Habari zetu Media

Habari zetu Media Habari za kitaifa,kimataifa,burudani na michezo hapa ndo mahala pale

kuwa wa kwanza kupata habari ziki kwa kutufuata katika mitandao yetu

Pita hapa kusoma magazeti leo July 29,2025
29/07/2025

Pita hapa kusoma magazeti leo July 29,2025


HABARI:Mahak**a ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Lindi, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Alli Ibrahimu Malinda (30), mkazi ...
23/07/2025

HABARI:

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Lindi, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela Alli Ibrahimu Malinda (30), mkazi wa Kijiji cha Ng’apa, baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 10.

Hukumu hiyo imetolewa leo Julai 23, 2025 na Hakimu Mkazi wa mahak**a ya hakimu mkazi mkoa wa Lindi Delphina Kimathi, baada ya ushahidi wa upande wa mashtaka kuthibitisha kosa hilo pasipo shaka yoyote.

Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, tukio hilo lilitokea Januari 6, 2025, usiku katika kijiji cha Ng’apa, wakati mtoto huyo akiwa usingizini. Malinda alitumia nafasi yake k**a mzazi na kutenda kitendo hicho cha unyama ndani ya nyumba yao ya familia.

Tembembela mitandao yetu kwa taarifa zaidi.



HABARI:Mkazi wa kijiji cha Madangwa, wilayani Lindi, Omari Said Bakari (35), amekutwa amefariki dunia kwa kujinyonga na ...
23/07/2025

HABARI:

Mkazi wa kijiji cha Madangwa, wilayani Lindi, Omari Said Bakari (35), amekutwa amefariki dunia kwa kujinyonga na mkanda wa suruali yake, baada ya kuufunga kwenye tawi la mti wa mkorosho kisha kujining’iniza.

Taarifa kutoka jeshi la polisi mkoa wa Lindi inasema tukio hilo limetokea Julai 22, 2025 majira ya saa tatu asubuhi na uchunguzi wa awali umeonesha kuwa marehemu alikuwa akipitia hali ya msongo wa mawazo kwa muda mrefu.

Ndugu wa karibu pamoja na majirani waliokuwa wakiishi naye wameeleza kuwa hali hiyo huenda ndiyo iliyomsukuma kuchukua uamuzi huo mgumu.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa hakuna dalili za tukio hilo kuhusishwa na vitendo vya uhalifu, na kwamba uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini kwa undani sababu za kisaikolojia au kijamii zilizochangia hatua hiyo.

Endelea kutembelea ukurasa wetu kwa taarifa zaidi.



HABARI: Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi linamshikilia mwanaume mmoja aitwaye Araba Samali Chichonyo (57), Kata ya Chinongw...
23/07/2025

HABARI:

Jeshi la Polisi mkoa wa Lindi linamshikilia mwanaume mmoja aitwaye Araba Samali Chichonyo (57), Kata ya Chinongwe, Wilaya ya Ruangwa kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 78, ambaye pia ni mkazi wa kata hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi tukio hilo limetokea usiku wa Julai 20, 2025, majira ya saa nne, nyumbani kwa muhanga, wakati walipokuwa wakinywa pombe ya kienyeji aina ya wanzuki.

Aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa mtuhumiwa alikuwa ameajiriwa na muhanga huyo kuchimba shimo la choo kwa makubaliano ya ujira wa shilingi elfu kumi. Awali, muhanga alimlipa mtuhumiwa shilingi elfu saba, na siku ya tukio alikabidhiwa shilingi elfu mbili kati ya elfu tatu zilizokuwa zimebaki. Baada ya kulipwa kiasi hicho, mtuhumiwa alielekea kununua pombe hiyo ya kienyeji na kuirejea nyumbani kwa muhanga, ambapo waliendelea kunywa pamoja na mume wa muhanga ambaye ni mlemavu wa macho.

Ilielezwa kuwa wakati wakiendelea na unywaji wa pombe, na mume wa muhanga akiwa amelewa na kupoteza fahamu, mtuhumiwa alitumia mwanya huo kumvamia muhanga. Alimshika kwa nguvu, kisha kumvua nguo ya ndani na kutekeleza kitendo hicho cha ukatili wa kingono ukumbini hapo walipokuwa wamekaa. Baada ya tukio hilo, mtuhumiwa alitoroka kusikojulikana.

Endelea kutembelea ukurasa wetu kwa taarifa zaidi.



HABARI:Mahak**a Kuu Kanda ya Mtwara imewahukumu kunyongwa hadi kufa askari wawili Gribet Kalanje (aliyekuwa OC-CID) na C...
23/06/2025

HABARI:

Mahak**a Kuu Kanda ya Mtwara imewahukumu kunyongwa hadi kufa askari wawili Gribet Kalanje (aliyekuwa OC-CID) na Charles Onyango (aliyekuwa Mkuu wa Kituo) kwa kosa la mauaji ya mfanyabiashara wa madini, M***a Hamisi Hamisi.

Kwa mujibu wa ushahidi uliowasilishwa mahak**ani, marehemu aliuawa kinyama kwa matumizi mabaya ya madaraka na nguvu kupita kiasi kutoka kwa askari hao waliokuwa na dhamana ya kulinda raia.

Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Hamidu Mwanga aliwaachia huru askari wengine watano baada ya kukosekana kwa ushahidi wa kutosha

Mfanyabiashara M***a Hamisi aliuawa mwaka 2022 na kisha pesa zake alizokuwa nazo kuchukuliwa na askari hao

Endelea kutembelea ukurasa wetu kwa taarifa zaidi



HABARI: Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Omari Said Jimajima (28), Mkazi wa Kijiji cha Mbangala, Wilaya ya Ruangwa, M...
16/06/2025

HABARI:

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Omari Said Jimajima (28), Mkazi wa Kijiji cha Mbangala, Wilaya ya Ruangwa, Mkoa wa Lindi amefariki Dunia Juni 14, 2025 akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Ruangwa baada ya kunywa sumu ya kuulia wadudu shambani

Taarifa kutoka Jeshi la polisi mkoa wa Lindi zinasema tukio hilo limetokea Juni 13, 2025 majira ya saa 6:00 mchana, akiwa katika shamba lake la zao la ufuta lililopo Kijiji cha Nachiungo.

Aidha inadaiwa marehemu kabla ya kufikia uamuzi huo alikuwa na mgogoro wa kifamilia na mchumba wake aliyekuwa akiishi naye kwa mwezi mmoja, aitwaye Fatuma, mkazi wa Kiwawa, Wilaya ya Lindi Vijijini, ambaye aliripotiwa kutoroka nyumbani Juni 9, 2025 majira ya saa mbili usiku.

Kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi wa kitabibu inaeleza kuwa chanzo cha kifo kilitokana na ini kushindwa kufanya kazi baada ya kuathirika na sumu hiyo. Mwili wa marehemu tayari umekabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya taratibu za mazishi.

Tembelea mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa Zaidi


HABARI: Jeshi la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Damiani Francis (38), mkazi wa Kijiji cha Chimbila B, wilayani Ruangw...
16/06/2025

HABARI:

Jeshi la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Damiani Francis (38), mkazi wa Kijiji cha Chimbila B, wilayani Ruangwa, kwa tuhuma za kumlawit kijana wa miaka 13.

Mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Juni 15, 2025 majira ya saa saba mchana baada ya kumvizia kijana huyo akiwa amelala ndani ya nyumba yao kisha kumbeba na kumpeleka nyuma ya nyumba hiyo na kuanza kumfanyia kitendo hicho.

Kwa mujibu wa taarifa za Polisi zimeleza kuwa mtuhumiwa alimbeba kijana huyo akiwa usingizini na kumpeleka nyuma ya nyumba hiyo, ambako alimvua nguo na kisha kumlawiti kwa nguvu. Kitendo hicho cha kikatili kimeripotiwa kuibua taharuki kubwa katika jamii ya Chimbila B, huku wakazi wakitoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua kali dhidi ya wahalifu wa makosa ya kingono, hususan dhidi ya watoto.

Jeshi la Polisi limeeleza kuwa uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa mtuhumiwa alitenda tukio hilo kwa makusudi na bila huruma, huku akiwa anafahamu fika madhara ya kitendo chake. Kijana huyo alipelekwa katika kituo cha afya kwa uchunguzi wa kitabibu, na hatua za kisheria dhidi ya mtuhumiwa zinaendelea kuchukuliwa.

Tembelea mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa Zaidi


UPDATE BAJETI YA SERIKALI 2025/2026: Serikali kupitia Bajeti ya mwaka 2025/2026, iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha Dkt....
13/06/2025

UPDATE BAJETI YA SERIKALI 2025/2026:

Serikali kupitia Bajeti ya mwaka 2025/2026, iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Nchemba, imetangaza mafanikio makubwa katika kuboresha huduma za afya nchini.

Kwa mujibu wa bajeti hiyo, vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoka 8,458 mwaka 2020 hadi kufikia 9,826 mwaka 2024. Aidha, hospitali zenye majengo ya huduma za dharura zimeongezeka kutoka saba (7) hadi hospitali 116 katika kipindi hicho.

Serikali pia imeongeza idadi ya magari ya kubeba wagonjwa kutoka 540 mwaka 2020 hadi magari 1,267 mwaka 2024, hatua inayolenga kuimarisha huduma za uokoaji na usafirishaji wa wagonjwa kwa haraka.

Uwekezaji huu mkubwa unalenga kuboresha ustawi wa wananchi na kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana hadi vijijini.

Kwa taarifa zaidi, tembelea mitandao yetu ya kijamii.



"Tunachokitaka CHAUMMA ni wanafunzi wanaokwenda shule, wagonjwa waliolazwa hospitalini pamoja na makundi maalumu wapate ...
15/05/2025

"Tunachokitaka CHAUMMA ni wanafunzi wanaokwenda shule, wagonjwa waliolazwa hospitalini pamoja na makundi maalumu wapate chakula, ila si kwa watu wote. K**a unataka kuja kudoea basi fanya ujanja wako ukadoee".
Hashim Rungwe Mwenyekiti CHAUMMA

Mwanamuziki Harmonize amekanusha kauli ya aliyekuwa msanii wake Ibraah ya kumdai kiasi cha Sh1 bilioni ili aweze kutoka ...
15/05/2025

Mwanamuziki Harmonize amekanusha kauli ya aliyekuwa msanii wake Ibraah ya kumdai kiasi cha Sh1 bilioni ili aweze kutoka katika lebo ya ‘Konde Gang’.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Harmonize ametoa maelezo kuhusu sakata hilo huku akiweka wazi hajui kuhusiana na andiko la Ibraah katika mitandao ya kijamii la kumdai Sh1 bilioni.

Akizungumza kuhusiana na ishu ya Basata kutoitikia wito huo ameeleza kuwa aliliwasilisha kwa menejimenti yake ili imwakilishe.

Aidha ameongezea kwa kueleza: “Nimemruhusu aende akafanye muziki wake and make sure (nitahakikisha) mnamsapoti pia."

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa tahadhari juu ya kuzorota kwa hali ya kifedha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia...
14/05/2025

Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetoa tahadhari juu ya kuzorota kwa hali ya kifedha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kufuatia kuongezeka kwa mapigano mashariki mwa nchi hiyo.

Kulingana na taarifa ya IMF baada ya ziara ya tathmini mjini Kinshasa, kuimarika kwa mashambulizi ya waasi wa M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda, kumesababisha kupungua kwa mapato ya serikali. Miji mikuu ya mashariki — Goma na Bukavu — iko chini ya udhibiti wa waasi hao, jambo lililosababisha kufungwa kwa ofisi nyingi za ukusanyaji mapato.

Mbali na hilo, serikali ya Congo iliondoa ushuru na VAT kwa bidhaa za chakula ili kupunguza gharama kwa wananchi, hatua ambayo imepunguza zaidi mapato ya ndani.

"Hali ya kiusalama imeongeza mzigo kwa bajeti ya taifa, huku matumizi ya kijeshi na mishahara ya askari wa usalama ikiongezwa ili kuimarisha morali," ilisema taarifa ya IMF.

IMF imeeleza kuwa imefikia makubaliano ya awali ya mapitio ya kwanza ya mpango wa msaada wa kifedha wa ECF, na serikali ya Congo imethibitisha kujitolea kuendeleza utekelezaji wa malengo ya kiuchumi kwa kuzingatia mazingira mapya ya vita.

Mpango huo unalenga kulinda uthabiti wa bajeti ya taifa huku ukitoa nafasi kwa matumizi ya haraka kwenye masuala ya kiusalama na misaada ya kibinadamu.

Umoja wa Mataifa na mataifa ya Magharibi yameendelea kushutumu Rwanda kwa madai ya kusaidia waasi wa M23 kwa silaha na wanajeshi. Rwanda imekanusha vikali madai hayo, ikisema inajihami dhidi ya mashambulizi kutoka jeshi la Congo na wanamgambo waliohusika katika mauaji ya kimbari ya 1994

HABARI: Kundi la Waafrikana (raia weupe wa Afrika Kusini) 59 limewasili nchini Marekani ambapo watapewa hadhi ya ukimbiz...
13/05/2025

HABARI: Kundi la Waafrikana (raia weupe wa Afrika Kusini) 59 limewasili nchini Marekani ambapo watapewa hadhi ya ukimbizi baada ya kudai kukumbwa na ubaguzi wa rangi nchini mwao.

Serikali ya Afrika Kusini imesema kundi hilo halipitii mateso yoyote ambayo yangestahili hadhi ya ukimbizi

Follow Us
Istagram
Facebook
Twitter
Youtube

Address

Mbinga

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Habari zetu Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share