Mbeya Press Club

Mbeya Press Club Ukurasa Rasmi Wa Klabu Ya Waandishi Wa Habari Mkoa Wa Mbeya.

WALIOTEULIWA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MAJIMBO YA MKOA WA MBEYAKatibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha ...
29/07/2025

WALIOTEULIWA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MAJIMBO YA MKOA WA MBEYA

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla leo Jumanne Julai 29, 2025 ametangaza majina ya walioteuliwa na CCM kwenda hatua inayofuata ya kura za maoni ya chama hicho.

AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYAWanafunzi watano wa Sekondari ya Chalangwa Wilaya ya Ch...
26/07/2025

AJALI YAUA WANAFUNZI WATANO WAKIKIMBIA MCHAKAMCHAKA, CHUNYA MBEYA

Wanafunzi watano wa Sekondari ya Chalangwa Wilaya ya Chunya Mkoani Mbeya wamefariki kwa kugongwa na basi lenye namba za usajili namba T 194 DCE aina ya YUTONG linalomilikwa na Kampuni ya Safina linalofanya safari zake Lualaje Mbeya Julai 26, 2025 majira ya saa 11:30 alfajiri barabara kuu ya Chunya Mbeya.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya ACP Wilbert Siwa amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambapo wanafunzi watano wamefariki papo hapo na majeruhi tisa wamepokelewa Kituo cha Afya Chalangwa.

Siwa amesema mara baada ya tukio dereva wa basi hilo alitoroka na juhudi za kumtafuta zinaendelea ambapo ametoa wito kwa madereva kuwa waangalifu wawapo barabarani na chanzo kikitajwa ni mwendo kasi na uzembe wa dereva.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/07/ajali-yaua-wanafunzi-watano-wakikimbia.html

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDEMahak**a Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 145...
10/07/2025

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI YA MDUDE

Mahak**a Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya imetupilia mbali maombi ya jinai namba 14538/2025 yaliyofunguliwa mei 17,2025 na Sije Mbughi mke wa Mpaluka Nyagali (Mdude) dhidi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Mkurugenzi wa mash*taka (DPP), Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya(RPC), Mkuu wa upelelezi Mkoa wa Mbeya (RCO) na askari Shaban Charo anayedaiwa kuwa ndiye aliyemchukua Mdude ambapo maombi yameanza kusikilizwa Juni 30, 2025 na kutolewa uamuzi Julai 9, 2025 na Jaji Said Kalunde.

Mleta maombi Sije Mbughi amewakilishwa na Wakili Bonifase Mwabukusi, Wakili Hekima Mwasipu na Wakili Solomon Kamunyu ambapo upande wa wajibu maombi umewakilishwa na Wakili Domick Mushi pamoja na Wakili Adalbert Zegge huku Sije akitaka mumewe kufikishwa mahak**ani na kufungulia mash*taka kwa mujibu wa sheria.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press Club.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/07/mahak**a-yatupilia-mbali-kesi-ya-mdude.html

Gwamaka Mwakambwe akiwa na mke wake baada ya kuchukua na kurejesha fomu kutia nia kugombea ubunge Jimbo la Rungwe.
04/07/2025

Gwamaka Mwakambwe akiwa na mke wake baada ya kuchukua na kurejesha fomu kutia nia kugombea ubunge Jimbo la Rungwe.

MASACHE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE WA JIMBO LA LUPA, CHUNYAMbunge wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka ...
30/06/2025

MASACHE ACHUKUA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE WA JIMBO LA LUPA, CHUNYA

Mbunge wa Jimbo la Lupa Masache Kasaka amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea nafasi ya ubunge wa Jimbo hilo kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM leo Juni 30, 2025.

MWALUNENGE AREJESHA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINIMwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mb...
30/06/2025

MWALUNENGE AREJESHA FOMU YA KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Mbeya Patrick Mwalunenge amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbeya Mjini leo Juni 30, 2025.

MHANDISI MARYPRISCA MAHUNDI ACHUKUA FOMU KUTETEA NAFASI YAKEMhandisi Maryprisca Mahundi amefika katika ofisi za UWT Mkoa...
29/06/2025

MHANDISI MARYPRISCA MAHUNDI ACHUKUA FOMU KUTETEA NAFASI YAKE

Mhandisi Maryprisca Mahundi amefika katika ofisi za UWT Mkoa wa Mbeya kuchukua fomu ya kugombea Ubunge Viti Maalum Mkoa wa Mbeya.

Mhandisi Mahundi amechukua fomu hiyo ili kutetea nafasi yake ambayo ameitumikia muhula mmoja wa miaka mitano (2020-2025).

MWANAHABARI AJITOSA KUMKABILI MEYA WA JIJI LA MBEYAMwandishi wa Habari, David Nyembe (kushoto), akikabidhiwa fomu ya kuo...
29/06/2025

MWANAHABARI AJITOSA KUMKABILI MEYA WA JIJI LA MBEYA

Mwandishi wa Habari, David Nyembe (kushoto), akikabidhiwa fomu ya kuomba ridhaa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Isanga kuchaguliwa kuwa mgombea udiwani wa Kata hiyo katika Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba mwaka huu.

Nyembe amekabidhiwa fomu na Katibu wa CCM Kata hiyo Golden Ndolela leo Juni 29, 2025.

Hadi kufikia leo majira ya saa nne asubuhi jumla ya wagombea watatu tayari wamechukua fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kuwania nafasi hiyo akiwemo aliyekuwa Meya wa Jiji la Mbeya Mh. Dormohamed Issa.

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA MATIBABU YA MACHO KWA WATOTOHospitali ya Rufaa ya Kanda Mb...
20/06/2025

HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA MBEYA YAPOKEA MSAADA WA VIFAA VYA MATIBABU YA MACHO KWA WATOTO

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya (MZRH) imepatiwa msaada wa vifaa tiba, vifaa saidizi na mashine ya kisasa ya Ultra Sound kwaajili ya kutoela matibabu ya macho wa watoto wanaofikishwa hospitali kwaajili ya matibabu, venye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100, kutoka kwa Shirika la Kilimanjaro Center for Community Ophthalmology (KCCO) k**a sehemu ya juhudi za kuboresha huduma za matibabu ya macho kwa watoto wa nyanda za juu kusini mwa Tanzania.

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Martin Mutayoba, Mwakilishi wa Shirika la KCOO Nyanda za Juu Kusini, amesema kuwa shirika hilo limekuwa likifanya kazi kwa karibu na hospitali (MZRH) kwa huduma za matibabu ya macho pia kupitia huduma mkoba za matibabu ya macho kwa watoto kwa ufanisi zaidi.

Ameongeza kuwa msaada huo ni matokeo ya ushirikiano wanaopatiwa hivyo amewataka watumiaji wa vifaa hivyo kuvihifadhi vizuri ili viendelee kufanya kazi kwa ubora.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press Club.

NJEZA ATEMBELEA WAFIWA AJALI ILIYOUA 29 MLIMA IWAMBIMbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini  Oran M. Njeza, amezitembele na ku...
18/06/2025

NJEZA ATEMBELEA WAFIWA AJALI ILIYOUA 29 MLIMA IWAMBI

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini Oran M. Njeza, amezitembele na kutoa mkono wa pole kwa familia za watu 29 waliofariki na majeruhi wa ajali.

Ajali hiyo ilitokea Juni 7, 2025 katika mtelemko mkali wa mlima Iwambi Wilaya ya Mbeya, baada ya ya lori lilokuwa limebeba shehena za unga kugonga magari mawili yakiwepo ya abiria.

Katika ajali hiyo watu 28 walipoteza maisha papo hapo na wengine tisa kujeruhiwa na kukimbizwa katika Hosptali Teule ya Ifisi Wilaya ya Mbeya.

Soma zaidi kupitia blog ya Mbeya Press Club.

Taarifa kwa wanahabari Mkoa wa Mbeya
13/06/2025

Taarifa kwa wanahabari Mkoa wa Mbeya

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYAMkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehama...
05/05/2025

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehamasisha wananchi kutumia fursa ya ujio wa Madaktari Bingwa Bobezi wa Dkt Samia kufanyiwa vipimo vya uchunguzi wa magonjwa.

Kambi ya madaktari bingwa bobezi imeanza leo Mei 5 mpaka Mei 9, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) kwa muda wa siku tano.

Amesema huduma hizo zitawanufaisha wananchi kutoka mikoa Nyanda za Juu Kusini ikiwepo Mbeya, Ruvuma Songwe, Songea Njombe.

Soma zaidi...
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/05/dc-malisa-wananchi-changamkieni-fursa.html

Address

Sokoine
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbeya Press Club posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbeya Press Club:

Share