MAWIO TZ

MAWIO TZ Karibu katika ukurasa huu maalumu wa MAWIO TZ, unaokuhabarisha Taarifa/Habari na Makala mbalimbali ndani na nje ya Tanzania 🇹🇿

01/06/2026

WATU WANNE WAMEFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA GARI KUACHA NJIA NA KUPINDUKA MKOANI MBEYA.

Mei 31, 2026 saa 9:10 alasiri huko maeneo ya maji mazuri katika barabara ya Mbeya – Chunya, Gari yenye namba za usajili T134DFB aina ya Mitsubishi Basi la abiria kampuni ya Mwasote likitokea Mbeya kuelekea Chunya likiendeshwa na dereva Nehemia Sanga [50] mkazi wa Uyole iliacha njia, kupinduka na kusababisha vifo vya watu wanne wanaume 3 na mwanamke 1 umri kati ya 35 – 40.

29/05/2026

Kamati ya Maandalizi ya Mpalano Festival imefika katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Rungwe, Mheshimiwa Jaffar Haniu, kwa ajili ya kufanya mazungumzo kuhusu ushiriki wa Wilaya ya Rungwe katika tamasha hilo kubwa la kiutamaduni na utalii. Ziara hiyo imelenga kuimarisha ushirikiano katika kutangaza vivutio vya utalii, utamaduni na fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya wilaya hiyo kuelekea Mpalano Festival 2026.

29/05/2026
29/05/2026

28/05/2026

RC MTANDA AWATAKA MAAFISA HABARI KUZIFANYIA KAZI TAARIFA ZA MITANDAONI KWA WAKATI

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewataka Maafisa Habari, Uhusiano na Mawasiliano kuisaidia serikali kwa kujibu shutuma zinazotolewa kwenye mitandao ya jamii kwa wakati ili umma uwe na taarifa rasmi na ufafanuzi wa masuala mbalimbali mara tu yanapoibuka.

Mhe. Mtanda ameyasema hayo leo tarehe 28 Mei, 2026 wakati akizungumza na uongozi wa Chama cha Maafisa Uhusiano, Habari na Mawasiliano (TAGCO) wa Serikali waliofika ofisini kwake kujitambulisha kufuatia kikao kazi kinachotarajiwa kufanyika mkoani tarehe 1-5 Juni, 2026.

28/05/2026

Kauli ya Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara Aman Golugwa Baada ya Mahak**a kutoa Uamuzi wa kesi ya mgawanyo wa Mali za CHADEMA

28/05/2026

MAHAKAMA YAFUTA KESI YA MGAWANYO WA MALI YA CHADEMA

Leo tarehe 28 Mei 2026 Mahak**a Kuu Masijala ya Dar es salaam imetoa uamuzi na kukubaliana na hoja CHADEMAkwamba kitendo cha waleta madai kushindwa kuonesha lini hasa madai yao yalianza kinainyima mahak**a nafasi ya kujiridhisha k**a kweli inayo mamlaka ya kusikiliza madai husika.

Kufuatia hali hiyo, kesi hiyo namba 8323\/2025 imefutwa rasmi leo.

KAMANDA KUZAGA AMPONGEZA ASKARI ALIYEOKOA MAISHA YA DEREVA BODABODA Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi M...
26/05/2026

KAMANDA KUZAGA AMPONGEZA ASKARI ALIYEOKOA MAISHA YA DEREVA BODABODA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga leo Mei 26, 2026 amempongeza kwa kumpa cheti cha pongezi Konstebo wa Polisi Baraka Wambura Nyakarungu kwa kitendo cha ujasiri alichofanya na kuokoa maisha ya mhanga wa ajali ya Pikipiki.

Konstebo wa Polisi Nyakarungu mnamo Mei 14, 2026 majira ya saa 12 alfajiri akiwa kwenye Daladala akitokea kazini kuelekea nyumbani alipofika eneo la Kilimo Uyole alikuta ajali iliyohusisha Gari ya abiria na Pikipiki na kumchukua majeruhi, kumfikisha kituo cha Polisi Uyole kwa ajili ya kupatiwa PF3 na kisha kumfikisha katika Hospitali ya Igawilo kwa matibabu.

Mhanga wa ajali hiyo alipatiwa matibabu na kwa sasa anaendelea vizuri. Jeshi la Polisi lina thamini na kutambua kazi mbalimbali zinazofanywa na Askari kwa kuzingatia Nidhamu, Haki, Weledi na Uadilifu.

25/05/2026

Mfanyabishara wa Nyumba ya kulala Wageni wilayani Kyela alalamikia utaratibu Mpya wa ulipaji kodi ya Kitanda

Address

Mbambo
Mbeya
53525

Telephone

+255676506998

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MAWIO TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MAWIO TZ:

Share