The Green Voice TV

The Green Voice  TV Karibu The Green Voice TV, usisahau ku "Subscribe" You tube channel yetu. "Yes we are Green".

14/08/2025

Katika hatua ya 16 bora Ndani ya Tulia Trust Uyole Cup inayofanyika Uwanja wa Mwawinji-Uyole ya Kati Kati ya African Boys na Naza Boys umemalizika Kwa Sare ya Kufungana gori 1 - 1

Katika hatua ya Matuta African Boys wamefanikiwa kupata ushindi.

MATOKEO PENATI

African Boys Pen 2
Naza Boys Pen 0

Cc Dr. Tulia Ackson

Mhe. Suma Fyandamo Atoa Heshima za Mwisho kwa Hayati Job Yustino Ndugai
10/08/2025

Mhe. Suma Fyandamo Atoa Heshima za Mwisho kwa Hayati Job Yustino Ndugai

10/08/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Pelynlp Jocktan, Kalapina Lesilwa, Mamy Rahma, Dev's Son

*VIJANA NA DEMOKRASIA: MSINGI WA MABADILIKO YA KWELI*✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻Demokrasia ni ngoma ya mabadiliko inayohitaji kila kijana k...
08/08/2025

*VIJANA NA DEMOKRASIA: MSINGI WA MABADILIKO YA KWELI*✍🏻✍🏻✍🏻✍🏻

Demokrasia ni ngoma ya mabadiliko inayohitaji kila kijana kucheza kwa hatua ya uelewa, si kwa midundo ya ushabiki. Ni mwaliko wa kuchagua kesho, si kusindikiza leo. Katika dunia inayosonga kwa kasi, vijana ndio pumzi ya taifa, lakini k**a hawatapaza sauti yao kupitia kura, taifa litabaki likilia kwa kimya kisichosikika.

Kura si kijikaratasi – ni silaha ya amani, ni saini ya maamuzi, ni mlango wa matumaini. Kwa vijana, kura ni zaidi ya haki – ni wajibu wa kizalendo. Kupiga kura ni kutangaza kwamba unaamini katika nguvu ya mabadiliko, na kwamba unaamini kesho inaweza kuwa bora zaidi k**a utaichangia leo.

> “Mabadiliko hayaji k**a mvua ya ghafla – huandaliwa, hupangwa, na huchaguliwa.”

Vijana wana elimu, wana nguvu, wana sauti, na wana ndoto. Sasa ni wakati wa kuzitumia hizo silaha nne kwa njia ya Demokrasia. Kupiga kura ni kutekeleza ndoto zako kwa vitendo. Ni kujenga taifa unalotamani kuliona — kwa kalamu yako, kwa fikra zako, kwa sauti yako.

Kwa hiyo, kila kijana anapaswa kujiuliza: Ninaitumiaje nafasi yangu ya kidemokrasia? Ninachagua kwa sababu ya ahadi tamu au kwa sababu ya historia ya utendaji? Maamuzi ya leo ni msingi wa maisha ya kesho. Na k**a kijana utatumia kura yako k**a zawadi ya hisia au kisasi, utalazimika kuishi na majuto yaliyojengwa kwa mikono yako mwenyewe.

> “Usisubiri kesho ijengewe na wengine, chukua tofali la kura yako, jenge na wewe.”

Kila kura ya kijana ni jiwe moja la kujenga daraja la kesho bora. Uamuzi wa leo unaweza kuwa uzuri wa kesho au majuto ya miaka mingi. Tusikubali kupoteza nafasi kwa maneno ya kupumbaza au ahadi za chupa tupu. Tusome, tuhamasike, na tupige kura kwa msimamo na maarifa.

> “Ukitaka mabadiliko, usisubiri viongozi waje – kuwa mmoja wao kwa kura yako.”

Kwa hiyo, vijana wote – wa vijijini na mijini, wa vyuoni na kazini, wa mitaani na majumbani – tuichukue Demokrasia k**a fursa ya kuandika historia, si kuisoma kwa huzuni. Tusikubali kuwa watazamaji

*Godlove Mwakibete Atembelea Makao Makuu ya CCM Mbeya*Leo, Godlove Mwakibete ametembelea Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Mbey...
06/08/2025

*Godlove Mwakibete Atembelea Makao Makuu ya CCM Mbeya*

Leo, Godlove Mwakibete ametembelea Makao Makuu ya CCM Mkoa wa Mbeya na kufanya mazungumzo na Katibu wa CCM wa Mkoa huo, wakijadili masuala mbalimbali ya kuimarisha chama, ikiwemo ulinzi na usimamizi wa Katiba na Kanuni za CCM. Katika mazungumzo hayo, Katibu alimpongeza Mwakibete kwa busara na hekima alizozionesha kwa kuungana na wale waliopata ushindi kwenye uchaguzi wa ndani ya chama, hatua inayoonesha ukomavu wa kisiasa na uzalendo kwa Chama Cha Mapinduzi.

Chief Godlove Mwakibete amekuwa mstari wa mbele katika kusaidia jamii, hususan watu wasiokuwa na uwezo kwa kuwapatia huduma mbalimbali k**a vile kusaidia shule, zahanati na shughuli nyingine za maendeleo. Mchango wake katika jamii umekuwa ukitambuliwa na kuheshimiwa na watu wa rika zote, hali inayodhihirisha moyo wake wa kujitoa kwa ajili ya maendeleo ya watu.

Licha ya jina lake kutokurudi katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM, Mwakibete alionesha ukomavu wa hali ya juu kwa kuahidi kushiriki kikamilifu katika kampeni za mgombea yeyote atakayepitishwa na chama, jambo linaloonesha uzalendo wa kweli na nia ya dhati ya kuona CCM inaendelea kushinda kwa kishindo.

01/08/2025

Mhe. Kasaka, aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Lupa, akiomba kura katika Kata ya Nkung’ungu, aliwahimiza wananchi wamrejeshe tena kwa kuwa anayo nia, uwezo na uzoefu wa kuendelea kusukuma mbele gurudumu la maendeleo, akiwakumbusha kuwa utumishi wake uliopita umeacha alama za kweli za maendeleo katika sekta za barabara, elimu na afya.

🕊️“ *UCHAGUZI NI DARASA LA AMANI, SI UWANJA WA VITA”*🕊️* ✍️ Imeandikwa na: Sibonike Nm📞 +255 766 830 011📧 mwajilalasibon...
30/07/2025

🕊️“ *UCHAGUZI NI DARASA LA AMANI, SI UWANJA WA VITA”*🕊️*

✍️ Imeandikwa na: Sibonike Nm
📞 +255 766 830 011
📧 [email protected]

🌅 Ninapochomoza alfajiri na kuona nuru ya Tanzania, moyo wangu huimba wimbo wa matumaini.
🌍 Tanzania ni ziwa la utulivu, mito ya mshik**ano, na mlima wa amani – tusiiharibu kwa maneno ya chuki wala mikono ya fitina.

🗳️ Uchaguzi si vita – ni sherehe ya demokrasia; si mpasuko – bali ni daraja la maamuzi;
Tofauti zetu ni k**a rangi za upinde wa mvua – zikikutana hutoa uzuri wa taifa letu.

🕊️ Tukemee matusi, tukatae vurugu; tupande mbegu ya heshima na tuvune maelewano.
Kwa sababu uchaguzi hupita, lakini jirani hubaki; chama hubadilika, lakini Tanzania hubaki daima.

🇹🇿 Tuwe walinzi wa amani – si kwa bunduki, bali kwa busara; si kwa silaha, bali kwa sauti ya maridhiano.
Kwa pamoja, tuchague kwa hekima, tupingane kwa hoja, na tuendelee kwa mshik**ano.

"Amani ni urithi wa mababu, tusiiuze kwa kelele za kisiasa."
"Uchaguzi ni k**a jua – kila mtu hulipata joto lake, tusizime taa ya umoja."
"Tanzania kwanza, mengine baadaye."

📌SEHEMU YA KWANZA 🔰Taarifa ya Wagombea walioteluliwa kugombea Ubunge ndani ya Chama Cha Mapinduzi.
29/07/2025

📌SEHEMU YA KWANZA

🔰Taarifa ya Wagombea walioteluliwa kugombea Ubunge ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

27/07/2025

Magali matano yahusika kwenye Ajali Moja Mbeya, mmoja amefariki papo hapo na wengine kujeruhiwa katika ajali ya gari lililofeli breki kugonga zaidi ya magari manne katika mteremko wa Nzovwe jijini Mbeya.Akizungumza baada ya kufanya uokozi eneo la Ajali Mrakibu wa Zimamoto na Uokoaji Gervas Fungamali Afisa Operesheni wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mbeya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo huku baadhi ya mashuhuda na manusura wa ajali hiyo wakielezea hali ilivyokuwa.

26/07/2025

MTIA NIA UBUNGE SONGWE ADAIWA KUTOA FEDHA KWA WAJUMBE WA CCM
Na Mwandishi Wetu, Songwe – Julai 25, 2025

Katika Kata ya Kapalala, Jimbo la Songwe, mtia nia wa nafasi ya Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Romwadi Mwang’amba Mwashuya, anadaiwa kuwagawia fedha baadhi ya wajumbe wa chama hicho ili kujipatia kura katika uchaguzi wa maoni unaotarajiwa kufanyika Julai 4, 2025.

Tukio hilo linadaiwa kutokea huku Chama Cha Mapinduzi kikiwa tayari kimetoa miongozo mahsusi kwa watia nia wote kusubiri mchakato rasmi wa uteuzi wa majina kabla ya hatua ya kupigiwa kura za maoni kuanza. Vitendo vya kugawa fedha vinaweza kufasiriwa k**a ukiukwaji wa maadili na kanuni za chama hicho tawala.

Wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema matendo ya aina hiyo yanadhoofisha misingi ya haki, usawa, na demokrasia ndani ya chama, na huweza kuchochea migogoro ya baada ya uchaguzi.

Hadi sasa, hakuna taarifa rasmi kutoka kwa uongozi wa CCM ngazi ya wilaya au mkoa juu ya tuhuma hizi, ingawa baadhi ya wanachama wameeleza kusikitishwa na kile walichokiita “mianya ya rushwa inayojificha k**a msaada.”

Chama cha Mapinduzi kimekuwa kikisisitiza nidhamu, uadilifu na kufuata taratibu katika mchakato mzima wa uchaguzi wa ndani, na mara kadhaa kimechukua hatua kali kwa wale wanaobainika kuvunja miongozo.

Tunaendelea kuwatafuta viongozi wa CCM ngazi ya wilaya pamoja na Ndugu Romwadi Mwang’amba Mwashuya ili kupata undani wa taarifa hizi na kujua msimamo wao kuhusu tuhuma zinazotajwa.

> "Kura Yangu, Hatima Yangu"Nchi ni k**a shamba — kila mpiga kura ni mkulima,Usipolima kwa hekima, huvuni maendeleo bali...
25/07/2025

> "Kura Yangu, Hatima Yangu"

Nchi ni k**a shamba — kila mpiga kura ni mkulima,
Usipolima kwa hekima, huvuni maendeleo bali majuto.

Leo tukawavue barakoa wagombea wa ahadi hewa,
Si kila anayecheka ni rafiki, si kila msemaji ni kiongozi!

Chagua kiongozi kwa hoja, si kwa hongo,
Kwa kazi, si kwa kahawa,
Kwa utu, si kwa ukabila.

Vijana — amkeni, kura si selfie, ni silaha!
Akina mama — msikubali vitenge mkasahau vijiji vyenu.
Wazee — kumbukeni miaka si sabuni ya kusafisha uongo.

Tanzania ni yetu — tusikubali kupigwa dana dana!
Tuchague kwa akili, si kwa mihemko.

2025 — Tunapiga kura kwa Maendeleo, Amani, na Ukombozi wa Fikira!

📝📝 na: Sibonike Nm
📞 +255766830011
✉️ [email protected]

Address

Rungwe
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Green Voice TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to The Green Voice TV:

Share