ALPHER TV

ALPHER TV ALPHER PODCAST MEDIA
C.E.O AND OWNER
PLATNUMZ
you can follow in social network
Instagram
YouTube

24/11/2025

Ocherio..... ゚viralシfypシ゚

Nani mwingine uvumilivu umemshinda k**a huyu jamaa 😅😅😅🤣🤣Huyo njo mondi tunaye mujuwa sisi
11/11/2025

Nani mwingine uvumilivu umemshinda k**a huyu jamaa 😅😅😅🤣🤣
Huyo njo mondi tunaye mujuwa sisi

Kiungo wa Klabu ya Simba SC, Kibu Denis, amepata pigo kubwa baada ya kufiwa na baba yake mzazi, Mzee Denis Prosper, aliy...
11/11/2025

Kiungo wa Klabu ya Simba SC, Kibu Denis, amepata pigo kubwa baada ya kufiwa na baba yake mzazi, Mzee Denis Prosper, aliyefariki dunia usiku huu mkoani Kigoma.

Taarifa hizo zimethibitishwa rasmi na Klabu ya Simba SC, ambayo imetoa salamu za rambirambi kwa Kibu pamoja na familia nzima ya marehemu, ikiwapa pole kwa msiba huu mzito na kuahidi kuwa nao katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo.

Kupitia taarifa hiyo, uongozi wa Simba SC umeomba Wanasimba wote pamoja na wapenda michezo kwa ujumla kuungana kwa sala na maombi kwa ajili ya Kibu na familia yake, ili wapate faraja na nguvu za kuvuka kipindi hiki cha majonzi.

🕯️ Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu Mzee Denis Prosper mahali pema peponi. Amina.


Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum tangu picha mjongeo...
22/10/2025

Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum tangu picha mjongeo wa tukio linaloonyesha mwanamke mmoja akimpiga mwenzake ilipoanza kusambaa ufuatiliaji umefanyika na aliyefanya kitendo hicho amefahamika majina yake, eneo analofanyia kazi na namba zake za simu.

Hatua stahiki zitachukuliwa kulingana na kinachonekana kufanyika kupitia picha mjengeo hiyo sambamba na ushahidi unaoendelea kukusanywa kutoka kwa watu mbalimbali walioshuhudia akiwepo aliyefanyiwa kitendo hicho pale atakapo patikana au atakapojitokeza.

Kwa anayemfahamu mwanamke huyo anayeonekana akipigwa amjulishe afike dawati la jinsia Polisi Msimbazi ili hatua ziendelee kuchukuliwa dhidi ya kitendo alichofanyiwa.

Jeshi la Polisi linaendelea kutoa wito kujiepusha na tabia za kujichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume na sheria za nchi na hakuna aliye juu ya sheria.

Imetolewa na:

Msemaji wa Jeshi la Polisi
Makao Makuu ya Polisi
Dodoma, Tanzania.

19/10/2025

HAKUTAKUWA NA NYWINYWI

17/10/2025

TANZANIA 👍

  Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imetangaza kupandisha kima cha chini cha m...
17/10/2025

Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu imetangaza kupandisha kima cha chini cha mshahara kwa sekta binafsi kutoka Shilingi 275,060 hadi Shilingi 358,322, ikiwa ni ongezeko la asilimia 33.4.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Ridhiwani Kikwete, ametoa kauli hiyo leo Ijumaa, Oktoba 17, 2025, na kuongeza kuwa ongezeko hilo kwa sekta binafsi ni utekelezaji wa matakwa ya kisheria.

Waziri Ridhiwani ameongeza kuwa Serikali inataka waajiri wote wa sekta binafsi kuhakikisha wanazingatia na kutekeleza kima hicho kipya cha mshahara kwa mujibu wa sheria na kuonya kuwa Ofisi yake haitasita kuchukua hatua kwa waajiri watakaokaidi au kushindwa kutekeleza agizo hilo kwa makusudi, akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kufuatilia kwa karibu utekelezaji wake.

Kima hicho kipya cha mshahara kitaanza kutumika rasmi Januari 1, 2026, kikilenga kuimarisha ustawi wa wafanyakazi na kuleta uwiano na ongezeko la mishahara ya watumishi wa umma lililotangazwa awali.

Msanii chipukizi, Bride Vuitton amewasilisha dai la haki miliki (copyright claim) YouTube dhidi ya wimbo mpya wa Nandy a...
28/09/2025

Msanii chipukizi, Bride Vuitton amewasilisha dai la haki miliki (copyright claim) YouTube dhidi ya wimbo mpya wa Nandy aliomshirikisha Jux, Sweety.

Kupitia dai hilo, Bride Vuitton ametoa siku 7 kwa Nandy kuondoa wimbo huo yeye mwenyewe kabla YouTube haijauchukua hatua ya kuufuta rasmi na kumpa Nandy ‘copyright strike.’

Kwa uchungu, Nandy ameandika:

“Mdogo wangu Bride Vuitton kutaka kuwa mkubwa kunahitaji juhudi. Kufika tulipo kunahitaji uwekezaji mkubwa sana. Na ukitaka kushikwa mkono, unashikwa kwa wema na sio kurudisha mtu nyuma!

Najua umeiona hii k**a trend ila hujui ni hasara kiasi gani umeiweka kwa huu wimbo. Unataka wimbo wangu ushushwe ili iwe story sababu una wimbo unaitwa Joro unahisi itakupa boost. Wala usijali – ungeweza leta hizo story bila kugusa investment niliyo fanya wala nisingekusumbua.

Najua unajitafuta, ila ulipofikia ni kutaka kuua ndoto yangu kabisa. Sasa basi sitakwasumbua – IT wangu wewe na walio kushauri kutaka kushusha video yangu mnaweza toa hiyo strike yenu. Niamini mdogo wangu, hiyo video ikishuka ukazika hela yangu chini, hata mama yako mzazi sitopokea msamaha wake.”

Tukio hili linakuja miezi michache tu baada ya wimbo mwingine wa Nandy, Tonge Nyama, kuondolewa YouTube na Mozee Kamana aliyedai msanii huyo alitumia brand yake kinyume cha sheria.

Kamana alienda mbali zaidi na kufungua kesi ya madai akitaka alipwe shilingi milioni 200.

Msanii mkubwa na Mwanasimba kindakindaki, Mbosso atakiwasha katika Simba Day 2025 itakayofanyika Septemba 10, 2025 kweny...
30/08/2025

Msanii mkubwa na Mwanasimba kindakindaki, Mbosso atakiwasha katika Simba Day 2025 itakayofanyika Septemba 10, 2025 kwenye Uwanja wa Mkapa.

Bila chuki wala fitina wasanii wa Tanzania wenye nguvu kimataifa ni watatu tu yani Diamond, Alikiba na Rayvanny kwa saba...
20/08/2025

Bila chuki wala fitina wasanii wa Tanzania wenye nguvu kimataifa ni watatu tu yani Diamond, Alikiba na Rayvanny kwa sababu zifuatazo na nitawapanga kwa namba.

1. DIAMOND PLATNUMZ
Huyu anakaa hapa kwa rekodi zake kubwa alizoweka kuanzia shows, tuzo na nguvu ya ushawishi na mpaka sasa bado amesimama k**a mwanamuziki mwenye nguvu zaidi kimataifa kutoka Tanzania.

2. ALIKIBA
Huyu anakaa namba mbili kwa makubwa aliyofanya zikiwemo shows za kimataifa na tuzo za kimataifa ambapo mpaka leo ukimtoa Diamond hakuna tena mwanamuziki mwingine aliyefanya mambo makubwa kumzidi yeye hili halihitaji unafiki Alikiba kukaa hapa ingawa kwasasa ameshuka sana na simuoni kwenye ushindani tena.

3. RAYVANNY
Hapa ukitaka kubisha unatakiwa uniambie unabisha kwasababu gani na k**a sio Rayvanny ni nani? Kwasababu Rayvanny amepata bahati ya kupanda majukwaa makubwa na kufanya kolabo kubwa hasa kupitia wimbo wake wa Tetema kitu ambacho kinamfanya kuwa mwanamuziki wa 3 kutoka Tanzania kufanya kolabo kubwa na kutumbuiza kwenye majukwaa makubwa. Sipendi kuihesabu Tuzo yake ya B.E.T sababu kipengele alichoingia hakina heshima kwasababu ni kipengere ambacho hakijumuishi wasanii wakubwa kutoka duniani bali ni wale wanaotazamiwa kukua ndio maana alishiriki kile kipengere kipindi anachipukia na sasa amekuwa hana tena nafasi ya kushiriki B.E.T sababu panatakiwa wale wasanii wakubwa ambao sio chipukizi. Kipengere alichoshinda Rayvanny ndicho alicho shiriki Abby Chams "Views Choice" wakati kutoka Afrika kipengere wanacho shiriki wasanii wakubwa ni "Best International Act" ambacho ukishinda unahesabika k**a namba moja Afrika kwahiyo siku akiwa mkubwa hapa Afrika mtamuona kwenye kipengere cha "Best International Act".

Kwenye hii orodha ukitaka msanii mwingine nje na hao aingie kwenye anga la kimataifa unatakiwa uje na data amefanya jambo gani huko kimataifa la kufanya aingie kwenye hiyo 3 bora sababu hapo hatupo kwenye ushabiki tupo kwenye uhalisia na data, ukibisha weka data watu wazione ili wakuamini. Ukiumia na hauna data unaruhusiwa kutukana tu maana mashabiki wa Bongo wanapenda tu umsifie msanii wake hata k**a hana alichofanya...

Alpher Platnumz ✍

 : Aliyekuwa mshambuliaji wa Singida Black Stars, Seleman Mwalimu 'Gomez' amejiunga na klabu ya Simba Sc kwa mkopo wa mw...
16/08/2025

: Aliyekuwa mshambuliaji wa Singida Black Stars, Seleman Mwalimu 'Gomez' amejiunga na klabu ya Simba Sc kwa mkopo wa mwaka mmoja akitokea klabu ya Wydad Casablaca inayoshiriki ligi kuu Nchini Morocco.

Gomez ambaye alijiunga na Wydad mwishoni mwa msimu uliopita anarejea Tanzania kwa mkopo huku akitarajiwa kuungana na mshambuliaji mwenzake Jonathan Sowah ambaye naye alikuwa Singida Black Stars.

Mwalimu alikuwa sehemu ya kikosi cha Wydad Casablanca kilichoshiriki michuano ya kombe la Dunia la FIFA ngazi ya klabu huko Marekani ambapo alicheza mechi mbili kati ya tatu za hatua ya makundi.

Address

Mjini
Morogoro

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00

Telephone

+255625788632

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ALPHER TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to ALPHER TV:

Share

Category