Habari 254tv

Habari 254tv Kisiwa Cha Burudani. News And Entertainment
(1)

YOUTUBE- 254
--------------------------------
Entertainment
Politic
Lifestyle
News
International & Local Content
Sports
Education
Events
Showbiz

29/07/2025
NI MARUFUKU WAGENI KUFANYA BIASHARA HIZI TANZANIA !Serikali ya Tanzania imepiga marufuku wageni kufanya biashara 15 ndog...
29/07/2025

NI MARUFUKU WAGENI KUFANYA BIASHARA HIZI TANZANIA !

Serikali ya Tanzania imepiga marufuku wageni kufanya biashara 15 ndogo na za kati nchini humo, hatua ambayo inaweza kuwalazimisha wafanyabiashara wengi kutoka Kenya wanaofanya biashara na wanaotaka kuanzisha biashara nchini humo kuweka pembeni malengo yao.

Kwa mujibu wa notisi iliyotolewa na waziri wa viwanda na Biashara wa Tanzania, Selemani Saidi Jafo, biashara hizo ziko chini ya sekta ya madini, utalii, kilimo, mazingira na teknolojia.

Biashara hizo ni pamoja na kuhamisha fedha kwa njia ya simu, ukarabati wa simu za mkononi na vifaa vya kielektroniki, biashara za saluni (isipokuwa zinafanywa hotelini au kwa madhumuni ya utalii), usafi wa nyumba, ofisi na mazingira, na uchimbaji mdogo wa madini.

Nyingine ni pamoja na huduma za posta na vifurushi, kuongoza watalii, kuanzisha na kuendesha stesheni za redio na TV, majumba ya makumbusho na maduka ya kudadisi, udalali wa biashara na mali isiyohamishika.

Wageni pia wamepigwa marufuku kufanya kilimo, shughuli za ununuzi wa mazao, umiliki au uendeshaji wa mashine au vifaa vya kamari, isipokuwa ndani ya kasino, na umiliki na uendeshaji wa viwanda vidogo. Mgeni atakayepatikana akifanya biashara hizi atatozwa faini ya hadi Tsh10 milioni (Ksh502,927) na kifungo kisichozidi miezi sita.

Kwa mujibu wa waziri huyo, raia yeyote wa Tanzania ambaye atapatikana akiwasaidia wageni kufanya biashara hizo atatiwa hatiani na kuadhibiwa kwa kifungo cha miezi mitatu jela, pamoja na faini ya Tsh5 milioni (Ksh251,463).

Tangazo hilo linakuja siku chache baada ya Wizara ya Fedha ya Tanzania, katika notisi ya mapema mwezi huu, kutangaza kwamba wageni wanaonuia kusafiri kuja nchini, kuanzia mwaka ujao, watatakiwa kulipa karibu Tsh. 115,000 sawa na Ksh5,700 za Kenya ili kununua bima ya lazima ya kusafiri kwa watalii. Kwa mujibu wa Wizara, hatua hiyo inanuia kuondoa mzigo kwenye mifumo ya afya ya umma nchini.

Maagizo hayo yamewasaza wananchi kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC); hata hivyo, wasafiri wanaoingia nchini kutoka nje ya EAC/SADC bado wanaweza kutakiwa kulipa ada hiyo.

Bima hiyo ilikuwa sehemu ya ajenda ya mwaka wa fedha wa 2025/2026 lakini ilisogezwa hadi Januari 2026 ili kutoa nafasi zaidi ya mashauriano na wadau.

MWANDISHI Fazul Khalid

29/07/2025

Kocha Mbobevu Rishadi Shedu Akiongelea Kandarasi Ya Wachezaji , Mchezaji Akipata Majeraha Katika Klabu Yake Na Bima Ya Afya Kwa Wachezaji. Pia Amegusia Viwanja Vyetu Na Uhuni Wa Mashabiki Wa Soka ( Football Hooliganism)....

Habari 254tv BongaTube Media

MOHAMMED BAJABER AMEGURA KIKOSI CHA HARAMBEE STARS ?Hali Ya Wasi Wasi Katika Kambi Ya Harambee Stars Ya Kenya Kuelekea C...
28/07/2025

MOHAMMED BAJABER AMEGURA KIKOSI CHA HARAMBEE STARS ?

Hali Ya Wasi Wasi Katika Kambi Ya Harambee Stars Ya Kenya Kuelekea CHAN 2024 Baada Ya Mshambuliaji Wa Police Fc Mohammed Bajaber Kukosa Kuonekana Kambini .

Mohammed Bajaber Amekuwa Mshambuliaji Muhimu Sana Kwenye Kikosi Hicho Na Ametarajiwa Kuonyesha Utemi Wake Uwanjani Katika Mechi Ya Ufunguzi CHAN 2024 Kati Ya Taifa La Kenya Na DRC Congo Na Mechi Zinginezo.

Duru Za Kuaminika Zinadokeza Kuwa Huenda Mohammed Bajaber Amejiunga Rasmi Na Klabu Ya Simba SC Tanzania Nchi Jirani Ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Hivo Basi Kumuacha Nje Ikikumbukwa CHAN Inahusisha Wachezaji Wa Ndani .

Mashabiki Wa Soka Nchini Kenya Wamekuwa Na Maoni Gongana/Tumbo Joto Huku Wengine Wakidai Mchezaji Husika Siye Mzalendo Na Alifaa Ahamie Baada Ya Mchuano Wa CHAN Kumalizika

MWANDISHI Fazul Khalid

28/07/2025

Aliwahi Kuwa Kocha Wa Klabu Ya Coastal Union Kutoka Tanga, Tanzania. Akanoa Vilabu Kadhaa Nchini Kenya Kam Vile KCB FC, Alaskan FC, Ulinzi FC NK. Wakati Fulani Akapewa Jukumu La Kulinoa Timu Ya Taifa The Harambee Stars ... Hapa Tunamrejelea Kocha Mbobevu Rishadi Shedu Kutoka Malindi Nchini Kenya. Tulikaa Kitako Naye Akatuadisia Mengi Kuhusu Maisha Yake Ya Ukocha , Mpira Wa Miguu !

BongaTube Media | Malindi Kenya Habari 254tv

Je ,Mchora Katuni Masoud Kipanya Amewasilisha Hoja Gani Hapa ?
27/07/2025

Je ,Mchora Katuni Masoud Kipanya Amewasilisha Hoja Gani Hapa ?

Nyota wa Bongoflava Juma Jux na mkewe Priscilla watangaza wanatarajia mtoto wao wa kwanza pamoja.Kongole Kwao !
25/07/2025

Nyota wa Bongoflava Juma Jux na mkewe Priscilla watangaza wanatarajia mtoto wao wa kwanza pamoja.

Kongole Kwao !

Wanaume ,Njooni Kwenye Kikao Hapa Kuna Mdahalo Pevu Inawahusu !
25/07/2025

Wanaume ,Njooni Kwenye Kikao Hapa Kuna Mdahalo Pevu Inawahusu !

Address

Mapumulo

Telephone

+254704000104

Website

https://www.youtube.com/@habari254

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari 254tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Habari 254tv:

Share