Mbeya Press Club

Mbeya Press Club Ukurasa Rasmi Wa Klabu Ya Waandishi Wa Habari Mkoa Wa Mbeya.

Pumzika kwa amani Kelvin Lameck
05/11/2025

Pumzika kwa amani Kelvin Lameck

27/10/2025

Askofu Mkuu wa Kanisa la General Mission Center Limited (GMCL) Nabii David Mpanji amewaasa watanzania wote kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura siku ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano Oktoba 29, 2025.

27/10/2025
23/10/2025

‘MAANDAMANO NA VURUGU VISEPEWE NAFASI SIKU NA BAADA YA UCHAGUZI’ VIONGOZI WA DINI

Jumuiya ya Maridhiano na Amani wa Mikoa Nyanda za Juu Kusini imewaasa wananchi kutokutoa nafasi ya kufanya maandamano na vurugu siku na baada ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA UYOLE AFANYA KAMPENI MGUU KWA MGUUMgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa...
12/10/2025

MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA UYOLE AFANYA KAMPENI MGUU KWA MGUU

Mgombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Ipyana Samson Njiku, ameendelea na kampeni zake za mguu kwa mguu kwa wananchi wa Jimbo la Uyole, ambapo leo ametembelea maeneo ya Kata ya Itezi na Igawilo akiwahamasisha wananchi kujiandaa kwa mabadiliko chanya kupitia uongozi makini na wenye dira ya maendeleo.

Akizungumza na wananchi katika maeneo mbalimbali , Njiku amesema kuwa endapo atapata ridhaa ya wananchi wa Uyole, ataweka kipaumbele katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo:

Ujenzi wa Soko la Kisasa na Kimataifa litakalowezesha wakulima na wafanyabiashara kuuza mazao yao ndani na nje ya nchi kwa urahisi, kuongeza ajira na kipato cha wananchi.

Soma zaidi kupitia blog ya Mbeya Press Club.

31/08/2025

“Nguvu ya pamoja ni muhimu sana katika kufanikisha ulinzi na usalama wa Waandishi wa Habari” - Wakili Onesmo Olengurumwa Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), akizungumza katika Mdahalo wa Kitaifa kuhusu Ulinzi na Usalama wa waandishi wa Habari ulifanyika jiji Dar es Salaam katika Ofisi za UNESCO, leo Agosti 29 2025.

Aidha, Wakili Olengurumwa amemueleza IGP Camilius Wambura ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Mdahalo huo kwamba, Jeshi la Polisi linapaswa kuwalinda Waandishi wa Habari kuelekea katika kipinidi cha Uchaguzi huku akiwaasa Waandishi wa Habari kuzingatia maadili ya uandishi wa habari k**a njia moja wapo ya kukaa katika mstari haki na kujilinda.tanzania






31/08/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa UTPC akizungumza kuhusu malengo ya msingi ya Mdahalo wa Kitaifa kuhusu ulinzi na usalama kwa Waandishi wa Habari.

Hata hivyo amesema kuwa msingi wa Midahalo uliyofanywa hapo hawali na jeshi la polisi ndio ambayo imetufikisha hapa leo hata tukaweza kukutana tena katika Ngazi ya Kitaifa.

Mdahalo huu umefanyika leo Agosti 29 katika Ukumbi wa Mikutano wa Shirika la UNESCO jijini Dar es Salaam.tanzania






31/08/2025

Mkuu wa Polisi Tanzania, IGP Camilius Wambura amewahakikishia ulinzi na usalama Waandishi wa Habari katika kipindi hiki cha uchaguzi na baada ya uchaguzi, huku akiahidi Jeshi la Polisi litaendelea kufanya midahalo na waandishi wa Habari katika masuala yanayohusu ulinzi na usalama wao.

IGP Wambura ameeleza hayo wakati akifungua Mdahalo wa kitaifa kuhusu Ulinzi na Usalama wa waandishi wa Habari uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam katika Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Mdahalo huo wa kitaifa ambao umeandaliwa kwa ushirikiano kati ya UTPC, THRDC na UNESCO ni sehemu ya utekelezaji wa Mradi wa Kuwajengea Uwezo Waandishi wa Habari ili Jamii iweze kupata Taarifa, Unaotekelezwa na Umoja wa Klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la International Media Support(IMS) kupitia ufadhili wa Ubalozi wa Uswizi na Umoja wa Ulaya (EU).

Mdahalo huo umehudhuriwa na washiriki zaidi ya 100 kutoka katika Taasisi za Kihabari, Vyombo vya Habari, Waandishi wa Habari, Wahariri, Wawakilishi kutoka taasisi za Serikali, Jeshi la Polisi, Wawakilishi kutoka balozi mbalimbali nchini na wadau wa maendeleo.


tanzania

TAARIFA KWA UMMA
29/08/2025

TAARIFA KWA UMMA

26/08/2025

WALIMU JIMBO LA UYOLE KUPEWA ‘IPHONE MACHO MATATU’

Mgombea Ubunge Jimbo la Uyole Jijini Mbeya kupitia tiketi ya chama Cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Ipyana Njiku jana Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya wananchi wa jimbo hilo katika Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Uyole iliyopo Halmashauri ya Jiji la Mbeya.

Akizungungumza na waandishi wa habari nje ya ofisi hizo Njiku ametaja baadhi ya vipaumbele vyake kuwa ni pamoja na kuboresha sekta ya elimu nchini kwa kuhakikisha anagawa kompyuta mpakato (Laptop) mashuleni pia kila kila mwalimu wa shule ya msingi na sekondari Jimboni humo atapata simu janja aina ya iPhone macho matatu.

PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINIMwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambay...
25/08/2025

PATRIC MWALUNENGE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE MBEYA MJINI

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ameteuliwa na chama hicho kugombea nafasi ya ubunge wa jimbo la Mbeya Mjini leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA UBUNGE, JIMBO LA UYOLEMwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mko...
25/08/2025

MWANDISHI WA HABARI KUCHUANA NA SPIKA TULIA UBUNGE, JIMBO LA UYOLE

Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma Taifa, Ipyana Samson Njiku, leo Agosti 25, 2025 amechukua fomu ya kugombea ubunge wa Jimbo la Uyole kupitia chama hicho.

Ipyana amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira yake ya kuwatumikia wananchi wa Uyole kwa uadilifu, uwajibikaji na kusimamia maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Amesisitiza kuwa chama chake kimejipanga kutoa mbadala mpya wa kiuongozi unaolenga kuleta matumaini mapya kwa wananchi.

Soma zaidi kupitia Blog ya Mbeya Press Club.
https://mbeyapresstv.blogspot.com/2025/08/mwandishi-wa-habari-kuchuana-na-spika.html

Address

Sokoine
Mbeya

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mbeya Press Club posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mbeya Press Club:

Share