Japhet Katana

Japhet Katana Empowering Lives Through the Gospel Of Jesus Christ. Building Faith, Transforming Hearts, and Revealing God’s Unfailing Love. Kindly Welcome.
❤️

Merry Christmas my people 👏🥰
24/12/2025

Merry Christmas my people 👏🥰

ZINGATIA MAMBO HAYA MUHIMU UNAPOTEMBELEA WAHITAJI:1. Fanya utafiti kujua mahitaji yao kabla ya kuwaendea.2. Tatua matati...
20/12/2025

ZINGATIA MAMBO HAYA MUHIMU UNAPOTEMBELEA WAHITAJI:
1. Fanya utafiti kujua mahitaji yao kabla ya kuwaendea.
2. Tatua matatizo yao ya muda mrefu hata kwa sehemu ukiwa na uwezo.
3. Acha keshi kidogo kwaajili ya mahitaji ya wahudumu wa kituo.

4. Si lazima upeleke vitu wakati mwingine wanahitaji msaada wa nguvu kazi wasaidie au wape ujuzi au kipawa chako
5. Sema nao neno la faraja na kuwatia moyo

Ukihitaji msaada wa kufahamu baadhi ya vituo ambavyo tumevifikia kwa matendo ya upendo au unataka kuwa unashiriki nasi tuwasiliane kwa namba zangu hapa chini.

Mawasiliano zaidi:
+255745746691
Japhet Katana

➡️ANAYEWASIKILIZA WATU NA KUTATUA MATAIZO YAO HUGEUKA KIONGOZI WAO.Mpendwa wangu katika jambo muhimu sana ambalo ningepe...
11/12/2025

➡️ANAYEWASIKILIZA WATU NA KUTATUA MATAIZO YAO HUGEUKA KIONGOZI WAO.

Mpendwa wangu katika jambo muhimu sana ambalo ningependa ufahamu ni kwamba, kuwasikiliza watu na kuwasaidia kutatua matatizo au kero zao ni kuwa kiongozi wao.

K**a akiwepo mtu anadhania kuwa kiongozi ni cheo amechelewa sana. Unaweza kuwa na madaraka na mamlaka lakini wewe si kiongozi. Uongozi ni ushawishi watu wasiposhawishika mioyo yao kukufuata huwezi kuwa kiongozi wao. Hatak**a utakaa katika cheo na ukawa na madaraka na ulinzi mkubwa. Nataka kukuonyesha jambo hili pia katika Neno la Mungu.

Alikuwepo mfalme Daudi mtu hodari, imara na zaidi ya hayo alikuwa amechaguliwa na Mungu kuwaongoza watu wake. Alikuwa na kijana wake aliyeitwa Absalomu huyu kijana alikuwa na kisasi na mwenzake aitwaye Amnoni ambaye walikuwa baba mmoja mama mbalimbali yaani kimahusiano Hawa walichangia baba. Ikatokea siku Huyu Amnoni akampenda Tamari mdogo wake na Absalomu ambaye ikafikia wakati akambaka.

Jambo hili lilimuumiza sana Absalomu kaka yake na Tamari, Baba yao mfalme aliposikia jambo hili hakulishughulikia kwa vyovyote. Kisasi kikakua ndani ya Absalomu kuna siku aliandaa karamu au sherehe watu wakaenda kusherekea na akamtaka Amnoni alewe sana Kisha akawaambia vijana wake mtoeni nje mkamwue.

Kweli Amnoni alipigwa na kitu kizito kichwani Pwaa..na akafa.

Baada ya jambo hilo Absalomu akakimbilia inchi ya mbali kumwepuka babaye mfalme Daudi. Baada ya muda mrefu kupita miaka mitatu kijana Absalom alikaa uhamishoni akataka kurudi kwa babaye. aliporudi babaye akawa hataki hata kuonana naye uso kwa uso.

Siku zikaenda kijana Absalomu alijua nguvu ya kusikiliza watu na kuwasaidia kutatua changanoto zao. Alinza kwenda langoni mwa mji kuingilia lango la kwenda kwa mfalme akawa akisikiliza matatizo ya watu hapo na kuwasaidia kutatua shida zao. Akawa akiwaambia kuwa wasingeweza kumuona mfalme heri shida zao awasaidie kuzitatua.

Hii ilipoendelea kwa muda wa miaka kadha Absalomu akawa na ushawishi mkubwa katika nchi yao. Akapanga njama za kumpindua mfalme Daudi babaye. Watu wengi wakamwamini na wakawa upande wake.

Kumbuka kilichompa ushawishi katika mioyo ya watu Absalomu ni kuwasikiliza watu na kuwapa au kuwasaidia kupata masuluhisho ya changamoto zao.

Soma kisa hiki na tafakari, kipo katika 2Samweli 10-15

2Samweli 15:2-
2. Tena Absalomu huondoka asubuhi na mapema, na kusimama kando ya njia ya lango; kisha ikawa, mtu ye yote aliyekuwa na neno, lililokuwa halina budi kufika kwa mfalme ili kuhukumiwa, Absalomu humwita mtu huyo kwake, na kumwuliza, Wewe u mtu wa mji gani? Naye akasema, Mtumwa wako ni mtu wa kabila fulani ya Israeli.

3. Naye Absalomu humwambia, Tazama, maneno yako ni mema yenye haki; lakini hapana mtu aliyeagizwa na mfalme kukusikiliza.

4. Tena Absalomu husema, Laiti mimi ningewekwa kuwa mwamuzi katika nchi hii, ili kila mtu mwenye neno au daawa aje kwangu, nimpatie haki yake!

5. Tena ikawa hapo alipokaribia mtu ye yote kumsujudia, hunyosha mkono wake, na kumshika, na kumbusu.

Unaona namna huyu ndugu alipata ushawishi juu ya watu kwa kuwajali, kuwasikiliza na kujaribu kutatua changamoto zao kwa kuwaonyesha upendo mkubwa.

Kuwasikiliza watu matakwa Yao kwa upendo na kuwasaidia kutatua matatizo yao huo ndiyo uongozi. Hata ukikalia kitu

Nilikuwa nasoma nikitafakari..
Ni ndugu Yako Japhet Katana, unaweza kufollow ukurasa wangu kwa mafundisho mbalimbali ya kujenga roho yako.
+255745746691
Japhet Katana
🇹🇿🇲🇼🇷🇼🇺🇬🇰🇪🇿🇲🇿🇦🇧🇮🇳🇦🇲🇿🇨🇩🇺🇸🥰

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Stan Bakola, Moshi Thomas Ally, Claud Mgaya, G*y Mollely,...
10/12/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Stan Bakola, Moshi Thomas Ally, Claud Mgaya, G*y Mollely, Mwajuma Ramadhani, Salome Longinus, Aisha Nudini, Vaileth Dickson, Mohamedi Ramadhani, Luliathy Hassan, Kassim Kiliani Mbowela, Huruma Haule

02/12/2025

LEO NAULIZA SWALI MOJA TU..
"K**A KWELI UNAMPENDA MUNGU HUWA UNAFANYA NINI KUTHIBITISHA HILO?"
👇👇

UNAUJUA MUUJIZA MKUBWA KULIKO YOTE?Rafiki yangu unaujua muujiza mkubwa kuliko yote? Unajua kuwa huu mujiza thamani yake ...
28/11/2025

UNAUJUA MUUJIZA MKUBWA KULIKO YOTE?

Rafiki yangu unaujua muujiza mkubwa kuliko yote?

Unajua kuwa huu mujiza thamani yake ni kubwa kuliko miujiza mingine yote ambayo ungeweza kuipokea?

Najua unatafakari najaribu kuona ukiwaza k**a rafiki yangu mmoja, ngoja nikupe kidogo tafakari yetu ilivyokuwa. Nilipozungumza naye kuhusu habari hii, kwanza aliguna na kukunja ndita usoni akiashiria mshtuko. Alaafu akajibu najua nikaanza kuhojiana naye..

Rafiki: muujiza huu mkubwa kuliko yote itakuwa ni kiwete kutembea au sio.

Mimi: Hapana labda fikiria tena..

Rafiki: Basi ni bubu kusema..

Mimi: Bado huu si muujiza mkubwa. Jaribu kufikiri zaidi..

Rafiki: oooh okay Kiziwi kusikia

Mimi: Hapana bado hautoshi kuwa muujiza mkubwa kuzidi yote. Fikiri zaidi..

Rafiki: basi aliyekufa kufufuliwa hapa nimekuweza waoooh kufufuliwa nasema..

Mimi: Bado huo sio muujiza mkubwa kuzidi yote?

Rafiki: Ninini basi? Naomba niambie...

Mimi: Ongeza kufikiri zaidi kidogo unakaribia kupata jibu...

Rafiki: Au ni ule Yesu kuwalisha watu 5000 kwa mikate mitano na samaki wawili.

Mimi: Hapana huu si muujiza mkubwa kuzidi yote.

Rafiki: Ooh basi Yesu kutembea juu ya maji na na kutuliza dhoruba ...

Mimi: Hapana bado huu si muujiza mkubwa kuzidi yote.

Rafiki: Ooh sawa basi naomba niambie namimi niujue..

Mimi: Sawa..

✍️ SASA NISIKILIZE KWA MAKINI NIKUAMBIE NI MUUJIZA UPI MKUBWA KUZIDI YOTE.

Kwanza kabisa kwanini nimesema kufufuliwa kutoka kwa wafu sio muujiza mkubwa kuzidi yote kwa kuwa hata aliowafufua Bwana Yesu bado walikufa tena. Mfano Lazaro.

Aliowaponya bado baada ya miaka mingi walikufa tena. Mfano mwanamke aliyetokwa na damu.

Wenye njaa waliopewa chakula bado kesho yake walihisi njaa na kuendelea kumfuata awape tena mkate.

Yesu kutuliza dhoruba ilitulia lakini mpaka leo bado kuna dhoruba baharini.

✍️SASA MUUJIZA MKUBWA NI HUU HAPA...

Warumi 10:9-10
9. Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
(That if thou shalt confess with thy mouth the Lord Jesus, and shalt believe in thine heart that God hath raised him from the dead, thou shalt be saved.)

10. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.
(For with the heart man believeth unto righteousness; and with the mouth confession is made unto salvation.)

✍️Muujiza huu unaitwa WOKOVU. yaani mpango wa Mungu kumtafuta mwanadamu aliyepotea katika dhambi(uasi) na kumpa tena mamlaka na kumrejesha katika hali yake ya mwanzo ya kuumbwa kwake yaani kumiliki na kutawala katika huu ulimwengu na zaidi ya hapo ni kumpa na uzima wa milele.

Kumbuka kwa kuamini moyoni mwako na kukiri kwa kinywa chako kuwa Yesu kristo ni Bwana, alikuja kukuokoa unaokolewa. Na jambo hili ni jambo la furaha mbinguni kuliko kiziwi akisikia, kiwete akitembea au kipofu kuona.

Tuone..
Luka 15:7 Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu.
(I say unto you, that likewise joy shall be in heaven over one sinner that repenteth, more than over ninety and nine just persons, which need no repentance.)

Kumbe aliyekuwa amepotelea dhambini akiamini akarejea kuamini mbinguni kuna furaha sana. K**a bado hujaamini nakukaribisha pokea muujiza huu mkubwa zifurahishe mbigu.

Kumbuka maneno ya Bwana Yesu kuwa yeyote atakayekunywa maji anayompa yeye hataona kiu tena.
Yohana 4:13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
(Jesus answered and said unto her, Whosoever drinketh of this water shall thirst again:) sehemunya mazungumzo ya Yesu na mwanamke msamalia..

Ukiamini ukampokea Yesu leo utumwa wa dhambi utaondoka, yaani KIU ya kufanya dhambi inayokutesa itaondoka utakuwa huru huru kweli kweli. Yohana 8:32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
(And ye shall know the truth, and the truth shall make you free.)

Mpendwa wangu dhambi huwezi kuishinda kwa kujitahidi pekee, unahitaji kuiamini injili Roho wa Mungu atakaa ndani yako na utaanza kuongozwa naye na itaanza kuwa rahisi sana kwako kushinda dhambi. Na kuishi vile Mungu atakavyo k**a alivyosema katika neno lake.

Ukiokolewa leo ndiyo bima au salama ya maisha yako hapa duniani na baada ya kuondoka duniani.

Rafiki yangu je, huu sio muujiza mkubwa kuliko yote?

Nakualika kumpokea Yesu Leo upokee muujiza huu mkubwa kuzidi yote. 👇

Fuatisha sala hii kwa sauti:
Sema,
BWANA YESU, NIMEKUJA KWAKO MIMI NI MWENYE DHAMBI. NINATUBU LEO DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAFISHE KWA DAMU YAKO YA THAMANI. NIPOKEE KATIKA UFALME WAKO NA JINA LANGU LIANDIKWE KWENYE KITABU CHA UZIMA. BWANA YESU NINAOMBA UNIJAZE NA ROHO WAKO MTAKATIFU NA UNIONGOZE SIKU ZOTE ZA MAISHA YANGU. NIMEOKOKA LEO
AMEN.

Hongera sana sasa umeokoka na umepokea MUUJIZA MKUBWA HUU.👏👏👏
Karibu kwenye familia ya waamini.

K**a umefuatisha sala hii, tuwasiliane nitakupa msaada zaidi wa mafundisho na kitabu cha kukusaidia kukua kiroho.

TUWASILIANE KWA NAMBA HIZI, UKIWEZA WHATSAPP ITAPENDEZA ZAIDI +255745746691

Follow ukurasa wetu huu kwa mafundisho zaidi: Japhet Katana FOLLOW

EV. KATANA JAPHET
UBARIKIWE SANA
🇹🇿🇲🇿🇰🇪🇿🇲🇳🇦🇿🇦🇷🇼🇧🇮🇺🇲🇺🇬🇨🇩🇲🇼❤️

SI JAMAA ALISEMA ANA DAMU YA KUNGURU‼️Katika moja ya simu nilipokea jana kwa bashasha na hamu kubwa kutaka kusikia yaliy...
19/11/2025

SI JAMAA ALISEMA ANA DAMU YA KUNGURU‼️

Katika moja ya simu nilipokea jana kwa bashasha na hamu kubwa kutaka kusikia yaliyojili ni hii, maana aliyepiga simu hii ni rafiki yangu sana..

Baada ya salamu kwa sekunde chache akaanza kunipa kisa kizima, si unamkumbuka yule jamaa kicheche alikuwa akiruka na mabinti lukuki? Mimi nikawa nauliza yupi huyo tena? anajibu yaani namaanisha yule jamaa kila unapokutana naye ni stori za mademu mara yule binti kisu mkali wa mtaa, Mimi nishatoka naye. Huku usoni anajawa na tabasamu kubwa akitaka kuonyesha k**a anafaiidi kwa matendo yake hayo na kuonyesha k**a ni mwanaume kweli kweli. Huku ukijaribu kumwonya juu ya mwenendo wake huo anawahi kusema "kumbe hujui mimi nina damu ya kunguru" Sasa Mimi nakupata si ungesema tuu yule Damu ya kunguru.. lakini yule tumemwonya mara nyingi sana lakini amekuwa sikio la kufa zaidi anatia pamba masikioni. unakumbuka mara ya mwisho tumemwambia damu yake hiyo iko siku itakuwa k**a ya kunguni? yes nakumbuka..

Mimi binafsi nikapata shauku ya kujua hiyo damu ya Kunguru ni damu ya jinsi gani? baada ya kuumiza kichwa na kuuliza watu wa mtaani ndipo nikajua kumbe anaposema ana damu ya Kunguru inamaana ana damu ya group "O" damu ya aina hii inaaminika ni ngumu kuchukua vimelea vya magonjwa au kuambukizwa magonjwa. pamoja na hayo bado tukawa tunamshauri kuwa unaweza usipate magonjwa kwa sababu ya damu yako k**a unavyosema, Kwa kebehi anaongezea kuwa anatumia mipira. Tunapokaza kumuuliza na dhambi je, unakinga na nini isikupate kwa matendo hayo machafu? maana ni amri ya Mungu kuwa Usizini.

Majibu yake ya mizaha na kusema haamini k**a inawezekana mtu kuishi hivi hivi. anazo sababu lukuki za wanasayansi anaaamini hawezi kuwa vizuri k**a hashiriki katika mambo yahusianayo na ngono. Anasingizia mara ooh sisi vijana damu zinachemka mara kufanya hivi nabadili oili, tunamwambia wewe si gari mpaka ubadili hizo oili lakini amekuwa akikaza shingo yake. Akisema nitaokoka lakini si sasa nitaokoka uzeeni sasa nile ujana kwanza. Tunaendelea kumpa majibu ya hoja ili abadilike, kuwa kwani wangapi vijana wameondoka hata bila kuzeeka wengine kiumri wadogo kuliko wewe unapaswa kubadilika sasa uokoke na umpokee Bwana Yesu awe Bwana na mwokozi wa maisha yako binafsi utashinda tamaa na kutumikishwa na dhambi nawe uwe huru k**a sisi. Anatamani lakini anatafakari kwa muda akiwa ameinamisha kichwa chini. Anasema lakini kweli mnachosema lakini nawaza naona k**a mimi sitaweza.. tunamwambia mwenyewe huwezi lakini ukiamini unapokea nguvu ya Roho Mtakatifu inakusaidia kuweza mwili wako na kuishinda dhambi inatusaidia wenzio pia. anawaza anasema nitaamua na mimi siku Moja..

Basi sasa juzi bwana eeh! si kaumwa ugonjwa ambao umemfanya kukiri na kuelewa yote tuliyokuwa tunamweleza ili abadilike. kuwa unayofanya huko sirini siku moja yatakuwa peupe. Si jamaa alikuwa anasema ana damu ya kunguru! Sasa yalipomfika ya mchozi na haja ndogo zikawa zinakwenda pamoja huku moyoni amejaa majuto na simanzi pesa zake zote katumia katika uzinzi kuharibu mabinti amekuwa kero hata wazazi mtaani kila akipita mtaani ananyooshewa vidole, akitazama hakuna alichopata zaidi ya aibu anayoendelea kuivuna kila kukicha. Ama kweli mwisho wa ubaya aibu.

Maana tulikuwa tunamwambia mara zote ndugu macho ya mwanadamu hayashibi pia wazuri wapo na wataendelea kuzaliwa je, utawamaliza wote mwenyewe? zaidi tukawa tunamwambia unachofanya ni mbegu utakuja kuvuna yaani unachotenda utatendewa pia. je, utafurahia kuvuna mbegu hii uipandayo? anakinja sura mithili ya kutafuna ndimu anasema kusema ule ukweli sitamani. Kawakatisha masomo mabinti wengi na anawatoto kila mtaa na hawatunzi anajisemea Kwa unyonge na sauti dhoofu isiyosikika vizuri kutoka kitandani pake, "nitakufa kwa majuto makubwa nimefanya mengi maovu, hata sijui sura yangu nitaiweka wapi mbele za muumba wangu.." anaongea maneno haha Kwa uchungu huku yakisindikizwa na machozi yanatiririka mpaka kidevuni.

Tunamwambia tena kila unapopata nafasi ya kuwa hai inamaana unayo nafasi yakutengeza njia yako na kuonyeka pia. Unaweza kutubu na hakika Mungu akakurehemu na kukufutia maovu yako hata akakuponya lakini, usiendelee na uovu uliokuwa ukitenda tubu kumaanisha kuziacha (Mithali 28:13,1Yohana1:9) Lakini ndugu kumbuka katika nafasi hii uliyonayo kuwa Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo shingo yake itavunjika ghafla wala hapati dawa.(Mithali 29:1)

Basi mwishoni tukaomba naye na kumwongoza Sala ya Toba akawa amempokea Yesu. Akawa amepata amaani moyoni na uhakika was maisha take ya Sasa hata baada ya kufa. Na tulimalizia kumwambia kuwa sasa amekuwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya ya kale yamepita tazama yamekuwa mapya. Tukamsisitiza asijihukumu binafsi na dhamiri yake akumbuke kuwa ameuvua utu was kale, Sasa akazane kusoma Neno la Mungu kuomba, ibada za binafsi na kujumuika na wengine hakika mengi tutazidi kumfundisha.

Imani yangu kuna jambo umejifunza ...

Nakutakia tafakari njema ni mimi ndugu yako nikupendaye sana, Ev. Katana Japhet. usiache kutembelea na kufollow ukurasa wetu Facebook Gospel Stewards Family - GSF uzidi kujifunza zaidi kila siku. pia Subscribe kwenye channel yetu YouTube GOSPEL STEWARDS TV pia huko kuna video nyingi 400+ za Mafundisho.

mawasiliano Zaidi nawe ukitaka kutengeneza njia yako:
©️+255745746691
Ev. Katana Japhet.🇹🇿
Hakuna Raha wala furaha na amani katika kutenda dhambi, jua kabusa ukiendelea kuilea dhambi itakuangamiza hatak**a ni sirini Bora ukajiweka wazi usaidiwe. Tunasema Dhambi inaanza na tamaa, inakomaa kuwa dhambi na mwishowe ni mauti. hero umesikia ujbe huu ni sauti ya Mungu inakuita utubu. ubarikiwe kuitikia wito. usikubali kuendeleaa kuwa mtumwa wa dhambi wakati msaada upo na unaweza kuishi maisha matakatifu.

.

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Costa Aba, Daviess Ke Busera, Sikha Mondal, Saimon Mtoto ...
19/11/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Costa Aba, Daviess Ke Busera, Sikha Mondal, Saimon Mtoto Wa Mungu, Anipha Frank, Martin Shakur, Tonny Mtiaa

14/11/2025

K**a unaamini katika kulindwa na Mungu hata uko hai leo, Basi SEMA Neno la shukrani kwa Mungu wako ✍️

Men Camp is around the corner kindly welcome
14/11/2025

Men Camp is around the corner kindly welcome

SEMINA: *NAMNA YA KUPOKEA MSAADA WA KIUNGU (HOW TO ACCESS DIVINE HELP)*KUTOKA: FAMILIA YA MAWAKILI WA INJILI (GOSPEL STE...
14/11/2025

SEMINA: *NAMNA YA KUPOKEA MSAADA WA KIUNGU (HOW TO ACCESS DIVINE HELP)*

KUTOKA: FAMILIA YA MAWAKILI WA INJILI (GOSPEL STEWARDS FAMILY -GSF)



MKUFUNZI: JAPHET KATANA

KARIBU DARASANI

Tuombe
Bwana Yesu mwema Asante kwa fursa hii ya uzima. Ninakutukuza kwa wema wako Asante kwa sababu unatufundisha ili tupate faida.
Ninaomba useme nasi katika majira haya tena.

Amen

Mpendwa wangu tulianza kujufunza kuhusu namna ya kupokea msaada wa kiungu katika siku kadhaa zilizotangulia, tumejifunza kuhusu Roho mtakatifu, ulinzi wa kiungu.
Nataka tusonge mbele tutazame jambo la tatu leo.

3. KIBALI CHA KIUNGU (DIVINE FAVOR)

Hii ni namna nyingine ambayo mwamini anapokea msaada wa Kiungu ni kupitia kibali cha kiungu.

Sasa unaweza kuwa unataka kujua kibali ni nini nataka tuanze na tafsiri nyepesi kabisa ya kawaida. Tunaposema kibali inamaana kitu kinachokufanya uruhusiwe kufanya jambo fulani katika eneo fulani. K**a unataka kusafiri nje ya nchi kwanza unapaswa kuwa na kitambulisho (passport) pia Visa kwa baadhi ya nchi huwezi kuingia bila visa. Hiki ni kibali cha kukufanya ukaruhusiwa kuingia katika nchi yao na kufanya shughuli zako kwa muda fulani.

Tukizungumzia katika usafiri kibali chako ni tiketi yako.

Mpendwa wangu sasa ninaposema kibali cha kiungu maana yake unapokea kukubalika kusikotokana na sababu au vigezo vya kawaida.

Usidhanie kila mtu anapata kazi sababu tu ya vyeti vyake bali sababu ya kibali pia.

Kuna watu akizungumza na mtu au akionwa tuu watu wanaanza kumtaka awe kiongozi wao hiki ni kibali, mara nyingi kinatokana na ukiroho.

K**a mtu hajui kanuni za ukiroho basi kibali chake kinaweza kupotezwa au kuibiwa, au kikaharibiwa na tabia zako mbaya.

Kumbuka kazi ya kibali ni kukufungulia milango ya fursa lakini tabia zako ndizo zitazifanya fursa hizo kukaa au kupotea.

Tusome andiko hili pamoja..

Zaburi 5:12
Kwa maana Wewe utambariki mwenye haki; Bwana, utamzungushia radhi k**a ngao.
(For thou, LORD, wilt bless the righteous; with favour wilt thou compass him as with a shield.)

Kiswahili neno lililotafsiriwa k**a radhi kingereza kinalitafsiri k**a kibali.

Unaona ukizungushiwa kibali k**a ngao ni wazi Kila mlango utakaokuwa unausogelea basi utakuwa unakufungukia.

Kibali cha Bwana ndicho humfanya mtu kukubalika kila anapokwenda ukifuatilia maisha ya Yusufu ndipo utaona hili kuhusu kibali likiwa halisi sana kila alipokuwa anakwenda anapata nafasi ya kuaminiwa na kuwa bora.

Mwanzo 39:3-6
3. Bwana wake akaona ya kwamba Bwana yu pamoja naye, na ya kuwa Bwana anafanikisha mambo yote mkononi mwake.

4. Yusufu akaona neema machoni pake, akamtumikia. Naye akamweka awe msimamizi juu ya nyumba yake, na yote yaliyomo akayaweka mkononi mwake.

5. Ikawa tokea wakati alipomweka awe msimamizi juu ya nyumba yake, na vyote vilivyomo, Bwana akabariki nyumba ya yule Mmisri kwa ajili ya Yusufu. Mbaraka wa Bwana ukawa juu ya vyote alivyokuwa navyo katika nyumba, na katika shamba.
6. Akayaacha yote aliyokuwa nayo mkononi mwa Yusufu; wala hakujua habari za kitu cho chote chake, ila hicho chakula alichokula tu.

Hiki ndicho kibali cha Mungu watu wanajiona salama wakifanya kazi nawewe.

Unaaaminika, watu wanaona mafanikio katika mambo unayoyasimamia.

Hakika Mungu akikuachilia kibali mambo ambayo wengine wanatumia nguvu nyingi na hata wasipate wewe yanakufuata yenyewe.

Kibali cha Bwana kinaweza kukufanya watu kukupa zawadi, tuzo, pongezi, fedha n.k

Natamani kila siku liwe kati ya maombi yako, kuombea kibali kwanza katika uso na mwili wako ili watu wakuonapo wapate kukukubali pasipo sababu, pili kibali katika jina lako. Ili linapotajwa liwe jina jema kwa kila anayelisikia.

Ukikosa kibali maisha yanakuwa magumu, inamaana unakuwa na roho ya Kaini u akataliwa kila unapojaribu kusogea unakataliwa.

Mpendwa wangu Yesu mwenyewe alikuwa na kibali ndio maana alimpendeza Mungu pamoja na wanadamu.

Luka 2:52
Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.
(And Jesus increased in wisdom and stature, and in favour with God and man.)

Namimi ni ombi langu kwa Mungu miaka yangu inapoongezeka yaani umri unapoongezeka hakika na kibali cha Bwana juu yangu kiongezeke.

Sijui wewe shauku yako ni ipi..

Mwanzo 39:21
Lakini Bwana akawa pamoja na Yusufu, akamfadhili, akampa kibali machoni pa mkuu wa gereza.
(But the LORD was with Joseph, and shewed him mercy, and gave him favour in the sight of the keeper of the prison.)

Unaona jambo moja kujua umepokea fadhili za Kiungu ni kupata kibali.

Kabla sijafikia mwisho yako mengi ningesema nawe kuhusu kibali.

Lakini kibali chanzo chake ni Mungu mwenyewe hivyo usiache kuomba kibali ili Mungu akufadhili nacho.

Japo la pili kibali huja kwa kutenda vyema au kutenda vema.
Mwanzo 4:7
K**a ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.

Mpendwa wangu yako mengi ningeweza kusema nawe lakini naomba kwa leo nikomee hapa.

Shauku yangu ujue kwamba unaweza kupokea msaada wa kiungu kupitia kibali.

Nakutakia tafakari njema, ni Mimi ndugu yako nikupendaye sana. Japhet Katana.

Unaweza kufuatilia semina hii moja Kwa moja kupitia WhatsApp group yetu Mawakili wa Injili, tuma jina lako na mahali ubapatikana kuja WhatsApp namba +255745746691

Barikiwa sana
🇹🇿🇰🇪🇲🇼🇲🇿🇺🇸🇺🇬🇨🇩🇳🇦🇷🇼❤️

Kwako first yearKaribu darasaniMafunzo kujiandaa na chuo+255752352116Tuna jina lako na chuo chako WhatsApp kujiunga na s...
13/11/2025

Kwako first year
Karibu darasani

Mafunzo kujiandaa na chuo
+255752352116
Tuna jina lako na chuo chako WhatsApp kujiunga na semina

Address

Tukuyu
Mbeya
EV.KATANAJAPHET

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Japhet Katana posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Japhet Katana:

Share