Greencity Tv Online

Greencity Tv Online Karibu
Kituo chako bora cha matangazo Online
Kawa Habari za MICHEZO, BURUDANI, MATUKIO na HISTORIA ungana nasi

TUNAKUA KIDIGITALI

NSSF YATANGAZA MSAMAHA KWA WAAJIRI WENYE MALIMBIKIZO YA MICHANGO NA TOZO ITOKANAYO NA UCHELEWESHAJI WA MICHANGOSwipe >>>...
04/06/2026

NSSF YATANGAZA MSAMAHA KWA WAAJIRI WENYE MALIMBIKIZO YA MICHANGO NA TOZO ITOKANAYO NA UCHELEWESHAJI WA MICHANGO

Swipe >>>

28/05/2026

TULIA TRUST UYOLE CUP 2026 YAZINDULIWA KWA KISHINDO MWAWINJI

Mashabiki wa soka jijini Mbeya wanatarajiwa kushuhudia burudani ya hali ya juu wakati Ligi ya Mpira wa Miguu ya Tulia Trust Uyole Cup 2026 itakapozinduliwa rasmi Mei 30, 2026 katika Uwanja wa Mwawinji kupitia mchezo wa Ngao ya Hisani utakaowakutanisha mabingwa wawili, Itezi FC dhidi ya Chipukizi FC.

Uzinduzi huo utaashiria mwanzo wa msimu mpya wa ligi hiyo maarufu inayoshirikisha jumla ya timu 34 kutoka maeneo mbalimbali, huku mashindano rasmi yakitarajiwa kuanza Juni 01, 2026.

Waandalizi wa mashindano hayo wameahidi ushindani mkubwa, vipaji vya kipekee pamoja na burudani safi kwa wakazi wa Uyole na maeneo ya jirani, wakilenga kuendelea kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo.

Tulia Trust Uyole Cup 2026 inatajwa kuwa moja ya ligi zenye mvuto mkubwa kwa vijana na jamii, huku wadau wa michezo wakitarajiwa kujitokeza kwa wingi kushuhudia ufunguzi huo wa kihistoria.

# mbeya

26/05/2026

MPALANO FESTIVAL MSIMU WA NNE 2026

Tamasha kubwa la MPALANO FESTIVAL linatarajiwa kufanyika tarehe 06 & 07 Mei 2026 katika mazingira mazuri ya Lake Nyasa Resort, kando ya Ziwa Nyasa. 🌊🔥

Tamasha hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na watu zaidi ya 2,000 kutoka maeneo mbalimbali kwa ajili ya burudani, utamaduni, vipaji na kujenga mahusiano ya kijamii. ✨

Taarifa hii imetolewa rasmi na Mkurugenzi wa tamasha hilo, Mr. Amos Asajile , ambaye amesema maandalizi yanaendelea vizuri kuhakikisha msimu huu wa nne unakuwa mkubwa na wa kipekee zaidi.






NyasaVibes 🌴

21/05/2026

Hii vita bado mbichi kwa wadau wa Soka Nchini

Mdau ameuliza ni goli lipi alistahili kumuonesha Nyota wa Soka Duniani aliyewasili siku chache hapa Nchini?

Wewe ungempa nani Tuzo?

16/05/2026
16/05/2026

BETIKA MBEYA TULIA MARATHON 2026

TRA MBEYA WASHIRIKI MBEYA TULIA MARATHON, LENGO LIKIWA NI KUTOA MSAADA KWA MLIPA KODI KWA KUTOA ELIMU NA KUTATUA CHANGAMOTO ZA ZINAZOWAKABILI WANANCHI AMBAO NI WALIPA KODI NA WANAOHITANI TIN PAMOJA NA LESENI.

16/05/2026

BETIKA MBEYA TULIA MARATHON 2026

MH. MSIGWA AMESEMA ISINGEWA ITIFAKI, ANGEKIMBIA KILOMETA 42 KWA NAMNA ALIVYO NA UWEZO MKUBWA WA MBIO

🇹🇿

15/05/2026

BEI YA KAKAO YAANZA KUPANDA TENA, WAKULIMA WAREJESHEWA MATUMAINI

Mh. Lutengano Mwalwibha pamoja na meneja wa moja ya maghala ya kakao lililopo Ntaba, Kata ya Kambasegela, wamethibitisha kuanza kuimarika kwa bei ya zao la kakao baada ya kushuka kwa kiwango kikubwa katika kipindi kilichopita.

Kwa sasa, bei ya ununuzi wa kakao imefikia zaidi ya shilingi 10,000 kwa kilo moja, ikiongezeka kutoka zaidi ya shilingi 5,000 ambapo ilikuwa imeshuka kwa kasi kubwa sana. Kabla ya kushuka huko, bei ya kakao ilikuwa ikifikia zaidi ya shilingi 15,000 kwa kilo.

Mh. Lutengano ameeleza kuwa kupanda kwa bei hiyo kunarejesha matumaini mapya kwa wakulima, huku waitarajie hali kuendelea kuwa nzuri zaidi katika soko la zao hilo muhimu la biashara.

📍 Ntaba – Kambasegela, Busokelo




15/05/2026

MH. MASACHE KASAKA AIBUA CHANGAMOTO YA UMEME MAENEO YA MIGODI CHUNYA

Masache Kasaka Mbunge wa Jimbo la Lupa – Chunya, ameipongeza Serikali kwa juhudi mbalimbali za maendeleo zinazoendelea kutekelezwa nchini.

Aidha, Mheshimiwa huyo ameieleza Serikali kuhusu changamoto ya ukosefu wa umeme katika baadhi ya maeneo ya migodi wilayani Chunya, akiiomba kupitia mamlaka husika kuhakikisha suala hilo linafanyiwa kazi kwa haraka.

Amesema upatikanaji wa umeme katika maeneo ya migodi utasaidia kuongeza uzalishaji, kuinua uchumi wa wananchi, pamoja na kuboresha shughuli za maendeleo katika maeneo hayo.

📍 Chunya, Tanzania




12/05/2026

SERIKALI YATOA MILIONI 780 KUKAMILISHA UJENZI WA KITUO CHA AFYA KISEGESE

Mh. Lutengano Mwalwibha amesema Serikali imetoa shilingi milioni 780 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya kilichopo Kata ya Kisegese, Halmashauri ya Busokelo.

Akitoa taarifa hiyo, Mheshimiwa huyo amesema hatua hiyo inalenga kuboresha huduma za afya kwa wananchi na kuhakikisha jamii inapata huduma bora karibu na maeneo yao.

Ameeleza kuwa kukamilika kwa kituo hicho kutasaidia kupunguza changamoto za wananchi kusafiri umbali mrefu kufuata huduma za afya, huku akiipongeza Serikali kwa kuendelea kuwekeza kwenye sekta ya afya vijijini.

📍 Kisegese – Busokelo, Tanzania




Address

Mbeya

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Greencity Tv Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Greencity Tv Online:

Share