01/06/2026
WATU WANNE WAMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI KUACHA NJIA NA KUPINDUKA MKOANI MBEYA.
Mei 31, 2026 saa 9:10 alasiri huko maeneo ya maji mazuri katika barabara ya Mbeya – Chunya, Gari yenye namba za usajili T134DFB aina ya Mitsubishi Basi la abiria kampuni ya Mwasote likitokea Mbeya kuelekea Chunya likiendeshwa na dereva Nehemia Sanga [50] mkazi wa Uyole iliacha njia, kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne wanaume 3 na mwanamke 1 umri kati ya 35 – 40.