18/05/2026
"BIASHARA ZAMESIMAMA, SERIKALI ISHUSHE MAFUTA!" β WADAU WA USALAMA NA USAFIRI KENYA WALIA KATIKA MGOMO MKUBWA.
Hali ya usafiri na biashara imeingia dosari kubwa nchini Kenya baada ya madereva na waendesha bodaboda kugoma kuingia barabarani na steshi, wakishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta.
Mgomo huo umeathiri mnyororo mzima wa kiuchumi, huku wafanyabiashara wa maeneo ya steshi (ikiwemo wauzaji wa simu na vifaa vya kielektroniki) wakilalamika kukosa wateja kabisa kwa sababu hakuna magari yanayoleta abiria kutoka maeneo k**a Nairobi na Bungoma.
"Sisi sanasana watu wa bodaboda huwa tunategemea magari... Serikali ikipunguza mafuta kidogo na wananchi tutarudi kupata mkate wetu," ameeleza mmoja wa wenyeviti wa bodaboda.
Wafanyabiashara wengine wameeleza kuwa kwa siku ya kawaida huingiza hadi KSh 500 au 700, lakini kutokana na mgomo huo, hadi mchana walikuwa hawajapata hata shilingi 50.
Tazama video hii fupi hapa chini usikie kilio chao kamili! π
Hali ni mbaya sana, hakuna biashara leo!" Hicho ndicho kilio cha wafanyabiashara, madereva, na waendesha bodaboda nchini Kenya kufuatia mgomo mkubwa wa usafi...