Habari zetu Media

Habari zetu Media Habari za kitaifa,kimataifa,burudani na michezo hapa ndo mahala pale

kuwa wa kwanza kupata habari ziki kwa kutufuata katika mitandao yetu

HABARI:Mahak**a Kuu Kanda ya Mtwara imewahukumu kunyongwa hadi kufa askari wawili Gribet Kalanje (aliyekuwa OC-CID) na C...
23/06/2025

HABARI:

Mahak**a Kuu Kanda ya Mtwara imewahukumu kunyongwa hadi kufa askari wawili Gribet Kalanje (aliyekuwa OC-CID) na Charles Onyango (aliyekuwa Mkuu wa Kituo) kwa kosa la mauaji ya mfanyabiashara wa madini, M***a Hamisi Hamisi.

Kwa mujibu wa ushahidi uliowasilishwa mahak**ani, marehemu aliuawa kinyama kwa matumizi mabaya ya madaraka na nguvu kupita kiasi kutoka kwa askari hao waliokuwa na dhamana ya kulinda raia.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Hamidu Mwanga aliwaachia huru askari wengine watano baada ya kukosekana kwa ushahidi wa kutosha

Mfanyabiashara M***a Hamisi aliuawa mwaka 2022 na kisha pesa zake alizokuwa nazo kuchukuliwa na askari hao

Endelea kutembelea ukurasa wetu kwa taarifa zaidi



HABARI: Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Omari Said Jimajima (28), Mkazi wa Kijiji cha Mbangala, Wilaya ya Ruangwa, M...
16/06/2025

HABARI:

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Omari Said Jimajima (28), Mkazi wa Kijiji cha Mbangala, Wilaya ya Ruangwa, Mkoa wa Lindi amefariki Dunia Juni 14, 2025 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa baada ya kunywa sumu ya kuulia wadudu shambani

Taarifa kutoka Jeshi la polisi mkoa wa Lindi zinasema tukio hilo limetokea Juni 13, 2025 majira ya saa 6:00 mchana, akiwa katika shamba lake la zao la ufuta lililopo Kijiji cha Nachiungo.

Aidha inadaiwa marehemu kabla ya kufikia uamuzi huo alikuwa na mgogoro wa kifamilia na mchumba wake aliyekuwa akiishi naye kwa mwezi mmoja, aitwaye Fatuma, mkazi wa Kiwawa, Wilaya ya Lindi Vijijini, ambaye aliripotiwa kutoroka nyumbani Juni 9, 2025 majira ya saa mbili usiku.

Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi wa kitabibu inaeleza kuwa chanzo cha kifo kilitokana na ini kushindwa kufanya kazi baada ya kuathirika na sumu hiyo. Mwili wa marehemu tayari umekabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Tembelea mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa Zaidi


HABARI: Jeshi la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Damiani Francis (38), mkazi wa Kijiji cha Chimbila B, wilayani Ruangw...
16/06/2025

HABARI:

Jeshi la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Damiani Francis (38), mkazi wa Kijiji cha Chimbila B, wilayani Ruangwa, kwa tuhuma za kumlawit kijana wa miaka 13.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Juni 15, 2025 majira ya saa saba mchana baada ya kumvizia kijana huyo akiwa amelala ndani ya nyumba yao kisha kumbeba na kumpeleka nyuma ya nyumba hiyo na kuanza kumfanyia kitendo hicho.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi zimeleza kuwa mtuhumiwa alimbeba kijana huyo akiwa usingizini na kumpeleka nyuma ya nyumba hiyo, ambako alimvua nguo na kisha kumlawiti kwa nguvu. Kitendo hicho cha kikatili kimeripotiwa kuibua taharuki kubwa katika jamii ya Chimbila B, huku wakazi wakitoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua kali dhidi ya wahalifu wa makosa ya kingono, hususan dhidi ya watoto.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa mtuhumiwa alitenda tukio hilo kwa makusudi na bila huruma, huku akiwa anafahamu fika madhara ya kitendo chake. Kijana huyo alipelekwa katika kituo cha afya kwa uchunguzi wa kitabibu, na hatua za kisheria dhidi ya mtuhumiwa zinaendelea kuchukuliwa.

Tembelea mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa Zaidi


UPDATE BAJETI YA SERIKALI 2025/2026: Serikali kupitia Bajeti ya mwaka 2025/2026, iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha Dkt....
13/06/2025

UPDATE BAJETI YA SERIKALI 2025/2026:

Serikali kupitia Bajeti ya mwaka 2025/2026, iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, imetangaza mafanikio makubwa katika kuboresha huduma za afya nchini.

Kwa mujibu wa bajeti hiyo, vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoka 8,458 mwaka 2020 hadi kufikia 9,826 mwaka 2024. Aidha, hospitali zenye majengo ya huduma za dharura zimeongezeka kutoka saba (7) hadi hospitali 116 katika kipindi hicho.

Serikali pia imeongeza idadi ya magari ya kubeba wagonjwa kutoka 540 mwaka 2020 hadi magari 1,267 mwaka 2024, hatua inayolenga kuimarisha huduma za uokoaji na usafirishaji wa wagonjwa kwa haraka.

Uwekezaji huu mkubwa unalenga kuboresha ustawi wa wananchi na kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana hadi vijijini.

Kwa taarifa zaidi, tembelea mitandao yetu ya kijamii.



"Tunachokitaka CHAUMMA ni wanafunzi wanaokwenda shule, wagonjwa waliolazwa hospitalini pamoja na makundi maalumu wapate ...
15/05/2025

"Tunachokitaka CHAUMMA ni wanafunzi wanaokwenda shule, wagonjwa waliolazwa hospitalini pamoja na makundi maalumu wapate chakula, ila si kwa watu wote. K**a unataka kuja kudoea basi fanya ujanja wako ukadoee".
Hashim Rungwe Mwenyekiti CHAUMMA

Mwanamuziki Harmonize amekanusha kauli ya aliyekuwa msanii wake Ibraah ya kumdai kiasi cha Sh1 bilioni ili aweze kutoka ...
15/05/2025

Mwanamuziki Harmonize amekanusha kauli ya aliyekuwa msanii wake Ibraah ya kumdai kiasi cha Sh1 bilioni ili aweze kutoka katika lebo ya ‘Konde Gang’.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Harmonize ametoa maelezo kuhusu sakata hilo huku akiweka wazi hajui kuhusiana na andiko la Ibraah katika mitandao ya kijamii la kumdai Sh1 bilioni.

Akizungumza kuhusiana na ishu ya Basata kutoitikia wito huo ameeleza kuwa aliliwasilisha kwa menejimenti yake ili imwakilishe.

Aidha ameongezea kwa kueleza: “Nimemruhusu aende akafanye muziki wake and make sure (nitahakikisha) mnamsapoti pia."

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa tahadhari juu ya kuzorota kwa hali ya kifedha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia...
14/05/2025

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa tahadhari juu ya kuzorota kwa hali ya kifedha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia kuongezeka kwa mapigano mashariki mwa nchi hiyo.

Kulingana na taarifa ya IMF baada ya ziara ya tathmini mjini Kinshasa, kuimarika kwa mashambulizi ya waasi wa M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda, kumesababisha kupungua kwa mapato ya serikali. Miji mikuu ya mashariki — Goma na Bukavu — iko chini ya udhibiti wa waasi hao, jambo lililosababisha kufungwa kwa ofisi nyingi za ukusanyaji mapato.

Mbali na hilo, serikali ya Congo iliondoa ushuru na VAT kwa bidhaa za chakula ili kupunguza gharama kwa wananchi, hatua ambayo imepunguza zaidi mapato ya ndani.

"Hali ya kiusalama imeongeza mzigo kwa bajeti ya taifa, huku matumizi ya kijeshi na mishahara ya askari wa usalama ikiongezwa ili kuimarisha morali," ilisema taarifa ya IMF.

IMF imeeleza kuwa imefikia makubaliano ya awali ya mapitio ya kwanza ya mpango wa msaada wa kifedha wa ECF, na serikali ya Congo imethibitisha kujitolea kuendeleza utekelezaji wa malengo ya kiuchumi kwa kuzingatia mazingira mapya ya vita.

Mpango huo unalenga kulinda uthabiti wa bajeti ya taifa huku ukitoa nafasi kwa matumizi ya haraka kwenye masuala ya kiusalama na misaada ya kibinadamu.

Umoja wa Mataifa na mataifa ya Magharibi yameendelea kushutumu Rwanda kwa madai ya kusaidia waasi wa M23 kwa silaha na wanajeshi. Rwanda imekanusha vikali madai hayo, ikisema inajihami dhidi ya mashambulizi kutoka jeshi la Congo na wanamgambo waliohusika katika mauaji ya kimbari ya 1994

HABARI: Kundi la Waafrikana (raia weupe wa Afrika Kusini) 59 limewasili nchini Marekani ambapo watapewa hadhi ya ukimbiz...
13/05/2025

HABARI: Kundi la Waafrikana (raia weupe wa Afrika Kusini) 59 limewasili nchini Marekani ambapo watapewa hadhi ya ukimbizi baada ya kudai kukumbwa na ubaguzi wa rangi nchini mwao.

Serikali ya Afrika Kusini imesema kundi hilo halipitii mateso yoyote ambayo yangestahili hadhi ya ukimbizi

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema yuko tayari kukutana na Rais Vladimir Putin wa Urusi nchini Uturuki Alhamisi ...
12/05/2025

Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine amesema yuko tayari kukutana na Rais Vladimir Putin wa Urusi nchini Uturuki Alhamisi wiki hii, kwa mazungumzo ya moja kwa moja ya kumaliza vita kati ya nchi hizo mbili.

Zelensky ameandika katika mtandao wa kijamii wa X kuwa wanasubiri usitishaji kamili na wa kudumu wa mapigano kuanzia leo, ili kutoa msingi unaohitajika kwa diplomasia.

Ameongeza kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo na mwenzake wa Urusi kwani hakuna maana yoyote ya kuendeleza mauaji ndani ya nchi zao.

Hata hivyo mpaka sasa hakuna majibu yoyote yaliyotolewa na Ikulu ya Urusi kuhusu utayari wa Rais Putin kukutana na Zelensky kwa mazungumzo.

Wiki iliyopita Rais Zelensky na baadhi ya viongozi wa Ulaya waliweka msimamo kwamba hakutafanyika mazungumzo yoyote kati ya pande hizo mbili hadi Rais Putin atakapokubali kusitisha mapigano kwa siku 30 bila masharti yoyote kuanzia leo Mei 12, 2025, jambo ambalo Urusi inadaiwa kulikataa.

Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kahama kimesema, Watia nia 9 wa nafasi za Ubunge na Udiwani Wilayani humo, wamebaini...
11/05/2025

Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kahama kimesema, Watia nia 9 wa nafasi za Ubunge na Udiwani Wilayani humo, wamebainika kujihusisha na vitendo vya kugawa Fedha kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM nyakati za usiku, kinyume na Maadili ya Chama

Katibu wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Chatwanga, amesema Wagombea hao wanatoka kwenye Majimbo yote matatu ya Wilaya hiyo: Kahama Mjini (5), Ushetu (2) na Msalala (2)

Ameeleza “Tumebaini baadhi ya watia nia wanazunguka usiku kwenye Kata mbalimbali kuwapa Wajumbe Fedha, wengine hadi Tsh. 10,000 ili wawapitishe kwenye mchakato wa ndani. Hii ni aibu, ni udhalilishaji na ni kinyume cha Maadili ya CCM. Chama hakiwezi kumvumilia Mgombea wa aina hiyo."

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amezindua Kituo Mama cha Gesi Asilia iliyoshindiliwa (CNG) ambacho kina uwezo wa...
09/05/2025

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amezindua Kituo Mama cha Gesi Asilia iliyoshindiliwa (CNG) ambacho kina uwezo wa kujaza Gesi Asilia magari 1200 kwa siku huku kikifanya kazi saa 24.

Kapinga amezindua kituo hicho leo Mei 9, 2025 jijini Dar es Salaam ambapo uzinduzi huo ulienda sambamba na uzinduzi wa basi la mfano la Kampuni ya Mabasi Yaendayo Haraka (UDART) ambalo linatumia nishati hiyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kapinga amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maono, mtazamo na maelekezo yake kwa Wizara ya Nishati ambayo yanaleta matokeo chanya kielelezo mojawapo kikiwa ni uzinduzi kwa kituo hicho cha CNG.

Ameeleza kuwa, kituo hicho kitakuwa na uwezo wa kujaza gesi kwenye magari nane kwa wakati mmoja, kuchochea ongezeko la vituo vingine vya CNG na kuwapatia huduma ya gesi watumiaji wengine k**a viwanda, shule na hoteli.

Awali Mkurugenzi wa Idara ya Biashara ya Mafuta kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Mhandisi Emmanuel Gilbert alisema kuwa kituo hicho kina uwezo wa kuzalisha CNG kiasi cha futi za ujazo milioni 4.2 sawa na kilo 120 kwa siku, kina pampu nne zenye jumla ya nozeli nane na hivyo kukifanya kituo kuwa na uwezo wa kuhudumia magari nane kwa wakati mmoja ambapo kwa siku kitatoa huduma kwa magari takriban 1200.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wazazi nchini kuzin...
09/05/2025

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amewataka wazazi nchini kuzingatia malezi na makuzi bora ya watoto tangu kipindi cha mimba hadi mtoto anapofikisha umri wa miaka 18.

Dkt. Gwajima amesema hayo Mei 08, 2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Familia itakayofanyika Mei 15, 2025.

Waziri Dkt. Gwajima amesema majukumu ya familia ni mengi lakini kubwa ni kutoa huduma ili kukidhi mahitaji ya watoto na familia sambamba na kusimamia malezi na makuzi mema ya watoto. Aidha, amesema familia ina jukumu la kurithisha mila na tamaduni nzuri kwa watoto na familia kwa ujumla kizazi hadi kizazi.

Ameongeza kwamba Taifa lolote lenye maendeleo endelevu ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hutokana na namna ambavyo watoto wamelelewa na kukuzwa kwa kuzingatia misingi ya malezi chanya inayoendana na maadili, mila na desturi njema za kitanzania.

Waziri Dkt. Gwajima amewahimiza Wazazi na Walezi kutimiza wajibu wao wa malezi na matunzo ya watoto ili kumkuza mtoto kuwa na tija kwa familia na taifa kwa ujumla ili kufanikisha hilo amewaomba wazazi kutenga muda wa kuzungumza na watoto wao mara kwa mara ili kuimarisha muunganiko (bond) baina ya mzazi na mtoto hasa kwa kuwekeza nguvu nyingi zaidi za malezi kwenye umri wa chini ya miaka 8 kipindi ambapo, ubongo unakua kwa asilimia 90.

Pia amewataka wazazi na walezi kujua maendeleo ya mtoto na changamoto zinazomkabili kwa wakati na kuzipatia ufumbuzi kabla hazijaleta madhara makubwa.

Akieleza jitihada za Serikali kupitia Wizara anayoisimamia kuwa inaendelea kuimarisha mifumo ya kisheria kwa kufanya marekebisho ya Sheria Tatu ambazo ni Sheria ya Mtoto, Sura ya 13, Sheria ya Makosa ya Kimtandao, Sura ya 443, na Sheria ya Msaada wa Kisheria, Sura ya 21 huku marekebisho hayo yakilenga kuondoa upungufu unaojitokeza katika utekelezaji wa masharti katika sheria husika ili kuimarisha ulinzi na maslahi bora ya mtoto.

Address

Mbinga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari zetu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share