Knews24

Knews24 We’re impartial and independent, and every day we create distinctive, world-class programmes and content which inform millions of people.

JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya limesema hivi karibuni wakati likiendelea na uchunguzi wa tukio la kuvamiwa na kujeruhiwa ...
10/05/2025

JESHI la Polisi Mkoa wa Mbeya limesema hivi karibuni wakati likiendelea na uchunguzi wa tukio la kuvamiwa na kujeruhiwa kwa Mfuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mpaluka Said Nyagali maarufu Mdude na watu wasiofahamika na kisha kutoweka naye kusikojulikana, wamejitokeza baadhi ya watu na viongozi wa CHADEMA na kutoa matamko mbalimbali ikiwemo kutaja baadhi ya majina ya Askari wakiwatuhumu kuhusika na tukio hilo bila kuwasilisha ushahidi wowote.

Kupitia taarifa ya leo Mei 10, 2025 iliyotolewa na Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga Jeshi hilo limetoa onyo kali kwa mtu au kikundi chochote cha watu wenye nia ovu kutojaribu wala kuthubutu kujihusisha na uhalifu wa aina yoyote ikiwemo kudhuru Askari ama familia za Askari.

Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeeleza kuwa kabla ya mtu au kikundi cha watu kufikiria kufanya hivyo, wajionye sana na wasifikiri kufanya kitendo hicho ni rahisi kwao huku likisisitiza kuwa halitasita kumchukulia hatua za kisheria na kumshughulikia mtu au kikundi chochote cha watu watakaojaribu kufanya uhalifu kutokana na matamko au kauli hizo zinazotolewa.


Kadinali Robert Prevost ametangazwa kuwa Papa mpya.Na kuanzia leo anajulikana k**a Papa Leo XIV.-Robert Kardinali Prevos...
08/05/2025

Kadinali Robert Prevost ametangazwa kuwa Papa mpya.
Na kuanzia leo anajulikana k**a Papa Leo XIV.
-
Robert Kardinali Prevost anatokea Chicago nchini Marekani, na hadi kuchaguliwa kwake alikuwa akihudumu k**a mkuu wa Dicastery wa kanisa kwa Maaskofu
-
-

Jeshi la Polisi nchini limeanzisha uchunguzi rasmi kufuatia tuhuma nzito zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii dhidi y...
04/05/2025

Jeshi la Polisi nchini limeanzisha uchunguzi rasmi kufuatia tuhuma nzito zilizotolewa kwenye mitandao ya kijamii dhidi ya askari wake wawili wanaodaiwa kuhusika na mazingira ya kutoweka kwa mwanaharakati Mdude Nyagali.

Kwa mujibu wa taarifa za awali, mwananchi mmoja ambaye jina lake bado linafuatiliwa kwa uchunguzi, alidai kuwa askari hao walimfuata na kumtaka kushiriki kwenye shughuli za kijajusi kwa ahadi ya malipo ya kifedha. Tuhuma hizo zimezua mjadala mpana miongoni mwa wananchi na wanaharakati wa haki za binadamu, wakitaka ukweli wa suala hilo kuwekwa wazi.

Taarifa kutoka Makao Makuu ya Polisi zimeeleza kuwa, tayari kikosi kazi maalum kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kimepelekwa katika mkoa wa Mbeya, ambako sakata hilo linadaiwa kutokea, ili kufanya uchunguzi wa kina.

"Wakati uchunguzi unaendelea, tunatoa rai kwa wananchi wote wenye taarifa muhimu kuhusu tukio hili kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kusaidia kufanikisha upatikanaji wa ukweli," imesema sehemu ya taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi hilo.

Mdude Nyagali, anayefahamika kwa sauti yake ya ukosoaji dhidi ya viongozi wa serikali kupitia mitandao ya kijamii, amewahi kuripotiwa kushikiliwa na vyombo vya dola katika nyakati tofauti. Tukio hili jipya limezusha maswali kuhusu usalama wa wanaharakati nchini na nafasi ya vyombo vya dola katika kulinda haki za kikatiba.

Mpaka sasa, bado haijafahamika rasmi mahali alipo Mdude wala hali yake, jambo linaloendelea kuzua hofu na wasiwasi kwa familia yake na jamii ya watetezi wa haki za binadamu.
tanzania

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Ha...
04/05/2025

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeamua kuwekeza kwenye sekta ya madini ili kuwawezesha wachimbaji wadogo kupata kipato na kujikwamua kiuchumi.

Amesema Serikali imenunua mitambo 15 ya kisasa ya uchenjuaji ambayo itasambazwa kwenye maeneo ya wachimbaji wadogo hivyo ametoa wito kwa wachimbaji hao kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na fursa hiyo.

Ameyasema hayo leo Jumapili (Mei 04,2025) wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Chingumbwa kitongoji cha Namungo Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi.

Kadhalika Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa Afisa Madini wa mkoa kuendelea na mpango wa kubaini maeneo yenye madini yatambulike na kisha kutoa leseni kwa wachimbaji wadogo ili waweze kufanya shughuli za uchimbaji.

“Pamoja na hili tumeamua maeneo yote ya madini yaliyochukuliwa leseni na hayajaendelezwa kwa muda mrefu, tutayachukua, tutayapima upya na kuyagawa kwa wachimbaji wadogo.”

"Serikali yenu inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia imenunua ndege maalum ambayo itasaidia kufanya tafiti ya kujua aina ya madini yaliyopo na kiwango chake na sisi huku Lindi itakuja kuruka, Ruangwa na maeneo ya Nachingwea”.

Akizungumzia sekta ya barabara, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali inaendelea na mipango ya kuziboresha barabara mbalimbali katika wilaya ya Ruangwa ili kuziwezesha kupitika wakati wote na hivyo kuwafanya wakazi wa maeneo hayo kufanya shughuli mbalimbali za kiuchumi.

Naye Kaimu Meneja wa Tanesco Mkoa wa Lindi Emmanuel Sengwaji amesema kuwa Wataalam wa Idara ya Miradi mikubwa kutoka Tanesco wamefanya uhakiki wa mahitaji ya umeme katika mkoa wa Lindi kutokana na ongezeko la wawekezaji katika mkoa huo “Tuliomba tujengewe laini la gridi ya Taifa itakayotoa umeme kutoka Masasi hadi Ruangwa katika eneo la Kitandi ili umeme huo uweze kusambazwa maeneo ya uwekezaji ikiwemo kwenye migodi ya iliyopo Kitongoji cha Namungo”.


Wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi wa kupotea kwa mwanaharakati na kada wa Chadema, Mdude Nyagali, viongozi...
03/05/2025

Wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi wa kupotea kwa mwanaharakati na kada wa Chadema, Mdude Nyagali, viongozi na wafuasi wa chama hicho Mkoa wa Mbeya wameanzisha jitihada za kumtafuta katika maeneo ya porini.

Msako huo umeanza baada ya viongozi sita wa Chadema, wakiwa na wafuasi 58, kuandamana leo mchana, Jumamosi, Mei 3, 2025, hadi Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, wakitaka kupata taarifa kuhusu mambo mawili.

Mambo hayo ni kwanza, hatua zilizofikiwa katika uchunguzi wa tukio la kupotea kwa Mdude Nyagali, na pili, kufuatilia makubaliano yao ya awali ya kushirikiana na Jeshi la Polisi katika juhudi za kumtafuta.

Akizungumza na Knews24 Media LTD, kwa njia ya simu leo Jumamosi, Mei 3, 2025, Katibu wa Chadema Mkoa wa Mbeya, Hamad Mbeyale, amesema kuwa kutokana na ukimya uliokuwepo kuhusu kupotea kwa Mdude Nyagali, leo baadhi ya viongozi na wafuasi 58 wa chama hicho wamelazimika kuandamana hadi Ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya.

"Tumeenda na madai mawili. La kwanza ni kuhusu makubaliano yetu na Jeshi la Polisi tuliyofikia jana, Mei 2, 2025, ya kushirikiana katika kumtafuta k**anda wetu Mdude, hasa walipokuwa eneo la tukio. Hata hivyo, hadi leo asubuhi hakuna dalili yoyote ya ushirikiano wala harakati zozote kutoka kwa Polisi," amesema Mbeyale.

Ameongeza kuwa lengo la maandamano hayo ni kufuatilia hatima ya kupatikana kwa kada huyo, pamoja na kupata uhakika wa usalama wao binafsi katika harakati wanazoendelea nazo.

Amesemawanachama na viongozi wa majimbo wameamua kuingia maporini kwa ajili ya kumsaka Mdude Nyagali, awe hai au amekufa.


Joseph Mbilinyi, anayejulikwa zaidi kwa jina la kisanii la "Sugu", ni msanii wa muziki wa Bongo Fleva na pia mfanyakazi ...
01/05/2025

Joseph Mbilinyi, anayejulikwa zaidi kwa jina la kisanii la "Sugu", ni msanii wa muziki wa Bongo Fleva na pia mfanyakazi wa kisiasa kutoka Tanzania. Hapa ni wasifu wake kwa ufupi:

Akifaamika Kwa jina kamili: Joseph Mbilinyi ambapo jiina la kisanii ufaamika Kwa jina la Sugu, tarehe ya kuzaliwa: 01 mei 1972, Mkoani Mbeya, Tanzania

Kwa upande wa Elimu, Amemaliza elimu yake ya sekondari na pia amesomea masuala ya biashara na ujasiriamali.

Kazi na safari yake , Sugu ni msanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, maarufu kwa nyimbo zake zinazogusa masuala ya kijamii, siasa, na maisha ya vijana.

-Pia ni mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini kwa kipindi cha miaka 2006 hadi 2015, akiwa mwanasiasa na kiongozi wa Chadema (Chama cha Demokrasia na Maendeleo).

Katika siasa, amejulikana kwa msimamo wake thabiti kuhusu haki za kijamii na utawala bora.

Sifa na mchango, Sugu ni msanii maarufu sana Tanzania, akieleza hisia za vijana na jamii kwa nyimbo zake.

Amejikita pia kwenye shughuli za kijamii na siasa, akitetea haki za wananchi na maendeleo ya jamii yake.

Maisha ya binafsi, Amekuwa mstari wa mbele kuhimiza maendeleo na haki za kijamii nchini Tanzania.

Joseph Mbilinyi (Sugu) ni msanii wa muziki wa Bongo Fleva, mbunge wa zamani, na kiongozi wa kisiasa mwenye ushawishi mkubwa nchini Tanzania.


Na Linda Akyoo - Tanga.Kufuatia uwepo wa maji mengi yanayotea (Mivujo) katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Tanga,Mamlaka...
25/04/2025

Na Linda Akyoo - Tanga.

Kufuatia uwepo wa maji mengi yanayotea (Mivujo) katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Tanga,Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (TANGA UWASA) imepokea vitendea kazi kutoka Mamlaka kubwa za Maji Nchini Uholanzi (VEi) Kwa lengo la kuzuia upotevu wa maji kwenye miundombinu ya TANGA UWASA.

Akizungumza na K- NEWS 24 MEDIA, Leo tarehe 25 Aprili, 2025.Mkurugenzi Mtendaji wa TANGA UWASA Eng.Geofrey Hilly ameishukuru sana VEi kwani vifaa walivyopatiwa vita rahisisha utendaji wa kazi wa Mamlaka katika swala Zima la kuzuia Mivujo.

"Nashukuru kwa kuwa vifaa hivi vitatusaidia sana katika kuboresha utendaji wetu,kwani tutapata taarifa za mivujo mapema kupitia simu zilizogaiwa kwa watumishi na baadhi ya wadau,lakini pia kuweza kufikia mivujo Kwa wakati kwa kutumia vifaa vya usafiri". Alisema Eng.Hilly.

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi kutoka VEi Eng. Violet Kazumba emeeleza kuwa VEi imeiwezesha TANGA UWASA kupata vifaa ambavyo vinaenda moja kwa moja kusaidia udhibiti wa maji yanayo potea na kusaidia Mapato ya Mamlaka.

Mradi huu wa VEi ulianza rasmi Mwezi Julai,2024 ambapo mpaka sasa unaendea kusaidia na kupunguza upotevu wa maji kwa wakati,Ambapo Leo VEi imetoa pikipiki tano(05),guta mbili(02) simu sitini (60) na TV mbili (02) vyenye gharama ya Shilingi Milioni sitini na mbili, laki Moja na elfu hamsini (62,150,000/=)



Watu wasiojulikana wamevamia nyumbani kwa Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini na kuteketez...
22/04/2025

Watu wasiojulikana wamevamia nyumbani kwa Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini na kuteketeza gari huku, waliokuwa ndani wakinusurika kuungua moto unaodaiwa kuwashwa usiku wa kuamkia leo Aprili 22, 2025.

Gari aina ya Nissan Ex-trail yenye namba za usajili T 566 CXL mali ya Bw.Philimon Mng'ong'o katibu mwenezi wa chama cha mapinduzi wilaya ya Mbeya mjini Mkoa wa Mbeya imechomwa moto majira ya saa kumi usiku wa kuamkia leo na watu wasiojulikana.

Katibu mwenezi wa CCM wilaya ya Mbeya mjini Bw.Mng'ong'o amesema majira ya saa kumi usiku, mke wake aliamka kwa ajili ya kufanya ibada ya maombi ndipo alipoona moto na kuamsha familia nzima na walipotoka njee walikuta ndoo ikiwa na mafuta ya petrol huku gari likiendelea kuteketea kwa moto.


16/04/2025
ALIYEKUWA KATIBU WA UWT BI. LUCIA SULLE  ALIYEPIGANIA MAISHA YAKE  AKIWA CHUMBA CHA MAHUTUTI KWA MUDA WA SIKU  THELATHIN...
01/04/2025

ALIYEKUWA KATIBU WA UWT BI. LUCIA SULLE ALIYEPIGANIA MAISHA YAKE AKIWA CHUMBA CHA MAHUTUTI KWA MUDA WA SIKU THELATHINI SITA (36) TANGU WAPATE AJALI TAREHE 25 FEB,2025 KWENYE ZIARA YA MWENYEKITI WA JUMUIYA YA WAZAZI CCM TAIFA BW.FADHILI MAGANYA ,AMEPOTEZA MAISHA NA KUFIKISHA IDADI YA WATU SITA (6) WALIOPOTEZA MAISHA KATIKA AJALI HIYO WAKIWEMO WAANDISHI WA HABARI WAWILI.

KATIBU WA SIASA,ITIKADI NA UENEZI MKOA WA MBEYA BW.CHRISTOPHER UHAGHILE AMETHIBITISHA KIFO CHAKE.

mbeya

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 14, 2025 amezindua msikiti wa Masjid Jaami’u Nuuril Hikma uliopo mtaa wa Yombo, T...
14/03/2025

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 14, 2025 amezindua msikiti wa Masjid Jaami’u Nuuril Hikma uliopo mtaa wa Yombo, Temeke jijini Dar es Salaam ambao umejengwa na Taasisi ya Al-Hikma
 
Akizungumza baada ya kuzindua msikiti huo, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa jamii na Watanzania watakaotumia msikiti huo kuutunza kwani kufanya hivyo ni njia ya kudumisha uhusiano na Mwenyezi Mungu na inahesabika k**a sadaka.
 
“Mtume Muhamad S.A.W anatufundisha pia kutunza nyumba za ibada, msikiti ni sehemu ya jamii na ni mahali pa ibada na umoja. Kupitia hadithi ya Bukhari, ni wajibu wa waumini kutunza msikiti, kuhakikisha kwamba ni sehemu safi, na inakidhi mahitaji ya ibada na mafunzo ya kiislamu.”
 
Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa msikiti ni kituo cha kiroho, kijamii, kiutamaduni na nyumba kwa ajili ya ibada na unatoa nafasi kwa waumini kushirikiana katika ibada, kujifunza, na kujenga jamii bora kwa kutoa huduma za kijamii.
 
Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa viongozi wa dini kuliombea Taifa pamoja na kukemea vitendo vyote visivyo mpendeza Mwenyezi Mungu.
 
“Tunajua mnaliombea Taifa hili, ila endeleeni kufanya hivyo ili utulivu huu uendelee, tuachane na mambo yatakayoleta adha kwenye jamii, tunafurahi mnavyohubiri amani na mshik**ano, Mwenyezi Mungu analipenda Taifa hili.”

Pia Mheshimiwa Majaliwa ameipongeza Taasisi ya Al-Hikma kwa ujenzi wa msikiti huo. “Ujenzi wa Msikiti huu ni ishara ya juhudi za taasisi hii katika kuimarisha misingi ya imani na maadili mema katika jamii”.

Kwa upande wake M***i na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt Abubakar Zuber Ali Mbwana amesema kuwa maendeleo sio ugomvi bali ni kufanya mambo yanayoonekana na  yanayompendeza Mwenyezi Mungu ikiwemo ujenzi wa msikiti “fitna, ugomvi, fujo kwenye misikiti hatutaki, tupendane na heshima itawale.”




Watu 33 wamenusurika kifo na mmoja kufariki dunia katika ajali ya gari aina ya Coasta inayofanya safari zake kutoka  Ile...
11/03/2025

Watu 33 wamenusurika kifo na mmoja kufariki dunia katika ajali ya gari aina ya Coasta inayofanya safari zake kutoka Ileje kwenda Mbeya baada ya kugongana na Katapila eneo la Msinde wilayani Momba Mkoani Songwe.

Akizungumza na mwanachi leo Marchi 11,2025 Mganga mkuu wa halmashauri ya mji wa Tunduma Sebastiani Siwale amethibitisha kupokea majeruhi hao hospitalini hapo baadhi yao wakiwa wamevunjika miguu na mikono.

Siwale amesema kati ya majeruhi hao 34 ,majeruhi 10 walikuwa na hali mbaya kwani walikuwa wamevunjika miguu na mikono na kupewa rufaa ya kwenda kupatiwa matibabu hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Songwe iliyopo Vwawa.

Amesema mwanamke mmoja amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu hospitalini hapo ambapo jeshi la polisi liliuchukua mwili wa marehemu na kuuhufadhi mochwari.

"Majeruhi 14 ambao ni miongoni mwa hao 34 wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa kwani walikuwa waendelea vizuri na wengine nane leo wataruhusiwa kwani wanaendelea vizuri," amesema Siwale.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani Songwe Augustino Senga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo Machi 10,2025 majira ya saa sita Mchana ambayo imehusisha gari Toyota Costa yenye namba za usajili T 691 na katapila ambalo halina namba za usajili mali ya Mchina ambalo kwa sasa linamilikiwa na Toronto.

Kamanda Senga amesema gari hilo mali ya Bobu Mwampashi lilikuwa linaendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Juma Rojala(47) ambaye naye alipata majeraha na anaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa Mkoa wa Songwe.

Amesema mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Sara Mzopola(37) amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya mji wa Tunduma iliyopo Mpemba

"Chanzo cha ajali hiyo kwa taarifa za awali ni kwamba dereva wa katapila akiwa anaendesha kuyumba na kupelekea kugongana na gari hilo na kusababisha majeraha kwa abilia na mwingine kufariki dunia," amesema Kamanda Senga.

Amesema jeshi la polisi linaendelea kumtafuta dereva wa katapila ambaye alikimbia baada ya kusababisha ajali ili hatua za kisheria zichukiwe dhidi yake.


Address

Mbeya
53121

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Knews24 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Knews24:

Share