masasione_onlinetv

masasione_onlinetv business number
Call: 0715 507 823 / 0656 733 060
MTWARA || MASASI

27/03/2026
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limemkamata Ibrahimu Nzumbi Mugendi (31) mkazi wa Kijiji cha Makere Wilaya ya Kasulu Mkoa...
27/03/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limemkamata Ibrahimu Nzumbi Mugendi (31) mkazi wa Kijiji cha Makere Wilaya ya Kasulu Mkoa wa Kigoma kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mtuhumiwa alifika Mkoa wa Mtwara tarehe 18.02.2026 na kufikia katika nyumba ya kulala wageni(jina limehifadhiwa) ilipofika tarehe 26.02.2026 mtuhumiwa alikwenda katika Ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Mtwara-Ofisi ya Katibu tawala wa wilaya na kuomba kibali cha kusaidiwa kupata michango ya fedha kutoka kwa watu binafsi na taasisi mbalimbali ndani ya wilaya ya mtwara kwa madai ya kuwa na changamoto ya kuongea (Bubu).

Mtuhumiwa alifanikiwa kupatiwa kibali hicho chenye Kumb na.B58/274/03/123 na kuanza kupita katika taasisi za serikali na kwa watu binafsi kwa lengo la kuomba michango hiyo.

Baada ya ufuatiliaji wa kina ilibainika kuwa mtuhumiwa hana changamoto yoyote ya ulemavu wa kuongea (Bubu) bali ameamua kutumia njia hiyo kwa lengo la kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mtuhumiwa amekamatwa tarehe 25.03.2026 katika nyumba ya kulala wageni(jina limehifadhiwa) akiwa na jumla ya Tsh. 1800,000/=(Millioni moja na laki nane) ambazo alikuwa amechangiwa na watu binafsi na taasisi mbalimbali ndani ya wilaya ya mtwara.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa mtuhumiwa amepita katika jumla ya taasisi kumi (10) za serikali na zile za watu binafsi.

Upelelezi utakapo kamilika mtuhumiwa atafikishwa kwenye mamlaka nyingine za kisheria.

Jeshi la Polisi mkoa wa mtwara linaendelea kufanya ufuatiliaji mkali dhidi ya baadhi ya watu wanaofanya utapeli na kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia kwa watu binafsi, pamoja taasisi mbalimbali.


Sponsored by

Kamati  ya kudumu ya Bunge ya  Maji na Mazingira imejadili na kuidhinisha Randama ya Makadirio ya Mapato  na Matumizi ya...
26/03/2026

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira imejadili na kuidhinisha Randama ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa mwaka
2026/27.

Randama imejadiliwa na wajumbe wa kamati hiyo ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Jackson Kiswaga (Mb) Bungeni Jijini Dodoma.

Mkurugenzi Msaidizi wa Mipango na Bajeti wa Wizara ya Maji Bw. Tedy Mwaijumba kwa niaba ya Waziri wa Maji amefanya wasilisho la Randama.

Randama imeainisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Maji kwa Mwaka 2026/2027, pia vipaumbele ikiwemo kuendelea na utekelezaji wa miradi ya maji ya vijiji 867, mabwawa 35 na Miradi 220 ya maji mijini, kuendelea kutekeleza mradi wa kimkakati wa Mpango wa Mtandao wa Taifa wa usambazaji maji (Gridi ya Maji ya Taifa), Matumizi ya Dira janja, kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji, kuimarisha uendelevu wa huduma za maji na uhimilivu wa mabadiliko ya tabianchi, kupunguza upotevu wa maji, kuendeleza vyanzo mbadala vya fedha ya utekelezaji wa miradi ya maji, kuimarisha Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Maji na kuimarisha mfumo wa uratibu wa utekelezaji wa miradi ya maji.

Kuidhinishwa kwa Randama hiyo na Kamati ya Maji na Mazingira kunatoa fursa kwa Wizara ya Maji kuandaa Hotuba ya Bajeti ya 2026/2027 ili kuwasilishwa katika bunge la Bajeti.

Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amemshukuru Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Jackson Kiswaga (Mb) na Wajumbe wote wa kamati kwa kujadili na kuidhinisha randama hiyo na kuahidi kuzingatia maoni ya kamati katika hotuba ya bajeti.


Sponsored by
Cc. .

Timu Ya Stand Fc Masasi Mabingwa Wa Mkoa Wa Mtwara Wameanza na Ushindi Wa Goli Mbili 2 Kwa Sifuri 0 dhidi ya FGA TALENTS...
14/03/2026

Timu Ya Stand Fc Masasi Mabingwa Wa Mkoa Wa Mtwara Wameanza na Ushindi Wa Goli Mbili 2 Kwa Sifuri 0 dhidi ya FGA TALENTS Fc ya Morogoro Kwenye Uwanja Wa Mwanakalenge Uliopo Bagamoyo Mkoani Pwani

Mchezo Huo Ulioanza Kutimua Vumbi Majira ya Saa 8 Mchana Wa Leo Umekuwa Mchezo Mzuri kwa Stand Fc Masasi ambapo Nahodha Wa Abdul Patrick (Tshishimbi) aliifungia Timu Yake Goli Zote mbili 2

Tshishimbi alifunga Goli la Kwanza dakika 19 ya Mchezo huku Goli la Mwisho akifunga kwenye Dakika za Nyongeza Ya Kipindi cha Pili cha Mchezo

Wawakilishi hao wa Mkoa Wa Mtwara Stand Fc Masasi itashuka tena Dimbani Siku Ya Tarehe 16 kumenyana na Friends Rangers Ya Dar Es Salaam kwenye Mashindano Hayo Ya Mabingwa Wa Mikoa.


Sponsored by

12/03/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limewakamata watu wawili kwa tuhuma za kujihusisha na wizi wa mali mbalimbali zikiwemo televisheni na mashine za michezo ya video katika Wilaya ya Masasi.
Watuhumiwa hao ni Seleman Mohamed Ahmad (22) mkazi wa Kijiji cha Upanga pamoja na Abubakari Mahamud (21) mkazi wa Kijiji cha Masasi Mbovu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Polisi, watuhumiwa hao walikamatwa wakiwa na mali zinazodhaniwa kuwa za wizi zikiwemo televisheni nne (04) za ukubwa wa inch 32, kati ya hizo tatu ni aina ya Alitop rangi nyeusi na moja aina ya Ailyons rangi nyeusi.
Aidha, polisi walikamata mashine ya kuchezea michezo ya video (PlayStation 4) aina ya Sony pamoja na pad 12 za kuchezea michezo hiyo, ambapo mbili zina rangi nyekundu, tatu rangi ya kijani na saba rangi nyeusi.
Jeshi la Polisi limesema linaendelea na uchunguzi zaidi ili kubaini chanzo cha mali hizo pamoja na kuwabaini wahusika wengine wanaoweza kuhusika na tukio hilo.

12/03/2026

Mahakama mbalimbali mkoani Mtwara zimewahukumu watu wanne vifungo vya muda mrefu jela baada ya kupatikana na hatia katika makosa mbalimbali ikiwemo mauaji, uhujumu uchumi, ujangili na dawa za kulevya.
Mahakama ya Wilaya ya Nanyumbu imemhukumu Hassan Issa Shaban (27) mkazi wa Kitongoji cha Nanyumbu kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya uhujumu uchumi na kupatikana na nyara za serikali ambazo ni nyama za wanyama pori pamoja na kumiliki silaha ndani ya hifadhi bila kibali.
Katika kesi nyingine, mahakama hiyo pia ilimhukumu Mwajuma Athuman Kais (38) mkazi wa Kitongoji cha Mtambaswala Kijiji cha Lukula kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na vipande 17 vya nyama ya mnyama pori aina ya nyati.
Aidha, Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mtwara imemhukumu Ally M***a Abrahaman (45) mkazi wa Kijiji cha Mbagala Mbuyuni Wilaya ya Nanyumbu kifungo cha miaka 12 jela baada ya kupatikana na hatia ya kosa la kuua bila kukusudia kufuatia tukio lililosababisha kifo cha mwanamke Catherine Said Chivale (69).
Katika tukio jingine, Mahakama ya Wilaya ya Mtwara imemhukumu Hawa Ally Nantoni (60) mkazi wa Bomba la Bure Magomeni kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kupatikana na dawa za kulevya aina ya bangi yenye uzito wa gramu 90.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limesema linaendelea kushirikiana na vyombo vingine vya dola katika kuhakikisha sheria zinafuatwa na wahalifu wanachukuliwa hatua kali za kisheria.

MBUNGE wa Jimbo la Masasi,ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Dkt.Leonard Akwilapo ameandaa hafla ya maalumu ya Iftari iliyow...
11/03/2026

MBUNGE wa Jimbo la Masasi,ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Dkt.Leonard Akwilapo ameandaa hafla ya maalumu ya Iftari iliyowakutanisha waumini wa dini ya kiislamu pamoja na wananchi mbalimbali wa jimbo la Masasi wakati wa mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.

Iftari hiyo imefanyika katika ukumbi wa Emirates uliopo mjini Masasi na kuudhuliwa na viongozi mbalimbali wa dini, viongozi wa serikali za mitaa,pamoja na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya jimbo la Masasi.

Akizungumza katika Iftari hiyo Mbunge huyo, Dk. Leonard Akwilapo amesema kuwa lengo la kuandaa Iftari hiyo ni kuendeleza mshikamano,upendo na umoja miongoni mwa wananchi wa Masasi bila kujali itikadi za kidini au kijamii sambasamba na kuijenga Masasi.

Amesema kuwa mwezi wa Ramahani ni kipini muhimu cha ibada,huruma na kusaidiana hivyo hafla hiyo imetoa nafasi kwa waumini wa kiislamu kufuturu pamoja na kuimarisha uhusiano baina ya viongozi na wananchi kwa kukaa pamoja na kubailishana mawazo.

Wananchi pamoja na viongozi wadini na serikali waliodhulia hafla hiyo ya iftari akiwamo mkuu wa wilaya ya Masasi, Rechel Kassanda wamempongeza Mbunge huyo, Dk.Akwilapo kwa kuandaa hafla hiyo ambayo imekutakunisha wananchi wa Masasi na viongozi wao na kuzungumza kwa lengo la kuindeleza Masasi.


Sponsored by

10/03/2026

JE UNAFAHAMU ALIKIBA NA DIAMOND NI MAJENERALI WA AFRIKA

Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi ambaye ni mbunge wa Jimbo la Masasi mjini mhe Dkt. Leonard Akwilapo ameka...
08/03/2026

Waziri wa ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi ambaye ni mbunge wa Jimbo la Masasi mjini mhe Dkt. Leonard Akwilapo amekabidhi baiskeli 10 kwa walemau wa viungo.

Tukio la kukabidhi limefanyika leo March 8.2026 katika ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Masasi mkoani Mtwara.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano hayo Dkt Akwilapo amesema wananchi wanahitaji furaha ili waendelee kuipa dhamana CCM ifikapo 20230.

Wakizungumza na wanahabari baadhi ya walemavu waliopata baiskeli hizo wamesema zitawasaidia kwa kiasi kikubwa katika shughuli zao za kiuchumi ukilinganisha na hapo awali ilikuwa ikiwawia vigumu.

Sponsored by

Leo March 8 ni siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa mdhamini wetu  tunamtakia maisha marefu yenye amani na upendo.  Sponsor...
08/03/2026

Leo March 8 ni siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa mdhamini wetu tunamtakia maisha marefu yenye amani na upendo.


Sponsored by

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa Mkoa wa Mtwara mwaka huu yamefanyika katika Wilaya ya Masasi kwenye Viwanja ...
08/03/2026

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa Mkoa wa Mtwara mwaka huu yamefanyika katika Wilaya ya Masasi kwenye Viwanja vya Sabasaba Masasi Mjini, yakihusisha mamia ya wanawake pamoja na wadau mbalimbali kutoka taasisi za serikali na zisizo za serikali.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Donald Msengi, ambaye aliongoza wananchi katika tukio hilo lililoambatana na shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi.
Shughuli za maadhimisho zilianza kwa maandamano yaliyowashirikisha wanawake kutoka makundi tofauti wakiwemo wafanyabiashara, vikundi vya wanawake wajasiriamali, watumishi wa umma, wanafunzi pamoja na wanachama wa mashirika mbalimbali. Maandamano hayo yalipita katika mitaa mbalimbali ya Mji wa Masasi kabla ya kuhitimishwa katika Viwanja vya Sabasaba.
Katika viwanja hivyo kulifanyika maonyesho maalum ya kazi na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa na wanawake wajasiriamali pamoja na taasisi za serikali na zisizo za serikali. Maonyesho hayo yalilenga kuonesha mchango wa wanawake katika maendeleo ya kiuchumi na kuhamasisha jamii kuunga mkono juhudi za wanawake katika shughuli za uzalishaji na biashara.
Aidha, maadhimisho hayo yalipambwa na burudani mbalimbali zikiwemo ngoma za asili, muziki na vikundi vya sanaa vilivyotumbuiza na kutoa ujumbe wa kuhamasisha haki, usawa na uwezeshaji wa wanawake na wasichana katika jamii.
Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara aliwahimiza wanawake kuendelea kushirikiana, kujituma katika shughuli za maendeleo na kutumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi huku akisisitiza umuhimu wa jamii kuendelea kulinda haki za wanawake na wasichana.
Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 Machi, yakilenga kutambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya jamii pamoja na kuhamasisha usawa wa kijinsia duniani.

Address

MASASI TOWN COUNCIL (MTC)
Masasi
MIGONGO

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when masasione_onlinetv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share