14/12/2025
EPISODE 96: NUSU BINADAMU NUSU MBWA MWITU
........................ILIPOISHIA..............
Askari aliyekua anatuchunga aliingia mule ndani kashika Rungu kwa ajili ya kutoa kipondo kwa anayetaka kubaka........SASA ENDELEA........
Yule askari alipofika mule ndani aliuliza ni nani aleyetaka kubaka, mfungwa niliyekua nampapasa nikiwa ndotoni alinipoint Mimi kisha yule askari alikuja kwa hasira.
"Unafikir huku kuna ufiraun k**a kule" kabla sijajitetea kuwa ni ndoto, nilipigwa rungu ya kwenye mbavu zikalia k**a mfuko wa simemti uliopigwa na ubao.
Maumivu makali yalipita ndani ya mbavu zangu, nikizuia upande huu napigwa kwingine, Wafungwa wengine k**a kawaida yao walicheka k**a hawana akili nzuri wakizani labda nilikia nataka kubaka kweli.
Baba Rahma alitamani anunue ile kesi tena lakini asingeweza kutokana na tulivyokuwa tumelala.
Nilipigwa mpaka alipochoka ndio nikamwambia.
"Afande unanionea tu, haikuwa lengo langu, kumfanyia vile ni ndoto tu" watu walicheka tena lakini yule askari alimuuliza niliyekua nampapasa
"Ilikua ndoto kweli huyu au makusudi" Mfungwa aliyenisemea kwamba nilitaka kumbaka alikaa kimya kidogo kisha akasema.
"Labda itakuwa ndoto kweli maana alivyokua ananipapasa na kunibusu alikua anataja jina la Rahma!" Vicheko vingine vilifatia yule askari nae akabaki kucheka nakuniacha na maumivu huku akimshtumu mfungwa aliyesema kuwa nataka kumbaka kumbe ilikua ndoto.
Usiku ule sikuwa na hamu ya kulala tena mauimivu yakiwa yametapakaa kila kona ya mwili wangu.
Nilimtazama Baba rahma alionekana kunitazama nanyeye kwa umakini akiwa anaonekana k**a kagundua kitu kwangu.
Nilienda kujikunja sehemu nyingne ya kulala huku nikitema mate kwenye sakafu ovyoovyo kila nilipokumbuka kuwa nimenyonya ndimi ya mwanaume mwemzangu tena ambae mswaki haujatiwa kinywani mwake siku nyingi.
Ilikua asubuhi ya siku nyingine tena,, ubaridi ukipuliza mpaka kwenye uwanja wa makwapa nikijikunja miguu ikakaribia kidevu kwa lile baridi.
Firimbi yakutuamsha haikuwa nyuma na wakati, mda ule ulikuwa kwa ajili ya kuamka na kunywa uji kisha kwenda kwenye ile kazi ya kupasua mawe.
Baada ya kuamka tulipewa uji kwani sisi tuliletewa mule ndani tukitengwa kabisa na wafungwa wale wakawaida.
Tulipomaliza tulianza kuongoza mstari mmoja kuelekea kwenye Karandinga k**a kawaida askari mmoja akiwa katangulia na mwingine nyuma yetu tukitembea. Katika mstari nyuma yangu alikua Baba rahma ambaye toka Jana usiku alionekana kanitilia wasiwasi.
"Kijana ni nini kimekufanya ukafika mpaka hii jela, si uliendaga NgoroNgoro?" Nilishtuka kusikia Sauti ikinena kwa kuniuliza swali lililoendana na ukweli wangu wa nilipotoka. Hakuwa mwingine ni Baba rahma aliyeniuliza Swali la namna ile.
"Ina maana Amenigundua mimi ni nani" nilijiuliza kimoyomoyo kabla sijamjibu kwan mida ile tuliongea kwa kunong'ona.
Kwa taharuki niliyopata sikuweza kumjibu wasi wasi ukanipanda kwamba amejua mimi ndio niliyeenda NgoroNgori ina maana ile ndoto ya jana yake usiku imemjulisha mimi ni nani baada ya kutaja jina la Rahma.
Tulifika kwenye karandinga wakati najiaanda kupanda walitokea askari wawil ambao niliwafahamu kwa sura wale waliozoea kunipeleka kwa mkuu wa magereza walisimama pembeni
"Afande Joshi tunamuomna namba mia mbili hamsini, Leo hatoenda huko" alisema askari mmoja aliyekuja kisha yule aliyekua anatuongoza kwenye karandinga, alitazama ule mstari.
"Namba mia mbili hamsini tokaaaa" nilijikausha k**a sikusikia kutokana nilijua kile ninachoitiwa na wale askar ni utumbo mtupu bora kwenda kupasua mawe.
Walisubri nitoke lakini sikutoka ghafla wale askari waliokuja wakanifata na kunishika kwa nguvu.
"Hivi wewe unaringia nini hapa jela mpaka unakua mbishi" aliniuliza askari mmoja aliyekuja kunichukua
"Naringia kuumbwa mwanaume la sivyo ungekuta nimekua mama yako" nilimjibu kwa jeuri akanitazama kwa hasira bila kunifanya chochote sikujua kwanini hawakuthubutu hata kunifinya na ukicha.
Wakat naondoka kutoka eneo la mstari Askari wa jana yake usiku nae alikua kwenye karandinga alipayuka
"Kumbe ni huyo aliyetaka kumbaka mwenzake akizani Rahma hahahahaha" maneno na kicheko chake kilisindikizwa na vicheko vya wafungwa.
Niligeuka nyuma kutazama, macho yangu yaligongana na mboni za baba Rahma aliyenitazama kwa wasiwasi.
Kichwani mwangu nikiwa natembea kuelekea kwa Mkuu wa magereza kwa mara nyingine nilijiuliza ananiitia nini wakati nilimktalia na kwanii ananitaka mimi tu.
Dakika chache baadae tulifika mlango mwa ofisi ya mkuu wa Gereza lakini siku hiyo mezani mwake kulikuwa na ugeni wa watu wawili mmoja kasimama kushoto kwakwe na mwingine kulia kwake, wamevaliza suti nyeusi iliyowabana kupindukia kufanya miili yao k**a jiwe ijichore vizuri nakuonesha miraba sita. Usoni sura zao hazikuonesha Tabasamu hata kidogo ikiwa imefunikwa na miwani mikubwa meusi.
Niliposimama mbele yao Mkuu akiwa kakaa kwenye kiti siku hiyo hata yeye hakuonesha tabasamu k**a ilivyokuwa awali hali iliyonitishia amani huku laptop nyekundu ikiwa imefunguliwa mezani mwake
"Mshikeni mikono" aliwaambia wale askari walionileta bila ya kubisha wale askari walinishika k**a vile niliiba chao.
Mkuu wa magareza alipoona nimeshikwa mkono aliwauliza wale wageni waliovalia suti.
"Vipi mnamuonaje"
"Boss mbona anaonekana bado dogo sana hakina afya imekuaje una mpa sifa zote" alijibu mmoja aliyesimama upande wa kuume kwake
"Ngoja utaelewa kwanini namuhitaji kwa hudi na uvumba" alipokwisha kusema hayo alinyanyua simu yake kisha akaiweka masikioni akitazama ile laptop
"Hey! Kishoka, mshakamilisha mission na mtandao mshauweka sawa" alimuuliza yule aliyekua anaongea nae kwenye simu lakini kwa kuwa hisia za kusikia kwangu zilikua kubwa nilisikia akijibiwa
"Ndio mkuu, tushamk**ata na tumemuweka online k**a unavyotuona"
"Safi sana basi jiandaen kwa lolote nitakalowaambia" aliposema hayo hakukata wala hakutua simu yake alinitazama Mimi
"Dominick kabla sijafanya tukio hili naomba unambie kwanza, utajiunga katika kundi langu au msimamo uko pale pale"
"Hivi wewe mkuu gani? Mkuu wa mabumbuwazi au? Nishakwambia Mimi siwezi na wala sintoweza kujiunga na kundi lako mbona waning'ang'ania" nilimjibu kwa jazba nikimkazia macho.
"Nafikiri hunielewi mimi vizuri sasa utanijua Mimi ni nani" vile vitisho niliona kawaida sana.
Alivyosema vile alinigeuzia ile laptop iliyokua mezani nikawa naingalia Mimi
"Unaona kinachoendelea sasa?' Aliniuliza akigusa kioo cha Laptop.
Hapo mwanzo sikuielewa ile video niliyokua naitazama mda ule.
Niliona watu waliovalia vinyago k**a majambazi wakiwa wamemzunguka mama mmoja aliyekaa kwenye kiti kafungwa kamba, huku minjemba ile ya kijambazi ikitunisha vizuri misuri yao.
Lakini nilipokuja kukazia macho vizur "Mungu wangu!!"alikua ni mama imma, Mama Dominick mama yangu mzazi ndio katekwa vile kafungwa k**a MTU anayesubiria kuchinjwa.
Jasho mda ule ule lilinitoka nisiamini kwamba wameweza kujua familia yangu iliko na kumteka mama yangu. Kwakweli moyo ulishtuka ingelikuwa nina ugonjwa wa moyo basi siku hiyo ingelikuwa ndio mwisho wangu wa maisha.
"Haya nambie umekubali ua haujakubali?" Aliniuliza tena kwa mara nyingine macho yangu hayakutoka kwenye kile kioo cha Laptop nikimtazama mama mzazi niliyepotezana nae siku nying
"Umemtoa wapi mama yangu, umewezaje kuijua familia yangu hakika ukimuua mama yangu nitakufanyia kitu kibaya" niliongea kwa hasira nikichanganya na huzuni.
Simu ile aliyokuwa anaongea nayo ikiwa haijakatwa bado nilimsikia akisema
"Kishoka naomba jiandae kumkata kidole kimoja kimoja Huyo mama mpaka nitakapokwambia acha" Ghafla ni k**a alikua ananisikika kwenye ile video nikiyokua naitazama.
Niliona Mmoja wa majambazi katoa kisu kisha akaulza mkono wa mama yangu kwenye meza iliyokua mbele yake akatenga kidole kcha mwisho cha mkono wa kushoto wa mama yangu, akawekea kisu juu yake k**a anataka kukata karoti.
"Subiri kwanza kabla hujafanya hivyo" aliamrisha tena mkuu wa magereza nikaona lile zoezi limesimama.
"Nakuuliza tena kwa Mara ya mwisho la sivyo nitaruhus mama yako akatwe, nahesabu moja mpaka tatu, unakubali ama unakataa?"
Kiukweli sio kwamba nilishindwa kukubali maoema lakini niliona k**a wananitania. Yule mkuu alianza kuhesabu moja, anaganda dakika moja kisha anendelea. Akifika mpaka mbili bado moyo wangu ulikataa kukubali, alipofika tatu mara aliwaruhusu.
nilitazama kwenye ile video niliona kidole cha mama yangu kikikatwa kikaruaka k**a mkia wa mjusi, damu zikatapaaka pale kwenye meza huku Ukelele mkali wa maumivu kutoka kinywani mwa mama yangu ukisikika sana katika ile video.
Kwa yale maumivu niliyopata baada ya kuona video mama yangu akikatwa kidole nilijikuta nguvu za kimbwa mwitu zimenijia ghafla, wale askari walionishika mkono niliwapushi nikawarusha kila mmoja ukutani mwake kwa kishindo kikubwa kisha nikaanza kutembea kueleka kwa yule mkuu kucha za kimbwa mwitu zikiwa zimetokea pamoja na meno.
Hasira nilizokuwa nazo kwenda kumdhuru mkuu na wenzake zilikatishwa baada ya kutazama ile video kuona mama yangu kawekewa kisj kwenye shingo k**a anataka kuchinjwa.
Mkono wangu wa kushkti ukiwa juu ya meza ya mkuu wa magereza kucha zimetobka mbao ya meza, mkono wangu wa kulia nilikua nimeunyanyua ili nimchane lakini yule Mkuu hakuogopa akaniambia.
"Safi sana nilikua najiuliza siku zote wewe ni nani mpaka uwe na nguvu hivi,Sasa endele unachotaka kufanya niruhusu mama yako mzazi auliwe". Hasira zilirudi zilipotoka mda ule waliovalia suti walikua makini namimi kwani nilifanana k**a mnyama walininyooesha bastola huku boss wao akiwa hana wasiwasi kwa kile kitendo
Nguvu ziliniishia mama yangu kaekewa kisu shingoni ili nikubali kujiunga kwenye kundi la kijambazi, wale askari nilio wapushi mpaka mda ule hawakuwa wameamka, huku mkuu wa gereza akianza kuhesabu moja mpaka tatu nisipokubali basi na shingo ya mama yangu itakatwa k**a kile kidole...........ITAENDELEA.