Simulizi Za Kusisimua za twitch

Simulizi Za Kusisimua za twitch Karibu Katika Ukurasa Wa Masimulizi Na Burudani Kwa Wakubwa Uelimike Na Kuchangamsha mwili Pia..

EPISODE 96: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU      ........................ILIPOISHIA..............Askari aliyekua anatuchun...
14/12/2025

EPISODE 96: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU

........................ILIPOISHIA..............
Askari aliyekua anatuchunga aliingia mule ndani kashika Rungu kwa ajili ya kutoa kipondo kwa anayetaka kubaka........SASA ENDELEA........
Yule askari alipofika mule ndani aliuliza ni nani aleyetaka kubaka, mfungwa niliyekua nampapasa nikiwa ndotoni alinipoint Mimi kisha yule askari alikuja kwa hasira.
"Unafikir huku kuna ufiraun k**a kule" kabla sijajitetea kuwa ni ndoto, nilipigwa rungu ya kwenye mbavu zikalia k**a mfuko wa simemti uliopigwa na ubao.
Maumivu makali yalipita ndani ya mbavu zangu, nikizuia upande huu napigwa kwingine, Wafungwa wengine k**a kawaida yao walicheka k**a hawana akili nzuri wakizani labda nilikia nataka kubaka kweli.
Baba Rahma alitamani anunue ile kesi tena lakini asingeweza kutokana na tulivyokuwa tumelala.
Nilipigwa mpaka alipochoka ndio nikamwambia.
"Afande unanionea tu, haikuwa lengo langu, kumfanyia vile ni ndoto tu" watu walicheka tena lakini yule askari alimuuliza niliyekua nampapasa
"Ilikua ndoto kweli huyu au makusudi" Mfungwa aliyenisemea kwamba nilitaka kumbaka alikaa kimya kidogo kisha akasema.
"Labda itakuwa ndoto kweli maana alivyokua ananipapasa na kunibusu alikua anataja jina la Rahma!" Vicheko vingine vilifatia yule askari nae akabaki kucheka nakuniacha na maumivu huku akimshtumu mfungwa aliyesema kuwa nataka kumbaka kumbe ilikua ndoto.
Usiku ule sikuwa na hamu ya kulala tena mauimivu yakiwa yametapakaa kila kona ya mwili wangu.
Nilimtazama Baba rahma alionekana kunitazama nanyeye kwa umakini akiwa anaonekana k**a kagundua kitu kwangu.
Nilienda kujikunja sehemu nyingne ya kulala huku nikitema mate kwenye sakafu ovyoovyo kila nilipokumbuka kuwa nimenyonya ndimi ya mwanaume mwemzangu tena ambae mswaki haujatiwa kinywani mwake siku nyingi.

Ilikua asubuhi ya siku nyingine tena,, ubaridi ukipuliza mpaka kwenye uwanja wa makwapa nikijikunja miguu ikakaribia kidevu kwa lile baridi.
Firimbi yakutuamsha haikuwa nyuma na wakati, mda ule ulikuwa kwa ajili ya kuamka na kunywa uji kisha kwenda kwenye ile kazi ya kupasua mawe.
Baada ya kuamka tulipewa uji kwani sisi tuliletewa mule ndani tukitengwa kabisa na wafungwa wale wakawaida.
Tulipomaliza tulianza kuongoza mstari mmoja kuelekea kwenye Karandinga k**a kawaida askari mmoja akiwa katangulia na mwingine nyuma yetu tukitembea. Katika mstari nyuma yangu alikua Baba rahma ambaye toka Jana usiku alionekana kanitilia wasiwasi.
"Kijana ni nini kimekufanya ukafika mpaka hii jela, si uliendaga NgoroNgoro?" Nilishtuka kusikia Sauti ikinena kwa kuniuliza swali lililoendana na ukweli wangu wa nilipotoka. Hakuwa mwingine ni Baba rahma aliyeniuliza Swali la namna ile.
"Ina maana Amenigundua mimi ni nani" nilijiuliza kimoyomoyo kabla sijamjibu kwan mida ile tuliongea kwa kunong'ona.
Kwa taharuki niliyopata sikuweza kumjibu wasi wasi ukanipanda kwamba amejua mimi ndio niliyeenda NgoroNgori ina maana ile ndoto ya jana yake usiku imemjulisha mimi ni nani baada ya kutaja jina la Rahma.
Tulifika kwenye karandinga wakati najiaanda kupanda walitokea askari wawil ambao niliwafahamu kwa sura wale waliozoea kunipeleka kwa mkuu wa magereza walisimama pembeni
"Afande Joshi tunamuomna namba mia mbili hamsini, Leo hatoenda huko" alisema askari mmoja aliyekuja kisha yule aliyekua anatuongoza kwenye karandinga, alitazama ule mstari.
"Namba mia mbili hamsini tokaaaa" nilijikausha k**a sikusikia kutokana nilijua kile ninachoitiwa na wale askar ni utumbo mtupu bora kwenda kupasua mawe.
Walisubri nitoke lakini sikutoka ghafla wale askari waliokuja wakanifata na kunishika kwa nguvu.
"Hivi wewe unaringia nini hapa jela mpaka unakua mbishi" aliniuliza askari mmoja aliyekuja kunichukua
"Naringia kuumbwa mwanaume la sivyo ungekuta nimekua mama yako" nilimjibu kwa jeuri akanitazama kwa hasira bila kunifanya chochote sikujua kwanini hawakuthubutu hata kunifinya na ukicha.
Wakat naondoka kutoka eneo la mstari Askari wa jana yake usiku nae alikua kwenye karandinga alipayuka
"Kumbe ni huyo aliyetaka kumbaka mwenzake akizani Rahma hahahahaha" maneno na kicheko chake kilisindikizwa na vicheko vya wafungwa.
Niligeuka nyuma kutazama, macho yangu yaligongana na mboni za baba Rahma aliyenitazama kwa wasiwasi.
Kichwani mwangu nikiwa natembea kuelekea kwa Mkuu wa magereza kwa mara nyingine nilijiuliza ananiitia nini wakati nilimktalia na kwanii ananitaka mimi tu.
Dakika chache baadae tulifika mlango mwa ofisi ya mkuu wa Gereza lakini siku hiyo mezani mwake kulikuwa na ugeni wa watu wawili mmoja kasimama kushoto kwakwe na mwingine kulia kwake, wamevaliza suti nyeusi iliyowabana kupindukia kufanya miili yao k**a jiwe ijichore vizuri nakuonesha miraba sita. Usoni sura zao hazikuonesha Tabasamu hata kidogo ikiwa imefunikwa na miwani mikubwa meusi.
Niliposimama mbele yao Mkuu akiwa kakaa kwenye kiti siku hiyo hata yeye hakuonesha tabasamu k**a ilivyokuwa awali hali iliyonitishia amani huku laptop nyekundu ikiwa imefunguliwa mezani mwake
"Mshikeni mikono" aliwaambia wale askari walionileta bila ya kubisha wale askari walinishika k**a vile niliiba chao.
Mkuu wa magareza alipoona nimeshikwa mkono aliwauliza wale wageni waliovalia suti.
"Vipi mnamuonaje"
"Boss mbona anaonekana bado dogo sana hakina afya imekuaje una mpa sifa zote" alijibu mmoja aliyesimama upande wa kuume kwake
"Ngoja utaelewa kwanini namuhitaji kwa hudi na uvumba" alipokwisha kusema hayo alinyanyua simu yake kisha akaiweka masikioni akitazama ile laptop
"Hey! Kishoka, mshakamilisha mission na mtandao mshauweka sawa" alimuuliza yule aliyekua anaongea nae kwenye simu lakini kwa kuwa hisia za kusikia kwangu zilikua kubwa nilisikia akijibiwa
"Ndio mkuu, tushamk**ata na tumemuweka online k**a unavyotuona"
"Safi sana basi jiandaen kwa lolote nitakalowaambia" aliposema hayo hakukata wala hakutua simu yake alinitazama Mimi
"Dominick kabla sijafanya tukio hili naomba unambie kwanza, utajiunga katika kundi langu au msimamo uko pale pale"
"Hivi wewe mkuu gani? Mkuu wa mabumbuwazi au? Nishakwambia Mimi siwezi na wala sintoweza kujiunga na kundi lako mbona waning'ang'ania" nilimjibu kwa jazba nikimkazia macho.
"Nafikiri hunielewi mimi vizuri sasa utanijua Mimi ni nani" vile vitisho niliona kawaida sana.
Alivyosema vile alinigeuzia ile laptop iliyokua mezani nikawa naingalia Mimi
"Unaona kinachoendelea sasa?' Aliniuliza akigusa kioo cha Laptop.
Hapo mwanzo sikuielewa ile video niliyokua naitazama mda ule.
Niliona watu waliovalia vinyago k**a majambazi wakiwa wamemzunguka mama mmoja aliyekaa kwenye kiti kafungwa kamba, huku minjemba ile ya kijambazi ikitunisha vizuri misuri yao.
Lakini nilipokuja kukazia macho vizur "Mungu wangu!!"alikua ni mama imma, Mama Dominick mama yangu mzazi ndio katekwa vile kafungwa k**a MTU anayesubiria kuchinjwa.
Jasho mda ule ule lilinitoka nisiamini kwamba wameweza kujua familia yangu iliko na kumteka mama yangu. Kwakweli moyo ulishtuka ingelikuwa nina ugonjwa wa moyo basi siku hiyo ingelikuwa ndio mwisho wangu wa maisha.
"Haya nambie umekubali ua haujakubali?" Aliniuliza tena kwa mara nyingine macho yangu hayakutoka kwenye kile kioo cha Laptop nikimtazama mama mzazi niliyepotezana nae siku nying
"Umemtoa wapi mama yangu, umewezaje kuijua familia yangu hakika ukimuua mama yangu nitakufanyia kitu kibaya" niliongea kwa hasira nikichanganya na huzuni.
Simu ile aliyokuwa anaongea nayo ikiwa haijakatwa bado nilimsikia akisema
"Kishoka naomba jiandae kumkata kidole kimoja kimoja Huyo mama mpaka nitakapokwambia acha" Ghafla ni k**a alikua ananisikika kwenye ile video nikiyokua naitazama.
Niliona Mmoja wa majambazi katoa kisu kisha akaulza mkono wa mama yangu kwenye meza iliyokua mbele yake akatenga kidole kcha mwisho cha mkono wa kushoto wa mama yangu, akawekea kisu juu yake k**a anataka kukata karoti.
"Subiri kwanza kabla hujafanya hivyo" aliamrisha tena mkuu wa magereza nikaona lile zoezi limesimama.
"Nakuuliza tena kwa Mara ya mwisho la sivyo nitaruhus mama yako akatwe, nahesabu moja mpaka tatu, unakubali ama unakataa?"
Kiukweli sio kwamba nilishindwa kukubali maoema lakini niliona k**a wananitania. Yule mkuu alianza kuhesabu moja, anaganda dakika moja kisha anendelea. Akifika mpaka mbili bado moyo wangu ulikataa kukubali, alipofika tatu mara aliwaruhusu.
nilitazama kwenye ile video niliona kidole cha mama yangu kikikatwa kikaruaka k**a mkia wa mjusi, damu zikatapaaka pale kwenye meza huku Ukelele mkali wa maumivu kutoka kinywani mwa mama yangu ukisikika sana katika ile video.

Kwa yale maumivu niliyopata baada ya kuona video mama yangu akikatwa kidole nilijikuta nguvu za kimbwa mwitu zimenijia ghafla, wale askari walionishika mkono niliwapushi nikawarusha kila mmoja ukutani mwake kwa kishindo kikubwa kisha nikaanza kutembea kueleka kwa yule mkuu kucha za kimbwa mwitu zikiwa zimetokea pamoja na meno.
Hasira nilizokuwa nazo kwenda kumdhuru mkuu na wenzake zilikatishwa baada ya kutazama ile video kuona mama yangu kawekewa kisj kwenye shingo k**a anataka kuchinjwa.
Mkono wangu wa kushkti ukiwa juu ya meza ya mkuu wa magereza kucha zimetobka mbao ya meza, mkono wangu wa kulia nilikua nimeunyanyua ili nimchane lakini yule Mkuu hakuogopa akaniambia.
"Safi sana nilikua najiuliza siku zote wewe ni nani mpaka uwe na nguvu hivi,Sasa endele unachotaka kufanya niruhusu mama yako mzazi auliwe". Hasira zilirudi zilipotoka mda ule waliovalia suti walikua makini namimi kwani nilifanana k**a mnyama walininyooesha bastola huku boss wao akiwa hana wasiwasi kwa kile kitendo
Nguvu ziliniishia mama yangu kaekewa kisu shingoni ili nikubali kujiunga kwenye kundi la kijambazi, wale askari nilio wapushi mpaka mda ule hawakuwa wameamka, huku mkuu wa gereza akianza kuhesabu moja mpaka tatu nisipokubali basi na shingo ya mama yangu itakatwa k**a kile kidole...........ITAENDELEA.

Finally  nimemalizana na elimu 😁..... Hakuna Cha urahisi dunian kiwe na matokeo mazuri ... Ni Mungu tu 🎓
12/12/2025

Finally nimemalizana na elimu 😁..... Hakuna Cha urahisi dunian kiwe na matokeo mazuri ... Ni Mungu tu
🎓

EPISODE 95: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU............................ILIPOISHIA.......................akanikaba roba ya ...
12/12/2025

EPISODE 95: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU
............................ILIPOISHIA.......................
akanikaba roba ya ukweli ya mikono iliyokommaa kwa sababu ya kupoga nyundo huku akinilazimisja nisema Mimi in nani au nimetumwa kumpeleleza.............SASA ENDELEA........


Kile kitendo cha baba rahma kunikaba kilifanya wafungwa wengine, kuanza kupiga mbinja na zogo, Baba rahma hakuwa wa kawaida toka awali lakini, alinishika kwa nguvu pamoja na afya yake ya mgogoro.
Ilichukua mda mfupi tulikua tushazungukwa na wafungwa pamoja na askari huku wafungwa saut zikitoka kwenye kinywa chao k**a waombelezaj wa msiba.
"Zipigwe, zipigwe!" Zile sauti zikanifanya nianze kuona ugomvi ule utakua mkubwa
"Mzee niache kwanza, ntakwambia Mimi in nani"nilmsemesha baba rahma aliyekua anaonekana mwekundu kwa kufura hasira.
"Na hapo hakuna kuachana hivihivi lazima mpigane mpaka damu ziwatoke haiwezekana mkaacha kaz kisa mpigane haya onesheni nani mbabe" ni sauti ya askari aliyeonekana ana umbo jembaba, kunfanya mifupa ya tata kuonekana, kanyonyoa ndevu pamoja na za kichwa lakini masharubu yalikua mengi k**a brash ya chachandu, rangi yake nyeusi ya kumeremeta mfano wa nyoka mweusi aliye juani.
Yale maneno aliyoesema yaliambatana na ya wafungwa wakifurahia kitendo kile k**a wameona njia ya peponi.
Nlijitahidi kumuhimiza baba Rahma aniachie lakini alionekana ni mfungwa aliyedata kutokana zile sauti zilipodhuru masikio yake aliacha kunikaba na kuanza kunirushia ngumi.
Alinipga ngumi za haraka haraka za kwenye taya kusababisha nidondoke chini kwa magoti nikitema mate yalitoka na damu, Vita vya panzi furaha kwa kunguru na kweli vile vita viliwafurahisha kuanzia askari mpaka wafungwa.
Baba Rahma alinipga teke la kwenye mbavu ikanifanya nibinuke. Kwakweli japo alikua ananipga lakini mawazo yangu hayakuwa eneo lile zile kelele nilihisi kwamba zilinisisitiza Rahma atakuja kuwa adui yangu.
Mda wote baba Rahma alikua ananipiga huku kichwa changu kiligonga kengele za Rahma.
Kilichosbabisha nirudi katika ufahamu wa kawaida ni pale baba rahma alipochukua kipande cha jiwe na kunipiga nacho kichwani kufanya niamke ile sehemu niliyolala k**a mtu aliyekuwa usingizini akamwagiwa maji.
Damu zilikua zinanichuruzika si puani wala mdomoni, nilipeleka mkono wangu mdomoni nikashika zile damu nikamuangalia aliyekua ananipiga hakuwa na nguvu ya kupigana na Mimi mpaka kunitoa damu, Alichukua jiwe lingine ili aje tens kunishambulia lakini, nilikunja ngumi kwa ajili ya kurudisha makombora kwa yule mzee japo sikuwa ninataka kumpiga.
Alipoona nimesimama alikuja kwa pupa lakini nlipokumbuka kwamba ni baba mkwe ile ngumi niliiikunjua aliponikaribia nikamshika shingo na kumyanyua juu juu k**a MTU aliyening'inizwa jambo ambalo liliwanyamazisha wale waliokuwa wanapiga kelele.
Nilihakikisha nimemkaba vya kutosha mpaka kuliachia jiwe lile ambalo alilishika.
Sikutamani kumpiga sehemu ya mwili wake kwani nilijua lazima nitamvumja ukitegema pale alipokuwa alikua kavunjika mguu, Baada ya dakika chache nilimuachia na kumpa k**a onyo kwamba nilikuwa nina uwezo wa kumpiga.
Mwili wangu haukauendana na matendo niliyokuwa nafanya kutokana na ubabe na ukatili usiolezeka.
Baba Rahma hakurudia tena kuja kupigaa akilala chini huku akikohoa kikohoz kikavu k**a ngoma za wimbo wa faifa.
Muda wa kurudi kwenye kazi ukawa umefika kila MTU alihitajika kurudi sehemu aliyokuwa awali lakin sisi tuliopigana Yale mawe tuliyivunja toka asubuhi yake yalifutwa na kuambiwa tuanze upya yan kumi na tano mengine.
Sikuona maajabu kuongezewa kwani ndio ilikuwa uonevu wa jela ile hasa ukizingatia, nilikua nimekataa ofa ya mkuu wa magereza.
Nilimnyooshea baba Raham mkono alipokua chini kwa nia ya kumyanyua
" Mimi sio mtu mbaya kwako huwenda baadae ndio utanielewa mimi ni nani, amka tukafanye kazi" alinitazama kwa jicho la kunistahi kisha akasahau k**a tulikua tuna ugomvi mda mfup uliopita, akanyoosha kiwiko chake na kunipa kiganja nilimvuta nakwenda sehemu ya awali tuliyokuwa tunapasua mawe.
Nguvu nilizokua natumia bado zilinisitiri katika kazi ile lakini siku zote bandu bandu humaliza gogo kwani zile nguvu kuna mda ziliisha nikawa napasua k**a binadamu wa kawaida jambo ambalo ilifika mpaka magahribi hatukuwa tumemaliza kupasua mawe licha ya kuwa tukiongezewa.
Kipenga kilicholia k**a tembo mwenye hasira kali kilipulizwa kabla jua halijazama vizuri katika blanket lake nakuwapa ishara kwamba kipenga kile ni cha mida ya kurudi katika Gereza japo nilikua mgeni katika mgodi ule wa mawe lakini kiashiria kile hakikuniacha katika kujua Alama za nyakati
Tulirudisha vifaa tulivyokuwa tunatumia kupasuliwa mawe, baada ya hapo tulipanda kwenye karandinga k**a tulivyoletwa awali, na kurejeshwa katika Jumba la kifahari la wafungwa kwa maana ya Gereza.
Mida tuliyofika ilikua ndio mida ya wafungwa kuhesabiwa, tulishuka nikizani nitapelekwa katika lile kundi nililozoea lakini tulivyoshuka tulihakikiwa pembeni ya like gari kisha tukaanza kupelekwa Upande mwingne wa majengo ambayo wale wenyeji wenzangu wa kupasua mawe walionekana wanajua eneo lile kasoro Mimi peke yangu ndio nilipatwa na bumbuwazi.
Tuliacha jengo la gereza nililozoea kulala k**a mita mia sita japo palikuwa ni eneo lile la gereza.
Tulifika katika chumba kimoja ndani yake kulikua kuna ngazi za kwenda chino k**a handaki lakini handaki lililoboreshwa kwani lilikua pana k**a chumba, refu kupitliza, taa za mwanga mweupe zikiwa juu ya paa refu hata hakuna atakeyefikia, jambo lilonishangaza ni kuwa hakukuwa na gagulo hata moja sio la kulalia wala kujifunikia.
Nilishangaa tulipofika wale wafungwa wengine walipanga mistari kusimama wakiangalia ukuta mfano wa majogoo yaliyotaka kupigana nami nikafata nyayo zao nikaenda kuwa MTU wa mwisho huku pembeni ya mstari nilisiomama mkono wangu wa kuume alisimama Baba rahma.
Askari aliyetusindikiza alishika kirungu chake akikipiga piga kwenye kiganja cha mkono wa kushoto, akitembea nyuma yetu huku kilio cha sakafu kilichotokana na kukanyagwa na buti lenye soli ngumu la yule askari ndio kilisikika kikisindikizwa na milio ya mbu walioamka kuona kitoweo kimekuja.alianza kurud tena alipotoka alipofika kati alisema kwa sauti ya juu
"Leo tunalalaje? Bendera au popo" baada ya kusema vile wafungwa waliitikia
"bendera" Nilishangaa nini maana ya kulala bendera, lakini matamanio yangu ya
Baada ya yule askari kutembea mpaka mwisho Matamanio yangu ya kujua kwamba nini maana ya mlalo wa bendera nilipata jibu baada ya kuona wafungwa wakiweka nyayo ya mguu wa kulia pembeni mwa goti la mguu wa kushoto na ule mguu wa kulia ukajikunja k**a, "V" au bendera kweli kutokana na mguu uliosimama.:
Nilishangaa kuona vile ikabdi nimuulize Baba rahma alieyekua pembeni yangu
"Kwani ndio tunalala hivi" baba rahma alionekana kunikataza kuongea lakini alikua ashachelewa sauti ile aliisiki Askari ndipo alipouliza
"Nani aliyeongea" wafungwa waliokuwa karibu walijubu kwa haraka huwenda walijua adhabu yake walaipaza sauti zao
"Mgeni"
yule askari alinifahamu akawa anakuja kwangu kwa hasira akiwa kaibetua rungu lake kwa ajili ya kutoa adhabu ya kunipiga marungu, Kabla hakufika vizuri cha kushangaza Baba rahma alisema kwa sauti ya unyonge.
"Sio mgeni ni Mimi hapa Afande" yule askari alisimama ghafla akamgeukia baba rahma nakumwambia
"Yani wewe kila siku una matatizo unajifanya hujui sheria za humu pumbavu si Jana tu ulishondwa kulala k**a popo shenzi" alivyosema hayo alimdondoshea rungu la mgongo baba rahma, ilimfanya adondoke chini nakuendelea kupigwa.
Kitendo kile kiliniumiza moyo yeye kupigwa kwa ajili yangu nilitamani nimpige yule askari lakini sikutamani kuharibu tena ama kuua.
Baada ya kipigo kile baba rahma alibadilishiwa adhabu na kuambiwa alale kipopo yani unaweka miguu ukutani kichwa chini ya sakafu kwa kusimama huku mikono umeiweka nyuma ya mgongo kwa hiyo mwili wote unategemea shingo k**a mguu.
Hakika nilona mateso lakini yale ya jela ya kisongo yalikua ya aina yake.
Tuliweka ile staili mpaka kufika nusu usiku ndio tuliporuhusiwa kulala kwenye sakafu yenye unyevu wa baridi bila ya kuongea na MTU. Kwakweli usiku ule ulikua mgumu kwangu nilizoea kulala kwenye gagulo lakini kulala kwenye sakafu vile nilitamani niamke usiku wa manane nipumzike kwa jinsi sakafu ilivyoumiza.
Kulipokucha k**a kawaida sisi hatukunywa uji na wale wafungwa wengine na ikawa sababu kwanini sikuwajua wale wafungwa wanaopasua mawe kutokana wao walitengwa. Baada ya kumaliza kunywa uji, tulipandishwa kwenye karandinga na kweda kule mgodi wa mawe kwa kibarua kizito kisichokuwa na ajira.Tulipofika kule wakat ule wa mapunziko ndio nikapata mda wakumuuliza baba rahma kwanini alisema yeye ndio kaoengea usiku ule wakati Mimi ndio niliyoongea.
Nakumbuka alisema maneno ambayo siwezi kuyasahau
"Kijana, mim nakuona bado mdogo sikutaman kukuona unapigwa na kulegezwa mifupa yako wakati una kazi ngumu hapo mbeleni, hivyo niliona bora Mimi niliyozoea niendelee kupigwa na pia umri wangu unaenda japo nina matumaini ya kutoka jela lakini najiona k**a maiti inayotembea, jitahidi utafanikiwa hapo baadae kwani hata machoni kwako nikikutazama unaonekana utakuja kuwa MTU wa heshima hapo baadae" kwakweli maneno ya Baba rahma yalinitia simanzi kubwa sana.Nilibaki kumtazama usoni mwake nisijue cha kumwambia.

Siku hiyo pia mchana ikapita bila kumaliza kupasua mawe yakizidi kuongezwa.Naikumbuka siku hiyo vizuri kwani kuna tukio ambalo sikutarijia kunitoke usiku wa siku hiyo.
Ilikua usiku sana tushamaliza adhabu ya kulala kwa mfano wa bendea iliyosimama sasa tulilala k**a kawaida tukirundikana sehemu moja kutokana na sheria ya siku hiyo.
Siku hiyo usingizi ulipo nipitia ilinijia ndoto ya ajabu sana.
************-*********
Niliota nikiwa niko chumbani na mtoto mzuri wa kiarabu sura yake haikuwa imepotea alikua ni Rahma amevalia bikini ya rangi ya chuichui iliyoendana na rangi ya kabati iliyofunika machungwa yake.
Nilikuwa nimejilaza juu ya kitanda kikubwa Rahma alinifata nilipolala akitambaa kwa magoti huku akisema.
"Mpenz wangu Domi, nilikumiss siku nyingi, nimemiss na mambo yako matamu" alipokuwa anasema hayo alifata moja kwa moja mpaka mdomoni nakuanza kunyonyana ndimi. Hakika raha ile niliikosa siku nyingi kwani ule utamu wa ulimi wa Rahma niliisikia mpaka kisogoni.
Nilimtoa jui nakumuweka ubavuubavu huku nampapasa sehemu za mwili wake nikitaja jina lake kwa mahaba.
"Rahma! Rahma bado we mtamu". Ghafla nikiwa katika raha zile nilishtukia napigwa kibao huku aliyenipiga akipaza sau "Afandee! Afandee! Huyu ananibaka" la hasha! Nilipokuja kudamka toka kwenye ile ndoto nilikua nimemshikilia mwanaume mwenzangu tuliyelala nae karibu huku mdomo wangu ukiwa karibu yake kanakwamba nilikua namnyonya kweli.
Nilibutuka nakumuachia nisiami ndoto ile Sauti ile ilimshtua kila mfungwa isitoshe kuacha yule mfungwa niliyemkumbatia pia Baba rahma alikua pembeni yangu upande mwingine.
Askari aliyekua anatulinda aliingia mule ndani kashika Rungu kwa ajili ya kutoa kipondo kwa anayetaka kubaka............ITAENDELEA........

EPISODE 94: NUSU BINDAMU NUSU MBWA MWITU ....................ILIPOISHIA.......................Aliongea hivyo akijiekea k...
09/12/2025

EPISODE 94: NUSU BINDAMU NUSU MBWA MWITU

....................ILIPOISHIA.......................
Aliongea hivyo akijiekea kidole pembeni ya kichwa mfano wa bastola akinitadhaharisha ataniua endapo nikisema taarifa zile...........SASA ENDELEA.........
Nilitoka mule ndani ya ofisi kichwa kikiwa kizito sana chai na mkate niliokula vyote vikiwa vimeyayuka tumboni.
Nje ya ofisi nilikuta wale askari walionileta wakinisubiri na ndio hao hao walinirudisha mpaka majengo ya wafungwa yalipo na kuniacha huko.
Siku hiyo kwangu ilikua ya aina yake nikawa mpole k**a ndio nimeingia jela siku hiyo nikiwa natafakri, kuwaza na kuwazua yale maneno ya Mkuu wa gereza.
Ilifika mpaka usiku nikawa sijalala kwenye virago vyagu mda ule nilikuwa ninavyo vingi kutokana ubabe wangu lakini kunguni hawakuujua ubabe wangu japo niliwazoea.
Ilifika mpaka usiku wa manane bado sijalala. Namba mia mbili ishirini alishtuka toka usingizini akanikuta bado sijalala ikabidi aniulize.
"Vili mchizi wangu mbona hujalala mpaka sa hizi, na unaonekana K**a una mawazo, umepata taarifa gani kwa mkuu Leo?" Yale maswali yake ni sawa yaliingia humu yakapenya kule kwani sikuthubutu kunyanyua mdomo wangu kumwambia.
"Ah kawaida tu bhna nimemkumbuka mama yangu nyumbani na mikwara ninayipigwa na mkuu wa jela kwa ajili ya ubabe wangu" nilimdanganya akasogea nakunishika bega.
"Usijali ndugu yangu haya ndio maisha ya jela, we kukaa miezi yote hiyo bado hujapazoea, sisi ndio familia yako, kwa hiyo embu lala ukifikiria sana miaka unayifungwa hautoimaliza utakufa kwa mawazo" alitoa maneno ya kunifariji pasipo kujua jambo lililokuwa linanitatiza ni tofauti kabisa na lile.Ili kumridhisha niliamua kulala lakini nilitamani pasikuche bila kupata jibu kamili.
Usiingizi ulinipitia nilikuja kuamshwa tena asubuhi ya siku nyingine na firimbi za askari wa zamu kwa ajili ya kwenda kuchukua uji.
Nilinyanyuka kwa uchovu sana kila nilipokumbuka suala la mkuu wa jela.
Nilijikongoja mpaka kwenye mstari na siku hiyo sikutaka kukaa mbele nikajichanganya kati ili wale askari wakija wasinipate kirahisi lakini ilikua ni sawa na kaniki kujificha katikati ya uwanja mweupe, kwani wale askari walikuja tena hawakunitafta Sana wakaniona.

Nilichukuliwa tena na wale askari mwendo wangu ukiwa ni wa kusuasua K**a vile ninapokwenda naenda chinjwa.
Tulifika mpaka kwenye ofisi K**a kawaida tukamkuta yule mkuu tafkri hakutoka pale, mavazi ndio yaliyomtofautisha jana yake. Baada ya kunifikisha askari wakatoka nje, kisha Mkuu alisimama nakunifata akinikaribisha tena kwenye sofa akicheka Cheka pasipo Mimi kucheka. Sikutaka kuplteza mda wake ama wangu kwani jibu nilikua nishalipata kabla hajafika kwenye sofa au kukaa nilimuongelesha.
"Mkuu!" Nlipomuita vile akasimama nakunigeukia.
"Niambie Dominick Leo haunywi chai?"
"Sina haja nayo, lakini nimefikiria ombi lako nimewaza sana nikawazua lakini kwakweli, nimeona ama kwa makubaliano yangu Mimi pamoja na ubongo wangu, siwezi kujiunga katika kundi lako" niliongea kwa ujasiri na jeuri K**a nilivyokuwa nawaoneshea wafungwa wezangu. Yule mkuu alibadilika sura akawa mwekundu aakanitazama kwa jicho kali ile sura ya furaha ikatoweka usoni mwake.
"Unasemaje Dominick? Acha utani bana, yani ofa zote nilizokupa bado hutaki?" Aliongea akijilazimisha tabasamu
"Ndio, sitaki, siwezi na sintokaa nijiunge na kundi la kigaidi" niliposema maneno hayo nikaanza kutembea kuondoka nje.
"Dominick, Dominick, haya utaijutia hii nafasi niliyokupa," alisema maneno K**a ya matisho lakini sikuyaweka maanani nikaendelea kutoka nje. Ata wale askari walishangaa
Ilibidi wanisimamishe nakuniuliza k**a kuna usalama huko ndani sikuwajibu kitu ikabidi mmoja arudi ofisini kwenda kuhakikisha. Lakini alipoingia alikaa k**a dakika tano k**a alikuwa anaambiwa kitu na mkuu kisha akatoka nakuniamrisha tuondoke tena kwa hasira sana kuliko walivyokuwa wakinichukua hapo awali k**a vile walingiwa na sumu kali.
Kwakuwa sikuwa nimekunywa chai, bado nilikuta foleni ya wafungwa kuchukua uji ipo, na nilipotaka kwenda kujiunga nao nilikatawazwa na wale askari, mmoja wapo akaniambia
"Bahati hairudi Mara mbili, Leo hautabaki huku ndani ya jela unabidi uungane na wafungwa wanaoenda kupasua mawe, twende ukatangulie kwenye gari." Nilishangaa kwa kupangiwa kazi ya kufanya na wafungwa ambao walizoea kwenda kupasua mawe wakiwa wanatoka asubuhi na kurud jioni.
Sikuwa na uwezo wa kubisha kwani askari waliobeba bunduki walizunguka kila kona walinipeleka mpaka kwenye karandinga la kuwababeba wafungwa nikafungwa nyororo zilizotambaa chino ya miguu kwa kila sehemu kuendana na idadi ya wafungwa watakaoingia ndani ya gari.
Nilikaa mule ndani ya gari mpaka wafungwa wengine walipomaliza kunywa uji na wale waliotakiwa kwenda kupasua mawe wakaletwa.
Sura zilizoletwa kwenye karandinga lile tangu niwe jela sikuwahi kuziona kwani walikua wamekomaa kila kona ya mwili wao, miili imewajaa ndiiiii! Na kila aliyengia kwenye gari alinitazama Mimi wala hakuonesha tabasamu, Lakini wote walioingia mule aliyenishangaza ni wa mwisho kuingia alikua kadhohofika sana, mguu akiwa anachechemea hata kupanda kwwnye lile gari alipanda kwa shida. Lakini taswira ya yule mtu nlikua naikumbuka alipomaliza kuingia kabisa na kutazamana nae looh! Alikua ni baba Rahma ambaye Mara ya kwanza kuingia jela Ya kisongo nilimuona akishuka katika karandinga lile Tulilopanda. Alikua amekonda amepoteza wadhifa wake wakuitwa mwarabu,pia kilichonishangaxa alionekana k**a hanikumbiki tena.
Sikukiwaza Sana kwani karandinga lile likikua lishaanza kutoka nje ya ukuta wa jela kuelekea sehemu ya mgodi wa mawe
Ilichukua takribani K**a nusu saa tukaanza kuingie eneo lilokuwa lina miamba ya mawe magumu kila kona likiwa limezunguka K**a uwanja wa Mpira.
Gari ilienda kupark sehemu ambayo pembeni kulijengwa k**a kibanda fulani cha mbao, Baada ya gari kusimama tulifunguliwa nyororo zilizokuwa miguuni mwetu kisha tukaanza kuhimizwa kushuka ndani ya karandinga lile
"Shuka haraka haraka we mwarabu koko"ni sauti ya askari aliyekua akiongea akiwahakiki wafungwa tunaoshuka. Mimi nikiwa wa mwisho. Mwarabu koko aliyekuwa akizungumziwa mda ule alikua ni baba yake Rahma. Nilijiulza imekuaje Muarabu kafungwa katika gereza la Tanzania na hakufikishwa kwenye mahak**a zao nilikosa jibu.
Nilipofikia zam yangu kushuka yule askari aliniagalia kidogo kisha akacheka kwa dharau.
"Yani wewe ndio ninayesikia mbabe wa jela ndogo,sasa huku ubabe wako njoo uoneshe mawe mbwa wewe" wakati anaesema alikua akanisukuma chini zaidi. Angelikuwa anajua namna nilivyo kwa undani asingelithubutu kushika hata pindo la nguo yangu.Lakini sikutaka Shari tena kwani nilijua naweza nikauawa kwa sababu nishaweka kinyongo na mkuu wa jela.
Tuliposhuka wote tulipanga mistari kwa ajili ya kuhakikiwa namba k**a kweli tuliokuja ndio wenyewe pia tumefika wote.Baada ya zoezi lile mmoja wa wafungwa alienda kutoa nyundo za kupasua mawe katika banda lile la mbao
"Haya kila mmoja atapita kuchukua nyundo pale nafirki mnajua utaratibu wa hapa, labda kwa mgeni, ukichukua nyundo unaenda katika kifusi cha Yale makubwa ukiwa na mwenzako mmoja utayapasua mpaka yaishe na yasipo isha Leo basi kesho yake utakuta umeongozewa k**a hayo" alinielekeza yule afande baada ya hivyo nilishanga kuona wafungwa wakikimbilia nyundo kisha kukimbia wawil wawili katika kila kifusi cha mawe ya kupasua.
Hata baba y Rahma akiwa bado anachechemea alichukua nyundo na kwenda kwenye kifusi ambacho hakikuwa cha kawaida kupasua mwenyew. Wenzake walikua wawili wawili lakini yeye alikua peke yake pia kifusi cha mawe ya wengine kilikua na mawe makubwa k**a matano, lakini kwake idadi yake ilikua yapata k**a mawe kumi na tano.
Nikiwa nashangaa vile nilishtuliwa kwa kuambia nikachukue nyundo. Niliendea nyundo iliyobaki kwani ni k**a zililekwa kwa idadi.
Nilivyoinyanyua sikutegemea k**a ingekuwa na uzito kiasi kile, kwa sababu nilizani nimebeba Kiroba cha kilo kumi za Michele.
Nilishika vizuri nikiangaza sehemu ya kwenda au kuanza sehemh yangu mwenyewe kwani wote walikua wawil kasoro baba Rahma ndio aliyekua peke yake.
Nikiwa nimekosa muelekeo pa kwenda k**a kuku aliyefunikwa mfuko mara sauti ya ukali ilisema.
"Weeee namba mia mbili hamsini, nenda kwa yule pale aliyokua peke yake" nilisimama vile vile nisijue ni Mimi naambiwa kwa sababu sikuwa nimeshika namba ya ya gerezani.Ghafla nilisikia nimeshikwa kalio kwa nguvu k**a mtu aliyebinya godoro nikageuka kwa hasira kutokana na ile dharau lakini nikakutana na sura ngumu ikichuruzika jasho, imevikwa gwanda la askari magereza.
"We ni namba ngapi" aliniuliza cheche za mate zikinirukia usoni.
Nikaanza kuhangaika kutafuta namba ilipo lakini nikakumbuka iko nyuma ya nguo ile ya magereza nikataka nivue nione, mara akanishika tena kalio. Kiukweli nilitamani nimpige yule askari nyundo afie mbali kwa kitendo kile cha kunishika kalio. Lakini sikuwa na budi kuwa mpole k**a panya aliyeona paka.
"Angalia hapo" aliniambia akinioesha upande wa kushoto mwa kifuani mwangu, nilipotazama ndio nikakuta namba iliyodariziwa kwa maandishi ya kijani.
"Hiyo namba ngapi?"
"Mia mbili hamsini" nilimjibu.
"Sasa mbona nimekuita halafu hujaenda"
"Sikuitambua"
"Sasa nenda kwa yule namba mia na kumi kapasue nae mawe ntakuongezea matano ya kutojua namba mpaka sasa ukiwa jela." Alinioneshea namba mia mbili na kumi ambaye alikua ni baba Rahma.
Nilichoka kabla ya kufanya kazi kuona napangiwa sehemu moja na baba rahma.
Sikuchoka kwa ajili ya yule MTU Bali kwa lile rundo la mawe la kupasua.
Nilitembea mpaka kile kifusi kilipo kisha nikamuangalia baba rahma ambaye alikua anapasua jiwe k**a vile analikuna. Alionekana mtu aliyechoka siku zote, hajiwezi wala afya isingeliweza kumfanya apasue mawe yote yale.
Nilisogeza jiwe moja pembeni lakini halikusoge kwa ukubwa.
Nilishika nyundo kwa mikono miwili kisha nikapandisha juu nikaishusha kwa nguvu zote lakin ile nyundo ilidunda k**a nimepiga mpira.
Wafungwa wengine kumbe walikuwa wananitazama mimi walinicheka mbaya hata baba rahma ambaye alikuwa anaonekana amechoka alitoa tabasamu la maumivu kuona msaidizi wake niliyekuja ni sifuri. Nilijaribu tena k**a safari tatu hali ikawa vile vile nikiangaliwa wengine wanamaliza jiwe la kwanza kwa fujo.
"Nina nguvu kwanini nisitumie hapa kuliko kuwadhuru nazo watu" nilijiongelesha nikiwa naliangalia lile jiwe kwa hasira.
Niliishika nyundo kwa nguvu macho yakiwa nimekazia lile jiwe huku nikivuta k**a hisia za mbwa mwitu.Ghfla macho yakaona wekundu na nguvu za ajabu zikaniingia kisha macho yakaona kawaida lakini zile nguvu nilizihisi bado ziko mwilini mwangu.
Nilipandisha ile nyundo juu kwa mara nyingine nilipoishusha hata mimi sikutegemea, jiwe lilipasuka mfano wa N**i iliyotoka juu sana na kudondokea kwenye upara wa jiwe gumu,
Lile jiwe kubwa ambalo si chini ya nyjndo ishirin ndio liweke nyufa lilichanika ama kupasuka vipande vipande kwa mshindo wanyundo moja tu.
Wale waliokuwa wakinicheka sasa wakaaanza kushangaa wakibeza nilibahatisha lakini zile nguvu hazikuniisha nikawa naenda jiwe moja baada ya jingine, kilichokuja kunisimamisha ni firimbi ambayo niliona wengine wakisimama ndio Mimi nikasimama nikiwa natirirka jasho lakini katika Yale mawe kumi na tano mimi nilikuwa nimepasua kumi na Baba Rahma mawili yakabaki matatu. Niliushangaza umati wa wafungwa eneo lile.

Mida ile ilikua yapata k**a saa sita mchana mbinja ilivyopigwa kwa wafungwa tuliokuwa tunapasua mawe ilisadikika ndio mida ya kupumzika na kutuliza makwapa kwenye kunyanyuka.
Kila mfungwa na mtu wake alikaa kwenye jiwe la kifusi chao, wakaanza kuelezena habar huku vidole vikiwa kwangu.
Nami nilienda kukaa katika jiwe moja wapo la kifusi chetu kisha nikamuona Baba rahma akija huku anacheka ile sura ya uchovu ikimpotea.
"Katika maisha yangu sijawahi ona MTU k**a wewe wallahi" aliongea akiwa anakaa juu ya jiwe la pembeni yangu, nikiwa simtazami kwani alikuwa bado hajanijua.
"Wee mbona waonekana mdogo, lakini una nguvu kubwa hivi eti" aliendele kuhoji
"Kawaida ni nguvu nilizo zaliwa nazo" nilimjibu. Tulianza kuuliza maswali kadha wa kadha haa Yale kuhusu sababu ya kupelekea mpaka kuingia jela. Lakini huwezi amini Baba rahma yule hakuwa ananikumbuka mpaka nikahisi ananifananisha lakini nilipokuja kuamini kwamba ni Baba rahma ni pale nilipomuuliza sababu iliyopelekea mpaka kuwa pale kwa sababu Mimi nlikua nimemdanganya nimeua MTU lakini hakuhoji nimemuuaje na ilikuaje mpaka nikaua.
"Sijui niseme nini mie, lakini huyu mtu siwezi msamehe hata kidogo"akijiweka sawa k**a ana jazba
"Wewe mia mbili........." Akatazama upande wa kushoto mwa kifuani mwangu kisha akaendelea
"Namba mia mbili hamsini Sie tumejuana Leo tu, lakini ninazokwambia hapa usimwambie MTU yoyote" niliitikia kwa kichwa nikiwa nakaa vizuri kuupata ule ubuyu.
"Mimi k**a unavyoniona sio mswahili k**a nyie, nilikuja huku kutafuta maisha lakini maisha yenyewe nilitafuta kiharamu, nilikua na maduka madogo madofo lakini nikaona hayatoshi nikaamua kujiingizakwenye uuzaj wa madawa ya kulevya, nikiwa natoa china au nchi nyingne naleta Tanzania.katika biashara hiyo nilikuwa Mimi na rafiki yangu mswahili alieniunganisha na kundi hilo tukawa tunasambaza wote. Lakini tulipokuja kutajirika ghafla mwenzangu akanitenga Kisa Mimi nilikua nimetajirika sana kuliko yeye,"alikohoa kikohozi kikavu akazidi kuendelea
"Sasa tulivyogombana na kwakuwa tulishakuwa matajiri Mimi nayeye tukawa na ushindani mkubwa ikapeleke tuwe na makundi ya kijambazi na madawa ya kulevya, pia ya utekaji ambao unalipwa, hayo makundi bado langu lilikua lina nguvu, ndipo Huyo mwenzangu akajiingiza katika vyombo vya usalama wa Tanzania kujifanya yeye k**a askari mzuri lakini njama yake ilikua ni kunishika mimi,. na kweli siku moja nikiwa nimejiandaa kusafirisha mwenyewe nilik**atwa uwanja wa ndege wakati miaka yote haikuwahi kunitokea" yale maneno yake yakanikumbusha lile gazeti nililosoma kuhusu kuk**atwa kwake nikamiini kwamba ndio yeye sio mwingine.
"Sasa ikawaje" nilizidi kumfukunyua ili nijue undani
"Ah! Hawa siwezi kuwasamehe kabisa labda nife kwa sababu pindi nilipokamtwa kundi langu lilitetereka ikapelekea kundi la huyo adui yangu kumuua mke wangu na kumteka mtoto wangu wa k**e" aliposema kuhusu mtoto wake wa k**e ni k**a alitonesha kidonda, mwili mzima ulinisisimka nikijua moja kwa moja atakua ni rahma
"Pole sana kwa huyo Ra...... Ah mtoto wako tuseme mpaka sasa hivi katekwa?" nilitaka kutaja jina la Rahma lakini nikakumbuka naongea na mwenye mbwa
"Kwani wewe unamjua mtoto wangu?" Aliniuliza k**a vile alinishtukia
"A.... A. ... Hapana mzee, nitawajuliwa wapi waraabu Mimi?" Nilisema nikijifanya k**a vile chizi au simjui
"Ndio walimteka na mtoto wa huyo rafiki ama adui yangu alitaka kumuoa, lakini kundi langu la kigaidi bado liko hai walienda kumuoko na kwa sasa amemaliza mafunzo ya vita huko urusi, sasa hivi ninavyoongea yupo china anapata mafunzo ya ngumi ili aje kulipiza kisasi cha mama yake na kuniokoa jela hilo ndio tegemeo langu lililobakia" nilipigwa na butwa kusikia vile nakujiuliza "Rahma anajua kupigana vita kwa ule upole wake? Rahama anajua kupigana k**a jet Lee ama Bruce Lee hapana niliona k**a sio baba Rahma au labda atakua Rahma mwingine.
"Kwani ana umri gani huyo mtoto wako wa k**e? Nilimuuliza
"Ana umri wa miaka kumi na saba tu, lakini atakua ni gumzo hii Tanzania haitapata ona"
"Hakuwa anasoma" nilitokwa na maswali mfululizo.
"Kwanini asisome wakati nilikua na hela, alikua anasoma shule ya secondary Ncha huko moshi vijiji alipapenda! anaitwa Rahma Mohammed, kidato cha tatu, lakini kutokana na kifo cha mama yake na Mimi kufungwa, kwa taarifa nilizopata hakutaka kusoma tena alitaka kulipiza kisasi kwa kundi zima waliofanya hayo hasa mkuu wa hilo kundi na wasaidizi wake, sikuweza kupinga lakini niliwambia kuwa kabla hajafanya hayo apitishwe urusi na china kwa ajili ya mafunzo makali akirudi huku hata Mimi baba hake anazweza kuniua nikimsaliti kwa ukatili atakaokua nao" kwakweli mda ule Tumbo lilinivuruga kwa taarifa za baba Rahma kweli niliamini ni rahma, lakini mbona anataka kuwa hivyo, au anggesubiri nitoke jela tulipize wote,
"Kwani huyo jambazi mkuuu au adui yenu wa kumlipiza kisasi ni nan?" Nilimuuliza kwa jazba ya kutaka namimi kulipiza nimsaidie Rahma
"Anaitwa Athumani said.....Nadhani hata wewe unajua"
"Hapana simjui" nilisema Yale kwani kweli jina lile lilikuwa geni kwangu. Lakini alitabasamu kisha akaniambia
"Nafikkiri hakuna anayepasua mawe bila kupita kwa huyo, we Mara ya mwisho ulipita ofisi ya nani kabla ya kuletwa kupausa mawe' alinirudishia swali
"Kwa mkuu wa magereza" nililijibu
"Yes! Yes! Huyo ndio Arthumani Saidi, lakini huku kajibadili anajiita Joseph urio, ndio mkuu wa majambazi na ndio adui yangu mkubwa, na ndio kasababisha mke wangu auliwe, yeye na kundi lake wamefanya niish maisha ya tabu, lakini kwa sasa nafua kiboko yake watakuja kuchinjwa k**a kuku" Aliongea maneno yale kwa hasira na jazba, alikua kashika kipande cha jiwe alikipasua ndani ya kiganja kwa hizo hasira.
Sikutegemea kwamba adui yake atakuwa ni yule mkuu wa magereza aliyenipa Chai ili nijiunge kwenye kundi lake kumbe ningekuwa ni adui mkubwa wa Rahma. Lakini sikujua kwamba yule Mkuu wa magereza na majambazi ana mtandao mkubwa mpaka kunifanya niweze kumtumikia hapo badae kwa atakachokifanya. Mimi niliona labda ile kukataa siku ile ingeniepusha kujiunga na kundi lao
"Kwani wewe Taarifa za mwanao unazitoa wapi" nilirudi katika maswali
"Kwani wew nani,umetumwa kunichunguza nini,eti wewe kijana" aliongea Baba rahma mda ule kwa taharuki kubwa akizani Mimi nimekuja kumchunguza. Alisimama kwa hasira akanikaba koo kwa nguvu ya mikono iliyokomaa kwa sababu ya kupiga nyundo,huku akinilazimisha niseme Mimi ni nani au nimetumwa kumpeleleza.............ITAENDELEA.....

Address

Jacaranda
Mbeya

Telephone

+255623216436

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi Za Kusisimua za twitch posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category