MAWIO TZ

MAWIO TZ Karibu katika ukurasa huu maalumu wa MAWIO TZ, unaokuhabarisha Taarifa/Habari na Makala mbalimbali ndani na nje ya Tanzania 🇹🇿

Watatu Wateuliwa na CCM kuwa Wagombea na Rasmi Kuipeerusha Bendera ya CCM ngazi ya Ubunge  katika Majimbo yao bila Kupin...
29/07/2025

Watatu Wateuliwa na CCM kuwa Wagombea na Rasmi Kuipeerusha Bendera ya CCM ngazi ya Ubunge katika Majimbo yao bila Kupingwa, na Kufanya kuwa ndio Majimbo Pekee ambayo yamekuwa na Wagombea Wachache zaidi kuelekea Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025

Wagombea hao ni:

Jimbo la Bukombe 1 - Dotto Mashaka Biteko
Jimbo la Mchinga 1 - Salma Rashid kikwete
Jimbo la Chalinze 1 - Ridhiwani Jakaya Kikwete

Pamoja na Majimbo hayo, Jimbo la Makambako nalo limeingia kwenye Orodha ya kuwa na Wagombea Wachache albapo ni Wagombea wawili tu, bao ni Daniel Chongolo na Deo Sanga

CCM yawateua 10 Kuchuana Ubunge Jimbo la Kongwa Dodoma.Wateule hao ni:(1) Ndugu Yustino NDUGAI(2) Ndugu Balozi. Emmanuel...
29/07/2025

CCM yawateua 10 Kuchuana Ubunge Jimbo la Kongwa Dodoma.

Wateule hao ni:
(1) Ndugu Yustino NDUGAI
(2) Ndugu Balozi. Emmanuel David Mwaluko Luhembe MBENNAH
(3) Ndugu Ngaya David MAZANDA
(4) Ndugu Deus Gracewell SEIF
(5) Ndugu Philip Eliud CHIWANGA
(6) Ndugu Paschal Joseph MAHINYILA
(7) Ndugu Dkt. Simon Saulo NGATUNGA
(8) Ndugu Dkt. Samora Stanley MSHANG’A
(9) Ndugu Isaya Mngurumi MOSES
(10) Ndugu Elias John MDAO

Sambba na hilo yafuatayo ni Majimbo yenye Wagombea zaidi ya 8 (
Majimbo 14):

Ilemela 9
Arumeru mashariki 8
Temeke 8
Kibamba 8
Kawe 8
Kinondoni 8
Dodoma mjini 8
Mwanga 8
Kilombero 8
Morogoro kusini 8
Mvomero 8
Itwangi 8
Bukene 8
Lushoto 8
Kiembe samaki 8
Handeni vijijini 8
Dimani 8
Kiembe samaki 8

Wabunge 7 wa awamu iliyoishia mwaka huu 2025, Majina yao yamekatwa na hawatakua Miongoni mwa wale  watakaochuana Kusaka ...
29/07/2025

Wabunge 7 wa awamu iliyoishia mwaka huu 2025, Majina yao yamekatwa na hawatakua Miongoni mwa wale watakaochuana Kusaka Kura ya Maoni ili Kuipeerusha Bendera ya CCM kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 katika Majimbo yao.

Na hawa ndio VIGOGO WA CCM WALIOACHWA KWENYE MCHUJO huo:

1: Luhaga Mpina - Jimbo la kisesa
2: January Makamba - Jimbo la Bumbuli
3: Josephat Gwajima - Jimbo la Kawe
4: Mrisho Gambo - Jimbo la Arusha Mjini
5: Christopher Olesendeka- Simanjiro
6: Anjelina Mabula - Ilemela
7: Seif Gulamali- Manonga

Na Wengine waliokatwa ni:

Pauline Gekul- Babati Mjini.
Lengai Olesabaya - Arumeru Magharibi
Stephen Byabato - Bukoba Mjini

Wagombea watano Kuchuana ndani ya CCM Kumpata Mgombea Mmoja atakaye peperusha Bendera ya CCM Jimbo la Busokelo kwenye Uc...
29/07/2025

Wagombea watano Kuchuana ndani ya CCM Kumpata Mgombea Mmoja atakaye peperusha Bendera ya CCM Jimbo la Busokelo kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025

Mkuu wa wilaya ya Kusini Unguja Othman Masudi amesisitiza kuendelea kudumisha na kuilinda tunu ya muungano ilioachwa na ...
26/07/2025

Mkuu wa wilaya ya Kusini Unguja Othman Masudi amesisitiza kuendelea kudumisha na kuilinda tunu ya muungano ilioachwa na waasisi wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Aman Karume pamoja na kuendelea kuimarisha amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu.

Ameyasema hayo katika mapokezi ya Jukwaa la walimu wazalendo kutoka mikoa 7 ya Tanzania bara waliowasili visiwani Zanzibar kwa ziara ya kikazi ya siku 3 itakayoangazia kubadilishana uzoefu,kutembelea maeneo ya kihistoria pamoja na miradi ya kimkakati inayotekelezwa na serikali chini ya Dr.Hussein Ally Mwinyi.
Aidha ameongeza kuwa Zanzibar katika sekta ya utalii inachangia pato la serikali kwa asilimia 30 kupitia utalii wa ndani hivyo kufanyika kwa ziara hiyo ni ishara ya muamko wa kufanya utalii wa ndani bila ya kutegemea wageni.

Hata hivyo katibu mtendaji wa taasisi ya Vijana nguvukazi kutoka kizimkazi Abuusuphian Yakuti Juma pamoja na mratibu wa jukwaa la walimu wazalendo kutoka Morogoro Mwl Kassimu Mandwanga wamesema ziara hiyo ina lengo la kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo baina ya walimu kutoka mikoa ya Tanzania bara na Zanzibar,kukuza utalii, kudumisha muungano na kuhamasisha dhana ya kushiriki uchaguzi.
Katika ziara hiyo ya Muungano kupitia Jukwaa la walimu wazalendo wanatarajia kutembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria katika mikoa ya Mjini Unguja,Kaskazini Unguja na Kusini Unguja,kuzuru kaburi la hayati Ally Hassan Mwinyi,mradi wa bandari,na kutembelea maeneo ya kasa.

Walimu hao ni kutoka mikoa ya Morogoro,Tanga,Pwani,Dar es salaam,Shinyanga,Mbeya na Kigoma ambapo wametembelea Zanzibar kwa mualiko rasmi wa Taasisi ya Vijana nguvu kutoka Kizimkazi mkoa wa Kusini Unguja.

Udiwani Viti Maalum Mufindi Wang'ara:Akitamgaza matokeo katibu mwenezi ccm mkoa Joseph lyata amesema jumala ya wajumbe 1...
22/07/2025

Udiwani Viti Maalum Mufindi Wang'ara
:
Akitamgaza matokeo katibu mwenezi ccm mkoa Joseph lyata amesema jumala ya wajumbe 1983 walishiriki wakiwemo 387 kutoka halmashauri ya mafinga mji na 1596 kutoka halmashauri ya mufindi
Ambapo asilimia 99 ya waliokuwa madiwani wa viti maalumu kipindi kilichopita katika wilaya ya mufindi mkoani iringa wamefanikiwa kutetea nafasi zao katika Kura za maoni wa chama cha mapinduzi ccm.

Mchezaji wa zamani mstaafu  wa timu ya Simba,Yanga na Timu ya Taifa Tanzania Zamoyoni Mogela  ameweka bayana sababu za k...
16/07/2025

Mchezaji wa zamani mstaafu wa timu ya Simba,Yanga na Timu ya Taifa Tanzania Zamoyoni Mogela ameweka bayana sababu za kushuka kwa vipaji vya michezo mkoa wa Morogoro kuwa ni kutokana na kudumaaa kwa vijana kwa kutokufanya mazoezi ya mpira na kuchezwa kwa ligi

Ameyasema hayo katika Fainali ligi daraja la Nnne wilaya ya kilosa ambapo amehudhuri kwaajili ya kuangalia vipaji vya wachezaji wachanga huku akiomba kuimarishwa kwa uongozi ili kuimarisha vipaji vinavyochipukia.

Katika fainali hizo timu ya Magomeni Academy wameibuka mabingwa wa wilaya kwa ushindi wa goli 2-0 dhidi ya Dumila Soccer Academy ambapo timu hizo zitawakilisha wilaya,katika ligi ya mabingwa wilaya kwa mkoa wa Morogoro.

orts

Watu watatu waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Polisi kwa matukio ya mauaji wamek**atwa kwenye oparesheni mbalimbali ya k...
14/07/2025

Watu watatu waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Polisi kwa matukio ya mauaji wamek**atwa kwenye oparesheni mbalimbali ya kudhibiti uhalifu na wahalifu iliyofanywa mkoani Morogoro.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari,Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mk**a amesema watuhumiwa hao walifanya matukio ya mauaji katika wilaya ya Gairo,Kilosa na Kilombero kwa nyakati tofauti ambapo uchunguzi wa awali wa chanzo cha matukio hayo ni wivu wa kimapenzi na shambulio la unyang’anyi wa kutumia silaha zenye makali.

Kamanda Mk**a amewataja watuhumiwa hao kuwa ni “Faraji Raymond Mwadanda(36)akituhumiwa kumuua mkewe aitwaye Frolenciana Edmund Kamunarelo(38),akimtuhumu kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine ,Mayunga John Mayunga(34)aliyekuwa akitafutwa kwa kosa la mauaji ya Halifa Mijuho Abdallah(19) ambapo alimkodi marehemu kutoka kijiji cha Msowero kwenda kijiji cha Kife wakiwa njiani alimnyang’anya pikipiki na kumshambulia na David William Makau (35)aliyekuwa akitafutwa kwa tuhuma za mauaji ya Wilson Dastan Simioni(38)marehemu alipigwa na kitu butu wakati anaendesha pikipiki na kupoteza mwelekeo na kuangua ndipo alipomvamia na kumjeruhi sehemu za mwili hadi kifo chake”.

Hata hivyo jeshi la polisi mkoa wa Morogoro linaendelea na uchunguzi wa tukio la mauaji ya Restuta Patrick Walela(50) mkazi wa Kilosa Mjini lilitokea usiku wa kumakia Julai 13 2025.
“Ni kwamba marehemu aliuawa kwa kukatwa na kitu chenye makali maeneo mbalimbali ya mwili wake na mume wake aitwaye Jmaes Daudi Lugembe(55) ambaye amek**atwa huku chanzo cha ugomvi ni mume akituhumiwa na mkewe kutokutunza familia na huku mke akituhumiwa na mumewe kwa ulevi na kurudi nyumbani usiku wa manane.”
“Uchunguzi na upelelezi wa matukio yote hayo unaendelea na baada ya kukamilisha uchunguzi maamuzi kwa mujibu wa sheria yatafanyika.”   
                     
Sambamba na hilo watuhumiwa 21 wamek**atwa kwa tuhuma za makosa ya utapeli kupitia oparesheni maalum ya jeshi la polisi mkoa wa Morogoro iliyowajumuisha askari wa makao makuu iliyofanyika Julai 2 hadi 11 katika maeneo ya Ifakara wilaya ya Kilombero,Msowero na Ludewa Wilaya ya Kilosa pamoja na Turiani wilaya ya Mvomero.

Mashindano  ya ligi ya Nishati safi Cup yamezinduliwa rasmi mjini Morogoro kwa Timu 32 kutoka  Kata 29 za Manispaa ya Mo...
12/07/2025

Mashindano ya ligi ya Nishati safi Cup yamezinduliwa rasmi mjini Morogoro kwa Timu 32 kutoka Kata 29 za Manispaa ya Morogoro zitakazoshiriki ligi hiyo ambapo zimepokea vifaa vya michezo ikiwemo jezi na mpira.

Akizindua Mashindano hayo Yaliyoratibiwa na Taasisi ya Mother of Mercy kwa kushirikiana na Manispaa ya Morogoro Katibu Tawala wilaya ya Morogoro mjini Ruth John amesisitiza suala la amani na utulivu kwenye mashindano hayo na kufanyika k**a yalivyokusudiwa kuhamasisha utunzaji mazingira na matumizi ya nishati safi bila kuingiza siasa.

Madereva bodaboda ni miongoni mwa wahamasishaji wataoshiriki ligi hiyo ambapo mshindi ataondoka na pikipiki mpya Kumalizika kwa msimu wa ligi hiyo kutatoa nafasi kwa washindi wa timu kuibuka na zawadi ikiwemo kitita cha shilingi milioni tano kwa mshindi wa kwanza.
Uzinduzi huo umetanguliwa na mazoezi kutoka Club za Jogging Morogoro pamoja na michezo mbalimbali ya kupiga danadana,kukimbia kwenye gunia pamoja na burudani kutoka kwa Balozi wa Mazingira Afande Sele.

Wachezaji wa zamani waliowahi kuchezea timu za ligi kuu Tanzania akiwemo Zamoyoni Mogela,Kudra Omary aliyewahi kuichezea Yanga,John Simkoko na wengineo watashiriki katika ligi hiyo ili kuibua vipaji kutoka kwa wachezaji wachanga pamoja na kuhamasisha wananchi kutumia nishati safi na kutunza mazingira ambapo miti 14,500 inatarajia kupandwa hadi kutamatika kwa ligi.

Chama Cha Wananchi(CUF) kimeweka wazi dhamira yao ya dhati ya kushiriki katika uchaguzi mkuu wa ambapo wamewakaribisha w...
11/07/2025

Chama Cha Wananchi(CUF) kimeweka wazi dhamira yao ya dhati ya kushiriki katika uchaguzi mkuu wa ambapo wamewakaribisha wanachama wanaotaka kujiunga na chama hicho huku wakiomba kulindwa kwa amani katika kipindi cha uchaguzi.
Mwenyekiti wa Chama cha wananchi CUF wilaya ya Morogoro mjini ambaye pia ni mjumbe wa baraza kuu CUF Taifa Rashid Athumani Mzalamo amesema chama hicho kinaingia katika uchaguzi wa mwaka 2025 licha ya changamoto zilizowahi kutokea kwa upande wao hivyo wameiomba tume huru ya uchaguzi kusimamia haki
“Sisi k**a chama cha siasa ngazi ya Taifa tumejipanga kuingia katika uchaguzi kadhalika ngazi ya wilaya hivyo natoa wito kwa wale wote ambao wanahitaji kuchukua fomu kugombea katika nafasi za uongozi udiwani na ubunge shime tunawakaribisha milango imefunguliwa.”
“Sisi k**a chama cha siasa hatuna masharti katika nafasi ya ugombea nafasi ya uongozi mwanachama yoyote atakayejiunga leo ana haki ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya taifa lake kupitia chama chetu.”
“Pia nitoe wito kwa viongozi na watawala kwa ujumla sisi k**a tunapoamua kuingia katika uchaguzi hali ya kuwa tunajua kwamba siku zote chama chetu kinakuwa cha kwanza kupata madhila katika uchaguzi,mwaka 1995 tumeingia katika uchaguzi matokeo hayakuwa mazuri kwa upande wa Zanzibar na vurugu nyingi zilitokea na wakatuita majina mabaya mabaya kwamba JANJAWIDI kwasababu ya kudai haki zetu,mwaka 2000 pia hivyo hivyo ingawa tulikuwa na nguvu kubwa kisiasa lakini siku zote tume ya uchaguzi haipo upande wetu,sisi hatukati tamaa ya kuingia katika nafasi za kugombea kwahiyo tunatoa wito kwa viongozi hususani mamlaka ya nchi kwamba walinde amani ya nchi kwa kutenda haki katika uchaguzi,sisi tutaingia katika uchaguzi tukishindwa tutakubali matokeo na k**a tutashinda tunaomba mamlaka iheshimu matokeo yetu”
Wanachama wa CUF wilaya ya Morogoro mjini wamesema wapo tayari kuwaunga mkono wagombea watakaopewa ridhaa ya kusimama katika nafasi hizo huku wakiwataka wenye nia kujiunga ili kusimamisha wagombea watakaoweza kusimamia haki na kujiletea maendeleo.
Chama cha wananchi CUF kitaendelea na zoezi la uchukuaji na urejeshaji wa fomu kadri wanachama watakavyojitokeza ambapo ukomo wa zoezi hilo

Jiji la Mbeya
05/07/2025

Jiji la Mbeya

Address

Mbambo
Mbeya
53525

Telephone

+255676506998

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MAWIO TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MAWIO TZ:

Share