MAWIO TZ

MAWIO TZ Karibu katika ukurasa huu maalumu wa MAWIO TZ, unaokuhabarisha Taarifa/Habari na Makala mbalimbali ndani na nje ya Tanzania 🇹🇿

BASHUNGWA APIGA KURA KARAGWEMgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Innocent Bashungwa ame...
29/10/2025

BASHUNGWA APIGA KURA KARAGWE

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Karagwe kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Innocent Bashungwa amepiga kura katika Kituo cha Ahakishaka, kata ya Nyabiyonza, wilayani Karagwe, leo 29 Oktoba 2025.

Bashungwa aliwasili mapema na kuungana na wananchi waliokuwa wakitekeleza haki yao ya kikatiba kwa kupiga kura ya Diwani, Mbunge na Rais, kisha akabadilishana salamu nao huku akisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, umoja na utulivu kipindi chote cha uchaguzi.

MGOMBEA UBUNGE CCM JIMBO LA UYOLE TAYARI AMESHAPIGA KURAMgombea Ubunge Jimbo la Uyole, Dkt. Tulia Ackson,amepiga kura le...
29/10/2025

MGOMBEA UBUNGE CCM JIMBO LA UYOLE TAYARI AMESHAPIGA KURA

Mgombea Ubunge Jimbo la Uyole, Dkt. Tulia Ackson,
amepiga kura leo katika Kituo cha Kupigia Kura cha Tambukareli,
kata ya Itezi Magharibi.
ackson

MBUNGE ALIEMALIZA MUDA WAKE KYELA APIGA KURAIkiwa ni siku ya tarehe 29/10/2025 Watanzania wakitumia siku hii kupiga kura...
29/10/2025

MBUNGE ALIEMALIZA MUDA WAKE KYELA APIGA KURA

Ikiwa ni siku ya tarehe 29/10/2025 Watanzania wakitumia siku hii kupiga kura kuchagua Viongozi wao,Tayari aliyekuwa Mbunge jimbo la Kyela 2020-2025 Ally Mlaghila Jumbe amepiga Kura katika Kituo cha Itunge Kijiji A kilichopo Kata ya Itunge Wilayani kyela maarufu kama kwa Pade.

Kwa taarifa mbalimbali zihusuzo zoezi zima la Uchaguzi Mkuu endelea kutufuatilia Mawio Tz.



Mnaitaje uko Kwenu
28/10/2025

Mnaitaje uko Kwenu

BUSOKELO WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURAKaimu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya Ndele Mwaselela (...
26/10/2025

BUSOKELO WAOMBWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA

Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Mbeya Ndele Mwaselela (Mnec) ameongoza ujumbe wa kuwaomba Wananchi wa Busokelo kujitokeza kwa wingi kupiga kura siku ya Jumatano ya Tarehe 29/10/2025 kwa ajili ya kuwachagua viongozi wanaotokana na chama hicho.

Kwa upande wake Mgombea Ubunge Jimbo la Busokelo Ndugu Lutengano George Mwalwiba amesema kuwa kipaumbele namba moja ni kuhakikisha maendeleo yanaletwa na wnaabusokelo wote walio ndani na nje ya Jimbo hilo.

Kwa taarifa zaidi tembelea chaneli yetu youtube Mawio Tz

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kupitia tiketi ya CHAUMMA ambaye ni katibu Mkuu wa Chama Mh.Salum Mw...
23/10/2025

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kupitia tiketi ya CHAUMMA ambaye ni katibu Mkuu wa Chama Mh.Salum Mwalim Leo October 22,2025 Ameendelea kuomba ridhaa kwa wananchi wa Jimbo la Tabora mjini ili kuweza kuchaguliwa kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania October 29 mwaka huu.

Mwalim amesema mkoa wa Tabora ni mkoa uliobarikiwa sanaa unaardhi zuri pia una Zao la tumbaku ambalo ni Zao la kimkakati endapo atapata ridhaa ya kuchaguliwa kuwa Rais atahakikisha anaweka Mazingira wezeshi kwa wakulima wa tumbaku pia atavunja bodi zote Za tumbaku ilikuruhusu soko huru,Pia Mwalim amesema kuwa suala la kutokuwa na ajira kwa vijana wengi hilo ni janga la Taifa hivyo atapo kuwa Raisi ndani ya siku mia moja Za mwanzo atahakikisha anaweka mazingira bora kwenye kilimo ilikutatua tatizo la ajira.


MHAGAMA AWAFUNDA WATENDAJI KATA NA VIJIJI UKUSANYAJI WA MAPATONa Ahadi Mtweve, Moshi DCMkurugenzi Mtendaji wa Halmashaur...
19/10/2025

MHAGAMA AWAFUNDA WATENDAJI KATA NA VIJIJI UKUSANYAJI WA MAPATO

Na Ahadi Mtweve, Moshi DC

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi, Ndugu Shadrack Mhagama, ameongoza kikao kazi maalum kilichowahusisha Watendaji wa Kata na Vijiji kutoka maeneo yote ya wilaya, kwa lengo la kufanya tathmini ya hali ya ukusanyaji wa mapato na kujadili mikakati ya kuongeza ufanisi katika usimamizi wa fedha za umma.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhagama aliwataka watendaji kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao kwa uaminifu, uwazi na kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma. Alisisitiza kwamba jukumu la ukusanyaji wa mapato ni la msingi katika uendelevu wa shughuli za maendeleo ya wananchi.

“Nawasihi watendaji wote muwe waaminifu katika kukusanya mapato ya serikali. Fedha hizi ni za wananchi na zinapaswa kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa. Ni jukumu letu kuhakikisha kila senti iliyokusanywa inaingia kwenye akaunti rasmi ya Halmashauri kwa wakati.” alisema Mhagama.

Aidha, Mhagama alitoa onya kali kwa watendaji wanaochelewesha kuwasilisha fedha zilizokusanywa au kutumia mapato kwa matumizi yasiyoruhusiwa, akibainisha kuwa hatua za kinidhamu na kisheria zitachukuliwa kwa yeyote atakayebainika kwenda kinyume na maagizo hayo.

“Hakutakuwa na huruma kwa mtumishi yeyote atakayebainika kutumia vibaya fedha za serikali au kuchelewesha kuziwasilisha. Halmashauri haitasita kuchukua hatua kali, ikiwemo kuwasilisha suala hilo katika vyombo vya uchunguzi.” aliongeza Mhagama.

Katika kikao hicho, washiriki walipata fursa ya kujadili changamoto zinazokabili ukusanyaji wa mapato, ikiwemo elimu ya ujazaji wa taarifa za ukusanyaji wa mapato kwenye mfumo wa FASS, ucheleweshaji wa baadhi ya makusanyo kutoka vyanzo vya ndani, pamoja na uelewa mdogo wa wananchi kuhusu wajibu wao wa kulipa kodi na ada.

Mmoja wa washiriki wa kikao hicho, Ndugu Seif Issa , Mtendaji wa Kijiji cha Sango, alisema kikao hicho kimekuwa muhimu kwani kimetoa mwongozo wa wazi juu ya namna bora ya kuboresha ukusanyaji wa mapato kwa njia za kidijitali na kuongeza uwazi katika matumizi.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktob...
13/10/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktoba 10,2025 akiwemo Meneja Mahusiano Mwandamizi wa NMB Josephine Kulwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Vijana katika Soko la Uhindini jijini Mbeya.

Baadhi ya wanafunzi na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Oktoba 10,2025 katika Viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Loleza waliotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

Matukio mbalimbali katika picha kwenye Banda la NMB Oktoba 10,2025 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

MAWAZIRI WAIMWAGIA PONGEZI BENKI YA NMB KWA UTENDAJI WAKE. Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira n...
13/10/2025

MAWAZIRI WAIMWAGIA PONGEZI BENKI YA NMB KWA UTENDAJI WAKE.

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Patrobas Katambi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Sera na Uratibu Zanzibar Hamza Hassan Juma wameimwagia pongezi Benki ya NMB kwa kuendelea kushirikiana kwa karibu na serikali kwa kutoa elimu ya kifedha kwa vijana ili kujikwamua kiuchumi.

Wameyasema hayo walipotembelea Banda la NMB kwenye maadhimisho ya wiki ya Vijana yanayoendelea viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

"Mmekuwa na sapoti kubwa kwa serikali kusaidia elimu ya kifedha kwa vijana, Vijana wengi kwa sasa wamejikwamua kiuchumi kutoka na elimu mnayotoa" alisema Waziri Katambi.

Kwa upande wake Waziri Hamza Hassan Juma amesema vijana wengi wa Kizanzibari wamejikita katika ujasiriamali kutoka na elimu kwa vijana inayotolewa na Benki ya NMB.

Akizungumza wakati akiwakaribisha Mawaziri hao, Meneja Mahusiano Mwandamizi wa NMB Josephine Kulwa alisema Benki hiyo imetumia fursa hii ya Wiki ya Vijana kutoa elimu ya kifedha ambako kwa sasa kuna akaunti maalumu inayowagusa bila a wanafunzi wa vyuo vikuu ya Mwanachuo Akaunti.

Amesema akaunti hizi ni rafiki kwa vijana na wanachuo ambapo wakifanya muamala kwa kutumia Mshiko Fasta wanarudishiwa asilimia 30.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktob...
13/10/2025

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa akiwa na baadhi ya Wadhamini wa maadhimisho ya wiki ya Vijana yaliyozinduliwa Oktoba 10,2025 akiwemo Meneja Mahusiano Mwandamizi wa NMB Josephine Kulwa wakati wa ufunguzi wa Wiki ya Vijana katika Soko la Uhindini jijini Mbeya.

Baadhi ya wanafunzi na wananchi waliohudhuria ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana Oktoba 10,2025 katika Viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya wakifuatilia kwa karibu hotuba ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Majaliwa aliyekuwa mgeni rasmi.

Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Wasichana Loleza waliotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

Matukio mbalimbali katika picha kwenye Banda la NMB Oktoba 10,2025 wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete ameipongeza Benki ya NMB kwa ku...
08/10/2025

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete ameipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kuwa karibu na Wananchi kwa kusogeza huduma kwa watu wa maeneo ya pembezoni.

Kikwete ameongea hayo alipotembelea Banda la NMB kwenye Maadhimisho ya wiki ya Vijana viwanja vya Soko la Uhindini jijini Mbeya.

Amesema Benki hiyo ambayo kwa asilimia kubwa inawahudumia watumishi wa umma imewafikia wateja wengi wa pembezoni na hivyo kuwavutia wateja wengi kufungua akaunti katika benki hiyo.

Akizungumza wakati akimkaribisha Waziri Kikwete, Meneja Mahusiano Mwandamizi wa Benki ya NMB Josephine Kulwa amesema kwa kuzingatia umuhimu wa Wiki ya Vijana nchini Benki ya NMB imeshiriki kikamilifu maadhimisho hayo sanjari na kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru ambapo Benki hiyo imekuwa mmoja wa Wadhamini wakuu.

Kulwa amesema Huduma za kibenki za NMB zimelenga pia makundi ya vijana,ikiwemo akaunti maalumu ya Mwanachuo Account, Chimbo la Chuo (GO na NMB) ambapo Mwanachuo akifanya muamala kwa Lipa Namba ya NMB hurudishiwa hadi asilimia 30 na mafunzo kwa vitendo.

Address

Mbambo
Mbeya
53525

Telephone

+255676506998

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when MAWIO TZ posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to MAWIO TZ:

Share