The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

23/08/2026

TUNGA SENTENSI MOJA

Singida BS 1-2 Simba SC

22/08/2026

SIMBA SC WAMEMSAJILI WATU WAKATI YANGA SC IKISAJILI WACHEZAJI HII NDIO TOFAUTI YA YANGA SC VS SIMBA SC

19/08/2026

MAREFA WA WANATUMIA AKILI ZAO AU UJUZI WALIOPATA DARASANI TUKIO. MOJA HUKUMU TOFAUTI

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Baba Tpack, Lilianially Amanz, Loth Mhadisa, Moses Mwenda...
19/08/2026

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Baba Tpack, Lilianially Amanz, Loth Mhadisa, Moses Mwendanabo, Arfa Nathra, Livinus Mnyambo, Qamna Boy, Boss Kyamaranga, Erick John, Hamisi Mohammed Mandi, Shebby Ally, Issa Imidi, M***a Hussein

18/08/2026

NBCPL: Walioumia kipindi cha kwanza ni wenye Dhahabu. WAZEE WA KATORO
FT : Namungo FC 1-0 Geita Gold

18/08/2026

*NI MUDA WA KUJIPATIA TIKETI YAKO HII SIO YA KUKOSA NI SHOW YA KIHISTORIA MKOA WA MBEYA πŸ“ŒSAMBA MELODY πŸ”₯* Samba melodie Kenny Lawrence Paul Mgaya Sibonike NM Vance Evance

*MASANDAWANA FC MABINGWA WA TULIA TRUST UYOLE CUP 2026 WABEBA KOMBE NA SHILINGI MILINI 10*Ligi ya Mpira wa Miguu ya Tuli...
17/08/2026

*MASANDAWANA FC MABINGWA WA TULIA TRUST UYOLE CUP 2026 WABEBA KOMBE NA SHILINGI MILINI 10*

Ligi ya Mpira wa Miguu ya Tulia Trust Uyole Cup 2026 imemalizika hii leo kwa Timu ya Masandawa Fc kuibuka Mabingwa kwa ushindi wa Penati 3-2 dhidi ya Airport Fc baada ya dakika tisini kumalizika kwa suluhu (0-0) katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Mwawinji Uyole ya kati.

Mabingwa wa Tulia Trust Uyole Cup 2026 Masandawana Fc wametwaa kombe na zawadi ya Shilingi Milioni 10 huku mshindi wa pili Airport Fc wakipata kitita cha Shilingi Milioni 5 huku zawadi mbalimbali za Mfungaji bora, Mchezaji bora, Kipa bora, Kocha bora ambao wote wamepata zawadi ya Shilingi laki moja na Kikundi bora cha Ushangiliaji kikipata shilingi laki mbili.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi kwa Bingwa na washindi wa tuzo mbalimbali amesema Taasisi ya Tulia Trust itaendelea na udhamini wa Mashindano haya wakati wote, huku akiweka wazi kuwa ligi hiyo itaendelea kuchezwa ndani ya uwanja wa Mwawinji na amewapongeza wafanyabiashara wanaotumia fursa hii kuongeza uchumi wao.

MAHUNDI AWASHTUA VIJANA IWAMBI KUTUMIA MICHEZO KUPATA AJIRA, KUJENGA IWAMBI BILA UHALIFUNaibu Waziri wa Maendeleo ya Jam...
16/08/2026

MAHUNDI AWASHTUA VIJANA IWAMBI KUTUMIA MICHEZO KUPATA AJIRA, KUJENGA IWAMBI BILA UHALIFU

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Mhandisi Maryprisca Mahundi amewataka amewataka vijana kutumia michezo k**a fursa ya kujipatia ajira na kujenga maisha yao, huku wakiepuka vitendo vya uhalifu ikiwemo wizi na ukatili wa kijinsia.

Naibu Waziri Mahundi ameyasema hayo wakayi akikabidhi vifaa vya michezo kwa timu 13 za Kata ya Iwambi jijini Mbeya.

Amesema michezo inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kuwaweka vijana pamoja, kuwajengea vipaji na kuimarisha amani na mshik**ano katika jamii huku akiwataka wananchi wa Iwambi kuunda timu moja imara itakayowakilisha kata hiyo katika mashindano mbalimbali na kuitangaza Iwambi kupitia michezo.

Aidha, amependekeza kuanzishwa kwa klabu ya mbio za pole (jogging) katika kata hiyo, akisema mazoezi ni muhimu katika kuimarisha afya na kusaidia jamii kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza kwani michezo inapaswa kuwa chombo cha kuimarisha upendo na mshik**ano ndani na nje ya Kata ya Iwambi, huku akitoa wito wa kushirikiana katika mapambano dhidi ya uhalifu.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Iwambi, Groria Ipopo Mwamajemba (Mchina), amemshukuru Mahundi kwa msaada huo, akisema amekuwa sehemu ya wakazi wa Iwambi na ameendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo katika kata hiyo.

Mwamajemba amesema kupitia michezo, vitendo vya uhalifu vimepungua kwa kiasi kikubwa katika Kata ya Iwambi, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwekeza katika michezo kwa vijana.

Mahundi ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya na Mkurugenzi wa Maryprisca Women Empowerment Foundation (MWEF), amekabidhi jozi mbili za vifaa vya michezo kwa kila timu pamoja na mpira mmoja kwa kila timu, katika hafla iliyofanyika katika Uwanja wa Sekondari Iwambi ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Diwani wa Kata ya Iwambi, Groria Ipopo Mwamajemba maarufu k**a Mchina, aliyeanzisha mashindano ya mpira wa miguu yaliyowakutanisha vijana kutoka mitaa mbalimbali ya kata hiyo

15/08/2026

πŸ”₯ SAMBA MELODY ANAKWALIKA UZINDUZI WA ALBUM YAKE! 🎢πŸ”₯ Samba melodie

Msanii SAMBA MELODY anatarajia kuzindua rasmi Album yake mpya, FROM USAFWANI, katika tukio kubwa litakalofanyika tarehe 5 Septemba katika ukumbi wa White House, Uyole.

Ni usiku maalum wa muziki, burudani na kusherehekea kazi mpya ya msanii huyu. Mashabiki wa muziki, wadau na wapenda burudani wote mnakaribishwa kufika kwa wingi kumpa sapoti SAMBA MELODY na kushuhudia uzinduzi huu wa kipekee.

πŸ“… TAREHE: 5 SEPTEMBA
πŸ“ ENEO: WHITE HOUSE, UYOLE
🎀 MSANII: SAMBA MELODY
πŸ’Ώ ALBUM: FROM USAFWANI
πŸ“Ί THE GREEN VOICE TV

πŸ”₯ Usikose! Fika kwa wingi, support SAMBA MELODY na uwe sehemu ya historia hii!

15/08/2026

πŸ”₯ SAMBA MELODY ANAKWALIKA UZINDUZI WA ALBUM YAKE! 🎢πŸ”₯

Msanii SAMBA MELODY anatarajia kuzindua rasmi Album yake mpya, FROM USAFWANI, katika tukio kubwa litakalofanyika tarehe 5 Septemba katika ukumbi wa White House, Uyole.

Ni usiku maalum wa muziki, burudani na kusherehekea kazi mpya ya msanii huyu. Mashabiki wa muziki, wadau na wapenda burudani wote mnakaribishwa kufika kwa wingi kumpa sapoti SAMBA MELODY na kushuhudia uzinduzi huu wa kipekee.

πŸ“… TAREHE: 5 SEPTEMBA
πŸ“ ENEO: WHITE HOUSE, UYOLE
🎀 MSANII: SAMBA MELODY
πŸ’Ώ ALBUM: FROM USAFWANI
πŸ“Ί THE GREEN VOICE TV

πŸ”₯ Usikose! Fika kwa wingi, support SAMBA MELODY na uwe sehemu ya historia hii!
Samba melodie

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share