MAWIO TZ

MAWIO TZ Karibu katika ukurasa huu maalumu wa MAWIO TZ, unaokuhabarisha Taarifa/Habari na Makala mbalimbali ndani na nje ya Tanzania 🇹🇿

TRA YAFANYA ZIARA YA KURUDISHA SHUKRANI KWA WALIPAKODIMamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Morogoro imefanya ziara y...
18/12/2025

TRA YAFANYA ZIARA YA KURUDISHA SHUKRANI KWA WALIPAKODI

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Morogoro imefanya ziara ya kutembelea walipakodi mbalimbali mkoani humo kwa lengo la kutoa pongezi na kurudisha shukrani kwa walipaji kodi kwa hiari bila shuruti.

Katika ziara hiyo, maafisa wa TRA wamepata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na walipakodi, wakiwapongeza kwa uzalendo wao na mchango mkubwa wanaoutoa katika maendeleo ya taifa kupitia ulipaji sahihi wa kodi. TRA imeeleza kuwa walipakodi hawa ni mfano wa kuigwa, kwani wanatekeleza wajibu wao wa kikatiba bila kusubiri ushawishi au hatua za kisheria.

Aidha, TRA Morogoro imesisitiza kuwa hatua hiyo ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha mahusiano mazuri kati ya mamlaka na walipakodi, pamoja na kujenga utamaduni wa kulipa kodi kwa hiari na uaminifu. Walipakodi waliotembelewa wameeleza kufurahishwa na kitendo hicho, wakieleza kuwa kinawapa motisha ya kuendelea kutimiza wajibu wao kwa uaminifu zaidi. na wamewashauri walipa kodi wengine waweze kutimiza wajibu wao kwa kulipa kodi kwani kodi hizo ndio maendeleo ya nchi yetu.

TRA imewahakikishia walipakodi kuendelea kutoa elimu ya mlipa kodi, huduma bora na ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha mazingira rafiki ya ulipaji kodi yanaimarika kwa maendeleo endelevu ya nchi yetu.

16/12/2025

Diwani wa kata ya Nsalaga jimbo la Uyole jijini Mbeya Clemence Mwandemba, amefanya kikao chake cha kwanza na wajumbe wa Baraza la maendeleo ya kata (WDC) akikabidhiwa rasmi ofisi na afisa mtendaji wa kata hiyo.

Katika kikao hicho cha kujitambulisha, Mheshimiwa Mwandemba ambaye pia ni Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Mbeya mjini, ameahidi kuhakikisha anawatumikia wananchi bila kuchoka kuhakikisha wanasikilizwa na kero zao zinatafutiwa ufumbuzi.

Pia ameishukuru Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania kwa kutoa mabillion ya fedha kwa ajili ya kata ya Nsalaga ikiwemo ujenzi wa ba barabara za lami na za vifusi, ujenzi wa shule mpya, uboreshaji miundombinu ya maji, umeme na maeneo mengine mbalimbali.

Amesema baadhi ya kero ambazo ni miongoni mwa agenda zake na tayari zimeanza kufanyiwa kazi ni pamoja na uboreshaji miundombinu ya barabara pamoja na vivuko na madaraja yake, umeme kuwafikia wananchi wote kutokana na kata hiyo kuendelea kukua kila uchao na kuendelea kuboresha sekta ya elimu.

Pamoja na hayo amewashukuru watumishi wote wa kata ya Nsalaga na mtangulizi wake Mchungaji David Ngogo (2020-2025) na wananchi kwa ujumla wao kwa ushirikiano katika kufanikisha miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake afisa mtendaji wa kata ya Nsalaga Uyole Joyce Gwega, amesisitiza kila mtaalam kukaa kwenye eneo lake kufanya kazi k**a anavyotakikana kwa mujibu wa sheria, kanuni na maadili ya utumishi wa umma ili kuwatumikia wananchi na kufikia maendeleo endelevu.

16/12/2025

HATUA ZACHUKULIWA DHIDI YA MAKOSA HATARISHI YA USALAMA BARABARANI.

Mkuu wa Kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Mbeya SSP Notker Kilewa kwa kushirikiana na timu kutoka Makao Makuu ya Kikosi cha usalama barabarani Dawati la Elimu kwa Umma, Desemba 16, 2025 ameendesha operesheni maalum ya kuzuia na kudhibiti makosa ya usalama barabarani katika barabara ya Mbeya - Chunya eneo la Lwanjilo.

Akizungumza mara baada ya Operesheni hiyo, SSP Kilewa amesema kuwa lengo ni kuzuia na kudhibiti makosa mbalimbali ya barabarani pamoja na kuchukua hatua dhidi ya madereva wasio tii sheria.

Miongoni mwa makosa yaliyok**atwa ni pamoja ni Mwendo kasi, "Overtaking" hatarishi, kuzidisha abiria, kuchanganya abiria na mizigo na ubovu wa gari.

MOROGORO: AJALI YA MOTO 9/12/2025Abiria 40 waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es salaam kuelekea Malinyi mkoani Morogoro wa...
09/12/2025

MOROGORO: AJALI YA MOTO 9/12/2025
Abiria 40 waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es salaam kuelekea Malinyi mkoani Morogoro wamenusurika kifo baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuwaka moto na kuteketea.

Kamanda wa polisi mkoani Morogoro Alex Mk**a amesema tukio hilo limetokaea Desemab 9 2025 majira ya asubuhi katika eneo la Maseyu kona kali ya Gwata wilaya ya Morogoro ambapo gari lenye namba za usajili T 957 DVR aina ya TATA lililokuwa likiendeshwa na dereva Halfan Omary liliwaka moto na kuteketea huku chanzo kikibainika kuwa ni hitilafu ya umeme wa gari hilo.

Aidha amebainisha kuwa katika ajali hiyo hakuna abiria aliyepata madhara ingawa mizigo na mali zingine za abiria ndani ya basi hilo zimeharibika na kuteketea.

Hata hivyo Kamanda Mk**a amesema jeshi la polisi Morogoro linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo la ajali na kuwak*mbusha wamiliki wa vyombo vya moto kuwa na utamaduni wa kufanya matengenezo ya mara kwa mara ya magari yao hasa yanayobeba abiria ili kuokoa maisha ya watu na mali zao.

07/12/2025

BODABODA RUNGWE WAPINGA VIKALI MAANDAMANO.

Waendesha pikipiki maarufu k**a bodaboda katika Kata ya Kiwira, Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya, wamepinga vikali wito wa kuandamana ambao umekuwa ukisambazwa kupitia mitandao ya kijamii hivi karibuni. Wakizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo maalumu ya udereva salama kwa madereva wa bodaboda wa kata hiyo, wamesema kuwa maandamano hayo yanaweza kuwaletea madhara makubwa, ikiwemo kukiuka sheria, kuharibu shughuli zao za kila siku na kuhatarisha usalama wao.

Mafunzo hayo yanatolewa na Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Mbeya na yamefadhiliwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mbunge wa Mbeya Mjini, Mhe. Patrick Mwalunenge. Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni muendelezo wa juhudi za kuhakikisha vijana wanaojishughulisha na usafirishaji wa bodaboda wanakuwa na uelewa sahihi wa kanuni za barabarani pamoja na kuimarisha usalama wao na wa abiria.

Akizindua rasmi mafunzo hayo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, ACP Benjamini Kuzaga, amemshukuru na k*mpongeza Mhe. Mwalunenge kwa kufadhili programu hiyo muhimu. Amesema kuwa mafunzo hayo yatachangia kwa kiasi kikubwa kupunguza ajali zinazohusisha bodaboda katika jamii, sambamba na kuongeza nidhamu na utii wa sheria miongoni mwa madereva.

Kamanda Kuzaga ameongeza kuwa kushirikiana na vijana hao katika kuwajengea uwezo ni njia madhubuti ya kuzuia vitendo vinavyoweza kuhatarisha amani, ikiwemo kushawishiwa kuingia kwenye maandamano yasiyo halali. Amesema jeshi la polisi linaendelea kuhimiza utulivu na kufuata sheria huku likitoa elimu juu ya madhara ya kujiingiza katika mienendo isiyo sahihi.

KHALID MATENGO ACHAGULIWA KUWA MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA MOROGOROKhalid Mohamed Matengo Amechaguliwa kuwa Mstahiki Meya ...
03/12/2025

KHALID MATENGO ACHAGULIWA KUWA MSTAHIKI MEYA MANISPAA YA MOROGORO
Khalid Mohamed Matengo Amechaguliwa kuwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro baada ya kupita katika uchaguzi ulifanyika wa nafasi za Umeya na Naibu Meya ambapo wagombea nane walikuwa wakiwania nafasi ya Umeya,na majina matatu yaliteuliwa na kuingia katika king’ang’anyiro cha ushindani.
Akiwa amechaguliwa kwa kura za kishindo baada ya kupata kura 34 kati ya 39 huku akifuatiwa na Milkiel Mansuet aliyepata kura 03 na Richard Mmanda akipata kura 02.
Mh.Matengo ni Diwani wa kata ya Mji Mkuu miongoni mwa kata 29 za Manispaa ya Morogoro akiwa ameingia kwenye nafasi za udiwani kwa kipindi cha awamu ya kwanza katika uchaguzi uliofanyika Novemba 29 2025.
Ushindi huu unadhihirisha imani kubwa kutoka kwa madiwani wenzake walionyesha imani kubwa isiyo ya bahati mbaya bali wakifahamu uwezo wake wa kiuongozi ,mienendo na utulivu asiye na majigambo wala majivuno pasi na kibri wala kuinua mabega ,kuheshimu kila mtu mkubwa kwa mdogo,uchapakazi mwenye fikra za kimaendeleo hivyo kuwa mtu sahihi wa kuongoza Manispaa hiyo.

https://youtu.be/WJPRKZsV3tE
03/12/2025

https://youtu.be/WJPRKZsV3tE

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Kyela Mkoani Mbeya Elias Mwanjala amejitokeza hadhara kutoa ufafanuzi wa kauli juu ya fedha shilingi milioni k*m...

03/12/2025

MASACHE KASAKA ATOA NENO SIKU YA UZINDUZI WA BARAZA LA MADIWANI

Mbunge wa Jimbo la Lupa Masache Njelu Kasaka Azungumza kwa mara ya kwanza na madiwani katika uzinduzi wa Baraza la Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Cc

27/11/2025

KYELA SASA RUKSA KAZI MASAA 24

Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Kyela Josephine Manase ameondoa agizo la kufanya kazi hadi saa sita za usiku Wilayani hapo kutokana na hali ya usalama ilivyokuwa baada ya kile kilichotokea oktoba 29.

Akizungumza na Wananchi wakati wa Ziara ya Waziri wa Vijana wilayani Kyela,Mheshimiwa Josephine Amesema kuwa kwa sasa wananchi wanaruhusiwa kufanya kazi kwa masaa 24 k**a ilivyokua awali.

27/11/2025

Wakili Boniface Mwabukusi Awavaa Polisi Awataka Kuacha Kushughulika na Siasa

DKT. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAZI CHA WAKUU WA MIKOAWAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 27, 2025 ameongoza k...
27/11/2025

DKT. MWIGULU AONGOZA KIKAO CHA KAZI CHA WAKUU WA MIKOA

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Novemba 27, 2025 ameongoza kikao kazi cha Wakuu wa Mikoa Tanzania bara, kikao hicho kimefanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma.

Address

Mbambo
Mbeya
53525

Telephone

+255676506998

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MAWIO TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MAWIO TZ:

Share