New Life Media

New Life Media Ukurasa maalumu wa habari, matukio na utafiti wa kina kuhusu taarifa mbalimbali za kidunia.

  YAKO, NDOTO YAKO.
01/07/2025

YAKO, NDOTO YAKO.

James Mapunda, Mtia nia nafasi ya Ubunge  Jimbo la Mbinga Vijijini, Akikabidhiwa fomu na katibu wa CCM Wilaya ya Mbinga,...
29/06/2025

James Mapunda, Mtia nia nafasi ya Ubunge Jimbo la Mbinga Vijijini, Akikabidhiwa fomu na katibu wa CCM Wilaya ya Mbinga, Ndugu Ally Simba, Ili Kuomba ridhaa kutoka kwa wanachama wa CCM, kumchagua kuwa mgombea atakaye ipererusha bendera ya CCM katika nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Mbinga Vijijini katika uchaguzi Mkuu 2025.

Makini, Jasiri, Mchapakazi, Msikivu na Mpenda Maendeleo #
na Tunatamba naye #
Tunaweza #

Luis Enrique kocha mwenye misimamo na kuamini falsafa yake hatimaye imemlipa vyema.
12/03/2025

Luis Enrique kocha mwenye misimamo na kuamini falsafa yake hatimaye imemlipa vyema.

Waama ninashauku dabali Mwenyezi Mungu Jalia Mwingi wa mbawazi na buruhani kwa afua na makadara yake ni yeye aliyemkirim...
11/08/2024

Waama ninashauku dabali Mwenyezi Mungu Jalia Mwingi wa mbawazi na buruhani kwa afua na makadara yake ni yeye aliyemkirimu hidaya ya uzima, pumzi na afya tele tele binti yangu kipenzi Judith Komba kutimiza mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwake agosti, 11, 2023 hadi hivi sasa.

Hakika katika ulimwengu huu wa makunjubo na harubu kwa kumjali kutayamamu na kujigagamiza bado anazikimbilia ndoto zake

Nayayuka

ulumbi kila pahala kwa Judy wake #
out kwa k**anda na man himself Jonijoo #
my beautiful and her mom and wife Editha #

MKUU WA WILAYA YA MBINGA ASHIRIKI KIKAO MAALUMU CHA BARAZA LA  MADIWANI WA HALMASHAURI YA MJI WA  MBINGA KUJADILI RASIMU...
04/03/2024

MKUU WA WILAYA YA MBINGA ASHIRIKI KIKAO MAALUMU CHA BARAZA LA MADIWANI WA HALMASHAURI YA MJI WA MBINGA KUJADILI RASIMU YA MPANGO WA BAJETI YA MWAKA WA FEDHA 2024/2025.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga *Mhe. Aziza Ally Mangosongo* amehudhuria kikao maalumu cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga kujadili rasimu ya mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi mdogo wa Halmashauri na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na baadhi ya wananchi.

Aidha, Akitoa salamu za serikali katika baraza hilo Mkuu wa Wilaya Mbinga, Alitumia nafasi hiyo kumshukuru Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa kutoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya halmashauri ambayo inaakisi ukuaji wa sekta mbalimbali ikiwemo afya,elimu,maji,kilimo, miundombinu.

Hata hivyo Mhe.Mangosongo Mkuu wa Wilaya ya Mbinga alisisitiza kwamba ili mikakati na mipango iliyopo iweze kuwa na ufanisi mzuri na itekelezeke ni lazima bajeti hiyo iendane na kasi ya ukusanyaji wa mapato sambamba na kubuni vyanzo vipya vya mapato vyenye tija.

Alikadhalika, Dc Mangosongo alitumia nafasi hiyo kuwataka viongozi kushirikiana katika kuhakikisha wafanyabiashara wanauza sukari kwa bei elekezi na kuthibiti uingizaji holela wa sukari kinyume na sheria pamoja kuwabaini wanaofanya vitendo hivyo ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa kwa kukiuka miongozo.

Akiwasilisha rasimu ya mpango wa bajeti, ndugu Paschal Masatu, Afisa mipango wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Alibainisha kwamba Halmashauri imekadiria kukusanya Tzs bilioni 3.4 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani kwa mwaka wa fedha 2024/25, Ikiwa ni ongezeko la 39.5% kutoka makadirio ya fedha kwa mwaka uliopita wa 2023/2024.

Mwisho nao Meneja wa taasisi za RUWASA, TARURA na MBIUWASA waliwasilisha bajeti zao ili baraza hilo liliridhie zipitishwe kwa ajili ya utekelezaji, Ambapo Meneja wa TARURA Wilaya ya Mbinga Mhandisi Oscar M***a alisema TARURA inatarajia kutumia Tzs bilioni 2.4 kwa mwaka fedha 2024/25 kwa ajili ya kufungua barabara mpya, ujenzi wa madaraja, vivuko, makaravati na matengenezo mengine.

Vilevile, Nae Meneja wa RUWASA Mhandisi Mashaka Sinkala alisema RUWASA inatarajia kutumia tzs Milioni 977 kwa ajili ya miradi mipya na kuboresha miundombinu Pamoja na hilo MBIUWASA nao wanatarajia kutumia zaidi ya Tzs Bilioni 4 kwa ajili ujenzi wa miradi mipya mikubwa ili kuhakikisha mji wa Mbinga unakuwa na huduma ya uhakika ya maji ili kuendana na kasi ya uchukuaji na mahitaji.

Imetolewa na
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga.
March 04, 2024.

MKUU WA WILAYA YA MBINGA AWATAKA WATENDAJI WA KATA KUHAKIKISHA SHULE ZOTE ZINAANZISHA MFUMO WA ELIMU YA KUJITEGEMEA ILI ...
19/12/2023

MKUU WA WILAYA YA MBINGA AWATAKA WATENDAJI WA KATA KUHAKIKISHA SHULE ZOTE ZINAANZISHA MFUMO WA ELIMU YA KUJITEGEMEA ILI KUJENGA UELEWA WA PAMOJA KUHUSU UMUHIMU WA LISHE BORA KUANZIA WAKIWA SHULENI.

Mkuu wa Wilaya ya Mbinga *Mhe. Aziza Ally Mangosongo* alitoa agizo kwa Watendaji kata kuhakikisha na kusimamia uanzishwaji wa mfumo wa elimu ya kujitegemea shuleni ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kupata uelewa kuhusu umuhimu wa lishe bora kuanzia wakiwa shuleni. Agizo hilo lilitolewa wakati wa kikao cha tathmini ya mkataba wa lishe ambacho hufanyika kila baada ya miezi mitatu (3), Ambapo kikao hicho kimefanyika katika ukumbi mdogo uliopo ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kuhudhuriwa na wajumbe wa lishe.

Aidha, Katika kikao hicho Mkuu wa divisheni ya lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga *Ndugu Judith Mushi* alibainisha kwamba kwasasa idara ya lishe inaendelea kutoa elimu kwa wajisiliamali na wafanyabiashara wenye mashine za kusaga kufunga vifaa maalumu vya kuchakata unga ili kuongeza virutubisho, Pamoja na kufanya ufuatiliaji wa kina shule kwa shule ili kuhakikisha wanafunzi wote wanapata chakula shuleni ili kuwaepusha na athari za udumavu na utapiamlo.

Hata hivyo, Mhe.Mangosongo aliwatia shime watendaji kata kufanya kazi kwa bidii kubwa ili kuunga mkono juhudi za *Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan* za kuhakikisha tunakuwa na kizazi cha watanzania ambao hawana athari za udumavu na utapiamlo ili waweze kufanya kazi za kuliletea taifa maendeleo, Sambamba na hilo alimpongeza balozi wa lishe ambaye ni diwani wa kitura *Mhe. Alex Ngui* kwa kazi kubwa anayoifanya ya kupita kila kijiji, mitaa kuhamasisha kuhusu umuhimu wa lishe bora.

Vilevile, Alisisitiza kudhibiti kikamilifu mianya ya upitishaji wa chumvi isiyo na madini joto kutumika shuleni na maeneo mengine, Pia aliwataka watendaji kata kuhakikisha kila shule inaklabu ya lishe iliyohai ambayo muda wote inatekeleza afua za lishe kwa vitendo, Sambamba na kuhamasisha wazazi wote kuchangia chakula shuleni ili kuondoa utoro unaosababishwa na kukosa chakula shuleni.

Mwisho, Mhe. Mangosongo alitumia nafasi kuwataka watendaji kata kwenda kusimamia mpango maalamu wa upandaji wa miti ya matunda kwa wanafunzi wote kuanzia shule za msingi na sekondari, Na kila mwanafunzi awe na mti wake ambao utaandikwa jina lake, Hivyo basi walimu kuhakikisha utunzaji wa miti hiyo ufanyike kwa ufasaha, Isipokuwa madarasa ya mitihani yasihusike na zoezi hili.

*Imetolewa na*
*Ofisi ya Mkuu wa Wilaya*
*Wilaya ya Mbinga*
*Disemba 18, Mwaka 2023*

17/10/2023
MKUU WA WILAYA MBINGA AHITIMISHA KAMPENI YA SIKU TATU (3) YA KUSIKILIZA NA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI KWA WANANCHI WA WIL...
13/10/2023

MKUU WA WILAYA MBINGA AHITIMISHA KAMPENI YA SIKU TATU (3) YA KUSIKILIZA NA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI KWA WANANCHI WA WILAYA YA MBINGA, ASISITIZA ELIMU ITOLEWE ZAIDI ILI KUONDOA KERO NA CHANGAMOTO HIZO.

Mkuu wa Wilaya Mbinga *Mhe. Aziza Ally Mangosongo* alihitimisha kampeni ya siku 3
ya kusikiliza na kutatua migogoro ya ardhi inayowakabili wananchi wanaomiliki ardhi katika maeneo mbalimbali ndani ya Wilaya ya Mbinga, kwa kukosa haki zao za msingi au kudhulumiwa ardhi zao pamoja na kupewa elimu kuhusu matumizi ya ardhi, gharama za hati miliki na kutambua vyombo vinavyotoa maamuzi kuhusu changamoto za ardhi.

Kampeni ya usikilizaji na utatuzi wa migogoro ya ardhi ilidumu kwa kipindi cha siku tatu (3), Lengo ni kutatua papo kwa hapo changamoto hizo na kutoa usuluhishi, Ambapo takribani ya watu zaidi ya 99 wamefikiwa na huduma hiyo sambamba na kupewa elimu kuhusu mambo mbalimbali yahusuyo umiliki wa ardhi, Zoezi hilo lilifanyika katika eneo la bustani za maua zilizopo pembezoni mwa barabara ya mbinga- mbamba-bay katikati ya Mji wa Mbinga.

Aidha, Akihitimisha kampeni hiyo Mkuu wa Wilaya, Mhe. Mangosongo alisema kwamba "Niwahakikishie tu sisi k**a serikali tupo kwa ajili ya kuwahudumieni wananchi, atupaswi kuwaona mkiteseka na changamoto zenu. K**a mjuavyo ardhi ni mtaji, ukiwa na ardhi ndio kila kitu, Hivyo basi kitendo cha ardhi kuwa chache na watu kuongezeka, migogoro mingi imeibuka, kwahiyo basi kampeni hii ni endelevu itakuwa ikifanyika mara kwa mara"

Sambamba na hilo maafisa ardhi kuendelea kutenda haki na kuhakikisha hati miliki za wananchi zinatolewa kwa wakati ili kuondoa usumbufu,Vilevile aliwataka wananchi kuacha tabia ya kujenga kwenye mabonde na miinuko

Mwisho, Aliwataka wananchi kufuata maelezo na miongozo inayotolewa na maafisa ardhi ili kuepuka migogoro baada ya kuuziana ardhi pamoja kufuata taratibu za umilikishwaji na upimaji, Alikadhalika aliwataka maafisa ardhi kujikita zaidi katika usuluhishi badala ya kuwa chanzo cha migogoro mingi ya ardhi.

Hata hivyo kampeni hiyo kwa siku zote tatu iliendeshwa na maafisa ardhi kutoka katika Halmashauri ya Wilaya na Mji Mbinga wakitoa elimu kuhusu mada mbalimbali ikiwemo za namna ya kupata hati miliki, Nyaraka muhimu zinazoitaji, sambamba na kutoa miongozo namna bora ya kumilikishwa ardhi.

*Imetolewa na*
*Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mbinga*
*Leo Oktoba 12 Mwaka 2023*

Address

Globally
Mbinga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when New Life Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share