01/06/2026
JIBRIL (AS) ni miongoni mwa viumbe watukufu na wakubwa walioumbwa na Allah (SW). Ndiye malaika mkuu ambaye Allah anazungumza naye na amempa dhamana ya kufikisha ujumbe (Wahyi) kwa Mitume na manabii, pamoja na malaika wengine.
Yeye ni kiongozi wa malaika wote, anayetiiwa kwa upendo na uaminifu wake mkubwa. Makazi yake yako chini ya Arshi ya Mwenyezi Mungu. Jina Jibril maana yake ni "Mja mwenye nguvu wa Allah".
Allah anamtaja katika Qur’an k**a "Al-Ruh" yaani "Roho" (Mtakatifu). Hii ni kwa sababu Jibril alileta Qur’an, ambayo ndiyo chanzo cha uhai wa kweli wa nyoyo zetu.
Mtume Muhammad ﷺ alipokuwa akimtaja Jibril au Nabii Ibrahim (AS), mara nyingi aliwatakia amani na rehema k**a anavyofanyiwa yeye mwenyewe. Jibril ametajwa kuwa ni ‘Inda dhi-l-Arshi Makiin’ – ‘mwenye cheo kikubwa mbele ya Mola wa Arshi’.
UMBO LAKE LA ASILI👉🏾Jibril AS alipoonekana katika umbo lake kamili la kimalaika, alikuwa mkubwa sana kiasi cha kujaza upeo wote wa macho (kufunika anga). Mtume ﷺ alimuona katika umbo hili mara mbili tu. Ana mbawa 600 zenye urembo wa kupendeza ambapo vito k**a rubi na lulu vilikuwa vikidondoka kutoka kwazo, zikiwaka kwa mwanga wa kijani kibichi.
UMBO LA KIBINADAM👉🏾 Umbo ambalo Jibril alikuwa akitokea nalo mara nyingi zaidi mbele ya Mtume ﷺ. Allah alikuwa akimtuma katika umbo la mtu mzuri sana. Kila alipokuja Madina au Makka katika umbo la binadamu, alikuwa akifanana na Sahaba Dihya bin Khalifa al-Kalbi (RA), ambaye alikuwa mtu mzuri (handsome) kuliko wote katika kabila lake, kiasi cha kuitwa "Yusuf wa watu wake." Dihya alikuwa sahaba mtiifu aliyeshiriki vita vingi kuanzia Uhud na kuendelea