Proudly Muslim

Proudly Muslim ALLAH AKUBAR if you are proud of been a Muslim. then let's show each and everyone one that LLAH ILLAH ILLA LLAHU

Allahamdulilah
01/12/2025

Allahamdulilah

1. ALIYE KWENYE KIPANDO amsalimie anayetembea, anayetembea AMSALIMIE ALIYEKAA.Mtume ﷺ  amesema: “Mpanda farasi amsalimie...
28/11/2025

1. ALIYE KWENYE KIPANDO amsalimie anayetembea, anayetembea AMSALIMIE ALIYEKAA.

Mtume ﷺ amesema: “Mpanda farasi amsalimie mtembea kwa miguu; mtembea kwa miguu amsalimie aliyeketi; na kundi dogo lisalimie kundi kubwa (la watu).''

Riyad as-Salihin 857

2. UKIINGIA KULALA, LALIA UPANDE WAKO WA KULIA.

Mtume ﷺ alikuwa akilala chini ubavu wake wa kulia na kusoma: “Allahumma aslamtu nafsi ilaika, wajjahtu wajhi ilaika, wa fawwadtu amri ilaika, wa ‘alja’tu zahri ilaika, raghbatan wa rahbatan ilaika, la malja’a wa lantu bilka illaika, la malja’a wa lantu bil’a illaika. nabiyyikal-ladhi arsalta"

Riyad as-Salihin 813

3. USIPUMUE NDANI YA MAJI unayokunywa na USISHIKE UTUPU WAKO kwa mkono wa kulia .

Mtume ﷺ amesema: “Unapokunywa (maji), usipumue ndani ya chombo, na unapokojoa usiguse uume wako kwa mkono wako wa kulia.

Chanzo: Al-Bukhari 5630

4. UKIKOJOA HAKIKISHA VITONE vya mkojo havikurudii kwenye mwili wako. Ni vizuri zaidi ukikojoa ukiwa umechuchumaa.

5. UKIMCHINJA MNYAMA hakikisha unatumia kisu kikali ili asipitie maumivu kwa kusugua sana shingo yake.

Ni vizuri kunoa kifaa chako kabla ya kufanya hilo ili kumpunguzia maumivu makali mnyama anayechinjwa.

6. HAIPENDEZI kulala KIFUDIFUDI, kulalia Tumbo

Imepokewa kutoka kwa Ya'ish bin Tikhfah Al-Ghifari (radhi za Allah ziwe juu yake) Baba yangu alisema: Nilikuwa nimelala msikitini kwa tumbo langu, ndipo mtu akanitikisa kwa mguu wake na kusema: "Kulala namna hii hakukubaliwi na Mwenyezi Mungu." Nikainua macho nikaona ni Mtume wa Mwenyezi Mungu (ﷺ)."

Chanzo Riyadh as-Salihin 817...

KIFO CHA UMAR BIN ABDUL'AZIZZama alipokuwa Umar bin Abdul'aziz yuko ktk sakaratul mauti wale waliokuwepo ktk chumba chak...
16/11/2025

KIFO CHA UMAR BIN ABDUL'AZIZ

Zama alipokuwa Umar bin Abdul'aziz yuko ktk sakaratul mauti wale waliokuwepo ktk chumba chake walikuwa wakimuambia sema Laa ilaaha illallah muhammaun Rasuulullah,

Umar akawaambia nilini nilisahau kutamka neno hilo mpaka mnanikumbusha kulitamka?

Kisha Umar akatazama mbinguni na macho yake yakawa wazi akasema, uzuri wako upo usoni mwangu, na upendo wako upo moyoni mwangu, na utajo wako upo kinywani mwangu,,,vipi sasa upotee mpaka nikumbushwe kukutaja?

Kisha akawataka wale waliohudhuria pale nyumban kwake akiwemo mke wake watoke nje ya chumba chake wamuache mwenyewe,

Mke wake Faatma bint Abdulmalik bin marwaan akamuuliza, ewe Amiri wa waumini kwanini unanitoa chumnani ktk kitambo hiki?

Akasema Umar hakika yangu mimi naona ktk chumba nyuso ambazo sio za kibinaadam wala kijini zenye kupenda dhikri na mambo mazuri,

Ndipo akatoka mke wake lakini hakuenda mbali akasimama mlangoni kwa nje kwani mume wake yuko ktk hali ambayo sio ya kuachwa mwenyewe,

Mke wake akatega sikio kwenye mlango wa chumba kile ili asikilize kinacho endelea,

Akamsikia mume wake akisema
Karibu Baba Adam
Karibu mwandani wa Allah Ibrahiim
Karibu Nabii M***a a.s
Karibu roho wa mungu issa a.s
Karibu mtukufu wa Darja Sayyidiy Rasuulullah
Kisha akanyamaza kitambo kidogo, akasema
Karibu malakul mauti, mgeni aliyekuja kwa wakati na hapo akatamka akasema Ash'hadu Allaa Ilaaha Illallah Wa Ash'hadu Anna Muhammadan Rasuulullah

Na hapo hapo ikatoka roho yake ktk mapafu yake.

(Allah Atupe Mwisho Mwema)
البداية والنهاية لإبن كثير

SWALI: Swali langu k**a mwanaume ameandika talaqa kwenye karatasi akasema namuacha mke wangu talaqa tatu je zinahesabiwa...
10/11/2025

SWALI: Swali langu k**a mwanaume ameandika talaqa kwenye karatasi akasema namuacha mke wangu talaqa tatu je zinahesabiwa talaqa tatu au moja?

JIBU: Talaka ya aina hii katika sheria inaitwa Twalaqul Bidi‘iy (Talaka ya Kuzuliwa) kwani huwa imekwenda kinyume na sheria tukufu ya Kiislamu. Na hii ni ima kumpatia talaka mke wako akiwa katika damu ya hedhi, nifasi au talaka tatu kwa mara moja au sehemu moja.

Wanazuoni wa Kiislamu wametofautiana k**a talaka tatu mara moja zinahesabiwa kuwa ni tatu au ni moja. Hii ni kwa sababu kila kundi limetoa ushahidi kwa rai zao. Lakini kauli yenye nguvu zaidi ni kuwa mume anayetoa talaka tatu kwa mara moja inahesabiwa kuwa ni talaka moja lakini atakuwa amefanya makosa na madhambi katika tendo lake hilo na inabidi aombe msamaha.

Wakati mmoja Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alipashwa habari ya kuwa kuna mtu aliyetowa talaka tatu kwa mara moja. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) alikasirika sana na kishaa akasema: “Mnachezea Kitabu cha Allah, nami bado nipo baina yenu”

Na katika mas-ala haya Allah ametuambia: “T'alaka ni mara mbili” (2: 229).

Hii inamaanisha moja baada ya nyingine na wala siyo kuzitoa kwa wakati mmoja.

Na hakika inaonyeshwa wazi wazi wakati wa Sheikh Ibn Taymiyah alipotoa rai hii alipingwa sana na wanazuoni wa wakati wake lakini wanazuoni wa sasa wameirudia kauli hiyo ambayo ndiyo yenye nguvu.

Na Allaah Anajua zaidi.

asalaam aleykum warahmatulah wabarakatuhtumeona mengi yametokea tumepoteza ndgu. jamaa na marafki wengine wapo ma hospit...
04/11/2025

asalaam aleykum warahmatulah wabarakatuh
tumeona mengi yametokea tumepoteza ndgu. jamaa na marafki wengine wapo ma hospital k**a we mzima sema
ALLAHAMDULILAH

Indeed
25/10/2025

Indeed

dua muhimu
25/10/2025

dua muhimu

Dua, Ni njia ya mawasiliano kati ya mtu na Mwenyezi Mungu, Inaweza kuwa ni kwa hitajio fulani katika maisha ya Mwanadamu...
23/10/2025

Dua, Ni njia ya mawasiliano kati ya mtu na Mwenyezi Mungu, Inaweza kuwa ni kwa hitajio fulani katika maisha ya Mwanadamu. Ni kiunganishi cha moja kwa moja kwa Mwenyezi Mungu na katika hizo dakika nne au tano za Dua mtu anaweza kuzungumza chochote. Iwe ni jambo linamtia wasiwasi, au jambo ambalo anataka kumshukuru Mwenyezi Mungu kutokana nalo.

Sasa ni nyakati gani nzuri za kuomba Dua?

1. Muda wa usiku (kuanzia baada ya Sala ya Ishaai hadi adhana ya Fajr

Aliulizwa Mtume ﷺ “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni du’a gani inayosikika?” Akasema: "Katika theluthi ya mwisho ya usiku,". Imepokewa na al-Tirmidhiy, 3499; Thuluthi ya mwisho kwa makadirio ni masaa mawili kabla ya Sala ya Fajr.

2. Siku ya Ijumaa.

Mtume ﷺ alizungumzia kuhusu siku ya Ijumaa na akasema: “Kuna saa moja siku ya Ijumaa na ikiwa Mwislamu ataipata wakati wa kuswali na akaomba kitu kutoka kwa Allaah hakika atatimiza mahitaji yake.' [Sahih al-Bukhari]

3. Mvua inaponyesha.

Kuna mambo mawili ambayo hayatakataliwa: du’a wakati wa Adhana na mvua inaponyesha.” ( Sahih na al-Albani katika Sahih al-Jami’, (3078).

4.Wakati wa Sujudu

Mtume ﷺ alisema “Mja huwa karibu zaidi na Mola wake pale anaposujudu, basi muombeni sana Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hapo. [Muslim, abu Daawuud, an-Nasa'i na wengineo, Swahiyh al-Jamiy 1175]

5. Wakati wa Kunywa Maji ya Zamzam

Jabir (r.a) amesimulia kuwa Mtume ﷺ amesema: “Maji ya Zamzam ni kwa ajili ya yale yanayonywewa. [Ahmad 3: 357 na Ibn Majah #3062]. Maana yake ni kwamba unapokunywa maji ya Zamzam unaweza kumuomba Allah (SWT) chochote unachopenda kupata au kufaidika na maji haya k**a vile uponyaji wa maradhi.... nk.

6- Wakati wa kusikia kuwika kwa jogoo

“Mnaposikia sauti ya jogoo, basi muombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake, kwani amemwona Malaika. (Imesimuliwa na al-Bukhari, 2304; Muslim, 2729)

Na Allaah Anajua Zaidi..

21/10/2025

Address

Kilombero
Morogoro

Telephone

+255659938442

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Proudly Muslim posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share