Proudly Muslim

Proudly Muslim ALLAH AKUBAR if you are proud of been a Muslim. then let's show each and everyone one that LLAH ILLAH ILLA LLAHU

Baada ya Takbira ya kwanza na kufunga Swala Muislam atasema moja kati ya Hizi Dua.1- Subhaanaka-LLaahumma wabihamdika wa...
17/09/2025

Baada ya Takbira ya kwanza na kufunga Swala Muislam atasema moja kati ya Hizi Dua.

1- Subhaanaka-LLaahumma wabihamdika watabaarakas-Smuka wa Ta’aalaaa Jadduka walaa ilaaha Ghayruka
-Abu Dawud (776) and at-Tirmidhi (243)

2- Allaahumma Rabba Jibraaiyla wa Mikaaiyla wa Israafiyla, faatwiras-samaawaati wal ardhw, ’Aalimal ghaybi wash-shahaadah, Anta Tahkmu bayna ’ibaadika fiymaa kaanuw fiyhi yakhtalifuwn. Ihdiniy limakhtulifa fiyhi minal haqqi biidhnika Innaka Tahdiy man Tashaau ilaa swiraatwil-mustaqiym
--Muslim (770)

3- Wajjahtu wajhiya liLLadhiy fatwaras-samaawaati wal ardhwa haniyfan wamaa ana minal mushrikiyn. Inna swalaatiy, wanusuky, wamahyaaya wamamaatiy liLLaahi Rabbil ‘aalamiyn. Laa shariyka Lahu wabidhaalika umirtu wa anaa minal Muslimiyn. Allaahumma Antal-Maliku laa ilaaha illa Anta. Anta Rabbiy wa ana ‘abduka, dhwalamtu nafsiy wa’taraftu bidhambiy faghfirly dhunuwbiy jamiy’an innahu laa yaghfirudh-dhunuwba illa Anta. Wahdiniy liahsanil-akhlaaqi laa yahdiy liahsanihaa illa Anta, waswrif ‘annyi sayyiahaa laa yaswrif ‘anniy sayyiahaa illa Anta. Labbayka wasa’dayka walkhayru kulluhu biyadika, wash-sharru laysa Ilayka, ana bika wa Ilayka, Tabaarakta wa Ta’aalayta, astaghfiruka wa atuwbu Ilayka
--Muslim (771) and an-Nasa’i (897)

4-Allaahu Akbar Kabiyraa, Allaahu Akbar Kabiyraa, Allaahu Akbar Kabiyrah, wal hamduliLLaahi kathiyraa, wal hamduliLLaahi kathiyraa, wal hamduliLLahi kathiyraa, wasubhaana-Allaahi bukratan wa aswiylaah, wasubhaana-Allaahi bukratan wa aswiylaah, wasubhaana-Allaahi bukratan wa aswiylaah. A’uwdhu biLLaahi minash-shaytwaani min nafkhihi wa nafthihi wa hamzihi
-Muslim (601)

Na Allaah Anajua Zaidi...

𝗗𝗨𝗔 𝗭𝗔 𝗞𝗨𝗝𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗜𝗝𝗜𝗖𝗛𝗢Jicho ovu (au kijicho au Husda) limetajwa katika Quran na Hadith, Kwa hivyo mtu ambaye ameath...
14/09/2025

𝗗𝗨𝗔 𝗭𝗔 𝗞𝗨𝗝𝗜𝗟𝗜𝗡𝗗𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗜𝗝𝗜𝗖𝗛𝗢

Jicho ovu (au kijicho au Husda) limetajwa katika Quran na Hadith, Kwa hivyo mtu ambaye ameathiriwa nayo lazima aombe ulinzi wa Mwenyezi Mungu.

1-
اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ أَنْ أَشْرِكَ بِكَ وأنا أَعْلَمْ، وَأَسْتَغْفِرُكَ لِما لَا أَعْلَم

Allaahumma ‘innii ‘a’uudhubika an ushrika bika wa anaa ‘a’lamu, wa astaghfiruka limaa laa ‘a’lamu.

Tafsiri: "Ewe Mwenyezi Mungu, najikinga kwako nisije nikakushirikisha na chochote nikijua, na nakuomba msamaha kwa nisiyoyajua.” Chanzo: Ahmad 4/403

2-
- بِسْمِ اللَّهِ الَّذِي لَا يَضُرُّ مَعَ اسْمِهِ شَيْءٌ فِي الأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ، وَهُوَ السَّمِيعُ العَلِيمُ

Bismillaahil-lathii laa yadhurru ma’as-mihi shay’un fil-‘ardhwi wa laa fis-samaa’i wa Huwas-Samii ‘ul- ‘Aliim.

Tafsiri: “Kwa Jina la Mwenyezi Mungu ambaye kwa Jina Lake hakuna kitakachodhuru katika ardhi wala mbinguni, Naye ni Mwenye kusikia, Mjuzi wa yote.”

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema kwamba kuisoma dua hii mara tatu asubuhi na jioni kutamlinda mtu, kiasi kwamba hakuna kitakachoweza kumdhuru, na wala asipate balaa. (Chanzo: Abu Dawud, Hadithi nambari 5088, Al-Tirmidhi, Hadithi nambari 3388)

3 -

أَعُوذُ بِكَلِمَاتِ اللَّهِ التَّامَّةِ مِنْ كُلِّ شَيْطَانٍ وَهَامَّةٍ وَمِنْ كُلِّ عَيْنٍ لاَمَّةٍ

A’uudhu bikalimaatil-laahit-taammaati wa min kulli shaitwaanin wa hamma, wa min kulli 'aynin lammah.

Najikinga kwenu kwa Maneno Kamilifu ya Mwenyezi Mungu, na kila shetani, na kila chenye kutambaa chenye sumu, na kila jicho baya - [Sunan Ibn Majah

09/09/2025
tushike udhu vema
09/09/2025

tushike udhu vema

tutende mema ili tupate mema
09/09/2025

tutende mema ili tupate mema

Unachopaswa kufanya wakati wa kupatwa kwa mweziWakati wa kupatwa kwa mwezi (khusuf), Utaswali Swala ya kupatwa kwa mwezi...
08/09/2025

Unachopaswa kufanya wakati wa kupatwa kwa mwezi

Wakati wa kupatwa kwa mwezi (khusuf), Utaswali Swala ya kupatwa kwa mwezi (Salatul Khusuf) Hii Ni Kutokana Na Mtume Rehma Na Amani Ziwe Juu Yake Amesema

"Hakika jua na mwezi ni miongoni mwa alama za Allah, havipatwi kwa sababu ya kifo cha mtu au maisha yake, lakini Allah anazionyesha waja wake. Basi mnapoyaona, simameni mkaswali, muombe, mkumbuke Allah."
(Bukhari & Muslim)

Ama kuhusu Dua ya kusoma wakati wa tukio hili Hakuna dua maalum iliyofundishwa moja kwa moja, lakini unaweza kusoma dua ya toba:

Allahumma ighfir li warhamni wa tub 'alayya, innaka anta At-Tawwab Ar-Rahim.

Ee Allah nisamehe, nihurumie, na nikubalie toba yangu. Hakika Wewe ni Mpokeaji toba na Mwenye kurehemu.

Pia Unaweza Kufanya Tasbih na dhikr:

Subhanallah, Astaghfirullah, La ilaha illa Allah, Allahu Akbar

Na Allaah Anajua Zaidi..

Wengi huuliza ni namna gani anaweza lipa Rakaa ikiwa kamkuta Imam ameipita Rakaa fulani za Swala. Tulisoma Maana ya Raka...
06/09/2025

Wengi huuliza ni namna gani anaweza lipa Rakaa ikiwa kamkuta Imam ameipita Rakaa fulani za Swala. Tulisoma Maana ya Rakaa na jinsi zilivyo na kwaku fahamu hilo basi hapa utajifunza namna ya kulipa Rakaa kwa idadi zake.

1. FAHAMU IDADI ZA RAKAA.
Lazima ujue kwamba swala fulani ina rakaa idadi fulani Mfano swala ya MAGHARIBI ina rakaa 3, ISHAAI ina rakaa 4, FAJR ina rakaa 2, DHUHR NA ASR zina rakaa 4. Hautakiwi kukosa Rakaa kwa idadi ya swala husika.

2. NGUZO ZA SWALA.
Hizi nguzo zipo 14 na wengine ni 15, hivyo katika ukurasa uliopita uliona nguzo hizo za swala na ni lazima mtu atimize nguzo zote za swala.

3. KIGEZO CHA KULIPA.
Ili uweze kulipa Rakaa unatakiwa uwe umepitwa na kitendo cha rukuu kwa Maana imam akiwa amesha itidal (kitendo cha kunyanyuka kutoka katika rukuu na kusimama) basi hapo utahesabu kwamba rakaa hiyo umeikosa.

4. UTAHESABU RAKAA KWA MFANO HUU
Mfano ni swala ya MAGHARIBI ina rakaa 3 kisha ukamkuta Imam amesujudu kisha akakaa tahiyyat na kisha baada ya Tahiyyat akainuka, unahisi utalipa rakaa ngapi? Ni rakaa mbili utalipa kwakuwa umeikosa rukuu ya ile rakaa ya pili.

5. USOMAJI WA SURAH
Katika swala ya rakaa 4, ikiwa mtu amekosa rakaa 3, basi Imaam anapomaliza kutoa salamu ya pili mwishoni mwa Swala, mtu huyu asimame na alipe rakaa tatu alizozikosa kwa namna ifuatayo: katika rakaa ya kwanza. Asome Surah Fatiha, na Surah nyingine, afanye rukuu na sajdah zake kisha akae kwa tahiyyat yake ya kwanza. Baada ya hapo, atoe rakaa yake ya pili na asome Surah Fatiha na Sura nyingine ndani vile vile. Baada ya rakaa hii ya pili ainuke kwa rakaa ya tatu m na asome tu Surah Fatiha. Baada ya rakaa hii, anatakiwa kukaa tahiyyat na kukamilisha Swala...

asalaam aleykum warahmatulah wabarakatuhTangazo kwa wana group ukhy(mwanaume) ama ukhty (mwanamke) kwa yeyote anae itaji...
05/09/2025

asalaam aleykum warahmatulah wabarakatuh
Tangazo kwa wana group ukhy(mwanaume) ama ukhty (mwanamke) kwa yeyote anae itaji ndoa nusra karibu inbox
1.ujitambulishe majina yako
2.unapoishi
3.miaka yako
4.familia (k**a una watoto au mke kwa wanaume
5.sifa za mwanaume au mwanamke unae muitaji
hii ni bure kuunganishwa ni BURE

Fadhila za Suwratul-FaatihahHii ni Suwrah iliyokuwa Adhimu na bora, kuliko Suwrah zote za Qur-aan, nayo ni miongoni mwa ...
02/09/2025

Fadhila za Suwratul-Faatihah

Hii ni Suwrah iliyokuwa Adhimu na bora, kuliko Suwrah zote za Qur-aan, nayo ni miongoni mwa Suwrah zenye majina mengi na miongoni mwa majina yake ni:

Al-Faatihah, Ummul-Qur-aan, AlhamduliLLaah, Asw-Swalaah, Ash-Shifaa, Ar-Ruqyah, Sab‘ul-Mathaaniy, Ummul-Kitaab. Haijateremka katika Tawraat wala katika Injiyl wala katika Zaburi mfano wake.

Utukufu na Fadhila za Suwratul-Faatihah unaelezewa katika Hadiyth nyingi, Na baadhi yake ni hizi zifuatazo:

1- Suwaratul-Faatihah Ni Shifaa (Poza)

Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba: Baadhi ya Maswahaaba (wakiwa safarini) walifika karibu na kabila fulani la Waarabu, wakakataa kuwapokea. Walipobakia katika hali hiyo, huku mkuu wao alitafunwa na nyoka (au nge). Wakasema: Je, mna dawa yoyote au tabibu? Wakajibu: Nyinyi mmekataa kutupokea kwa hiyo hatutamtibu mgonjwa wenu hadi mtulipe! Wakakubali kuwapa kundi la kondoo. Mmoja wa Swahaaba akaanza kumsomea Suwratul-Faatihah huku akikusanya mate na kumtemea (mahali alipotafunwa). Mgonjwa akapona kisha watu wake wakawaletea kondoo lakini wakasema. Tusiwachukue mpaka tumuulize Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Walipomuuliza alicheka akasema: “Mmejuaje kuwa Suwratul-Faatihah ni ruqya? Wachukueni na nigaieni sehemu yangu.” [Al-Bukhaariy]

2- Suwratul-Faatihah: Swalaah Haitiimi Bila Kuisoma

‘Ubaadah bin Swaamit (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakuna Swalaah kwa asiyesoma (ndani yake) Ufunguo wa Kitabu.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

3- Suwratul-Faatihah Ni Aayah Saba Zinazokaririwa:

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

"Na kwa yakini Tumekupa (Aayaat) Saba zinazokaririwa (kusomwa) na Qur-aan Adhimu."

‘Ulamaa wa Tafsiyr akiwemo Imaam As-Sa’diy na Ibn Kathiyr, wamenukuu kuwa hizo ni ima Suwrah Saba za mwanzoni au ni Aayat Saba za Suwratul-Faatihah kwa kuwa zinakaririwa kusomwa katika Swalaah.

Na Allaah Nimjuzi Zaidi..

enhee twambie ilikuaje 😂
27/08/2025

enhee twambie ilikuaje 😂

tunaomba majibu
25/08/2025

tunaomba majibu

Address

Kilombero
Morogoro

Telephone

+255659938442

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Proudly Muslim posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category