BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA BOMBA FM RADIO broadcasting live from MBEYA CITY - TANZANIA.(Iringa,Mbeya,Rukwa,Njombe & Ruvuma). Tus

Leo ni siku kubwa kwa Wakulima, Wafugaji na Wavuvi tukisherehekea Sikukuu ya 88 2025.
08/08/2025

Leo ni siku kubwa kwa Wakulima, Wafugaji na Wavuvi tukisherehekea Sikukuu ya 88 2025.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb)...
06/08/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (Mb), kwa masikitiko makubwa ametangaza kifo cha Spika Mstaafu na aliyekuwa Mbunge wa Kongwa, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai.

Mheshimiwa Ndugai amefariki dunia leo, Jumanne ya tarehe 06 Agosti, 2025 katika Jiji la Dodoma.

“Kwa masikitiko makubwa naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika Mstaafu, Mheshimiwa Job Ndugai, kilichotokea leo Jijini Dodoma,” amesema Dkt. Tulia Ackson.
✍️

KURA ZA MAONI KATA YA MKWAJUNIWajumbe katika kata ya Mkwajuni wilayani Songwe wamempitisha aliyekuwa Diwani wa Kata hiyo...
05/08/2025

KURA ZA MAONI KATA YA MKWAJUNI

Wajumbe katika kata ya Mkwajuni wilayani Songwe wamempitisha aliyekuwa Diwani wa Kata hiyo na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa, Ndugu Shaibath Kapingu baada ya kuibuka na ushindi mkubwa kwa kupata kura 951 kati ya kura halali 998.

Kapingu amewashinda watia nia wenzake, Jackline Mwageni aliyepata kura 22, na Faraja Lyanzile aliyepata kura 14 huku kura 11 zikiharibika.

SHAIBATH KAPINGU atapeperusha bendera ya CCM kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika mwezi Octoba 29,2025.

KURA ZA MAONI JIMBO LA MBEYA MJINI.Bendera ya CCM katika Jimbo la Mbeya Mjini, sasa itapeperushwa na Patrick Mwalunenge ...
05/08/2025

KURA ZA MAONI JIMBO LA MBEYA MJINI.

Bendera ya CCM katika Jimbo la Mbeya Mjini, sasa itapeperushwa na Patrick Mwalunenge ambaye ameongoza kwa kura 3,360 kati ya kura 5,211 zilizopigwa, ambapo watiania walikuwa sita.

Kwa mujibu wa katibu wa CCM wilaya ya Mbeya mjini MOHAMED MAVALLAH wengine ni Dk Mabula Mahande aliyepata kura 1,133, Shambwee Sh*tambala kura 392, Charles Makipesile (133), Sofia Malingumu (100) na Elizabeth Thobias kura 56.

KURA ZA MAONI JIMBO LA UYOLE.Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini, Mohammed Mavallah amesema Jimbo ...
05/08/2025

KURA ZA MAONI JIMBO LA UYOLE.

Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mbeya Mjini, Mohammed Mavallah amesema Jimbo la Uyole lilikuwa na wapiga kura 5 148, ambapo Dk Tulia amepata kura 4,830.

Amesema katika Jimbo hilo, watiania walikuwa watatu wakiwa ni Dk Tulia aliyeongoza akifuatiwa Dk Seria Masole aliyepata kura 275 na Emir Sanga aliyepata 35.

MBEYA: Afisa Mahusiano wa chuo Cha Uhasibu Arusha Stella Kalinga akitoa maelezo Kwa mwananchi aliyetembelea Banda Hilo k...
04/08/2025

MBEYA: Afisa Mahusiano wa chuo Cha Uhasibu Arusha Stella Kalinga akitoa maelezo Kwa mwananchi aliyetembelea Banda Hilo katika viwanja vya Nane Nane Mbeya.

MAONESHO YA WAKULIMA 88 KATIKA VIWANJA VYA JOHN MWAKANGALE JIJINI MBEYA.Baadhi ya wananchi wakipata maelezo katika Banda...
04/08/2025

MAONESHO YA WAKULIMA 88 KATIKA VIWANJA VYA JOHN MWAKANGALE JIJINI MBEYA.

Baadhi ya wananchi wakipata maelezo katika Banda la Wakala wa Misitu Tanzania Kanda ya Nyanda za Juu kusini

MBEYA: ZOEZI LA KURA YA MAONI JIJINI MBEYA.Mtia nia wa nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama Cha Mapinduzi (C...
04/08/2025

MBEYA: ZOEZI LA KURA YA MAONI JIJINI MBEYA.

Mtia nia wa nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, leo tarehe 4 Agosti 2025, ameshiriki kupiga kura ya maoni katika Kituo cha St. Agrey, Mkoani Mbeya, kwa ajili ya kuwachagua Diwani wa Kata ya Itezi na Mbunge wa Jimbo la Uyole kupitia CCM.

🙌KALI ZA BOMBA 💥TOP 10 WEEK HII🔊 Kutoka Jijini Mbeya🇹🇿 Karibu tuzihesabu joints Kali 10 za week📻🔥💥4more info's za kiburu...
02/08/2025

🙌KALI ZA BOMBA 💥TOP 10 WEEK HII🔊 Kutoka Jijini Mbeya🇹🇿 Karibu tuzihesabu joints Kali 10 za week📻

🔥💥4more info's za kiburudani tuguse hapa 🔊New joints💥 Artists scandals 🔥Tuguse hapaaa📻104.1Mhz

Tusikilize now Kwa kubofya link hii

https://radio.garden/listen/bomba-fm-104-1/rGZunUau

💥WAPENDA BURUDANI WOTE TUNAPOA HAPA🔥
Ibrah Dank 🇹🇿 🎛️
🎙️

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA 📻 104.1MHZ 🔥

UNYADEEEE 🙌 UNYADEEEE 🙌

LEO NI SIKU YA MASHUJAA TANZANIA Siku ya Mashujaa Tanzania huadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Julai. Ni siku ya kitaifa y...
25/07/2025

LEO NI SIKU YA MASHUJAA TANZANIA

Siku ya Mashujaa Tanzania huadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Julai.

Ni siku ya kitaifa ya heshima na kumbukizi kwa Watanzania wote waliopoteza maisha yao au walioshiriki kwa ujasiri katika kuilinda na kulitumikia Taifa letu la TANZANIA hasa wanajeshi waliopigania uhuru na waliolinda mipaka ya taifa katika nyakati za vita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr SAMIA SULUHU HASSAN ndiye mgeni rasmi wa siku hii katika mnara wa Mashujaa jijini Dodoma.

MOHAMED HUSSEIN AAGA RASMI BAADA YA  KUITIMIKIA SIMBA MIAKA 11.Aliyekuwa nahodha wa klabu ya Simba SC, Mohamed Hussein, ...
19/07/2025

MOHAMED HUSSEIN AAGA RASMI BAADA YA KUITIMIKIA SIMBA MIAKA 11.

Aliyekuwa nahodha wa klabu ya Simba SC, Mohamed Hussein, ameaga rasmi klabu hiyo baada ya kuhudumu kwa takribani miaka 11 akiwa sehemu ya kikosi cha timu hiyo maarufu barani Afrika.

Katika taarifa yake ya kuagana, Mohamed Hussein amesema kipindi chote ndani ya klabu hiyo kimejaa furaha, huzuni, shangwe, vifijo, nderemo na wakati mwingine masikitiko. Ameeleza kuwa msingi wa utumishi wake Simba SC ulikuwa ni uaminifu, weledi wa hali ya juu na kujituma kwa kiwango kikubwa kuipigania nembo ya klabu hiyo.

“Wahenga walisema kila lenye mwanzo halikosi mwisho. Leo nawaaga rasmi. Haya ni maamuzi yaliyolenga maendeleo yangu binafsi, maslahi yangu binafsi na weledi wangu uliotukuka,” amesema Hussein.

Ametumia fursa hiyo kuwashukuru viongozi wa klabu, benchi la ufundi, na watumishi wa idara ya uendeshaji kwa ushirikiano waliompa katika kipindi chote alichokuwepo ndani ya klabu hiyo. Pia, amewashukuru mashabiki wa Simba SC kwa mapenzi na uungwaji mkono waliompa, huku akiwahakikishia kuwa naye atabaki kuwa nao kwa moyo wake wote.

✍️

Iko powa ni post

LINDI: Watoto watatu wa familia moja wamekutwa wamefariki dunia baada ya nyumba waliyokuwa wanaishi kuungua moto.Kwa muj...
17/07/2025

LINDI: Watoto watatu wa familia moja wamekutwa wamefariki dunia baada ya nyumba waliyokuwa wanaishi kuungua moto.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, John Imori amesema kuwa tukio hilo limetokea Julai 16, 2025 saa 11 jioni katika Kijiji cha Nambilanje.

Watoto waliofariki dunia ni Membe Ndama (7), Mwaru Ndama (2)na Sayi Ndama (1)walikuwa wakiishi na wazazi wao katika Kijiji cha Nambilanje, Wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi.

Hata hivyo kamanda Imori ameeleza kuwa baba na mama wa watoto hao walitoka kwenda kuchota maji na kuchimba viazi hivyo waliwaacha watoto hao nyumbani, ambapo Sayi alikuwa amelala na wenzake walikuwa wakicheza nje ya nyumba hiyo.

Kamanda Imori amesema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni moto uliokuwa kwenye jiko la mawe kushika nyasi za ukuta wa ndani ya nyumba na kusababisha nyumba kuungua.

Miili ya marehemu hao imefanyiwa uchunguzi na Daktari Ezekia Ambekile wa Hosptali ya Wilaya ya Ruangwa na kubaini kuwa chanzo cha vifo ni kukosa hewa baada ya kuungua moto.

Address

P O Box 579
Mbeya
255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 00:30

Telephone

+255753451045

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA:

Share

Category