BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA BOMBA FM RADIO broadcasting live from MBEYA CITY - TANZANIA.(Iringa,Mbeya,Rukwa,Njombe & Ruvuma). Tus

Karibu usikilize Bomba FM Radio 104.1 MHz Mbeya, tukiwa mubashara kutoka Tanganyika Packers, Kawe Jijini Dar es Salaam, ...
07/06/2026

Karibu usikilize Bomba FM Radio 104.1 MHz Mbeya, tukiwa mubashara kutoka Tanganyika Packers, Kawe Jijini Dar es Salaam, kwenye Kongamano Kubwa la Kula Mwili na Damu ya Yesu Kristo.

Kongamano hili linaongozwa na Mtumishi wa Mungu, Mtume Boniface Mwamposa "Bulldozer", likiwa na maelfu ya waumini waliokusanyika kushiriki ibada hii maalum ya kiroho.

Endelea kuwa nasi kupitia Bomba FM Radio 104.1 MHz Mbeya kwa matangazo ya moja kwa moja, mahubiri, maombezi na matukio yote yanayoendelea katika kongamano hili kubwa.

Bomba FM Radio — Elimisha, Burudisha

06/06/2026

Agnes Obeid Ole, mkazi wa wilaya ya Chunya mkoani Mbeya amelia machozi ya furaha mbele ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba baada ya kusikilizwa kero yake na kutolewa uamuzi kwamba mdaiwa atafutwe na amlipe sh. milioni 181 anazozidai.

"Kamanda wa Polisi mtafute huyo bwana. Mahak**a ilikwishatoa hukumu na ikampa mama ushindi. Asakwe popote alipo, arudishe vifaa na arudishe fedha za huyu mama," amesema Waziri Mkuu na kuamsha shangwe kwa wananchi waliokuwepo.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Juni 6, 2026 wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya soko la Ifunda, wilayani Iringa, mkoani Iringa.

Akielezea kero yake, Bi. Agnes amesema kuwa kabla mume wake hajafariki, walikuwa wanachimba dhahabu kwenye mgodi wao huko Chunya lakini walimuomba rafiki yao, Bw. Lelevasi Fishulo mwenye mashine za kuchenjua washirikiane naye ili baadaye wagawane naye faida.

"Tulipata sh. milioni 362 lakini akasema amepata dharura na akaomba atulipe baadaye. Tukamkubalia. Mgao wetu ulikuwa sh. milioni 181 lakini siku ya kulipwa mume wangu akafariki, kwa hiyo nikaacha kufuatilia sababu ya maombolezo."

Bi. Agnes anasema baada ya mwaka mmoja kupita akamfuata kudai hela yake lakini hakumpa. "Nikaenda Serikali ya kijiji akaitwa kwa miezi mitatu hakutokea, nikaenda polisi akaitwa lakini ikapita miezi minne hakutokea ndipo nikaenda mahak**ani kwa masuala ya mirathi," amesema.

05/06/2026

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Zungu amewataka wabunge kuhakikisha wanatumia lugha za kibunge pindi wanapochangia hoja mbalimbali bungeni, badala ya kutumia lugha zinazoweza kudhalilisha au kukiuka kanuni na miongozo ya bunge.

Spika Zungu ameyasemaleo Juni 05,2026 bungeni jijini Dodoma baada ya Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini, Ado Shaibu, kuhoji matumizi ya baadhi ya maneno yaliyotolewa wakati wa mijadala ya Bunge.

05/06/2026

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza leo Juni 05,2026 kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira duniani jijini Dodoma.

05/06/2026

Tenga Dakika 1 kuabufi pamoja na Mtumishi wa Mungu,MTUME MWAMPOSA BULLDOZER

Ni wakati wa Sala ya Baba Yetu na  “Baba yetu uliye mbinguni,Jina lako litukuzwe.Ufalme wako uje.Mapenzi yako yatimizwe ...
05/06/2026

Ni wakati wa Sala ya Baba Yetu na

“Baba yetu uliye mbinguni,
Jina lako litukuzwe.
Ufalme wako uje.
Mapenzi yako yatimizwe duniani k**a huko mbinguni.
Utupe leo riziki yetu ya kila siku.
Utusamehe makosa yetu,
k**a sisi nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
Usitutie majaribuni,
bali utuokoe na yule mwovu.
Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.”

04/06/2026

Mwamposa aishungulikia Ngoma ya majini

MALANGO YAKO YAMEFUNGUKA DODOMA! 🔥Siku 3 za neema, maombi na mafundisho ya kipekee zimewadia. Usikose kukutana na Mtume ...
04/06/2026

MALANGO YAKO YAMEFUNGUKA DODOMA! 🔥

Siku 3 za neema, maombi na mafundisho ya kipekee zimewadia. Usikose kukutana na Mtume Boniface Mwamposa (Bulldozer) katika mkutano mkubwa wa kiroho utakaofanyika Dodoma kuanzia tarehe 18 hadi 20 Juni 2026.

Karibu upokee neno, maombi na mguso wa Mungu katika siku hizi maalum za uamsho.

📍 Chamwino, Dodoma
📅 18–20 Juni 2026
🕗 Saa 8:00 Mchana
Malango yako yamefunguka, sasa ni wakati wako wa kuvuka kwenda hatua nyingine!

04/06/2026

Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba amesema mpaka kufikia sasa Tanzania haina kisa chochote cha ugonjwa wa Ebola na kwamba tayari serikali inaendelea kuchukua tahadhari ikiwemo kutoa elimu kwa Wananchi.

Dkt. Nchemba ameyasema hayo wakati akijibu swali la mbunge katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo bungeni jijini Dodoma.

04/06/2026

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Musa Zungu, amewaonya wabunge wanaokiuka taratibu za Bunge kwa kutohudhuria vikao bila sababu za msingi, wakiwemo baadhi ya wabunge waliokwenda kuishangilia timu ya taifa ya vijana ya Serengeti Boys kwa kusafiri nje ya nchi bila kupata kibali kutoka kwa Spika k**a kanuni zinavyoelekeza.

Spika Zungu ameyasema hayo leo Juni 04,2026 bungeni jijini Dodoma na kuagiza kuwa wabunge wote waliokwenda kuishangilia Serengeti boys wanapaswa kuandika barua ya kujieleza.

Amesema kuwa nidhamu na uwajibikaji ni muhimu ili kuhakikisha shughuli za Bunge zinaendelea kwa ufanisi na kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Address

P O Box 579
Mbeya
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA:

Share

Category