BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA

BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA BOMBA FM RADIO broadcasting live from MBEYA CITY - TANZANIA.(Iringa,Mbeya,Rukwa,Njombe & Ruvuma). Tus

09/12/2025

Mwandishi wetu Godwill Kamendu ameendelea kutembelea maeneo mbalimbali ya jiji la Mbeya.
Hata hivyo licha ya ukimya uliotawala amefanya mahojiano na mmoja wa wafanyabiashara wa nyama ambaye yeye ameamua kuingia kazini hii leo.

Bomba Fm inakutakia heri ya Uhuru wa Tanzania Bara hii leo Disemba 09,2025 ambapo tunaadhimisha miaka 64 tangu mwaka 196...
09/12/2025

Bomba Fm inakutakia heri ya Uhuru wa Tanzania Bara hii leo Disemba 09,2025 ambapo tunaadhimisha miaka 64 tangu mwaka 1961.

09/12/2025

Tazama hali ilivyo hii leo mapema kabisa asubuhi katika jiji la Mbeya hususani katika maeneo ambayo yamekuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu ikiwemo eneo la Kabwe.

Hii inafuatia kuwepo kwa vuguvugu lililokuwa linaendelea mitandaoni kuhusu maandamano ya disemba 09,2025, ambapo hata hivyo serikali imesema hakuna maandamano yoyote yaliyoratibiwa kisheria.

Mapema leo mwandishi wetu Godwill Kamendu amepita maeneo mbalimbali ya jiji la Mbeya kukujuza hali ilivyo.

08/12/2025

Mtume Mwamposa Aombea Amani kwa Taifa la Tanzania

Dar es Salaam — Mtumishi wa Mungu, Mtume Mwamposa, ameendelea kuliweka Taifa la Tanzania katika maombi, safari hii akiombea amani iendelee kutawala kila kona ya nchi.

Akizungumza wakati wa ibada iliyofanyika Kawe jijini Dar es Salaam, Mtume Mwamposa Aliwataka waumini kuendelea kusimama katika maombi, akisisitiza kuwa amani ni zawadi muhimu inayopaswa kulindwa na kuthaminiwa na Watanzania wote.

08/12/2025

Mtume Mwamposa Aomba Hekima ya Mungu Kutawala Tanzania

Dar es Salaam — Mtume Mwamposa ameomba hekima ya Mungu itawale nchini Tanzania, akisisitiza umuhimu wa amani na umoja wakati wa kipindi hiki.

Kauli hiyo ameitoa katika ibada kubwa iliyofanyika Kawe, jijini Dar es Salaam, na kuhudhuriwa na mamia ya waumini kutoka sehemu mbalimbali za Tanzania.

Katika mahubiri yake, Mtume Mwamposa aliwahimiza waumini kuendeleza maombi kwa ajili ya taifa, akisema hekima ya Mungu ndiyo msingi wa kuongoza nchi katika mwelekeo sahihi.

Mji wa Pemba nchini Msumbiji umegeuka kitovu cha mkutano wa kiroho baada ya Mtume Mwamposa kuanza kongamano lake kubwa l...
06/12/2025

Mji wa Pemba nchini Msumbiji umegeuka kitovu cha mkutano wa kiroho baada ya Mtume Mwamposa kuanza kongamano lake kubwa la injili lililovuta maelfu ya waumini.

Katika mkutano huo uliojaa shangwe, nyimbo za kusifu na mahubiri yenye nguvu, watu mbalimbali walitoa ushuhuda wa kupokea faraja, uponyaji na nguvu mpya za kiroho. Wengine waliangua kilio cha furaha, wengine wakishangilia baada ya kudai kuponywa magonjwa yaliyowasumbua kwa muda mrefu.

Mkutano huu unaokamilika leo umeiweka Pemba kwenye ramani ya matukio makubwa ya kiroho Afrika Mashariki na Kusini, huku watu wakiendelea kumiminika kutoka maeneo ya jirani.

Kwa waliohudhuria, tukio hili wanasema limekuwa “tetemeko la kiroho”—na wengi wakisema, “kesi zao zimekwisha.”

29/11/2025

MBEYA: Mkuu wa Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya Jaffar Haniu amekabidhi hati za hakimiliki za kimila 200 kwa Wananchi wa kijiji cha Itete wilayani Rungwe.

24/11/2025

MBEYA: Wananchi wa maeneo mbalimbali jijini Mbeya wameamka leo asubuhi wakishuhudia hali ya hewa yenye ukungu mzito uliotanda katika mitaa mingi ya jiji.

Ukungu huo umeanza kujitokeza mapema asubuhi na kusababisha baadhi ya shughuli za usafiri kwenda taratibu kutokana na uoni hafifu barabarani.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA.Mnamo Novemba 18, 2025 saa 3:00 asubuhi huko Kitongoji na Kijiji cha Isaka, Kata...
21/11/2025

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA.

Mnamo Novemba 18, 2025 saa 3:00 asubuhi huko Kitongoji na Kijiji cha Isaka, Kata ya Nkunga, Tarafa ya Ukukwe, Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya. Mtoto mwenye umri wa miaka 02 aitwaye Devina Derick Iman aliyekuwa mkazi wa Kitongoji cha Ipoma alinyongwa hadi kufa kwa kutumia Kamba ya Manila na Baba yake mzazi aitwaye Derick Iman Mwangama [23] mkazi wa Kijiji cha Mpandapanda Wilayani Rungwe.

Awali kabla ya tukio, Baba mzazi wa mtoto huyo alikwenda nyumbani kwa mama mzazi wa mtoto aitwaye Violeth Edward [19] Mkazi wa Isaka na kumchukua mtoto huyo kwa nguvu na kisha kutokomea kusikojulikana hadi alipokutwa ameuawa na mwili wake kutelekezwa kando ya Mto Kiwira.

Aidha, baada ya tukio hilo Derick Iman Mwangama naye alijinyonga hadi kufa kwa kutumia Kamba ya Manila kwenye mti wa mparachichi kando kando ya mwili wa mtoto wake.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa kifamilia baina ya wazazi wa mtoto huyo ambao wametengana.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa wazazi kutatua migogoro yao ya kifamilia kwa njia sahihi kwa kushirikisha watu wa karibu na kukaa meza ya mazungumzo ili kupata suluhisho kwa njia ya Amani na kuepusha madhara makubwa k**a haya yaliyotokea.

19/11/2025

DAR ES SALAAM: Mtumishi wa Mungu Mtume Boniface Mwamposa "Bulldozer" ameonesha kukerwa na baadhi ya Wanaume ambao hawajitumi kutafuta maisha na badala yake kutegemea Wanawake waliofanikiwa kifedha.

19/11/2025

DODOMA: Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma limethibitisha kifo cha Emmanuel Mathias Matebe maarufu k**a MC Pilpili mkazi wa Swaswa Jijini Dodoma na Dar es Salaam, ambapo Novemba 16, 2025 marehemu alifariki katika kituo cha Afya Ilazo akiwa anapatiwa matibabu.

Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Dodoma Wiliam Mwanafupa amesema kuwa Kabla ya kufikwa na umauti, msaidizi wa Mc Pilipili Hassan Ismail alipigiwa Simu na watu asiowafahamu na kuomba wakutane na baada ya muda walifika watu watatu asiowafahamu wakiwa na Mc Pilipili ndani ya gari ndogo nyeupe na walimkabidhi akiwa na hali mbaya na wao kuondoka.

Jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi zaidi ili kuwatia nguvuni wale wote waliohusika na tukio hilo.

Address

P O Box 579
Mbeya
255

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 00:30

Telephone

+255753451045

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to BOMBA FM RADIO 104.1 Mhz MBEYA:

Share

Category