24/02/2026
AK**ATIKA K**A SAMSON
Taarifa kubwa duniani kwa sasa ni kifo cha Nemesio Oseguera Cervantes(El Mencho) ambae alikuwa mlanguzi mkubwa wa madawa ya kulevya na kiongozi wa genge la Jalisco New Generation Cartel(CJNG) nchini Mexico ambae aliuawa na Jeshi la nchi hiyo. Leo Februari 24,2026 Waziri wa Ulinzi wa Mexico, Ricardo Trevilla Trejo amesema walipata kujua alipokuwa El Mencho kupitia mshirika wa karibu wa mwanamke wake ambae alikuwa amekutana nae Februari 20, 2026.
Akizungumza na vyombo vya habari leo Trevilla amesema “Tarehe 20 Februari, kupitia kazi ya ujasusi wa kijeshi, mshirika wa kuaminika wa mmoja wa wapenzi wa Mecho alitambuliwa. Mshirika huyo alimpeleka kwenye kituo kilichopo katika kijiji cha Talpa, Jalisco. Huko Mencho alikutana naye pamoja na huyo mwenzi wake.” Anaeleza Trevilla kuwa baada ya taarifa hizo kujulikana kikosi kilichojumuisha helikopta sita na askari wa vikosi maalum kiliwasili kimyakimya katika eneo la operesheni ili kudumisha usiri na watu kushtukia tukio.
Anaeleza zaidi kuwa El Mencho aliondoka eneo hilo na kuacha kundi lililokuwa na kiasi kikubwa cha silaha na shambulio lilikuwa la vurugu sana lililofanywa na watu wahalfu waliopangwa ambapo wanajeshi wa vikosi maalum walifanikiwa kuzuia mashambulizi hayo. Baada ya hali kudhibitiwa wahudumu wa afya wa kijeshi walielekea mahali alipokuwa El Mencho na walinzi wake ambapo walinzi wawili waliojeruhiwa. Kutokana na hali aliyokuwa nayo El Mencho waligundua kuwa ilikuwa lazima kuwahamisha kwa sababu walikuwa katika hali mbaya sana.
Msaada wa helikopta uliombwa ili kuwapeleka katika kituo cha matibabu huko Jalisco. Na baadae El Mencho, walinzi wake wawili na afisa aliyejeruhiwa walihamishwa. Kwa bahati mbaya, walifariki dunia wakiwa njiani. Funzo: Usimwamini mwanamke .