Greencity Tv Online

Greencity Tv Online Karibu
Kituo chako bora cha matangazo Online
Kawa Habari za MICHEZO, BURUDANI, MATUKIO na HISTORIA ungana nasi

TUNAKUA KIDIGITALI

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imetangaza kuanzia mwezi July mwaka huu imeaandaa mpango wa usajili na utambuzi...
14/04/2025

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imetangaza kuanzia mwezi July mwaka huu imeaandaa mpango wa usajili na utambuzi wa Watu wote wenye umri kuanzia 0 hadi miaka 18 ili kuwezesha upatikanaji wa Jamii Namba pamoja na wageni wote wanaoingia nchini na kukaa chini ya miezi sita.

Mkurugenzi Mkuu wa NIDA,James Kaji amesema hayo leo April 14,2025 Jijini Dar es salaam huku akisema dhamira yao na Seriiali kwa ujumla ni kuona kila Mtanzania anapata kujulikana na kufikiwa na huduma za msingi zikihitajika na kila kitambulisho kilichotengenezwa kinachukuliwa na Mhusika na hasa ikizingatiwa Serikali imetumia fedha nyingi kutengeneza.

Kaji amesema kuanzia May 01, 2025 NIDA itasitisha rasmi matumizi ya Namba ya Utambulisho wa Taifa (NINs ) kwa wote ambao walitumiwa ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (sms) lakini hawakujitokeza kuchukua vitambulisho vyao na kwamba yule ambaye matumizi ya namba yake ya NIDA yatafungwa hatoweza kuitumia namba hiyo kwa ajili ya huduma yeyote.

Kaji amesema tangu kuanza kwa zoezi hilo kuanzia mwezi January hadi kufikia March mwaka huu jumla ya Wananchi 1,88060 sawa na asilimia 157 ya Wayu wote walikuwa hawajachukua vitambulisho vyao licha ya kutumiwa ujumbe mfupi (sms) “Kwa mujibu wa takwimu hizi idadi ya Wananchi waliojitokeza kuchukua vitambulisho baada ya kupokea sms ni 565,876 sawa na asilimia 30 tu ya Watu wote waliotumiwa na kupokea sms”

UGONJWA MPYA KUCHUKULIWA TAHADHALI MAPEMA       Wizara ya Afya imesema hadi kufikia sasa jumla ya Wahisiwa wawili wameth...
12/03/2025

UGONJWA MPYA KUCHUKULIWA TAHADHALI MAPEMA


Wizara ya Afya imesema hadi kufikia sasa jumla ya Wahisiwa wawili wamethibitika kuwa na ugonjwa wa Mpox nchini hii ni baada uchunguzi wa maabara kufanyika baada ya Wizara kupitia mifumo yake ya ukusanyaji wa taarifa na ufuatiliaji wa magonjwa kupokea taarifa za uwepo wa Wahisiwa wenye dalili za vipele usoni, mikononi, miguuni na sehemu nyingine za mwili.

Taarifa iliyotolewa leo March 10,2025 na Waziri wa Afya, Jenista J. Mhagama imesema dalili hizo za Wahisiwa ziliambatana na homa, maumivu ya kichwa, vidonda kooni, maumivu ya viungo vya mwili ikiwemo misuli na mgongo ambapo kati ya Wahisiwa hao mmoja ni Dereca wa magari ya mizigo aliyetoka nchi jirani kuja Dar es salaam.

“Baada ya kupokea taarifa za wahisiwa, sampuli zilichukuliwa na kupelekwa Maabara ya Taifa kwa uchunguzi, March 9, 2025 uchunguzi wa kimaabara
umethibitisha kuwa Wahisiwa wawili wana maambukizi ya virusi vinavyosababisha ugonjwa wa Mpox”

“Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI na vituo vyote vya kutolea huduma za Afya, inaendelea na ufuatiliaji, uchunguzi na utambuzi kubaini k**a kuna Wahisiwa wengine ili waweze kupatiwa huduma stahiki, chanzo cha ugonjwa huu ni wanyama jamii ya nyani, ambapo binadamu huweza kuupata kutokana na shughuli zinazoweza kusababisha kugusana na wanyama, majimaji au nyama za wanyama wenye maambukizi, endapo binadamu akipata maambukizi hayo anaweza kumwambukiza Mtu mwingine kwa kugusana moja kwa moja”

“Kwa taarifa hii, Wizara ya Afya, inawahakikishia Wananchi kuwa Serikali imejipanga kudhibiti ugonjwa huu na hasa kutokana na uzoefu tulionao wa kudhibiti magonjwa ya mlipuko, Serikali inaendelea kuimarisha ufuatiliaji wa magonjwa katika ngazi zote, upimaji wa Watu wanaoingia na kutoka kupitia mipaka ya nchi, kuimarisha utoaji wa elimu ya afya na kuhamasisha jamii ili kuwawezesha Wananchi kuchuka hatua za kujikinga”

MHE. DR TULIA ACKSON MSIBANI KWA MCHENGERWA       Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa ...
24/02/2025

MHE. DR TULIA ACKSON MSIBANI KWA MCHENGERWA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amehani msiba na kushiriki dua ya kumuombea Alhaj Omary Mchengerwa, Baba mzazi wa Mhe. Mohamed Mchengerwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo Mjini Makkah, Saudi Arabia, alipokuwa akitekeleza ibada ya Umrah.

Dua hiyo imefanyika leo, tarehe 24 Februari 2025, nyumbani kwa Mhe. Waziri Mchengerwa, Masaki, Jijini Dar es Salaam.

WATU 17 WAKIWEMO VIONGOZI WA LBL MKOA WA MBEYA WAMEKATWA NA JESHI LA POLISI KWA KUSHIRIKIANA NA TCRA NA BANK KUU        ...
21/02/2025

WATU 17 WAKIWEMO VIONGOZI WA LBL MKOA WA MBEYA WAMEKATWA NA JESHI LA POLISI KWA KUSHIRIKIANA NA TCRA NA BANK KUU

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na TCRA na Benki ya Tanzania wamefanikiwa kuwak**ata Watu 12 kwa tuhuma za kujihusiha na utapeli Kwa njia ya mtandao kupitia kampuni ya inayofahamika kwa jina la LEO BENETH LONDON maaruku k**a LBL .

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro SACP Alex Mk**a amesema Watu hao wamek**atwa wakiwashawishi Watu kujiunga na kampuni hiyo inayoendesha biashara hiyo mtandaoni bila ya kuwa na kibali kutoka Benki Kuu jambo ambalo ni kosa kisheria ambapo baadhi yao wamekutwa na Vijana zaidi ya 100 wakiwa wamewafungia ndani na kuwapa elimu namna ya kufanya biashara hiyo kwa madai ya kuwapa ajira.

Amesema biashara hiyo inachezwa mtandaoni ambapo Watu wanatakiwa kutazama video fupi ndipo wapate fedha ambapo wanatakiwa kutoa kiingilio kuanzia Tsh. 50,000, laki 1.5 na Tsh. 540,000 na kwamba baadhi ya Watuhumiwa wamekutwa tayari wamechukua Tsh. milioni 20 ambazo tayari zipo mtandaoni na kuwaahidi kuwa watakuwa Mabilionea.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linawashikilia Watuhumiwa watano akiwemo Gerald Masanya (31) Meneja wa Kampuni ya LBL Mbeya, Mkazi wa Nsalaga, Saphina Mwamwezi (23) Sekretari, Mkazi wa Ituha, Edda William (29) Mkazi wa Uwanja wa Ndege wa Zamani, Yohana Mkinda (29) Mkazi wa Tukuyu na Macrine Sinkala (23) Mkazi wa Nsalaga kwa tuhuma za kujihusisha na biashara hiyohiyo ya upatu mtandaoni bila kuwa na kibali wakitumia kampuni iitwayo LBL MBEYA MEDIA LIMITED.


DKT. TULIA AWATAKA WANA-CCM KUYASEMA MAZURI YA SERIKALI       Mjumbe wa Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Chama cha Mapin...
19/02/2025

DKT. TULIA AWATAKA WANA-CCM KUYASEMA MAZURI YA SERIKALI

Mjumbe wa Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) taifa ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mlezi wa CCM Mikoa ya Kusini na Kaskazini Unguja, Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amewataka Wanachama wa Chama hicho kusimama kifua mbele katika kuyasema mazuri yanayofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Dkt. Tulia ameyasema hayo leo tarehe 19 Februari, 2025 wakati akizungumza na Wana-CCM mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Kaskazini Unguja iliyokuwa na lengo la kukagua miradi mbalimbali ya Chama hicho katika Mkoa huo.

Aidha, Dkt. Tulia amewasisitiza Wanachama wa Chama hicho kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura katika tarehe zilizopangwa ili kufanikisha ushindi wa kishindo katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025.

Dkt. Tulia amesisitiza umuhimu wa Wanachama hao kuendelea kuwa wamoja wakati wote na kuepuka kutengeneza makundi yasiyo na tija kwa Chama na taifa. Kufanya hayo itasaidia kuunga mkono kazi nzuri inayofanywa na Chama hicho chini ya Viongozi wao wakuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapunduzi Zanzibar.

Sambamba na hayo, Dkt. Tulia ametoa mchango wa Shilingi Milioni tano (Tsh: 5,000,000/-) kwa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Kaskazini Unguja ili kuunga mkono ujenzi wa jengo la kitega Uchumi la Wanachama hao.



✍️ Wamzi Hassan

MWANAUME MMOJA ASAFIRI KILOMETA 11000, KUCHOMA MOTO NYUMBA YA X WAKE       Mwanaume mmoja huko Marekani aliyetambulika k...
19/02/2025

MWANAUME MMOJA ASAFIRI KILOMETA 11000, KUCHOMA MOTO NYUMBA YA X WAKE

Mwanaume mmoja huko Marekani aliyetambulika kwa jina la Harrison Jones amek**atwa na kushtakiwa kwa makosa sita ya jaribio la mauaji baada ya kudaiwa kuendesha gari zaidi ya kilomita 1100 ili kuchoma moto nyumba ya mwanaume mmoja wa Pennsylvania ambaye alikuwa akiwasiliana na mpenzi wake wa zamani, polisi wamesema.

Moto uliripotiwa katika nyumba ya Merganser Way huko Bensalem, Pennsylvania, muda wa saa 11 asubuhi tarehe 10 Februari, na kupelekea vikosi vya zimamoto kufika mahali hapo, kulingana na taarifa ya Idara ya Polisi ya Bensalem iliyotolewa Jumatatu.

Wapelelezi baadaye walibaini kuwa moto huo uliwashwa kwa makusudi, Picha za uchunguzi kutoka nyumba za jirani zilionyesha gari aina ya sedan nyeusi ikisimama karibu na makazi hayo saa 11 asubuhi, mtu mmoja alishuka kutoka kwenye gari akiwa amebeba kitu, akaelekea kwenye nyumba hiyo na kurudi kwenye gari hilo dakika 15 baadaye.

Muda mfupi baada ya mshukiwa kutoroka eneo hilo, mlipuko mkubwa uliteketeza nyumba hiyo kwa moto.

Wachunguzi walitumia kamera za makutano ya mji kufuatilia gari hiyo nyeusi yenye namba za usajili wa Michigan, ambayo iliwaongoza mpaka Michigan. Uchunguzi zaidi umebaini kuwa Harrison Jones, ambaye anaishi huko huko Michigan, alikuwa mpenzi wa zamani wa mwanamke ambaye alikuwa anawasiliana na Merganser Way anayeishi kwenye nyumba aliyochoma moto

Maafisa katika jimbo la Michigan walipata kibali cha kutafuta makazi ya Jones, ambapo waligundua vifaa vya kuvunja kufuri, simu ya mkononi, kompyuta na alama ya kuungua kwenye mkono wa Jones ambaye kwasasa amek**atwa na kushtakiwa kwa makosa sita ya jaribio la mauaji

✍ Wamzi Hassan

15/02/2025

Ibaada ni muhimu 😆🤣😂

BINTI TANZANIA NG'ARA CAMPAIGN SEASON FOUR_____________________________________    Ni msimu mwingine wa kuwaonesha upend...
02/02/2025

BINTI TANZANIA NG'ARA CAMPAIGN SEASON FOUR
_____________________________________

Ni msimu mwingine wa kuwaonesha upendo Mabinti wanafunzi wanaotoka kwenye Familia Duni, karibu tushiriki pamoja kuwanunulia Taulo za K**e (PADS).

Unaweza kuchangia PADS moja kwa moja au Pesa kwa thamani ya Pads kiasi ulichoguswa, Mungu akubariki sana.

☎️PADS____ Piga 0693073237 Utukabidhi mchango wako
💵PESA____ Lipa kwa M-Pesa mitandao Yote
Namba __ 35246112
Jina: WAMZI H. MWANGOMO


01/11/2024

YOU HEARD...!!!!

Tuambie Msimu Mwingine Wa *Tulia Trust Village* Ndani ya Kata ya Mwasenkwa Jijini Mbeya.

Unatamani Kuona Kitu Gani Kikifanyika Kwenye Kijiji Chenye Asili Yake.

Tumefika Tulia Trust Village Kuona Maendeleo na hivi Karibuni Tunakwenda Kufunga Tulia Trust Village.


Dr. Tulia AcksonDr. Tulia Ackson Tulia Ackson

DIAMOND PLATNUMZ AMEGAWA AJIRA KWA WASHINDI WA TULIA STREET TALENT COMPETITION 2024, AMETANGAZA KUWEKA TAWI LA LEBO YA W...
27/10/2024

DIAMOND PLATNUMZ AMEGAWA AJIRA KWA WASHINDI WA TULIA STREET TALENT COMPETITION 2024, AMETANGAZA KUWEKA TAWI LA LEBO YA WASAFI JIJINI MBEYA.

Leo Oktoba 27. 2024 umetamatika msimu wa 5 wa TULIA STREET TALENT COMPETITION 2024, ambapo mgeni rasmi wa mashindano hayo allikuwa Msanii nyota wa Muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz mbaye ni Mkurugenzi wa WASAFI MEDIA na Lebo ya WASAFI CLASSIC BAND (WCB).

Akiongea na washiriki pamoja na Wanambeya wote waliohudhulia kwenye uwanja wa T.IA Mbeya mjini, ambapo mashindano hayo yamefanyikia. Ametoa pongezi kwa waandaaji wa mashindano hayo ambo ni Taasisi ya TULIA TRUST , kwa namna inavyofanya kazi kubwa na nzuri kwa kuibua vipaji mbalimbali wakiwemo Wachekeshaji (Comedians), Waimbaji (Musicians), Wachezaji (Dancers), Wanamitindo (Model & Fashion) na MaDJ.

Pia ametoa pongezi kwa Mkurugenzi wa TULIA TRUST ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya mjini, Spika wa Bunge la JMT na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (I.P.U) Mh. Dkt Tulia Ackson Dr. Tulia Ackson , kwa kazi kubwa ya kuwafanya Kipaumbele Wananchi wote hususani wa jimbo lake kwani anafanya mengi mazuri na yenye tija. Amewataka Wananchi kuendelea kumuamini na kutokumpoteza, kwani Mh. Dkt Tulia ni Kiongozi hodari na Shujaz na Mwenye Koneksheni (connections) hivyo mambo mengi yapo safi na Mbeya imetulia.

Diamond Platnumz ameongeza kuwa kwa sasa ana mpango wa kufungua tawi la Studio za Wasafi Record jijini Mbeya, lengo likiwa ni kuendeleza vipaji vilivyopo. Ametangaza kuwa Washindi kila kategori iliyokuwa inashindaniwa, atatoa fulsa huku Mshindi wa kategori ya DJ ametangazwa kuajiriwa WASAFI FM, Mshindi wa kategori ya Comedy kuajiriwa na CHEKA TU, Washindi wa kategori ya Dancers nafasi ya kwanza na ya Pili kushiriki kwenye Video yake atakayotoa hivi karibuni na Washindi wa kategori ya Fashion wa kwanza na wa Pili kulipwa ili kumbunia Mavazi kwaajili ya Show zilizo mbele yake mwezi Novemba.

  Bunge la Kitaifa limeafiki uteuzi wa Profesa Kithure Kindiki kuwa Naibu Rais mteule wa Kenya baada ya jina lake kuwasi...
19/10/2024


Bunge la Kitaifa limeafiki uteuzi wa Profesa Kithure Kindiki kuwa Naibu Rais mteule wa Kenya baada ya jina lake kuwasilishwa na Rais William Ruto. Wabunge 236 walipiga kura ya 'Ndiyo' kuafiki uteuzi wa Kindiki
Jina lake sasa litawekwa katika gazeti rasmi la serikali na kisha kuapishwa kuanza kuhudumu k**a Naibu Rais .

Katiba inasema pindi rais anapowasilisha uteuzi kwenye Bunge, wabunge watapiga kura ya kulikataa au kuliidhinisha jina hilo. Pia hakuna sharti la kura ya thuluthi mbili.
“Prof. Kindiki, ambaye kwa sasa anahudumu k**a Waziri wa Mambo ya Ndani na Utawala wa Kitaifa, atahitaji idhini kutoka kwa Bunge la Kitaifa kabla ya kushika nafasi ya Naibu Rais. Bunge lazima lipigie kura uteuzi ndani ya siku 60 baada ya kupokea jina hilo.

Baada ya kuidhinishwa, mteule atateuliwa rasmi na Rais kuwa naibu wake. Ingawa Katiba haijaweka bayana muda wa uteuzi huu, unatarajiwa kutokea mara baada ya kuidhinishwa na Bunge.
Katika maandalizi ya uchaguzi mkuu wa 2022, Kindiki alikuwa miongoni mwa waliopendekezwa kuwa mgombea mwenza wa Ruto lakini hatimaye akaamua kumchagua Gachagua.

Baadaye alielezea kwamba alimchagua Gachagua kwa sababu ya umri wake na alifikiri wangeelewana zaidi. Mwanzoni mwa kuondolewa kwa Gachagua, kulikuwa na mazungumzo ya Kindiki kuwa ndiye anayefuata kuchukua nafasi yake.

Bunge la Seneti lilipiga kura ya kumtimua Naibu Rais Rigathi Gachagua kufuatia mchakato wa siku mbili uliohusisha ushahidi wa kina . Gachagua aliondolewa baada ya Maseneta kuunga mkono sababu tano kati ya kumi na moja zilizowasilishwa na Mbunge wa kibwezi kaskazini Mwinge Mutuse.

       Bunge la seneti nchini Kenya Alhamisi lilipiga kura na kuidhinisha kuondolewa ofisini kwa Naibu Rais Rigathi Gach...
18/10/2024


Bunge la seneti nchini Kenya Alhamisi lilipiga kura na kuidhinisha kuondolewa ofisini kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua, kutokana na mashtaka 5 kati ya 11 yaliyowasilishwa dhidi yake, katika hatua ambayo haijawahi kushuhudiwa.

Maseneta 54 kati ya 67 walipiga kura ya kumfukuza Gachagua kwa shtaka la kwanza la "ukiukaji mkubwa wa katiba", zaidi ya theluthi mbili ya idadi inayohitajika kisheria, na kumfanya kuwa naibu rais wa kwanza kulazimishwa kuondoka madarakani kwa mashtaka k**a hayo. Ni hatua ambayo baadhi ya wachambuzi wa kisiasa wanasema huenda ikaitumbukiza nchi hiyo ya Afrika Mashariki katika mzozo wa kisiasa.

Bunge la Kitaifa lilipiga kura wiki jana kumshtaki Gachagua, ambaye alimsaidia Rais William Ruto kushinda uchaguzi miaka miwili iliyopita lakini ameshambuliwa na washirika wa rais kwa madai ya kukosa uaminifu na msururu wa maoni ya uchochezi ya umma.
“Kulingana na hilo, Mheshimiwa Rigathi Gachagua... anakoma kushikilia wadhifa huo,” alisema Spika wa Seneti Amason Kingi.

Mchakato huo hata hivyo, hautakomea hapo. Gachagua amewasilisha maombi kadhaa kupinga shinikizo la kumtimua mamlakani, na jaji mkuu ameteua jopo la majaji watatu kusikiliza hoja zilizowasilishwa.

Gachagua, ambaye amekanusha madai hayo, alipaswa kujitetea dhidi ya mashtaka katika Seneti Alhamisi alasiri kabla ya upigaji kura. Alipokosa kufika, wakili wake Paul Muite alisema naibu huyo wa rais alikuwa amelazwa hospitalini akiwa na maumivu makali ya kifua, na kuitaka Seneti kusitisha shughuli kwa siku kadhaa. Lakini seneti ilikataa kufanya hivyo, na kupelekea timu ya wanasheria wa Gachagua kupinga hatua hiyo na kuondoka bungeni.

Dan Gikonyo, daktari anayemtibu Gachagua, aliwaambia wanahabari kuwa mwanasiasa huyo alilazwa katika hospitali ya Nairobi akiwa na tatizo la moyo Alhamisi mchana, lakini sasa yuko sawa na kuna uwezekano atalazimika kusalia hospitalini kwa saa 24-72. Kwa mujibu wa katiba ya Kenya, rais ana uhuru wa kumteua naibu mwingine baada ya seneti kuchukua hatua k**a hiyo.

☆ Wamzi Hassan

Address

Mapumulo

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Greencity Tv Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Greencity Tv Online:

Share