Mlimba tv

Mlimba tv MLIMBA TV ni tv ya mitandao ya kutoa habari na matukio kokote duniani tell the most difficult stories. Join us!

For more breaking news updates follow ,mlimba tv,


MAWASILIANO 0684495100, [email protected],

13/06/2026
Happy Birthday Deus liganga mwandishi wa habari kutoka  mlimba , home boy wa moro mungu akutunze .
11/06/2026

Happy Birthday Deus liganga mwandishi wa habari kutoka mlimba , home boy wa moro mungu akutunze .

11/06/2026

Sikia hii kwa faida Yako na ndugu na jamaa.

📍Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis M***a Omar (Mb), amewasilisha Mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Mapato na...
11/06/2026

📍Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis M***a Omar (Mb), amewasilisha Mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2026/2027, ambapo amesema Serikali inatarajia kukusanya na kutumia jumla ya shilingi trilioni 62.33, ikiwa ni ongezeko la asilimia 10.3 ikilinganishwa na bajeti ya mwaka 2025/26.

Mhe. Balozi Omar amesema kuwa, mapato yanatarajiwa kuwa shilingi trilioni 46.79 ambapo mapato ya kodi ni shilingi trilioni 36.99, mapato mengine ni shilingi trilioni 9.24 (ikijumuisha mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa shilingi trilioni 1.977) na misaada kutoka kwa washirika wa maendeleo shilingi bilioni 563.1.

Aidha aliongeza kuwa Ili kuendana na dhamira ya kujitegemea katika uendeshaji wa Serikali na maendeleo, takribani robo tatu ya bajeti yote ya mwaka 2026/27, sawa na asilimia 74.2 inatarajiwa kugharamiwa na mapato ya ndani.

“Matumizi na uwekezaji katika mali zisizo za kifedha yanakadiriwa kuwa shilingi trilioni 54.50 pasipo kujumuisha malipo ya mtaji wa deni la Serikali. Kati ya kiasi hicho, stahiki za watumishi ikijumuisha michango ya pensheni ni shilingi trilioni 10.13, gharama za bidhaa na huduma shilingi trilioni 5.22, malipo ya riba ni shilingi trilioni 6.86, ruzuku shilingi trilioni 25.32, mafao na misaada ya kijamii shilingi trilioni 1.01, uwekezaji katika mali zisizo za kifedha shilingi trilioni 2.33 na gharama nyingine shilingi trilioni 3.63.” alisema Mhe. Balozi Omar

Aliongeza kuwa kulingana na makadirio ya mapato na matumizi hayo, kunajitokeza nakisi kwenye bajeti ya shilingi trilioni 7.71 na Serikali itaendelea kugharamia nakisi ya bajeti kwa kutumia mikopo kutoka vyanzo vya ndani na nje kwa kuzingatia Mkakati wa Muda wa Kati wa Kusimamia Deni la Serikali (2025/26 – 2027/28).

Mhe. Balozi Omar alisema kuwa, Katika mwaka 2026/27, Serikali inatarajia kukopa jumla ya shilingi trilioni 15.54 ambapo Kati ya kiasi hicho, mikopo ya ndani ni shilingi trilioni 6.56, mikopo ya nje yenye masharti nafuu shilingi trilioni 6.55 na mikopo ya nje yenye masharti ya kibiashara shilingi trilioni 2.43. Aidha, Serikali inakadiria kulipa malipo ya mtaji kwa mikopo iliyoiva shilingi trilioni 7.84.

11/06/2026
Mwigizaji Mkongwe wa Filamu Nchini, Issa Joseph maarufu k**a Mzee Onyango amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Juni 11, ...
11/06/2026

Mwigizaji Mkongwe wa Filamu Nchini, Issa Joseph maarufu k**a Mzee Onyango amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Juni 11, 2026 katika Hospitali ya Jeshi Lugalo, Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Msiba wa Mzee Onyango upo Kawe jirani na Viwanja vya Gofu vya Lugalo, mlimba tv imezungumza na Mtoto wa marehemu, Joshua Joseph Issa ambaye amesema Baba yake alikuwa akiugua kwa muda na umauti ulimkuta majira ya saa 8 usiku akiwa Hospitalini hapo.

Pia amesema kuwa familia bado inaendelea na vikao vya maandalizi ya mazishi na kwamba taarifa rasmi kuhusu ratiba na taratibu za mazishi zitatolewa baadaye kwa umma.

Kwa upande wake, Rafiki wa karibu wa marehemu na Mwigizaji mwenzake wa muda mrefu, Mahamood Marijebi maarufu k**a Mwita Mwaranya, amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo hicho.

Address

MLIMBA TV
Morogoro
023

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mlimba tv posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mlimba tv:

Share