SokaPlace

SokaPlace Pata Habari za Michezo kila siku kutoka katika vyanzo mbali mbali vya Duniani


Brand Ambassador
Mwanjelwa Agrovetcenter
(1)

06/06/2026

🗣️ Mshambuliaji wa Tanzania Prisons, Geoffrey Manyasi, amesema kwa sasa akili na nguvu za wachezaji wote zimeelekezwa kwenye michezo mitano iliyobaki msimu huu, ambayo itaamua hatma ya timu hiyo kubaki katika Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ameeleza kuwa kila mchezo uliosalia ni muhimu kwao na wanapambana kuhakikisha wanakusanya pointi za kutosha ili kujiweka salama dhidi ya hatari ya kushuka daraja.

06/06/2026

🎙️ Afisa Habari wa Tanzania Prisons, Alexander Ngelela, amesema uongozi wa klabu hiyo umeamua kuwaongezea hamasa wachezaji kwa kuwaahidi bonasi nono katika michezo mitano iliyobaki ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Ngelela amesema bonasi hiyo ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha timu inapambana kwa nguvu zote katika mechi zilizosalia ili kujinusuru na hatari ya kushuka daraja. Kwa sasa Tanzania Prisons ipo kwenye vita ya kusaka pointi muhimu katika hatua za mwisho za msimu.

"Uongozi umeweka mazingira mazuri kwa wachezaji na umeahidi bonasi nzuri ili kuongeza morali na ari ya kupambana katika michezo iliyobaki. Kila mmoja anatambua umuhimu wa mechi hizi kwa mustakabali wa klabu," amesema Ngelela.

Tanzania Prisons inakabiliwa na michezo muhimu ya mwisho ya ligi ambayo itaamua hatma yao ya kubaki Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao.


Sponsored by

Naibu Waziri Mwinjuma Aridhishwa na Ufungaji Viti MkwakwaniSerikali  itaendelea kuboresha viwanja mbalimbali vya michezo...
06/06/2026

Naibu Waziri Mwinjuma Aridhishwa na Ufungaji Viti Mkwakwani

Serikali itaendelea kuboresha viwanja mbalimbali vya michezo nchini ili viweze kutumika katika michuano ya kimataifa hata baada ya Mashindano ya Kombe la Mataifa Afrika mwaka 2027 (AFCON 2027).

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma, mara baada ya kutembelea na kukagua usimikaji wa Viti katika Uwanja wa CCM Mkwakwani, jijini Tanga

Mhe. Mwinjuma ameupongeza Uongozi wa uwanja huo chini ya Meneja Nassoro Makau, kwa kufanya ubunifu mkubwa wa kuvipanga vizuri viti kwa rangi, ikiwa ni viti vilivyotolewa na Serikali katika uwanja wa Benjamin Mkapa, hatua inayoupendezesha uwanja huo wa kihistoria.

Amesema, uboreshaji wa viwanja vya michezo nchini ni sehemu ya maono ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye Serikali yake ya Awamu ya Sita imewekeza kwa kiwango cha hali ya juu katika ukarabati wa viwanja k**a Uhuru na Mkapa, pamoja na ujenzi wa uwanja mpya wa kisasa Arusha.

"Zoezi la usimikaji wa viti hapa Mkwakwani limefanyika kwa ukamilifu mkubwa. Serikali kwa kushirikiana na wadau itaona namna ya kukamilisha sehemu iliyobaki kadiri rasilimali zitakavyopatikana. Nawaomba wananchi na wapenda michezo kutunza miundombinu hii na kuepuka uharibifu ili viwanja vyetu viwe endelevu," amesisitiza Mwinjuma.

Ametoa wito kwa sekta binafsi na wadau mbalimbali wa soka nchini kujitokeza kushirikiana na Serikali ili kuweka nguvu ya pamoja katika kukamilisha maeneo madogo yaliyobaki uwanjani hapo ili kuendana na kasi ya soko la soka la kisasa duniani.

Akiwasilisha taarifa ya ukarabati huo, Meneja wa Uwanja wa CCM Mkwakwani, Nassoro Makau, alisema kuwa katika awamu ya kwanza, Serikali iliwaletea jumla ya viti 6,500 ambavyo vimeshafungwa kikamilifu, huku kukiwa na upungufu wa viti 2,500 ili kukamilisha maeneo yote.

Makau alifafanua kitalamu kuwa viti hivyo vimeshafungwa kwenye Jukwaa Kuu (Main Stand), jukwaa la Reli Moja na Reli Mbili, huku jukwaa maarufu la "Urusi" likiwa ndilo eneo pekee lililobaki ambalo halijafungwa viti kwa sasa. Baada ya ukarabati huu, uwezo wa uwanja huo sasa utakuwa ni kubeba watazamaji 9,000 waliokaa kwenye viti.

06/06/2026

Haya Hapa Magazeti Yote Michezo Leo

⚽Kamata Matokeo ya Kandanda JanaWORLD: Friendly InternationalFT Czech Republic 3-1 GuatemalaFT Mexico 5-1 SerbiaFT Qatar...
06/06/2026

⚽Kamata Matokeo ya Kandanda Jana

WORLD: Friendly International
FT Czech Republic 3-1 Guatemala
FT Mexico 5-1 Serbia
FT Qatar U20 0-2 Wales U19
FT Serbia U17 2-1 Romania U17
FT Singapore 1-2 China
FT Hong Kong 2-0 Mongolia
FT Thailand 2-2 Kuwait
FT Indonesia 3-0 Oman
FT Belarus U21 2-0 Kazakhstan U21
FT Uzbekistan U23 0-1 Japan U21
FT Russia U21 5-1 Iraq U23
FT USA U20 1-0 Georgia U21
FT Albania U17 1-4 Bulgaria U17
FT Montenegro U21 1-1 Cyprus U21
FT Tajikistan 3-1 India
FT USA U18 0-2 Sweden U18
FT Tunisia U20 1-0 Algeria U20
FT Belarus 4-1 Syria
FT Georgia 2-0 Bahrain
FT USA U21 3-1 Ukraine U21
FT Slovakia 2-2 Montenegro
FT Algeria U23 2-0 Mauritania U23
FT Moldova 2-2 Bulgaria
FT Russia 3-0 Burkina Faso
FT San Marino 1-2 Bangladesh
FT Hungary 2-1 Finland
FT Azerbaijan 0-2 Malta
FT Benin 1-1 Niger
FT Central Africa 1-1 Togo
FT Slovenia U21 1-1 Albania U21
FT Angola 1-1 Mauritania
FT Puerto Rico 0-3 Saudi Arabia
FT Canada 1-1 Ireland
FT Haiti 1-2 Peru

ALGERIA: Ligue 1
FT Khenchela 1-0 Rouisset
FT Mostaganem 2-2 El Bayadh
FT Paradou 0-2 ES Setif
FT MC Alger 2-0 A*O Chlef
FT Kabylie 0-0 CR Belouizdad
FT Saoura 3-1 Constantine

📅 Kamata Ratiba ya Kandanda Leo

WORLD: Friendly International
07:30 Vanuatu vs Fiji
14:30 Myanmar vs Guam
16:00 Belgium vs Tunisia
17:00 Armenia vs Kazakhstan
17:30 Kyrgyzstan vs Palestine
18:00 Ethiopia vs Malawi
19:00 Sierra Leone vs Liberia
20:00 British Virgin Islands vs Bonaire
20:00 Gibraltar vs Cayman Islands
20:45 Portugal vs Chile
20:45 Romania vs Wales
21:00 Albania vs Luxembourg
21:30 USA vs Germany
22:00 Panama vs Bosnia & Herzegovina
22:00 Switzerland vs Australia
23:00 Bolivia vs Scotland
23:00 Cape Verde vs Bermuda
23:00 England vs New Zealand
23:00 Qatar vs El Salvador
00:00 Chile U20 vs Brazil U20
00:00 Jamaica vs South Africa
01:00 Brazil vs Egypt
01:00 Venezuela vs Turkey

ALGERIA: Ligue 1
19:00 Olympique Akbou vs Ben Aknoun
20:00 Oran vs USM Alger

DR CONGO: Ligue 1 Championship Group
16:00 Simba vs St Eloi Lupopo
17:00 Aigles du Congo vs AS Vita Club


Photo Credits
Sponsored by

05/06/2026

Mchezaji wa klabu ya Tanzania Prisons, Lambarti Sabiyanka, amesema kwa sasa timu imejipanga vizuri kuhakikisha haishuki daraja, huku akisisitiza kuwa wataingia kwa nguvu zote katika michezo yao ijayo ili kupata matokeo mazuri na kuendelea kubaki Ligi Kuu Bara.
"Tumejipanga vizuri na tupo tayari kupambana katika michezo ijayo. Lengo letu ni kuhakikisha Tanzania Prisons inabaki Ligi Kuu na tutapambana hadi dakika ya mwisho kufikia malengo yetu,"

Amesema Sabiyanka.


Sponsored by

05/06/2026

🗣️ Kocha Mkuu wa Tanzania Prisons, Shadrack Nsajigwa, amesema kikosi chake kinaingia kwenye michezo iliyosalia ya Ligi Kuu kikiwa na kauli mbiu ya "Hatushuki Daraja", huku akisisitiza kuwa kila mchezaji amejipanga kupambana kwa nguvu zote kuhakikisha timu inabaki salama msimu huu.

Nsajigwa amesema ushindani wa ligi ni mkubwa, lakini ana imani na uwezo wa wachezaji wake katika kutafuta matokeo mazuri kwenye mechi zijazo na kutimiza lengo la kubaki Ligi Kuu.

🔥 Kauli mbiu yao kwa sasa ni moja tu: HATUSHUKI!

05/06/2026

Mshambuliaji wa klabu ya Tanzania Prisons, Samson Mbangula, amesema kwa sasa Ligi Kuu Tanzania Bara ina ushindani mkubwa sana, huku akisisitiza kuwa hakuna timu yenye uhakika wa kubaki salama kutokana na tofauti ndogo ya pointi zilizopo kati ya timu nyingi kwenye msimamo wa ligi.

Amesema kila mchezo uliosalia ni muhimu Kwao na wanapaswa kupambana kwa nguvu ili kuhakikisha wanasalia Ligi Kuu Tanzania Bara

Mbangula amewaomba Mashabiki wa klabu Hiyo kuendelea kuwapa sapoti kwani wao ni watu Muhimu Kwenye Timu Yao ya Tanzania Prisons


Sponsored by

Mambo yanaendelea kunonga Uwanja wa Benjamin Mkapa Picha Kwa Hisani ya
05/06/2026

Mambo yanaendelea kunonga Uwanja wa Benjamin Mkapa

Picha Kwa Hisani ya

🔵 RASMI: Azam FC Yaongeza Mkataba wa Florent Ibenge hadi 2028Baada ya kuzagaa kwa tetesi zinazomuhusisha kocha Florent I...
04/06/2026

🔵 RASMI: Azam FC Yaongeza Mkataba wa Florent Ibenge hadi 2028

Baada ya kuzagaa kwa tetesi zinazomuhusisha kocha Florent Ibenge na uwezekano wa kujiunga na Timu ya Taifa ya Mali, Azam FC imeweka wazi msimamo wake kwa kumuongezea mkataba kocha huyo hadi mwaka 2028.

Uamuzi huo unaonesha imani kubwa ambayo klabu hiyo inaendelea kuwa nayo kwa kocha huyo raia wa DR Congo, huku ikisisitiza kuwa ni sehemu muhimu ya mradi wa muda mrefu wa Azam FC kuelekea mafanikio makubwa zaidi.

Ibenge ataendelea kuiongoza Azam FC katika safari ya kutimiza malengo yake ya ndani na kimataifa. 🔥💙


Sponsored by

Address

Mbeya

Telephone

+255753201831

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when SokaPlace posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to SokaPlace:

Share