22/09/2025
SIKU YA NNE YA KAMPENI ZA MGOMBEA UBUNGE WA CCM JIMBO LA MBARALI, MHE. BAHATI KENETH NDINGO
Leo ikiwa ni siku ya nne tangu kuanza kwa kampeni za Mgombea Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Mbarali, Mhe. Bahati Keneth Ndingo ameendelea na ziara zake za kuomba kura kwa wananchi kupitia mikutano ya kijiji kwa kijiji katika Kata ya Chimala.
Katika ziara hiyo, Mhe. Ndingo ametembelea vijiji vya Mengele, Isitu, Igumbilo, Chimala, Lyambogo na Muwale, ambapo alipata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na wananchi pamoja na wanachama wa chama hicho.
Akiwa katika mikutano hiyo, Mhe. Ndingo amewaomba wananchi kuwaunga mkono na kuwachagua wagombea wanaotokana na CCM katika nafasi za Urais, Ubunge, na Udiwani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.
Baadhi ya wananchi walitumia nafasi hiyo kuuliza maswali na kuwasilisha kero mbalimbali, ikiwemo changamoto ya ukosefu wa umeme katika baadhi ya maeneo pamoja na ubovu wa miundombinu ya barabara.
Akijibu hoja hizo, Mhe. Ndingo ameeleza kuwa serikali ya CCM inaendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha kuwa huduma za msingi k**a umeme na barabara zinaboreshwa huku akiahidi kushirikiana na wananchi na viongozi wa maeneo husika kuhakikisha changamoto hizo zinapatiwa suluhisho la kudumu.
Mhe. Bahati Keneth Ndingo amewahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi ili kuwachagua viongozi wa CCM wanaosimamia maendeleo ya kweli na utekelezaji wa Ilani ya chama, akisisitiza kuwa maendeleo endelevu yanahitaji ushirikiano wa karibu kati ya viongozi na wananchi.
Aidha, Mhe. Bahati Ndingo ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuendelea kuleta fedha nyingi za miradi katika Kata ya Chimala, hususan kwenye sekta za Elimu na Afya, ambazo zinaendelea kuboresha maisha ya wananchi.
Mwisho, Mhe. Ndingo amewashukuru wananchi na wanachama wa CCM kwa kuendelea kukiamini chama hicho, huku akiahidi kuwa CCM itaendelea kuwa karibu na wananchi na kutatua changamoto zao kwa vitendo kupitia mipango