Sanuka Sports News

Sanuka Sports News Habari zote za michezo ulimwenguni utazipata hapa...

KWA MATANGAZO YA AINA YEYOTE PIGA 👇

Call : +255622147696

Tanzania 🇹🇿
(4)

Ameandika George Ambagile kutoka Wasafi FM radio ✍️ 🚨 Kiuchezaji Mohamed Doumbia ni bora zaidi ya Neo Maema (timu ikiwa ...
23/10/2025

Ameandika George Ambagile kutoka Wasafi FM radio ✍️ 🚨

Kiuchezaji Mohamed Doumbia ni bora zaidi ya Neo Maema (timu ikiwa na mpira) ila ila kitakwimu Neo Maema ni zaidi ya Mohamed Doumbia.

Neo Maema ana assists mbili huku Mohamed Doumbia akiwa hana assist hata moja.

🚨 :- Kipa namba moja wa klabu ya Mbeya City Beno David Kakolanya, ndiyo kinara wa Cleansheets katika Ligi Kuu Tanzania B...
23/10/2025

🚨 :- Kipa namba moja wa klabu ya Mbeya City Beno David Kakolanya, ndiyo kinara wa Cleansheets katika Ligi Kuu Tanzania Bara mpaka sasa akiwa amefanya hivo katika michezo mitatu msimu huu.

Kakolanya amepata Cleansheets kwenye mchezo dhidi ya Fountain Gate, Yanga SC na KMC FC huku akiruhusu mabao kwenye mchezo dhidi ya Azam FC na Tz Prisons katika Derby ya Mbeya.

Kipa huyo anawazidi Djigue Diarra (Yanga), Amas Obasogie (Singida BS), Jean Amonome (TRA United), Costantine Malimi (Mtibwa Sugar), Erick Johola (Mashujaa FC) na Ally Salim (Dodoma Jiji) ambao wote wana Cleansheets mbili mbili.

Nyanda huyo ameisaidia timu yake kukusanya alama saba baada ya michezo mitano na kwa sasa ndio vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu.

Jina la Kakolanya si geni katika masikio ya wadau wa soka kwani alianzia Tanzania Prisons kabla ya kutua Yanga , Simba na Singida BS ya mkoani Singida na kisha kutimkia kwa wauaji wa kusini Namungo FC kabla ya kurejea huko maskani kwao jijini Mbeya.

🚨 :- Nyota wa kimataifa wa klabu ya Yanga raia wa Ivory Coast Pacome Zouzoua amekiri kuwa kila mtu ameumizwa na matokeo ...
23/10/2025

🚨 :- Nyota wa kimataifa wa klabu ya Yanga raia wa Ivory Coast Pacome Zouzoua amekiri kuwa kila mtu ameumizwa na matokeo ya mchezo wa Ugenini dhidi ya Silver Strikers na wamejipanga kushinda ili kurejesha heshima na kufuzu hatua ya Makundi.

"Kila mmoja ameumizwa na yale matokeo, wote kwenye timu tulikuwa k**a tumepata taarifa mbaya ambayo hatukuitarajia, tumejua wapi tulikosea na tutarekebisha.

"Walishinda kwao na sisi tunarudi nyumbani tutakuwa mbele ya mashabiki wetu, tunataka kurudisha heshima ya klabu hii na furaha ya mashabiki wetu, tunataka kushinda ili twende makundi,"

🚨"Hakuna mtu anayeweza kulipa kiingilio akamuonye Boyeli, hiyo timu ni ya thamani ya bure ndiyo maana wakaamua kutangaza...
23/10/2025

🚨"Hakuna mtu anayeweza kulipa kiingilio akamuonye Boyeli, hiyo timu ni ya thamani ya bure ndiyo maana wakaamua kutangaza bure"

Ahmed Ally (Afisa habari wa klabu ya Simba SC)

🚨 :- Baada ya yanga sc kutangaza mechi yao dhidi ya silver strikers hakuna kiingilio sasa Klabu ya soka ya Azam fc imeta...
23/10/2025

🚨 :- Baada ya yanga sc kutangaza mechi yao dhidi ya silver strikers hakuna kiingilio sasa Klabu ya soka ya Azam fc imetangaza kuwa mchezo wake wa marudiano kufuzu Makundi Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya KMKM hautakua na kiingilio kwa majukwaa ya mzunguko.

Klabu hiyo imeeleza kuwa, ofa hiyo ya kuingia kushuhudia mchezo huo bure haitahusisha majukwaa yote ya watu maalum (V.I.P), ambapo Azam FC wamesema kuwa watatoa kadi maalum kwa watu wote watakaoingia kwenye eneo la majukwaa hayo.

🚨 :- Nyota wa zamani wa Ajax na Chelsea,Hakim Ziyech (32),amejiunga na Wydad Casablanca kwa mkataba wa mwaka mmoja.CC
22/10/2025

🚨 :- Nyota wa zamani wa Ajax na Chelsea,Hakim Ziyech (32),amejiunga na Wydad Casablanca kwa mkataba wa mwaka mmoja.

CC

🚨 :- Huko nchini Msumbiji ni k**a Luis Miquissone mchezaji wa zamani wa Vilabu vya Mamelodi Sundowns, Simba SC na Al Ahl...
21/10/2025

🚨 :- Huko nchini Msumbiji ni k**a Luis Miquissone mchezaji wa zamani wa Vilabu vya Mamelodi Sundowns, Simba SC na Al Ahly nik**a amejipata upya akiwa na klabu yake ya Ud Songo inayoshiriki ligi kuu nchini Msumbiji.

Luis ndiye kinara anayeongoza kwa utupiaji wa magoli ndani ya ligi kuu ya nchini Msumbuji akiwa amefunga magoli (8) kwenye michezo 14 UD-SONGO wakiwa wanaongoza ligi hiyo vile vile.

📷:- Muonekano mpya wa mshambuliaji wa klabu ya Yanga SC raia wa Zimbabwe Prince Mupumelelo DUBE.
20/10/2025

📷:- Muonekano mpya wa mshambuliaji wa klabu ya Yanga SC raia wa Zimbabwe Prince Mupumelelo DUBE.

20/10/2025

🔴🟡...TUSIBWETEKE HAWA NSINGIZINI HOTSPURS WANAJUA BOLI:- AhmedY AllY

-Mkuu wa idara ya habari wa klabu ya Simba SC Ahmedy Ally amewataka mashabiki wa Simba SC kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo wa marejeano dhidi ya Nsingizini Hotspurs ya Eswatini kwani bado ni mchezo mgumu kwa pande zote mbili.

📸 Mashabiki wa Nsingizini mara baada ya kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Simba Sc Hawaamini macho yao
20/10/2025

📸 Mashabiki wa Nsingizini mara baada ya kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Simba Sc

Hawaamini macho yao

Ameandika George Ambagile kutoka Wasafi FM radio ✍️ 🚨 -Tumezoea kuiona Simba ikitumia viungo wawili wakabaji katikati (d...
19/10/2025

Ameandika George Ambagile kutoka Wasafi FM radio ✍️ 🚨

-Tumezoea kuiona Simba ikitumia viungo wawili wakabaji katikati (double pivot), lakini wiki mbili zimemtosha Pantev kuamua kutumia kiungo mmoja wa ukabaji leo (single pivot) Naby Camara.

Aliamini kwenye kasi yake, uwezo wake wa kuanzisha mashambulizi kutoka chini, na wepesi wake ambao aliamini angeutumia k**a silaha kwenye kukaba. Huyu ni versatile kweli japo kwangu sioni akifanikiwa akiwa na Naby pekee.

Simba imezoea kutumia mabeki wa pembeni zaidi
Kapombe na Zimbwe zamani, kwa sasa Mligo kutengeneza mashambulizi kupitia pembeni ila leo muda mwingi timu imecheza katikati ya mistari (between the lines).

Baada ya mchezo dhidi ya Al Hilal, Dimitar Pantev alisema anataka timu yake icheze kwa kupenya kati ya mistari, kila mchezaji akiwa na uwezo wa kufanya hivyo. Aliona Simba ina aina hiyo ya wachezaji alipokutana nao kwenye mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa.

Utakuwa umeelewa kauli ya kocha mzuri anatafuta mfumo unaoendana na wachezaji waliopo kikosini
Ukisubiri mfumo wako utafutwe na wachezaji, utachelewa kujenga timu ilimkuta Fadlu.

Kwa nini Wilson Nangu leo mbele ya Chamou?
Nangu anatumia mguu wa kushoto zaidi, jambo linalomfanya yeye na Rushine wawe na uhuru , kwa kuwa wakitanua uwanja ataisaidia timu kupiga pasi haraka kila mtu akiwa upande wake.

Chamou anatumia mguu mmoja wa kulia pekee; mipira mingi alikuwa akipoteza upande wa kushoto, hata kwenye kukaba alikuwa anateseka pia.

Wilson Nangu ametoa kitu tofauti akiwa na mpira mguuni, wakati De Reuck akiwa ni pressing resistant CB anayejua kuua shinikizo la wapinzani na kucheza kwenye maeneo finyu.

Viungo wanne wa kati kwenye mfumo wa 4-1-4-1 Ahoua, Mutale, Maema, na Mpanzu wanashikiliwa na Selemani mwalimu juu, kwa nini?
Pantev alikuwa na dhamira ya kuudhibiti mchezo (control the game) kutokea juu: tupress kwa nguvu, tukae na mpira muda mwingi, na tusiwaruhusu wapinzani kufikilia kushambulia watuwaze sisi tu kwanza.

Hints kutoka kwa Pantev

🚨 :- Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwenye makazi nchini Msumbiji anayewakilisha Ufalme wa Eswatini na Jamhur...
19/10/2025

🚨 :- Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwenye makazi nchini Msumbiji anayewakilisha Ufalme wa Eswatini na Jamhuri ya Madagascar, Mhe. Hamad Khamis Hamad ametutembelea kambini na kuongea na wachezaji kuelekea mchezo wa leo Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Nsingizini Hotspurs

Address

Mgulasi
Morogoro

Telephone

+255676440118

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sanuka Sports News posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share