The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu kinatarajiwa kufanyika Oktoba 14, 2025 katika uwanja wa Sokoine, ambapo Mge...
13/10/2025

Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu kinatarajiwa kufanyika Oktoba 14, 2025 katika uwanja wa Sokoine, ambapo Mgeni Rasmi atakuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kaulimbiu ya Mwenge mwaka huu inawahimiza Watanzania wote kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo Oktoba 29, 2025, kuhakikisha sauti zao zinasikika katika kujenga mustakabali wa taifa.

04/10/2025

Meneja Mkuu Dimitar Pentev akiwa na msaidizi wake, Boyko Kamenov wamewasili nchini kuanza majukumu yao ya kikazi.

04/10/2025
04/10/2025

Mbunge mteule wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya, Suma Ikenda Fyandomo, ameendelea na harakati za kampeni ndani ya kata ya Iponjola kwa kutoa wito wa kura za kishindo kwa mafiga matatu ya ushindi. Amehimiza wananchi kuonesha mshik**ano wao kwa kumchagua Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Ubunge CPA Anton Mwantona na Diwani Banunu ili kuhakikisha maendeleo yanayoshuhudiwa sasa yanaendelezwa kwa kasi kubwa zaidi.

Aidha, kupitia mkutano huo wa hadhara, Fyandomo amewataka wananchi wa Iponjola kudumisha mshik**ano na mshikikiano kwa kuendelea kuombea amani ya Tanzania. Amesema bila amani hakuna maendeleo, na ndiyo msingi unaowezesha utekelezaji wa miradi ya barabara, maji, elimu na afya kufanyika kwa ufanisi katika kila kijiji na kata.

02/10/2025

IBUNGILA YAMWAGA SHANGWE: CPA MWANTONA NA MAMA SAMIA WAMEJIBU SAUTI ZA WAZEE

Katika kijiji cha Ibungila, upepo wa shangwe na furaha unavuma k**a ngoma za asili zilizoamshwa na ushindi wa kijani. Wazee waliwahi kutoa kilio chao – maji, umeme na barabara – leo hawadai tena, maana waliyoyasema yamekuwa mwili na damu.

CPA Anton Mwantona, akiwa bega kwa bega na Mama Samia Suluhu Hassan, wamethibitisha kuwa ahadi si ndoto bali ni matunda yanayoonja kila kaya. Vituo vya maji vimewaka k**a chemchemi za matumaini, nyaya za umeme zimeshinda giza, na barabara zimefungua njia mpya za biashara na maendeleo.

Wananchi wa Ibungila sasa hawasemi “tutangoja,” bali wanasema “tunakula matunda ya kazi ya Mama Samia na CPA wetu Mwantona.” Ni ishara ya upendo, ni ishara ya ushindi, ni ishara ya kura za kishindo zinazokuja kwa kishangwe.

🟢💪 Ibungila imesema, kazi iendelee – kura zote kwa Mama Samia na CPA Mwantona!

Wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu ujao utakaof...
23/09/2025

Wananchi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kushiriki uchaguzi mkuu ujao utakaofanyika tarehe 29 Oktoba, kwa ajili ya kuwachagua viongozi watakaosimamia maendeleo ya kweli katika maeneo yao.

Wito huo umetolewa na Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbarali, Mhe. Bahati Keneth Ndingo, katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Kapunga, Kata ya Itamboleo, ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa kampeni za kijiji kwa kijiji.

Katika mkutano huo, Mhe. Bahati Keneth Ndingo alipata nafasi ya kuzungumza moja kwa moja na wananchi wa vijiji vyote vinavyounda kata ya Itamboleo ambapo alieleza mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya CCM, hususan ndani ya uongozi wa Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ikiwemo miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika kata hiyo

Mhe. Ndingo aliwahakikishia wananchi kuwa serikali ya CCM itaendelea kuboresha huduma za msingi k**a, Umeme,Maji na Miundombinu ya barabara huku akisisitiza kuwa barabara ya Itamboleo – Kapunga ipo kwenye mpango wa kuwekwa lami, k**a sehemu ya juhudi za Rais Samia katika kuimarisha miji inayokuwa kwa kasi ya maendeleo.

Aidha, Mhe.Bahati Ndingo alitoa pongezi kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uamuzi wake wa busara wa kurejesha vijiji 29 kati ya 34 vilivyokuwa kwenye hifadhi ya Ruaha, hatua ambayo imewawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji mali.

Akihitimisha ziara yake ya siku ya sita katika kata hiyo, Mhe. Ndingo aliwashukuru wananchi wa Itamboleo kwa kuendelea kuiamini CCM huku akiahidi kuwa chama hicho kitaendelea kuwa karibu na wananchi na kutatua changamoto zao kwa vitendo kupitia mipango madhubuti ya maendeleo.

Katika upepo wa hamasa na shamrashamra za kisiasa, mgombea Ubunge wa Jimbo jipya la Uyole, Spika wa Bunge la Jamhuri ya ...
23/09/2025

Katika upepo wa hamasa na shamrashamra za kisiasa, mgombea Ubunge wa Jimbo jipya la Uyole, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, ameibua kishindo na kuwasha moto wa siasa tarehe 22 Septemba 2025 alipowasili Kata ya Nsalaga, Mbeya. Viwanja vya Shule ya Msingi Itezi viligeuka kuwa bahari ya watu, wakishangilia jina la Tulia na CCM huku wakibeba mabango na kuvaa rangi za chama chao tawala.

Kwa sauti yenye uzito wa matumaini, Dkt. Tulia alisisitiza kuwa njia pekee ya maendeleo ya kweli na kasi ni kuhakikisha wananchi wa Uyole wanampigia kura za kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan katika nafasi ya Urais, sambamba na yeye katika nafasi ya Ubunge pamoja na madiwani wa CCM. Alisema wazi kuwa Jimbo la Uyole bado lina kiu ya huduma za msingi, na anayejua kutuliza kiu hiyo si mwingine bali ni Rais Samia kwa ushirikiano wake wa karibu na wabunge na madiwani wa chama hicho.

Akijibu kwa kishindo cha shangwe, umati wa wananchi ulitikisa anga kwa nderemo, ukibeba ujumbe mmoja: "Tulia na Samia, maendeleo kwa kasi mpya!"

Dkt. Tulia hakusita kujipambanua kwa vitendo akieleza safari yake ya miaka mitano ya kuliongoza Jimbo la Mbeya Mjini lenye Kata 32, akisema aliwahi kupeleka miradi ya maendeleo iliyoacha alama isiyofutika. Kwa kujiamini aliahidi kuwa Uyole lenye Kata 13 pekee litakuwa kazi nyepesi kwa mikono yake ya ujasiri na mshirikiano wa Rais Samia.

Mwisho wa mkutano huo uligeuka kuwa tamasha la matumaini; nyimbo za CCM ziliimbwa kwa sauti moja, vijana walicheza kwa mitindo ya kishujaa, na wazee walitupa dua njema. Ishara zote zikibeba ujumbe mmoja: Uyole iko tayari, Tulia yupo mstari wa mbele, Samia ndiye dira ya maendeleo

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbarali kupitia CCM, Mhe. Bahati Keneth Ndingo, ameendelea na kampeni zake kata ya Imaliloson...
23/09/2025

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Mbarali kupitia CCM, Mhe. Bahati Keneth Ndingo, ameendelea na kampeni zake kata ya Imalilosongwe katika siku ya tano ya kampeni za kijiji kwa kijiji. Ametembelea vijiji vya Urunda, Mahongole, Warumba, Imalilo Songwe na Mwanavala, akizungumza na wananchi na kueleza mikakati ya maendeleo kupitia Ilani ya CCM 2025-2030.

Katika mikutano hiyo, Mhe. Ndingo alimsifia Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ya kupeleka miradi ya maendeleo Mbarali, hasa katika elimu, afya na miundombinu. Amesema mshik**ano wa Rais Dkt. Samia, wabunge na madiwani wa CCM ndiyo siri ya kasi ya maendeleo yanayoonekana sasa katika jimbo hilo.

Wananchi walieleza changamoto zao ikiwemo ukosefu wa umeme na ubovu wa barabara, ambapo Mhe. Ndingo aliwahakikishia kuwa CCM itaendelea kushughulikia kero hizo. Aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi Oktoba 29, 2025 kuwachagua wagombea wa CCM katika nafasi zote ili kuendeleza ushindi wa maendeleo.

SIKU YA NNE YA KAMPENI ZA MGOMBEA UBUNGE WA CCM JIMBO LA MBARALI, MHE. BAHATI KENETH NDINGOLeo ikiwa ni siku ya nne tang...
22/09/2025

SIKU YA NNE YA KAMPENI ZA MGOMBEA UBUNGE WA CCM JIMBO LA MBARALI, MHE. BAHATI KENETH NDINGO

Leo ikiwa ni siku ya nne tangu kuanza kwa kampeni za Mgombea Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Mbarali, Mhe. Bahati Keneth Ndingo ameendelea na ziara zake za kuomba kura kwa wananchi kupitia mikutano ya kijiji kwa kijiji katika Kata ya Chimala.

Katika ziara hiyo, Mhe. Ndingo ametembelea vijiji vya Mengele, Isitu, Igumbilo, Chimala, Lyambogo na Muwale, ambapo alipata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na wananchi pamoja na wanachama wa chama hicho.

Akiwa katika mikutano hiyo, Mhe. Ndingo amewaomba wananchi kuwaunga mkono na kuwachagua wagombea wanaotokana na CCM katika nafasi za Urais, Ubunge, na Udiwani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Baadhi ya wananchi walitumia nafasi hiyo kuuliza maswali na kuwasilisha kero mbalimbali, ikiwemo changamoto ya ukosefu wa umeme katika baadhi ya maeneo pamoja na ubovu wa miundombinu ya barabara.

Akijibu hoja hizo, Mhe. Ndingo ameeleza kuwa serikali ya CCM inaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha kuwa huduma za msingi k**a umeme na barabara zinaboreshwa huku akiahidi kushirikiana na wananchi na viongozi wa maeneo husika kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa suluhisho la kudumu.

Mhe. Bahati Keneth Ndingo amewahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi ili kuwachagua viongozi wa CCM wanaosimamia maendeleo ya kweli na utekelezaji wa Ilani ya chama, akisisitiza kuwa maendeleo endelevu yanahitaji ushirikiano wa karibu kati ya viongozi na wananchi.

Aidha, Mhe. Bahati Ndingo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za miradi katika Kata ya Chimala, hususan kwenye sekta za Elimu na Afya, ambazo zinaendelea kuboresha maisha ya wananchi.

Mwisho, Mhe. Ndingo amewashukuru wananchi na wanachama wa CCM kwa kuendelea kukiamini chama hicho, huku akiahidi kuwa CCM itaendelea kuwa karibu na wananchi na kutatua changamoto zao kwa vitendo kupitia mipango

13/09/2025

SIMBA DAY

13/09/2025

WEWE UNGEIPA JINA GANI???

13/09/2025

YANGA SC KWA MKAPA

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Green Voice TV:

Share