28/11/2025
Upendo huleta amani kutoka kwenye moyo wa mwenye haki, k**a Dunia tungeishi kwa Upendo na sio kwa kum-bania mwezako anapohitaji haki basi Dunia ingekuwa sehemu Bora zaidi ya sasa.
Watu wanateseka kwenye maisha kwa kukosa haki ambayo ingewapa amani, huwezi kuwa kwenye amani ndani ya mahusiano k**a uliyenaye hataipa haki nafasi ila k**a akijua thamani ya haki basi atajua haki Yako kwake ni kuwa na amani yenye furaha na sio maumivu yenye majuto.
Mda mwingine kinachofanya watu wasiwe waaminifu kazini au kwenye biashara tunazowaweka ni kwasababu mioyo yao imejaa hofu ya kukosa haki, muda mwingi anawaza ubaya kuliko mema... Anawaza k**a atafanya haki alafu ukaja kumtoa bila kujiweka sawa, anawaza k**a itatokea mmegombana itakuwaje. Kwahiyo matokeo yake ni yeye kutoka kwenye misingi ya haki ya mali Yako na kujipa haki ambayo itamfaya lolote likitokea basi iwe hivyo (hapo ndio mtu anaanza kuingiza ujanja).