BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA BOMBA FM RADIO broadcasting live from MBEYA CITY - TANZANIA.(Iringa,Mbeya,Rukwa,Njombe & Ruvuma). Tus

21/08/2026

Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imemruhusu mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa kwanza wa kutenganishwa na pacha aliyeungana aina ya parasitic conjoined twins, baada ya kuendelea vizuri kwa siku 10 tangu kufanyika kwa upasuaji huo wa kihistoria.

Mtoto huyo alifanyiwa upasuaji huo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, ikiwa ni hatua muhimu katika historia ya huduma za ubingwa na ubingwa bobezi wa matibabu nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa ya Muhimbili iliyotolewa leo, Agosti 21, 2026, mtoto huyo ameendelea vizuri baada ya kutenganishwa na pacha huyo na sasa ameruhusiwa kuendelea na matibabu na uangalizi akiwa nyumbani.

Upasuaji huo wa kutenganisha pacha wa aina ya parasitic conjoined twins umeelezwa kuwa ni miongoni mwa hatua kubwa katika maendeleo ya huduma za kibingwa nchini, huku ukionesha uwezo wa wataalamu wa afya kufanya upasuaji changamani unaohitaji utaalamu wa hali ya juu.

Mafanikio hayo yanaongeza matumaini kwa watoto wenye changamoto zinazohitaji huduma maalumu za upasuaji, pamoja na kuonesha umuhimu wa kuendelea kuimarisha huduma za kibingwa na ubingwa bobezi katika hospitali za Tanzania.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Sophia Kumbuli, amefariki dunia leo August 21, 2026 katika Hospitali ya ...
21/08/2026

Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi, Sophia Kumbuli, amefariki dunia leo August 21, 2026 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa iliyotolewa na kitengo cha Mawasiliano Serikalini cha Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda imeeleza kuwa Kumbuli amefariki dunia akiwa katika matibabu, bila kueleza zaidi kuhusu ugonjwa uliokuwa ukimsumbua.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda, Brian Severe, ametoa pole kwa Watumishi wa halmashauri hiyo, familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu kufuatia msiba huo.

Marehemu Sophia Juma Kumbuli alikuwa akiongoza Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda tangu mwaka 2021 hadi kifo chake leo Agosti 21, 2026.

Pia aliwahi kuwa Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Chunya mkoani Mbeya.

21/08/2026

Nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Brazil na klabu ya Barcelona Ronaldinho ametua nchini Italia baada ya kusaini rasmi mkataba wa kujiunga na klabu ya Ravenna FC inayoshiriki ligi daraja la tatu Serie C.

Ronaldinho anarejea kusakata kabumbu ikiwa takribani miaka 11 tangu alipocheza mechi yake ya mwisho ya kulipwa akiwa na klabu Fluminense mwaka 2015.

Mashabiki wengi wa soka duniani wameshangazwa na hatua ya Ronaldinho kurejea dimbani ambapo kwa sasa ana umri wa miaka 46.

21/08/2026

Ni wakati wa Sala ya Baba Yetu na

“Baba yetu uliye mbinguni,
Jina lako litukuzwe.
Ufalme wako uje.
Mapenzi yako yatimizwe duniani k**a huko mbinguni.
Utupe leo riziki yetu ya kila siku.
Utusamehe makosa yetu,
k**a sisi nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
Usitutie majaribuni,
bali utuokoe na yule mwovu.
Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.”

21/08/2026

Kuna siri ya kumiliki

21/08/2026

LISSU ANA KESI YA KUJIBU

Mahak**a Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam imetoa uamuzi katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, na kusema ana kesi ya kujibu.

Uamuzi huo unamaanisha kuwa Mahak**a imeona kuna ushahidi wa msingi uliowasilishwa na upande wa mashtaka unaompa Lissu nafasi ya kuingia katika hatua ya utetezi. Hata hivyo, hii si hukumu kwamba amepatikana na hatia.

Baada ya uamuzi huo, Lissu ameiambia Mahak**a kuwa atajitetea mwenyewe na ameomba mashahidi 11 waitwe kutoa ushahidi upande wake.

Miongoni mwa majina aliyoyataja ni Rais Samia Suluhu Hassan, aliyekuwa Makamu wa Rais Philip Mpango, aliyekuwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Mkuu wa Jeshi la Polisi Camillus Wambura, Mkuu wa Majeshi Jenerali John Mkunda pamoja na viongozi mbalimbali wa CHADEMA.

Lissu pia amelalamikia kuzuiwa baadhi ya viongozi wa CHADEMA ambao anawahitaji k**a mashahidi kumtembelea akiwa kizuizini, akiiomba Mahak**a itoe amri ili aweze kuonana nao.

Sasa kesi inaingia katika hatua mpya—hatua ya utetezi, ambapo Lissu atapata nafasi ya kujibu ushahidi uliotolewa na Jamhuri na kuwasilisha mashahidi wake mbele ya Mahak**a.

🎙️✍️Mc Kamendu

🎶🔥 GOSPEL FLAVOUR – BURUDANI LA DUNIA 🔥🎶Unataka kufahamu habari mbalimbali za burudani, taarifa za waimbaji wa nyimbo za...
21/08/2026

🎶🔥 GOSPEL FLAVOUR – BURUDANI LA DUNIA 🔥🎶

Unataka kufahamu habari mbalimbali za burudani, taarifa za waimbaji wa nyimbo za Injili, nyimbo mpya (Joints) na matukio yanayoendelea kwenye muziki wa Injili?

📻 Tune in kupitia Bomba FM 104.1MHz Mbeya kwenye kipindi cha Gospel Flavour.

🎤 Tukutane na Princess Melina akizungumzia muziki wake na safari yake ya huduma ya uimbaji.

🎙️ Host: Ibrah Dank
🕖 Muda: 7:00 Mchana - 8:00 Mchana

🔥 Bomba FM – Elimisha. Burudisha. 🔥

21/08/2026

Kesi ya Tundu Lissu: Mbivu na Mbichi Kujulikana Leo

Leo ndiyo siku iliyokuwa ikisubiriwa katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu.

Baada ya upande wa Jamhuri kufunga ushahidi wake na Lissu kusema hana kesi ya kujibu, Mahak**a Kuu inatarajiwa kutoa uamuzi iwapo Lissu ana kesi ya kujibu na hivyo kuingia katika hatua ya utetezi, au k**a upande wa mashtaka umeshindwa kuweka msingi wa kesi.

Ulinzi umeimarishwa ndani na nje ya Mahak**a, huku baadhi ya wanaotaka kuingia wakielezwa kuwa ukumbi umejaa.

Kwa kifupi, leo ndiyo siku ya kujua k**a Lissu ataendelea na hatua ya kujitetea au kesi yake itasimama hapa.

Macho na masikio yote sasa yanaelekezwa Mahak**ani, kusubiri uamuzi wa Majaji.
🎙️ ✍️ Mc Kamendu

Nyota wa zamani wa Brazil, Ronaldinho, mwenye umri wa miaka 46, amerejea kwenye soka la ushindani baada ya kusaini mkata...
21/08/2026

Nyota wa zamani wa Brazil, Ronaldinho, mwenye umri wa miaka 46, amerejea kwenye soka la ushindani baada ya kusaini mkataba na Klabu ya Ravenna inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu nchini Italia (Serie C).

Ronaldinho hajacheza mchezo wa soka la ushindani tangu mwaka 2015 alipokuwa akiichezea Fluminense ya Brazil.

Sasa anarejea Italia kwa mara nyingine baada ya kuitumikia AC Milan kati ya mwaka 2008 na 2011.

Klabu ya Ravenna imesisitiza kuwa ujio wa Ronaldinho si kwa ajili ya matangazo au kampeni ya kimasoko, bali atashuka dimbani katika mchezo rasmi wa kiushindani.

21/08/2026

Watumishi wawili wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya wameondolewa kazini kutokana na kukiuka taratibu na miongozo ya utumishi, ikiwemo utoro wa muda mrefu kazini.

Hatua hiyo imechukuliwa katika kikao cha robo ya nne cha mwaka cha Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo, ambapo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya, Aida Haule, amesema baraza limefikia uamuzi huo baada ya jitihada mbalimbali za kuwashawishi watumishi hao kurejea kazini kushindikana.

Kwa mujibu wa Haule, miongoni mwa sababu zilizotolewa na mmoja wa watumishi hao ni suala la ndoa, ambapo alieleza kuwa ameshindwa kuendelea na kazi kutokana na kutakiwa na mume wake kutofanya kazi.

Amesema baraza halifurahishwi na kuwaondoa watumishi kazini, lakini wakati mwingine hulazimika kuchukua hatua kwa kuzingatia sheria, miongozo na taratibu za utumishi.

“Baraza hili linaendeshwa kwa miongozo, taratibu na sheria. Kuna watumishi mbalimbali wanakiuka miongozo, taratibu na sheria na sisi k**a wawakilishi wa wananchi hatutamani kuona watumishi wanaondolewa kazini, lakini inakuwa haina budi,” amesema Haule.

Address

P O Box 579
Mbeya
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA:

Shortcuts

Share

Category