Simulizi Za Kusisimua za twitch

Simulizi Za Kusisimua za twitch Karibu Katika Ukurasa Wa Masimulizi Na Burudani Kwa Wakubwa Uelimike Na Kuchangamsha mwili Pia..

EPISODE 62: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU                 .......ILIPOISHIA......... Aliposema maneni hayi niliona nyewe...
03/10/2025

EPISODE 62: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU


.......ILIPOISHIA.........
Aliposema maneni hayi niliona nyewel na shuka la kimai likienda katika ule mparangani wa lile joka, huko nje kelele za wamama ng'ombe, na wazee pamoja na watoto ndio zilizonidonisha chozi hasa pale lisoyani kuniacha kanifunga............SASA ENDELEA.....
Nilitafuta jitihada za kujikwamua kile kitanzi cha mikono na miguu kwa jina lingine iliitwa (KUDU). Ni mda sio mrefu tu ndio vidonda vilitibiwa, lakini vilianza kuvuja damu tena nikiwa najizungusha na kutapa tapa pale chini ili nitoea kamba.
Nikiwa pale kwenye giza nilisikia sauti ya mtoto mchanga ikilia pembeni kidogo kwenye giza lillozidi kuliko pale nilipikuwa. Sauti yake ilifanana na k**a mtu aliyejifungua siku za karibuni au siku hiyo.
Kelele za kule nje na zile za yule mtoto mchanga zilifanya nianze kujinyanyua ata nikae kwa magoti
"Ntapata wapi panga au kisu nijifungue mimi" nilijisemea moyoni nikianganza huku na kule ili nione kitu cha kujifunga lakini sikubahatika kuona ata ncha ya upanga wala chupa, zaidi ya ngozi zilizotandikwa chini pamoja na vibuyu.
"Hapana sikubali watu wanakufa kisa ujio wetu lazima niwasaudie" niliwaza hayo nikiwa naisugua mikono ambayo mda ule ilikua ishatoa alama za michubuko kwa kuisugua kwa nguvu. Nilianza kukaza mikono k**a naitanua kwa nyuma nikajikuta napata maumivu nakubwa sana. Kichwa nimekilaza chini bado, nilpigwa na butwaa baada ya mwanga wa mwezi kumulika pale niliko k**a niko nje halafu mngurumo mkali ukiwa juu yangu, nilijiuliza swali ambalo sikuweza kujijibu mapema kwa kile nilichokiona.
Matone ya maji yalinidondokea. Wazo lilinijia kwamba ni mvua inanyesha lakini imepitaje wakati nilikua ndani pia kusingeweza kupita mvua.
Niligeuza shingo kuangalia juu kumekuaje mpaka nadondokewa na maji, macho yangu yalitwama kwenye mznuguko wa maji, huku miraba ya mtelezo ikionekana.
Lilikua ni lile joka la ajabu ambalo ni k**a kambale, yule joka alitoa paa la nyumba nililiokuwepo kisha akawa ananitazama na jicho lake lenye kiini cha kijani,, nilihisi mkojo kwa sababu mojakwamoja alikua aniangalia mimi akitaka kunimeza.
Zile kambba ndio zilinifanya nisiweze kukimbia nikajikuta nagala gala chini kwa kuona kifo mbele yangu sauti ya yule mtoto bado ilisikika kwa sana.
Nilianza kuona yule joka akianza kuleta kichwa chake akipanua mdomo uliojaa damu za watu na wanyama wa eneo lile. Bado kule nje wamasai walipiga yowe.
Lisoyani alinifunga kamba lakini hakufnikiwa kumthibiti nyoka mpaka kujua niliko, ina maana na yeye kaliwa au kashachukuliwa na kupelekwa na yule joka karudi tena kwa ajili ya kunimaliza,, nilijiuliza maswali hayo like joka likiwa lishafikisha kichwa karibu yangu kabisa yani yale maji yaliokua yanamzunguka yalinimwagikia k**a naogeshwa na ndoo na bado yeye hayakumuisha kabisa.
Sikuona msaada wowote zaidi ya kufunga macho ili nikifungua nijikute ndani ya tumbo la nyoka au ku*imu. Nilitamani ata niongee kihisia na lisoyani ila zile kelele nisingeweza kufanya vile
Nilifunga macho kisha nikamuomba mungu wangu kwa mara ya mwisho ndipo nikasubiri kifo
Ilichukua dakika k**a mbili bado sikuona tukio la kumezwa na yale maji sikuyasikia tena yananimwagikia,, ile hali ilinishtua kidigo ikanipelekea nifungue panzia la macho yangu tena.
Macho yalipokuwa wazi nilitazama juu sikumuona tena lile joka zaidi ya kuona nyota na mbalamwezi. Ilikua ni hali ya kushangaza kwangu iweje nimuoene mda ule na kwa sasa simuoni.Lakini ghafla nilisikia sauti ya lile joka nje na pia sauti k**a ya lisoyani. Kwa kuwa hisia zangu za kusikia zilikua kubwa kuliko binadamu wa aina yeyote yule hivyo ikawa naisikia ipasavyo bali kelele za watu zilinizingua.
Sauti ya lisoyani haikuwa ile ya kuongea. Ilikua ni sauti ya samaki ambayo naweza kusema ni mru*i mwembamba wa aina yake. Ambao mru*i huo huwa anaubania kuupiga au kuukatisha katisha. Sijui labda wavuvi wanaijua hiyo sauti.
Niliposikia ile sauti nilijua moja kwa moja kwamba ndio maana lile joka liliondoka maana ile sauti ya samaki ya Lisoyani ilimsaidia kumjua alipo.
"Lisoyani, ndio anaenda kuchukuliwa?!!!!!!" nilijiuliza kwa mshangao.
Nilijijua kwamba mimi ni mbwa mwitu na pia ba nguvu kuliko bindamu wa kawaida ata k**a nisipo badilika. Zile kamba alizonifunga Lisoyani zisingeweza kunizuia mpaka mtu aje kunifungua. Ni bora nijiumize nibadilike kuwa Mbwa mwitu kuliko nibaki vile vile watu na yule mtoto mchanga pale chini wakiwa wanalia.
Nilijikusanya nyama, misuli mifupa yani namaanisha nilijivuta nguvu kwa kutoa pumzi kubwa mara mbili.
Baada ya kufanya vile nilianza kujitanua ile mikono niliyofunga ambayo ndio kiungio cha kamba ya miguu. Japo maumivu yalizidi ila wakati uke nilijitolea.
Nilijitanua mishipa ya damu ikawa inatokeza kuanzia ya kichwa mpaka mwilini. Joto kali likinijia huku nikihisi mwili unatanuka. Zile zilikua dalili tosha za mimi kukaribia kuwa mbwa mwitu. Sikutaka kubadilika mwili mzima lakini wakati nakata zile kamba nilihisi macho yanabadilika ila nilijizuia kwa kuivuta taswira ya sura ya Lisoyani.
Ilichukua dakika mbili kucha za mikono zikatokeza na mda ule ule zile kamba zilikatika mfano wa u*i wa kushinoa nguo. Nilichuchumaa chini hali ikitaka kuendelea kubadilika. Kucha zangu nilizizamisha kwenye udongo,huku maumivu ya kubadlika yakinizidi na mimi nikizidi kujizui nisiendelee kubadilika.
Kiukweli ilikua ni mara yangu ya kwanza kujizuia kuendelea kubadiluka katika umbo la kimbwa mwitu, kwani haikuchukua ata dakika tano nilishangaa kuona kucha zikirudi zenyewe. Ile hali ata mimi niliifurahia sana kuona kwamba sasa naweza nikajizuia na ninaweza kujiweka mbwa mwitu.

Baada ya kuona kwamba nimerudi kawaida nilinyanyuka haraka kwenda kwa yule mtoto mchanga anayelia.
Nilifika katika lile eneo alilokua cha Ajabu nilikumta katika k**a kabeseni fulani. Mawazo yangu nilijua lina maji ila nilipo tumbukizqla mikono nilikuta ni mafuta meng sana yalijazwa k**a maji na yule mtoto akiwa ndani.
Nilijiuliza kwanini yupo mule na ukicheki ata kitovu chake hakijakatika vizuri.
Sikuwa na muda wa kupoteza kumjadili yule mtoto japo mpaka leo hii huwa inanitatiza.
Nilichoamua nilimbeba vile vile na mafuta yake kisha kulikua na shuka nyingine ya kimasai maeneo yale niliichukua ni kumviringishia kwa usalama zaidi maana mama na ndugu zake wamekimbia kwa ajili ya lile joka.
Nilipomaliza kufanya vile nilianza kutoka nje ambapo nilipokelewa na moshi mzito wa baadhi ya nyumba kuungua huku baadh ya wamasai wanakimbia. Ilikua ni k**a vita eneo lile kwani ata wale walio aminiwa ni walinzi nao walijikuta wakiliwa na lile joka kambale.
Nilizisikia sauti ya mngurumo wa lile koka mbele kidogo,, ambapo sikuweza kuliona kwa juu kwa ajili wa moshi wa pale.
Mtoto akiwa mkononi bila kujali nilipiga hatua za farasi kukimbia kuelekea kule kwenye uwanja wa mapambano. Njiani kila niliyekutana nae alikllia sana huku wengine wakililia ng'ombe zao, na wengine wakilia vibanda vyao, nafsi iliniuma sana ni bora ata nnbgekua kwetu kuliko unafika ugenini walipoishi kwa amani ila unaleta maaafa makubwa kwa muda mfupi,

Nilipita vibanda kadhaa nikikitiza maz**i ya ng'ombe ambayo hayakuwa na ng'ombe..
Mbio zangu ziliishia ukingoni baada ya mbele yangu kukutana na lile joka halafu chinu kulikua na baadhi ya wamasai wakilipiga na mikuki na sime japo hawakumuambulia ata kumgusa zaidi ya wao ndio walikua wanailiwa. Lakini yule joka alionesha hapambani tena bali alikua anaelekea kwenye ile njia ya ziwa tulikotoka na LISOYANI. Nilijitahidi kumuangalia sana k**a nitamuona LISOYANI lakini sikuweza kumuona ata kwenye lile kundi.
Nilizidi kuendelea kwenda katika ile vita nikijipenyeza hivyo hivyo..........ITAENDELEA......
NAPENDA KUWAOMBA RADHI KWA KUCHELEWA KWA SIMULIZI ZA HUMU NDANI,,

Ahsanteni NAWAPENDA WOTE.....

03/10/2025

IJUMAA KAREEM

EPISODE 61: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU                .......ILIPOISHIA......... Mpaka nilipochoka nikaamua kutafuta ...
26/09/2025

EPISODE 61: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU


.......ILIPOISHIA.........
Mpaka nilipochoka nikaamua kutafuta ulimi wake ulipo nikaanza kuunyonya.........SASA ENDELEA.....

Ulikua mtamu sana zaidi ya asali ndio maana wengine husema mapenzi ni zaidi ya asali lakini umpate anayejua na kuyamudu.

Ghafla tukiwa tunafanya vile lle panzia la ngozi lilifunguliwa
"Alarikoni! Alarikoni!"
Alikua ni yule masai mzee ambaye ni kiongozi akiita lile jina alilonigea.
Tuliachanisha midomo yetu haraka na kwa aibu japo Lisoyani alinogewa sana kwa asababu alikua kanishika shingo kafunga macho hataki niache.
"Umeamuka" aliniuliza yule masai
"Ndio, ahsante sana kwa matibabu na chakula" nilizuga na yale maneno bado aibu ilkinijaa machoni kwani nilijua fika lazima atakua ameniona.
"Sasa twende nje, tukasherekee wote," alisema yule masai akininyooshea mkono nimshike.
Mda huu Lisoyani nae alikua amekaa pembeni kidogo nami bila kusita nilimshika mkono yule mzee nikaanza kunyanyuka yeye akifanya k**a ananivuta japo hakuwa na nguvu sana.
Niliponyanyuka Lisoyani nae alinyanyuka tukaanza kutembea kutoka nje.
Tulifika nje ambako kulikua na wamasai wengi wamekaa na wengine wakisimama wakichzea kwa kuruka juu,, moto mkubwa na mkali ulikua umezungukwa pia nyama ilikua kati inachomwa.
Wamasai wengine waliotuona walitutazama kila aliyeniangalia alibaki kunishangaa k**a ni mtu flani wa majaabu. Nakumbuka kuna katoto kamoja cha kimasai kalikuja kunikumbatia miguu huku kananiangalia na kucheka. Nilitabasamu ila kabla sijamshika yule mzee mmasai alimfukuza.
Tulizunguka lile kundi tukafika sehemu kuna kiti kikubwa na kilichokua hakina mtu na viti viwli vya pembeni vilikua na wale wamama walionipa dawa.
Tulisogezwa mpaka pale kwenye kile kiti kisha yule mzee alisimama mbele Akanishika mkono vizuri akanyamazisha wale wamasai
"Nyamazeni,watu wote niwatambulishe kwenu, shujaa wetu,," (ALIONGEA KIMASAI LAKINI BAADA YA KUYASHIKA YALE MANENO NILITAFUTA MMASAI ANAYEJUA KISWAHILI ANITAFSIRIE) baada ya kusema vile wale wamasai wote walinyamaza wakatuangalia sisi.
"Huyu kijana mnayemuona hapa ndio aliyemuua mamba, ameingia kijijini kwetu amepotea" miguno na kilugha vilisikika kiongozi akaendelea
"Wamepotea na rafiki yake huyu hapa," alisema hayo akimshika mkono lisoyani akaunyanyua juu kile kitendo cha kuunyanyua mkono wa lisoyani ilipiga radi kali na ya ajabu kwenye anga wingu k**a la mvua likatanda ghafla.

Ile hali ilinishtua sana sio mimi tu ata yule kiongozi wa kimasai na wamasai wote waliangalia juu kwa mshangao wakizozana ile hali imetokeaje.
Lisoyani nae alionesha kuwa na wasi wasi tukatazamana.Baada ya kushusha ule mkono wa Lisoyani ilipita k**a sekunde thelathini hali ikarudi kuwa shwari k**a hapo awali hapo ndipo kila mmoja alianza kutilia shaka k**a lisoyani japo wamasai wengi waliona ile ni k**a kawaida tu.
Yule kiongozi alinyamazisha tena akaendelea
"Wageni hawa wamekuja na ishara ya kuwa kutanyesha mvua kubwa hapo baaadae ambayo ilikosekana kwa miaka mingi, hivyo tuishi nao vizuri mpaka watakopoondoka kwao" wote walipiga makofi na vigelegele mpaka mwenyewe nilifurahi kwani niliogopa nikaona huwenda watamtilia shaka Lisoyani
Baada ya vike aliitisha mtu mmoja aje na kikombe flani kisha yule mtu alipokuja alichukua kile kikombe kilichokua na kitu ndani akaanza kunikabidhi mimi.
"Kunywa hii,inaonesha kuwa umekubali kuwa katika jamii yetu" aliposema vile nilikichukua kisha nikapeleka mdomoni. Nilipokunywa niligundau ilikua ni damu mbichi sijui ya ng'ombe au myama gani ila ilichanganywa na chumvi.
Nilishusha haraka nikataka kumkabidhi lakini akaniambia tena
"Mpe na iyo rafiki yako nae anywe" hapo ndio ikawa kazi kwani sikuwahi kumuona lisoyani ata siku moja akinywa kitu hata maji, ile damu aisee nikaona mtihani.

Sikuwa na budi kwani ata Lisoyani nae Alinyoosha mkono akitaka kuchukua mwenyewe. Nilimkabidhi akapeleka kile kikombe bila wasi wasi wowote.
Cha kushangaza baada ya kufikisha kwenye mdomo hakukitoa mda ule ule aliinywa, alipokuja kukirudisha kikombe, hakikua na damu hata kidogo tena alijilamba kabisa midomo yake.
Kiukweli nilibaki kumshangaa ila kwa wale wamasai walimfurahia na kumpigia vigele gele zaidi kuliko mimi. nikajikuta nacheka huku najiuliza maswali mengi kuhusu kile ktendo alichokunywa damu nyingi mbele yangu,
Tulipomaliza kabisa kufanya vile tuliruhusiwa kwenda kukaa na wamasai wengine waliokua wamezunguka pale.
Nilimshika mkono lisoyani kisha nikaangaza macho sehemu ya kukaa nikamuna yule mtoto mdogo aliyenishika mwanzo anatabasamu akiwa amekaa na yeye na wenzake. Nilianza kutembea kwenda pale alipo kisha tulipofika tulikaa chini
"Mambo" nilimsalimia yule dogo lisoyani akiwa pembeni, lakini yule dogo hakuitikia kiswahili matokeo yake alianza kuongea kimasai ikawa lugha gongana.
"We lisoyani mbona ulikunywa ile damu k**a ndio chakula chenu?" Niliimuliza Lisoyani baada ya kuacha kuongea na yule dogo
"Haha! Nilijua tu utashangaa ila mimi nilipokunywa nimeipenda japo, sijawahi kunywa kule, nimetokea kuipenda tu tamu sana" alinijibu bila wasi wasi wowote.
"Khaa! Hujui ile ni mbichi" nilizidi kumuuliza
"Ata k**a, ila nimeipenda," lisoyani alizidi kunishangaza kuniacha mdomo wazi
Mda ule alitazama wale wamasai wanaocheza na wanaume wanaoruka juu.Alionesha kufurahia ile michezo kwani alinisahau ata kuniangalia akawa anapata mzuka wa kuruka.

Sikujua kwamba ndio tabasamu la mwisho mwisho kuona kwake akifurahia na mimi akiwa ana furaha kubwa namna ile. Nami ikabidi niangalie wale wamasai kumsapoti yeye.

Ilipita k**a dakika kumi tukiwa tunanogewa na michezo ya pale kila mtu alikua ana furaha yake kutuonaa sisi. Lakini furaha yetu ilikuja kuwa kilio, masikitiko, lawama na majonzi makubwa.

Mara ghafla Kwenye z**i la ng'ombe ambalo lilikua mita chache kutoka pale wale ng"ombe walianza kulia k**a wamevamiwa na kitu . Ng'ombe waliokua na nguvu walianza kuvunja mbao za lile z**i.

Kila mmoja aliyekua katika mkusanyiko ule alishtuka na kunyazama kisha nikaona watu wanaanza kukimbilia kule kwenye z**i hasa yule mzee nahisi walijua labda ni wezi wa mifugo kwa sababu walisikija waliojua kiswahili wakisema
"Mwisi! Mwisi" wakienda kule kwenye z**i kulikokua na giza kidogo.
Nilisimama na Lisoyani maana pale chini tulikua tunakanyawa
"Nini tena hiyo Dominick?" Aliniuliza tukiangalia wale watu wanapoenda
"Sijajua Lisoyanu labda ni we...." kabla sijamaliza ulisikika mngurumo mkali sana ukiambatana na radi k**a ile ya Lisoyani pia wale wamasai waliku wameenda kwenye z**i walirudi tulipokua kwa kasi ya ajabu k**a wanakimbizwa.
Tukiwa tumesiman ile sauti ya mngurumo ilisika juu tukaanza kuanyanyua macho kuangalia.

Loo! Sikuwahi kuona kiumbe wa aina ile. Alikua ni mfano wa nyoka sio nyoka au kambale sio kambale kwani aliku ana sharubu k**a kambale na kichwa ka cha nyoka kakinyoosha juu akiwa mrefu na mnene k**a nyoka aina ya Anakonda.
Mdomonu alikua amechafuka damu na ng'onbe walliomezwa mda ule walinasa katika meno yake ni zaidi ya hamsini kwani walijaa mdomoni k**a z**i. Hiyo haitoshi cha kuogopa zaidi
Alizungukwa na maji yani ule mviringo wake wa nyoka wote ulizungukwa na maji k**a anayembelea maji, mpaka kwenye kichwa kilikua kimezungukwa na mviringo wa maji.
Nguvu za miguu ziliinisha Lisoyani nae alionesha k**a anashangazwa na k**a yule nyoka kambale ana mfahamu.

Mara alinishika mkono na kuanza kunikimbiza mda huu yule nyoka kambale akiwa anendelea kuaharibu kijiji na kuwala watu pamoja na mifugo iliyokua karibu yake.
LISOYANI alinikimbiza akinishika mkono nisijue kwanini kafanya vile.
Tuliiingia katika nyumba moja tofauti na ile ya yule kiongozi ambapo hakukuwa na mtu yeyote zaidi ya giza la umbali nahis watu waliokua mule ndani walikimbia kutpkana na ile balaa ya mda ule.
Tulipoinga kabsa lisoyani alinikalisha chini
"Dominick tulia hapa, sitaki uingie katika hii vita, yule ni mnyama kutoka kwenye falme ya CHINGWENE katumwa aje kunitafuta, haya ndio madhara ya mimi kuwa duniani,, na akikuona wewe lazima akuue maana atakua amelishwa damu yako ikiyobaki kwenye tenga ndio maana anaua kila mtu mpaka apate damu yako," aliongea haraka haraka maneno yaliyonishangaza sana. Kumbe ndio maana alikua kashtuka alipomuona.
Lakini tatizo langu nilikua mbishi sana sikutaka kuona anakufa hivi hivi au anaondoka
"Hapana Lisoyani kwanini nisiende kukusaidia na pia kuwasaidia hawa watu?"
"Hapaaaaaanaaa, Dominick lazima utakufa jamani......" Wakati anaongea vile alitazama pembeni sikujua aliona nini,
Alitoka kidogo akaenda ile sehemu akarudi na kamba fulani ya ng'ombe
"LISOYANI unataka kufanya nini?" Nilimuuliza lakini kabla hajanijibu alinirukia akanigeuza nyuma kwa nguvu nikalala na tumbo.
Alivuta mikono yangu nyuma k**a ananifunga pingu ile kamba aliyoishika akaaanza kunifunga. Hapo ndipo nikaona ukichaa wa Lisoyani.
"Tafadhali lisoyani usinifunge niache tu" nilianza kuongea kwa ukali na msisitizo lakini Lisoyani alinizidi nguvu maradufu akafanikiwa kufunga mikono kwa nyuma nikijarubu kujinasua lakini la hasha ilikua kiboko
"Utanisamehe Dominick sina chaguo lingine"alisema hayo akishika miguu yangu na kufunga na ile ile kamba jumla alifunga miguu na mikono sehemu moja yani ni zaidi ya mwizi au mateka. Alipomaliza kunifunga alinigeuza taratibu nilipogeuka nilikuta anadondosha chozi jekundu.
"Kwanini unanifanyia hivi Lioyani" nlimuuliza nami nikilia kwa uchungu
"Hiyo yote kwa sababu nakupenda sana Dominick" alisema maneno hayo akanirukia mdomoni na kunipa mate chozi lake likadondoka kwenye shavu langu. Alilinibusu sekunde k**a ishrini kisha alitoka Midomoni mwangu, akaanza akutoka nje.
"LISOYANI LISOYANI TAFADHALI USINIACHE" niliita kwa nguvu akiwa amefika mlangoni akanigeukia chozi likizidi kumtoka radi na ngurumo zikitanda eneo lile
"Nakupenda sana, ata k**a nisiporudi au kufa endelea kunipenda milele ipi siku utaniona" ni maneno ambayo aliniambia lisoyani mpaka leo hii napata imani ya maneno yale kuwa ipo siku nitamuona.

Aliposema maneno hayo niliona nywele na shuka la kimai likienda katika ule mparangano wa lile joka, huko nje kelele za wamama ng'ombe, na wazee pamoja na watoto ndio zilizonidondosha chozi hasa pale Lisoyani kuniacha kanifunga..........ITAENDELEA......

26/09/2025

MPO ONLINE NIWASHUSHIE EPISODE INAYOFUATA. .

EPISODE 60: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU            .......ILIPOISHIA.........Mda huu tulikua tushaanzakukaribia kwenye...
25/09/2025

EPISODE 60: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU


.......ILIPOISHIA.........
Mda huu tulikua tushaanza
kukaribia kwenye nyumba fupi na
zilizoezekwa kwa nyasi huku maz**i
ya ng'ombe yakiwa yamechukua eneo
kubwa sana........SASA ENDELEA....
Nilishushwa chini na wale wamasai walionibeba wakizidi kuimba na kuweka mabezi ya nyimbo za kimasai ambazo mara nying huwa nazisikia kwenye maredio au kuangaliaa kwenye televisheni lakini siku hiyo nilizisikia na kuonaa
laivu.
Baada ya kushushwa nilimkimbilia Lisoyani ambaye mda wote tangu nibebwe alikua anacheka na kutabasamu sana
"Vipi mbona una furaha sana" nilimuuliza nikiwa nimeshamkaribia tukiendelea kwenda kutembea.
"Yani wewe umejifanya umemuua mamba halafu umebebwa mimi niliyeua natembea kwa miguu ata hawanithamini" alisema maneni hayo akiwa amepitisha mkono wake kati kati ya mkono wangu k**a bibi harusi na bwana harusi.
"Hamna unajua nini Lisoyani mimi niliona kwamba nikisema ni wewe watatilia mashaka, kwa hiyo zile sifa ikabidi nibebe mimi ili waniamini kwa sababu mwanaume huku duniani ndio anatakiwa awe na sifa k**a hizo" nilimjibu lisoyani mda huu wanakijiji wa eneo lile walianz kuungana na sisi kwa kuwa walimuona yule mamba, Kichwani mwangu nilihisi lazima tutakua tunaenda kwa kiongozi wa kijiji au mwenyekiti. Kwa kuwa jamii k**a zile lazima kuwe na kiongozi na endapo kukiwa na tatizo lolote basi huwa lazima lianzie kwake.
"Dominick huku ndio kwenu?" Aliniuliza kwa sauti ya juu Lisoyani mpaka nikashtuka kwani sikutegemea k**a atapayuka vile.
"Duh! Kwanini umeniuliza hivyo?"
"Hapana naona k**a tunaenda sehemu halafu wewe unafurahi k**a unakujua"
"Sio hivyo lazima nifurahi kwa sababu nimerudj duniani, na hawa ata siwajui ila nafikri watanisaidia kunipeleka nyumbani kwetu kwani nikishajua niko wapi nitaweza kwenda ata mwenyewe" nilimueleza Lisoyani kwa upana na urefu ili aelewe vizuri

"Anhaa kumbe" mda huu tulikua tushafika kwenye nyumba fupi kubwa iliyoezekwa na nyasi huku, ukuta wake ulikua umerembwa na kinyesi cha ng'ombe ambacho kikikauka huwa k**a simenti fulani. Lakini niliiona kwa pembeni kwa sababu mbele yangu niliku nimezuiwa na wale wamasai waliombeba mamba.
Tulisimama wale wamasai nilisikia wanamtupa yule mamba chini kisha mmoja aliongea baada ya wote kukaa kimya
"Mwenyekiti ya boma, njoo kuna ugeni umetokea hapa" baaada ya kusema maneno yale nilisikia k**a mtu anatoka kwani ata zile nyimbi zao hazikuwa na milango bali ni k**a panzia la ngozi.
Yule mtu alitoka japo nilijaribu kumchungulia, ila sikumuona vizuri kutokana na urefu wa wale wamasai. Mara yule aliyeitwa aliropoka kwa ngivu kwa kimasai k**a kashangaa kitu fulani
"Nani kamuuua huyo mnyama anayekula ng'ombe zetu, nimpe zawadi" baada ya kusema vile sikuona mtu yeyote anajibu cha zaidi niliona wale wamasai wakifanya njia k**a wanatuekea njia. Walivyofabya vile ndio nikaona sura ya yulr mmasai, alikua mweusj na uso uliong'aa k**a kapaka mafuta meng huku, nywele zake zilikua nyeupe. Baada ya kutuona mimi na Lisoyani alituangalia kwa mshangao sana
"Hawa ni wakina nani?" Aliuliza akituoneshea kidole
"Huyu ndie aliyemuu huyo mnyama"alisema yule mmasai mmoja kile kitendo kikamshangaza yule mmasai mzee ambaye ndio k**a kiongozi wao.Alianza kutufata pale tulipokua tumesimama Lisoyani akiogopa kidogo. Alitembea k**a miguu yake ilikua na stroke flan yani inatetemeka.
Hatua kadhaa aliku ashatufikia kwanza alinitazama mimi, kisha akamtaza lisoyani ghafla alinishika masikio. Kidogo nikimbie kusema labda anataka kunitoboa k**a walivyo wao ila nikashanga akawa anayashika kuyapapasa.
"Wewe ndio umeua ile kweli" aliniuliza swali hiyo baada ya kughndua kuwa sisi sio wamasai kwa sababu hatukufanania na wao.
Nilisita kujibu kidogo kisha nilimuitikia kwa kichwa k**a ishara ya kukubali ndio mimi. Nilivyofanya vile yule mzee

Alicheka ile mbaya, kile kitendo kiliwashangaza wale wamasai wengine pamoja na mimi. Alicheka sana akachanganya na kicheko cha kimasai
"Umewesaje kuuaa hiyo" aliniuliza mda huu akicheka taratibu, sasa sikuelewa labda aliona utani au aligindua kwamba siwezi kwa ajili ya umbo langu.
"Nilimyonga mpaka akafa" nilimjibu kwa ufupi
"Basi wewe ni AIKORI" aliniambia neno la kimasai ambalo baada ya kuja kuuliza niliambiwa maana yake ni SHUJAA,
"Mimi ndio mkubwa ya boma yote hapa, kwa hiyo matatiso yako nawesa nikasikilisa ulipotoka mpaka umefika hapa" yule masai alijitambulisha kweli kwamba yeye ndio k**a mkuu wa pale au ndio mwenye ng'ombe nyingi kuliko wote, kwa hiyo ndio maana alikua kiongozi wa maboma eneo lile
"Aaah! Sisi tulipotea njia maana tulikuja katika mbuga za Ngorongoro ndio tulipotelea huko" nilimwambia kwa msisitizo na ishara ili aelewe zaidi
"Umetokea wapi" aliniuliza
"Nimetokea Moshi tulikuja kwa utalii huku"
"Visuri sana, mimi nitakupa wewe msaada, lakini sio leo kwa sababu usafiri wa kwenda kupata gari za kwend Moshi hauko na pia ni mbali" aliniambia meneno yalinichosha kidogo ila kwa upande mwingine yalinipa matumaini ya kupata msaada.
"Hiyo ni bibi yako?" Aliniuliza swali lililonifanya nishangae kwani alisema yale akimuoneshea kidole Lisoyani. Ata nae Lisoyani alishtuka.
"Bibi?" nilimuliza k**a sijasikia kwa kuwa aliyempointi hafananii na bibi
"Ngarawai!!! Nyinyi kwa swahili iko sema mke" nilicheka kidogo baada ya kujua ana maanisha nini. Nilimtazama Lisoyani nae vile vile alikua anatabasamu.
"Hapana ni rafiki yangu tulitepoteana nae" nilimjibu uwongo wa ukweli pasipo kujua yule ni jini la maji. Aliizidi kuniangalia akifurahia uwepo wangu. Mara alianza kuangalia kwenye mbavu zangu kisha alinifata kwa kasi akafungua lile shuka la kimasai. Alivyofunua na mimi ndio niliona anatazama nini
Kumbe kile kidonda cha mbavuni kilikua kinamwaga damu sana mpaka kuloanisha lile shuka ndio maana yule masai aliona. Sio hivyo tu kulikua na vidonda vingne vimejaa kila sehemu yule masai ikabidi ashangea inakuaje bina vidonda vikubwa k**a vile halafu naongea kawaida. Ata mimi ile hali ilishangaza kwani sikusikia maumivu yotote mda ule ni michirizi ya damu tu ndio ilitoka.
"Umeumia sana,, unatakiwa kutibiwa mara moja" alisema vile kisha aliongea wa sauti ya juu k**a anaita jina. Sekunde chache badae walitokeza wamama wawili kisha walipotufikia waliongea kimasiai wakutuacha njia panda mimi na Lisoyani.
Walijibizana k**a dakika mbili kisha alitugeukia sisi akatuambia tuwafate wale wamama.
Mimi sikusita nilianza kupiga hatua kisha Lisiyabi nae alifata kwa nyuma tukaanza kuwafata wale wamama nikichechemea mguu niliong'atwa kidogo na mamba.
Kwa nyuma tuliacha majibizano na mizozi bainaa ya wazee wa kijiji na yule mkuu pia wale vijana walio tuleta.

Tulipiga hatua chache kisha tuliingia katika ile nyumba kubwa lakini vidirisha na fremu za milango ilikua ndogo huku paa lilikua karibu sana kusababisha wao wainame k**a wanaingia kwenye pango.
Mule ndani kulikua na la giza wastani, cha kushangaza mule mule ndani kulikua na mbu*i na ngozi zimetandikwa pembeni, k**a mkeka wa kulalia na mbu*i walikua karibu huku vinyesi na harufu kali ikitapaa pale.
Walifika katika ngozi moja iliyotandikwa kisha wakasimama wakatuangalia mda ule mimi na Lisoyani tulisimama tukivumilia ile harufu kali ya mule ndai ila Lisoyani alionesha k**a hakuhisi sana k**a mimi nilivyohisi.
"Wewe njoo hapa" aliongea mama mmoja wa kimasai akinioneshea kiidole mimi.
Niliwafata pale walikosimama. Nilipofika waliniamrisha nilale kwenye ile ngozi nami bila kipingamizi nilifanya vile japo sikuiamini sana ile ngozi lakini wanasema ukishi kwenye kundi la viziwi lazima nawewe ufanye k**a viziwi ili uendane nao hivyi kwangu ile harufu nilijitahidi sana kuimudu niwe k**a wao.
Baada ya kulala, niliona mmoja anaenda kwenye k**a vyombo kisha alirudi na kibuyu kadogo akakifungua na kunikabidhi.
Nilipokichukua alinionesha ishara ya kuwa ninywe.Kwanza nilisita kufanya vile nikamuangalia lisoyani.
Lisoyani alionesha hana wasi wasi na ile dawa kwani nae alinionesha ishara ya kuwa niendele kunywa.
Nlipo ona vile nilianza kupeleka mdomoni japo nilipofiksha karibu na mdomo kile kibuyu kilitoa harufu kali ya dawa ya mitishamba. Nilijikaza kiume hivyo hivyo kisha nikaipeleka mdomoni na kunywa.
Kwakweli ile ilikua ni dawa chungu kuliko zote unazozifahamu kwani nilipokunya nilihisi kam nakunywa shubiri au mualovera mpaka mwili ulisisimka.
Nilipokunywa fundo moja yule mama alikichukua kile kibuyu kisha wakaanza kuniangalia k**a Tv nisijue kwanini wanafanya vile.
Ilipita k**a sekunde thelathini, macho yakawa yanaanza kuwa mazito yani kuona sioni vizuri k**a usingizi wa ghafla unaninyemelea.Nilijitahidi kujikaza nisifunge macho ila wale wamama wakinasai walinikazia macho huku mimi nikizidiwa na usingizi mzito.
Haikichukuwa mda pala pale usingizi ulinipitia sikujua kilichoendelea.
*****
Nilikuja kupata nafuu au fahamu baada ya kusikia kelele za miguno na vishindo vyawatu k**a wanaruka nje, nilifungua macho kuangalia nikaona ni moto umewasha halafu pembeni yangu alilala mtu.
Nilimuangalia yule mtu nikaona nywele nikagundua kwamba ni Lisoyani. Nilinyanyuka upande wa mbavu zikiuma ila nilipoangalia niliona kuna majani yameganda kwenye vidonda mfano wa dawa za miti shamba.
Nilipokaa vizuri karibu na mimi pia niliona nyama kubwa iliiyichomwa vizuri pamoja na kisu na kibakuli chenye supu iliyopoa.
Nilimuamsha Lisoyani aliyekua amelala usingizi kabisa.
"Lisoyani?! Nilimuita nikiwa namshika bega nikimtingisha. Sikumuita hata mara ya pili mda ule ule aliamka k**a kakurupushwa.
"Dominick, umeamka mhh ndio nililetewa supu nikunyweshe ila nikaona mpaka uamke sijui ishapoa"
Aliongea mfululizo akiendeaa ile bakulli ya supu.
"Achana nayo kwanza, mbona kuna kelele za nyimbo huko njee, na sa hv n mda gan?"
"Jamani wewe huoni ni Usiku? Na huko nje wanacheza ngoma zao na yule mamba wamemchuna ngoz nyama wanamla,nyie binadamu mnakula kila kitu yani"
"Kwa hiyo wewe umekula nini, Lisoyani?" Nilimuulza nikiwa nasogea karibu nae.
"Nishwakwambia inaweza kupita ata mwezi sijala,, na hapa sijaona chakula changu kwa hiyo siwezi kula,, embu kunywa hii supu" alinijibu akanikabidhi lile bakuli la supu.nililichukua nakuanza kunywa japo ilikua ya baridi lakini niliinywa k**a maji kwani nilikua na njaa sana. Kabla hajafanya chochote nilichukua kile kisu kisha nikakata mnofu wa nyama iliyonona na kuchomwa vizuri.
Nilikata pande kubwa nikaanza kula k**a mbwa aliyekua na njaa mda mrefu.
"Hee binadamu ndio mnakulaga hivi mkiwa Duniani?"
Nilishtukia naulizwa swali na lisoyani nikiwa katika pilika pilika za kuparamia ile nyama bila mapumziko.
Nilisimamisha nyama mdomoni nikaanza kuona aibu tulipokutana macho kwa macho na lisoyani.
"Ha...pana" nilimjibu hamu ya kula ile nyama tena ilikata maana nilishajiabisha mbele ya mrembo k**a yule.
"Haya endelea kula"
"Usijali, nishashiba" nilimjibu nikarudisha ile nyama chini.
"Mbona hivyo sasa ata hujala sana embu kula huko" aliniambia hayi akiwa anachukua ile nyama.
Nilishika mkono wake nikamzuia asiendelee kuchukua.
Nilipofanya vile aliniangalia tena kisha akajikuta anaanza kusogeza uso wake karibu yangu.
"Dominick bado natamani kile kitendo ulichonipa siku zile, natamani unipe tena zaidi, sintojali kwamba nitabadilika wala kudhurika ila nifanye nifurahie kuwa nawewe, nimetoroka na kuacha ufalme wetu kwa ajili yako na pia ni kwa ajili unioneshe mapenzi yako, sijaja huku kwa ajili ya kuona dunia na watu hapana, nimekuja kwa ajili yako" yalikua ni maneno ya utuluvu na utashi wa hali ya juu, sijui alisoma wapi maneni matamu k**a yale yaliyonisismua nywele, nilibaki tu nakodoa macho nisijue ata nimjbu nini Lisoyani. Sikuweza kumuahidi kwamba nitamuoa wala kumfanya wa milele, pia mara nyingi yeye ndio alinonesha upendo na maneno matamu kuliko mimi nilimsubiri yeye ndio aanze. Hilo nalijutia leo kwamba ile nilifanya makosa ata leo hii kumkosa lisoyani. Kiukweli k**a una mpenzi anakupenda ata k**a humpendi sana hakikisha unamuonesha ata mapenzi kidogo ya dhati umgariji na kumpa ahueni ya kuhisi k**a yeye pia anapendwa hilo ndio nilijifunza kutoka kwa Lisoyani.
"Dominick Nakupenda" alirudia neno hilo tena siku ile huku akinishika nyuma ya shingo akisogeza katika midomi yake. Ile ndio ilikua furaha ya lisoyani kuona mimi nikumbatie na pia kumpa denda. Kwa hiyo alivyonivuta nikajua anataka nini sikusubiri atumie nguvu zake kunisogeza bali nilipeleka haraka midomo yangu ikagota kwenye midomo milaini na mekundu ikiwa imerembwa na meno meupe k**a jiwe la (CRISTAL) na yaliyopangika vizuri.
Nilitumbukiza wake mdomo wa chini katika kinywa changu kisha na yeye altumbukiza wa juu katika kinywa chake ndipi tukaanza kubadilisha midomo na mate. Mpaka nilipochoka nikaamua kutafuta ulimi wake ulipo nikaanza kuunyonya, ...........ITAENDELEA.........

Address

Jacaranda
Mbeya

Telephone

+255623216436

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi Za Kusisimua za twitch posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category