
20/09/2025
DAR ES SALAAM: Mtumishi wa Mungu kutoka madhabahu ya Inuka Uangaze, Mtume Boniface Mwamposa maarufu k**a Bulldozer, amerejea nchini akitokea Brazil ambako alienda kutangaza injili ya Bwana Yesu Kristo.
Katika huduma hiyo aliyoiongoza, amesema Mungu ametenda mambo makuu kwa kuwagusa watu wengi waliokusanyika kusikia neno la wokovu.
Akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere, Mtume Mwamposa amesema watu wa Brazil wamepokea wokovu, wameponywa huku wengine wakifunguliwa vifungo vya kiroho.
Amesema matukio hayo ni ishara ya nguvu ya Mungu inayoendelea kufanya kazi hata katika mataifa ya mbali.
Kurejea kwake kumeambatana na furaha kubwa kwa waumini na wafuasi wake hapa nchini, ambao wameonyesha shukrani kwa kile walichokiita ushindi wa injili na kwamba hatua hiyo ni kielelezo cha kazi ya Mungu kupitia kwa Mtumishi wao.