Mbeya Press Club

Mbeya Press Club Ukurasa Rasmi Wa Klabu Ya Waandishi Wa Habari Mkoa Wa Mbeya.

31/08/2025

“Nguvu ya pamoja ni muhimu sana katika kufanikisha ulinzi na usalama wa Waandishi wa Habari” - Wakili Onesmo Olengurumwa Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), akizungumza katika Mdahalo wa Kitaifa kuhusu Ulinzi na Usalama wa waandishi wa Habari ulifanyika jiji Dar es Salaam katika Ofisi za UNESCO, leo Agosti 29 2025.

Aidha, Wakili Olengurumwa amemueleza IGP Camilius Wambura ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Mdahalo huo kwamba, Jeshi la Polisi linapaswa kuwalinda Waandishi wa Habari kuelekea katika kipinidi cha Uchaguzi huku akiwaasa Waandishi wa Habari kuzingatia maadili ya uandishi wa habari k**a njia moja wapo ya kukaa katika mstari haki na kujilinda.tanzania






31/08/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC akizungumza kuhusu malengo ya msingi ya Mdahalo wa Kitaifa kuhusu ulinzi na usalama kwa Waandishi wa Habari.

Hata hivyo amesema kuwa msingi wa Midahalo uliyofanywa hapo hawali na jeshi la polisi ndio ambayo imetufikisha hapa leo hata tukaweza kukutana tena katika Ngazi ya Kitaifa.

Mdahalo huu umefanyika leo Agosti 29 katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika la UNESCO jijini Dar es Salaam.tanzania






31/08/2025

Mkuu wa Polisi Tanzania, IGP Camilius Wambura amewahakikishia ulinzi na usalama Waandishi wa Habari katika kipindi hiki cha uchaguzi na baada ya uchaguzi, huku akiahidi Jeshi la Polisi litaendelea kufanya midahalo na waandishi wa Habari katika masuala yanayohusu ulinzi na usalama wao.

IGP Wambura ameeleza hayo wakati akifungua Mdahalo wa kitaifa kuhusu Ulinzi na Usalama wa waandishi wa Habari uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam katika Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Mdahalo huo wa kitaifa ambao umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya UTPC, THRDC na UNESCO ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuwajengea Uwezo Waandishi wa Habari ili Jamii iweze kupata Taarifa, Unaotekelezwa na Umoja wa Klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la International Media Support(IMS) kupitia ufadhili wa Ubalozi wa Uswizi na Umoja wa Ulaya (EU).

Mdahalo huo umehudhuriwa na washiriki zaidi ya 100 kutoka katika Taasisi za Kihabari, Vyombo vya Habari, Waandishi wa Habari, Wahariri, Wawakilishi kutoka taasisi za Serikali, Jeshi la Polisi, Wawakilishi kutoka balozi mbalimbali nchini na wadau wa maendeleo.


tanzania

TAARIFA KWA UMMA
29/08/2025

TAARIFA KWA UMMA

26/08/2025

WALIMU JIMBO LA UYOLE KUPEWA ‘IPHONE MACHO MATATU’

Mgombea Ubunge Jimbo la Uyole Jijini Mbeya kupitia tiketi ya chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Ipyana Njiku jana Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya wananchi wa jimbo hilo katika Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Uyole iliyopo Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Akizungungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi hizo Njiku ametaja baadhi ya vipaumbele vyake kuwa ni pamoja na kuboresha sekta ya elimu nchini kwa kuhakikisha anagawa kompyuta mpakato (Laptop) mashuleni pia kila kila mwalimu wa shule ya msingi na sekondari Jimboni humo atapata simu janja aina ya iPhone macho matatu.

PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINIMwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambay...
25/08/2025

PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ameteuliwa na chama hicho kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA UBUNGE, JIMBO LA UYOLEMwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mko...
25/08/2025

MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA UBUNGE, JIMBO LA UYOLE

Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.

Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press Club.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/08/mwandishi-wa-habari-kuchuana-na-spika.html

CALL FOR CONSULTANCY SERVICE
21/08/2025

CALL FOR CONSULTANCY SERVICE

WALIOTEULIWA KUGOMBEA NAFASI ZA UBUNGE KUPITIA VITI MAALUMU WANAWAKE MKOA WA MBEYA
30/07/2025

WALIOTEULIWA KUGOMBEA NAFASI ZA UBUNGE KUPITIA VITI MAALUMU WANAWAKE MKOA WA MBEYA

WALIOTEULIWA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MAJIMBO YA MKOA WA MBEYAKatibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha ...
29/07/2025

WALIOTEULIWA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MAJIMBO YA MKOA WA MBEYA

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla leo Jumanne Julai 29, 2025 ametangaza majina ya walioteuliwa na CCM kwenda hatua inayofuata ya kura za maoni ya chama hicho.

AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYAWanafunzi watano wa Sekondari ya Chalangwa Wilaya ya Ch...
26/07/2025

AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYA

Wanafunzi watano wa Sekondari ya Chalangwa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wamefariki kwa kugongwa na basi lenye namba za usajili namba T 194 DCE aina ya YUTONG linalomilikwa na Kampuni ya Safina linalofanya safari zake Lualaje Mbeya Julai 26, 2025 majira ya saa 11:30 alfajiri barabara kuu ya Chunya Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.

Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/07/ajali-yaua-wanafunzi-watano-wakikimbia.html

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDEMahak**a Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 145...
10/07/2025

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDE

Mahak**a Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 14538/2025 yaliyofunguliwa mei 17,2025 na Sije Mbughi mke wa Mpaluka Nyagali (Mdude) dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa mash*taka (DPP), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya(RPC), Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) na askari Shaban Charo anayedaiwa kuwa ndiye aliyemchukua Mdude ambapo maombi yameanza kusikilizwa Juni 30, 2025 na kutolewa uamuzi Julai 9, 2025 na Jaji Said Kalunde.

Mleta maombi Sije Mbughi amewakilishwa na Wakili Bonifase Mwabukusi, Wakili Hekima Mwasipu na Wakili Solomon Kamunyu ambapo upande wa wajibu maombi umewakilishwa na Wakili Domick Mushi pamoja na Wakili Adalbert Zegge huku Sije akitaka mumewe kufikishwa mahak**ani na kufungulia mash*taka kwa mujibu wa sheria.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press Club.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/07/mahak**a-yatupilia-mbali-kesi-ya-mdude.html

Address

Sokoine
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbeya Press Club posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbeya Press Club:

Share