03/06/2026
Wadau wa elimu kutoka HakiElimu pamoja na Child Support wameeleza kuwa kampeni ya kufanya vipimo kwa watoto imekuwa na mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya ujifunzaji kwa watoto wenye uhitaji maalumu.
Wakizungumza kuhusu matokeo ya kampeni hiyo, wadau hao wamebainisha kuwa utambuzi wa mapema wa changamoto mbalimbali zinazowakabili watoto umesaidia kuwezesha upatikanaji wa huduma stahiki za kielimu na kijamii, hali ambayo imeongeza fursa za watoto hao kushiriki kikamilifu katika masomo.
Aidha, wamefafanua kuwa kampeni hiyo imechangia kuongeza uelewa kwa wazazi, walimu na jamii kuhusu mahitaji ya watoto wenye uhitaji maalumu, jambo lililosaidia kupunguza vikwazo vinavyoweza kuathiri maendeleo yao ya elimu.
Kwa mujibu wa wadau hao, ongezeko la ushiriki wa watoto wenye uhitaji maalumu katika shughuli za shule na kijamii ni ishara ya mafanikio ya juhudi zinazoendelea kufanyika katika kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma katika kupata haki ya elimu.
Wametoa wito kwa jamii kuendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali zinazotoa huduma kwa watoto ili kuhakikisha watoto wenye uhitaji maalumu wanapata msaada unaohitajika kwa wakati, hivyo kuwawezesha kufikia ndoto na malengo yao ya maisha.
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Maulid Surumbu, amezitaka halmashauri nchini kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalumu wanapatiwa mazingira bora na rafiki yatakayowawezesha kupata elimu yenye usawa na fursa sawa za maendeleo k**a watoto wengine. Akizungumza katika uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya ujenzi na matumizi ya vituo vya upimaji wa watoto ESRACs uliofanyika katika Shule ya Msingi Mwenge, alisema utambuzi wa mapema wa changamoto kwa watoto ni hatua muhimu katika kujenga msingi imara wa elimu, kukuza vipaji na kuhakikisha watoto hao wanapata huduma stahiki zitakazowasaidia kufikia ndoto zao.