FikraZangu MaishaYangu

FikraZangu MaishaYangu THINK POSITIVE. Join us: FIKRA ZANGU MAISHA YANGU.
(1)

Mtaani kuna watu wengi sana wenye vipaji vikubwa lakini miaka nenda miaka rudi wapo palepale yaani hawapigi hatua.Kuna m...
20/02/2025

Mtaani kuna watu wengi sana wenye vipaji vikubwa lakini miaka nenda miaka rudi wapo palepale yaani hawapigi hatua.

Kuna mtu ni mchezaji mzuri sana wa mpira wa miguu lakini hata kwenye timu ya mtaani kwao hapati nafasi ya kucheza.

Kuna mtu ni muimbaji mzuri na ana nyimbo nyingi zenye mafunzo na burudani lakini hata studio hajawahi kufika ila ukimuuliza atakwabia "mimi najua sana kuimba siku nikisema niingie studio Mondi mwenyewe haniwezi."

Sawa kipaji unacho lakini kipaji peke yake hakiwezi kukupa mafanikio yoyote k**a usipokubali kulipa gharama.

Kuna mambo mengi yanayoweza kukufanya ufanikiwe kupitia kipaji lakini leo tunashare machache tu k**a ifuatavyo;

1. Gundua kipaji chako, - Hii ni hatua ya mwanzo kabisa ya kufahamu wewe una kipai gani. Je, kucheza mpira, kuimba au kuogelea?

2. Fanya mazoezi, - Ukishagundua una kipaji gani pili unapaswa kujua ni mazoezi ya aina gani yatasaidia kukuza kipaji chako.

3. Jitokeze hadharani, - Kipaji hakiwezi kukutoa hapo ulipo k**a utabaki nacho chumbani. Toka nje, onesha watu uwezo ulionao ili waone uimara wako na yapi madhaifu yako kusudi wakurekebishe uzidi kuboresha kipaji chako.

4. Tafuta connection (ungana na watu.) - Siku zote hakuna mafanikio ya mtu mmoja. Tafuta watu wa kushirikiana nao au watakaokuwa tayari kukushika mkono na kufanikisha safari yako ya mafanikio kupitia kipaji chako.

5. Tafuta pesa, - Siku hizi kila kitu kinahitahi pesa. Bila pesa utashindwa kufanya vitu vingi sana muhimu katika kipaji chako.
MFANO: Mwanamuziki anahitaji pesa kwaajili ya kulipia studio, kushoot videos, mavazi, gharama za digital platforms nk.

NB: Mafanikio sio jambo la mojakwamoja bali ni mchakato wa muda mrefu ambapo ndani yake kuna kupanda na kushuka. Usisahau kuna kudhurumiwa pia but stay focused.

Usiruhusu kukata tamaa hatak**a umeshindwa kutoka mara ngapi. Jenga imai kuwa ipo siku kipaji chako kitakufikisha kwenye nchi ya ahadi na kula matunda ya jitihada zako.

MUNGU akubariki sana utimize ndoto zako.

Kila mtu anapenda maisha mazuri na kila mtu anapenda vitu vizuri. Kila mtu anapenda mke mzuri na kila mtu anapenda mume ...
20/02/2025

Kila mtu anapenda maisha mazuri na kila mtu anapenda vitu vizuri. Kila mtu anapenda mke mzuri na kila mtu anapenda mume mzuri.

Tukiwa shuleni kila mtu alipenda kupata Division I au First Class ya 5.0 GPA lakini sio wote tulifanikiwa kupata.

Tulipo hapa kila mtu anapenda aishi miaka mingi na hata siku akifa anapenda aende mbinguni lakini sio wote tutakao uona ufalme wa Mungu.

Neno linasema
MATHAYO 7:21
"Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni."

Hapa tunajifunza kwamba kusema tu kwamba mimi nataka kuwa tajiri hakuwezi kukufanya wewe uwe tajiri.

Kusema tu kwamba mimi nataka kufaulu mitihani ya shule au chuo hakutoshi kukufanya wewe ufaulu.

Kusema tu kwamba mimi nataka kumuoa au kuolewa na fulani haitoshi kukufanya wewe kuoa au kuolewa na mtu huyo.

Matokeo mazuri ya kila jambo yana kanuni na hata kufeli pia kuna kanuni.

Maranyingi mtu anapata kile anachostahili na sio kile anachokipenda.

Ukiona mtu amepata kile asichostahili basi kuna mawili aidha amepata bahati au kuna nguvu zisizo halali zimetumika na kutumia nguvu zisizo halali ni lazima kutaleta madhara makubwa siku za mbeleni.

Furaha isiyotokana na haki haiwezi kudumu.

Tujifunze kulizika na kile MUNGU anachotujalia na tushukuru kwani ndicho tunachostahili kupata kinyume na hapo tutaishia kumkufuru yeye aliyetujalia.

K**a mafanikio uliyonayo ndio yale uliyotaka au k**a mume / mke uliyenae ndio yule uliyemtaka piga goti mwambie MUNGU Ahsante.

Lakini k**a bado ulivyo leo si vile unavyotaka kuwa endelea kuomba naye MUNGU atakupa unachostahili lakini hakikisha unafanana na kile unachokiomba.

Huwezi kupata mke mwema wakati wewe sio mwema wala huwezi kupata mume bora wakati wewe sio bora. Utapata unachostahili.

Neno linasema
Mathayo 7:6
"Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua."

Hivyo basi MUNGU hakupi unachotaka, anakupa unachostahili.

Don't forget to follow my page for more educative topics. Ahsante.

George Francis

Usipange kujuta hata siku moja eti kwasababu mume aliyekupa ujauzito amekukimbia au mume uliyezaa nae amekuacha na amekw...
20/02/2025

Usipange kujuta hata siku moja eti kwasababu mume aliyekupa ujauzito amekukimbia au mume uliyezaa nae amekuacha na amekwenda kuoa mtu mwingine.

Usione aibu hata kidogo eti watu watakuonaje au watasema nini kuhusu wewe kutokuolewa na mwanaume uliyezaa nae.

Ndoa ni mpango wa Mungu unaofanikishwa na watu wa jinsia mbili tofauti waliokubaliana kwa hiyari kuishi maisha ya mke na mume siku zote za maisha yao.

Ndoa ni agano takatifu ambalo Mungu amelibariki.

Kwa kusudi la MUNGU mtoto anapaswa atokane na ndoa na haipaswi kushiriki tendo la ndoa kabla ya ndoa na ndio maana likaitwa tendo la ndoa.

Lakini kutokana na madhaifu ya kibinadamu tunajikuta tunafanya zinaa na hata kuzaa kabla ya ndoa.

Neno linasema
1 Wakorintho 7:1
"Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke."

Kabla ya ndoa neno linatuhasa tusigusane.

1 Wakorintho 7:3
"Mume na ampe mkewe haki yake, na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake."

Baada ya ndoa ndio mume na mke wanapaswa kupeana haki ya ndoa.

Waebrania 13:4
"Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu."

Sasa imeshatokea zinaa imefanyika na mtoto amepatikana.
SWALI: Je, ufanye nini?

Single mother, narudia tena usijilaumu, usilie, usijihukumu wala usilazimishe ndoa na huyo uliyezaa nae.

K**a upo tayari na yeye yupo tayari kuoana basi ni jambo zuri na Mungu azidi kuwabariki. Lakini k**a haupo tayari au yeye hayupo tayari USILAZIMISHE.

Mrudie MUNGU, Jitunze, Jithamini Na Usifanye Tena Zinaa. Omba Ukiamini Na Mungu Atakupa Mtu Sahihi Wa Kuoana Nae.

K**a kuna madhaifu kadhaa ambayo pengine yalimfanya baba wa mtoto ashindwe kuanzisha maisha ya pamoja na wewe jitahidi urekebishe na uwe mwanamke bora zaidi ya alivyokukuta.

Kataa zile story za mashoga zako au ndugu zako eti kuna mganga mmoja mzuri twende nikupeleke mwambie nenda mwenyewe NDOA HAILAZIMISHWI.

Shirikiana vizuri na mzazi mwenzako katika malezi na matunzo bora ya mtoto. Usikubali kutumika tena kingono.
TUNZA THAMANI YAKO.

Mwenyezi MUNGU awabariki single mothers wote na awatimizie aja zenu zilizo njema.

Prepared By George Francis

"Ni muhimu kuweka malengo katika maisha. Malengo ni k**a ramani inayokuongoza katika safari ya mafanikio.Huwezi kufaniki...
14/02/2025

"Ni muhimu kuweka malengo katika maisha. Malengo ni k**a ramani inayokuongoza katika safari ya mafanikio.

Huwezi kufanikisha malengo yako kwa kulala na kuamka, wala kwa uchawi au nguvu za giza.

Kuna mambo ya msingi ya kuzingatia ili kutimiza malengo yako.

Hapa tunakwenda kujifunza mambo machache, ambayo ukiyazingatia nina uhakika kwa neema ya Mungu, malengo yako yatakwenda kutimia

Wote na tuseme "AMINA"

1. BIDII
Ili kutimiza malengo yako inahitajika kuwa na bidii katika kukitafuta kile unachokitaka.

Neno la Mungu linasema
"Mkono wa mwenye bidii utatawala, bali mvivu atalipishwa kodi."
MITHALI 12:24

"Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa masikini, bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha."
MITHALI 20:4

Soma MITHALI 11:27, 12:27, 13:4, 16:26, 21:5 & 22:29.

Bidii itakufanya uweze kutawala au kuwa tajiri. Kwenye kila unachohitaji kistawi katika maisha yako, ukiweka bidii utafanikiwa.

2. UTULIVU
Kuna methali inasema
"haraka haraka, haina baraka."

Hivyo, usifanye kazi kwa pupa bali weka umakini ili upate hata nafasi ya kurekebisha unapofanya makosa.

Neno la Mungu linasema,
"Basi twawaagiza hao na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo watende kazi kwa UTULIVU na kula chakula chao wenyewe."
2WATHESALONIKE 3:12

Ukikosa utulivu unaweza kuacha ulichopaswa na kufanya usichopaswa kutenda kwaajili ya Ustawi wa malengo yako.

3. SUBIRA NA UVUMILIVU
Kuna msemo unasema "subira yavuta heri."
Mafanikio ya kweli yanahitaji muda ili kuleta matokeo mazuri. Ukikosa subira na uvumilivu unaweza kukata tamaa ikiwa imebaki hatua moja tu kuanza kula matunda ya kazi yako.

Neno linasema,
"Angalieni twawaita heri wao waliosubiri...."
YAKOBO 5:11

"Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu."
LUKA 21:19

Subira itakusaidia kuokoa kile ambacho kwa kukata tamaa ungekipoteza.

"Mvumilivu hula mbivu"

Neno linasema
"Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho ndiye atakayeokoka."
MATHAYO 24:3

"Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi."
WAEBRANIA 6:15

Tukiwa na BIDII, UTULIVU, SUBIRA na UVUMILIVU, mafanikio kwetu ni swala la muda tu.

Tuendelee kupambana na Mungu awabariki sana."


So we have to Learn.

George Francis

Ujumbe kwaajili ya VIJANA wa kiume.1. Usiwe single. - Miaka 18-25 ni umri ambao umeshaanza kukomaa kimwili na akili Kwa ...
14/02/2025

Ujumbe kwaajili ya VIJANA wa kiume.

1. Usiwe single. - Miaka 18-25 ni umri ambao umeshaanza kukomaa kimwili na akili Kwa kiasi fulani. Kiwango cha hisia katika umri huu huwa ni kikubwa sana. Ukishindwa kuzitawala vyema hisia zako utajikuta nje ya group.

2. Usionge kupitiliza. - Huo ni umri wa kuanza kutunza fedha kwaajili ya kesho yako hivyo nidhamu ya fedha inahitajika kwa kiasi kikubwa. Timiza majukumu yaliyo ndani ya uwezo wako tu, yale yaliyo nje ya uwezo wako kubali yapite tu.

3. Kuwa na mpenzi mmoja tu. - Mpenzi mmoja anatosha kwa afya. Mahusiano mengi yatakupotezea muda, fedha na heshima pia ni hatari kwa afya. Kumbuka tiba ya UKIMWI bado haijagundulika.

4. Tongoza wanawake wengi. -Usishagae, sijakosea kuandika. Nilichoandika ndicho ninachomaanisha. Tongoza zaidi wanawake wenye hadhi ya juu kuliko wewe. Hii itakusaidia ukomae kiakili na ujifunze kuyakubali maumivu ya kukataliwa. Soma tena namba 3. ๐Ÿ˜€

5. Tumia kinga. - Usisahau condom k**a bado hujajiandaa kuwa baba au shauriana na mpenzi wako mkubaliane njia salama zaidi ya uzazi wa mpango. Kuwa baba ukiwa bado hujajipanga kutachelewesha hatua moja nyuma kuelekea ndoto zako zinazohitaji fedha ili kuzitimiza.

6. Usimtambulishe kwa wazazi. - Wazazi wako sio watoto wadogo. Ni dharau kuwaonesha wazazi mpenzi ambaye huna lengo la kuoana nae. Nenda kamtambulishe siku ukishakuwa tayari kuanza nae maisha ya ndoa.

7. Usianzishe mahusiano na mashangazi. - Katika umri wako acha kudate na malaya wala wanawake waliokuzidi umri. Kataa kabisa kulelewa.

8. Usiangalie picha za utupu. - Acha kabisa kuangalia picha wala video za utupu. Hakuna raha yoyote kwa mwanaume aliyekamikika kuangalia mwanaume mwingine akifanya mapenzi. Ni mashoga pekee wanaofurahia kuangalia uume wa mwanaume mwingine.

9. Acha kujichua. - Sabuni haiwezi kuwa mbadala wa mwanamke. Kujichua hakuwezi kukupa raha ambayo ungeipata kwa kushiriki tendo la ndoa. Kujichua kunaharibu nguvu za kiume na kufanya mkemia mkuu ashindwe kusimama vizuri. K**a unaupenda urijali wako acha kabisa kujichua na fanya mazoezi. Soma point namba 1.

10. TAFUTA PESA. - Zingatia sana point hii ndio maana nimeandika kwa herufi kubwa. PESA, PESA, PESA.

Kizazi cha 2000s ni kilizazi kinachotawaliwa na mapenzi zaidi kuliko upendo. Mabinti wadogo kutoka kimapenzi na wazee im...
14/02/2025

Kizazi cha 2000s ni kilizazi kinachotawaliwa na mapenzi zaidi kuliko upendo.

Mabinti wadogo kutoka kimapenzi na wazee imekuwa sio kitu cha kushangaza au vijana wadogo kutoka na mishangazi sio story tena, ni jambo la kawaida kabisa.

Shilingi elf 3 imekuja kuharibu kila kitu na kufanya mahusiano yasiwe na maana tena kwa vijana wasiopenda majukumu na wadada wavivu ambao wameamua kugeuza miili yao k**a kitega uchumi.

Siku hizi vijana hawatongozi tena wanawake mara mbilimbili, wanajaribu maramoja tu na mwanamke akiringa hawana tena muda wa kurudi mara ya pili.

Ukimkataa asubuhi usiku utamkuta na shilingi elf 3 yake anaruka na madada poa. Magonjwa yataishaje kwa staili hii?!! ๐Ÿค”

Mitaa imejaa uzinzi. Ngonjera za miguno zina mashabiki wengi, kuliko mahubiri ya neno la Mungu. It's too sad. ๐Ÿ˜ญ

Ni ngumu kumjua yupi yupo real na yupi ni fake kwasababu tabia na mienendo zinafanana. Binti anayevaa nguo ndefu na majuba kujisitiri nyakati za mchana ndiye huyo usiku anajiuza.

Shilingi elf 3 imewaponza wale mabrother men wanaopenda mteremko na ofa ya bia za bure huko club na kwenye madundo ya mtaani.

Lakini selikari inajua na kila mtu anajua madhara ya shilingi elf 3 kwenye kizazi hiki. Bad enough, hakuna mtu anayejali.

Je, nini kifanyike ili kutatua changamoto hii?

NB:
Ukisoma Bila Kutafakari Huwezi Kunielewa.

FOLLOW George Francis

ใ‚šviralใ‚ท

Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu,wanawake waliopewa talaka wangoje mpakahedhi tatu zipite.Na waume wao wana haki zaidi ya kuw...
10/02/2025

Kwa mujibu wa Qur'an Tukufu,
wanawake waliopewa talaka wangoje mpaka
hedhi tatu zipite.

Na waume wao wana haki zaidi ya kuwarejesha katika muda huo, k**a wakitaka isilahi au kuwaacha kwa wema.

Qur'an inasema,
"Talaka ni mara mbili. Kisha ni kukaa kwa wema au kuachana kwa vizuri."
โš–๏ธSoma (Sura 2 aya 229).

Mwanamke aishapo kupewatalaka, basi mpaka siku ya hedhi yake zifikapo na kuisha,huhesabiwa talaka moja.

Hata hedhi ya pili kuwa ni talaka yapili. Mpaka hedhi ya tatu k**a mume akimrudia kabla yakwisha muda wake huwa ni mkewe.

Lakini hedhi ya tatu ikiisha
na mume hakumrudia mkewe huwa si mkewe tena, na hapondiyo huhesabiwa amekwisha mwacha.

Na k**a mke ana
mimba pia anatakiwa kuweka wazi.

Katika kipindi cha utolewaji wa TALAKA hizo, mwanaume anapaswa kuwa anahesabu siku za eda.

Lakini pia mwanaume hawapaswi kumtoa mwanawake katika nyumba yake wala mwanawake hapaswi kutoka mwenyewe mpaka muda wa siku za eda upite na hatimae kuachana kwa wema.

Katika Suratul Baqarah sura ya 2:232, Qurโ€™ani inasema:

ูˆูŽุฅูุฐูŽุง ุทูŽู„ู‘ูŽู‚ู’ุชูู…ู ุงู„ู†ู‘ูุณูŽุงุกูŽ ููŽุจูŽู„ูŽุบู’ู†ูŽ ุฃูŽุฌูŽู„ูŽู‡ูู†ู‘ูŽ ููŽู„ูŽุง ุชูŽุนู’ุถูู„ููˆู‡ูู†ู‘ูŽ ุฃูŽู†ู’ ูŠูŽู†ู’ูƒูุญู’ู†ูŽ ุฃูŽุฒู’ูˆูŽุงุฌูŽู‡ูู†ู‘ูŽ ุฅูุฐูŽุง ุชูŽุฑูŽุงุถูŽูˆู’ุง ุจูŽูŠู’ู†ูŽู‡ูู…ู’ ุจูุงู„ู’ู…ูŽุนู’ุฑููˆูู

โ€œMnapokuwa mmewataliki wake zenu, na wamemaliza eda zao, ama kaeni (warejeeni) nao kwa wema au waacheni kwa wema.

Msiwashikilie kwa nguvu ili muwatese, hamuwarejei wala hamuwaachi."

Mume k**a umeamua kumrea mkeo baada ya TALAKA ya kwanza au ya pili basi mrejee na kuishi nae kwa wema.

Lakini k**a umeamua kumwacha mojakwamoja pia mwache kwa wema.

Katika uislamu, mwanamke anawezakujikomboa kwa kudai talaka na kurudisha mahari aliyopewa na mumewe.

Lakini mwanamume mcha Mungu, anatakiwa kusamehe kurejeshewa mahari kutokana na hali ya kimaisha ya mke japokuwa kupokea ni haki yake.

Qurโ€™ani Tukufu inasema;

ูˆูŽูƒูŽูŠู’ููŽ ุชูŽุฃู’ุฎูุฐููˆู†ูŽู‡ู ูˆูŽู‚ูŽุฏู’ ุฃูŽูู’ุถูŽู‰ูฐ ุจูŽุนู’ุถููƒูู…ู’ ุฅูู„ูŽู‰ูฐ ุจูŽุนู’ุถู ูˆูŽุฃูŽุฎูŽุฐู’ู†ูŽ ู…ูู†ู’ูƒูู…ู’ ู…ููŠุซูŽุงู‚ู‹ุง ุบูŽู„ููŠุธู‹ุง

โ€œVipi mnaweza kunyangโ€™anya mahari (mliyowapa) na hali mmeshaingiliana nao, na wamechukua kwenu ahadi thabiti (ya kuwalipa mahari kamili)
โš–๏ธSuratul Nisaa, 4:21.

Mume mwenyewe akimwacha mkewe, mahari hairudishwi.

Mahak**a katika kesi ya MWINYIHAMISI KASIMU vs ZAINABU BAKARI, (1985) TLR 217,   iliamua kwamba, ili kutoa amri ya TALAK...
10/02/2025

Mahak**a katika kesi ya MWINYIHAMISI KASIMU vs ZAINABU BAKARI, (1985) TLR 217,
iliamua kwamba, ili kutoa amri ya TALAKA k**a ilivyo kwa mujibu wa kifungu cha 107(3) cha Sheria ya Ndoa,
Ni lazima kwanza ijirizishe mambo yafuatayo,

(i). Wanandoa walioana chini ya sheria ya kiislamu.

(ii). Bodi ya usuluhishi ya ndoa imethibitisha kuwa imeshindwa kuwasuluhishwa wanandoa husika.

(iii). Pamoja na Bodi ya usuluhishi kushindwa kusuluhisha, lakini mmoja ya wanandoa amefanya kitendo ambacho kwa mujibu wa sheria za kiislamu kinatosha kuvunjika kwa ndoa husika.

Katika kesi hii, Mahak**a haikuizinisha TALAKA kwasababu hakukuwa na kitendo kinachoonesha kuvunjika kwa ndoa chini ya sheria ya kiislamu.

Katika kesi hii, Mahak**a ya mwanzo ilikataa ombi la TALAKA la mwanamke na hata alipokata rufaa Mahak**a ya wilaya, ombi la TALAKA lilikataliwa pia.

Lakini hakimu alishauri kwamba, kwasababu ndoa yao ilikuwa ni ya kiislamu Bi Zainabu anaweza kupata TALAKA k**a ataamua kujikului kwa kurudisha mahari ambayo mwanaume alitoa.

Hiki ni miongoni mwa vitendo ambavyo mwanamke anaweza kufanya k**a anataka TALAKA kwa mujibu wa kifungu cha 107(3)(c) cha Sheria ya Ndoa.

TALAKA inaruhusiwa kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu na kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa.

Binadamu huwa tunabadilika, hivyo kuliko kuvumilia maudhi na karaha zisizokwisha na mwisho kuuana, ni afadhali kuachana kwa amani.

Kabla ya kufikia maamuzi ya kuachana mume na mke kwanza wanahimizwa kupatana.

TALAKA inakuja baada kushindikana kwa mapatano.

Mume na mke wakishindwa kupatana watawaita watu wawili, mmoja wa upande wa mke na mwingine wa upande wa mume.

Kusudi baada ya kuchunguza ugomvi wao, wajaribu kila njia kuwapatanisha na endapo
hawakupatana basi wenyewe sasa wataamua k**a kuachana na waachane kwa wema.

Katika uislamu kuna utaratibu wa TALAKA tatu.

Mume akitoa Talaka ya kwanza na ya pili anaweza kumrejea mkewe k**a wakikubaliana kurejeana na kuishi pamoja.

Lakini mume akimwacha mke kwa Talaka tatu hawezi kumrejea mkewe hadi mke huyo aolewe tena na mtu mwingine na washiriki tendo la ndoa, kisha waachane kwa Talaka ndipo mwanaume uweze kumwoa tena kwa kufuata utaratibu wa kufunga ndoa katika uislamu.

ุงูŽู„ุณูŽู„ุงู…ู ุนูŽู„ูŽูŠู’ูƒูู… ูˆูŽุฑูŽุญู’ู…ูŽุฉู ุงูŽู„ู„ู‡ู ูˆูŽุจูŽุฑูŽูƒุงุชูู‡ูโ€ŽAs-salฤmu alaikum wa-rahmatullahi wabarakฤtuh. โ€Peace be upon you as ...
10/02/2025

ุงูŽู„ุณูŽู„ุงู…ู ุนูŽู„ูŽูŠู’ูƒูู… ูˆูŽุฑูŽุญู’ู…ูŽุฉู ุงูŽู„ู„ู‡ู ูˆูŽุจูŽุฑูŽูƒุงุชูู‡ูโ€Ž

As-salฤmu alaikum wa-rahmatullahi wabarakฤtuh.
โ€
Peace be upon you as well as God's mercy and blessings.

Amani iwe juu yako pamoja na rehema na baraka za Mwenyezi Mungu.

Ahsante kwa kuendelea kufuatilia mada mbalimbali Mwenyezi Mungu alizonifunulia kuziandaa na kukuletea katika page zangu mbalimbali.

Leo naomba tukumbushane kuhusu TALAKA na taratibu zake kwa mujibu wa sheria (sharia) za dini ya kiislamu.

Ndoa ya kiislamu ni miongoni mwa ndoa zinazotambulika kisheria kwa mujibu wa Sheria ya Ndoa.

Ndoa ya kiislamu ni ile inayofungwa kwa kufuata taratibu zinazokubalika katika dini ya kiislamu.
โš–๏ธKifungu cha 25(3)(b) cha Sheria ya Ndoa.

Ndoa inatokana na makubaliano ya hiyari kati ya mwanamume na mwanamke bila kushinikizwa na mtu yeyote.

Katika uislamu, Mwanamume anaruhusiwa kuoa wake zaidi ya mmoja hadi wanne.

Muhimu ni kuwa na uwezo wa kuwapa matunzo na huduma zote kwa kuzingatia haki na usawa bila ya upendeleo.

Ndoa iliyofungwa kwa mujibu wa dini ya kiislamu inaweza kuvunjwa kwa kufuata taratibu za kisheria ka mujibu wa dini ya kiislamu.

K**a ilivyo katika ndoa nyingine, uislamu pia unaruhusu mume na mke kuachana kwa TALAKA kwa kuzingatia utaratibu.

TALAKA kutoka neno la kiarabu ุทู„ุงู‚) au talaaq ni utaratibu wa kuvunja ndoa baina ya mume na mke kabla mume au mke kufariki.

Sheria ya ndoa imeweka utaratibu au masharti ya kuvunja ndoa iliyofungwa kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.

Mahak**a ni lazima ijirizishe kuwa,
(i).Ndoa ilifungwa kwa mujibu wa dini ya kiislamu.
โš–๏ธ Kifungu cha 107(3)(a) cha Sheria ya Ndoa.

(ii). Bodi ya usuluhishi ya ndoa imethibitisha kuwa imeshindwa kusuluhisha na imetoa hati kwamba imeshindwa kusuluhisha wanandoa hao.
โš–๏ธ Kifungu cha 107(3)(b) cha Sheria ya Ndoa.

(iii). Mmoja kati ya wanandoa amefanya kitendo kinachoonesha kuvunjika kwa ndoa hiyo kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislamu.
โš–๏ธ Kifungu cha 107(3)(c) cha Sheria ya Ndoa.

Mfano: Mwanaume amempa mkewe talaka kwa mujibu wa dini k**a vile talaka ya kwanza, talaka ya pili na ya tatu kabla ya amri ya TALAKA ya Mahak**a kutolewa.

Inaendelea....


So we have to Learn.

DUNIA UWANJA WA VITA, MWISHO WETU KABURINI.Mwenyezi Mungu amemfurahisha sana mwanadamu kwa kumuweka duniani na kumpa mam...
07/02/2025

DUNIA UWANJA WA VITA, MWISHO WETU KABURINI.

Mwenyezi Mungu amemfurahisha sana mwanadamu kwa kumuweka duniani na kumpa mamlaka ya kuitawala dunia na vitu vyote vilivyomo duniani.

Mwanadamu anaumia sana kuona kuwa kuna siku ya mwisho itakayo mtenganisha na dunia.

Mwenyezi Mungu amemfanya mwanadamu kuwa kiumbe chenye ufahamu mkubwa kuliko kiumbe kingine chochote kilichoumbwa na Mwenyezi Mungu.

Ni kiumbe kilichopewa mamlaka ya kuitawala Dunia na kila kilichopo ndani yake.

Lakini ajabu ya yote mwanadamu huyu amekuwa kiumbe chenye tamaa na chenye kutaka mamlaka makubwa zaidi ya haya aliyopewa.

Pamoja na kupewa mamlaka makubwa lakini bado kuna baadhi ya wanadamu wanatamani kuwa na mamlaka ya kupanga hata ridhki za watu. Yaani nani apate na nani akose, nani aendelee kuishi na nani uwe mwisho wake wa maisha yake hapa duniani.

Mwanadamu ni kiumbe chenye wivu sana. Wengi wao hawatamani kabisa kuona mwingine amepata, wanajiona wao ndio wanastahili kupata pekee.

Yaani k**a ni pesa wawe nazo wao tu au k**a ni majumba na magari ya kifahari wawe nayo wao tu. Wanachukia sana kuona wengine wanapiga hatua nzuri za maendeleo.

Wanadamu tunasahau kwamba kila mtu amepangiwa fungu lake. Kufanikiwa Kwa mtu mwingine hakuwezi kuharibu mafanikio yako.

Lakini kikubwa zaidi tutambue kuwa pesa, majumba na magari ya kifahari hatuzikwi nayo wala hayatusaidii chochote siku pumzi yetu itakapokata.

Mwisho wetu ukifika, kila tulichomiliki duniani tutakiacha hapahapa. Mbinguni tunaenda na amali njema tu.

Waliolala makaburini nao walikuwa hai k**a sisi. Walikuwa na mali na vitu vingi vya thamani k**a wewe au zaidi yako.

Lakini leo hawapo nasi tena, wameondoka wameacha kila kitu. Wameacha hata zile mali walizozipambania kwa guvu kubwa au hata kumwaga damu za watu.

Ndugu yangu mpendwa, ebu kabla hujaaribu maisha ya watu wengine, tafakari japo kidogo tu kuhusu KIFO.

Tafakari kwamba kuna siku utakufa.

1. Je, dhuruma yako kwa nafsi za watu zitakupeleka wapi?

2. Je, roho za watu ulizotoa au unazotaka kutoa zitakufaha kitu gani?

3. Je chuki, roho mbaya na ushirikina unaowatendea wengine utakusaidia nini?

4. Ujasiri au hicho kiburi cha kutenda maasi unakitolea wapi?

Address

Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FikraZangu MaishaYangu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to FikraZangu MaishaYangu:

Share