Jensen Tv

Jensen Tv Podcast for Entertainment, Interviews, Articles & Reality shows, Celebrities Gallery
For promotion DM or WhatsApp 0764290055

23/12/2025

Tupate Burudani kidogo....

Kipekee, napenda kuwapongeza wote waliopo nyuma ya Founders Exhibition Awards  , kuanzia walio leta wazo la Tuzo hizi, l...
23/12/2025

Kipekee, napenda kuwapongeza wote waliopo nyuma ya Founders Exhibition Awards , kuanzia walio leta wazo la Tuzo hizi, lakini wote ambao waliamua, au kuthubutu kuanzisha jambo hili from ideal to acts na wengine wote, Hongereni na Mungu awabariki tuta wa support.

Huu ni msimu wa pili tangu kuanzishwa kwa tuzo hizi, lakini ni event ambayo imekua na mvuto wa kipekee, ushindani na ushawishi mkubwa, Ni mashindano ambayo ukiangalia yamelenga kuaminisha vijana katika kile wanachokifanya, kuanzia ubunifu, ujasiriamali, maudhui na Biashara.

Mashindano haya yatakua chachu kwa vijana wengi sana kujituma na kuanza kuamini katika ndoto zao, tuzo ni thamani ya kile unachokifanya, unapopewa tuzo ni ishara tosha kuwa wewe ni mshindani na unachokifanya kinaonekana.

Categories, zimepangiliwa vizuri na hata washindani wenyewe wanaona usawa mfano kijana k**a siku zote nimekua nikijivunia jitihada anazozifanya kuonesha ni jinsi gani anaipenda kazi yake na taaluma yake, Pia mtu k**a kuchukua tuzo ya mtangazaji chaguo la watu haina kipengele.

Nadhani sasa hii ni fursa mpya, ni jukwaa jipya kwa sisi vijana wenye ndoto kufanya vitu kwa ubunifu mkubwa ili tuweze kuwa na ushindani thabiti na kujitengenezea safasi katika Jamii zetu.

Ni nafasi sahihi pia kwa wafanya biashara, taasisi, na makampuni kujitangaza na kuwekeze katika event hii kwani ni tuzo ambazo zimezidi kupokelewa kwa ukubwa na mda si mrefu zinaweza kutazamwa kwa ukubwa zaidi.

Hongera sana.


Kuna generation nyingi za burudani nchini ambazo zimeacha legacy katika tasnia ya muziki hapa nchini, watangazaji mbalim...
23/12/2025

Kuna generation nyingi za burudani nchini ambazo zimeacha legacy katika tasnia ya muziki hapa nchini, watangazaji mbalimbali waliweza kufanya vitu tofauti katika kiwanda cha burudani vitu ambavyo kwakiasi kikubwa vimeacha alama na kuweka njia kwa generation nyingine.

Mtu k**a nk hawa nimewataja kwa maana ya generation tofauti tofauti, kuna hapa Salama Jabir, anabaki k**a nguzo ya vijana wengi uwezo wake wa kuuliza maswali ambayo wengine wangeogopa basi yeye anakuuliza k**a swali la kawaida.

Sasa mimi nakuletea hii Gen Z generation, na moja kwa moja nakupeleka hadi hapa nataka nakukutanisha na kipaji cha kipekee sana, ambacho naamini akiendelea kupata airtime ya kutosha basi anakwenda kupanda mbegu ambayo soon matunda yake tutayaona katika vipindi vya burudani, ambavyo miaka ya hivi karibuni vilionekana kupoteza mvuto.

Huyu ni @

1. Ubunifu kwenye interview.

Hizi sifa zote nitaelezea kwa kumlejea , Kipindi hiki vijana wengi wanajitafuta kwenye utofauti ukizingatia na Generation ambayo kila mtangazaji wa burudani alitaka asikike k**a Bdozen, Kennedy the remedy, Adam Mchomvu, Dullah planet au Salama, hawa wasasa wanaishi kwenye u unique.

Style ya Dar Boi, kwanza yuko Slow kwenye kuongea na anakusikiliza then anauliza tena sio wakubishana, Always he sounds in the same tone, sio wa kupayuka au kuongelea puani.

Anauliza maswali ambayo wasikilizaji wangetamani kusikia, sio mtu wa udaku sana ila yuko deep sana kuhakikisha unapata burudani.

2. Fashionable.
"Music and fashion are inseparable " Vijana wanaofanya entertainment wana drip sana, ni wanyama na inatakiwa hivyo kwasababu hata wasanii wanao wa interview inawapa somo kuwa lazima niwe na mwonekano huu. Hapa Dar Boi ni mnyaka kabisa.

3. Voice Over & Event Hosts (MC)
Uwezo wa kufanya PA, Kufanya matangazo na Promotion lakini pia kusimamia shows.

Miaka mi 5 mbele kila radio itakuwa na Mtangazaji aina ya Dar Boi, sio kwa ubaya lakini kitu kizuri kinaishi, sio kwa kumuiga ufanyaji kazi wake, lakini watangazaji wengi watajitafuta kupitia style yake ya utangazaji.

Mimi ni mjumbe tuu naitwa

Mwaka 2025, umekuwa mwaka bora sana kwa upande wa Comedy wengi wamejitahidi kutengeneza maudhui ya kufurahisha na ku eli...
20/12/2025

Mwaka 2025, umekuwa mwaka bora sana kwa upande wa Comedy wengi wamejitahidi kutengeneza maudhui ya kufurahisha na ku elimisha.

Kwa mtazamo wako nani anastahili tuzo ya mchekeshaji bora?

na

Kwa upande wako nani anastahili tuzo ya msanii bora mwaka huu hapa nchini?                 ❤️💞❤️
20/12/2025

Kwa upande wako nani anastahili tuzo ya msanii bora mwaka huu hapa nchini?

❤️💞❤️

Huyu ni Queen of Bongo movie ( horror movie) je, Ume mtambua??Mtag......
17/12/2025

Huyu ni Queen of Bongo movie ( horror movie) je, Ume mtambua??
Mtag......

Kalamu yangu ya Pongezi kwa  King Pusi ni msanii wa vichekesho nchini na Mzaliwa wa Kigoma, Alianza kufahamika zaidi baa...
10/12/2025

Kalamu yangu ya Pongezi kwa

King Pusi ni msanii wa vichekesho nchini na Mzaliwa wa Kigoma, Alianza kufahamika zaidi baada ya kuonekana katika official video ya CHIBONGE ya marioo, Abbah, Gnako na Bayster best, Lakini pia maudhui yake binafsi ya kuigiza na wanawake wenye makalio makubwa.

Kipindi flani niliona interview za king pusi kwenye baadhi ya media nyingi tu hapa nchini. Interview ambazo jamaa alikua anaongea kwa maumivu makubwa sana ya kuhisi kutengwa na alikua anasema anapitia kipiti kigumu sana, kwani kazi zilikua haziendi na engagement ilikua ndogo sana.

King pusi alilia kwenye interview akidai hata msanii k**a marioo ambaye alifanya kazi yake bila malipo yoyote bado nayeye alikua amemtenga hata akimpigia simu hazipokelewi.

Basi, baada ya kuonana kelele sio kazi yake, akaamua kurudi upya kwenye game hapa akarudi na mtindo mpya wa kuigiza vitendo bila sauti, kitu ambacho kimemrudisha kwenye game kwa ukubwa zaidi.

Mpaka sasa Ana Views 1B kwenye jukwaa la Facebook pekee, hii ni ishara ya ukomavu na mafanikio, kuna vitu lazima upitie ili uweze kuwa bora zaidi ya mwanzo.

HONGERA SANA KING PUSI 🤴 👑

Kwamba ni kweli mmetumiss au mnataka tuanze kupost mtuache tena?Weka Playlist yako kwa comment.
15/10/2025

Kwamba ni kweli mmetumiss au mnataka tuanze kupost mtuache tena?

Weka Playlist yako kwa comment.

21/08/2025

Address

Ilomba
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jensen Tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jensen Tv:

Share