The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

05/06/2026

Magoli Bora Kabisa Yaliyowahi Fungwa Kwenye Kombe la Dunia”, Magoli bora duniani
Best World Cup Goals
FIFA World Cup Highlights
:

05/06/2026

CLATOUS CHAMA AWASILI MO ARENA TAYARI KWA TIZE NA KIKOSI CHAKE

EZEKIEL Gwatengile, Afisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, akiwa na Waheshimiwa Wabunge Mhe. Patali Shida Pat...
05/06/2026

EZEKIEL Gwatengile, Afisa kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira, akiwa na Waheshimiwa Wabunge Mhe. Patali Shida Patali (Mbeya Vijijini) na Mhe. Timida Fyandomo (Mbunge wa Vijana), ambao pia ni wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira, walihudhuria maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa JKCC jijini Dodoma. Hafla hiyo ilihusisha viongozi na wadau mbalimbali wa mazingira kutoka maeneo tofauti nchini, ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha uhifadhi wa mazingira na usimamizi endelevu wa rasilimali za asili.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Emmanuel Nchimbi, ambaye alisisitiza umuhimu wa kulinda mazingira na kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji kwa maendeleo endelevu ya taifa. Alitoa wito kwa wananchi na viongozi kushirikiana katika kulinda mazingira ili kuhakikisha rasilimali hizo zinawanufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Uongozi wa Simba umeacha uamuzi wa hatma ya makipa Kassali Djibril na Mousa Camara kwa benchi la ufundi chini ya kocha S...
04/06/2026

Uongozi wa Simba umeacha uamuzi wa hatma ya makipa Kassali Djibril na Mousa Camara kwa benchi la ufundi chini ya kocha Steve Barker baada ya mikataba yao kufika ukingoni mwisho wa msimu.

Hii ni kutokana na kanuni ya usajili inayoruhusu kipa mmoja wa kigeni pekee. Camara aliwahi kuongoza Simba fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika, huku Kassali akipata mafanikio makubwa akija dirisha dogo, akifanikisha cleansheet 12.

Mwenyekiti Bodi ya Wakurugenzi Simba, Crescentius Magori, amesema uamuzi wa mkataba mpya utategemea matokeo ya mechi tano za mwisho.




04/06/2026

AHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA KWA MAUAJI YA MZAZI MWENZAKE NA MWANAFUNZI CHUNYA

Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imemhukumu Barnaba Daud Mtweve (56), mkazi wa Chunya, kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kuua watu wawili na kujaribu kumuua mtoto wake. Hukumu hiyo ilitolewa Juni 3, 2026 na Jaji Mfawidhi Joachim Charles Tiganga.

Mahakama ilielezwa kuwa Machi 31, 2024, Mtweve aliingia usiku nyumbani kwa aliyekuwa mzazi mwenzake Herriety Lupembe (37) na kuwaua Lupembe pamoja na Ivone Tatizo (15), mwanafunzi wa Kidato cha Pili, kwa kuwapiga kichwani kwa kitu butu. Aidha, alimjeruhi mtoto wake Harris Barnaba (06) kabla ya kufunga milango kwa nje na kutoweka na funguo. Waendesha mash*taka waliomba adhabu kali ili iwe fundisho dhidi ya vitendo vya mauaji na ukatili kwa watoto katika jamii.

04/06/2026

🎤👑 Lady JayDee And The Band wameanza kutonesha kiu ya mashabiki kwa ladha ya muziki wa kiwango cha juu! Malkia wa Bongo Fleva, Lady Jaydee, ambaye ameendelea kutamba kwa zaidi ya miaka 25 katika muziki wa Tanzania, anaonekana kuja na kazi nyingine itakayogusa mioyo ya wengi.

🎤 LADY JAYDEE ARUDI KIVINGINE!
🔥 MALKIA WA BONGO FLEVA AFUNGUA UKURASA MPYA
👑 LADY JAYDEE AND THE BAND WATIKISA TENA🎶 LADHA YA KIBAO KIPYA YAWASISIMUA MASHABIKI🔥 MALKIA AMERUDI, UPO TAYARI?
🎤 SAUTI YA DHAHABU YARUDI KWA NGUVU

04/06/2026

Mnamo Nov 1, 1995, Mchezaji wa Brazil Leonardo Araujó, Alifunga Bao Ambalo hadi Leo linatajwa kuwa ni moja ya Bao bora zaidi kuwahi kutokea Duniani, Goli hili liliitwa "JUGGLING GOAL" na Lilifungwa Katika ligi ya Japani (J.LEAGUE), Ambapo Leonardo Alikuwa Akicheza klabu ya (KASHIMA ANTLERS) dhidi ya "YOKOHAMA FLÜGELS" . Una maoni Gani katika Hilo..?

POLISI MBEYA WAKAMATA WATUHUMIWA 871 WA UHALIFU MWEZI MEIJeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limetangaza kuwa limewakamata wat...
04/06/2026

POLISI MBEYA WAKAMATA WATUHUMIWA 871 WA UHALIFU MWEZI MEI

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limetangaza kuwa limewakamata watuhumiwa 871 wa makosa mbalimbali katika mwezi Mei 2026, ikiwemo mauaji, wizi, ubakaji, dawa za kulevya na umiliki haramu wa silaha.

Miongoni mwa waliokamatwa ni Baraka Mwakatobe (31) na Said Baraka (39), wakazi wa Dodoma, waliokutwa wakisafirisha boksi 403 za vipodozi vyenye viambata sumu vilivyopigwa marufuku nchini kupitia Kizuizi cha Polisi Chimala. Pia walikutwa na vitenge na vikoi vilivyoingizwa nchini bila kulipiwa ushuru.

Aidha, Polisi wanamshikilia Shaban Safari (48) wa Kyela kwa tuhuma za kukutwa na kete 27 za dawa za kulevya aina ya he**in pamoja na gramu 2 za bangi. Katika mwezi huo huo, watuhumiwa 20 walikamatwa na kilo 12.24 za bangi, wawili wakikamatwa na lita 30 za gongo, huku wawili wengine wakikamatwa na gobole lenye risasi saba.

Kwa upande wa mahakama, kesi 224 zilifikishwa mahakamani ambapo 122 zilimalizika kwa wash*takiwa kutiwa hatiani. Pia, Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imemhukumu kunyongwa hadi kufa Barnaba Daud Mtweve (56) wa Chunya kwa kosa la kuwaua watu wawili na kujaribu kumuua mtoto wake mwaka 2024. Polisi pia wamewafungia leseni madereva tisa kwa makosa hatarishi ya usalama barabarani na kuwataka wananchi kuendelea kushirikiana katika mapambano dhidi ya uhalifu.

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share