08/05/2026
Anaitwa RAMADHANI CHOBWEDO.
Sijuwi kwanini lakini ila ndo hivyo nasikia SIMBA SC wamemsajili CHOBWEDO na wameshamaliza nae ila nataka kuongea kitu kwamba hawa wachezaji wanaowika kwenye hizi timu za chini au za level ya kati hasa watanzania hawa, wakisajiliwa kwenye hizi timu kubwa Huwa wanapotea sana .
Mfano mzuri KARABAKA,SALAMBA CHIKOLA,na wengine wengi tu huwa wanapotea sana ,hii ni Kwa sababu wapokuwa kwenye timu zenye presha ndogo Huwa wanakuwa comfortable sana hata wakifanya makosa,mfano wakikosa goli huwa haichukuliwi Kwa uzito sana kwa hakuna anaewapa presha hiyo ila badala yake wanapata backup nzuri kutoka Kwa makocha na kuwafanya wajiamini na kuongeza bidii ya kupambana .
Sasa hii haitokei wanapokuja timu hizi kubwa,huku watu wanataka ugeuka malaika yaani kila kitu ufanye Kwa usahihi ukikosea kidogo tu ,full matusi mara presha nyingi kutoka Kwa Mashabiki,sasa hii haiwi afya Kwa Mchezaji yaani badala mmtengeneze ndo kwanza mnampoteza.
Mfano mzuri MWANENGO Kuna siku alikosa nafasi sikumbuki vizuri ilikuwa game dhidi ya nani mtanikumbusha kwenye comments , baadaya hapo watu walimwandama Kwa maneno mpaka ikabidi kocha asimweke kabisa mpaka juzi alivyoanza kumrudisha kwenye game.
Kelele nyingi ndo zimemwondoa CHIKOLA YANGA SC,watu wanataka afike aanze kuwaka kitu ambacho sio kirahisi hivyo.
Nataka kuamini kwamba k**a OKELO angekuwa mtanzania Kwa kipindi alichopitia pale YANGA SC asingekuwa tena tegemeo pale YANGA SC , ishu ni kwamba tunawavumilia wageni ila wazawa hata hatuna mda nao .
Ndo maana nasema k**a CHOBWEDO anaenda SIMBA SC labda Kwa sababu ya hela ila sioni akipata nafasi ya moja Kwa moja kwenye kikosi Cha kwanza, labda awe backup ya mtu hata akiwa backup ukumbuke SIMBA SC ina mawinga wengi sana na wako vizuri na CHOBWEDO anawazidi mbio tu .
Abaki tu TRA