Habari zetu Media

Habari zetu Media Habari za kitaifa,kimataifa,burudani na michezo hapa ndo mahala pale

kuwa wa kwanza kupata habari ziki kwa kutufuata katika mitandao yetu

Pita hapa kusoma magazeti leo July 29,2025
29/07/2025

Pita hapa kusoma magazeti leo July 29,2025


HABARI:Mahak**a ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Lindi, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Alli Ibrahimu Malinda (30), mkazi ...
23/07/2025

HABARI:

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Lindi, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Alli Ibrahimu Malinda (30), mkazi wa Kijiji cha Ng’apa, baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10.

Hukumu hiyo imetolewa leo Julai 23, 2025 na Hakimu Mkazi wa mahak**a ya hakimu mkazi mkoa wa Lindi Delphina Kimathi, baada ya ushahidi wa upande wa mashtaka kuthibitisha kosa hilo pasipo shaka yoyote.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, tukio hilo lilitokea Januari 6, 2025, usiku katika kijiji cha Ng’apa, wakati mtoto huyo akiwa usingizini. Malinda alitumia nafasi yake k**a mzazi na kutenda kitendo hicho cha unyama ndani ya nyumba yao ya familia.

Tembembela mitandao yetu kwa taarifa zaidi.



HABARI:Mkazi wa kijiji cha Madangwa, wilayani Lindi, Omari Said Bakari (35), amekutwa amefariki dunia kwa kujinyonga na ...
23/07/2025

HABARI:

Mkazi wa kijiji cha Madangwa, wilayani Lindi, Omari Said Bakari (35), amekutwa amefariki dunia kwa kujinyonga na mkanda wa suruali yake, baada ya kuufunga kwenye tawi la mti wa mkorosho kisha kujining’iniza.

Taarifa kutoka jeshi la polisi mkoa wa Lindi inasema tukio hilo limetokea Julai 22, 2025 majira ya saa tatu asubuhi na uchunguzi wa awali umeonesha kuwa marehemu alikuwa akipitia hali ya msongo wa mawazo kwa muda mrefu.

Ndugu wa karibu pamoja na majirani waliokuwa wakiishi naye wameeleza kuwa hali hiyo huenda ndiyo iliyomsukuma kuchukua uamuzi huo mgumu.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa hakuna dalili za tukio hilo kuhusishwa na vitendo vya uhalifu, na kwamba uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini kwa undani sababu za kisaikolojia au kijamii zilizochangia hatua hiyo.

Endelea kutembelea ukurasa wetu kwa taarifa zaidi.



HABARI: Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi linamshikilia mwanaume mmoja aitwaye Araba Samali Chichonyo (57), Kata ya Chinongw...
23/07/2025

HABARI:

Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi linamshikilia mwanaume mmoja aitwaye Araba Samali Chichonyo (57), Kata ya Chinongwe, Wilaya ya Ruangwa kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 78, ambaye pia ni mkazi wa kata hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi tukio hilo limetokea usiku wa Julai 20, 2025, majira ya saa nne, nyumbani kwa muhanga, wakati walipokuwa wakinywa pombe ya kienyeji aina ya wanzuki.

Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa mtuhumiwa alikuwa ameajiriwa na muhanga huyo kuchimba shimo la choo kwa makubaliano ya ujira wa shilingi elfu kumi. Awali, muhanga alimlipa mtuhumiwa shilingi elfu saba, na siku ya tukio alikabidhiwa shilingi elfu mbili kati ya elfu tatu zilizokuwa zimebaki. Baada ya kulipwa kiasi hicho, mtuhumiwa alielekea kununua pombe hiyo ya kienyeji na kuirejea nyumbani kwa muhanga, ambapo waliendelea kunywa pamoja na mume wa muhanga ambaye ni mlemavu wa macho.

Ilielezwa kuwa wakati wakiendelea na unywaji wa pombe, na mume wa muhanga akiwa amelewa na kupoteza fahamu, mtuhumiwa alitumia mwanya huo kumvamia muhanga. Alimshika kwa nguvu, kisha kumvua nguo ya ndani na kutekeleza kitendo hicho cha ukatili wa kingono ukumbini hapo walipokuwa wamekaa. Baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alitoroka kusikojulikana.

Endelea kutembelea ukurasa wetu kwa taarifa zaidi.



Address

Mbinga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari zetu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share