BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA BOMBA FM RADIO broadcasting live from MBEYA CITY - TANZANIA.(Iringa,Mbeya,Rukwa,Njombe & Ruvuma). Tus

DAR ES SALAAM: Mtumishi wa Mungu kutoka madhabahu ya Inuka Uangaze, Mtume Boniface Mwamposa maarufu k**a Bulldozer, amer...
20/09/2025

DAR ES SALAAM: Mtumishi wa Mungu kutoka madhabahu ya Inuka Uangaze, Mtume Boniface Mwamposa maarufu k**a Bulldozer, amerejea nchini akitokea Brazil ambako alienda kutangaza injili ya Bwana Yesu Kristo.

Katika huduma hiyo aliyoiongoza, amesema Mungu ametenda mambo makuu kwa kuwagusa watu wengi waliokusanyika kusikia neno la wokovu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, Mtume Mwamposa amesema watu wa Brazil wamepokea wokovu, wameponywa huku wengine wakifunguliwa vifungo vya kiroho.

Amesema matukio hayo ni ishara ya nguvu ya Mungu inayoendelea kufanya kazi hata katika mataifa ya mbali.

Kurejea kwake kumeambatana na furaha kubwa kwa waumini na wafuasi wake hapa nchini, ambao wameonyesha shukrani kwa kile walichokiita ushindi wa injili na kwamba hatua hiyo ni kielelezo cha kazi ya Mungu kupitia kwa Mtumishi wao.

SONGWE: AMANI NA USALAMA KIWE KIPAUMBELE CHETU WAKATI NA BAADA YA UCHAGUZI.Maafisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbal...
31/08/2025

SONGWE: AMANI NA USALAMA KIWE KIPAUMBELE CHETU WAKATI NA BAADA YA UCHAGUZI.

Maafisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali wametakiwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na maadili katika kutekeleza majukumu yao ya kazi hususani katika kipindi cha kampeni na siku ya uchaguzi mkuu Oktaba 29, 2025 ili ufanyike kwa amani na utulivu.

Akizungumza Agosti 30, 2025 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Augustino Senga na askari hao, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwa na nidhamu, uwajibikaji na kuzingatia misingi ya haki wakati wote, hasa wakati huu wa mchakato wa uchaguzi ambao unahitaji umakini na weledi mkubwa.

Kamanda Senga amehimiza askari wa Jeshi la Polisi kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha kuwa usalama wa wananchi unazingatiwa katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, ili kutoa huduma bora kwa jamii wakati wote, bila kuvunja maadili ya kazi zao.

Hata hivyo amewakumbusha askari kuwa, pamoja na majukumu yao ya kawaida, wanapaswa kuwa tayari na maandalizi ya usalama kwa ajili ya ziara Mheshimiwa Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye anatarajiwa kufika Mkoani Songwe Septemba 03, 2025 kwa ajili ya kampeni za uchaguzi.

MBEYA: Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mgombea Ubunge jimbo la Mbeya Mjini Bw. Patri...
28/08/2025

MBEYA: Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mgombea Ubunge jimbo la Mbeya Mjini Bw. Patrick Mwalunenge amerejesha fomu tume huru ya Taifa ya uchaguzi jimbo la Mbeya mjini ya kugombea nafasi ya ubunge tarehe 27.08.2025 .

Bw.Patrick baada ya kurejesha fomu ameendelea kusisitiza mshik**ano ndani ya chama na kuvunja makundi ya wagombea.

SHINYANGA: Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Elizabeth Maneno Mkazi wa kijiji cha Itwangi Halmashauri ya Manispaa...
26/08/2025

SHINYANGA: Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la
Elizabeth Maneno Mkazi wa kijiji cha Itwangi Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga, ametoa kero yake kwa Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro akidai kuwa mume wake amekuwa akimfukuza nyumbani na kutaka kuchukua mali zote baada ya kuoa mke mwingine huku ndoa yao ikiwa na zaidi ya miaka 40 sasa.

Hayo yamejiri katika mkutano ulioitishwa na Mkuu wa wilaya kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi wa kata ya Itwangi ambapo mama huyo amejitokeza na kueleza kuwa mume wake ameuza mali walizotafuta pamoja ikiwemo Ng'ombe, viwanja, mashine pamoja na samani za ndani k**a kabati na makochi.

Elizabeth amesema aliolewa na mume wake ambaye ni mwalimu mstaafu tangu mwaka 1978 na wamekuwa wakikaa pamoja lakini mara baada ya kupata mafao ya kustaafu kazi yake alioa mwanamke mwingine huko Magu na kwa sasa wametumia mali zote huku akitaka kumfukuza aondoke nyumbani licha ya ndugu wa mume wake kumtaka asitoke.

Kutokana na maelezo hayo Mkuu wa wilaya Julius Mtatiro akatoa maagizo kwa mkuu wa Polisi wilaya, pamoja na gavana kumtafuta mume wa mama huyo ambaye kwa sasa yuko Magu kwa mke mdogo na kuletwa mbele yake ili kufanya uchambuzi wa kina ya namna wanavyoishi nyumbani kwa msaada wa mwanasheria wa halmashauri.

SHINYANGA: Pendo Methusela (37) Mkazi wa kata ya Masekelo, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga akituhumiwa ...
26/08/2025

SHINYANGA: Pendo Methusela (37) Mkazi wa kata ya Masekelo, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga akituhumiwa kumjeruhi kwa kumkata na wembe sehemu mbalimbali za mwili wake, Timithoy Magesa (35) na kusababisha kifo chake.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi tukio hilo limetokea Agosti 23, 2025 usiku katika nyumba ya wageni ya Bwashee iliyopo kata ya Ndala Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga.

Kamanda Magomi amebainisha kuwa kabla ya mauaji hayo, Pendo alipigiwa simu na mwanamke mwingine kwa kutumia simu ya marehemu, akimuonya aachane naye kwa madai kwamba ndiye anayempenda na baada ya muda Timothy (marehemu), alimtafuta Pendo na kumtaka wakutane katika nyumba hiyo ya kulala wageni ili wazungumze.

Amesema baada ya kukutana walianza kugombana kuhusu mwanamke aliyempigia simu, hali iliyosababisha Pendo kutumia wembe aliokuwanao kumkata Timothy katika mkono wake wa kushoto pamoja na tumboni hali iliyosababisha kuvuja damu nyingi.

Imeelezwa kutokana na majeraha hayo, marehemu alifariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga, na kueleza kuwa chanzo cha tukio hilo limetokana na wivu wa kimapenzi.

ARUSHA: Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha Justine Masejo amesema wanafanya uchunguzi wa kina kuhusu tukio la kujeruhiwa kw...
26/08/2025

ARUSHA: Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha Justine Masejo amesema wanafanya uchunguzi wa kina kuhusu tukio la kujeruhiwa kwa risasi kijana mmoja katika eneo la Sombetini jijini Arusha usiku wa kuamkia Agosti 24, 2025.

Kamanda Masejo amesema kijana aliyejeruhiwa ametambuliwa kwa jina la Bakari Daud (18), mkazi wa Sombetini, ambaye anadaiwa kupigwa risasi mguuni na Abdulaziz Abubakari (30), maarufu k**a Dogo Janja.

imeelezwa kuwa kijana Bakari, akiwa na mwenzake, alidaiwa kutaka kumvamia Dogo Janja mkazi wa Levolosi, wakati akishuka kwenye gari ambapo katika hali ya kujihami, Abdulaziz (Dogo janja) alitumia silaha aliyokuwa nayo na kumjeruhi Bakari.

Hata hivyo tayari watu wawili wanashikiliwa na jeshi la Polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo, huku hatua za kisheria zikiendelea kuchukuliwa.

MBEYA: Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi...
25/08/2025

MBEYA: Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku Tarehe 25/08/2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.

Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.

NJIKU anatarajia kupambana na Wagombea wengine kutoka vyama mbalimbali akiwemo mgombea wa CCM ambaye ni Spika wa umoja wa mabunge Duniani Dr. Tulia Ackson.

MBEYA: Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini mkoani Mbeya, Dkt. Tulia Ackson tarehe 25 Agosti 2025, amechukua fomu ya...
25/08/2025

MBEYA: Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini mkoani Mbeya, Dkt. Tulia Ackson tarehe 25 Agosti 2025, amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya wananchi wa jimbo jipya la Uyole katika Uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.

Dkt. Tulia amechukua fomu hiyo katika ofisi za tume huru ya Uchaguzi zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya. .ackson

SIKU YA NNE HII LEO "OPERATION WASHA TAA KARAGWE" chini ya Mtumishi wa Mungu Mtume Boniface Mwamposa "Bulldozer " wa Mad...
23/08/2025

SIKU YA NNE HII LEO "OPERATION WASHA TAA KARAGWE" chini ya Mtumishi wa Mungu Mtume Boniface Mwamposa "Bulldozer " wa Madhabahu ya Inuka Uangaze

Unaweza kufuatilia Matangazo ya moja kwa moja kupitia Bomba Fm 104.1 Mhz

MBEYA: Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Wakili msomi Beno Malisa Agosti 22, 2025 amemkabidhi boti moja mpya PB.44 ULINZI Kamanda wa...
23/08/2025

MBEYA: Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Wakili msomi Beno Malisa Agosti 22, 2025 amemkabidhi boti moja mpya PB.44 ULINZI Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga.

Akikabidhi boti hiyo kwa Jeshi Mkoa wa Mbeya, Malisa amelitaka Jeshi hilo kuitumia vizuri boti hiyo katika kuimarisha doria za ziwa nyasa Wilayani Kyela na kutokomeza uhalifu.

Hata hivyo Malisa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura kwa kutimiza ahadi ya kutoa boti kwa ajili ya kuimarisha ulinzi Ziwa Nyasa na kuahidi kuitunza na kuitumia vizuri kwa malengo yaliyokusudiwa.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya SACP Benjamin Kuzaga amesema kuwa Boti hiyo inakwenda kuimarisha ulinzi Ziwa Nyasa kupitia doria za pamoja za Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama, JWTZ, Uhamiaji na TRA.

Ziwa nyasa ni miongoni mwa maziwa makuu nchini ambalo sehemu ya Ziwa hilo ni nchi jirani ya Malawi na Mkoa wa Njombe na Ruvuma hivyo uwepo wa Boti hiyo ni mikakati ya kuimarisha ulinzi na kudhibiti uhalifu wa majini.

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania David Misime amesema Jeshi lipo tayari kuhakikisha amani na utulivu kuelekea uchaguz...
18/08/2025

Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania David Misime amesema Jeshi lipo tayari kuhakikisha amani na utulivu kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.

Hata hivyo amewataka wanaotumia Mitandao ya kijamii vibaya waache mara Moja kwani hawatakuwa salama.

Operation washa taa Kila mkoa moto umewaka jijini MWANZA (KONGAMANO KUBWA LA KESI YAKO IMEKWISHA) .Leo ni siku ya pili a...
15/08/2025

Operation washa taa Kila mkoa moto umewaka jijini MWANZA (KONGAMANO KUBWA LA KESI YAKO IMEKWISHA) .

Leo ni siku ya pili ambapo Mtumishi wa Mungu Mtume mwamposa BULLDOZER wa madhabahu ya inuka uangaze yupo tayari kukuhudumia muda huu

Tune BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

Gusa link hii ujiunganishe kwa Imani ufunguliwe

https://radio.garden/listen/bomba-fm-104-1/rGZunUau

Arise AndShine Tanzania

Address

P O Box 579
Mbeya
255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 00:30

Telephone

+255753451045

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA:

Share

Category