02/10/2025
TRA MKOA WA MBEYA WATOA ELIMU YA NAMNA AMBAVYO WAFANYA BIASHARA WA MTANDAONI WANAWEZA KUWA SEHEMU YA KUCHANGIA KODI NCHINI.
Elimu hii iliyoambatanishwa na mafunzo ya Matumizi sahihi na salama ya mitandao, pia wamezitaja faida endapo mfanya biashara mtandaoni atazipata endapo atakuwa rasmi katika kulipa kodi.
Faida hizo ni k**a vile
1. Kupata utambulisho wa Kisheria
2. Kuaminika kwa wateja na washirika
3. Kupata Fulsa na Mikopo na Ruzuku
4. Ushiriki katika tenda na wazabuni
5. Kuepuka adhabu za kisheria
6. Kupata alama nzuri ya kikodi
7. Historia ya kifedha iliyowazi
6. Ulinzi wa Biashara yako na
8. Usaidizi wa moja kwa moja kutoka TRA
Pamoja na faida hizo, Meneja wa TRA Mkoa wa Mbeya Bw. Lukas Shaban amesema sasa TRA Mkoa wa Mbeya wameanzisha Dawati maalumu ili kuwasaidia wafanyabiashara wa mtandaoni. Dawati hili linashughulika na elimu pamoja na changamoto zote, ili kuhakikisha kila mmoja anaweza kulipa kodi yake kwa heari na kwa moyo.
Ameongeza kuwa TRA ni rafiki wa mfanya biashara, hivyo kukiwa na jambo lolote la sintofahamu lenye lengo la kudhoofisha ulipaji wa kodi basi fika ofisini mila ipo wazi.