26/05/2025
KATIBU MTENDAJI MKUU WA TIMU YA MBEYA CITY FC AELEZEA MAFANIKIO YA CLUB IKIWA CHAMPIONSHIP NA MIPANGO MADHUBUTI BAADA YA KUPANDA LIGI KUU TANZANIA BARA.
Mara baada ya timu ya Mbeya City FC kupanda Daraja, C.E.O wa timu hiyo Ndg. Ally Nnunduma ameambia Greencity TV Online kuwa wakiwa Ligi ya Championship yapo mafanikio walioyoyapata k**a timu.
"Mbeya City FC kwa msimu wa 2024/2025 tukiwa kwenye mapambano ya kutaka kupanda Ligi Kuu, tunamshukuru Mungu tumepanda moja kwa moja tukiwa nafasi ya Pili kwa Point 68 nyuma ya Mtibwa wenye Point 71. Niwapongeze Wachezaji, Benchi na mashabiki pia kwakuwa kwanza tumepoteza mechi mbili tu ligi nzima, tumeshinda mechi 8 za Away na tumefanikiwa kwa vinara wa Magoli 68 huku anaetufuatia akiwa na magoli 58. Hatukuishia hapo kwakuwa sisi ndiyo timu pekee Championship, tumekuwa na mashabiki wengi kwenye mechi zetu kuliko timu yoyote kwenye Ligi hiyo."
"Sasa tumerejea Ligi Kuu tunazidi kusisitiza kuwa kwenye mji wao kuna kijiji chetu, tunaongeza kuwa sasa tutaenda kuwa na vijiji vyetu kwenye kila mji. K**a kulikuwa kijiji kimoja sasa vitakuwa kumi zaidi, hivyo tumejipanga vizuri sana. Kurejea kwetu Ligi Kuu ni kuwa tunaelewa changamoto zote na mahitaji yote muhimu, hivyo tutahakikisha hatusogei kwenye hatari ya kucheza Play Off kabisa." Ameongea Ally Nnunduma
Mara baada ya timu ya Mbeya City FC kupanda Daraja, mashabiki na wadau wa timu hiyo wameandaa hafla mbili kwa nyakati tofauti ili kujipongeza. Ambapo Wapenzi na mashabiki wa soka wanaalikwa sana, Tar 31/05/2025 sherehe zitafanyika ndani ya NEW CITY PUB. Baada ya hapo pia Tar 14/06/2025, sherehe zitaenda kufanyikia kwenye Fukwe za Ziwa Nyasa (Matema.
Ndg. Ally Nnunduma ametosha shukurani za dhati kwa Mbunge wa jimbo la Mbeya Mjini, Spika wa Bunge la JMT na rais wa I.P.U Mh. Dkt. Tulia Ackson, Meya wa Jiji la Mbeya Mh. Dormohamed Issa, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mh. Dkt. Juma Z. Homera, Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya Ndg. John Nchimbi, Viongozi wa Kimila wakiongozwa na Mzee Roket Mwashinga, Viongozi mbalimbali wa Dini, Wakuu wa Idara zote na Viongozi wote wa Ofisi ya halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa namna walivyotoa mchango na ushirikiano kuhakikisha timu inapata mafanikio.