Jensen Tv

Jensen Tv Podcast for Entertainment, Interviews, Articles & Reality shows, Celebrities Gallery
For promotion DM or WhatsApp 0764290055

20/04/2026

Full video and copyright are under

Nyanda za juu kusini tunapaswa kumshukuru sana mnyalu  kwakua hana tamaa ya kuhama makazi na kwenda Dar, nadhani anajua ...
05/04/2026

Nyanda za juu kusini tunapaswa kumshukuru sana mnyalu kwakua hana tamaa ya kuhama makazi na kwenda Dar, nadhani anajua akiondoka yeye basi nyanda za juu kusini tunabaki kujivunia maparachichi tu.

B2K, ndio msanii pekee anamwonekano wa ki sanii na ki star na anaishi misingi ya ya Sanaa, kuanzaia kuvaa (outfit looks), photo shoot, yaani kwa maana nyepesi na ya kawaida wasanii wengi nyanda za juu kusini hawajui kuvaa kumshinda B2K, haajui ku organise events kumzidi B2K, hata interview B2K anawazidi vingi sana.

Seriousness, B2K ndio msanii mwenye uthubutu zaidi wa kuweka bajeti kubwa kufanya audio na video kwa producers na directors wakubwa kuliko msanii yeyote nyanda za juu kusini.

B2K, kwasasa ni miongoni mwa wasanii bora 20 nchini licha ya kwamba haishi Dar wala hapewi airtime na media kubwa, ndio msanii anaongoza mauzo kwenye majukwaa yote ya mziki, kuanzia single, collaboration na Albums hakuna msanii anamgusa sio tu wa nyanda za juu kusini hata waliopo Dar.

Bila kusahau B2K ni msanii pekee ambaye ameningia kwenye charts kubwa za mziki katika radio kubwa nchini k**a clouds fm, na radio nyingine kubwa.

Nadhani sasa ni wakati wa B2K kupewa crown yake k**a miongoni mwa wasanii bora nchini na sio nyanda za juu kusini pekee.

Pokea maua yako mnyalu

Wahenga waliwahi kusema kwamba "Mtu Chake" wakiwa na maana kwamba hata k**a utaona kitu hakina thamani kwako basi fahamu...
05/04/2026

Wahenga waliwahi kusema kwamba "Mtu Chake" wakiwa na maana kwamba hata k**a utaona kitu hakina thamani kwako basi fahamu kuwa mwenye nacho anaijua thamani yake kwahiyo ukimuona nacho usione k**a anajivuna au kujisikia.

Sasa hii imethibitika baada ya mpenzi na mzazi mwenza wa RAYVANNY kumvaa vikali mtangazaji , na hii ni mara baada ya mtangazaji huyo kupost ujumbe ulio ashiria kuwa aliyepaswa kupewa heshima ni na sio kwani sio yeye aliyeandaa show hiyo.

Fahvanny, amemjia juu kwa kumtumia jumbe mbalimbali DM za kuonesha namna ambavyo amechukizwa na chapisho hilo, na kuliona k**a limejaa chuki na ni dharau kwa Rayvanny.

Wewe mtazamo wako ni upi katika hili?
Video ya show nimepost kwenye post ya nyuma 🔙🔙🔙.

05/04/2026

Pongezi nyingi kwa msanii kwa mwendelezo wake mzuri kwenye matamasha makubwa duniani.

Hii ni show iliyoandaliwa na msanii kutokea Congo 🇨🇩 katika ukumbi wa Accour Arena mjini Paris nchini Ufaransa.

Kumbuka hapa sio Mbeya wala Nzovwe ni mbali na nyumbani.

05/04/2026

Star wa muziki nchini ameweza kushirikishwa na kundi la muziki wa injili kutoka nchini Burundi 🇧🇮 .band kupitia wimbo wao wa Mimi ni Nani. Wimbo ambao hivi sasa umekuwa ukifanya vizuri kwenye majukwaa mbalimbali ya mziki na mitandao ya kijamii ikiwemo Tiktok.

Hii imekua kawaida sana kwa wasanii wa gospel kufanya remix na wasanii wa secular ikiwa ni sehemu ya kukuza na kueneza kazi kwa wafuasi wengi zaidi wa imani tofauti, tumeshuhudia wasanii wengi wakifanya hivyo na sio jambo geni wala la ajabu.

Mbosso, ame share verse yake ambayo ni rasmi ipo kwenye remix ya wimbo huo. Unampa asilimia ngapi mbosso kwenye mziki huu wa Dini?

Tuna watakia kheri ya Pasaka wakristo wote Ulimwenguni.  Furahieni Mwanzo mpya katika kristo Yesu.
05/04/2026

Tuna watakia kheri ya Pasaka wakristo wote Ulimwenguni. Furahieni Mwanzo mpya katika kristo Yesu.

Baada ya mafanikio makubwa ya wimbo wa "Enjoy" ambao Jux alimshirikisha Diamond platinumz, wasanii hao waliendelea kufan...
03/04/2026

Baada ya mafanikio makubwa ya wimbo wa "Enjoy" ambao Jux alimshirikisha Diamond platinumz, wasanii hao waliendelea kufanya kazi zao binafsi hali ambayo watu wengi wakawa wanaongea kwamba huenda wasanii hao hawako sawa kwasasa.

Kupitia kipindi cha Exclusive cha Wasafi, msanii Diamond platinumz alimjibu mtangazaji Lil Ommy kwamba, kuna watu ambao walitaka kuleta mpasuko kati yake na Jux, na akasema wako sawa wala hakuna tofauti yoyote kati yao.

Sasa kuthibitisha hilo, Diamond platinumz amemshirikisha Jux kwenye wimbo wake mpya unaoitwa "Joy".

Una upa asilimia ngapi wimbo huu 10/10



28/03/2026


Leo nakusogezea moja kati ya wimbo bora sana katika kiwanda cha burudani ya wimbo ambao haujawahi kuchuja na hauta kuja kuchuja kamwe.

Karim, ni wimbo unaohusu kumtumaini Mungu katika nyakati zote, haijalishi unapitia nini lakini ukimtegemea Mungu ananjia nyingi za kukusaidia au kuku kutanisha na msaada. Usitegemee akili zako bali Muumba.

Tangu wimbo huu ulipoachiwa uliweka alama kubwa kwa msanii alikiba kwani ilikua ni storytelling ya kumhusu kijana ambaye alikua anaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu, na hii ilikua ni wakati ambao wimbo k**a ulikua na simulizi nzuri sana.

Tunatoa heshima kwa king kiba kwa wimbo utakaoishi milele, Enjoy.

Chuck Norris, mwigizaji maarufu wa Marekani na mtaalamu wa mapigano, alifariki tarehe 19 Machi 2026, (Jana) akiwa na umr...
20/03/2026

Chuck Norris, mwigizaji maarufu wa Marekani na mtaalamu wa mapigano, alifariki tarehe 19 Machi 2026, (Jana) akiwa na umri wa miaka 86. Alifariki asubuhi ya Alhamisi huko Hawaii, akiwa na familia yake karibu.

Taarifa ya kifo chake imethibitishwa na familia yake kupitia account yake rasmi ya Instagram, Katika taarifa hiyo imeeleza kuwa alifariki siku ya jana lakini kwasababu maalumu waliamua kukaa kimya kwanza.

Tasnia ya mapigano na movie, imempoteza moja kati ya alama mhimu na nguzo imara katika kiwanda cha movie, Chuck Norris alifanya vizuri kupikia kazi zake k**a vile "Delta Force 2" "Walker, Texas Ranger" na "Missing in Action". Familia inaomboleza kumpoteza Baba, Babu, Kaka na kiongozi. Lakini wanamshuku kwa maisha yake hapa duniani.

Tunatoa pole kwa wadau wa filamu na mashabiki wa movie ulimwenguni.

#

17/03/2026

Moja kati ya show ambazo kijana kutokea Tandale aliiwakilisha nchi ipasavyo ni hii show, wakati wa kukaribishwa kwenye stage, walisikika mashabiki wakimfananisha yeye na Michael Jackson, na akatumbuiza wimbo wa "Kidogo" ambao ameshirikiana na kundi maarufu la mziki Africa P square ambao na wao pia wamekuwa wakifananishwa na MJ.

One of the Top Top, and classic performance ever, from Diamond platinumz, Unakumbuka hii show ilikua kwenye tukio gani na ulikua mwaka gani?

Address

Ilomba
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jensen Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jensen Tv:

Share