Nkiliye Media

Nkiliye Media Official page Nkiliye Media
NEWS & UPDATE | LIVE EVENT | LIVE PROGRAM |
INTERVIEWS

Upendo ni Nguvu inayobadilisha Dunia,Hakikisha sehemu ya maisha yako yanakamilishwa na upendo.
18/04/2025

Upendo ni Nguvu inayobadilisha Dunia,
Hakikisha sehemu ya maisha yako yanakamilishwa na upendo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika, Dkt. Zarau Kibwe, amepongeza uongozi wa Rais  akieleza kuwa ni ch...
13/03/2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika, Dkt. Zarau Kibwe, amepongeza uongozi wa Rais akieleza kuwa ni chanzo cha kuongezeka kwa kiwango cha mkopo ambacho Tanzania inaweza kupata kutoka Benki ya Dunia, kutoka Dola bilioni 5 (zaidi ya Shilingi trilioni 10) hadi Dola bilioni 12 za Marekani (zaidi ya Shilingi trilioni 25).

"Sijui huko nyumbani k**a mnaliona au kulizungumza hili. Katika muda mfupi ambao Rais Samia ameingia madarakani, ukomo wa Tanzania kwenye uhusiano wake na Benki ya Dunia umeongezeka kutoka dola bilioni tano hadi bilioni 12. Hili si jambo la kawaida," amesema Kibwe.

Kwa upande wake, Waziri Ulega amempongeza Kibwe kwa kushika wadhifa huo mkubwa k**a Mtanzania, akisema kuwa Watanzania wanajivunia mafanikio yake. Pia, ametumia fursa hiyo kueleza maendeleo ya miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia, ikiwemo ujenzi wa barabara, mwendokasi na madaraja.

Ulega amegusia changamoto ya wakandarasi wa kigeni kuchelewesha miradi, akipendekeza kwamba wanapaswa kufungua akaunti Tanzania ili kuwezesha malipo kufanyika haraka na miradi isikwame.

Katika majibu yake, Kibwe amemhakikishia Waziri Ulega kuwa Benki ya Dunia itaendelea kushirikiana na Tanzania, huku akimpongeza kwa msukumo mkubwa katika sekta ya ujenzi.

"Niliona mabadiliko makubwa Dar es Salaam na nikaambiwa ‘there is a new sheriff in town’. Hongera sana kwa kazi nzuri, mambo yako yanaonekana," amesema Kibwe.

Benki ya Dunia pia imethibitisha kuunga mkono mradi mkubwa wa barabara kuelekea Kusini mwa Tanzania, ikiwemo ujenzi wa Daraja la Mzinga eneo la Kongowe, Dar es Salaam.

Kibwe ni Mtanzania wa pili kushika wadhifa huo wa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika inayohusisha takribani nchi 23. Mtanzania wa kwanza alikuwa Christopher Kahangi aliyeshika wadhifa huo kati ya mwaka 1968 hadi mwaka 1970.

UWANJA WA AFCON ARUSHA WAFIKIA 25%Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serika...
04/02/2025

UWANJA WA AFCON ARUSHA WAFIKIA 25%

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa amesema ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Arusha unaotarajiwa kutumika kwa ajili ya mashindano ya Fainali za AFCON 2027 umefikia 25% za ujenzi wake.

Msigwa amesema hayo leo tarehe 3 Februari 2025 wakati alipotembelea na kukagua maendeleo ya Mradi wa ujenzi wa uwanja huo unaojengwa katika kata ya Olmoti jijini Arusha.

Aidha, Msigwa amemtaka mkarandarasi anae Jenga uwanja huo wa kisasa wa Michezo wa Arusha kuongeza Kasi zaidi kwa kuzingatia viwango.

Yanga Sc yauwasha Moto dhidi ya Kagera Sugar   FT: Yanga SC 4-0 Kagera Sugar⚽️ Mzize⚽️ Mudathir⚽️ Pacome (p)⚽️ Musonda
02/02/2025

Yanga Sc yauwasha Moto dhidi ya Kagera Sugar

FT: Yanga SC 4-0 Kagera Sugar
⚽️ Mzize
⚽️ Mudathir
⚽️ Pacome (p)
⚽️ Musonda

"Wafanyabiashara wengi wa biashara ndogo na za kati tunakimbia kulipa kodi, naomba mshirikiane nasi kwa kiwango unachoza...
31/01/2025

"Wafanyabiashara wengi wa biashara ndogo na za kati tunakimbia kulipa kodi, naomba mshirikiane nasi kwa kiwango unachozalisha lipa kidogo kwa serikali ili mambo yaweze kuwa mazuri zaidi, mkifanya hivyo tunailinda nchi yetu na kuwa ombaomba na kupunguza mikopo, tunakopa kujenga, tunakopa kuitengeneza nchi, mwingine huko asiyejua anasimama hii serikali kazi kukopa tu, kwani tunakopa kwenda kununua sare za harusi?, tunakopa kujenga reli , barabara, mashule na huduma za afya, tunakopa kuufanya mji wa Dar es Salaam na Dodoma ziwe capital za kuheshimika tunakopa kukuza hadhi ya nchi yetu, tunakopa kwa sababu," -Rais

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, imesaini hati ya Maku...
30/01/2025

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, imesaini hati ya Makubaliano ya Ushirikiano na Serikali ya Shirikisho la Jamhuri ya Somalia kupitia Wizara ya Elimu, Utamaduni na Elimu ya Juu kuhusu kukieneza Kiswahili na Utamaduni wake nchini Somalia.

Hati hiyo ya makubaliano ya ushirikiano imetiwa saini leo Januari 29, 2025 katika ukumbi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Jumuiya Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam, pande hizo mbili zimekubaliana kukieneza Kiswahili na Utamaduni wake nchini Somalia, kwa kutumia mbinu anuai k**a vile matumizi ya TEHAMA.

Aidha, maeneo mengine ya ushirikiano huo ni kuzalisha na kuuza machapisho ya Kiswahili, Wataalamu wa Tanzania kujifunza Kisomali na kuwezesha huduma za tafsiri na ukalimani kupitia kubadilishana wataalamu na kuwezesha tafiti.

Serikali imesema inaendelea kusimamia na kuhakikisha viwanja vinavyojengwa na vinavyokarabatiwa kwa sasa vinazingatia mi...
29/01/2025

Serikali imesema inaendelea kusimamia na kuhakikisha viwanja vinavyojengwa na vinavyokarabatiwa kwa sasa vinazingatia miundombinu ya watu wenye mahitaji maalumu na kuweza kutumika na makundi yote ikiwemo watu wenye ulemavu.

Kauli hiyo imetolewa Bungeni leo tarehe 29 2025 na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na michezo, Mhe Hamis Mwinjuma wakati akijibu swali la Mbunge Mwatatu Mbarak Khamis aliyetaka kujua Serikali imejipangaje kuhakikisha kuwa viwanja vya michezo kwa watu wenye ulemavu vinaendelea kuwepo na vinaimarishwa.

Mhe mwinjuma ameongeza kuwa Uzingativu huo unatolewa pia kwa wadau na taasisi zote zinazomiliki na kuendesha miundombinu ya michezo kuhakikisha wanaweka maeneo maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu kuweza kushiriki wakati wa matukio ya kimichezo k**a ambavyo imewekwa katika uwanja wa Benjamini Mkapa, Dar es Salaam na uwanja unaoujengwa jijini Arusha, Samia Suluhu Stadium.

Aidha, amesema Wizara imeendelea kutoa vifaa vya michezo kwa watu wenye mahitaji maalumu hasa katika ngazi ya timu za Taifa ndani ya kundi hili maalum ili kuwawezesha kutumia viwanja vilivyopo.

  Moto wa Arsenal umewaka kwa maajabu FULL TIME: Arsenal 2-1 TottenhamSon⚽Gabriel⚽Trossard⚽
16/01/2025

Moto wa Arsenal umewaka kwa maajabu

FULL TIME: Arsenal 2-1 Tottenham
Son⚽
Gabriel⚽
Trossard⚽

Jeshi la Polisi mkoa wa Tanga linamsaka Mwita Yoba, kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba na kusababisha vifo vya watu wanne...
31/12/2024

Jeshi la Polisi mkoa wa Tanga linamsaka Mwita Yoba, kwa tuhuma za kuchoma moto nyumba na kusababisha vifo vya watu wanne, ambao ni mama na watoto wake watatu.

Akizungumza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga Almachius Mchunguzi, amesema tukio hilo limetokea Desemba 30 mwaka huu saa 10:45 alfajiri katika Kitongoji cha Kwedichocho ,Kijiji cha Manga wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Aliwataja waliofariki kuwa ni Pili Saguge(28),mkulima na mkazi wa Kwedichocho (mama), Chacha Nyabilenga, Jane Nyabilenga na Makabala Nyabilenga.

Aidha Kamanda huyo alisema kwamba baada ya kufanya tukio hilo mtuhumiwa alitoroka na kutokomea kusikojulikana.

Kamanda Mchunguzi amesema chanzo cha mauaji hayo ni mtuhumiwa kuishtumu familia hiyo kwa madai ya kumuua mtoto wake kwa sumu hali iliyomsukuma kutekeleza mauaji hayo kwa kulipiza kisasi.

Watu tisa wamefariki dunia baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria kutoka Tarakea wilayani Rombo mkoani Kilima...
26/12/2024

Watu tisa wamefariki dunia baada ya gari aina ya Noah walilokuwa wakisafiria kutoka Tarakea wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro kugongana uso kwa uso na basi la Ngasere lililokuwa likitokea Dodoma kuelekea Rombo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Mkuu wa wilaya ya Rombo, Raymond Mangwala amesema kuwa tukio hilo limetokea leo Desemba 26, 2024 katika maeneo ya Tarakea.

Amesema kuwa, katika ajali hiyo watu tisa ambao ni wanaume watano na wanawake wanne waliokuwa katika Noah walifariki dunia papohapo na kuna majeruhi mmoja ambaye amekimbizwa hospitali ya Huruma kwa matibabu.

Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa, chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi ambapo dereva wa Noah alikuwa akilipita gari jingine ndipo alipokutana na basi na Ngasere na kugongana nalo uso kwa uso.

Unajua Kuhusu Msimamo wa Kundi A Mpaka sasa ukoje?Upo hivi👇1. Constantine    -  Alama 62. Simba  -   Alama 63. Bravos Do...
15/12/2024

Unajua Kuhusu Msimamo wa Kundi A Mpaka sasa ukoje?
Upo hivi👇

1. Constantine - Alama 6
2. Simba - Alama 6
3. Bravos Do Maquis - Alama 3
4. CS Sfaxien - Alama 0

FT: Simba Sc 🇹🇿 2-1 🇹🇳 CS Sfaxien
02’ H Haji
07’ 90+8 Kibu D

Jeshi la Hapo jana lilitoa taarifa kuhusu Ajali ya Basi lililokuwa limebeba wabunge.“Kikubwa chanzo cha ajali hiyo ni de...
07/12/2024

Jeshi la Hapo jana lilitoa taarifa kuhusu Ajali ya Basi lililokuwa limebeba wabunge.

“Kikubwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa basi la Shabiby ambalo lilikuwa limebeba wabunge na maafisa wengine wa bunge ni uzembe wa kutochukua tahadhari wakati akipishana na gari lililokuwa mbele yake hivyo kugongana na lori hilo, ajali imesababisha mpaka sasa tuna majeruhi 19 kwa taarifa za awali, wabunge 16 maafisa wengine wabunge wawili pamoja na dereva na wote wanaendelea na matibabu’

Alisema Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma SACP George Katabazi kuhusu ajali ya basi la Wabunge iliyitokea mapema jana maeneo ya Kongwa, Dodoma, Katabazi na tayari wanamshikilia dereva wa gari la Shabiby kutokana na uzembe barabarani na kutochukua tahadhari, pia akatoa rai kuwa Jeshi la Polisi halitosita kuchukua hatua kwa yoyote asiyezingatia sheria za barabarani.

Address

Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nkiliye Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nkiliye Media:

Share