Mbeya Press Club

Mbeya Press Club Ukurasa Rasmi Wa Klabu Ya Waandishi Wa Habari Mkoa Wa Mbeya.

Taarifa kwa wanahabari Mkoa wa Mbeya
13/06/2025

Taarifa kwa wanahabari Mkoa wa Mbeya

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYAMkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehama...
05/05/2025

DC MALISA: WANANCHI CHANGAMKIENI FURSA UJIO MADAKTARI BINGWA BOBEZI 36 MBEYA

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Beno Malisa, amehamasisha wananchi kutumia fursa ya ujio wa Madaktari Bingwa Bobezi wa Dkt Samia kufanyiwa vipimo vya uchunguzi wa magonjwa.

Kambi ya madaktari bingwa bobezi imeanza leo Mei 5 mpaka Mei 9, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya (Mbeya RRH) kwa muda wa siku tano.

Amesema huduma hizo zitawanufaisha wananchi kutoka mikoa Nyanda za Juu Kusini ikiwepo Mbeya, Ruvuma Songwe, Songea Njombe.

Soma zaidi...
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/05/dc-malisa-wananchi-changamkieni-fursa.html

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAKANUSHA KUMKAMATA MDUDEJeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lakanusha taarifa zinazosambaa katik...
02/05/2025

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAKANUSHA KUMKAMATA MDUDE

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya lakanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii zikidai Askari Polisi kuhusika na tukio la kuk**atwa kwa Mpaluka Said Nyagali maarufu k**a Mdude.

Soma zaidi...
https://www.youtube.com/watch?v=MiKuUOBac6Y

MADAKTARI BINGWA BOBEZI WA SAMIA KUWEKA KAMBI HOSPTALI YA RUFAA MKOA MBEYAMadaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wanatara...
02/05/2025

MADAKTARI BINGWA BOBEZI WA SAMIA KUWEKA KAMBI HOSPTALI YA RUFAA MKOA MBEYA

Madaktari bingwa bobezi wa Mama Samia wanatarajia kuweka kambi ya siku tano ya kufanya uchunguzi wa magonjwa mbalimbali katika Hosptali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Kambi hiyo imeratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Hosptali ya Rufaa kanda ya nyanda za juu kusini katika mikoa ya Songwe, Njombe, Songwe na Mbeya .

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 2, 2025, Mganga mfawidhi wa Hosptali ya Rufaa Mkoa wa Mbeya Dkt. Abdallah Mmbaga amesema kambi hiyo itaanza Mei 5 mpaka 9 mwaka huu.

Soma zaidi kupitia blog ya Mbeya Press Club.

JOWUTA, THRDC WALAANI WANAHABARI KUKAMATWA NA KUPIGWAChama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) na...
26/04/2025

JOWUTA, THRDC WALAANI WANAHABARI KUKAMATWA NA KUPIGWA

Chama cha Wafanyakazi katika Vyombo vya Habari Tanzania (JOWUTA) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binaadamu nchini (THRDC) wamelaani kuanza kuibuka matukio ya waandishi wa habari na watangazaji kuk**atwa na baadhi kupigwa na hata kuharibiwa vifaa vyao vya kazi na vyombo vya dola.

Kauli ya kulaani imetolewa leo Aprili 25 mwaka huu na Mwenyekiti wa JOWUTA M***a Juma leo mkoani Mbeya, wakati wa mafunzo kwa wanahabari kuhusu uandishi wa habari za uchaguzi, ulinzi na usalama kazini.

Mafunzo hayo yamehusisha waandishi kutoka mikoa ya Mbeya, Iringa na Njombe, ambapo Juma amesema matukio ya kuk**atwa, kupigwa na kuharibiwa vitendea kazi hayakubaliki katika nchi inayojinadi kuwa inazingatia misingi ya kidemokrasia.

Soma zaidi kupitia blog ya Mbeya Press Club.

Mada: Mzazi/ Mlezi afanye nini ili kumlinda mtoto wake dhidi ya ukatili wa kingono?Maoni yako yatasomwa kupitia 104.1 Bo...
21/04/2025

Mada: Mzazi/ Mlezi afanye nini ili kumlinda mtoto wake dhidi ya ukatili wa kingono?

Maoni yako yatasomwa kupitia 104.1 Bomba FM.











“KWENYE UCHAGUZI HUU TUWE WATU WA KUSAMEHEANA” ASKOFU PANGANI Katika kuadhimisha Sikukuu ya Pasaka, Askofu wa Kanisa la ...
20/04/2025

“KWENYE UCHAGUZI HUU TUWE WATU WA KUSAMEHEANA” ASKOFU PANGANI

Katika kuadhimisha Sikukuu ya Pasaka, Askofu wa Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la kusini magharibi Robert Pangani amewataka waumini, viongozi wa serikali na dini kuwa na moyo wa msamaha k**a ambavyo Mungu alivyousamehe ulimwengu kupitia Yesu Kristo aliyekufa na kufufuka kwa ajili ya mwanadamu.

Wito huo ameutoa katika maadhimisho ya ibada ya Sikukuu ya Pasaka iliyofanyika katika kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi Ushirika wa Ibala ulipo Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Soma zaidi kupitia blog ya Mbeya Press Club.

Heri Ya Sikukuu Ya Pasaka🔔⛪️
20/04/2025

Heri Ya Sikukuu Ya Pasaka🔔⛪️

Tunakutakia Ijumaa Kuu Njema🙏🏾🔔⛪️
18/04/2025

Tunakutakia Ijumaa Kuu Njema🙏🏾🔔⛪️

"TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI, ILA TUNATAKA MABADILIKO HAYA" CHAUMMAPamoja na kuthibitisha kushiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu...
09/04/2025

"TUPO TAYARI KWA UCHAGUZI, ILA TUNATAKA MABADILIKO HAYA" CHAUMMA

Pamoja na kuthibitisha kushiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu, Chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kimependekeza na kuishauri Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi baadhi ya mambo kufanyiwa marekebisho kabla ya zoezi hilo.

Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi Mkuu Oktoba 25 mwaka huu kuwapata madiwani, wabunge na Rais, huku Chama hicho kikitarajia kusimamisha wagombea katika nafasi zote.

Soma zaidi kupitia blog ya Mbeya Press Club.

Tanzania Malezi Summit 2025 -MMMAM         @
05/04/2025

Tanzania Malezi Summit 2025

-MMMAM





@

Eid Mubarak 🕌
30/03/2025

Eid Mubarak 🕌

Address

Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbeya Press Club posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbeya Press Club:

Share