Wamzi Cosmetics Mbeya

Wamzi Cosmetics Mbeya ✍️UKURASA WA DUKA MTANDAO LA UREMBO NA VIPODOZI ORIGINAL
πŸ‡ΉπŸ‡Ώ BIDHAA ZETU NI:
1. PERFUME
2. VIPODOZI NA
3.

VIFAA VYA SALON

Tupo Mwanjelwa Mbeya Mjini
☎️ 0743 18 1985 au 0742 116 359

KARIBU SANA MTEJA WANGU

14/06/2025

Karibu sana
Kwa mawasiliano 0742116359

Kuna aina mbili za Vita ambazo hutuwia ugumu kujua namna ya kupambana nazoTumekuwa tunatumia Silaha za Kimwili kwenye Vi...
04/06/2025

Kuna aina mbili za Vita ambazo hutuwia ugumu kujua namna ya kupambana nazo

Tumekuwa tunatumia Silaha za Kimwili kwenye Vita ya Kiroho na
Tumekuwa tunatumia Silaha za Kiroho kwenye Vita ya Kimwili

Mungu atufungue Macho ya Rohoni πŸ™πŸΎ

Nawapenda sana

Kivipi sas πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜‚πŸ€£
28/05/2025

Kivipi sas πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜‚πŸ€£

TABIA ZA WATU WALIOKOSA UTU;       Unapopambana kuyafikia mafanikio, watakudharau,  kukupuuza na kukubeza. Wanacho amini...
27/05/2025

TABIA ZA WATU WALIOKOSA UTU;

Unapopambana kuyafikia mafanikio, watakudharau, kukupuuza na kukubeza. Wanacho amini ni kwamba wewe utabaki hivo ulivo, hutafanikiwa.

Ukifikia na ukafanikiwa, hao hao ndio wakwanza kujifanya wanakujua. Ukionesha huna mwitikio juu ya mahitaji yao kwako, watakusema vibaya na kukudhihaki ila hawata kata tamaa ya kuhitaji msaada toka kwako.

Jitahidi usiyakumbuke mabaya ya mtu juu yako, maana ni chachu ya ladha ya maish yako.

Usilipe ubaya kwa Ubaya baali, ushinde ubaya kwa wema.

MUNGU NIPE MWISHO MWEMA πŸ™πŸ™πŸ™

KATIBU MTENDAJI MKUU WA TIMU YA MBEYA CITY FC  AELEZEA MAFANIKIO YA CLUB IKIWA CHAMPIONSHIP NA MIPANGO MADHUBUTI BAADA Y...
26/05/2025

KATIBU MTENDAJI MKUU WA TIMU YA MBEYA CITY FC AELEZEA MAFANIKIO YA CLUB IKIWA CHAMPIONSHIP NA MIPANGO MADHUBUTI BAADA YA KUPANDA LIGI KUU TANZANIA BARA.

Mara baada ya timu ya Mbeya City FC kupanda Daraja, C.E.O wa timu hiyo Ndg. Ally Nnunduma ameambia Greencity TV Online kuwa wakiwa Ligi ya Championship yapo mafanikio walioyoyapata k**a timu.

"Mbeya City FC kwa msimu wa 2024/2025 tukiwa kwenye mapambano ya kutaka kupanda Ligi Kuu, tunamshukuru Mungu tumepanda moja kwa moja tukiwa nafasi ya Pili kwa Point 68 nyuma ya Mtibwa wenye Point 71. Niwapongeze Wachezaji, Benchi na mashabiki pia kwakuwa kwanza tumepoteza mechi mbili tu ligi nzima, tumeshinda mechi 8 za Away na tumefanikiwa kwa vinara wa Magoli 68 huku anaetufuatia akiwa na magoli 58. Hatukuishia hapo kwakuwa sisi ndiyo timu pekee Championship, tumekuwa na mashabiki wengi kwenye mechi zetu kuliko timu yoyote kwenye Ligi hiyo."

"Sasa tumerejea Ligi Kuu tunazidi kusisitiza kuwa kwenye mji wao kuna kijiji chetu, tunaongeza kuwa sasa tutaenda kuwa na vijiji vyetu kwenye kila mji. K**a kulikuwa kijiji kimoja sasa vitakuwa kumi zaidi, hivyo tumejipanga vizuri sana. Kurejea kwetu Ligi Kuu ni kuwa tunaelewa changamoto zote na mahitaji yote muhimu, hivyo tutahakikisha hatusogei kwenye hatari ya kucheza Play Off kabisa." Ameongea Ally Nnunduma

Mara baada ya timu ya Mbeya City FC kupanda Daraja, mashabiki na wadau wa timu hiyo wameandaa hafla mbili kwa nyakati tofauti ili kujipongeza. Ambapo Wapenzi na mashabiki wa soka wanaalikwa sana, Tar 31/05/2025 sherehe zitafanyika ndani ya NEW CITY PUB. Baada ya hapo pia Tar 14/06/2025, sherehe zitaenda kufanyikia kwenye Fukwe za Ziwa Nyasa (Matema.

Ndg. Ally Nnunduma ametosha shukurani za dhati kwa Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Spika wa Bunge la JMT na rais wa I.P.U Mh. Dkt. Tulia Ackson, Meya wa Jiji la Mbeya Mh. Dormohamed Issa, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Dkt. Juma Z. Homera, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Ndg. John Nchimbi, Viongozi wa Kimila wakiongozwa na Mzee Roket Mwashinga, Viongozi mbalimbali wa Dini, Wakuu wa Idara zote na Viongozi wote wa Ofisi ya halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa namna walivyotoa mchango na ushirikiano kuhakikisha timu inapata mafanikio.

SHOWER GELS
25/05/2025

SHOWER GELS

Us  πŸ™…πŸΎβ€β™‚οΈπŸ‡ΉπŸ‡ΏShujaa Asia / Mwenyekiti Mkoa wa MbeyaShujaa Bulugu /Mwenyekiti SMAUJATA TaifaMe / N-Katibu Idara SMAUJATA Ta...
18/05/2025

Us πŸ™…πŸΎβ€β™‚οΈπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

Shujaa Asia / Mwenyekiti Mkoa wa Mbeya
Shujaa Bulugu /Mwenyekiti SMAUJATA Taifa
Me / N-Katibu Idara SMAUJATA Taifa
Mr. Salum / Kutoka Ofisi ya Afisa Maendeleo Mkoa wa Mbeya

We're ready For the Mission πŸ‡ΉπŸ‡Ώ
God with Us

Ahsante sana Shujaa Bulugu A.K.A Ngamia kwa kututembelea nduguzako, Umetuonesha upendo Mkuu πŸ™πŸΎπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡ΏπŸ‡ΉπŸ‡Ώ

πŸ₯Š *KUBALI YAISHE, HUU MCHEZO HAUTAKI HASIRA* πŸ₯‡πŸ’ͺ🏾πŸ₯Š__________________πŸ₯Š__________________    Ule wakati uliosubiriwa na wap...
13/04/2025

πŸ₯Š *KUBALI YAISHE, HUU MCHEZO HAUTAKI HASIRA* πŸ₯‡πŸ’ͺ🏾πŸ₯Š
__________________πŸ₯Š__________________

Ule wakati uliosubiriwa na wapenzi pamoja na mashabiki wa mchezo wa NDONDI, mchezo unaobeba hisia za watazamaji.

Watu wote wa ndani na nje ya Mbeya, sasa *THE GREEN FITNESS GYM*, wameamua kuwarejeshea furaha baada ya miaka zaidi ya mitano kutokuwepo.
__________πŸ₯Š_________πŸ₯Š_________πŸ₯Š____________
Usiku wa *THE GREEN FITNESS GYM BOXING NIGHT* , ngumi zitapigwa mpaka mwenye mbio akimbie ulingo πŸ€£πŸ˜‚πŸ’ͺ🏾.

Tarehe: 26 April 2025
Muda: Saa 12:00 Jioni mpaka Saa 06:00 Usiku
Location; NEW CITY PUB, Mwanjelwa Mbeya Mjini.

πŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯Š
Bei ya Tickets;
REGULAR TZs 15,000/=
V. I. P TZs 50,000/=
V. V. I. P TZs 100,000/=

Kwa maelezo zaidi
Call / Wasap ☎️ 0757465781 au 0747371148

πŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯Š
NB: *WADHAMINI MILANGO IKO WAZI*

_MBIO ZAKO NDIYE MKOMBOZI WAKO_ πŸ€£πŸ˜‚πŸ€£
πŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯ŠπŸ₯Š

25/03/2025

Ila wanyakyusa πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜‚πŸ€£

BINTI TANZANIA NG'ARA CAMPAIGN Msimu wa Nne, March 2025    Kwanza niwashukuru sana  wadau wote wa kampeni yetu BINTI TAN...
10/03/2025

BINTI TANZANIA NG'ARA CAMPAIGN Msimu wa Nne, March 2025

Kwanza niwashukuru sana wadau wote wa kampeni yetu BINTI TANZANIA NG'ARA CAMPAIGN, kwa kushiriki kikamilifu ili kuzifufua ndoto za Mabinti wanafunzi wale wote wasiojiweza kikamilifu.

Kwa kauli mbiu ya siku ya Wanawake Duniani, isemayo "WANAWAKE NA WASICHANA 2025; TUIMARISHE HAKI, USAWA NA UWEZESHAJI ". Tumeungana nao msimu huu wa nne, kwa kutambua nafasi ya mwanamke kwenye Jamii.

Michango yenu imeweza kuwapa furaha sana, hakika jambo jema na lenye faraja kwao. Nimepokea salamu zao za kuwashukuru sana, wamewaombea baraka na mafanikio kila mlipotoa pakaongezeke.

Pia tuliambatanisha na utoaji wa Elimu ya;
1. Elimu ya Afya ya Mwili ( Personal Hygiene), ili kupunguza au kuondokana na Magonjwa k**a (U.T.I) Maambukizi kwenye njia ya mkojo na (V.F.I) Maambukizi ya Fangasi kwenye via vya uzazi vya mwanamke.
Elimu hii ilitolewa na mtaalamu wa Afya ya magonjwa ya kuambukiza na Naibu Katibu wa Idara ya Jinsia, Wazee na Watoto SMAUJATA Taifa Mr. WAMZI HASSAN na
2. Elimu ya Ukatili kwenye Jamii, ili kuwapa ufahamu na kuwataka waweze kutoa taarifa waonapo ukatili na viashilia vyake. Ambapo waliweza kuijua maana ya Ukatili na kuzijua aina nne za Ukatili ambazo ni
A. Ukatili wa Kimwili
B. Ukatili wa Kingono
C. Ukatili wa Kisaikolojia na
D. Ukatili wa Kiuchumi
Elimu ya Ukatili ilitolewa na Mwenyekiti wa SMAUJATA Mbeya mjini Shujaa MUSA MGALA

NOTE; Elimu zote zilitolewa kwa wanafunzi wote na jinsi zote wa Shule ya Sekondari ya Forest, iliyopo Mbeya Mjini.

Shukurani zetu ziwafikie (Community Officers) ma Afisa Maendeleo ya Jamii, Waalimu na ma Afisa Elimu wote kwa ushirikiano mkubwa wanaotupa. Tumekuwa tukishirikiana nao kikamilifu, kuhakikisha Jamii hasa wanafunzi wanapewa kipaumbele kupata Elimu ya maswala ya Afya na Ukatili ili kupanda mbegu njema ya Wazalendo kwenye Taifa Letu.

Mungu awabariki sana wote mnaotuunga mkono, sisi k**a BINTI TANZANIA NG'ARA CAMPAIGN tunawaombea baraka kutoka kwa Mungu.

Imetolewa na Mkurugenzi mratibu wa kampeni na mdau wa Uzalendo na Ustawi bora wa Jamii Tanzania.
Mr. Wamzi Hassan

πŸ™‹πŸΎβ€β™€οΈBINTI APEWE KIPAUMBELE
πŸ™…πŸΎβ€β™€οΈHEDHI SALAMA FURAHA YA BINTI
πŸ™…πŸΎβ€β™€οΈKATAA UKATILI, WEWE NI SHUJAA
πŸ‡ΉπŸ‡ΏHEKIMA NA UMOJA, USHINDI NA USHUJAA SMAUJATA

03/03/2025

Bidhaa zipo Dukani karibuni sana

☎️0743181985

02/03/2025

Ee! Ee..! πŸ€£πŸ˜‚
Ubhusuli ubhusuliii yeeilaa πŸ€£πŸ˜‚πŸ€£πŸ˜‚
Ee parrrangi πŸ€£πŸ˜‚πŸ€£πŸ€£

Address

Mbeya

Telephone

+255693073237

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wamzi Cosmetics Mbeya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Wamzi Cosmetics Mbeya:

Share