The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

12/12/2025

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi, akisaini kitabu cha maombolezo alipofika nyumbani kwa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Peramiho, Marehemu Jenista Mhagama, eneo la Itega jijini Dodoma, Marehemu Jenista Mhagama alifariki tarehe 11 Desemba, 2025 jijini Dodoma.✍️✍️

12/12/2025

RIP JENISTA MHAGAMA

10/12/2025

MAPINDUZI MAKUBWA KWENYE MFUMO WA ELIMU TANZANIA 🔥🔥🔥📌

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, amesema Serikali inajiandaa kuanza utekelezaji wa mageuzi makubwa ya mfumo wa elimu yatakayobadilisha muundo uliodumu kwa zaidi ya nusu karne. Akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 10, 2025, katika Kituo cha Urithi wa Ukombozi jijini Dar es Salaam, Profesa Mkenda amesema mfumo wa sasa wa 7+4+2+3+ ulianza kutumika kati ya mwaka 1965 na 1968 chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere. Amesema chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, Serikali inakuja na mfumo mpya wa 6+4+2/3+3+, ambao utaifanya elimu ya msingi kuwa miaka sita badala ya saba. Mfumo huo pia utaanzisha elimu ya lazima ya miaka 10, tofauti na mfumo wa sasa wenye miaka saba. Kwa mujibu wa Profesa Mkenda, utekelezaji wa mwanzo umeanza kupitia mitaala mipya kwa wanafunzi wa darasa la tatu ambao ifikapo mwaka 2027 watakuwa wa kwanza kufikia darasa la sita na kufanya mtihani wa kupima uwezo kabla ya kuendelea moja kwa moja na elimu ya sekondari ya kati hadi kidato cha nne. Utekelezaji rasmi wa mfumo mpya kitaifa unatarajiwa kuanza mwaka 2028.

KWA TIZE HILI UNAIONA WAPI TAIFA STARS AFCON
10/12/2025

KWA TIZE HILI UNAIONA WAPI TAIFA STARS AFCON

10/12/2025

YANGA SC YAMTAJA MPANZU-"Elie Mpanzu ni mchezaji mzuri", Ali Kamwe - Meneja wa HAbari na Mawasiliano Yanga CC:

10/12/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Marry Timotheo, Mkazi wa Garijembe Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya Mtoto wake aitwaye Scola Athanas Mwaba [10] aliyekuwa Mwanafunzi wa Darasa la Nne katika Shule ya Msingi Ngonde.

Tukio hilo limetokea Disemba 09, 2025 saa 6:30 mchana katika Kijiji cha Garijembe, Kata na Tarafa ya Tembela, Wilaya ya Mbeya baada ya Marry Timotheo [Mama mzazi wa marehemu] kumuadhibu kwa kumpiga kwa kitu kizito kichwani kwa madai ya utukutu.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni kujichukulia ni sheria mkononi kwa kumuadhibu mtoto wake kwa kumpiga hadi kufa na kisha kuutupa mwili wake shambani jirani na nyumba yake kwa kushirikiana na jirani yake aitwaye Sharifa Nzalanje, Mkazi wa Garijembe ambaye pia anashikiliwa na Jeshi la Polisi.

Upelelezi unakamilishwa ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi ya watuhumiwa.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa baadhi ya wazazi na walezi kuacha vitendo vya kujichukulia sheria mkononi kwa kutoa adhabu kali kwa watoto na badala yake watoe adhabu za kuwarekebisha na kuwafundisha mienendo na maadili mema ili kuepuka madhara yanayoweza kuwapata ikiwemo kupoteza maisha au kupata ulemavu.

10/12/2025

Kocha wa Timu ya Taifa Miguel Gamondi akizungumzia kikosi cha wachezaji 28 watakaoshiriki Fainali za AFCON 2025, Morocco na maandalizi yaliyoanza Cairo, Misri

Big thanks to Mac Macfor all your support! Congrats for being top fans on a streak 🔥!
10/12/2025

Big thanks to Mac Mac

for all your support! Congrats for being top fans on a streak 🔥!

10/12/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene amewashukuru watanzania kwa kuonyesha utulivu na uzalendo katika kuilinda amani ya Tanzania na kudumisha utulivu wakati nchi ikienda kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania. Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa ukaguzi wa hali ya ulinzi na usalama katika mitaa mbalimbali ya jijini Dar es Salaam huku Vyombo vya Ulinzi na usalama vikiendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo tofauti nchini ambapo wananchi nao wametoa maoni yao.

10/12/2025

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. George Simbachawene amewashukuru watanzania kwa kuonyesha utulivu na uzalendo katika kuilinda amani ya Tanzania na kudumisha utulivu wakati nchi ikienda kuadhimisha miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania. Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa ukaguzi wa hali ya ulinzi na usalama katika mitaa mbalimbali ya jijini Dar es Salaam huku Vyombo vya Ulinzi na usalama vikiendelea kuimarisha ulinzi katika maeneo tofauti nchini ambapo wananchi nao wametoa maoni yao.

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Green Voice TV:

Share