SokaPlace

SokaPlace Pata Habari za Michezo kila siku kutoka katika vyanzo mbali mbali vya Duniani


Brand Ambassador
Mwanjelwa Agrovetcenter

Kiungo wa Yanga, Duke Abuya, Asaini Mkataba Mpya Hadi 2027Kiungo mahiri wa klabu ya Yanga SC, Duke Abuya, ameongeza mkat...
27/07/2025

Kiungo wa Yanga, Duke Abuya, Asaini Mkataba Mpya Hadi 2027

Kiungo mahiri wa klabu ya Yanga SC, Duke Abuya, ameongeza mkataba mpya utakaomfanya kuendelea kuitumikia timu hiyo ya Jangwani hadi mwaka 2027.

Abuya ambaye amekuwa nguzo muhimu katikati ya dimba tangu alipotua klabuni hapo, ameonyesha kiwango cha juu msimu huu na kuwavutia mashabiki wa Yanga kutokana na ubora wake katika kupiga pasi, kutuliza mchezo na kusaidia safu ya ushambuliaji.


Sponsored by

🏆 MLAPANGILWA CUP – LUdende, Ludewa🔁 Second Leg | Mechi ya LeoFT: Madindo 3️⃣ - 1️⃣ LudendeAgg: Madindo 6️⃣ - 5️⃣ Ludend...
27/07/2025

🏆 MLAPANGILWA CUP – LUdende, Ludewa
🔁 Second Leg | Mechi ya Leo

FT: Madindo 3️⃣ - 1️⃣ Ludende
Agg: Madindo 6️⃣ - 5️⃣ Ludende

✅ Madindo yasonga mbele hadi NUSU FAINALI!

✅ Hatua ya Robo Fainali imekamilika leo kwa timu 4 kutinga Nusu Fainali, nazo ni:

1️⃣ Mkongobaki
2️⃣ Mahanje (Mapogoro)
3️⃣ Maholong’wa
4️⃣ Madindo

📅 Sasa inasubiriwa droo rasmi kujua nani atakutana na nani kwenye michezo ya nusu fainali ambayo inatarajiwa kuanza kuchezwa wikendi ijayo!

🔖 Sponsored by
⚽🔥

Matukio  mbalimbali wakati wa utoaji zawadi za mashindano ya CECAFA yaliyoshirikisha Nchi tatu ikiwa ni sehemu ya maanda...
27/07/2025

Matukio mbalimbali wakati wa utoaji zawadi za mashindano ya CECAFA yaliyoshirikisha Nchi tatu ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya fainali za CHAN 2024

📰 CECAFA 3 Nations TournamentStars Ni Mwendo wa Pointi Tatu!🔚 Full Time:🇹🇿 Tanzania 2️⃣ - 1️⃣ Senegal 🇸🇳⚽️ Wafungaji wa ...
27/07/2025

📰 CECAFA 3 Nations Tournament
Stars Ni Mwendo wa Pointi Tatu!

🔚 Full Time:
🇹🇿 Tanzania 2️⃣ - 1️⃣ Senegal 🇸🇳

⚽️ Wafungaji wa Tanzania:

Sopu

Baka


📢 Sponsored by
📲 |

🟡🟢 RASMI: Klabu ya Yanga SC imetangaza kukamilisha usajili wa kinda mahiri Abubakar Nizar, aliyekuwa akiitumikia Azam FC...
27/07/2025

🟡🟢 RASMI: Klabu ya Yanga SC imetangaza kukamilisha usajili wa kinda mahiri Abubakar Nizar, aliyekuwa akiitumikia Azam FC, kwa mkataba wa miaka mitatu (3).

Chipukizi huyo anaungana na Wananchi kuelekea msimu mpya akiwa na kiu ya mafanikio na kuimarisha safu ya kikosi cha mabingwa hao wa kihistoria.

Abubakar Nizar ni Mwananchi 👊💚💛


Sponsored by

ASANTE JONATHAN SOWAH👉Kutoka Uongozi wa Singida BS unawataarifu mashabiki, wapenzi na wadau wote wa soka kuwa umeridhia ...
27/07/2025

ASANTE JONATHAN SOWAH

👉Kutoka
Uongozi wa Singida BS unawataarifu mashabiki, wapenzi na wadau wote wa soka kuwa umeridhia Simba SC kumsajili mchezaji wetu tegemeo Jonathan Sowah kwa uhamisho wa kudumu kwa MAKUBALIANO MAALUM.

Makubaliano haya yamefikiwa baina ya Mlezi wa Singida BS na Rais wa Heshima wa Simba SC pamoja na uongozi wa vilabu hivi.

Tunamtakia Jonathan Sowah kila la heri katika changamoto mpya na tunamshukuru kwa kuitumikia vyema klabu yetu katika kipindi chote alichokuwa nasi.

Imetolewa na Uongozi wa Klabu
Idara ya Habari na Mawasiliano
Singida Black Stars SC
27 Julai 2025

Magazeti Michezo Leo   Sponsored by
27/07/2025

Magazeti Michezo Leo


Sponsored by

Ukiwa Kijana, kuwa Mfano wa Kuigwa!K**a kijana wa taifa hili, unapaswa kuwa mfano bora kwa vijana wenzako—kuwapa sababu ...
27/07/2025

Ukiwa Kijana, kuwa Mfano wa Kuigwa!

K**a kijana wa taifa hili, unapaswa kuwa mfano bora kwa vijana wenzako—kuwapa sababu ya kuamini kuwa mafanikio yanawezekana, hatua kubwa zinaweza kupigwa, na ndoto zinaweza kutimia.

Klabu ya Yanga SC imempata kijana wa mfano—Hersi Said. Kiongozi kijana ambaye amekuwa chachu ya mabadiliko makubwa katika tasnia ya soka nchini Tanzania. Ameonyesha kuwa vijana wakipewa nafasi, wakaaminiwa, na kuungwa mkono, wanaweza kupeleka taifa hili mbali katika sekta mbalimbali.

Hersi, wewe ni shujaa. Wewe ni kielelezo cha uthubutu, maono, na mapenzi ya kweli kwa taasisi unayoiongoza. Endelea kuupiga mwingi—Tanzania inakuona, na Yanga SC inaendelea kufaidika na uongozi wako wa mfano.

Leo unatimiza miaka kadhaa tangu kuzaliwa kwako. Tunamuomba Mwenyezi Mungu azidi kukulinda, kukuongoza na kukutunza katika safari yako ya maisha. Wananchi wa Yanga SC na Watanzania kwa ujumla, tunajivunia kuwa na kiongozi kijana k**a wewe.

Leo dunia inaitazama Tanzania kwa namna tofauti. Dunia inaitazama Yanga SC k**a klabu kubwa, imara na yenye maono—na yote haya ni matokeo ya uongozi wako makini na thabiti.


Enjoy Your Birthday Rais Wa Kabumbu 🎂🎂
Endelea kuwa mwanga kwa kizazi cha sasa na kijacho.

🔵 Rasmi: Azam FC Yamtangaza Kocha Msaidizi MpyaKlabu ya Azam FC imemtangaza Kocha Addis Worku 🇪🇹 kutoka Ethiopia kuwa Ko...
26/07/2025

🔵 Rasmi: Azam FC Yamtangaza Kocha Msaidizi Mpya

Klabu ya Azam FC imemtangaza Kocha Addis Worku 🇪🇹 kutoka Ethiopia kuwa Kocha Msaidizi wa kikosi hicho.

Worku ataungana na Kocha Mkuu Florent Ibenge, kuendelea kuimarisha benchi la ufundi la matajiri hao wa Chamazi katika maandalizi ya msimu mpya.

📌
Sponsored by

26/07/2025

Shabiki maarufu wa Simba SC, Mandala, atoa kauli ya kushangaza

"Niko tayari kuvaa jezi ya Yanga kwa siku moja, mbele ya mashabiki, k**a Simba haitafanikiwa kumsajili Faisal Salum 'Fei Toto' kutoka Azam FC katika dirisha hili la usajili."

Mandala, anayejulikana kwa mapenzi yake makubwa kwa klabu ya Simba SC, amesema ana imani kubwa kuwa uongozi wa Simba hautakubali kumpoteza Fei Toto ambaye kwa sasa yupo Azam FC, lakini anahusishwa kwa karibu na Simba.

Ameongeza kuwa Fei Toto ni mchezaji mwenye kipaji kikubwa na uzoefu wa kutosha ndani ya Ligi Kuu, na kwamba kumsajili itakuwa hatua kubwa kwa Simba kurejesha uimara wa kiungo.

Hata hivyo, kauli yake imezua mijadala mitandaoni huku baadhi ya mashabiki wakiona ni kujitwisha presha isiyo ya lazima wakati mchakato wa usajili bado unaendelea kwa siri kubwa.

> "Simba ni kubwa, na natumaini wataonyesha ubora wao kwenye dirisha hili. K**a tukimkosa Fei Toto, basi nitavaa hiyo jezi ya Yanga k**a nilivyoahidi," alisema Mandala kwa kujiamini.


(Sponsored by

🟢 AMKA NA HIZI kutoka SOKAPLACE ⚽🔊 Habari Moto Moto za Soka la Bongo na CHAN 2025🔵 Baraka Maranyingi Aongeza Mkataba Mbe...
26/07/2025

🟢 AMKA NA HIZI kutoka SOKAPLACE ⚽

🔊 Habari Moto Moto za Soka la Bongo na CHAN 2025

🔵 Baraka Maranyingi Aongeza Mkataba Mbeya City

Klabu ya Mbeya City imefanya maamuzi mazito kwa kumwekea mezani mkataba mpya beki wao tegemeo, Baraka Maranyingi, aliyesaidia kuipandisha timu hiyo Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

🔴 Simba SC Yaimarisha Ngome – Hussein Abeli Asaini Tena

Licha ya tetesi, Klabu ya Simba haina mpango wa kumuacha golikipa wake mahiri Hussein Abeli, ambaye sasa ameongeza mkataba mpya.

⚫ Ismaily Mgunda Arudi Nyumbani – Mashujaa FC

Baada ya kuachana na AS Vita ya DR Congo, kiungo Ismaily Mgunda amerudi kwenye klabu yake ya zamani Mashujaa FC ya Kigoma k**a mchezaji huru.

🔴⚪ Davis Charles Semfuko Ajiunga na Simba SC

Kikosi cha Simba SC kinazidi kuimarika baada ya kiungo wa Coastal Union, Davis Charles Semfuko, kukamilisha uhamisho kujiunga na Wababe hao wa KariaKoo.

⚪ Pamba FC Yaitafuta Saini ya Faria Odongo

Klabu ya Pamba FC ya Jiji iko mbioni kumsajili mlinzi Faria Odongo kutoka Singida Black Stars. Usajili huu utaiimarisha safu ya ulinzi ya Pamba kuelekea msimu mpya.

🟡🟢 Yanga SC Yamkabidhi Jezi Namba 8 – Lassine Kouma Atua

Yanga SC imemtangaza rasmi Lassine Kouma kutoka Stade Malien ya Mali k**a mrithi wa jezi namba 8.

🟣 JKT Tanzania Yatoa Thank You kwa wachezaji hawa hapa

Sixtus Sabilo
Ismail Aziz Keder
Matheo Anthony
George Wawa
Ismail Saleh
Siraji Juma
Martin Kigi

🟢 Aliyekuwa mkurugenzi wa ufundi na kocha msaidizi wa Yanga, Abdulhamid Moalin, hatakuwa sehemu ya benchi msimu ujao. Nafasi yake inatarajiwa kuchukuliwa na Paul Matthews (53), ambaye atatangazwa rasmi hivi karibuni.

🌍Mashindano ya CHAN 2025 yanakaribia Kiingilio cha chini kwa mashabiki kitakuwa ni Shilingi 2,000 kwa mzunguko

💰 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, ameahidi

Tsh Milioni 10 kwa kila goli la Taifa Stars hatua ya makundi Milioni 20 kwa kila goli hatua ya nusu fainali Bonasi ya Milioni 200 ikifika nusu fainali Milioni 500 ikifika fainali Na BILIONI 1 iwapo Taifa Stars watatwaa taji

🙏 Special thanks kwa Mbeya, wadhamini wetu wa muda wote.

Address

Mapumulo

Telephone

+255753201831

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SokaPlace posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SokaPlace:

Share