30/01/2026
Katika hatua muhimu mnamo January 29, 2026, serikali ya kijeshi ya bukinafaso inayoongozwa na Captain Ibrahim Traore,
imetangaza rasmi kuvifuta vyama na vikundi vya siasa nchini humo, ikiambata na kufutwa kwa sheria iliyokuwa ikisimamia uendeshaji wake,
serikali iliidhinisha muswada wa kufuta sheria zilizopo za vyama vya siasa, ufadhili wa umma, na hadhi rasmi ya "Kiongozi wa Upinzani,
huku mali zote zilizokuwa zikimilikiwa na vyama hivyo zikihamishiwa serikalini,
Waziri Emile Zerbo alisema uvunjaji huo ulikuwa muhimu kwa sababu vyama "vimekengeuka" vimetoka katika misingi yao ya awali, wanachokifanya sasa ni kuchochea migawanyiko ya kitaifa, na kudhoofisha mifumo ya kijamii",
huku akisisitiza kuwa uamuzi huo unalenga kujenda umoja na mshikamono wa kweli ki taifa,
Captain Traore amekosoa hadharani muundo wa demokrasia, akisisitiza kwamba “hakuna nchi inayoweza kuendeleza chini ya mfumo wa demokrasia” na kubainisha utawala wake k**a "mapinduzi maarufu, yanayoendelea" badala ya mfumo wa kidemokrasia,