mgusi Cliford Masinde.

Kauli mbiu ya Uchaguzi 2025:"Kura yako ni haki yako,jitokeze Kupiga Kura"

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI WAMETAKIWA KUVIISHI VIAPO.Hayo yamesemwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbulu Vij...
04/08/2025

WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI WAMETAKIWA KUVIISHI VIAPO.

Hayo yamesemwa na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbulu Vijijini Ndugu Joseph Sambo leo 04/08/2025 wakati akifungua mafunzo ya Wasimamizi wa Uchaguzi ngazi ya kata yanayotarajia kufanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 04/08 hadi 06/08/2025 katika Ukumbi wa Fffars uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Akizungumza na washiriki wa Mafunzo hayo Ndugu.Sambo amesisitiza umuhimu wa Wasimamizi wa Uchaguzi kuwa Waadilifu na waaminifu katika shughuli za uchaguzi.

“Kwa kuzingatia masharti ya ibara ya 74(6) ya Katiba ya Jmahuriy a Muungano wa Tanzania yam waka 1977,Tume Huru ya Taifa ndiyo yenye jukumu la kusimamia na kuratibu uendeshaji wa uchaguzi wa Rais,Wabunge na Madiwani kwa Tanzania Bara.Mmepewa dhamana kubwa sana,nyaeti na muhimu kwa mustakabadhi wa taifa letu,twendeni tukaifanya kazi hii kwa uzalendo kubwa kwaajili ya maslahi mapana ya taifa letu na Watanzania kwa ujumla,”.Alisema Ndugu Sambo.

Kabla ya Mafunzo hayo Wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi walikula kiapo cha kutunza siri na Kujitoa uanachama mbele ya Hakimu mkazi Mhe. Mgusi Cliford Masinde

KAULI MBIU: “Kura yako ni haki yako,jitokeze Kupiga Kura.”
Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania@followersChama Cha MapinduziOfisi ya Rais - TamisemiIkulu TanzaniaIkulu MawasilianoMbulu DCMBULU KWETUHAYDOM JAMII FORUM@followers

MBULU DC YATOA VYETI VYA PONGEZI KWA VIJANA WA HAMASA WA MWENGE WA UHURU 2025.Na, Magreth Mbawala, Mbulu DC.Mkuu wa Wila...
31/07/2025

MBULU DC YATOA VYETI VYA PONGEZI KWA VIJANA WA HAMASA WA MWENGE WA UHURU 2025.

Na, Magreth Mbawala, Mbulu DC.

Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe.Michael Semindu leo Julai 31,2025 amekabidhi vyeti vya pongezi kwa vijana 130 wa hamasa walioshiriki katika mapokezi na kuukimbiza Mwenge wa Uhuru 2025.

Hayo yamefanyika mapema leo katika viwanja vya Haydom huku zoezi hilo likiwa limetanguliwa na Jogging,usafi wa mazingira Kituo cha polisi na stendi ya zamani,kugawa vyeti na mwisho kushiriki chai ya pamoja.

“Nawaahidi nyinyi nyote mtakwenda Mkoani Mbeya mwezi Oktoba kwenda kuzima Mwenge wa Uhuru,hivyo mjiandae vema”.alisema Mhe.Semindu.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Ndugu Abubakar Kuuli, aliwapongeza sana hamasa kwa ushiriki mzuri kwenye Mwenge wa Uhuru na kuwaambia kuwa wanawahitaji sana kwenye matukio mengi na sio Mwenge tu hivyo waendelee na mazoezi wasikae tu.

Aidha,Mratibu wa Mwenge wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Bw. Edes Melly alisema wametoa vyeti hivyo vya pongezi k**a motisha kwa vijana na pia kutii agizo la mkimbiza Mwenge kitaifa Ndugu Ismail Ally Ussi kuwa juhudi za vijana wa hamasa zitambulike.






Karibu Banda la Nanenane la Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu
31/07/2025

Karibu Banda la Nanenane la Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu

SERIKALI YATOA FEDHA YA VIFAA TIBA VYA SHILINGI MILIONI 200 KWA KITUO CHA AFYA HAYDOM.Na, Magreth Mbawala, Mbulu DC.Mgan...
30/07/2025

SERIKALI YATOA FEDHA YA VIFAA TIBA VYA SHILINGI MILIONI 200 KWA KITUO CHA AFYA HAYDOM.

Na, Magreth Mbawala, Mbulu DC.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Daktari Shedrack Makonda amepokea fedha na kununua vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi Milioni 200 kwa ajili ya kituo cha afya Haydom, ikiwa ni fedha kutoka Serikali kuu.

Hayo yamesemwa leo Terehe 30/7/2025 na Daktari Makonda akiwa ofisini kwake Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu.

Aidha, baadhi ya vifaa vilivyonunuliwa ni pamoja na Genereta kubwa, mashine ya kufulia, vitanda vya kujifungulia, vitanda na magodoro ya kulalia kwa ajili ya wodi, friji la kuhifadhi dawa, friji la kuhifadhi damu,mashine ya kufisha vidudu (sterilizer machine),drums za vyombo na vifaa vingine mbalimbali.

“Tulipanga bajeti ya Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya vifaa tiba kwenye Kituo cha Afya Haydom na tunashukuru serikali kuu imeleta yote na kufanikisha ununuzi wa vifaa tiba”. Alisema Dr.Makonda.

Mwisho, wananchi wa Kata ya Haydom wameishukuru Serikali kwa kuwaletea huduma za afya kwa karibu.

MWENGE WA UHURU WILAYA YA MBULU 2025
21/07/2025

MWENGE WA UHURU WILAYA YA MBULU 2025

KWAHERI MWENGE WA UHURU MKOA WA MANYARA.Na,Magreth Mbawala,Mbulu DC.Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Queen Sendiga leo Tarehe...
19/07/2025

KWAHERI MWENGE WA UHURU MKOA WA MANYARA.

Na,Magreth Mbawala,Mbulu DC.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe.Queen Sendiga leo Tarehe 19/7/2025 amekabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego katika Kijiji cha Sagara Wilayani Singida.

Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Manyara uliwasili Tarehe 12 Julai na kuhitimisha mbio zake Tarehe 18 Julai.Ambapo Jumla ya Miradi 53 ilikaguliwa na Mwenge wa Uhuru uliridhia miradi yote hiyo kwa asilimia 100.

Sambamba na hilo Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2025,Ndugu Ismail Ally Ussi alimshukuru Mhe.Mkuu wa Mkoa pamoja na viongozi wote kwa mapokezi mazuri na ushirikiano walioonyesha kipindi chote wakiwa ndani ya Mkoa wa Manyara.

Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu walivyojitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru jana Tarehe 17/7/2025.
18/07/2025

Wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu walivyojitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru jana Tarehe 17/7/2025.

KWAHERI MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU.Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe.Michael Semindu leo  Tarehe 18/7/2025...
18/07/2025

KWAHERI MWENGE WA UHURU HALMASHAURI YA WILAYA YA MBULU.

Mkuu wa Wilaya ya Mbulu Mhe.Michael Semindu leo Tarehe 18/7/2025 amekabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang Mhe. Almishi Hazali.

Mwenge wa Uhuru ulikimbizwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu siku ya jana Tarehe 17/7/2025 huku miradi yake yote 6 ikiwa imekubaliwa na kupitishwa kwa asilimia 100.

Leo Tarehe 17/7/2025 Mwenge wa Uhuru umezindua Daraja la Mawe Garkawe lenye thamani ya Shilingi Milioni 470.Daraja hili ...
17/07/2025

Leo Tarehe 17/7/2025 Mwenge wa Uhuru umezindua Daraja la Mawe Garkawe lenye thamani ya Shilingi Milioni 470.Daraja hili lina urefu wa mita 38.

Daraja hili litanufaisha watu takribani elfu 50 katika kata za Maretadu,Hayderer,Maghang na Labay.

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025 ARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI DAMBIYA-HAYDOMNa,Magreth Mbawala,Mbulu DCKiongozi w...
17/07/2025

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2025 ARIDHISHWA NA MRADI WA MAJI DAMBIYA-HAYDOM

Na,Magreth Mbawala,Mbulu DC

Kiongozi waMbio za Mwenge Kitaifa 2025 Ndugu Ismail Ally Ussi ameridhishwa na mradi wa Maji wa Dambiya-Haydom katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu ambao umegharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 41.2.

Hayo yamezungumzwa leo mara baada ya kumaliza
kukagua mradi huo ambao unatarajia kuwahudumia wananchi wa Vijiji 21 na watu takribani 133,737.

Sambamba na hilo Kiongozi huyo ameridhishwa na namna RUWASA wanavyosimamia Mradi huo mkubwa na wa gharama nyingi na kuwasisitiza wamalize Mradi kwa wakati ili Wananchi wanufaike na huduma hiyo.

Pia Kiongozi wa Mwenge ameupongeza uongozi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu chini ya Mkurugenzi wake Abubakar Kuuli kwa usimamizi mzuri wa mradi huo.






Address

Manyara

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255743583078

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbulu dc posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbulu dc:

Share

Category